001 FM

001 FM Uketo Wa Mwambao🌓...Kituo Bomba Kutoka Pwani Ya Kenya Kwa Habari Na Burudani!šŸ“»

Je, katika mila za Pwani ni sawa kumtemea mate mtoto? šŸ¤”Unajua maana na sababu ya desturi hii katika jamii zetu?Tuma maon...
15/08/2026

Je, katika mila za Pwani ni sawa kumtemea mate mtoto? šŸ¤”
Unajua maana na sababu ya desturi hii katika jamii zetu?

Tuma maoni yako na ushiriki nasi moja kwa moja ndani ya Asili ya Pwani, ukiwa na Miraj Guo kuanzia 10:00 AM – 1:00 PM.
šŸ“ž Piga simu: 0104 001 001
🌐 Sikiliza mubashara: 001fm.co.ke/listen-live

Haya wiki ndio ishaisha ivyo yani namaanisha ni Friday ungana nami malkia Ummy Francis ndani ya Mishemishe Midmorning Sh...
14/08/2026

Haya wiki ndio ishaisha ivyo yani namaanisha ni Friday ungana nami malkia Ummy Francis ndani ya Mishemishe Midmorning Show from 10am-1pm

we start driving your weekend crazy in a special way.

Asilimia kubwa ya shida unayopitia na inayokuumiza kichwa sana kwa sasa ni gani?

Tegea https://www.001fm.co.ke/listen-live
Whatsapp 0104 001001

Furahi-day Halisi ndani ya MORNING CHILLS šŸ”„Tukaribishe weekend na motivation na good vibes kwenye Morning Chills. Sema n...
14/08/2026

Furahi-day Halisi ndani ya MORNING CHILLS šŸ”„
Tukaribishe weekend na motivation na good vibes kwenye Morning Chills. Sema ni kubayaaaā° 7:00am – 10:00am with SHORT J.O Mwenyewe -Joshua ochieng šŸŽ§
šŸ’¬ WhatsApp: 0104 001001
šŸ“” Listen live šŸ‘‰www.001fm.co.ke/listen-live

It's a TBT ndani ya Alhamisi ya kale mila na tamaduni za kizamani mziki wa kikale pia from 10am-1pm nae malkia Ummy Fran...
13/08/2026

It's a TBT ndani ya Alhamisi ya kale mila na tamaduni za kizamani mziki wa kikale pia from 10am-1pm nae malkia Ummy Francis tukiserebuka kwenye mishemishe midmorning show

Ni kipi kilikua kikitendeka hapo kitambo na siku hakitendeki tena na kimeleta mabadiliko?

Tegea https://www.001fm.co.ke/listen-live

Whatsapp 0104 001001

Waziri wa Utumishi wa Umma, Geoffrey Ruku, ameongeza wito wake kwa wakazi wa Mt Kenya Mashariki kujitengenezea njia yao ...
13/08/2026

Waziri wa Utumishi wa Umma, Geoffrey Ruku, ameongeza wito wake kwa wakazi wa Mt Kenya Mashariki kujitengenezea njia yao wenyewe ya kisiasa na kimaendeleo.

Ruku amesema eneo hilo linapaswa kuwa na mwelekeo unaolenga maslahi ya wakazi wake, badala ya kusubiri maamuzi ya kisiasa kutoka kwa maeneo mengine.

Amesisitiza umuhimu wa wakazi wa Mt Kenya East kujitathmini, kuunganisha nguvu zao na kuamua aina ya uongozi na ajenda ya maendeleo wanayotaka kuelekea uchaguzi wa 2027 na miaka inayofuata.

Kwa upande wa maendeleo, Ruku amesema eneo hilo linahitaji kuweka vipaumbele vyake na kuhakikisha kuwa rasilimali na fursa zinazopatikana zinatumika kuboresha maisha ya wananchi.

Wito huo unajiri wakati ambapo siasa za Mlima Kenya zimeanza kushika kasi, huku viongozi kutoka maeneo mbalimbali wakijaribu kujenga ushawishi na kuelekeza jamii kuhusu mwelekeo wa kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2027.

