SIFA FM Marsabit

SIFA FM Marsabit SIFA 101.1 FM Marsabit is a radio station serving communities living in and outside Marsabit County.

WE ARE HIRING....SIFA FM MARSABIT JOB VACANCY.POST: RADIO PRESENTER/PRODUCER.SIFA FM MARSABIT is seeking to urgently fil...
04/07/2025

WE ARE HIRING....
SIFA FM MARSABIT JOB VACANCY.
POST: RADIO PRESENTER/PRODUCER.
SIFA FM MARSABIT is seeking to urgently fill the positions of Samburu presenter/producer. If you believe you have what it takes to fill the above position, you are invited to apply for the position.
Qualifications for the Radio Presenter/producer Job
• Passion for radio and production.
• Diploma or Degree or an equivalent in Mass Communication/media studies or a related discipline from a recognised institution.
• Must be innovative and creative.
• Have a good command of Samburu, Swahili and English languages. Any other native language spoken in Marsabit County will be an added advantage.
• Strong writing, editing and analytical skills
• Ability to moderate a talk show/interview.
• Ability to work extra/odd hours.
• Clear understanding of media laws and ethics
• Self-driven, assertive, punctual and organized.
• Must have a nose for news, broad and strategic thinker and pay attention to detail.
• Must demonstrate a professional approach and appearance including enthusiasm, drive, commitment, honesty, trust, and loyalty.
KEY RESPONSIBILITIES
1. Hosting a continuity radio programme.
2. Involvement in production work.
3. Team player in news and marketing department.
4. Involvement in attaining ministry’s, goals, mission and vision.
APPLICATION PROCEDURES
If you are interested and qualified, please email or send a 5-10 minutes audio recording of yourself ( A demo of continuity programme and interview you hosted),your CV, Application Letter and other relevant testimonials to [email protected] or drop a hard copy of your application at Sifa FM Marsabit studio at Bi High/Teachers Sacco Plaza, 1st floor, room no. 11 .
Address your application to Sifa FM Station manager and for Postal Address:
TO THE MANAGER,
SIFA FM MARSABIT.
PO BOX 21514-0055
NAIROBI.
Only shortlisted candidates will be contacted.
N/B: Internship and attachment vacancies available.

30/06/2025

One of the greatest transformations I experienced was in my confidence. I used to be extremely shy. I feared standing in front of people or even being seen

Sheria ya Ardhi ya mwaka 2016 ilileta mageuzi makubwa katika usimamizi wa ardhi nchini Kenya, kwa kuigawa katika makundi...
23/06/2025

Sheria ya Ardhi ya mwaka 2016 ilileta mageuzi makubwa katika usimamizi wa ardhi nchini Kenya, kwa kuigawa katika makundi matatu: ardhi ya jamii, ardhi ya binafsi, na ardhi ya umma. Licha ya mabadiliko haya, jamii nyingi bado hazijapata maarifa sahihi ya jinsi ya kusajili ardhi yao ya kijamii kisheria ili kunufaika ipasavyo.

Ili kusaidia kuziba pengo hili la uelewa, shirika la Namati liliandaa warsha maalum jijini Nairobi, likishirikiana na wanahabari na viongozi wa jamii kutoka pembe mbalimbali za nchi. Lengo ni kuimarisha uelewa na ushirikiano katika kusimamia haki za ardhi na mazingira ikiwemo miradi ya Pesa ya Hewa (Carbon credit).

“Tuliona umuhimu wa kuwaleta pamoja wanahabari na viongozi wa jamii ili kujadili namna bora ya kusimamia haki za ardhi na kuhakikisha jamii zinasikika katika miradi ya maendeleo ya mazingira.” Derrick Muhandia kutoka shirika la Namati:

JE, WAJUA?
Tangu mwaka 2013, Kenya imepokea takriban billioni 1.7 za Kenya (sawa na dola milioni 11.5 za Marekani) kupitia miradi ya uhifadhi wa mazingira wa Pesa ya Hewa (Carbon credit), fedha ambazo zimekuwa msaada mkubwa kwa jamii, hasa katika maeneo ya wafugaji.

