09/05/2026
Waziri wa vyama vya ushirika na biashara ndogondogo MSME Wyckliffe Oparanya amewataka vijana kukumbatia biashara na kilimo ili kunufaika na mipango ya serikali ya kuinua viwango vyao vya maisha.
Akizungumza kwenye hafla ya kuhamasisha wakulima wa kahawa Butula mapema leo, Oparanya vilevile amewasuta viongozi wa chama cha ODM kwa kuwaondoa baadhi yao mamlakani akisema, hatua hiyo imewapa wakati mgumu, haswa katika eneo la magharibi ambayo ni ngome ya chama hicho, wanapotangamana na wananchi mashinani na hata kuelezea sera za serikali ikizingatiwa kuwa wamo ndani ya makubaliano ya broad based goverment pamoja na chama tawala cha UDA.
Amewataka viongozi wa ODM kushirikiana na kuondoa mgawanyiko ndani ya chama hicho ili kafanikisha uchaguzi mkuu ujao na kisha kutatua changamoto zinaikumba baada ya uchaguzi.
updates
Like || Comment || Follow