Radio Mchungaji 94.5 FM.

Radio Mchungaji 94.5 FM. Radio Mchungaji is a Commercial Radio Station owned and operated by the Catholic Diocese of Maralal.
(1)

19/07/2025

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI.*

*DOMINIKA YA KUMI NA SITA KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA C.*

*JULAI 20 2025.*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANI πŸ’š*
*MATENDO YA ROZARI πŸ“Ώ: MATENDO YA UTUKUFU*

*MADA YA DOMINIKA:*

```UKARIMU NA USUKIVU WA NENO.```

*_Somo la kwanza na Injili vimehusishwa na mada ya ukarimu. Ukarimu ulio tayari na hiari ni ishara ya huduma kwa jirani zetu. Ukarimu ulioonyeshwa na Abrahamu kwa wageni wake ni mfano mzuri. Hadithi ya Martha na Maria inasisitiza kwamba huduma, hata huduma kwa Kristo, haiwezi kutenganishwa na usikivu wa Neno lake. Mtakatifu Paulo ni mfano wa huduma kwa wenzake. Hii ndio tunaweza kuchukua kutoka somo la pili._*

*ANTIFONA YA KUINGIA: Zab 54:6, 8*
_Tazama, Mungu ananisaidia, Bwana ananitegemeza mimi. Kwa moyo mkunjufu nitakutolea sadaka, nitalisifu jina lako, ee Bwana, maana ni jema._

*KOLEKTA*
```Ee Bwana, uwabariki watumishi wako, na uwaongezee kwa huruma vipaji vya neema yako, ili, wakiwa na ari katika matumaini, imani na mapendo, wadumu daima katika kuzishika kiaminifu amri zako. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...```

*SOMO LA KWANZA*
Mwanzo 18:1-10a

_Bwana, usinipite mtumishi wako._

*Somo katika kitabu cha Mwanzo*

Siku ile: Bwana alimtokea Abrahamu kwenye mwaloni wa
Mamre. Abrahamu alikuwa amekaa mlangoni pa hema yake, saa ya joto la mchana. Akainua macho, akaona watu watatu wamesimama mbele yake. Alipowaona, alipiga mbio akatoka
mlangoni pa hema, akawakaribia, akainama mpaka chini. Akasema, "Bwana wangu, k**a nimekupendeza machoni pako, usinipite mtumishi wako bila kushinda kwangu. Nitaamuru walete maji kidogo, mpate kuosha miguu, na kupumzika
chini ya mti. Nami nitaleta mkate, mpate kuburudisha moyo, halafu mtaendelea na safari yenu, iliyowafikisha karibu na mtumishi wenu." Wakasema, "Vema, fanya k**a ulivyosema!" Abrahamu akaenda kwa haraka hemani kwa Sara, akasema,
"Twaa upesi vipimo vitatu vya unga, uukande, ufanye mikate." Kisha Abrahamu akaenda mbio kwenye kundi la wanyama
wake, akachukua ndama mchanga aliye mzuri; akampa
mtumishi, naye akafanya haraka kumwandaa. Akatwaa siagi.
na maziwa, na yule ndama aliyemwandaa, akawaandikia
vyote mbele yao; yeye akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala. Halafu wakasema, "Sara, bibi yako yupo wapi?" Akajibu, "Yumo hemani." Mgeni akamwambia, "Nitarudi kwako mwaka ujao, wakati huu huu; na hapo mkeo Sara atakuwa
na mtoto wa kiume."

*Neno la Bwana.*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 15:2-3a, 3bc-4ab, 5 (K. 1a)

*K. Ee Bwana, nani atakayekaa katika hema yako?*

Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, / atendaye haki, na asemaye ukweli kutoka moyoni;
hasingizii kwa ulimi wake.
*K.*

Hamtendei mwenzake uovu, /wala hamsengenyi jirani yake;
machoni pake fisadi hudharauliwa,
Bali huwaheshimu wamchao Bwana.
*K*

Hakopeshi fedha yake kwa riba,
ala hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na kosa.
Anayefanya hayo, hatatikisika milele.
*K.*

*SOMO LA PILI*
Wakolosai 1:24-28

_Fumbo lile lililofichwa tangu milele kuwa vizazi vyote sasa lakini limefunuliwa kwa watakatifu wake._

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Wakolosai*

Ndugu zangu: Sasa nafurahi kuvumilia mateso kwa ajili yenu. Hivyo ninatimiza katika mwili wangu yaliyopungua katika
mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani Kanisa, ambalo mimi nimefanywa mtumishi wake kwa kadiri ya agizo Mungu alilonipa kwa ajili yenu, ili nilitimilize neno la Mungu, yaani
fumbo lile lililofichwa tangu milele kwa vizazi vyote. Sasa
lakini limefunuliwa kwa watakatifu wake ambao ametaka
kuwaonyesha utajiri wa utukufu wa fumbo lenyewe kati ya watu wa mataifa; yaani Kristo ndani yenu, matumaini ya utukufu. Yeye tunamhubiri sisi, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumpeleka kila mmoja angali amekamilika katika Kristo.

