16/08/2026
Showbuzz TV Updates
Baraka De Prince afichua yote aliyodai kufanyiwa na Alikiba baada ya kuchaguliwa na kampuni ya muziki ya Sony kuwakilisha Tanzania!
Katika mahojiano hayo, Baraka De Prince alieleza kuwa jina lake lilipendekezwa na Alikiba mwenyewe ili awe miongoni mwa wasanii watakaoshiriki katika mradi wa Sony.
Hata hivyo, Baraka anadai mambo yalibadilika baada ya kuchaguliwa kushiriki katika mradi huo mkubwa.
"Kwenye project hiyo, nilichaguliwa kushiriki. Jamaa akaanza kunionyesha maneno ya chini chini, ilhali sisi tulikuwa timu moja," alisema Baraka.
Baraka aliendelea kueleza kuwa alikuwa na uhusiano mzuri na watu wa karibu wa Alikiba na hakuwahi kujihusisha na mambo ya sh**ha.
Pia alifichua kuwa alifika hatua ya kujitenga kabisa na kundi la Alikiba kutokana na maneno na vitendo ambavyo alikuwa akivipitia.
Kwa mujibu wa maelezo yake, baadhi ya watu walianza kumtukana kwenye mitandao ya kijamii na hali hiyo ilimuumiza zaidi.
Baraka pia aligusia suala la imani, akisema ametokea katika familia ya Kikristo na haamini katika uchawi au nguvu za giza.
"Hatuaamini mambo ya uchawi. Sisi Wakristo tunaamini katika kumuomba Mwenyezi Mungu," alisema.
Je, unadhani tofauti kati ya Baraka De Prince na Alikiba ilianza baada ya mradi wa Sony, au kuna jambo lingine lililokuwa nyuma ya pazia?
Maoni yako ni yapi?
Tanzania MusicUpdates