SIFA FM Marsabit

SIFA FM Marsabit SIFA 101.1 FM Marsabit is a radio station serving communities living in and outside Marsabit County.

03/06/2026

KWS YAWAONDOA NYATI WALIOVAMIA ENEO LA HULAHULA NA KUZUA TAHARUKI.

Kufuatia taharuki iliyotokana na uvamizi wa nyati katika eneo la Hulahula, kaunti ndogo ya Marsabit ya kati, gatuzi la Marsabit, idara ya kulinda wanyama pori nchini KWS imewahakikishia wananchi kuwa hali hiyo imethibitiwa.

Hii ni baada ya kundi la nyati kuvamia eneo hilo hapo jana na juzi usiku.

Akizungumza afisini mwake, Naibu mkurugezi mkuu wa hifadhi ya wanyamapori eneo la Kaskazini mwa Kenya, Bakari Chongwa, amewahakikishia wakaazi wa eneo hilo kwamba tayari maafisa wa kulinda wanyamapori wamefanikiwa kuwarudisha nyati hao kwenye

Hata hivyo Bakari ametoa wito kwa wananchi kujiepusha na hatua zinazopelekea uharibifu wa ua la mbuga haswa kwa kuingiza mifugo wao mbugani.

MWANAUME ASHTAKIWA KATIKA MAHAKAMA YA MARSABIT KWA WIZI WA KIMABAVU. Mwanaume mmoja amefikishwa katika mahakama ya Marsa...
03/06/2026

MWANAUME ASHTAKIWA KATIKA MAHAKAMA YA MARSABIT KWA WIZI WA KIMABAVU.

Mwanaume mmoja amefikishwa katika mahakama ya Marsabit kwa shtaka la wizi wa kimabavu.

Feisal Gollo mwenye umri wa miaka 31 anakabiliwa na shtaka la kumuibia kimabavu, Abdi Nuno, Simu ya rununu yenye thamani ya shilingi alfu 24,339,charger yake pamoja na shilingi alfu moja mia tano pesa taslimu.

Mkasa huo ulitokea Mei, 23 mwaka huu wa 2026 katika lokesheni ya Mountain, kaunti ndogo ya Marsabit Central, gatuzi la Marsabit, majira ya saa tatu usiku.

Hata hivyo, akifika mbele ya hakimu mkaazi wa mahakama ya Marsabit, Edward Oboge, mshukiwa Gollo amekanusha shtaka dhidi yake.

Mahakama inasubiri ripoti ya idara ya probation kabla ya kutoa uamzi kuhusu ombi la kuachiliwa kwa bondi kwa mshukiwa huyo.

Kesi hiyo itatajwa June, 16 mwaka huu wa 2026.

Africa Challenge is now LIVE!Join the conversation as we discuss the Climate Crisis & Solutions and explore how climate ...
03/06/2026

Africa Challenge is now LIVE!

Join the conversation as we discuss the Climate Crisis & Solutions and explore how climate change is impacting our lives, communities, and relationships.

Tune in now and share your thoughts.

https://youtu.be/czg_gpGPfKI

Join Lina Mwamachi and Immanuel Mwakori as they discuss Climate cha...

MULTI-AGENCY TEAM RECOVERS STOLEN LIVESTOCK IN MARSABIT COUNTY.A multi-agency security team has successfully recovered 2...
02/06/2026

MULTI-AGENCY TEAM RECOVERS STOLEN LIVESTOCK IN MARSABIT COUNTY.

A multi-agency security team has successfully recovered 251 sheep and goats that had been stolen by suspected bandits in Loiyangalani Sub-County.

As the pursuit intensified, the officers tracked the stolen animals to the Lokilipi and Sarima areas, where they encountered armed bandits, leading to a confrontation marked by an exchange of gunfire. This forced the suspects to abandon the livestock and flee.
The 251 animals have been placed under police custody pending identification, verification, and eventual handover to their rightful owners.

This successful operation serves as yet another demonstration of the National Police Service's continued crackdown on banditry and stock theft, reaffirming its commitment to restoring security and protecting life and property.

Source: National Police Service

01/06/2026

AHADI KOCHOKOCHO: Miradi ya serikali ya kitaifa ikiwemo kukamilisha kwa ujenzi wa barabara ya North Horr- Maikona, ujenzi wa barabara ya Bank Quarters-Badassa-Songa, barabara ya Odha-Ganaba, Makao kwa wakimbizi wa ndani kwa ndani wa Saku, ujenzi wa uwanja wa ndege, ununuzi wa Feri itakayohudumu kwenye ziwa Turkana, ujenzi wa shule eneo la Dasnach na Ell-Molo Bay, ni miongoni tu mwa ahadi za rais William Ruto kwa wakaazi wa Marsabit kupitia hotuba ya Gavana Mohamud Mohammed Ali wakati wa sherehe za Madaraka mjini Marsabit.

01/06/2026

Gavana wa Marsabit, Mohamud Mohhmed Ali akielezea kuhusu ugatuzi ilivyopiga jeki miradi ya maendeleo Kaskazini mwa Kenya wakati wa sherehe za 63 za Madaraka, mjini Marsabit.

