Uvoro TV Business .

  • Home
  • Uvoro TV Business .

Uvoro TV Business . Kenya region.
(3)

Uvoro TV is among Kenya's best TV channels broadcasting in English & kiswahili.We take pride in the provision of indispensable source of information, music, and entertainment while strengthening the civic and cultural life of the larger Mt.

Leo, jamii ya Wadi ya Mutira katika Kaunti ya Kirinyaga imekusanyika kwa huzuni na mshik**ano kumwaga machozi ya mwisho ...
21/07/2025

Leo, jamii ya Wadi ya Mutira katika Kaunti ya Kirinyaga imekusanyika kwa huzuni na mshik**ano kumwaga machozi ya mwisho kwa Peter Macharia Mugo, kijana mwenye matumaini na ari ya maisha ambaye maisha yake yalikatizwa ghafla na afisa wa polisi asiye na nidhamu kutoka Kituo cha Polisi cha Kagumo.

Wakazi wa eneo hilo walikusanyika kwa wingi kuomboleza maisha ya kijana huyo, wakielezea masikitiko yao na kuitaka serikali kuhakikisha haki inatendeka. Familia na marafiki wamesisitiza haja ya uchunguzi wa kina kufanywa na hatua kali kuchukuliwa dhidi ya waliohusika.


Rais wa zamani wa Chama cha Wanasheria nchini (LSK), Eric Theuri, amekosoa vikali hatua ya serikali kuwafungulia waandam...
21/07/2025

Rais wa zamani wa Chama cha Wanasheria nchini (LSK), Eric Theuri, amekosoa vikali hatua ya serikali kuwafungulia waandamanaji waliok**atwa mashtaka yanayohusiana na ugaidi, akiitaja hatua hiyo kuwa "ya kuchekesha" na isiyo na msingi wowote wa kisheria.

Akizungumza katika mahojiano na moja wapo wa kituo cha habari, Theuri alitaja kisa cha mwanaharakati Boniface Mwangi, aliyek**atwa usiku wa Jumamosi nyumbani kwake Lukenya, Kaunti ya Machakos, na maafisa wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) kwa madai ya “kuchochea ugaidi” wakati wa maandamano ya tarehe 25 Juni.

Theuri alisema kuwa kutumia sheria za ugaidi katika mazingira hayo ni matumizi mabaya ya sheria kwa kiwango kikubwa, na kwamba hatua hiyo inaweza kuchochea hasira zaidi miongoni mwa wananchi badala ya kushughulikia sababu halisi za machafuko.


Mwenyekiti wa Shirikisho la Judo, Maluki, achaguliwa kuwa Rais mpya wa Kamati ya Olimpiki ya Kitaifa ya Kenya (NOC-K).  ...
21/07/2025

Mwenyekiti wa Shirikisho la Judo, Maluki, achaguliwa kuwa Rais mpya wa Kamati ya Olimpiki ya Kitaifa ya Kenya (NOC-K).



"Wananchi wa Embu hawajapewa ufafanuzi wa kutosha kuhusu Bajeti ya 2025,"Ni kauli ya Hon. Pithon Muchoki alipokuwa akiho...
21/07/2025

"Wananchi wa Embu hawajapewa ufafanuzi wa kutosha kuhusu Bajeti ya 2025,"

Ni kauli ya Hon. Pithon Muchoki alipokuwa akihojiwa na Embu FM, ambapo alieleza kuwa wakaazi wa Embu hawajapokea maelezo ya kina kuhusu Bajeti ya Mwaka 2025 – licha ya kuwa bajeti hiyo ina athari kubwa kwa maendeleo yao ya kila siku.

Muchoki alisema kuwa ni muhimu wananchi waelewe jinsi fedha za umma zinavyotengwa na kutumika, ili wawe na nafasi ya kushiriki kwa uelewa katika maendeleo ya kaunti.

Aidha, alieleza kuwa ana matumaini ya kuwania kiti cha Seneta mwaka wa 2027, akiahidi kuhudumia wakazi wa Embu kwa uwazi, uwajibikaji na utetezi wa maslahi yao katika Bunge la Seneti.


Chama cha Democracy for the Citizens Party (DCP) kinachoegemea upande wa Naibu Rais Rigathi Gachagua, kimewasilisha wago...
18/07/2025

Chama cha Democracy for the Citizens Party (DCP) kinachoegemea upande wa Naibu Rais Rigathi Gachagua, kimewasilisha wagombea wake wa kwanza kushiriki katika chaguzi ndogo zijazo kwa ajili ya kujaza nafasi wazi za uongozi.

