SIFA FM Marsabit

SIFA FM Marsabit SIFA 101.1 FM Marsabit is a radio station serving communities living in and outside Marsabit County.

Kaunti ya Marsabit imesajili idadi ndogo sana ya wapigaji kura wapya kufikia sasa tangu zoezi hili lilipoanza mwezi mmoj...
30/10/2025

Kaunti ya Marsabit imesajili idadi ndogo sana ya wapigaji kura wapya kufikia sasa tangu zoezi hili lilipoanza mwezi mmoja uliopita.

Kufikia sasa ni wapigaji kura wapya 274 pekee wamesajiliwa.

Msimamizi wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kaunti ya Marsabit, Sanchan Lokadio amesema tume hiyo inanuia kusajili wapigaji kura wapya alfu 40 ili idadi ya wapigaji kura jimboni kuwa alfu mia mbili kufikia mwaka wa 2027.

Kaunti ya Marsabit ina jumla ya wapigaji kura 166,000 waliosajiliwa.

Lokadio anahoji kuwa changamoto kubwa wanayoshuhudia ni kwamba zoezi la usajili linafanyika mijini katika afisi za IEBC ili hali idadi kubwa ya wananchi wanapatikana sehemu za mashinani.

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi waliona vitambulisho kujitokeza kwa wingi ili kusajiliwa.

Meneja huyo wa IEBC Marsabit pia amewahamasisha wale wanataka kubadilisha vituo vyao vya kupiga kura kufanya hivyo katika afisi za IEBC katika maeneo bunge yote 4 ya kaunti hii ya Marsabit.

Mapema mwezi huu, naibu gavana wa Marsabit, Solomon Gubo na viongozi wengine walitoa wito kwa tume ya IEBC kuelekea maeneo ya mashinani ili kusajili wapigaji wapya badala ya kuendesha zoezi hilo katika afisi zao mijini.

30/10/2025

HUDUMA ZA AFYA MARSABIT ZAENDELEA KUATHIRIKA, WANAHARAKATI WAKITAHA HATUA ZA DHARURA KUCHUKULIWA KUSITISHA MGOMO WA MAAFISA WA KLINIKI.

Lalama zinaendelea kutolewa kuhusiana na ukosefu wa huduma muhimu za afya kwa wagonjwa wakati huu ambapo maafisa wa kliniki wanaendelea na mgomo katika kaunti hii ya Marsabit.

Watatezi wa haki za binadamu wanataka hatua za dharura kuchukuliwa ili kusitisha mgomo huo.

Akizungumza na vyombo vya habari hapa mjini Marsabit, mwasisi na pia mratibu wa shirika la kutetea haki za binadamu, Centre For Research Rights & Development, Mohammed Hassan ameelezea hofu ya wagonjwa kukosa huduma kutokana na mgomo huo ambao sasa umedumu mwezi mmoja.

Mwanaharakati huyo analalama kuwa serikali ya kaunti imefeli kutekeleza matakwa ya wahudumu hao wa afya licha ya kutia saini mkataba wa maelewana.

Aidha kuna hofu kuwa huenda hali ikawa mbaya zaidi iwapo madaktari wataungana na maafisa hao wa kliniki kwa mgomo.

Hii ni baada ya madktari kutoa makataa ya siku 21 matakwa yao kutekelezwa la sivyo wataanza rasmi mgomo wao.

MVUA KUBWA YATATIZA USAFIRISHAJI WA MTIHANI WA KPSEA NA KJSEA KATIKA BAADHI YA MAENEO KAUNTI YA MARSABIT.Shughuli za mit...
29/10/2025

MVUA KUBWA YATATIZA USAFIRISHAJI WA MTIHANI WA KPSEA NA KJSEA KATIKA BAADHI YA MAENEO KAUNTI YA MARSABIT.

Shughuli za mitihani ya kitaifa ya gredi ya sita na tisa zinaendelea vyema katika kaunti hii ya Marsabit.

Hata hivyo mvua kubwa ambayo imeshuhudiwa katika baadhi ya maeneo imesababisha mafuriko ya mito na kutatiza usafirishaji wa makaratasi ya mitihani katika baadhi ya maeneo.

Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika ni pamoja na Laisamis, Songa, Shurr na North Horr.

Mkurugezi wa elimu kaunti ya Marsabit Peter Magiri, amefichua kuwa makaratasi ya mtihani yalichelewa kufika katika shule ya msingi ya Shurr hadi majira ya saa tatu asubuhi kutokana na changamoto hiyo.

