
15/09/2025
NACADA YAZINDUA KAMPENI YA KUKABILIANA NA DAWA ZA KULEVYIA MARSABIT.
Mamlaka ya Kitaifa ya Kupambana na Matumizi ya Pombe na Dawa za Kulevya-NACADA imezindua kampeni ya siku tano ya kuhamasisha vijana na umma kwa ujumla kuhusu madhara ya dawa za kulevya kaunti ya Marsabit.
Uzinduzi huo umeongozwa na kamshina wa kaunti hii, James Kamau na mkurugenzi NACADA hapa jimboni Abdub Wako.
Akizungumza na vyombo vya habari wakati wa hafla hiyo kamishna Kamau amesema zoezi hilo litaendeswa katika kaunti zote ndogo jimboni.
Kamau wamewarai vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya.
Amebaini kuwa kuna mianya mpakani mwa Kenya na Ethopia ambayo imekuwa ikitumika na walanguzi kuingiza dawa hizo nchini, huku oparesheni kali ikiendelea kukabiliana na ulanguzi wa mihadarati.
Kwa upande wake mkurugenzi NACADA amewarai vijana kuwa mstari wa mbele kukabiliana na dawa za kulevya, huku akihoji kuwa vijana ni nguzo ya jamii kwani ndio kizazi cha sasa na matumaini ya kizazi kijacho.
Abdiaziz Boru katibu katika bunge la vijana, Saku Youth Assembly amewataka vijana kuchukua fursa hiyo kujinasua kutoka kwa matumizi ya dawa za kulevya .
Ni kauli iliyotiliwa mkazo na Peter Noor ambaye ni mojawapo ya waliokuwa wathiriwa wakuu wa matumizi ya dawa za kulevya jimboni.