DCP kimemteua wakili Edgar Busiega kuwania kiti cha ubunge cha Malava, Kaunti ya Kakamega, na Aden Mohamed kuwania ubunge wa Banisa, Kaunti ya Mandera.

Kwa mujibu wa chama hicho, zaidi ya Wakenya milioni 1.8 tayari wamesajiliwa kuwa wanachama ndani ya muda wa miezi miwili tangu kuzinduliwa kwake.

Naibu kiongozi wa chama hicho, Cleophas Malala, alisema kuwa DCP itawasilisha wagombea katika kila uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika, ikiwemo maeneo yanayojulikana kuwa ngome za wafuasi wa Rais William Ruto.

“Tumeamua kuwa tutashiriki katika chaguzi ndogo zote nchini – viti vyote 22 vya MCA pamoja na viti sita vya ubunge. Hata katika eneo la Nyanza, tutatoa wagombea,” alisema Malala.

Aidha, Malala aliwataka makamishna wapya wa IEBC kuanza kazi mara moja kwa kuhakikisha uwazi, uwajibikaji, na uadilifu katika mchakato wa uchaguzi. Alisisitiza pia haja ya kuchukuliwa hatua kali dhidi ya viongozi waliodai kuwa uchaguzi wa mwaka 2027 utavurugwa.

“Tunaitaka IEBC ianze kuchukua hatua sasa. Tutaandikisha malalamiko rasmi dhidi ya wabunge waliotoa matamshi ya kuhatarisha amani kuhusu uchaguzi ujao,” alisema.



Mahak**a yamwachilia Mbunge wa Naivasha, Jayne Kihara, kwa dhamana ya kibinafsi ya Shilingi 50,000, akisubiri uamuzi wa ...
18/07/2025

Mahak**a yamwachilia Mbunge wa Naivasha, Jayne Kihara, kwa dhamana ya kibinafsi ya Shilingi 50,000, akisubiri uamuzi wa iwapo atashtakiwa kwa kosa la tabia ya kuudhi. Kesi yake imepangwa kusikilizwa tarehe 29 Julai.



Tume ya Huduma kwa Walimu (TSC) imetangaza kuanza kwa mafunzo ya kitaifa ya kuwawezesha upya walimu wa shule za upili, k...
18/07/2025

Tume ya Huduma kwa Walimu (TSC) imetangaza kuanza kwa mafunzo ya kitaifa ya kuwawezesha upya walimu wa shule za upili, k**a sehemu ya maandalizi ya kutekeleza Elimu Inayozingatia Umahiri (CBE) chini ya Mtaala wa CBC.

Mafunzo haya ya ana kwa ana yanatarajiwa kuanza tarehe 28 Julai hadi 15 Agosti 2025, na yatafanyika katika vituo maalum vilivyoteuliwa katika kaunti mbalimbali nchini.

Kulingana na waraka wa ndani uliotumwa kwa Maafisa wa Elimu wa Kanda na Kaunti, mafunzo haya yanalenga walimu wa shule za sekondari za kawaida, taasisi za Elimu Maalum (SNE), na vituo vya mafunzo ya kiufundi.

“Maafisa wa kaunti watahitajika kuwachagua walimu watakaopokea mafunzo haya pamoja na wakufunzi wa walimu,” waraka huo unasema kwa sehemu.

Lengo kuu la mpango huu ni kuwaandaa walimu kufundisha kwa mujibu wa njia mpya za masomo zinazopaswa kutekelezwa katika shule za upili chini ya mfumo wa CBC. Walimu watakaoshiriki watapangwa katika makundi matatu makuu ya ujifunzaji.



Chama cha Usalama wa Boda Boda nchini Kenya (BAK) kimemkosoa vikali mshauri mkuu wa masuala ya kikatiba wa Rais William ...
18/07/2025

Chama cha Usalama wa Boda Boda nchini Kenya (BAK) kimemkosoa vikali mshauri mkuu wa masuala ya kikatiba wa Rais William Ruto, Makau Mutua, kufuatia wito wake wa hivi majuzi wa kutaka marufuku ya boda boda katika miji mikuu na miji midogo nchini.

Kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa X mnamo Alhamisi, Julai 17, 2025, Mutua aliwatuhumu waendeshaji boda boda kuwa wachochezi wa “vurugu, ukiukaji wa sheria, uharibifu wa mandhari ya miji, na ukosefu wa nidhamu” barabarani. Alidai pia kuwa miji ya kisasa haipaswi kuwa na kile alichokiita “machafuko ya mijini,” akisema sekta hiyo inaharibu sura na utendakazi wa miji ya Kenya.

“Nimeshawishika kwamba boda boda zote zinapaswa kupigwa marufuku barabarani katika miji mikuu na midogo ya Kenya,” alisema Mutua.

Kauli hiyo ilizua upinzani mkali na kuchochea mjadala mpya kuhusu nafasi ya sekta ya boda boda katika mfumo wa usafiri nchini.


Manyatta MP Gitonga Mukunji summoned to appear at DCI headquarters Nairobi  today at 10am
17/07/2025

Manyatta MP Gitonga Mukunji summoned to appear at DCI headquarters Nairobi today at 10am

Waziri wa Afya Aden Duale na Gavana Anyang’ Nyong’o Wazuru Kituo cha Afya cha Railways Kukagua Mchakato wa KidijitaliWaz...
16/07/2025

Waziri wa Afya Aden Duale na Gavana Anyang’ Nyong’o Wazuru Kituo cha Afya cha Railways Kukagua Mchakato wa Kidijitali

Waziri wa Afya Aden Duale, kwa ushirikiano na Gavana wa Kisumu Profesa Anyang’ Nyong’o na viongozi wengine, walifanya ziara katika Kituo cha Afya cha Railways mnamo Julai 16, 2025, ili kufuatilia utekelezaji wa mifumo ya kidijitali katika sekta ya afya.

Ziara hiyo ilikuwa sehemu ya mpango wa kidijitali wa huduma za afya katika Kaunti ya Kisumu, pamoja na uzinduzi wa rasmi wa Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA).

Hatua hiyo inalenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kupitia matumizi ya teknolojia ya kisasa, huku serikali ikijitahidi kuimarisha usimamizi wa sekta ya afya kote nchini.


Familia ya Marehemu James Nayo Yataka Haki Baada ya Kuuawa Wakati wa Maandamano ya Saba SabaFamilia ya marehemu James Na...
16/07/2025

Familia ya Marehemu James Nayo Yataka Haki Baada ya Kuuawa Wakati wa Maandamano ya Saba Saba

Familia ya marehemu James Nayo, aliyeuawa kwa kupigwa risasi wakati wa maandamano ya Saba Saba wiki iliyopita mjini Naivasha, inaitaka serikali kuhakikisha haki inatendeka.

Kwa mujibu wa ripoti ya upasuaji wa mwili (postmotem), Nayo alipigwa risasi kutoka nyuma, na risasi hiyo ikapenya hadi kutoka tumboni.

Familia hiyo imesema imeachwa na majonzi makubwa na sasa inataka uchunguzi huru na wa haraka kufanyika ili waliomhusika wawajibishwe kisheria.


Wakazi wa Korompoi Wachoma Lori na Kufunga Barabara ya Namanga Baada ya Ajali ya KusikitishaWakazi wenye ghadhabu wa ene...
16/07/2025

Wakazi wa Korompoi Wachoma Lori na Kufunga Barabara ya Namanga Baada ya Ajali ya Kusikitisha

Wakazi wenye ghadhabu wa eneo la Korompoi waliwaka hasira na kulichoma lori moja, kisha wakafunga barabara kuu ya Namanga kwa zaidi ya saa tatu, baada ya ajali mbaya iliyogharimu maisha ya mama na binti yake.

Kwa mujibu wa mashuhuda, wawili hao walikuwa wakivuka barabara wakati walipogongwa na lori hilo, na kufariki dunia papo hapo. Tukio hilo lilizua taharuki kubwa, huku wakazi wakikusanyika na kuchoma lori lililosababisha ajali hiyo.

Ili kuonyesha hasira zao, wakazi waliziba barabara kwa kutumia mawe, matairi na miti, na hivyo kusababisha msongamano mkubwa wa magari katika barabara hiyo inayotumika sana na wasafiri kati ya Kenya na Tanzania.

Maafisa wa polisi walifika eneo hilo na kufanya juhudi za kutuliza hali pamoja na kurudisha usalama. Wametangaza kuwa uchunguzi wa kina umeanzishwa kubaini chanzo kamili cha ajali hiyo na kuchukua hatua stahiki dhidi ya wahusika.



Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvoro TV Business . posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvoro TV Business .:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share