Lakini sasa kuna changamoto kubwa:
Baada ya uamuzi wa Mahak**a ya Mazingira na Ardhi ya Isiolo tarehe 24 Januari 2025, shirika la kimataifa la Verra limesitisha malipo yote ya miradi ya carbon credit.

Viongozi wa jamii, k**a James Lengojine, anasema kuwa uamuzi huu wa kusimamisha malipo kwa jumla ni wa kudhulumu, kwani:
Si jamii zote zilizohusika katika kesi hiyo, Jamii nyingi k**a za Wamaasai, Waborana na Wasamburu tayari zilikuwa zikifaidika na malipo hayo kwa kununua mahitaji ya msingi k**a chakula, maji na elimu, Kusimamisha malipo kumevuruga maendeleo yaliyokuwa yameanza kuonekana.

Endelea kufuatilia SIFA FM Marsabit kwa taarifa zaidi kuhusu haki za ardhi, mazingira, na maendeleo ya jamii yetu.

15/06/2025

Heri ya Siku ya akinababa kwa mababa wote!
Tunapowasherehekea leo, tunakumbushwa maneno ya Mithali 20:7 – “Mwenye haki huenenda katika unyofu wake; watoto wake wamebarikiwa baada yake.”

Asanteni kwa upendo wenu, uongozi na imani. Mungu aendelee kuwatia nguvu muendelee kuwa mwanga kwa familia zenu.

BANGI KILO 350 YA THAMANI YA SHILINGI MILIONI 10.5 YANASWA KULE ELLEBOR, SOLOLO.Maafisa wa polisi wamefanikiwa kunasa ba...
02/06/2025

BANGI KILO 350 YA THAMANI YA SHILINGI MILIONI 10.5 YANASWA KULE ELLEBOR, SOLOLO.

Maafisa wa polisi wamefanikiwa kunasa bangi yenye thamani ya shilingi milioni 10.5 ikatika eneo la Ellebor, kaunti ndogo ya Sololo, gatuzi hili la Marsabit.

Bangi hiyo vifurushi 72 ilikuwa imepakiwa kwa magunia 12 yenye uzito wa takriban kilo 350, ilinaswa na polisi wa akiba NPR mwendo wa saa tisa alfajiri ya leo Jumatatu.

Bangi hiyo inaaminika ilikuwa ikisafirishwa kutoka taifa jirani la Ethiopia kwa kutumia gari aina ya Toyota Land cruiser.

Akithitibisha mkasa huo,naibu kamishna wa kaunti ndogo ya Sololo Edward Goko, amewapongeza maafisa wa NPR kwa kukabiliana na washukiwa wa ulunguzi wa miharati na kupelekea kuk**atwa kwa mmoja wao.

Kamanda wa polisi kaunti ndogo ya Sololo, Joseph Nthiga kwa upande wake amesema mshukiwa aliyek**atwa kwa sasa anapokea matibabu chini ya ulinzi mkali wa polisi na anatarajiwa kufikishwa mahak**ani pindi atakapopata nafuu.

Kwa hii sasa gari na bangi iliyonaswa inazuiliwa na maafisa wa polisi k**a ushahidi.

Naibu kamishana Goko aidha ametoa wito kwa serikali kuwaongeza maafisa wa akiba katika mpaka wa Kenya na Ethiopia ili kupiga jeki juhudi za maafisa wa polisi kukabiliana na visa vya uhalifu.

Idara ya polisi imezidisha opersheni ya kusaka walanguzi wa binadamu na mihadarati katika kaunti ya Marsabit , kwenye mpaka wa Kenya na Ethiopia kwenye oparesheni Ondoa Jangili.