*Neno la Bwana.*

*SHANGILIO LA INJILI*
Tazama Luka 8:15

*Aleluya. Aleluya.*
Heri watu wenye kulisikia neno, na kulishika kwa moyo
mzuri na mwema; wakatoa mavuno kwa uvumilivu.
*Aleluya.*

*INJILI*
Luka 10:38-42

_Martha alimkaribisha. Maria amelichagua fungu lililo jema._

*Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Luka*

Wakati ule: Yesu aliingia katika kijiji kimoja; huko mwanamke, Jina lake Martha, akamkaribisha nyumbani mwake. Naye alikuwa na dada, jina lake Maria aliyeketi miguuni pa Bwana, akisikiliza
maneno yake. Lakini Martha akishughulikia utumishi mwingi,
akamwendea akasema, "Bwana., hujali kwamba dada yangu ameniacha nitumikie peke yangu? Basi, umwambie anisaidie." Bwana akajibu, akamwambia, "Martha, Martha, unajishughulisha
na kujisumbua kwa mambo mengi. Lakini kuna jambo moja tu lahitajika. Maria amelichagua fungu lililo jema, nalo
halitaondolewa kwake."

Injili ya Bwana.

13/07/2025
13/07/2025

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI*

*DOMINIKA YA KUMI NA TANO KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA C*

*JULAI 13 2025*

*RANGI YA LITURUJIA: KIJANI πŸ’š*
*MATENDO YA ROZARI πŸ“Ώ: MATENDO YA UTUKUFU*

*MADA YA DOMINIKA:*

```KURITHI UZIMA WA MILELE.```

*_Upendo wetu kwa Mungu, tunajifunza kutoka kwenye Injili ya leo, utatathminiwa kuendana na mtazamo Wetu kwa watu. Dini ya kweli ni dini ya upendo, sio ya maneno tu. Msamaria alikuwa na uwezo wa kushirikΔ± katika huruma ya Mungu kwa watu wote. Somo la kwanza linatuambia kwamba amri haziletwi kutoka nje lakini zinatoka mioyoni mwetu. Somo la pili ni sambamba na mada hii. Yesu anashika nafasi ya kwanza katika kupenda ndugu zake. Alikuwa "Msamaria" wa kwanza wa kweli._*

*ANTIFONA YA KUINGIA: Taz.Zab 17:15*
_Nikutazame uso wako katika haki, niamkapo nishibe kwa kuiona sura yako._

*KOLEKTA*
```Ee Mungu, unawaonyesha mwanga wa ukweli wako wale wanaopotea, ili waweze kurudi kwenye njia ya haki; uwawezeshe wote ambao, kwa imani wanayoungama wanahesabiwa kuwa Wakristo, wayakatae mambo yanayopingana na jina hilo, na kuyafuata yale yanayopatana nalo. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...```

*SOMO LA KWANZA*
Kumbukumbu la Torati 30:10-14

_Neno lipo karibu nawe kusudi ulitimize kwa matendo._

*Somo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati*

Musa alinena na watu akawaambia: "Itiini sauti ya Bwana Mungu wenu, na kushika amri zake na maagizo yake, yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria hii, Mrudieni Bwana Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa roho yenu
yote. Kwa maana amri hii ninayokuamuru leo haipiti nguvu zako usiiweze. Haiko angani hata useme, Nani atakayepanda kwa ajili yetu huko angani akatuletee tupate kusikia na kuitenda?" Haiko mbali ng'ambo ya bahari hata useme, Nani atakayekwenda huko ng'ambo ya bahari akatutafutie tupate kuisikia na kuitenda?" Kwa kuwa neno lipo karibu nawe, lipo kinywani mwako, lipo moyoni mwako kusudi ulitimize kwa matendo,"

*Neno la Bwana.*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
Zaburi 69:14 na l7, 30-31, 33-34, 36ab na 37 (K. 32)

*K. Enyi wanyonge, mtafuteni Mungu, na mioyo yetu itahuishwa.*

Sala yangu inakuelekea, ee Bwana,
wakati wa neema yako.
Ee Mungu, unisikilize kwa wema wako mkubwa,
kwa uaminifu wako wenye kuniokoa.
Ee Bwana, unisikilize, maana fadhili zako ni bora;
kwa wingi wa rehema zako uniangalie.
*K.*

