IMELA SHOW

IMELA  SHOW Imelashow is a gospel show which brings together all its audience together as a family.

  is a gospel show which bring together all its funs and other people together as a family. IMELA means thank you God i therefore invite you for this wonderful show every Sunday from 7pm to 10pm.

06/07/2025
15/04/2025

Leo tunazungumzia UAMINIFU KATIKA NDOA.

13/04/2025

Leo ni Jumapili ya Mtende, siku ambayo Wakristo duniani hukumbuka kwa shangwe kuu kuingia kwa Yesu Kristo katika mji wa Yerusalemu.

Alikuja si kwa farasi wa kifalme, bali kwa mwana-punda — ishara ya unyenyekevu, amani, na upendo.
Watu walimtandika mavazi yao, wakamtupia matawi ya mitende njiani, wakisema kwa sauti kuu:
“Hosana! Abarikiwe ajaye kwa jina la Bwana!”

Lakini pia ni siku ya kutafakari.
Kwa sababu wale waliompokea kwa shangwe… baadaye wengine walipaza sauti zao wakisema, “Msulubishe!”
Ni ukumbusho kwetu kwamba mioyo ya watu hubadilika — lakini upendo wa Mungu hubaki thabiti.

Jumapili ya Mtende hutufundisha kuwa:
🕊️ Unyenyekevu ni nguvu, si udhaifu.
🕊️ Yesu anapokuja katika maisha yetu, si kwa kishindo cha dunia — bali kwa upole unaobadilisha ndani.
🕊️ Na kuwa na Yesu hakumaanishi kutembea bila dhiki, bali ni kuwa na amani hata katikati ya mateso.

Wiki Takatifu inaanza leo.
Ni safari ya kiroho kuelekea Msalabani — na hatimaye, kwenye tumaini la Ufufuo.
Hebu tujiandae, kimwili na kiroho. Tuwe tayari kupokea mfalme wa amani katika maisha yetu, familia zetu, na taifa letu.

16/02/2025

Kuna ahadi nyingi za Mungu katika Maandiko. Katika kila ahadi, Mungu anaahidi kwamba jambo fulani litafanyika (au halitafanyika) au litapeanwa au kutimia. Hizi sio ahadi duni, ahadi za kawaida k**a vile tunavyofanya mara nyingi; ahadi hizi za Mungu ni ahadi thabiti, ahadi zisizo na shaka zilizotolewa na Mungu mwenyewe. Kwa sababu Mungu ni mwaminifu

16/02/2025

Good morning na karibu kwenye kipindi hewani na Jumapili ya Baraka karibu tubarikiwe pamoja.
Tunajua Mungu anapenda kuwabariki watu. Hata anawapa mvua kwa wenye haki na wasio haki. Anapenda kubariki kadri anavyoweza. Baraka moja tunayopokea, kwa mfano, ni uvumilivu na subira yake – hata kuwapa wanadamu karne kadhaa wakati mwingine ili watubu kabla ya kuwahukumu, inajulikana sana. Anapenda kufanya mambo kwa watu. Mungu anapenda kubariki na KUWA baraka. Sasa fikiria hili: anasema pia anataka sisi tuwe k**a Yeye na anafanya iwezekane kupitia roho yake ndani yetu.

13/02/2025

It is and too karibu ndani ya kipindi hewani kuanzia 7.00pm hadi 10.00pm uweze kupata uhondo na burudani. Unawakilisha maeneo gani leo hii?.

09/02/2025

Good evening how was your Sunday, karibu ndani ya kipindi naye
tumshukuru Mungu kwa umbali huu ametufikisha, ni hapa ndani ya 99.9 Radio Domus Fm

09/02/2025

AMETUONA MUNGU NIO MAANA TUNAMPA SIFA NA UTUKUFU

26/01/2025

Jioni nyingine ya kushukuru Mungu na amekuwa wa rehema Maishani mwetu karibu ndani ya kipindi hewani na na tuweze kubarikiwa pamoja.
leo niko na wasanii wa nyimbo za Injili.
una swali gani kwao SMS/WHATSAPP NI 0794468768

26/01/2025

Je, Mungu ananipenda kweli?
Mara nyingi tunaambiwa kwamba “Mungu anakupenda” na “Mungu ni upendo”. Lakini je, hiyo ni kweli? "Upendo" wake uko wapi tunapokutana na nyakati ngumu? Ninawezaje kuwa na uhakika kwamba Mungu ananipenda kweli?
Mawazo ya aina hii yanapotokea, jambo bora zaidi kufanya ni kwenda kwa Neno la Mungu.

19/01/2025

VITA UNAVYOPITIA MAISHANI VINAKUIMARISHA. USIOGOPE.

12/01/2025

Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu mwingi wa huruma na neema. Mvumilivu na mwingi wa upendo na kweli Zaburi 86:15.
Tazama kuwa Biblia haisemi Mungu ana huruma, ambacho kingekuwa kizuri, ila inasema Mungu amejaa huruma.

