Michezo Online News

Michezo Online News Michezo Online News ni nyumbani kwa habari na matukio kemkem ya spoti yanayotokea humu nchini, barani Afrika na duniani kote

 Mazungumzo yamefanyika kati ya Wolves na Nuno Espirito Santo ya kuchukua tena mikoba ya ukufunzi dimbani Molineux.Nuno ...
14/10/2022



Mazungumzo yamefanyika kati ya Wolves na Nuno Espirito Santo ya kuchukua tena mikoba ya ukufunzi dimbani Molineux.

Nuno aliondoka Wolves miezi 7 iliyopita lakini inafahamika kuwa moyo wake uko kwenye kuungana tena na klabu hiyo.

 N'golo Kante ameripotiwa kupata majeraha na anatarajiwa kuwa nje kwa mechi tano ijayo ya Chelsea.Mfaransa huyo, 31, pia...
14/10/2022



N'golo Kante ameripotiwa kupata majeraha na anatarajiwa kuwa nje kwa mechi tano ijayo ya Chelsea.

Mfaransa huyo, 31, pia sasa atakuwa shakani kwa Kombe la Dunia ambalo litaanza Novemba 20 nchini Qatar.

 Bao la muda wa ziada la Scott Mctominay lilipatia Manchester United pointi tatu muhimu dhidi ya timu shupavu ya Omonia ...
14/10/2022



Bao la muda wa ziada la Scott Mctominay lilipatia Manchester United pointi tatu muhimu dhidi ya timu shupavu ya Omonia Nicosia kutoka Cyprus.

Kipa wa Nicosia Francis Uzoho aliokoa mikiki 12 wakati wa mechi hiyo ya Ligi ya Europa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Old Trafford, Uingereza.

 Ni siku 39 kabla ya  Je, wajua kuwa mwaka 2010 dhidi ya Mexico, Siphiwe Tshabalala alikuwa Mwafrika Kusini wa 7 kufunga...
13/10/2022



Ni siku 39 kabla ya

Je, wajua kuwa mwaka 2010 dhidi ya Mexico, Siphiwe Tshabalala alikuwa Mwafrika Kusini wa 7 kufunga bao kwenye Kombe la Dunia?


 Bingwa wa Olimpiki na Dunia wa mita 1,500 Faith Chepng'etich kwa mara nyingine ameteuliwa kuwania Tuzo ya Mwanariadha B...
13/10/2022



Bingwa wa Olimpiki na Dunia wa mita 1,500 Faith Chepng'etich kwa mara nyingine ameteuliwa kuwania Tuzo ya Mwanariadha Bora wa Dunia kwa Wanawake 2022.

Chepng’étich mwenye umri wa miaka 28 atachuana na wanariadha wengine tisa bora kuwania tuzo hiyo ambayo mshindi wake atafichuliwa kwenye mitandao ya kijamii ya Riadha ya Dunia mapema mwezi Desemba.

 Klabu ya Soka ya Kakamega Homeboyz  imetangaza rasmi kustaafu kwa beki wao Benjamin Oketch Papali.Beki huyo mkongwe amb...
13/10/2022



Klabu ya Soka ya Kakamega Homeboyz imetangaza rasmi kustaafu kwa beki wao Benjamin Oketch Papali.

Beki huyo mkongwe ambaye amekuwa na "Abana Beingo" kwa miaka 5 iliyopita ananing'iniza buti zake baada ya miaka 15 ya mafanikio.

Hapo awali amezichezea Chemilil Sugar FC, Bidco United FC na Sher Karuturi Sports.

 Club Brugge inakuwa timu ya pili ya Ubelgiji katika historia kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya   baada ya Genk baada ya ku...
12/10/2022



Club Brugge inakuwa timu ya pili ya Ubelgiji katika historia kufuzu kwa hatua ya 16 bora ya baada ya Genk baada ya kulazimisha sare ya 0-0 nchini Madrid.

Napoli pia wametinga hatua ya 16 bora baada ya kuipepeta Ajax kwa mabao 4-2.

 Gabriel Jesus hakufanya mazoezi leo lakini Arsenal wanasema anapumzishwa tu kabla ya mechi ya Leeds wikendi hii.Hataraj...
12/10/2022



Gabriel Jesus hakufanya mazoezi leo lakini Arsenal wanasema anapumzishwa tu kabla ya mechi ya Leeds wikendi hii.

Hatarajiwi kusafiri kwenda Norway kwa mchezo wa Ligi ya Europa dhidi ya Bodo/Glimt Alhamisi usiku.

 Manchester City na Real Madrid zimefuzu kwa hatua ya 16 bora ya Ligi ya klabu Bingwa Ulaya UEFA.Madrid ndiyo timu pekee...
12/10/2022



Manchester City na Real Madrid zimefuzu kwa hatua ya 16 bora ya Ligi ya klabu Bingwa Ulaya UEFA.

Madrid ndiyo timu pekee ambayo imefuzu hatua zote za makundi tangu msimu wa 1992/93 wakati kombe la Ulaya lilipobadilisha jina na kuwa Champions league.

 Kylian Mbappé hafurahishwi na Paris Saint-Germain na anataka kuondoka klabuni hapo haraka iwezekanavyo.Paris Saint-Germ...
11/10/2022



Kylian Mbappé hafurahishwi na Paris Saint-Germain na anataka kuondoka klabuni hapo haraka iwezekanavyo.