Hata hivyo Magiri amewahakikishia watahiniwa kuwa baraza la mitihani nchini KNEC linatumia ndege ya helkopa kusafirisha makaratasi ya mitihani katika maeneo yanayokumbana na changamoto ya usafiri kutokasna na athari ya mvua.

Watahiniwa 8,514 wanashiriki mtihani wa KPSEA katika vituo 206 vya mtihani kote jimboni.

Aidha watahiniwa 6,325 wa gredi ya tisa wanafanyai mtihani wa KJSEA katika vituo 168 vya mtihani.

WITO WATOLEWA KUZIBA MIANYA YA DHULMA ZA WATOTO MSIMU HUU WA LIKIZO NDEFU. Machifu, wazazi, walezi na wadau mbali mbali ...
29/10/2025

WITO WATOLEWA KUZIBA MIANYA YA DHULMA ZA WATOTO MSIMU HUU WA LIKIZO NDEFU.

Machifu, wazazi, walezi na wadau mbali mbali wametakiwa kuwa wangalifu ili kulinda maslahi ya watoto wakati huu wa likizo ndefu ya Desemba na mwaka mpya.

Hii ni kutokana na hofu ya kuongezeka kwa visa vya dhulma dhidi ya watoto haswa ndoa za mapema iwapo hatua za dharura hazitachukuliwa.

Mkurugezi wa elimu kaunti ya Marsabit, Peter Magiri amewapa changamoto wadau wote kushirikiana katika kutunza na kulinda maslahi ya watoto.

Ni kauli ambayo imekaririwa afisa wa kulinda maslahi ya watoto katika shirika la SIF, Charles Nyakundi ambaye ameomba ushirikiano kati ya wadau mbali mbali kuzuia na kuripoti visa vya dhulma za watoto.

Nyakundi ameongezea kwa kuelezea jinsi sera ya kulinda haki za watoto itasaisia pakubwa kukabiliana na changamoto hiyo.

SEKTA YA WATOTO YAPIGWA JEKI KWA UZINDUZI WA SERA YA KULINDA MASLAHI YAO GATUZI LA MARSABIT.Shirika lisilolakiserikali l...
29/10/2025

SEKTA YA WATOTO YAPIGWA JEKI KWA UZINDUZI WA SERA YA KULINDA MASLAHI YAO GATUZI LA MARSABIT.

Shirika lisilolakiserikali la SIF kwa ushirikiano na wadau wengine limezindua sera ya kulinda maslahi na haki ya watoto.

Uzinduzi wa sera hiyo almarufu Child safeguarding policy umefanyika hapa mjini Marsabit na kushirikisha wadau wa sekta mbali mbali ikiwemo idara ya elimu, walimu, maafisa wa utawala, miongoni tu mwa watetezi wa haki na maslahi ya watoto jimboni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa sera hiyo afisa wa kulinda maslahi ya watoto katika shirika hilo, Charles Nyakundi amesema mwongozo hu utawasaidia watoto na washikadau kutambua jinsi ya kuripoti visa vya dhulma dhidi ya mtoto.

Naye mkurugezi wa elimu kaunti ya Marsabit, Peter Magiri amepongeza hatua hiyo akisema itasaidia kuziba pengo kubwa lilopo katika kuripoti na kushughulikia masilahi ya watoto.

Kwa hii sasa shirika la SIF linawafadhili watoto 200 mayatima kujikimu kimaisha na kuendelea na masomo yao katika maeneo bunge ya Saku na Laisamis.

Kutokna na hitaji kubwa la watoto mayatima na wanaotoka katika mazingira magumu jimboni, mkurugezi wa elimu Marsabit, ametoa wito kwa shirika hilo kupanua mradi wake hadi maeneo mengine ya kaunti haswa katika maeneo ya mashinani.

Ni ombi ambalo limeridhiwa na afisa wa kulinda maslahi ya watoto katika shirika hilo, Charles Nyakundi.

Asante kwa kuendelea kutusikiza.Ili kutangaza nasi biashara, wasiliana kupitia nambari : +254 110267885
27/10/2025

Asante kwa kuendelea kutusikiza.

Ili kutangaza nasi biashara, wasiliana kupitia nambari : +254 110267885

MTIHANI WA KPSEA NA KJSEA WAANZA VYEMA KAUNTI YA MARSABIT.Mtihani wa gredi ya tisa KJSEA na ule wa gredi ya sita KPSEA k...
27/10/2025

MTIHANI WA KPSEA NA KJSEA WAANZA VYEMA KAUNTI YA MARSABIT.