JE! NITUMIE MBINU GANI KUPIGANA NA KUSHINDA VITA VYA KIROHO? 1️⃣Kila vita unayoiona kwenye ulimwengu wa mwili, imeanzia ...
05/01/2025

JE! NITUMIE MBINU GANI KUPIGANA NA KUSHINDA VITA VYA KIROHO?
1️⃣Kila vita unayoiona kwenye ulimwengu wa mwili, imeanzia kwenye ulimwengu wa roho.(Waefeso 6:12)
✅Kwakuwa vita huwa inaanzia rohoni,hivyo usipende kupigana kimwili. Utashindwa tu.
Shughulika na chanzo(source), ili upate utatuzi wa kudumu.
2️⃣Hakuna mtu duniani ambaye hana maadui,hivyo kila mtu ana vita yake.
✅Ndio maana hakuna mtu ambaye anakubalika na watu wote dunia nzima.
✔️Mungu aliye hai mwenyewe hakubaliki na wanadamu wote. Wengine wanamkataa kabisa kabisa(Yohana 1:11). Sembuse wewe mpendwa wangu?
3️⃣Kinachotofautiana kati ya mtu na mtu kuhusu vita na maadui, ni idadi ya maadui,majira na aina ya vita wanazokutana nazo.
✅Wewe unapopigwa vita eneo fulani, unakuta mwenzako anapigwa vita eneo lingine, yaani tofauti na lako.
✔️Wewe unapopigana vita kipindi fulani,unakuta mwenzako ndio anapumzika kipindi hicho au bado haijainuka vita juu yake.
4️⃣Thamani ya ulichobeba ndani yako(ulichobebeshwa na Mungu kwenye maisha yako) ndicho kinachoongeza ukubwa wa vita yako.
✅Hivyo usijaribu kujilinganisha vita yako na ya mtu mwingine, kwasababu hamfanani. Usiseme "why me?"
5️⃣ Shetani anapokupiga vita, ujue kabisa kwamba anawinda ulichobeba ndani yako.
✍️Shetani hawezi kutumia nguvu nyingi na muda mwingi kupambana na wewe k**a hakuna kitu cha thamani alichoona ndani yako.
Angalia mfano wa Rahabu yule kahaba,angalia mfano wa Sauli(Paulo) n.k
6️⃣Mungu anaporuhusu vita ije kwako,huwa anakuwa amekusudia kukusogeza karibu na yeye na pia kukuimarisha kiimani.
✔️Yakobo 1:1-4, Ayubu 23:10
Daudi alikutanishwa kwanza na simba na dubu,kabla ya kupambanishwa na Goliathi.
7️⃣Shetani anapoinua vita juu yako,huwa anakusudia kukuweka mbali na Mungu na kukuondoa kwenye mstari.
✅K**a kuna kitu ambacho Mungu amekupa ukifanye ili kiwe mkondo wa kupitishia baraka kuja kwenye maisha yako,basi shetani atahakikisha unaacha kufanya hicho kitu.(Yohana 10:10)
8️⃣ Kadri unavyozidi kumjua Mungu katika maisha yako, na neema yake inavyoongezeka juu yako, ndivyo ambavyo aina ya maadui inavyobadilika.
✅Kabla haujaokoka unakuta ulikuwa na maadui ambao hawajaokoka, ukiokoka uwe na uhakika kwamba bado utapigwa vita na wenzako waliookoka. Utapigwa tu vita na wapendwa wenzako.
9️⃣Eneo lolote uliloitiwa na Mungu kwenye maisha yako, lina vita yake.
♨️K**a ni Muhubiri,utakutana na vita kutoka kwa Wahubiri wenzako.
K**a ni Mwimbaji,utakutana na vita kutoka kwa Waimbaji wenzako.
K**a ni mfanya biashara,utakutana na vita kutoka kwa Wafanya biashara wenzako.
K**a ni Mfanyakazi,utakutana na vita kutoka kwa Wafanyakazi wenzako.
K**a ni kiongozi,utakutana na vita kutoka kwa viongozi wenzako.
✔️Pia tambua kuwa vita nyingine utakutana nayo kutoka kwa watu tofauti na wito wako.
1️⃣0️⃣Ni hatari sana kutojipanga mapema kukutana na vita ya nyumbani mwako(watu wa karibu na wewe).
✅Biblia iko wazi kabisa kwamba adui wa mtu niyule wa nyumbani mwake (Mathayo 10:36).
Vita inayotoka nyumbani mwako ndio vita mbaya zaidi. Yusufu alipigwa vita na ndugu zake wa damu. Kwahiyo,jipange mapema kwamba vita ya nyumbani mwako ipo na inakupasa kushinda.
1️⃣1️⃣Vita huwa inakuja kwa sura tofauti tofauti,na sio kwa sura moja tu.
Inaweza ikaja kwa sura ya;
✓Kukataliwa
✓Kudharauliwa
✓Kusingiziwa
✓Kutengwa/kubaguliwa n.k
❌Hivyo,usitegemee kwamba vita itakuja tu kwa namna ulivyozoea.
1️⃣2️⃣ Ni hatari sana kumuweka Mungu aliye hai pembeni na kuanza kupigana vita kimwili(kupigana kwa kutumia nguvu zako mwenyewe).
✅Watu wengi waliookoka nimeona wakipigwa kwasababu tu ya kumuweka Yesu pembeni.
Nakushauri,kamwe usije ukaruhusu neno hili likaingia kwenye maisha yako, "Navua kwanza Wokovu/Wokovu naweka kwanza pembeni ili nipambane na mtu fulani".UTAPIGWA TU.Wokovu hauendi hivyo.
1️⃣3️⃣Usipigane vita kwa mazoea, usikimbilie kumdharau mpinzani wako, na wala usipigane vita kwa kutegemea uzoefu wako.
✅Goliathi alipigwa na kijana Daudi,kwa makosa hayo(1Samweli 17:1..).
Mungu hatuelekezi kwa habari ya kumdharau shetani,ila anatuahakikishia kwamba tukimkaribia yeye,basi tunakuwa na uhakika wa kumshinda shetani(Yakobo 4:7).
