Dawati La Michezo

Dawati La Michezo Hii ni Tovuti ya Michezo na Burudani.

29/09/2025
Shirikisho la Mchezo wa Tong Il-Moo-Do nchini Kenya(KTMF) likishirikiana na Shirika la Kijamii la Brilliant Feminine wam...
29/09/2025

Shirikisho la Mchezo wa Tong Il-Moo-Do nchini Kenya(KTMF) likishirikiana na Shirika la Kijamii la Brilliant Feminine wameungana kwa madhumuni ya kupinga na kupiga vita dhidi ya Unyanyasaji wa Kijinsia(GBV) katika Kaunti ya Samburu. Ushirikiano huo pia utaendeleza kampeni za kuhakikisha wanawake wanawezeshwa ili kujinasua kiuchumi.
Ushirikiano huo wa kipekee kati ya KTMF na Shirika hilo la Brilliant Feminine, lenye makao makuu yake katika Kaunti ya Samburu, utatumia mchezo huo wa Tong Il-Moo-Do katika harakati za kupinga visa vya Unyanyasaji wa Kijinsia(GBV) vilivyokidhiri miongoni mwa jamii na kuwapigia debe wanawake wawezeshwe kiuchumi.

KTMF imeamua kutumia mchezo wa Tong Il-Moo-Do k**a silaha dhidi ya visa vya Unyanyasaji wa Kijinsia(GBV) likishirikiana na Shirika hilo la Brilliant Feminine ambalo lilianzishwa kwa lengo la kuwatetea wanawake wawezeshwe kiuchumi na kupiga vita dhidi ya Unyanyasaji wa Kijinsia(GBV). Shirika la Brilliant Feminine lilianzishwa kwa pamoja na Twalib Rashid na Halima Abdikadir ambaye ndiye Mkurugenzi Mtendaji. Ushirikiano wao na KTMF ni hatua kubwa katika lengo lao la kutengeneza mazingira salama kwa wanawake katika Kaunti ya Samburu.

KTMF na Brilliant Feminine waliamua kushirikiana wakati wa Mashindano ya Kimataifa ya Mbio za Ngamia ya Maralal(Maralal International Camel Derby) yanayofanyika kila mwaka, katika Kaunti ya Samburu. Mashindano hayo yalivutia watu mashuhuri akiwemo Waziri wa Utalii na mbuga za Wanyama pori Rebecca Miano, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Waziri Miano alisifu ushirikiano wa pamoja kati ya KTMF na Shirika la Brilliant Feminine katika jitihada zao za kupiga vita visa vya Unyanyasaji wa Kijinsia(GBV) na kuhakikisha wanawake wanawezeshwa kiuchumi, kwa kutumia michezo, hususan mchezo wa Tong Il-Moo-Do.
Wakati wa Maralal International Camel Derby, KTMF ilionyesha mafunzo ya mchezo wa Tong Il-Moo-Do k**a mchezo wa nidhamu, na kuonyesha mbinu za kujikinga na kujiamini ikiwa ni mchezo muhimu katika kuwawezesha wanawake.

Mafunzo hayo yaliongozwa na Naibu Katibu wa Shirikisho la Mchezo wa Tong Il-Moo-Do nchini Kenya(KTMF) Elvis Malipe Ole Mpakuanik, aliyesaidiwa na walimu katika mchezo huo, Salma Ali Abdallah pamoja na Lorna Apiyo Abiero.
Katika hafla hiyo, KTMF ilitangaza kuanzishwa kwa klabu mpya ya mchezo wa Tong Il-Moo-Do kwenye Kaunti ya Samburu ambayo itasaidia pakubwa jamii ya Samburu kupata mafunzo ya kimbinu zaidi.

23/09/2025

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Ufaransa anayeichezea klabu ya Paris Saint-Germain PSG Ousmane Dembélé, mwenye umri wa miaka 28, ametwaa Tuzo ya Mwanasoka Bora barani Ulaya ya Ballon D’Or, upande wa wanaume, ya mwaka huu 2025.

