06/04/2026
Rais wa Cameroon Paul Biya amemteua mwanae Franck Emmanuel Biya kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri na Mkuu wa Majeshi.
Hivi karibuni Bunge la Cameroon liliidhinisha kwa wingi marekebisho ya Katiba ili kurejesha nafasi ya Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais atachukua kiti cha Urais moja kwa moja ikiwa Rais Paul Biya atakufa, kujiuzulu, au kutokuwa na uwezo.
Kulingana na sheria, Makamu wa Rais atateuliwa na kuachishwa kazi na Rais na atahudumu kwa muda uliosalia wa muhula wa Rais wa miaka saba endapo Rais atashindwa kuhudumu katika wadhifa wake.
Kurejeshwa kwa Makamu wa Rais kunaashiria marekebisho ya kwanza ya katiba ya Cameroon tangu mwaka 2008 wakati ukomo wa mihula ya Urais ulipotupiliwa mbali hatua iliyozua maandamano nchi nzima.
Makamu wa Rais hapo awali alikuwa sehemu ya muundo wa utawala wa Cameroon lakini ulifutwa mwaka 1972 kufuatia kura ya maoni ya Katiba.
✍🏾mwandishi-Maulid Kitenge
picha kwa hisani