04/09/2026
...MATESO YAKO SI YA BURE. Warumi 5:1-5
Basi, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo. Kwa kupitia kwake tumepata njia ya kufikia neema hii ambayo inatuwezesha kusimama imara, tukifurahia tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu. Zaidi ya hayo, pia tunafurahia mateso yetu kwa sababu tunafahamu kuwa mateso huleta subira na subira huleta uthabiti wa moyo na uthabiti wa moyo hujenga tumaini. Tukiwa na tumaini hatuwezi kukata tamaa kwa sababu Mungu amekwisha kumimina upendo wake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ni zawadi tuliyopewa na Mungu. Kupitia kwa changamoto unazopitia Mwana Ligi, Mungu anapata nafasi ya kukutengeneza. Anatengeneza imani, subira na unakuwa mtu ambaye si wa kukata tamaa. Kuna watu ambao ni wa kukata tamaa mbio sana sababu kuna darasa hawajapitia. Kubali hayo mateso yakutengeneze. Tukutane Galilaya!
Mama Taifa Evah Mwalili
Follow Radio 47 page: https://igit.me/lMsI3
X: x.com/Radio47_Kenya
TikTok: https://igit.me/wHdwb
Instagram: https://igit.me/x07C7
YouTube: https://m.youtube.com/
Join WhatsApp channel: https://rb.gy/iwp64y
Watch shows LIVE: www.radio47.fm