Nami, niliye mnyonge na mgonjwa;
ee Mungu, wokovu wako unilinde,
nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,
nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
*K.*

Enyi wanyonge, tazameni, furahini;
enyi mtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe!
Maana Bwana huwasikia wahitaji,
wala hawadharau wafungwa wake.
*K.*

Maana Mungu atasalimisha Sioni,
ataijenga upya miji ya Yuda.
na wazao wa watumishi wake watairithi:
na wenye kulipenda jina lake watakaa humo.
*K.*


*SOMO LA PILI*
Wakolosai 1:15-20

_Katika yeye vitu vyote vimeumbwa._

*Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Wakolosai*

Kristo Yesu ndiye mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa maana katika yeye vitu vyote vimeumbwa vilivyomo mbinguni na duniani, vionekanavyo na
isivyoonekana, wenye enzi, wenye utawala, wenye ukuu na wenye mamlaka. Vyote vimeumbwa kwa nguvu yake yeye na kwa a ajili yake. Naye alikuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushik**ana pamoja ndani yake. Yeye mwenyewe ni kichwa cha mwili, yaani Kanisa. Yeye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili awe wa kwanza katika yote. Kwa maana Mungu alipenda utimilifu wote ukae ndani yake. Na kwa ajili yake amepatanisha naye vyote vilivyoko duniani na mbinguni, kwani ameleta amani kwa damu ya msalaba wake.

*Neno la Bwana.*

*SHANGILIO LA INJILI*
Tazama Yohane 6:63c, 68c

*Aleluya. Aleluya.*
_Maneno yako, ee Bwana, ni roho, pia ni uzima; wewe unayo maneno ya uzima wa milele._

*INJILI*
Luka 10:25-37

_Jirani yangu ni nani?_

*Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Luka*

Wakati ule: Mwanasheria mmoja alisimama amjaribu Yesu, akasema, "Mwalimu, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?" Yesu akamwambia, "Imeandikwa nini katika Sheria? Wasomaje?" Naye akajibu, "Umpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote, na jirani yako k**a unavyojipenda mwenyewe." Akamwambia, "Umejibu sawasawa; fanya hivyo na utaishi." Yeye lakini akitaka kujidai haki, akamwuliza Yesu, na jirani yangu ni nani?" Yesu akajibu akisema, "Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko akakutana na wanyang'anyi. Nao wakamvua nguo, wakamtia majeraha, wakaenda zao wakimwacha karibu ya kufa. Kwa bahati kuhani alishuka kwa njia ile, alipomwona, alipitia kando. Kadhalika Mlawi alifika mahali pale, alipomwona, akapitia kando. Lakini Msamaria mmoja alikuwa akisafiri, na alipofika mahali pale, akamwona, akashikwa na huruma. Akamkaribia, akamfunga majeraha yake, akayatia mafuta na divai. Kisha akamweka juu ya mnyama wake, akampeleka katika nyumba ya wageni,
akamwuguza. Siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba, akisema, 'Mtunze, na yote utakayotumia zaidi nitakulipa nitakaporudi. Waonaje? Katika hao watatu ni nani aliyekuwa jirani wa yule aliyeshambuliwa na wanyang'anyi?" Akajibu, Ndiye aliyemfanyia huruma." Yesu akamwambia, "Nenda, kafanye vivyo hivyo."

*Injili ya Bwana.*

ππ‘π„π€πŠπˆππ† 𝐍𝐄𝐖𝐒!𝐏𝐨𝐩𝐞 π‹πžπ¨ π„π«πžπœπ­π¬ π‚πšπ­π‘π¨π₯𝐒𝐜 πƒπ’π¨πœπžπ¬πž 𝐨𝐟 πŠπšπ©π¬πšπ›πžπ­, 𝐍𝐚𝐦𝐞𝐬 𝐁𝐒𝐬𝐑𝐨𝐩 𝐉𝐨𝐑𝐧 𝐊𝐒𝐩π₯𝐒𝐦𝐨 π‹πžπ₯𝐞𝐒 𝐚𝐬 𝐅𝐒𝐫𝐬𝐭 𝐁𝐒𝐬𝐑𝐨𝐩Pope Leo has ...
10/07/2025

ππ‘π„π€πŠπˆππ† 𝐍𝐄𝐖𝐒!

