Kamulungu Tv

Kamulungu Tv NEWS | DIGITAL ADVERTISEMENTS | SPECIAL AND EXCLUSIVE INTERVIEWS | ENTERTAINMENT

Kamulungu Tv - Umo Wa Mukamba

Guess the Celebrity 🤣🔥🔥🔥
08/05/2026

Guess the Celebrity 🤣🔥🔥🔥

🔥🔥🔥🔥
08/05/2026

🔥🔥🔥🔥

President William Ruto is set to address the Tanzanian Parliament today at 11.00 am.
05/05/2026

President William Ruto is set to address the Tanzanian Parliament today at 11.00 am.

Kitui 2027 mnapea nani Governor?
04/05/2026

Kitui 2027 mnapea nani Governor?


TWATAKA HAKI KWA WALIOUAWA TSEIKURU, GAVANA MALOMBE!By Kamulungu Tv TeamGavana wa kaunti ya Kitui Dkt. Julius Malombe am...
02/05/2026

TWATAKA HAKI KWA WALIOUAWA TSEIKURU, GAVANA MALOMBE!

By Kamulungu Tv Team

Gavana wa kaunti ya Kitui Dkt. Julius Malombe ametoa wito kwa vyombo vya kiusalama kuimarisha usalama ipasavyo kwenye maeneo ya mpakani mwa kaunti za Kitui na Tana River huku akilaani mauaji ya watu saba yaliyoshuhudiwa hivi maajuzi katika eneo la Kwa Kamari, kwenye wadi ya Tseikuru Mwingi kaskazini katika kaunti ya Kitui.

Malombe aliyasema haya hii leo kwenye hafla ya misa ya wafu ya saba hao iliyofanyika katika shule ya msingi ya Tseikuru kuko huko Mwingi kaskazini akitaka haki kwa familia zilizopoteza wependwa wao.

Haya yanajiri huku viongozi tofauti waliohudhuria hafla hiyo wakizidi kulaani kisa hicho cha kinyama huku wenyeji wakiishi kwa woga wa kuvamiwa kufuatia kisa hicho cha uvamizi wa awali.

End.

MISA YA WAFU TSEIKURU!!! By Kamulungu Tv TeamMisa ya wafu kwa watu saba waliouawa   na watu wanaokisiwa kuwa walisha nga...
02/05/2026

MISA YA WAFU TSEIKURU!!!

By Kamulungu Tv Team

Misa ya wafu kwa watu saba waliouawa na watu wanaokisiwa kuwa walisha ngamia katika eneo la Kwa Kamari kwenye wadi ya Tseikuru, katika eneobunge la Mwingi Kaskazini katika kaunti ya Kitui wiki iliyopita, imefanyika hii leo katika shule ya msingi ya Tseikuru kwenye soko la Tseikuru huko Mwingi kaskazini.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na gavana wa kaunti ya Kitui Dkt. Julius Malombe, Mwakilishi wa k**e katika kaunti hiyo ya Kitui Dkt. Irene Kasalu, mbunge wa eneobunge hilo la Mwingi kaskazini Mhandisi Paul Nzengu, mawaziri kadhaa kutoka kaunti ya Kitui kati ya viongozi wengine.

End.

KALONZO ALAANI MAUAJI TSEIKURU! By Kamulungu Tv TeamKinara wa chama cha Wiper Dkt. Stephen Kalonzo Musyoka amelaani kisa...
30/04/2026

KALONZO ALAANI MAUAJI TSEIKURU!

By Kamulungu Tv Team

Kinara wa chama cha Wiper Dkt. Stephen Kalonzo Musyoka amelaani kisa cha kuuliwa kwa wananchi 7 katika soko la Kwa Kamari kwenye wadi ya Tseikuru kule Mwingi kaskazini, katika kaunti ya Kitui Jumamosi lililopita.

Aidha, kinara huyo wa Wiper kwenye kikao na wanahabari hii leo Alhamisi pale SKM Command Centre jijini Nairobi, amemuomba Inspekta jenerali wa polisi Douglas Kanja kuwatuma maafisa wa polisi katika vituo vya polisi vilivyojengwa na serikali ya kaunti ya Kitui kwenye mpaka wa Kitui na TanaRiver.

End.

MADUKA YAPORWA MJINI MWINGI KITUI, MAANDAMANO YAKICHACHA!!! By Kamulungu Tv TeamMaduka kadhaa ya wafanyibiashara wenye a...
29/04/2026

MADUKA YAPORWA MJINI MWINGI KITUI, MAANDAMANO YAKICHACHA!!!

By Kamulungu Tv Team

Maduka kadhaa ya wafanyibiashara wenye asili ya kisomali mjini Mwingi katika eneobunge la Mwingi ya kati katika kaunti ya Kitui hii leo mchana yalivunjwa na bidhaa zote zilizokuwa ndani zikabebwa na wananchi waliokuwa wakiandamana mjini Mwingi, waandamanaji hao wakilalamikia kuuawa kwa wananchi wa jamii ya Akamba na walisha ngamia mpakani mwa kaunti ya Kitui na ile ya Tanariver siku za hivi maajuzi.

Wakati uo huo barabara zote zilifungwa huku waandamanaji hao mjini Mwingi wakichunguza kwa makini endapo kuna gari lolote lililombeba abiria mwenye asili ya kisomali au hata dereva mwenye asili hiyo huku maafisa wa usalama wakiwa ange kudhibiti hali.

End.

Address

Nairobi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kamulungu Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kamulungu Tv:

Share