30/07/2026
● TUSEMEZANE,
Habari ya adhuhuri, hii ni ripoti ambayo kwa mzazi yeyote inachoma sana moyo. Ni uchungu sana kulipa karo, kununua baadhi ya vinavyohitajika shuleni japo si vyote maana maisha ya sasa wengi wetu tunajaribu sana kadri ya uwezo wetu angalau kuenda na wakati.
kisa cha Brenda, mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyepotea kwao na hatimaye imesemekana alionekana maeneo ya Malindi, kuna tetesi kwamba jamaa mmoja alijinyakulia na siwezi sema amemuoa, la hasha. Hatuna ushahidi huo, ila kisheria na katiba ya nchi, mkikaa pamoja miezi 3 au zaidi nyinyi ni wachumba tayari, mnapaswa kuitwa wanandoa.
Ila ni mwanafunzi! Hii huwenda ikaleta maana ingine hasa k**a serikali itaingililia kati na iwapo, familia ya msichana huyu itachukua hatua za kisheria.
K**a wazazi, usifurahie mambo k**a haya, ukiwa na ufahamu saidia familia hii kutegua kitendawili cha mwana wao. M'barikiwe.