𝐏𝐨𝐩𝐞 π‹πžπ¨ π„π«πžπœπ­π¬ π‚πšπ­π‘π¨π₯𝐒𝐜 πƒπ’π¨πœπžπ¬πž 𝐨𝐟 πŠπšπ©π¬πšπ›πžπ­, 𝐍𝐚𝐦𝐞𝐬 𝐁𝐒𝐬𝐑𝐨𝐩 𝐉𝐨𝐑𝐧 𝐊𝐒𝐩π₯𝐒𝐦𝐨 π‹πžπ₯𝐞𝐒 𝐚𝐬 𝐅𝐒𝐫𝐬𝐭 𝐁𝐒𝐬𝐑𝐨𝐩

Pope Leo has officially erected a new Catholic Diocese, the Catholic Diocese of Kapsabet, making it the 28th diocese in the country. The new ecclesiastical jurisdiction has been carved out of the Catholic Diocese of Eldoret and will encompass the entire Nandi County.

The Holy Father has appointed Rt. Rev. John Kiplimo Lelei, the current Auxiliary Bishop of Eldoret, as the founding bishop of the Diocese of Kapsabet.

Radio Mchungaji, Sauti ya Nyikani.

06/07/2025

JUMAPILI YA 14 KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA.

Karibu kwenye adhimisho la Misa takatifu ikiadhimishwa naye Padre Naftali Lotukoi moja kwa moja kutoka Parokia ya Watakatifu Petro na Paulo, Maralal.

Thank you for following and supporting this live broadcast through Paybill Number:4069627 Account name: Radio Mchungaji. God bless you and have a blessed Sunday.

06/07/2025

JUMAPILI YA 14 KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA.

Karibu kwenye adhimisho la Misa takatifu ikiadhimishwa naye Padre Naftali Lotukoi moja kwa moja kutoka Parokia ya Watakatifu Petro na Paulo, Maralal.

29/06/2025

SHEREHE YA WAT. PETRO NA PAULO.

Karibu kwenye adhimisho la Misa takatifu ya Sherehe ya Wat. Petro na Paulo moja kwa moja kutoka ukumbi wa Allamano katika Parokia ya Maralal. Misa takatifu inaadhimishwa naye Askofu Hieronymus Joya IMC, Askofu wa Jimbo Katoliki la Maralal.

Paybill number: 4069627
Account name: Radio Mchungaji

28/06/2025

SHEREHE YA UPADRISHO YA MASHEMASI MICHEAL LOISIAE LEKASUYAN NA NAFTALI LOWOI LOTUKOI MOJA KWA MOJA KUTOKA PAROKIA YA WAT. PETRO NA PAULO, MARALAL IKIADHIMISHWA NAYE ASKOFU HIERONYMUS JOYA IMC, ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI LA MARALAL.

Paybill Number: 4069627
Account Name: Radio Mchungaji

28/06/2025

SHEREHE YA UPADRISHO YA MASHEMASI MICHEAL LOISIAE LEKASUYAN NA NAFTALI LOWOI LOTUKOI MOJA KWA MOJA KUTOKA PAROKIA YA WAT. PETRO NA PAULO, MARALAL IKIADHIMISHWA NAYE ASKOFU HIERONYMUS JOYA IMC, ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI LA MARALAL.

22/06/2025

SHEREHE YA BIKIRA MARIA CONSOLATA.

Karibu kwenye adhimisho la Misa takatifu ya Sherehe ya Bikira Maria Consolata, moja kwa moja kutoka Parokia ya Bikira Maria Consolata, Suguta Mar Mar.

BREAKING.21.4.2025POPE FRANCIS HAS RESTED.At 9:45 AM on Easter Monday, Cardinal Kevin Farrell, Camerlengo of the Apostol...
21/04/2025

BREAKING.

21.4.2025

POPE FRANCIS HAS RESTED.

At 9:45 AM on Easter Monday, Cardinal Kevin Farrell, Camerlengo of the Apostolic Chamber, spoke these words at the Casa Santa Marta:

"Dearest brothers and sisters, with deep sorrow I must announce the death of our Holy Father Francis. At 7:35 this morning, the Bishop of Rome, Francis, returned to the house of the Father. His entire life was dedicated to the service of the Lord and of His Church. He taught us to live the values of the Gospel with fidelity, courage, and universal love, especially in favor of the poorest and most marginalized. With immense gratitude for his example as a true disciple of the Lord Jesus, we commend the soul of Pope Francis to the infinite merciful love of the One and Triune God."

The Vatican has confirmed the death of the Holy Father, marking a moment of profound grief for the entire Catholic Church and the global community.

We ask all the faithful and people of goodwill to join in prayer for the repose of his soul. May the Lord, in His infinite mercy, grant him eternal rest and reward him for his tireless service to the Church and humanity.

Eternal rest grant unto him, O Lord, and let perpetual light shine upon him. May he rest in peace. Amen.

Vatican News

Address

Maralal

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Mchungaji 94.5 FM. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Mchungaji 94.5 FM.:

Share

Category