03/06/2026
π§π· Casemiro amezungumzia hali ya Neymar na kuwataka watu wasimweke presha kubwa kwa sasa.
Kiungo huyo amesema kila wanapofika kwenye mikutano ya waandishi wa habari, swali kubwa huwa ni kuhusu Neymar pekee, ilhali yeye ni mmoja tu kati ya wachezaji 26 wa kikosi cha Brazil.
Casemiro amesisitiza kuwa kwa sasa jambo muhimu zaidi kwa Neymar ni kupona majeraha yake na kurejea mazoezini taratibu. Anaamini hakuna haja ya kukimbilia kumtaka awe nyota wa timu mara moja.
π£οΈ βLazima iwe hatua kwa hatua. Kwanza arudi kwenye afya nzuri, kisha ndipo tufikirie kuhusu kuwa mhusika mkuu wa timu.β
Kwa kifupi, Casemiro anataka Neymar apewe muda wa kutosha kupona na kurejea akiwa katika kiwango chake bora bila shinikizo la haraka. π§π·β¨
Ili kupata updates za michezo follow Cresta Media
π§π·π₯