Ruku amesisitiza kuwa Mt Kenya East ina uwezo wa kujiamulia mustakabali wake, ikiwa viongozi na wananchi wataungana katika kuweka ajenda inayolenga maendeleo na maslahi ya eneo hilo.


Kiongozi wa Wengi katika National Assembly of Kenya na Mbunge wa Kikuyu, Kimani Ichung’wah, amesema ana imani kuwa serik...
13/08/2026

Kiongozi wa Wengi katika National Assembly of Kenya na Mbunge wa Kikuyu, Kimani Ichung’wah, amesema ana imani kuwa serikali ya Broad-Based Government itashinda Uchaguzi Mkuu wa 2027 na kuendelea kuongoza nchi.

Ichung’wah amesema ushirikiano kati ya serikali ya Kenya Kwanza na chama cha ODM umeunda nguvu kubwa ya kisiasa ambayo, kwa mtazamo wake, inaweza kuwa muhimu katika uchaguzi ujao.

Kiongozi huyo amesema serikali imekuwa ikitekeleza ajenda zake na inaamini kuwa rekodi ya mafanikio iliyopatikana hadi sasa itawapa msingi wa kuwaeleza Wakenya kile ambacho imefanya na mipango iliyo nayo kwa siku zijazo.

Amesema muungano huo pia unaendelea kushirikiana na wananchi katika maeneo mbalimbali ili kueleza sera na miradi ya serikali, huku akisisitiza kuwa bado kuna muda wa kutosha kabla ya uchaguzi wa 2027.

Ichung’wah amesema serikali inaamini kuwa ushirikiano huo umeleta utulivu wa kisiasa na kuunganisha nguvu za viongozi kutoka pande mbalimbali za kisiasa.

Kwa mujibu wa Ichung’wah, lengo ni kuendelea kushirikiana na Wakenya, kusikiliza changamoto zao na kueleza hatua ambazo serikali imechukua katika kushughulikia masuala yanayowagusa.

Kauli yake inajiri wakati ambapo vyama na makundi mbalimbali ya kisiasa tayari vimeanza kujiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa 2027, huku suala la muungano wa kisiasa likiwa miongoni mwa masuala yanayotarajiwa kuamua mwelekeo wa siasa nchini.


Malalamiko ya wateja kuhusu data bundles kuisha ndani ya muda mfupi yameifanya Safaricom kutoa maelezo kuhusu sababu zin...
13/08/2026

Malalamiko ya wateja kuhusu data bundles kuisha ndani ya muda mfupi yameifanya Safaricom kutoa maelezo kuhusu sababu zinazoweza kuchangia matumizi ya data kwa kasi.

Wateja kadhaa wamekuwa wakilalamikia kuona vifurushi vyao vya intaneti vikiisha haraka, wakati mwingine ndani ya dakika chache baada ya kuvinunua au kuanza kutumia huduma za mtandao.

Safaricom imeeleza kuwa matumizi ya data yanaweza kutofautiana kulingana na shughuli zinazofanywa kwenye simu. Kutazama video, kutumia mitandao ya kijamii, kupakua mafaili, kusikiliza muziki na kutumia programu zinazofanya kazi nyuma ya pazia ni miongoni mwa shughuli zinazoweza kutumia data kwa kiwango kikubwa.

Pia, baadhi ya programu zinaweza kuendelea kutumia data hata wakati mtumiaji hazitumii moja kwa moja, hasa pale ambapo automatic updates, backups au video za ubora wa juu zimewezeshwa.

Kampuni imewahimiza wateja kufuatilia matumizi yao ya data kupitia mipangilio ya simu na kuweka vizuizi kwa programu zinazotumia data nyingi.

Wateja pia wanashauriwa kuangalia ni programu zipi zinazotumia data nyingi na kuzima matumizi ya data ya nyuma ya pazia pale ambapo hayahitajiki.

Safaricom imesema kuelewa matumizi ya data na kufuatilia programu zinazotumia bundles kwa wingi kunaweza kuwasaidia wateja kudhibiti matumizi na kupata thamani zaidi kutoka kwa vifurushi vyao.