Paris Saint-Germain wanahisi kuwa anaweka shinikizo kwa kilabu lakini hawana nia ya kumuuza Mbappé mnamo Januari.

 FA inakagua ripoti ya waamuzi kufuatia mzozo kati ya Gabriel na Jordan Henderson huko Emirates siku ya Jumapili.Tayari ...
11/10/2022



FA inakagua ripoti ya waamuzi kufuatia mzozo kati ya Gabriel na Jordan Henderson huko Emirates siku ya Jumapili.

Tayari wameanza kukusanya taarifa kutoka kwa wachezaji wote wawili.

11/10/2022



Trent Alexander-Arnold na Joel Matip wako nje kwa wiki mbili katika pigo lingine kwa Liverpool kabla ya mechi ya Jumapili dhidi ya Manchester City huko Anfield.

Luis Diaz tayari anatarajiwa kuwa nje hadi baada ya Kombe la Dunia kufuatia jeraha la goti alilopata katika mechi ya kichapo cha 3-2 dhidi ya Arsenal siku ya Jumapili.

Hata hivyo, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alifanyiwa uchunguzi baada ya mechi hiyo, ambayo imebaini kuwa hakuna upasuaji utakaohitajika.

Wachezaji wote watatu hawatapatikana huku Liverpool wakiwakaribisha mabingwa City kwenye Uwanja wa Anfield siku ya Jumapili, wakiwa nyuma ya kikosi cha Pep Guardiola kwa pointi 13 huku wakiwa na mchezo mkononi.

  Mwenyekiti wa Wolves Jeff Shi amesafiri kwa ndege hadi Uhispania kwa mazungumzo na Julen Lopetegui kuhusu nafasi ya me...
11/10/2022



Mwenyekiti wa Wolves Jeff Shi amesafiri kwa ndege hadi Uhispania kwa mazungumzo na Julen Lopetegui kuhusu nafasi ya meneja iliyoachwa wazi.

Lopetegui ndiye mgombea nambari moja wa Wolves ambaye alivutia uongozi wa klabu hiyo walipozungumza naye kwa mara ya kwanza kuhusu kuwa meneja wao mwaka 2016.

Lopetegui mwenye umri wa miaka 56 aliachishwa kazi na Sevilla wiki iliyopita na sasa yuko huru kupatikana iwapo atataka kazi hiyo.

 A.Madrid wamekamilisha usajili wa Antoine Griezmann kwa mkataba wa miaka 4 wenye thamani ya €20M na €4M za nyongeza.Bar...
10/10/2022



A.Madrid wamekamilisha usajili wa Antoine Griezmann kwa mkataba wa miaka 4 wenye thamani ya €20M na €4M za nyongeza.

Barcelona walikuwa wamemsajili miaka 3 iliyopita kwa €120M.

 Jamal Musiala amepimwa na kukutwa na COVID-19.Fowadi huyo wa FC Bayern anaendelea vizuri na kwa sasa anajitenga nyumban...
10/10/2022



Jamal Musiala amepimwa na kukutwa na COVID-19.

Fowadi huyo wa FC Bayern anaendelea vizuri na kwa sasa anajitenga nyumbani.

 West Brom imemtimua meneja mkongwe Steve Bruce baada ya kuhudumu kwa miezi 8 kufuatia misukosuko katika michuano hiyo a...
10/10/2022



West Brom imemtimua meneja mkongwe Steve Bruce baada ya kuhudumu kwa miezi 8 kufuatia misukosuko katika michuano hiyo ambayo imeiacha klabu hiyo kwenye eneo la kushushwa daraja.

Kocha wa vijana wa chini ya miaka 21 Richard Beale atasimamia masuala ya kikosi cha kwanza kwa muda, akisaidiwa na James Morrison na Gary Walsh.

Mchakato wa kuajiri Meneja mpya sasa unaendelea na uteuzi utathibitishwa kwa wakati ufaao.

 Brighton wametangaza kuwa nyota wa Zambia Enock Mwepu amelazimika kustaafu akiwa na umri wa miaka 24 kufuatia kugunduli...
10/10/2022



Brighton wametangaza kuwa nyota wa Zambia Enock Mwepu amelazimika kustaafu akiwa na umri wa miaka 24 kufuatia kugundulika kuwa na ugonjwa wa kurithi wa moyo.

Hali hiyo, ambayo inaweza kuwa mbaya zaidi baada ya muda, itamweka Enock katika hatari kubwa ya kupata mshtuko mbaya wa moyo ikiwa ataendelea kucheza.

 Klabu ya Arsenal bado inazidi kuselelea kileleni mwa jedwali la EPL kwa alama 24 baada ya kuwapepeta Liverpool mabao 3-...
10/10/2022



Klabu ya Arsenal bado inazidi kuselelea kileleni mwa jedwali la EPL kwa alama 24 baada ya kuwapepeta Liverpool mabao 3-2 dimbani Emirates.

Man City, Spurs, Chelsea na Man United wanawafuata unyo unyo kwa alama 23, 20 16 na 15 mtawalia na kufunga kikundi cha tano bora.

Address

Nairobi

Telephone

+254780965500

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Michezo Online News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share