Nyota huyo za zamani wa Barcelona alishinda Tuzo hiyo baada ya kuisaidia PSG kutwaa mataji yote ya Ufaransa msimu uliopita 2024/2025 kwa kushinda Ligi Kuu ya Ufaransa Ligue 1, Kombe la Coupe de France, French Super League pamoja na lile taji la Michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Msimu huo uliopita pia Dembélé, aliyezaliwa na mama kutoka Mauritania na Senegal na baba kutoka Mali, alishinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Ufaransa Ligue 1 na Tuzo ya Mfungaji Bora wa Ligue 1 na Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Kocha Mkuu wa PSG Mhispania Luis Enrique, alishinda Tuzo ya Kocha Bora kutokana na kiwango bora PSG ilikionyesha msimu uliopita ikiwa chini yake.
Dembélé alitwaa Tuzo baada ya kuwashinda Lamine Yamal wa Barcelona na Vitinha wa Paris Saint-Germain PSG, Mohamed Salah wa Liverpool alikuwa wa nne huku Mbrazil Raphinha, akimaliza wa tano.

Yamal alishinda Tuzo ya Mchezaji Bora kijana ya Kopa Trophy kwa mara ya pili, Gianluigi Donnarumma wa Manchester City alitwaa Tuzo ya Mlinda Lango Bora ya Yashin Trophy kwa mara ya pili huku Tuzo ya Mfungaji Bora ya Gerd Müller Trophy ikichukuliwa na Viktor Gyökeres wa Sweden na Arsenal, aliyefunga mabao 54 katika mechi 52 kwenye michuano yote, akiwa na klabu ya Sporting Lisbon ya Ureno.
, , ,

Timu ya Naivas Supermarket FC ilizawidiwa runinga kubwa ya kisasa aina ya 4K UHD TV na vipasa sauti vya kidigitali aina ...
21/09/2025

Timu ya Naivas Supermarket FC ilizawidiwa runinga kubwa ya kisasa aina ya 4K UHD TV na vipasa sauti vya kidigitali aina ya XBoom portable Bluetooth kutoka kwa Kampuni ya kutengeneza vifaa vya kutumia nguvu za umeme ya LG Electronics.
Naivas Supermarket FC ilitunukiwa zawadi hizo baada ya kuicharaza timu ya LG/Opalnet FC mabao 4-1 katika mechi maalum ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Sameer Business Park, Jijini Nairobi.

Timu ya LG/Opalnet FC ni muungano wa wafanyakazi wa Kampuni ya LG Electronics pamoja na wale wa kutoka Opalnet Ltd. Kampuni ya Opalnet Ltd ni washirika wakubwa wa kibiashara wa LG Electronics ambao pia ni wasambazaji wa vifaa vya LG Electronics.

Kampuni ya LG Electronics ndio iliyoandaa mechi hiyo kwa madhumuni ya kuonyesha moyo wa kirafiki katika ushindani wa kibiashara kwa kuwashirikisha wafanyakazi wa duka kubwa la jumla la Naivas Supermrket. Kampuni ya LG Electronics ilitumia soka kuonyesha nguvu ya mchezo huo kuunganisha watu kwa kuwaleta pamoja.

Rais wa Kampuni ya LG Electronics Ukanda wa Afrika Mashariki, Donghun Lee, alisifu michuano hiyo kwa kuitaja k**a kichocheo cha kuleta umoja miongoni mwa wafanyakazi.

“Michezo uleta umoja na ushirikiano katika mashirika, na tumekubushwa kuwa mashindano ni jukwaa la kuwaunganisha watu pamoja. Michuano hii imeimarisha ushirikiano wetu pamoja na kampuni ya Naivas na imesaidia pakubwa timu zetu zote kuwa kitu kimoja katika siku za usoni,” Alisema Lee.

Lee aliendelea kuongeza. “Mashindano haya ni ya kwanza kuandaliwa na yametusongeza karibu na washirika wetu na kujenga mfumo wa ikolojia(ecosystem) kwa upana zaidi ambayo pia inakumbatiwa na washirika wao.
Tunaposhirikiana pamoja, huwa tunaimarisha uhusiano wetu wa kibiashara na kujenga utamaduni wa ushirikiano unaofaidisha kila mmoja aliyeusishwa.

