27/10/2022
CHIPUKIZI AWEKEZE KWENYE AUDIO PLATFORMS AMA AENDELEE KUBAHATISHA KWA YOUTUBE?
Tumeona wasanii wakubwa hapa nchini na ughaibuni. Wanapoachilia ngoma, huitanguliza kwenye mitandao ya kidijitali k**a vile boomplay, spotify, audiomack, itune na platform nyinginezo kabla kuiachilia video kwenye youtube
Je umuhimu wake u wapi?.
Mitandao hii pia imeonekana kuleta kipato kizuri kulingana na mipangilio na ushambazaji wa mziki.
Je Machipukizi wahamie kuwekeza kwenye mitandao hii ama waendelee kubahatisha hapo tu kwa youtube?.
Ukiangalia wasanii chipukizi wanategemea kupush mziki wa audio kwa youtube, ambapo mwisho wa siku hawafikishi kiwango cha kuvuna fedha kutoka kwa mtandao huo.
Wengi sio kupenda kwao, ukosefu wa fedha nzuri za kufanya video yakuridhisha mashabiki .
Kwa hesabu ya haraka, chipukizi kutoa video nzuri ya ngoma itamgharimu kitita cha takribani Ksh 30k kwa minajili ya kujenga brand nzuri ili kuwaridhisha mashabiki.
Je hii mitandao ya Spotify,Boomplay inagharimu shilingi ngapi katika harakati ya kusambaza nyimbo hizi?.
Sidhani k**a zinafikia fedha za kutoa video.
Machipukizi wakiwaza mara mbili na kufikiria njia ya kupata kipato kutoka kwa platforms hizi basi watapiga hatua kitaaluama na kunufaika na vipaji vyao.
Tusishikilie mtandao mmoja unaotuziba macho tukakosa kuona kwengine kuliko na matumaini.
Mwandishi.Levis Jilani.
(Endapo uko na maoni yoyote yale, tutumie kwenye message pamoja na picha yako, ili tuzidi kuelimishana na kufahamishana)