Mtihani wa gredi ya tisa KJSEA na ule wa gredi ya sita KPSEA katika kaunti hii ya Marsabit umeanza vyema mapama leo.

Mkurugezi wa elimu kaunti ya Marsabit Peter Magiri amesema Baraza la mtihani nchini KNEC limeweka mikakati kabambe kuhakikisha mtihani huo unafanyika bila matatizo.

Amebaini kuwa kutokana upana wa kaunti hii, baraza la mitihani nchini limetuma ndege ya helkpta inayotumika kusafirisha makaratasi ya mtihani katika maeneo ya mbali k**a vile Illeret na Dukana.

Magiri aidha ameonya wakuu wa shule pamoja na wasimizi wa mitihani hiyo dhidi ya kuhusika na visa vya udanganyifu.

Ni swala ambalo limeongezewa sauti na kamishna wa kaunti ya Marsabit, James Kamau ambaye pia amewahakikishia usalama watahiniwa na wasimamizi wa mitihani.

Kaunti ya Marsabit ina watahiniwa 8,514 waliosajiliwa kufanya mtihani wa KPSEA katika vituo 206 vya mtihani kote jimboni.

Aidha watahiniwa 6,325 wa gredi ya tisa wanashiriki mtihani wa KJSEA katika vituo 168 vya mtihani kote jimboni.

Wakati uo huo, mtihani wa kitaifa KCSE practical unaendelea vyema katika vituo 51 kote jimboni.

Jumla ya watahiniwa 4,126 wamesajiliwa kushiriki mtihani huo mwaka huu katika kaunti hii ya Marsabit.

Wito umetolewa kwa serikali ya kitaifa na zile za kaunti kutekeleza usajili wa jumla wa watu wanaoishi na ulemavu katika...
25/10/2025

Wito umetolewa kwa serikali ya kitaifa na zile za kaunti kutekeleza usajili wa jumla wa watu wanaoishi na ulemavu katika hatua ya kukabiliana na changamoto wanazokumbanazo watu hao kupokea hudumu muhimu nchini.

Watu wanaoshi na ulemavu haswa vijana katika kaunti ya Marsabit wamelalama kuwa wanakumbana na changamoto chungu nzima wakati wa kusajiliwa hali inayowaathi kupokea huduma za serikali.

Wakizungumza hapa mjini Marsabit, vijana hao wametaka data au takwimu kamili ya watu waoishi na ulemavu kutambuliwa na aina ya ulemavu wao.

John Boru Galgallo ni mkaazi wa Marsabit anayeishi na ulemavu.

Miongoni mwa changamoto wanazokumbana nazo kusajiliwa ni pamoja na ukosefu wa vifaa na wataalamu wa kuchunguza aina ya ulemavu wanaokumbana nao pamoja na ukosefu wa ufahamu kuhusu umuhimu wa zoezi hilo.

Aidha mwakilishi wa vijana wanaoshi na ulemavu hapa mjini Marsabit, Robata Kuro amelalama kuhusu idadi kubwa ya vijana walioachwa nje katika mpango wa inua jamii.

Hata hivyo afisa wa idara ya maendeleo ya jamii kaunti ya Marsabit, Aila Habiba amekiri kwamba idadi ndogo sana ya watu wanaoishi na ulemavu walipokea fedha kwenye mpango wa inua jamii jimboni.

Wakati uo huo watu wanaoshi na ulemavu wanataka haki zao kuzingatiwa pamoja na kukabiliana na unyanyapaa.

Halima Osman na John Boru Galgallo ni vijana wanaoshi na ulemavu hapa mjini Marsabit.

KNCHR IKISHIRIKIANA NA WADAU MARSABIT, WAWEKA MIKATI YA KUKABILIANA NA FGM NA DHULMA ZINGINE ZA JINSIA WAKATI HUU WA LIK...
24/10/2025

KNCHR IKISHIRIKIANA NA WADAU MARSABIT, WAWEKA MIKATI YA KUKABILIANA NA FGM NA DHULMA ZINGINE ZA JINSIA WAKATI HUU WA LIKIZO NDEFU.

Mikakati kabambe imeweka kukabiliana na visa vya ukeketaji na ndoa za mapema katika kaunti ya Marsabit wakati huu ambapo shule zinamefungwa kwa likizo ndefu ya muhula tatu.

Wadau wa kukabiliana ukeketaji wakiongozwa na Tume ya kitaifa ya haki za kibinadamu nchini-KNCHR wamebaini kuwa visa vya ukeketaji katika kaunti ya Marsabit vingali vya kiwango cha juu ikiwa ni asilimia 86.