Shughuli hii inatupa fursa ya kuonyesha bidhaa zetu tofauti tofauti na kutoa mawazo mapya ya vile tutayawasilisha kwa wateja wetu tena kwa ukubwa zaidi,” aliongeza Lee.
Naye Mkuu wa Utawala wa Kampuni ya Naivas, Charles Mukuha, pia aliunga mkono kauli ya Donghun Lee, kwa kusisitiza kuwa mashindano hayo yanaonyesha sura halisi ya falsafa ya kampuni ya Naivas kuhusu jamii na ushirikiano.

“Hii mechi ilikuwa ni furaha ya umoja na ushik**ano wetu, na pia ilionyesha dhamani yetu tuliyonayo kwa wateja wetu ilhali mchezo huu pia ulitujenga kati yetu. Tumefurahi kwa kushirikiana pamoja na kampuni ya LG East Africa na tunalenga kushirikiana kwa pamoja zaidi katika siku za usoni,” Mukuha alikariri.
, , , , , ,

08/09/2025

Watimka mbio Peter Mwangi na Fridah Ndida waling’ara katika mbio za maandalizi za Kilomita 21 za Standard Chartered Nairobi Marathon zilizofanyika Parklands Sports Club Jijini Nairobi nchini Kenya.
Katika mbio hizo, zilizowavutia zaidi ya wanariadha 1500, Fridah alitumia muda wa dakika 77 na kuibuka bingwa katika kitengo cha wanawake huku Mwangi akitwaa ushindi kwa upande wa wanaume baada ya kutimka mbio hizo kwa muda wa dakika 65.

Baada ya kushinda mbio hizo, Mwangi alisema ushindi wake ni ishara tosha kuwa yuko tayari kwa mashindano makubwa yajayo ya marathon.
“Kushinda kwangu leo kumenipa faraja kubwa na kunifanya nijiamini licha ya ushindani uliokuwepo huku nikijianda kushiriki kwenye mashindano yajayo makubwa yatakayofanyika mwezi Oktoba. Nina matumaini nitafanya vizuri,” Mwangi aliiambia Radio Mabingwa.
Wanariadha hao walitumia mbio hizo kwa minajili ya maandalizi ya mapema kabla ya kushiriki kwenye mbio za mashindano makubwa ya makala ya 22 ya Standard Chartered Nairobi Marathon ya mwaka huu, yatakayoandaliwa Jumapili ya Oktoba 26, 2025 kwenye eneo la Uhuru Gardens, Jijini Nairobi.

Mbio nyingine za maandalizi ya mapema yatakayofuata, yatakayofanyika kabla ya mashindano makubwa ya makala ya 22 ya Standard Chartered Nairobi Marathon 2025, yataandaliwa Karura Forest, ndani ya kambi ya matibabu ya Kibera Nairobi kisha ifuatiwe na mbio za satellite run ya Mombasa.

Mbio za mwaka huu zinatarajiwa kuwavutia zaidi ya wakimbiaji 30,000 ambao watashiriki katika vitengo mbalimbali, vya Wanawake na Wanaume, k**a vile mbio za marathon za kilomita 42, mbio za half marathon za kilomita 21, mbio za kutembea za kilomita 10 na mbio za kilomita 10 za wanariadha wanaoishi na ulemavu watakaotumia viti vya magurudumu.

Madhumuni ya mbio za mwaka huu za Standard Chartered Nairobi Marathon ni kukusanya zaidi ya kima cha Ksh.70 milioni kusaidia mradi wa Kimataifa wa Standard Chartered’s Futuremakers ulioanzishwa kwa lengo la kuwawezesha vijana, hususan wanawake na watu wanaoishi na ulemavu, kupitia elimu, ajira na ujasiriamali.
Mradi huo ulioanzishwa na benki hiyo ya Standard Chartered, pia unasaidia kizazi kijacho kupata ujuzi, kuimarisha uwezo wao wa kupata ajira na kuanzisha biashara.

Katika mbio za makala ya 21 za Standard Chartered Nairobi Marathon zilizofanyika mwaka jana 2024, Ksh.48 milioni zilikusanywa na kuwekezwa moja kwa moja kwenye mradi wa Futuremakers programmes.
Benki ya Standard Chartered ndio udhamini mbio hizo za Standard Chartered Nairobi Marathon kila mwaka.
, , , , , , , ,

02/09/2025

Radio Mabingwa is an online swahili radio station focusing primarily on sports news, updates, interviews, features, talk shows and analyses.

Address

Mombasa
80100

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dawati La Michezo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share