❌Hakuna mwanadamu ambaye ana uwezo wa kupigana na shetani kwa kutumia nguvu zake mwenyewe.
1️⃣4️⃣Usipende kuingilia vita ambayo haikuhusu, na Mungu aliye hai hajakuruhusu kuingilia.
✅Watu wengi wa Mungu wanapenda kuingiliavita ambazo haziwahusu,na matokeo yake ni kwamba vita zinawageukia wao,na zinawaelemea.
✅Biblia inakataza kuingilia vita ambayo haikuhusu na Mungu hajakuruhusu uingilie. (Mithali 26:17)
1️⃣5️⃣ Vita inapokulemea,usitafute tafute tu msaada kienyeji,kwasababu unaweza ukamshirikisha adui mwingine vita uliyonayo.
✅Sasa hapo kutakuwa na shida kubwa zaidi,kwasababu utafikiri anakusaidia,kumbe anakupa mbinu za kuhakikisha unashindwa(Mithali 27:6).
✔️Omba msaada wa Mungu aliye hai ili akuongoze mahali pa kupata msaada.
1️⃣6️⃣Unapopitia vita kwenye maisha yako,usiruhusu uchungu na hasira vitawale moyo wako.
✅Hivyo vitu ni hatari sana, kwasababu vinamfanya Mungu aliye hai akae mbali na wewe na hivyo inakuwa ni rahisi zaidi maadui kukushambulia.
Ayubu 21:25
1️⃣7️⃣Kadri unavyokaribia kupokea muujiza wako kutoka kwa Mungu aliye hai,ndivyo vita yako inapoongezeka.
✅Ukiona vita inaongezeka kwenye huduma yako,kazi yako,biashara yako, ndoa yako n.k, UJUE MUUJIZA WAKO UPO KARIBU.
✅Kwahiyo, unapoona vita inaongezeka usife moyo,usikate tamaa, ila tambua kuwa kuna kitu kuzuri kinakuja mbele yako na shetani amekiona ndio maana anakupiga sana vita ili upishane nacho.
1️⃣8️⃣Kadri vita inavyozidi kuongezeka, mkaribie zaidi Mungu, badala ya kukata tamaa na kujitenga na Mungu.
✅Mkaribie zaidi Bwana wa vita(Kutoka 15:3)
Unapogigana vita,na adui akaona umemshinda, huwa anakaa pembeni kwa muda na kukusubiri saa ukichoka, yaani umekuwa dhaifu.
2Samweli 17:2
1️⃣9️⃣Unapopigana vita vya kiroho,uwe mwangalifu sana mwilini pia.
✅Shetani akishindwa rohoni huwa anakimbilia mwilini. Kuwa makini huko barabarani unakopita kwasababu unaweza ukakuta unagongwa na gari au pikipiki.
Kabla ya kuanza vita yoyote ile, jitahidi kuomba ulinzi wa damu ya Yesu kwa ajili yako,kazi yako,biashara yako,ndoa yako,masomo yako,familia yako.
✔️Usipofanya hivyo, shetani ataenda kushambulia maeneo hayo wakati wewe unapigana nae eneo lingine.
2️⃣0️⃣Vita inapokuja kwako kwa kupitia mtu yeyote yule,usimtazame huyo mtu yeye k**a yeye kwa kuangalia nafasi yake,ila mtazame kwanza shetani alipita kwake.
✅Yesu alimuona shetani akiingia kwenye mawazo ya Petro na akamwambia rudi nyuma yangu shetani(Mathayo 16:23, Marko 8:33). Hakumwambia rudi nyuma yangu Petro,kwasababu alijua kuwa shetani kamwingia Petro.
✅Shetani anaweza akapita kwa mume wako,mke wako,rafiki yako,ndugu yako,mtumishi mwenzako.
Kumbuka: Mtu wa karibu na wewe ndio rahisi zaidi kutumiwa na adui,kuliko mtu ambaye hauna ukaribu nae.
2️⃣1️⃣Katikati ya vita unayopitia,usiache kufanya kitu ambacho Mungu aliye hai amekuitia kufanya katika maisha yako.
✔️Wewe fanya kwa nguvu zako zote na kwa uaminifu mkubwa.
✅Mara nyingi adui anapoinua vita juu yako huwa anataka kukupotezea muda wako.
✅Tambua kuwa, sio kila vita unatakiwa kupigana, hasa vita ya maneno. Utapoteza muda wa kumzalia Mungu matunda katika maisha yako na pia utamtenda tu Mungu wako dhambi(Mithali 17:19).
📝Naomba uyakumbuke hayo mambo 21 kila siku katika maisha yako. Yaandike kwenye vibao vya moyo wako.
📌K**a upo kwenye vita kali,nakuombea kwa Bwana Yesu, ILI USHINDE HIYO VITA NA MUNGU ALIYE HAI ATUKUZWE KUPITIA WEWE, NA K**A UMECHOKA NAKUOMBEA UPEWE NGUVU MPYA(ISAYA 40:31), NA K**A UMEISHIWA MBINU BASI NAKUOMBEA ILI BWANA YESU AKUPE MBINU MPYA ZA KUWASHINDA MAADUI ZAKO.
📌Oooh! Yote katika yote,tambua kuwa MUNGU ALIYE HAI HUWA ANAANDAA MEZA MBELE YA WATESI WAKO(ZABURI 23:5),HUWA HAWAONDOI DUNIANI MAADUI ZAKO,NDIO MAANA KUNA ADUI ZAKO AMBAO ULITAMANI WANGEKUFA NA WENGINE ULIWAOMBEA KABISA ILI WAFE,LAKINI MUNGU AMEWAACHA HAI HADI SASA.
🖍️Mpendwa wangu katika Kristo Yesu,siku zote elewa kuwa,K**A HAKUNA MAADUI,BASI HAKUNA KUANDALIWA MEZA.
♿Je! Unataka Mungu aandae meza mbele yako na kikombe chako kifurike baraka zake?, k**a jibu lako ni ndio, basi maadui ni lazima ukutane nao.
💪💪Siku zote tukiwa ndani ya Kristo,TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA,KWAKE YEYE ALIYETUPENDA.
Mungu akubariki Sana!