Akizungmza hapa mjini Marsabit, mratibu wa tume ya kitaifa ya haki za Kibinadamu ukanda wa Kaskazini mwa Kenya, Hassan Abdi Omar amefichua kuwa mila na tamaduni pamoja na itikadi za kidini ni miongoni tu mwa maswala makuu yanayochochea ukeketaji na ndoa za mapema miongoni mwa jamii ya Marsabit.

Aidha watu wanaoishi na ulemavu ni miongoni mwa wathiriwa walio katika hatari na madhara makuu ya ukeketaji kaunti ya Marsabit k**a anavyoelezea mwakilishi wa vijana wanaoshi na ulemavu Marsabit na pia mwasisi wa shirika la Connect us to Network, Halima Osman.

Wadau wameafikiana kushirikiana katika uhamasisho wa kukabiliana na dhulma dhidi ya wasichana haswa wakati huu wa likizo ndefu.

Rafaela Matacho ni chifu wa Hula Hula, eneo bunge la Saku kaunti ya Marsabit.

Afisa huyo wa serikali ya utawala amesema akina mama na jamii kwa jumla watakuwa mstari wa mbele katika kukabiliana na dhulma za jinsia kutokana na madhara yake.

Kwa upande wake afisa wa idara ya maendeleo ya jamii, Ailo Habiba amesema wataziba mianya iliyopo ikiwemo visa vya wakaazi wa kaunti hii huvuka mpaka hadi taifa jirani la Ethiopia au kutekeleza ukaketaji kisiri ili kuepuka mkono mrefu wa sheria.

Habiba amesema uhamasisho unaendelea katika jamii kukabiliana na mbinu tofauti zinazotumika kuendeleza dhulma dhidi ya wasichana ikiwemo utekelezaji wa sheria.

HOFU YA ONGEZEKO LA VISA VYA UGONJWA WA SARATANI YA KOO NA TUMBO KARGI.Wakazi wa Kargi, eneo bunge la Laisamis kaunti ya...
24/10/2025

HOFU YA ONGEZEKO LA VISA VYA UGONJWA WA SARATANI YA KOO NA TUMBO KARGI.

Wakazi wa Kargi, eneo bunge la Laisamis kaunti ya Marsabit wanahofia kuhusiana na ongezeko la visa vya ugonjwa wa saratani ya koo na tumbo.

Wakaazi hao wanahofia huenda maradhi hayo yanatokana na vifaa au kemikali ambazo zilizikwa ardhini eneo hilo miaka ya zamani wakati wa uchunguzi wa kutafuta madini k**a vile mafuta.

Wakiwasilisha lalama zao kwa k**ati ya tume ya kitaifa ya ardhi nchini inayochunguza dhulma za kihistoria za ardhi, wakaazi hao wanataka uchunguzi kutekeleza ili kubaini kiini kamili kinachochangia ongezeko la ugonjwa huo eneo hilo.

Akiwasilisha lalama za jamii ya Rendille kwa jopo kazi hilo, aliyekuwa mhudumu mkuu wa afya katika zahanati ya Kargi na pia mwakilishi wa wadi wa zamani wa South Horr , Asunta Galgitele amedai kuwa zaidi ya watu alfu moja wamefariki kutokana na ugonjwa wa saratani eneo hilo.

Jamii hiyo sasa inapendekeza serikali kuu kutekeleza uchunguzi wa kina kwa vyanzo vya maji, mchanga pamoja na nyasi katika eneo hilo ili kubaini kiini cha maradhi hayo na wathiriwa kufidiwa.

Mwenyekiti wa jopo kazi la tume ya ardhi ya kushughulikia dhuluma za kihistoria nchini, Profesa James Tuitoek amehakikishia umma kuwa lalama hizo na zingine walizopokea zitachunguzwa na mapendekezo yao kutolewa ifikiapo mwezi ujao wa Novemba mwaka huu.

23/10/2025

Tume ya ardhi nchini-NLC imepokea maoni ya umma kuhusu dhulma za kihistoria za ardhi katika kaunti ya Marsabit.

Shughuli hiyo ambayo imefanyika hapa mjini Marsabit imehusisha k**ati ya tume ya kushughulikia dhuluma za kihistoria na jamii za kaunti ya Marsabit ambazo zilikuwa zimewasilisha lalama zao kwa tume hiyo.

