Syaga Digital

Syaga Digital SYAGA DIGITAL | Digital Stories & Social Media Education | Helping you grow, create & connect online

SURA YA TATU:Baada ya kumaliza kufua nguo za mtoto, mikono ilikuwa imechoka sana. Viganja vilianza kupasuka, na sabuni i...
16/11/2025

SURA YA TATU:

Baada ya kumaliza kufua nguo za mtoto, mikono ilikuwa imechoka sana. Viganja vilianza kupasuka, na sabuni ilikuwa imeikausha ngozi na kuifanya iwashwe. Lakini sikulalamika. Nilijifuta mikono kwa kipande cha kitambaa na nikaingia ndani kumwambia Wakili Gina.

“Mama... nimemaliza kufua,” nilisema kwa sauti ya chini, nimesimama kwenye mlango wa jiko.

Hakuniangalia hata. Macho yako busy kwenye simu yake. “Vizuri. Sasa nenda jikoni ukaoshe sahani zote. Hakikisha sufuria zinang’aa, la sivyo...”

Nikatikisa kichwa na kuingia.

Wakati huo, tumbo langu linaunguruma kwa njaa. Sikuwa nimekula chochote tangu asubuhi. Lakini chakula kilikuwa si kitu cha kwanza kwenye akili yangu. Nilitaka nimalize kila kazi ninayopewa kabla sijakumbana na kelele tena.

Nilimaliza kuosha vyombo, nikasafisha kaunta za jikoni, na kufagia. Hatimaye nikakaa na kula wali uliobaki kwenye sufuria. Ulikuwa wa baridi na hauna ladha, lakini ulikuwa bora kuliko kutokula kabisa. Angalau tumbo langu linapata kitu.

Baada ya kula, nikaenda chumbani kwangu, nikachukua begi la shule, na kuanza kufanya home work. Ilikuwa tayari ni usiku sana, zaidi ya saa nne. Usingizi ulinitesa, lakini nilijilazimisha kumaliza.

Kabla sijalala kwenye godoro langu dogo, nikapiga magoti pembeni ya kitanda na kusali.

“Mungu baba, naomba nilinde tena usiku huu. Tafadhali usiruhusu nipoteze tumaini. Nimechoka, lakini bado naamini kwako. “

Nikazungumza na Mungu k**a rafiki pekee niliyekuwa naye.

Asubuhi iliyofuata, niliamka mapema sana k**a kawaida. Nilifagia sebuleni, nikaweka viti vizuri, nikasafisha mbele ya nyumba, kisha nikaingia jikoni kutayarisha uji wa mtoto. Baada ya kufanya kila kitu, nikajiandaa kwenda shule. Msaidizi wa nyumbani alikuwa amepumzika tu. Sijui labda alikuwa amepewa adhabu, lakini nilifanya kila kitu ili kuepuka matatizo.

Shuleni hakukuwa rahisi pia. Walimu wangu bado walikuwa wanalalamikia maendeleo yangu.

“Ulikuwa mmoja wa wanafunzi wetu bora,” mwalimu wangu wa Kiingereza alisema kwa huzuni. “Tumaini, kuna nini kinachokusumbua?”

Sikuweza kujibu. Nikaangalia chini, kwenye miguu yangu.

Ningewezaje kueleza kuwa usiku wangu nautumia kufua nguo na kudeki? Kwamba silali kwa wakati, moyo wangu umechoka, na akili yangu haina nafasi ya kusoma?

Wakati wa mapumziko, nikakaa peke yangu chini ya mti wa muembe. Rebecca alikuwa ameenda kununua vitafunwa, lakini mimi sikuwa na pesa. Niliangalia juuangani, nikiyafikiria maisha yangu.

Nilirudi nyumbani baadae alasiri. Nilipofungua mlango, nilimuona Bwana Amos—yule aliyewahi kuniita “malikia wake”—amekaa sebuleni anaangalia TV. Nikatabasamu na kukaa karibu yake, nikiamini tutaongea na kucheka k**a zamani.

Lakini hakuniangalia hata.

“Tafadhali Tumaini, niko bize sasa hivi. Sina muda wa kuchezea,” alisema.

