Dawati La Michezo

Dawati La Michezo Hii ni Tovuti ya Michezo na Burudani.

09/01/2026
09/01/2026

Hili bao la penalti hii iliyopigwa lilikataliwa na refa kwa kisingizio kuwa mpigaji alikiuka sheria za mpira, kisha refa huyo akaamuru penalti hiyo irudiwe, iliporudiwa, mpigaji akapoteza penalti hiyo. Je, refa alikuwa sahihi kwa mujibu wa sheria za soka ama alimdhulumu mpigaji penalti hiyo?

09/01/2026

Mechi za Hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 nchini Morocco, zinaanza rasmi Ijumaa hii ya Januari 9 hadi Jumamosi hii ya Januari 10, 2026.





06/01/2026
06/01/2026

Mtangazaji wa mpira Japhet Kahindi ‘Makanaky’ akijukumika katika mchezo wa fainali baina ya Power United FC na Young Strikers FC kuwania taji la Kenga Wehu Super Cup ya wadi ya Rabai Kisurutini, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Ludwig Krapf eneobunge la Rabai Kaunti ya Kilifi, siku ya Alhamisi ya Januari 1, 2026.

06/01/2026
06/01/2026

Mbunge wa eneo la Rabai katika Kaunti ya Kilifi nchini Kenya Anthony Kenga Mupe ‘Ngangari’ akiwasalimia wachezaji wa Power United FC kwenye Uwanja wa Ludwig Krapf kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali ya michuano ya Kenga Wehu Super Cup ya wadi ya Rabai Kisurutini, siku ya Alhamisi ya Januari 1, 2026. Power United FC ilitwaa ubingwa kwa kuishinda Young Strikers FC mabao 3-2 kupitia mikwaju ya penalti baada ya timu hizo kutoka suluhu katika muda wa kawaida.

05/01/2026

Mbunge wa eneo la Rabai katika Kaunti ya Kilifi nchini Kenya Anthony Kenga Mupe ‘Ngangari’ akiwasalimia wachezaji wa Young Strikers FC kwenye Uwanja wa Ludwig Krapf kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali ya michuano ya Kenga Wehu Super Cup ya wadi ya Rabai Kisurutini, siku ya Alhamisi ya Januari 1, 2026. Power United FC ilitwaa ubingwa kwa kuishinda Young Strikers FC mabao 3-2 kupitia mikwaju ya penalti baada ya timu hizo kutoka sare ya bila kwa bila katika muda wa kawaida.

05/01/2026
05/01/2026

Mtangazaji wa mpira Japhet Kahindi ‘Makanaky’ (aliyevaa kofia) akitangaza mechi ya ufunguzi ya Michuano ya UNGA NI TAIFA SUPER CUP 2025 kati ya Sparki Youth FC na Kisauni Hope FC mchezo wa Kundi A uliopigwa kwenye Uwanja wa Mombasa Sports Club, siku ya Jumapili ya Novemba 23, 2025. Makanaky alipiga kazi hiyo akiwa pamoja na mtangazaji wa Mo Radio, Omar Mazera. Katika mechi hiyo, Sparki Youth FC iliichapa Kisauni Hope FC manao 2-1.

Address

Mombasa
80100

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dawati La Michezo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share