Paris Saint-Germain (PSG) imefanikiwa kutetea taji la UEFA Super Cup baada ya kuichapa Aston Villa 2-1 katika mchezo mka...
13/08/2026

Paris Saint-Germain (PSG) imefanikiwa kutetea taji la UEFA Super Cup baada ya kuichapa Aston Villa 2-1 katika mchezo mkali uliowavutia mashabiki wa soka.

PSG ililazimika kufanya kazi kwa bidii kupata ushindi huo, huku Aston Villa ikitoa upinzani mkali na kufanya mchezo huo kuwa wa kusisimua hadi dakika za mwisho.

Ushindi huo umeifanya PSG kutwaa taji la UEFA Super Cup kwa mara ya pili mfululizo, ikiendelea kutawala mashindano hayo baada ya mafanikio yake ya awali.

Mbali na ubingwa, ushindi huo umeipa PSG zawadi kubwa ya kifedha, huku Aston Villa nayo ikiondoka na kiasi kikubwa cha fedha licha ya kupoteza mchezo huo.

Mafanikio hayo yanaongeza thamani ya msimu kwa PSG, ambayo imeendelea kujenga rekodi yake katika soka la Ulaya. Kwa upande wa Aston Villa, timu hiyo inaweza kujivunia kampeni iliyoiwezesha kufika katika hatua ya kuwania taji, licha ya kushindwa kulinyakua.


Gavana wa Homa Bay Gladys Wanga amewaonya wakazi wa kaunti hiyo kuhusu uwezekano wa shughuli za Linda Mwananchi kuathiri...
13/08/2026

Gavana wa Homa Bay Gladys Wanga amewaonya wakazi wa kaunti hiyo kuhusu uwezekano wa shughuli za Linda Mwananchi kuathiri utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wanga amesema kuwa idadi kubwa ya watu kujitokeza katika shughuli hiyo inapolenga Homa Bay inaweza kuvuruga shughuli za kawaida na kuhatarisha miradi ambayo kaunti imekuwa ikitekeleza kwa manufaa ya wananchi.

Gavana huyo amewataka wakazi kuzingatia masuala ya maendeleo na kuhakikisha kuwa shughuli za kisiasa haziathiri mipango ya kaunti, ikiwemo miradi inayolenga kuboresha huduma kwa wananchi.

Kauli yake inajiri wakati ambapo Linda Mwananchi inaelekeza shughuli zake kuelekea Homa Bay, hatua inayotarajiwa kuvuta idadi kubwa ya wafuasi na viongozi wa kisiasa.

Wanga amesema wananchi wana haki ya kushiriki katika shughuli za kisiasa, lakini amesisitiza umuhimu wa kulinda maendeleo ya kaunti na kuhakikisha kuwa miradi iliyopangwa haiathiriwi na mikutano ya kisiasa.

Gavana huyo pia amesisitiza kuwa maendeleo ya Homa Bay yanapaswa kupewa kipaumbele, huku akiwataka wakazi kuwa makini wanaposhiriki katika shughuli zinazoweza kuathiri utulivu na utekelezaji wa mipango ya kaunti.


13/08/2026

Vurugu zilitokea nje ya Bunge la Kaunti ya Mombasa hapo jana wakati vijana pamoja na watetezi wa haki za binadamu walipowasilisha mapendekezo kuhusu masuala yanayowakabili vijana katika Kaunti ya Mombasa. Kundi hilo lilikuwa limefika katika Bunge hilo kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Vijana na kutaka vijana washirikishwe zaidi katika uongozi, utungaji wa sera na maamuzi yanayohusu mustakabali wao.
Hata hivyo, muda mfupi baada ya kuwasilisha mapendekezo yao kwa uongozi wa Bunge la Kaunti, vurugu zilizuka nje ya majengo hayo baada ya kundi la watu wanaodaiwa kuwa na silaha kuwavamia waandamanaji. Baadhi ya vijana walilazimika kutawanyika kutafuta usalama, huku baadhi wakidaiwa kupoteza simu na mali zao. Vijana na watetezi wa haki za binadamu wamekashifu tukio hilo na kusisitiza kuwa walikuwa wamekusanyika kwa amani kutekeleza haki yao ya kushirikisha viongozi kuhusu masuala yanayowahusu.

Address

Likoni/Approved Area
Mombasa
42729-80100

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when 001 FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to 001 FM:

Share

Category