NIMEPEWA KUSHINDA NA MUNGUMungu anavyokutazama wewe ni tofauti na binadamu wakutazamavyo, upo mtazamo ambao umejiwekea k...
05/01/2025

NIMEPEWA KUSHINDA NA MUNGU
Mungu anavyokutazama wewe ni tofauti na binadamu wakutazamavyo, upo mtazamo ambao umejiwekea kwenye maisha yako lakini Mungu ana mtazamo wake juu yako, Mtu wa ndani wa Daudi aliona ushindi japokùwa hakuwa na silaha yoyote ya kupigana vita.
Sauli alipewa kushinda mbele ya adui zake wote, Je wewe ni nani au nini kilichokushinda? Je ni maisha yanakuhubiria kushindwa?
Mungu akupe kushinda kila unapokwenda kwa jina la Yesu, Biblia inasema Daudi alipewa kushinda vita kila njia aliyoiendea, japokuwa hakuwa na mafunzo ya vita alipigana vita vilivyowashinda wengine. 2Samwel 8:6 "14

Unataka Mungu akufanyie nini Mwaka wa 2025 na akifanya utamshukuru kiaje?
29/12/2024

Unataka Mungu akufanyie nini Mwaka wa 2025 na akifanya utamshukuru kiaje?

29/12/2024

Kila mtu aliyepata kuishi amenufaishwa na wema wa Yehova. Zaburi 145:9 yasema: “BWANA ni mwema kwa watu wote.” (Italiki ni zetu.) Ni mifano ipi inayoonyesha kwamba wema wake unamnufaisha kila mtu? Biblia inasema hivi: “Hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa nyinyi mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamfu.” (Matendo 14:17) Je, umewahi kufurahia chakula kitamu? Hakungekuwa na chakula chochote k**a Yehova hangekuwa mwema na kubuni mzunguko wa maji safi na “majira yenye kuzaa matunda.” Yehova amewatendea watu wote wema, hata wale wasiompenda. Yesu alisema hivi: “Hufanya jua lake lichomoze juu ya watu waovu na wema na kufanya mvua inyeshe juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.”—Mathayo 5:45.

17/12/2024

Ann kutoka kisii amekataliwa na wazazi wake na hajui afanyeje. Anataka ushauri.

LETS DISCUSS TERRITORIAL DEMONS/SPIRITS “Territorial spirits” is a term some Christians use to identify demonic occupati...
27/10/2024

LETS DISCUSS TERRITORIAL DEMONS/SPIRITS

“Territorial spirits” is a term some Christians use to identify demonic occupation of a specific geographic location. Ironically, it is also a term pagans use to describe an otherworldly presence believed to be residing in a specific geographical location.

Kumshukuru Mungu kwa ushuhuda wa matendo yake kwakoKumshukuru Mungu kwa ushuhuda ni kurudi kwenye madhabahu ya Mungu ili...
27/10/2024

Kumshukuru Mungu kwa ushuhuda wa matendo yake kwako

Kumshukuru Mungu kwa ushuhuda ni kurudi kwenye madhabahu ya Mungu iliyotumika kukuvusha ili kumrudishia Mungu utukufu kwaajili ya matendo yake ya ajabu kwenye maisha yako.