Heri ya Siku ya  !Kutoka kwetu wote hapa SIFA FM Marsabit, tunasherehekea roho ya uhuru na umoja. Asanteni sana wasikili...
01/06/2025

Heri ya Siku ya !
Kutoka kwetu wote hapa SIFA FM Marsabit, tunasherehekea roho ya uhuru na umoja. Asanteni sana wasikilizaji na wadhamini wetu kwa msaada wenu wa daima. Mungu ibariki Kenya! 🇰🇪

Michael Kwoba Meneja wa Kituo, Sifa FM Marsabit

A Day of Gratitude and Testimonies!Earlier today, we were honored to welcome the Executive Director of Trans World Radio...
27/05/2025

A Day of Gratitude and Testimonies!

Earlier today, we were honored to welcome the Executive Director of Trans World Radio Kenya, Dr. Bernice Gatere, alongside the General Manager of Sifa FM Stations, Tish Munga, for a powerful moment of reflection and thanksgiving.

Listeners and pastors from across the region shared moving testimonies of how Sifa FM Marsabit and impactful programs produced by TWR K- Trans World Radio Kenya have transformed lives and strengthened faith in the community.

Sifa FM Marsabit, which began as a vision, has now served this community for over 10 years, becoming a trusted voice of hope.We are humbled to be a platform where the Word of God continues to reach hearts and change lives.

As Sifa FM Marsabit and part of the larger TWR Kenya family, we extend heartfelt thanks to the Marsabit Pastors' Fellowship and to you, our loyal listeners, for your continued support, prayers, and partnership.

WITO WA AMANI MARSABIT.Wakaazi wa kaunti hii ya Marsabit wametakiwa kudumisha amani.Aidha idara ya polisi imetakiwa kuwa...
21/05/2025

WITO WA AMANI MARSABIT.

Wakaazi wa kaunti hii ya Marsabit wametakiwa kudumisha amani.

Aidha idara ya polisi imetakiwa kuwasaka na kuwak**ata wahusika wote wa mzozo wa kijamii katika eneo la Dukana, eneo bunge la North Horr.

Uhasama huo ulipelekea mauwaji ya watu 4 na mwingine kujeruhiwa siku za hivi karibuni.

Gavana wa kaunti ya Marsabit, Mohamud Ali amepongeza wakaazi wa kaunti hii kwa kudumisha amani tangu ghasia mbaya zaidi kuwahi shuhudiwa jimboni wakati wa kipindi cha mwaka 2021-2022.
Kamishna wa kaunti ya Marsabit, James Kamau upande wake amewahakikishia raia kuwa wahusika wote wa mauwaji watachukuliwa hatua za kisheria.

Amesema usalama umeimarisha eneo hilo huku akionya wanasiasa na wachochezi kwamba watakabiliwa vikali.

KAUNTI YA MARSABIT INA UWEZO NA FURSA KUBWA YA UWEKEZAJI, ASEMA GAVANA ALI.Gavana wa kaunti ya Marsabit, Mohammed Mohamu...
21/05/2025

KAUNTI YA MARSABIT INA UWEZO NA FURSA KUBWA YA UWEKEZAJI, ASEMA GAVANA ALI.

Gavana wa kaunti ya Marsabit, Mohammed Mohamud Ali amesema kaunti hii ya Marsabit inajivunia raslimali nyingi na fursa kubwa za uwekezaji.

Akizungumza kwenye maonyesho ya kibiashara, Marsabit county trade fair and Exhibition hapa mjini Marsabit gavana Ali amesema gatuzi hili linamiliki mali na asili ya kiwango kikubwa ikiwemo madini k**a dhahabu na upepo unaotumika na kampuni kubwa zaidi Barani Afrika kuzalisha kawi kwa kutumia upepo.

Hata hivyo kiongozi wa kaunti amehoji kuwa idadi kubwa ya watu wanadhana potovu kuhusu uwezo wa eneo hili la Kaskazini mwa Kenya.

