14/06/2026
π€ SHOWBUZZ TV | BURUDANI
Msanii Emkay Emkay ameweka wazi kuwa yupo tayari kuachia wimbo wake mpya unaoitwa "SHINE" akimshirikisha rapa nguli wa Kenya King Kaka, lakini ametoa sharti moja kwa mashabiki wake.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Emkay amesema kuwa mara tu kazi yake ya "KOROGESHEN" itakapofikisha watazamaji 100,000, ndipo atadondosha rasmi wimbo huo mpya unaosubiriwa kwa hamu.
Tangazo hilo limeibua msisimko mkubwa kwa mashabiki, wengi wakionesha hamu ya kusikia ushirikiano huo kati ya Emkay Emkay na King Kaka, ambao unatarajiwa kuleta ladha ya kipekee kwenye muziki wa Afrika Mashariki.
Je, KOROGESHEN itafikisha 100K kwa haraka na kuufungua mlango wa kuachiwa kwa SHINE? Muda ndio utakaotoa majibu.
π Una matarajio gani kuhusu wimbo wa SHINE Ft King Kaka? Tuambie kwenye maoni.
EastAfricanMusic EntertainmentNews