UFANISI WA UGATUZI NA HATUA ZILIZOPIGWA KIMAENDELEO UKANDA WA KASKAZINI MWA KENYA ZASHEHENI HOTUBA ZA VIONGOZI KWENYE SH...
01/06/2026

UFANISI WA UGATUZI NA HATUA ZILIZOPIGWA KIMAENDELEO UKANDA WA KASKAZINI MWA KENYA ZASHEHENI HOTUBA ZA VIONGOZI KWENYE SHEREHE ZA MADARAKA MARSABIT.

Ugatuzi umefanikisha pakubwa ujio wa maendeleo katika maeneo kame na nusu kame yaliyokuwa yametengwa na kusalia nyuma kimaendeleao.

Ndio kauli za baadhi ya viongozi katika eneo la Kaskazini mwa Kenya.

Akihutubia wananchi katika maandimisho ya sherere za 63 za siku kuu ya Madaraka katika uwanja wa michezo wa Marsabit, gavana Mohammud Mohammed Ali amesifia ugatuzi na utawala wa sasa katika hatua kubwa zilizopipwa kwa miradi ya maendeleo eneo kame alaamrufu ASAL.

Gavana Ali pia amepigia debe miradi ya maendeleao inayotekelezwa na serikali ya kitaifa katika kaunti ya Marsabit.

Kwenye sherehe hiyo iliyoongozwa na kamishna wa kaunti ya Marsabit Stanely Kamand na gavana Mohamud Mohammed Ali viongozi hao wamepigia upato miradi tofauti ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya kitaifa.

Gavana Ali amesema rais William Ruto ameamrisha kuharakishwa kwa ujenzi wa barabara ya North Horr- Maikona.
Pia amesema serikali kuu inanua kujenga barabara ya kutoka Bank Quarters kupitia Badassa hadi Songakwa kuweka lami ili kurahisisha usafiri na kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikishuhudiwa katika barabara hiyo.

Amebaini kuwa miongoni mwa barabara zingine zitakazo pigwa lami ni ya kutoka Odha hadi Ganaba.

Kiongozi wa kaunti amefichua kuwa rais Ruto ameamrisha ununuzi wa feri ili kurahisisha usafiri kati ya majimbo ya Marsabit na Turkana kupitia ziwa Turkana huku akiahidi shilingi milioni 50 kwa ujenzi wa shule eneo la Dasnach na Ell-Molo.

Kuhusu swala la kuwapa makao wakimbizi wa ndani kwa ndani, gavana Ali amesema serikali ya Rais William Ruto imeahidi kuwapa makao wakimbizi wa ndani kwa ndani katika eneo bunge la Saku.
Amesema serikali imetenga kima cha shilingi milioni 100 kwa shughuli hiyo, sawa na ujenzi wa uwanja wa ndege.

Ametangaza kuwa rais Ruto anatazamiwa kuzuru kaunti hii mwezi ujao wa Julai mwaka huu.

Kuhusu utata wa umiliki wa maeneo ya Titu na Basir, gavana Ali amewahakikishia wakaazi wa Marsabit kuwa swala hili tayari limetatuliwa na sehemu hizo kutambulika kuwa kwenye himaya ya kaunti ya Marsabit.

Ameongeza kuwa serikali kuu itaifanya Basir kuwa lokesheni na viongonzi wa utawala kutumwa eneo hilo.

Apart from weather changes, how has climate change affected life and relationships in your community?Join us on this wee...
01/06/2026

Apart from weather changes, how has climate change affected life and relationships in your community?

Join us on this week’s Africa Challenge as we discuss the climate crisis, its impact on society, and practical solutions for a more resilient future.

Share your thoughts in the comments and be part of the conversation.

Tunapoadhimisha siku hii muhimu katika historia ya taifa letu, tunajivunia hatua kubwa ambazo Kenya imepiga katika kujen...
01/06/2026

Tunapoadhimisha siku hii muhimu katika historia ya taifa letu, tunajivunia hatua kubwa ambazo Kenya imepiga katika kujenga umoja, maendeleo na matumaini kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Sifa FM Stations tunawatakia Wakenya wote Siku njema ya Madaraka iliyojaa amani, furaha na baraka tele.

Mungu Ibariki Kenya.

29/05/2026

Jumatano hii kwenye Africa Challenge tutajadili Mazingira na Hatua za Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi. Tutachunguza umuhimu wa kulinda mazingira yetu na uhitaji wa haraka wa kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. Kipindi hiki kitaangazia changamoto kuu za kimataifa na za ndani zinazoathiri mifumo ya ikolojia, jamii, na vizazi vijavyo.

📻 Sikiliza kupitia: 107.7 Voi | 101.1 Marsabit / Kakuma / Garissa / Tana River / Lamu | 101.9 Lodwar | 101.7 Wajir | 100.7 Mandera

Address

Mosque Road
Marsabit
60500

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SIFA FM Marsabit posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SIFA FM Marsabit:

Share