MAFUNDISHO KUHUSU MAOMBI“Kisha Yesu akawapa wanafunzi wake mfano ili kuwaonyesha kuwa yawapasa kuomba pasipo kukata tama...
27/10/2024

MAFUNDISHO KUHUSU MAOMBI
“Kisha Yesu akawapa wanafunzi wake mfano ili kuwaonyesha kuwa yawapasa kuomba pasipo kukata tamaa” (Luka 18:1).

Maombi ni jambo la muhimu sana katika maisha ya ukristo. Mambo mengine yote k**a, kusoma Biblia, kuiheshima Siku ya Jumapili, kusikiliza mahubiri, kuenda kanisani na hata kula meza ya Bwana, ni mambo ambayo yanakuja baada ya maombi.
Haya mambo yote ni ya muhimu sana, lakini maombi ni ya muhimu Zaidi.

Mafundisho: KUMSHUKURU MUNGU kwa DHATIKumshukuru Mungu imekuwa utamaduni na taratibu za ibada za dini mbalimbali. Lakini...
20/10/2024

Mafundisho: KUMSHUKURU MUNGU kwa DHATI
Kumshukuru Mungu imekuwa utamaduni na taratibu za ibada za dini mbalimbali. Lakini je! Kumshukuru Mungu kuna maana gani? Au umuhimu wake ni nini? Nimetamani tujifunze hili jambo ambalo Daudi amesisitiza mara nyingi katika Zaburi akisema “nitamshukuru BWANA kwa ajili ya haki yake na nitaliimbia sifa jina la BWANA Aliye Juu Sana” (Zaburi: 7:17) Na pia Daudi anahimiza watu wengine wamshukuru Mungu kwa kusema “Mshukuruni BWANA, kwa kuwa ni mwema, upendo wake wadumu milele.” (Zaburi 118:1)

Kati ya mambo mengi muhimu nataka tuone haya machache kwa ufupi:

i). Huwezi kumshukuru Mungu kwa DHATI k**a HUNA cha kushukuru

K**a kuna jambo gumu ni kushukuru kwa DHATI kwa ajili ya jambo ambalo hulijui. Kwa kweli utabaki kushukuru kwa sababu mtumishi wa Mungu amesema “mshukuruni Mungu” na wewe ghafla unaanza “asante Yesu, asante Yesu, asante Yesu”, lakini hayo maneno yanatoka hapo kinywani tu na wala sio Moyoni kwa sababu ndani ya MOYO wako HUONI kitu Mungu amefanya na ukijaribu kuvuta hisia haziji basi unaanza tu kushukuru k**a kasuku. Ukiangalia hapo pembeni unaona mwenzako anashukuru huku machozi yanamtoka, japo wote wawili mnatamka maneno yale yale “asante Yesu, asante Yesu”. Sasa kuna tofauti ya “asante Yesu” ya kwako na ya mwenzako. Na tofauti haiko katika maneno yenu ila MIOYO yenu. Kumbuka kulia sio ishara ya SHUKURANI ya dhati japo inawezakuwa pia.

Daudi anasema “Msifuni BWANA. Mshukuruni BWANA, kwa kuwa ni mwema, upendo wake wadumu milele. Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya BWANA au kutangaza kikamilifu sifa zake?” (Zaburi 106:1,2) “Mshukuruni BWANA, kwa kuwa Yeye ni mwema, upendo wake hudumu milele. Waliokombolewa wa BWANA na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka katika mkono wa adui, wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.” (Zaburi 107:1-3).

K**a UMEONA wema wa Mungu, Upendo wa Mungu, na Matendo ambayo Mungu amekutendea, ukienda mbele zake kwa kumshukuru, utagundua HUNA maneno ya kusimulia huo ukuu wake, ndio maana watu wengi sana wakianza kumshukuru Mungu kwa DHATI huanza kulia tu. Hebu chukua muda kutafakari mambo MENGI ambayo Mungu amekutendea na nenda mbele zake kwa DHATI kabisa KUSHUKURU tu, sio kuomba, zama katika Moyo wako kushukuru huku ukibeba hayo mambo mbele za Mungu na Roho Mtakatifu atakusaidia kuona kitu Daudi anasema hapa.