Akiongoza zoezi hilo mwenyekiti wa jopo kazi la tume ya ardhi ya kushughulikia dhulma za kihistoria nchini, Profesa James Tuitoek amefichukua kuwa tume hiyo ilikuwa imepokea lalama 3,743 za dhulma za kihistoria kote nchini, idadi kubwa ya lalama hizo ikitoka ukanda wa Pwani mwa Kenya.

Kati ya madai 3,743 yaliyopokelewa kote nchini, kaunti ya Marsabit iliwasilisha lalama tatu, mbili kutoka jamii ya Borana na Rendille zilizopatikana kuwa na uzito wa kuchungunza zaidi.

Akiwasilisha lalama za jamii ya Rendille kwa jopokazi hilo, aliyekuwa seneta wa kaunti ya Marsabit Godana Hargura, ametoa mapendekezo manne kwa tume hiyo kuzingatia katika kuhakikisha jamii hiyo inapataka haki kwa ardhi ya jamii ambayo aidha imesajiliwa k**a ardhi ya umma au ya jamii nyingine ili hali ni mali asili ya jamii ya Rendille.

Miongoni mwa mapendekezo hayo ni kurejesha ardhi ya Losai National reserve kwa jamii hiyo, kurejesha baadhi ya maeneo ya Marsabit National reserve kwa jamii hiyo, sawa na eneo la Ngurunit kutoka kaunti ya Samburu hadi kaunti ya Marsabit na pia jina la ziwa Turkana kurejeshewa jina lake la hapo awali la lake Rudolf.

Nayo jamii ya Borana ikiwakilishwa na mwenyekiti wa baraza la jamii hiyo hapa Saku, Dida Halake inamapendekezo matatu ambayo vile vile yanahusu ardhi ya hifadhi ya Marsabit National reserve na ardhi nyingine ya jamii jimboni.

Jamii hiyo inataka wathiriwa waliofanyiwa dhulma za kihistoria za ardhi kufidiwa na pia ardhi ya Jirime na ile ya Marsabit national reserve kurejeshewa jamii ya Borana.

Kamati ya tume ya ardhi ya kushughulikia dhuluma za kihistoria nchini, imehakikishia umma kuwa itafanya uchunguzi wa kina kuhusu lalama zilizowasilishwa kwa tume hiyo na kutoa mapendekezo k**ali yatakayo tumika kusuluhisha dhulma za kihistoria.

Hata hivyo masuala ambayo yanahusu asasi zingine za serikali k**a tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC sawa na bunge la seneti, tume hiyo itawasilisha mapendekezo yake jinsi ya kutatua madai ya lalama hizo.

BABA NA MWANAWE WA KIUME WAUWAWA BAADA YA BOMU LA ZAMANI KULIPUKA KARARE.Watu wawili wameuwawa baada ya kilipuzi kinacho...
22/10/2025

BABA NA MWANAWE WA KIUME WAUWAWA BAADA YA BOMU LA ZAMANI KULIPUKA KARARE.

Watu wawili wameuwawa baada ya kilipuzi kinachokisiwa kuwa bomu la zamani kulipuka katika kijiji cha Lekaritinya, eneo la Karare, kaunti ya Marsabit.

Akithibitisha mkasa huo, k**anda wa polisi kaunti ya Marsabit, Leonard Kimaiyo amesema wawili hao, baba wa umri wa miaka 34 na mwanawe wa kiume wa miaka 4 walifariki papo hapo wakati kifaa hicho kililipuka ndani ya nyumba yao.

Mkasa huo uliotokea majira ya saa kumi na moja jioni leo Jumanne ulisababisha nyumba yao kuharibika vibaya.

Kulingana na ripoti ya polisi, baba marehemu aliokota kifa hicho kinacchokisiwa kuwa bomu la zamani kabla ya kupeleka nyumbani.
Aidha alipojaribu kuvunja kifaa hicho alichokisia kuwa ni cha thamana, kililipuka na kumuuwa pamoja na mwanawe papo hapo.

Maafisa wa polisi wa jinai na wataalamu wa kutegua mabomu kutoka jeshi la Kenya-KDF wanaendelea na uchunguzi kubaini aina ya kifaa hicho.

Kamanda Kimaiyo hata hivyo amethahadharisha umma dhidi ya kuukota vifaa vinavyokisiwa kuwa mabomu ya ardhini ya zamani ambavyo huenda vikahatarisha maisha yao.

Address

Mosque Road
Marsabit
60500

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SIFA FM Marsabit posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SIFA FM Marsabit:

Share