Nikasimama taratibu na kuondoka. Machozi yalijaa machoni..
Nikaingia chumbani na kufungua vitabu vyangu. Sikutaka kulifikiria. Nilitaka kusoma na kusahau matatizo yangu.
Mtoto alikuwa na msaidizi wa nyumbani. Nikasikia wanacheka na kucheza.
Lakini amani haikudumu.
Baada ya saa moja, nikasikia mlango wa mbele unagongwa kwa nguvu. Bi Gina alikuwa amerudi kutoka kazini, na kwa sauti ya hatua zake, nikajua kuna jambo. Ilikuwa ni k**a amebeba hasira za ofisini kuja nazo nyumbani.
Nikakaa kimya chumbani kwangu, nikajifanya sijaona. Mara ghafla—

BANG!

Mlango ukafunguliwa kwa nguvu, na kabla sijasema “Shikamoo mama,” kofi moto likatua kwenye shavu langu.

PAAHH!!

Nikapiga yowe na kushika uso wangu.

“Hujasikia nilipokuita?” akafoka.

“S-sikusikia mama... nilikuwa nasoma,” nilijibu kwa kigugumizi, machozi tayari yanatiririka.

Kabla sijamaliza kusema, kofi lingine likaja. PAAHH!!

“Nyamaza! Kwa hiyo mimi muongo? Mtoto wa hovyo kweli wewe! Umeanza kuwa na kiburi ndani ya nyumba yangu, eeh?”

Nikataka kuzungumza, kuomba msamaha, lakini mdomo wangu unatetemeka. Nilikuwa nalia bila kujizuia. Shavu langu lilikuwa linawaka moto. Mwili wangu wote ukawa unatetemeka kwa hofu.

Alinishika kwa mkono na kunivuta hadi jikoni. “Nenda ukaoshe chupa ya mtoto! Msichana mvivu!”

Nilifanya alivyosema, nikiwa bado nalia. Chupa ilikuwa safi, lakini niliiosha tena mara tano ili kuhakikisha.

Nilipokuwa naiosha, nikanong’ona, “Mungu naomba nisaidie... nimechoka... nisaidie...”

Nilipomaliza, nikaenda chumbani kwangu na kufunga mlango kimya kimya. Nikakaa kitandani na kulia k**a mtoto mchanga. Moyo wangu ulikuwa mzito. Uso wangu ulikuwa umevimba. Nafsi yangu haikuwa na amani tena.

Nilitazama darini na kujiuliza, “Kwa nini mimi? Nimekosea nini? Kwa nini nateseka hivi?”

Nikalia hadi usingizi ukanipitia.
Hakuna aliyekuja kuniangalia.
Hakuna aliyeniuliza k**a nipo salama... Kwao, nilikuwa k**a mzigo tu.
Lakini kwangu, bado niliamini kitu kimoja...
Tumaini... Kwa sababu hicho ndicho kitu pekee kilichobaki.

Inaendelea...

SURA YA PILI:Bibi T**i alifika alfajiri moja ya mapema. Alikuwa ni mama yake Wakili Gina, lakini tofauti na binti yake, ...
13/11/2025

SURA YA PILI:

Bibi T**i alifika alfajiri moja ya mapema. Alikuwa ni mama yake Wakili Gina, lakini tofauti na binti yake, moyo wake ulikuwa wa dhahabu. Tangu alipoingia tu ndani ya nyumba, nilihisi k**a nimeanza kupumua tena. Alikuwa mtu pekee aliyeniona binadamu. Kila mara alikuwa ananiulizia, k**a nimekula, na wakati mwingine ananiita chumbani kwake kwa ajili ya kuzungumza. Alinifanya nitabasamu tena, hata k**a ni kwa muda mfupi.

Bibi T**i ndiye aliyekuwa anamhudumia mtoto wao mchanga. Dada wa kazi, kazi yake ilikuwa kusafisha nyumba na kupika tu.

Siku moja asubuhi, nilipokuwa nafanya kazi za shule sebuleni, nilisikia sauti ya Wakili Gina kutoka chumbani kwa mtoto.

“Tumaini! Tumaini!! Njoo hapa haraka!” aliita kwa hasira. Nikakimbia haraka.

“Abee mama,” ingawa alikuwa ameniambia nisiendelee kumuita mama.

“Chukua haya mapuu ya mtoto ukayatupe, wewe mtoto haramu!” alifoka huku ananionyesha daipa chafu.

Niliganda kwa sekunde moja. Kifua changu kilijaa maumivu. Mtoto haramu? Amesema kweli hivyo?