ii). Ukubwa wa SHUKURANI zako unategemea UKUU wa Mungu unaouona

“BWANA ni nguvu yangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.” (Zaburi 28:7) Daudi alipita VIPINDI ambavyo aligundua, “kwa kweli hapa sio nguvu zangu ila ni nguvu za Mungu”, alipotizama hayo mambo, anasema “moyo wangu unaruka kwa furaha, nami nitamshukuru Mungu kwa wimbo”. Sasa mafanikio yetu yamekuwa KIKWAZO cha kumshukuru Mungu kwa DHATI kwa sababu mara nyingi tumeona jinsi ambavyo tumefanikiwa kwa JITIHADA zetu au kwa misaada ya watu FULANI. Kila ukitafakari HATUA za maisha yako moyoni unasema “kwanza familia yetu tuna akili sana, wote tunefaulu tu, ndio maana hata sasa nimefaulu”, au “kwa kweli namshukuru sana fulani, k**a asingenilipia ada ungekuta sijasoma”, au “nafahamiana na fulani, naye anacheo kikubwa, ndio maana niliweza kuvuka mahali fulani”, au “kwa kweli nimefanya kazi kwa bidii sana, vyeti vyangu ni vizuri sana, hii nafasi ya uongozi katika ofisi ni halali yangu”, au “ndugu hapa mjini ni kufahamiana, usipomfahamu mtu utapata shida”, nk. Katika MAMBO yote hayo HUKUMWONA Mungu ila NGUVU zako, JITIHADA zako, nk. na ukiambiwa “mshukuru Mungu”, huku ndani unakuwa mkavu sana kwa sababu huoni ni kwa namna gani Mungu amekupitisha hadi hapo ulipo, bali watu na pesa zao, au jutihada zako.

Hebu fikiri Daudi anasema “nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti” na sasa amepita yuko ng’ambo. Hebu fikiri kiwango cha SHUKURANI atakacho kimimina kwa Mungu wake? Sasa kumbuka wakati anapita katika hayo MAGUMU kiasi cha kuona “mauti”, ndani ya moyo wake anapata FARAJA kwa sababu anaona “ulinzi wa gongo na uongozi wa fimbo yake”, anapata furaja japo ADUI wamemzunguka, hadi pale “mezani pake”, anaposema “sasa ngoja nile”, adui zake wapo hapo pia! Na hawamtakii mema, wanataka kumwamngamiza. Mungu anampigania katika hizo HATUA zote na sasa yuko nga’ambo! Hebu fikiri kiwango cha shukurani kwa Mungu ambazo Daudi atamimina? Sasa mara nyingi sana tumefunika macho na masikio yetu, tumejitahidi kwa njia zetu za uovu au akili zetu na tumefanikiwa hapa na pale na hatukumwona Mungu, tunajiona sisi na watu wengine tu. Sasa nisikilize vizuri, hata k**a hukumwona Mungu akikupigania jua hapo ulipo sio wewe mwenyewe na hukufanikiwa kwa nguvu zako. Mwombe Mungu akupe kuona MKONO wake ulivyokupigania ili uweze kuwa na SHUKURANI za dhati mbele zake.

Daudi anasema “Nayainua macho yangu nitazame vilima, msaada wangu utatoka wapi? Msaada wangu hutoka kwa BWANA, Muumba wa mbingu na dunia.” (Zaburi 121:1). Ukiyatizama maneno haya ya Daudi utapata picha ya mtu aliyoko mahali kusiko na watu, peke yake na ametingwa. Sasa usifikiri Daudi alikuwa peke yake kwa jinsi ya mwilini. Lakini Moyo wake ulikuwa umemwelekea Bwana kwa kiwango kwamba anaona MSAADA wake WOTE unatoka kwa Bwana. “akiinua macho anaona milima tu”, sasa hebu fikiri amepanda hiyo milima na yuko “kileleni”, halafu anasogea mbele za Mungu kwa shukurani? Nataka uone tofauti ya shukurani na shukurani ili ujifunze KUMSHUKURU Mungu kwa dhati.

iii). Kuna uhusiano wa KUMPENDA Mungu na kiwango cha SHUKURANI umpazo

Watu wengi sana HUENDA mbele za Mungu kwa MAOMBI kwa bidii sana wakiwa na SHIDA, UHITAJI, VITA, nk. Wakati wakiwa katika KUOMBA na KUFUNGA, huwa wanakuwa WATAKATIFU sana. Wanajitahidi kusoma Neno na kukaa karibu na Mungu. Wakifanikiwa KUPATA walichokuwa wanaomba, wanamshukuru Mungu na kuweka SILAHA chini. Sasa wanashangilia ushindi na kumsahau Mungu wao na wengine kwa KUPITIA hizo NAFASI, VYEO na MALI walizokuwa wanamlilia Mungu, sasa wanamtenda Mungu dhambi. Hakuna tena shukuruni ndani ya mioyo yao sasa ni KIBURI na kuwatizama wengine k**a HAWANA imani!

Kwa upande wa pili, kuna watu wengine pia HUENDA mbele za MUNGU kuomba juu ya mahitaji mbali mbali, vita, cheo, pesa, nk. WANAPOFANIKIWA huuona UKUU wa Mungu na KUMSHUKURU Mungu kwa DHATI kabisa. Yale mambo ambayo Mungu amewafanyia yanawavuta KARIBU zaidi na Mungu. Hayo mambo yanawafanya wanazidisha UPENDO wake kwa Mungu na wanazidi KUMTUMAINI na kutangaza UKUU wa Mungu.

