IBUKA FM RADIO

IBUKA FM RADIO Ibuka FM ni redio ibuka katika shirika la Popular News MEDIA ambayo itakujuza masuala yote ibuka, ikufahamishe, ikuelimishe na ikupe burudani tosha!

This page is specifically designed for matters as encouragement, empowering and motivation. No insults or hate speech.

04/12/2025

🌟 LIVE VIRTUAL WORKSHOP! 🌟
Attention Senior & Junior School Parents!
Don’t miss out on this insightful and eye-opening conversation happening LIVE right here on the Ibuka FM page on Saturday, 6th December 2025 2pm-5.30pm.

You’ll also have a chance to join the discussion and be heard LIVE via a Google Meet link!

🎓 Senior School Transition is a timely and important topic—
So let’s talk, let’s interact, let’s ask questions, and let’s get guided!

👉 Mark your calendars!
👉 Invite other parents!
👉 Be part of the conversation!

04/12/2025

Yesu haya ni matendo yako ゚viralシfypシ゚viralシalシ

HAWAKO!// Fununu za upungufu wa walimu katika shule za ngazi ya Senior umezua  tumbo joto huku wataalam katika elimu wak...
04/12/2025

HAWAKO!// Fununu za upungufu wa walimu katika shule za ngazi ya Senior umezua tumbo joto huku wataalam katika elimu wakipendekeza kwamba mfumo unaotumika katika vyuo — yaani kuhudumia masomo kwa zamu au part-time — uingizwe katika shule za “senior school” hasa katika masomo maalum k**a sayansi (STEM), kazi za ufundi na sanaa — ambapo walimu wenye ujuzi wa kuhudumia masomo haya ya kitaalamu ni wachache, Hii itaruhusu walimu/wahadhiri wenye ujuzi maalum (mfano katika STEM, mandarin, sanaa, ufundi, michezo na maudhui ya vocational.) kushiriki masomo bila hitaji la ajira kamili. Wataalam hao pia wameonya kuwa kuwalazimisha walimu wa kawaida au waliohitimu hivi karibuni kufundisha masomo mengi kwa wakati mmoja kutaathiri ubora wa elimu na utekelezaji kamili wa mkondo wa Senior School. Duru zimedokeza kuwa tayari kuna uhaba wa aghalabu walimu elfu 58,590 katika shule za ngazi ya 'Senior School nchini.

//UTALIPA UMALIZE NA ULIPE TENA HALAFU UPOTEZE! Malamishi kuhusu mikopo ya shylock yazua wasiwasi na maswali mengi.  Map...
03/12/2025

//UTALIPA UMALIZE NA ULIPE TENA HALAFU UPOTEZE! Malamishi kuhusu mikopo ya shylock yazua wasiwasi na maswali mengi. Mapema leo, Mahak**a ya Nairobi ilitoa hukumu ya kihistoria dhidi ya wakili aliyeuawa Mathew Kyalo Mbobu, na kutangaza kuwa mkataba wa mkopo wenye viwango vya riba kinyume cha sheria na kuamuru kurejeshwa kwa mali yake iliyonyakuliwa na wakopeshaji

03/12/2025

//KUMBE WANAOKUTEGEMEA NI WENGI HIVI? Aliyekuwa naibu wa rais na kiongozi wa chama jipya cha DCP afurahishwa na hatua za Obina Tv .

//WATOTO WANATUULIZA NA SISI HATUJUI!! Baadhi ya wazazi waliozungumza na Ibuka FM mapema leo wanasema kuwa watoto wao wa...
02/12/2025

//WATOTO WANATUULIZA NA SISI HATUJUI!! Baadhi ya wazazi waliozungumza na Ibuka FM mapema leo wanasema kuwa watoto wao wanawauliza iwapo watabebwabebwa k**a wenzao wa K.C.P.E.

30/11/2025

//KUTOKA NDANI KABISA! Jamaa huyo ambaye ameonekana kuwa mchangamfu na mwenye haiba katika sanaa ya usogora kanisani ameusisimua mtandao. Wengi wakisema kuwa hii ni kumtumikia Mungu kutoka ndani ya roho!

30/11/2025

//NA WAKO? //Wakenya wamemuuliza Rais Ruto mtandaoni baada ya kuwashauri vijana waliohitimu umri wa kuoa na kuolewa wafanye hivyo!

//  2025//LIZAR SCHOOL NAIVASHA YAFUNGUA MILANGO KWA WAZAZI WA SENIOR SCHOOL MJINI NGONG–NAIROBILizar School, ambayo mak...
29/11/2025

// 2025//
LIZAR SCHOOL NAIVASHA YAFUNGUA MILANGO KWA WAZAZI WA SENIOR SCHOOL MJINI NGONG–NAIROBI
Lizar School, ambayo makao yake makuu yapo Naivasha, imeendelea kujipambanua k**a taasisi inayotanguliza maandalizi bora ya wanafunzi na kutoa matokeo ya juu kitaaluma. Kwa miaka mingi, shule hii imekuwa kwenye ramani ya matokeo bora ya K.C.P.E, ambapo idadi kubwa ya wanafunzi wake wamekuwa wakijiunga na shule za kitaifa.
Kupitia ukurasa wao wa Facebook jioni hii, uongozi wa Lizar School umewaalika wazazi wote katika mkutano maalum utakaofanyika kesho tarehe 30/11/2025 katika CITAM Ngong Town. Mkutano huo umeandaliwa kwa lengo la:
• Kuwapa wazazi uelewa kwa upana kuhusu mwelekeo wa Senior School;
• Kujibu maswali mbalimbali kutoka kwa wazazi wanaotaka kupata ufafanuzi zaidi;
• Kuwajulisha kuhusu miundombinu mipya iliyowekwa na Lizar School
• Kueleza njia za kitaaluma (pathways) ambazo shule imeamua kuendeleza katika ngazi ya Senior School.
Lizar School imehimiza wazazi kujitokeza kwa wingi ili wapate taarifa sahihi kuhusu maandalizi hayo muhimu kwa watoto wao. Haijabainika wazi iwapo uhamasisho huo utakuwa mubashara.

27/11/2025

WALITOA BRIFIKESI MBILI NA WAKACHOMA// Gari lenye dhamani ya pesa nyingi linaloaminika kumilikiwa na kiongozi maarufu nchini limeteketezwa na wahuni katika kituo cha kibiashara cha Chebwayi eneo bunge la Malava katika mshike mshike wa uchaguzi mdogo unaoendelea leo.

MSIBA MARA TISA// Familia moja magharibi ya Kenya eneo la Webuye Sango imegubikwa na simanzi  baada ya watu wanane wa fa...
26/11/2025

MSIBA MARA TISA// Familia moja magharibi ya Kenya eneo la Webuye Sango imegubikwa na simanzi baada ya watu wanane wa familia moja waliokuwa wakisafiri kuhudhuria mazishi ya nyanya yao mkongwe kupata ajali mbaya kwenye baraste ya Nakuru-Nairobi. Wakenya wamekuwa na huzuni na hisia tata

24/11/2025

//GIVE IT TO ME OR DIE! Raia huyo wa kigeni kwenye video alionekana akimpapasa yule dereva wa teksi kabla ya kumkapa koo. Wakenya wamehuzunika na kisa hicho japo duru zinadokeza kuwa kisa hicho kimefanyika ughaibuni...

Address

Nairobi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IBUKA FM RADIO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to IBUKA FM RADIO:

Share