Gavana Ali aidha amesema kaunti hii ya Marsabit inauwezo mkubwa wa kuzalisha chakula cha kulisha taifa hili kutokana na ukubwa na rotuba nzuri ya ardhi yake iwapo mabwawa ya kunyunyizia maji yatachimbwa.

Kiongozi wa kaunti pia amewaarifu wakaazi wa kaunti ya Marsabit kwamba serikali kuu inatarajia kukamilisha ujenzi wa uwanja wa michezo wa Marsabit chini ya miezi mitatu ijayo.

Kuhusu ombi la wafanyibiashara wa miraa kutengewa mahali pa kufanyia biashara , gavana Ali amesema vibanda vitajengwa nyuma ya uwanja wa michezo ili biashara hizo ziendelezwe eneo hilo.

Wakati uo huo, gavana Ali amewahakikishia wanaofaidika na ufadhili wa masomo kupitia Marsabit County scholarship fund kwamba wanatarajia kupokea ufadhili huo kuanzia wiki ijayo baada ya magavana kutia saini mwafaka.

WAKAAZI WA DAKABARICHA WANDELEA KUUMIA KUTOKANA NA KUFUNGWA KWA ZAHANATI ENEO HILO, HUKU GAVANA ALI AKIAHIDI MALIPO KWA ...
21/05/2025

WAKAAZI WA DAKABARICHA WANDELEA KUUMIA KUTOKANA NA KUFUNGWA KWA ZAHANATI ENEO HILO, HUKU GAVANA ALI AKIAHIDI MALIPO KWA MMLIKI WA ARDHI HIYO.

Kutokana na kufungwa kwa zahanati ya Dakabaricha, eneo bunge la Saku, kaunti ya Marsabit kutokana na utata wa umiliki wa ardhi, serikali ya kaunti ya Marsabit imesema kuwa iko tayari kutafuta mwafaka ili zahanati hiyo kufunguliwa.

Hii ni baada ya wenyeji na wakaazi wa eneo hilo kulalama kukosa huduma za afya kutokana na zahanati hiyo ya serikali ya kaunti kufungwa.

Mmiliki wa ardhi alifunga zahanati hiyo kwa madai kuwa serikali ya kaunti ilikuwa imefeli kumlipa ada ya kununua ardhi hiyo.

Hata hivyo gavana wa kaunti ya Marsabit amewahahakishia wananchi kuwa fedha zimetengwa katika bajeti ya kipindi cha kifedha mwaka 2025-2026 kwa minajili ya malipo ya ada ya ardhi hiyo.

Amemtaka mmiliki wa ardhi hiyo kuruhusu raia kupokea matibabu huku serikali ikiwema mipango ya kulipa pesa ifikapo mwezi Juni mwaka huu.

Hapo awali mmiliki wa ardhi hiyo, mwalimu Jarso Dube Godana alidai kuwa serikali ya kaunti ilikuwa imefeli kumlipa pesa kwa muda wa miaka kumi iliyopita.

Jarso alidai kuwa aliamua kufunga zahanati hiyo kutokana na serikali ya kaunti kutompa sikio wala kutekeleza ahadi ya kulipa ada ya kununua ardhi hiyo miaka kumi iliyopita sasa.

Mwakilishi wa wadi ya Marsabit ya kati, Jack Elisha alikuwa ametoa wito kwa serikali ya kaunti kuingilia kati swala hilo ili wananchi kupokea huduma za matibabu.

WACHOCHEZI NA WAHUSIKA WA UHASAMA WA KIJAMII DUKANA WAONYWA, HUKU WATU 26 WAKICHUNGUZWA.Washukiwa 26 ikiwemo wanasiasa w...
19/05/2025

WACHOCHEZI NA WAHUSIKA WA UHASAMA WA KIJAMII DUKANA WAONYWA, HUKU WATU 26 WAKICHUNGUZWA.

