Shabiki Sugu

Shabiki Sugu Mazungumzo na mashabiki nguli wa Soka⚽️ Mjadala|Kilio|Hisia|Msongo wa mawazo|Furaha na mengine mengi

“Football can be cruel sometimes…”Matukio haya mawili yanafanana sana! Kwakuwa ni k**a kisu kikali kilichowakata maini n...
15/05/2024

“Football can be cruel sometimes…”

Matukio haya mawili yanafanana sana! Kwakuwa ni k**a kisu kikali kilichowakata maini na kuwakata tamaa mashabiki wa soka, wachezaji na makocha wao! Baada ya ile “save” ya karne kutoka kwa Kipa wa Argentina Emmy Martinez katika mechi ya kombe la dunia, hapo jana Steffan Ortega wa Manchester City nae alifanya “save” kubwa na muhimu sana katika mechi yao dhidi ya spurs!

Kwa wale wapenzi wa soka basi wanatambua kua save hii ya Ortega iliwaliza sio tu mashabiki wa Spurs kwa kukosa nafasi wazi ya kufunga goli bali pia iliwakatisha tamaa ya kutwaa Unbingwa wa Uningereza timu ya Arsenal!

Huu ulikuwa unyama mwingi kutoka kwa walinda lango hawa wawili!

UNAI EMERY APEWE MAUA YAKE!!Aston Villa yajikatia tiketi ya kushiriki michuano ya Vilabu bingwa ulaya msimo ujao kwa mar...
14/05/2024

UNAI EMERY APEWE MAUA YAKE!!

Aston Villa yajikatia tiketi ya kushiriki michuano ya Vilabu bingwa ulaya msimo ujao kwa mara ya kwanza kuanzia mwaka wa 1982.

Hii ni baada ya Tottenham kupokea kipigo cha bao mbili bila jibu ugani kwao dhidi ya magwiji Manchester City. Matokeo haya yanampa furaha shabiki wa Aston Villa kwa kuzipiku timu kubwa k**a vile Man u, chelsea na tottenham!

Kazi nzuri sana kutoka kwa Unai Emery!

MAHASIMU WA JADI WA ‘NORTH LONDON’ KUUNGANA LEO HII!Kweli mambo ni kangaja huenda kisha yakaja na leo yamewajia mashabik...
14/05/2024

MAHASIMU WA JADI WA ‘NORTH LONDON’ KUUNGANA LEO HII!

Kweli mambo ni kangaja huenda kisha yakaja na leo yamewajia mashabiki wa arsenali ya kule uingereza na hata wa humi nchini! Maelfu ya mashabiki wa arsenal wakiongozwa na wachezaji wao nyota wa zamani Mesut Ozil na Theo Walcott, waungana na mahasimu wao wa Tottenham Hotspurs katika mechi yao dhidi ya Manchester City hapo leo usiku!
Wanabunduki wananawaombea ushindi watani wao ili iwawezeshe wao kuipiku Man City pale juu kileleni! Endapo Spurs itafanikiwa kuifunga City, basi Arsenal itasalia kieleleni mwa ligi ikiwa na alama moja zaidi ya City huku wote wakibakisha mechi moja!
Je Spurs itawasaidia Arsenal ama Man City wataibuka washindi na kuzidisha kasi yao katika msimamo wa ligi? Usikose mechi hii ya leo usiku mana yajayo yanafurahisha sana👍👍

Karibu katika Podcast ya Shabiki Sugu ambapo tunaipaza sauti ya kilio cha mashabiki nguli wa soka!Wafuasi sugu wa timu z...
12/05/2024

Karibu katika Podcast ya Shabiki Sugu ambapo tunaipaza sauti ya kilio cha mashabiki nguli wa soka!
Wafuasi sugu wa timu za soka huwa wanapitia kiasi kikubwa cha msongo wa mawazo wakati wanatizama timu zao zikisakata soka hasaa pale timu hizo zikiwa hazifanyi vizuri! Shabiki Sugu Podcast inawapa fursa mashabiki kutoa hisia zao za ndani kuhusu timu zao! Tunakuletea makala mbalimbali yakiwemo: Kilio, historia, mtazamo, mjadala, mafanikio, furaha na mengine mengi kutoka mashabiki wa vilabu vya humu nchini na hata vile vya ulaya na kwengineko! Ungana nasi mana yajayo yanafurahisha mno!

Address

Mombasa

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shabiki Sugu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shabiki Sugu:

Share

Category