Katika haya makundi mawili ya watu, kiasi cha SHUKURANI zao kwa Mungu kinaathiriwa na UPENDO wao kwa Mungu. Na kinachoonyesha kwamba kundi la kwanza hawampendi Mungu ni matendo yao. Yesu anasema “mkinipenda mtazishika amri zangu”, na pia tunasoma, “tukipenda ulimwengu na mambo yake [uzinzi, tamaa mbaya, nk.], kumpenda Mungu hakumo ndani yetu”. Sasa unajua huwezi kumshukuru kwa dhati mtu usiye mpenda! Na ukimshukuru, utamshukuru kwa muda huo tu mfupi akiwa hapo na akikupa kisogo unasahau habari yake. ILA mtu unayempenda, ULE upendo unawaka kila saa ndani, na unakumbuka yale mambo mazuri aliyokutendea, moyoni kunajaa shukurani kila mara, kwa sababu ya UPENDO!

iv). Sio mambo YANAYOKUFURAHISHA tu yanastahili shukurani

Tunahimizwa na kuambiwa “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” (1Wathesalonike 5:18). K**a kuna wakati mgumu unapoenda mbele za Mungu au unaona kabisa hapa NIMEPIGWA, au nimeshindwa, halafu unaambiwa eti, “shukuru tu maana hayo ni mapenzi ya Mungu!” Ndipo utagundua kwamba hata kushukuru nako kunahitaji IMANI! Hebu tuangalie mfano wa Ayubu kidogo. “Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washik**ana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe. Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena k**a mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.” (Ayubu 2:9,10). K**a kuna mahali ambapo unahitaji IMANI ni pale mambo yanapoenda vibaya halafu “usimtende Mungu dhambi kwa kinywa chako” bali umshukuru. Na Ibilisi anajua hii siri, anapoona umefika mahali pa kuanguka, anakuja k**a mke wa Ayubu, kukuzomea na kukuonyesha “ona sasa umeshindwa hapo na unasema umeokoka?”. Ayubu akaona ni UPUMBAVU tu kumshukuru Mungu wakati ukipata mema ila mabaya yakija haushukuru! Akasema “Bwana alitoa na sasa ametwaa, Jina lake lihimidiwe.” Kumbuka siku zote, shukurani utoayo kwa DHATI katika kipindi k**a hiki cha mapito magumu ina THAMANI kubwa mbele za Mungu kuliko ile shukurani ya kushangilia USHINDI.

v). Kumshukuru Mungu kwa DHATI kunategemea IMANI yako kwa Mungu

Imani ni kuwa na “HAKIKA ya mambo ya jayo na ni BAYANA ya mambo yasiyoonekana”. Huwa nasikia mara nyingi watumishi wengi wa Mungu wanasisitiza kukiri UPONYAJI au MAJIBU ya maombi yako, na hata KUSHUKURU kwamba Bwana ametenda. Nilichogundua ni kwamba k**a huna IMANI ya kwamba UMEPOKEA huwezi kushukuru kwa DHATI. Kumbuka ni vigumu kutafsiri IMANI, ila anayeamini anajua kwamba anaamini au la! Sasa ukifika mahali una MASHAKA ndani yako, kwamba “hayo uliyoomba yamekuwa yako”, ni vyema kushukuru ila nakushauri UENDELEE kuomba hadi utakapo sikia KIBALI cha ndani, ule uthibitisho wa ndani kwama TAYARI imekuwa, sasa hapo endelea kushukuru kwa maana katika hatua hiyo unaweza kumshukuru Mungu kwa DHATI. Sasa sikukatazi kumshukuru Mungu katika HALI zote, ni vyema kabisa kufanya hivyo, ila kuna namna unaenda mbele za Mungu na unasikia “kufunguka huku ndani”, hiyo ni hatua nzuri sana ya kumimina shukurani. Pili, imekupasa kujua KUSHUKURU hakumpindishi Mungu kufanya kitu ambacho hajakusudia kufanya. Kuna idadi kubwa sana ya watu hawasimami katika nafasi zao na kutimiza wajibu wao ila wako busy KUSHUKURU kwa miujiza na ahadi zisizo wahusu wakidhani zitakuwa zao. Uwe na hekima, usipoteze muda. Tafuta uso wa Mungu na tembea katika kusudi lake nawe utafanikiwa na UTAMSHUKURU Bwana Mungu wako aliyekuvusha.

Mungu atusaidie kuona hii siri katika kumshukuru katika mambo yote na tusikose SHUKURANI za DHATI mbele zake kila siku. AMEN.

   inang'oa nanga hadi saa tatu ukiwa naye Keitany Kevin . Ni bible verse gani hukuinua sana.swali kuu la kujiuliza kati...
20/10/2024

inang'oa nanga hadi saa tatu ukiwa naye Keitany Kevin . Ni bible verse gani hukuinua sana.
swali kuu la kujiuliza katika maisha yetu
Wafilipi 1: 6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu”

07/10/2024

Deputy President Rigathi Gachagua Adressing The Nation

06/10/2024

Mgeni wetu amewasili na tunaingia ndani ya ndani ya Radio Domus Fm, Unatupata ukiwa wapi na swali gani unataka kuuliza mgeni wetu

Kesho ndani ya Radio Domus Fm Keitany Kevin atakuwa na Msaani wa Nyimbo za Injili kuanzia saa kumi na mbili.
05/10/2024

Kesho ndani ya Radio Domus Fm Keitany Kevin atakuwa na Msaani wa Nyimbo za Injili kuanzia saa kumi na mbili.