Washukiwa 26 ikiwemo wanasiasa wanachunguzwa kuhusiana na mzozo wa kijamii ambao umesababisha mauwaji ya watu 4 na mwingine kujeruhiwa eneo la Dukana, kaanti ya Marsabit.

Vyombo vya usalama vimeonya kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.

Kamishna wa kaunti ya Marsabit, James Kamau amewataka wote wanaliotajwa kwa kuhusishwa na mzozo huo kuandikisha taarifa kwa idara ya upepelezi.

Wanasiasa aidha wameonywa dhidi ya kujihusisha na visa vya uchochezi badala yake wahusike katika mikakati ya kurejesha hali ya kawaida na amani.

Jamii husika pia zimeonywa dhidi ya kuchukulia hatua za kisheria mikononi mwao.

Serikali ya kaunti kwa upande wake imezitaka jamii zinazozozana kuruhusu mazungumzo ya kuleta amani, uwiyano na utangamano.

Waziri wa utawala na amani kaunti ya Marsabit, Amina Chala amewataka raia kuwa na subra wakati asasi za serikali zinaendelea na uchunguzi kuhusu waliotekeleza mauwaji hayo.

Ni kauli ambayo imekariiriwa na mwanachama wa k**ati ya amani jimboni Nuria Gollo.

Serikali ya kaunti ya Marsabit aidha inashirikiana na wadau wengine ili kutoa msaada kwa kibinadamu kwa wathiriwa.

Wakati uo huo viongozi wa kaunti hii wametakiwa kushikana mikono ili kuhakikisha hali ya kawaida na amani inarejea jimboni.

MZOZO WA KIJAMII DUKANA, WATU WANNE WATHIBITISHWA KUUWAWA.Watu wanne wamethibitishwa kuuwawa na mwingine mmoja kujeruhiw...
19/05/2025

MZOZO WA KIJAMII DUKANA, WATU WANNE WATHIBITISHWA KUUWAWA.

Watu wanne wamethibitishwa kuuwawa na mwingine mmoja kujeruhiwa kutokana na mzozo wa kijamii katika eneo la Dukana, eneo bunge la Horr Kaskazini, gatuzi la Marsabit.

Nyumba kadhaa za jamii zinazozozana zimeteketezwa kwa moto na kupelea waathiriwa kukimbilia usalama wao katika kituo cha polisi cha Dukana.

Akithibitisha mkasa huo, kamishna wa kaunti ya Marsabit, James Kamau amesema mzozo huo umesababishwa na mauwaji ya wanaume wawili na watu wasiojulikana siku mbili zilizopita.

Katika mkasa wa kwanza, kamishna Kamau amesema miili ya vijana wawili ilipatikana katika eneo la Qorqa, kule North Horr kabla ya mkasa wa pili wa ulipizaji kisasia katika eneo la Dukana uliopelekea mauwaji ya watu wengine wawili.

Aidha mama mmoja mjamzito pia aliftyuliwa risasi na kujeruhiwa vibaya kutoka na mzozo huo.

Kwa upende wake, naibu mwenyekiti wa k**ati ya amani kaunti ya Marsabit, Adan chukulisa amelaani mauwaji hayo huku akitaka wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.

Naibu kamishna wa kaunti ndogo ya Dukana, Peter Kimani amesema mikakati imeweka ili kurejesha hali ya amani na usalama katika eneo hilo.

Aidha k**ati ya usalama kaunti ya Marsabit na Dukana imewahakikishia wananchi kuwa maafisa wa kutosha wa polisi wametumwa katika eneo la mkasa.

Wananchi pia wametakiwa kujiepusha na uvumi ambao huenda ukasababisha hofu zaidi.

Mauwaji na uhasama huo umejiri siku chache baada ya waziri wa usalama wa ndani, Kipchumba Murkomen kuzuru kaunti ya Marsabit wiki jana kwa ziara ya kiusalama.

Address

Mosque Road
Marsabit
60500

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SIFA FM Marsabit posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SIFA FM Marsabit:

Share