03/06/2026
KWS YAWAONDOA NYATI WALIOVAMIA ENEO LA HULAHULA NA KUZUA TAHARUKI.
Kufuatia taharuki iliyotokana na uvamizi wa nyati katika eneo la Hulahula, kaunti ndogo ya Marsabit ya kati, gatuzi la Marsabit, idara ya kulinda wanyama pori nchini KWS imewahakikishia wananchi kuwa hali hiyo imethibitiwa.
Hii ni baada ya kundi la nyati kuvamia eneo hilo hapo jana na juzi usiku.
Akizungumza afisini mwake, Naibu mkurugezi mkuu wa hifadhi ya wanyamapori eneo la Kaskazini mwa Kenya, Bakari Chongwa, amewahakikishia wakaazi wa eneo hilo kwamba tayari maafisa wa kulinda wanyamapori wamefanikiwa kuwarudisha nyati hao kwenye
Hata hivyo Bakari ametoa wito kwa wananchi kujiepusha na hatua zinazopelekea uharibifu wa ua la mbuga haswa kwa kuingiza mifugo wao mbugani.