29/09/2024

HESHIMA YAKO IPO KWENYE KUMTAFUTA MUNGU TU
Waamuzi 11:1-3
1 Basi huyo Yeftha, Mgileadi, alikuwa mtu shujaa sana, naye alikuwa ni mwana wa mwanamke kahaba; Gileadi akamzaa Yeftha.
2 Mkewe huyo Gileadi akamzalia wana; na hao wana wa mkewe hapo walipokuwa wamekua wakubwa wakamtoa Yeftha, na kumwambia, Wewe hutarithi katika nyumba ya babaetu; kwa sababu wewe u mwana wa mwanamke mwingine.
3 Ndipo Yeftha akawakimbia hao nduguze, akakaa katika nchi ya Tobu; na watu mabaradhuli walikwenda na kutangamana na Yeftha, wakatoka kwenda pamoja naye.
Kuna vipindi huwezi kuvivuka katika kukua kiroho, kwakua kuna changamoto ambazo ni lazima zikutokee ili uweze kukua kiroho.
Keitany Kevin

SIMAMA KATIKA NAFASI YAKO KUMTUMIKIA MUNGU.MATHAYO 5:11-12Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila nen...
15/09/2024

SIMAMA KATIKA NAFASI YAKO KUMTUMIKIA MUNGU.
MATHAYO 5:11-12
Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.
KARIBU NDANI YA KIPINDI HEWANI NA Keitany Kevin HADI SAA TATU USIKU NDANI YA Radio Domus

I sometimes feel short of being the best, but I never fell short of giving it my best.
11/08/2024

I sometimes feel short of being the best, but I never fell short of giving it my best.

14/07/2024

Kuujua Upendo wa Kristo Yesu alionyesha upendo wa kujidhabihu kwa njia bora sana. Kujidhabihu ni kutanguliza mahitaji na masilahi ya wengine bila ubinafsi.

14/07/2024

KUNA SIRI GANI KWENYE KUSIFU NA KUABUDU

Tumeona asilimia kubwa ya watu ambao wametenda dhambi au kufanya makosa huja kuomba msamaha wakati hali zao za kimaisha ...
30/06/2024

Tumeona asilimia kubwa ya watu ambao wametenda dhambi au kufanya makosa huja kuomba msamaha wakati hali zao za kimaisha zimekuwa mbaya, kwa mfano kupatwa na magonjwa, kufirisika kiuchumi, kufukuzwa kazi, n.k.
Sasa hapa hawa watu wanaosukumwa na matatizo au shida zao kuja kuwaomba msamaha walio wakosea huwa ni vigumu kujua wana maanisha au hawamaanishi, kwani unaweza kuwasamehe lakini baada ya hali yao kuwa nzuri wanarudia Tabia zao zile zile, hivyo Wewe mtoa msamaha kwa watu k**a Hawa, ishi nao kwa makini sana na muachie Mungu maisha yake huyo mtu
Ni vyema mtu ukaomba msamaha ukiwa katika hali yako ile ile uliyomtendea mtu kosa, au ukiwa kwenye hali nzuri, kwani msamaha wako utakuwa na uzito na utaonekana umejinyenyekeza sana tofauti na ukisubiri upatwe na mabaya kwani hapo utaonekana umenyenyekezwa na matatizo. Mara nyingi hiari ya mtu iko kwenye mafanikio yake, k**a yuko kwenye matatizo mara nyingi huwa si hiari yake kufanya maamuzi.

Si kila anayesamehe amesamehe kweli, na si kila anayeomba msamaha huwa anamaanisha.Kusamehe ni kinyume cha kuhukumu. Mtu...
30/06/2024

Si kila anayesamehe amesamehe kweli, na si kila anayeomba msamaha huwa anamaanisha.
Kusamehe ni kinyume cha kuhukumu. Mtu asipokusamehe maana yake ameamua kukuhukumu. Penye msamaha pana kuwekwa Huru, Na mahali pasipokuwepo msamaha pana hukumu.
Mathayo 7:1 "Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi."
Hii ina maana usipo samehe kamwe nawe huwezi kusamehewa. Hii ina maana gani? Kile unachomtendea mwenzio ndicho utakacho tendewa.

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHAMsamaha ni neno linalomaanisha "Kuachilia"Luka 6:37 ".achilieni nanyi mtaachiliwa."Sasa jiulize...
30/06/2024

NGUVU NA FAIDA ZA MSAMAHA
Msamaha ni neno linalomaanisha "Kuachilia"
Luka 6:37 ".achilieni nanyi mtaachiliwa."
Sasa jiulize msamaha ulianzaje!?
Ungana nami Keitany Kevin kwenye kipindi hewani hadi 9pm ndani ya Radio Domus

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IMELA SHOW posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to IMELA SHOW:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share