08/04/2026
✅ 𝐀𝐘𝐀𝐍𝐀 𝟖𝐓𝐇 𝐀𝐏𝐑𝐈𝐋 𝐖𝐑𝐈𝐓𝐓𝐄𝐍 𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄𝐒✅
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟏
Kefa na Tinah walikuwa na mazungumzo marefu sana. Tinah akamwambia Kefa, “Mimi si Kylian. Kylian alikimbia akaenda kwa Robert, lakini mimi Tinah sikufukuzwa. Nilienda kwa Robert bila mtu kunizuia.”
Tinah akaendelea, “Sikiza Kefa, wewe huwezi kumuelewa Kylian. Imagine uamke siku moja ukambiwe Mbalamwezi ni babako… utachanganyikiwa tu. Yafaa uelewe Kylian.”
Kefa akamwambia Tinah, “Unajua kesho tulikuwa tunakwenda na Annalisa na wengine Zanzibar, Tanzania. Lakini kwa sababu hawako, itabidi nizirarue tu hizi tiketi.”
Tinah akamuuliza, “Mbona unazirarua? Unaweza pata mtu muende naye…”
Kefa akamjibu, “Sidhani naweza pata mtu… unless awe wewe maybe.”
Tinah kwanza akashtuka, lakini akarelax. Akakumbuka amekuwa akitaka kwenda Zanzibar sana, akamwambia Kefa, “Kama ilikuwa uende kesho, then I’m in with you. Tutaenda wote.”
Tinah… hiyo ilikuwa **mistake kubwa sana**.
Kefa alikuwa anataka kumaliza Robert tu! Baaaaasi! Ba! Baaaaaaasi!
Mara tu Tinah alipoondoka, Kefa alipiga simu jamaa fulani na kumwambia, “Guess what? Amekubali. Kumbe anapenda tu wababa na soft life. Plan yetu iko exactly k**a tulitaka.”
Tinah maskini wa Mungu… ameshanazwa vibaya 😂.
Upande mwingine, Saida amekuja kuona Tyrone. Anajifanya hataki, anamwambia hataingia ndani… lakini deep down anajua by now anapaswa kuwa **ndani ndani ndani** ya serikali 🤣🤣. Hatimaye waliingia ndani kuongea.
Annalisa naye anarudi kwake. Alitoka jana jioni, akaenda kwa Robert akagongwa hadi asubuhi. Sasa ndio anarudi kwa Kefa na kumuita “babe”.
Annalisa anaita kimya… “Babe?” tena. Kimya. Akashangaa mbona hakuna mtu. Akafungua mlango akaingia ndani. Kefa hayuko!
Kumbe Kefa alikuwa nje. Alirudi na kumkuta Annalisa chumbani. Annalisa akajitetea, “Daddy, pole nililala nje… I just wanted sometime alone.”
Kefa akamuuliza, “Ooh, so ukaamua kuwa na ‘sometime alone’ na baby daddy?”
Annalisa akamwambia, “Zii! Sikulala kwa Robert. Nililala hotel.”
Kefa akasema, “Ni sawa, haina shida.”
Annalisa akadhani kila kitu kiko sawa, akamwambia, “Babe, with everything going on, I think we need to have a break.”
Kefa akashangaa, “Break tena? Yani issue ya jana tu umeshaitisha break? Unajua break ni kuenda kugongewa wewe 🤣🤣🤣”
Kefa akamwambia, “Ni sawa. Ni juu umeamua. Sina la kusema na ninarespect decision yako.”
Annalisa akaenda chumbani kufunga vitu aondoke 🤣🤣🤣
Huh! She never saw what was coming…
**𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄 𝟐**
Tyrone alijieleza kwa Saida na kumwambia anataka kurekebisha mambo na yeye ni remorseful sana. Aliomba sana, anataka tu kuwa katika maisha ya bintiye.
Saida akamuuliza, “Hukusikia jana Asha akisema hataki?”
Tyrone akamwambia, “Mama Asha, hata nimepiga magoti. Kupitia kwako najua atanisamehe.”
Saida akaona enyewe Tyrone amepiga magoti na anahitaji kusamehewa… lakini punde si punde, mlango ukabishwa.
Tyrone akafungua mlango… guess who? **Serena** 🤣🤣
Tyrone akamuuliza, “Unatoka nini hapa?”
Serena akamwambia, “Babe kwani hukunimiss?”
Tyrone akamwambia, “Wewe ndio mistake kubwa zaidi niliyowahi fanya. Wewe ni immature na childish. Nisiwai taka kukuona tena.”
Serena akamuuliza, “Kwani unaniambia hivi kwa sababu ya Saida?”
Tyrone akamjibu, “Huo upuzi wako sitaki. Enda tafuta bosko mwingine huko nje!”
Annalisa naye alijaribu kutoka… alishtuka! Kefa amemshika na kumwambia, “Sikiza huku, mimi ndiye nitaamua wakati wa kuenda.”
Kefa akaanza kumnyonga Annalisa… lakini kwa bahati ya Mungu, Robert alikuwa anamfuata Annalisa. Alifika na kumkuta akinyongwa, akamtandika Kefa!
Kefa akaachana na Annalisa na kugeukia Robert. Ndani ya dakika chache, Kefa alikuwa amechafua Robert mangumi ya majembe kwa mbavu mbavu 🤣🤣
Ilibidi Annalisa atafute chuma amgonge Kefa aanguke, kisha wote wawili na Robert ni kuhepa wahepe juu ni kubaya bwana 🤣🤣🤣 Robert amelimwa vibaya sana.
Sabina naye aliamua kutafuta mganga aitwaye Billy Miya amsaidie na uganga ili ndoa yake na Tyrone irudi 🤣🤣🤣🤣 Woiye mapenzi.
Saida alikuja kuongea na Asha na kumwambia, “Babako anataka kukuona. Bado yuko shuleni na huyo huyo babako mwenye humtaki ndiye analipa fee, usisahau hilo.”
Asha akamwambia, “Ma’am sikiza, nilisema na nilimaliza. Wewe k**a unataka kurudi kwa Tyrone nenda. Mimi na Ray tuko sawa hapa.”
Asha **hataki kitu chochote** na Tyrone.