“Gina, umesemaje?” Bibi T**i aliuliza kwa hasira, akainuka kutoka kitandani alikokuwa amelala.

Sikusubiri. Nilichukua daipa haraka na kutoka nje. Mikono yangu ilikuwa inatetemeka, si kwa sababu ya uchafu, bali kwa sababu ya hilo neno. Neno hilo lilinichoma moyo mno.

“Kwa nini umemwita hivyo?” Bibi T**i alimkemea binti yake kwa hasira.

“Mama tafadhali, usianze,” Gina alijibu huku anapepesa macho.

“Unajua huyu binti unayemdhalilisha ndie sababu ya wewe kuwa na mtoto leo? Unakumbuka kabla Tumaini hajaja hapa, ulikuwa unalia kila siku ukitamani mtoto? Umesahau jinsi madaktari walivyokuambia kuwa huwezi kuzaa?”

“Mama, acha hizo hadithi zako. Mungu ndiye aliyenipa mtoto kwa wakati wake, si kwa sababu ya huyu mtoto yatima.”

“Sikiliza Gina,” mama yake akasema kwa sauti ya juu, “Sitakaa kimya nikiangalia unamnyanyasa huyu mtoto na kumuona k**a takataka. Kamwe! Ukimuita mtoto haramu tena, iwe niko hapa au la, utaona nitakachokufanyia. Huyu mtoto ni baraka. Baraka halisi kwenye hii familia.”

Sikuyasikia hayo yote. Nilirudi ndani, lakini nilikuwa nimesimama nyuma ya korido, nasikiliza. Macho yangu yamejaa machozi.

Lakini kwa masikitiko, Bibi T**i alikaa kwa wiki mbili tu. Alipoondoka, mateso yakarudi k**a kawaida.

Shuleni, mambo yalikuwa yanaharibika. Sikuweza tena kuzingatia masomo yangu. Hata kusoma sikutamani tena. Mawazo yangu yalikuwa mbali, ninafikiria jinsi ya kuishi nyumbani. Nilianza kufeli karibia kila somo.

Siku moja, mwalimu wangu wa darasa, Bi Okenge, alinita pembeni.

“Tumaini, kuna nini kinachokusumbua? Ulikuwa na akili sana. Nini kimetokea sasa?”

Nikajitahidi kutabasamu. “Sijui, mwalimu.”

Akatikisa kichwa kwa huzuni na kuondoka.

Hata baba yangu, Bwana Amos, hakujali tena. Hakuangalia hata matokeo yangu. Mtu yule aliyekuwa ananisaidia kazi za shule sasahivi ananiona k**a mzigo..

Rebecca, rafiki yangu wa karibu shuleni, alikuwa anahangaika sana. Siku moja baada ya shule, akaniuliza tena.

“Tumaini,naomba uniambie ukweli. Kuna nini kinachokusumbua?”

Nikamtazama machoni. Macho yake yalikuwa na huruma na upendo. Kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu, nikatamani kuzungumza.

“Mimi si yule unayemfikiria,” nikasema kwa sauti ya kutetemeka. “Sio mtoto wao. Wazazi wangu wa kweli waliniacha nikiwa mtoto mchanga.”

Aliziba mdomo kwa mshangao.

“Nini? Unamaanisha kweli?”

Nikatikisa kichwa. “Nimekuwa nikiishi kwa maumivu. Wale walionichukua, hawanipendi tena. Walinijali hadi walipopata mtoto wao.”

“Oh Tumaini...” Rebecca akanikumbatia kwa nguvu. “Pole sana. Hustahili haya.”

Machozi yakaanza kunitiririka bila kujizuia. Nilikuwa nimeyazuia kwa muda mrefu.

Kilichoniumiza zaidi kilitokea mchana mmoja wa jua kali. Nilirudi kutoka shule nikiwa nimechoka na jasho linanitiririka. Nguo zimelowana, miguu inauma, na sikuwa nimekula chochote.

Nilitua begi la shule na kukaa kwenye kiti kupumzika kwa dakika tano tu.

“TUMAINI!!!”

Alikuwa Wakili Gina tena. Nikasimama taratibu.

“Abee mama.”

“Nenda ukafue nguo za mtoto haraka. Zipo bafuni.”

“Lakini mama... dada wa kazi si—”

Akanikatisha.

“Unanijibu? Mimi ndie niliyekuleta wewe duniani kuwa mtoto haramu? Fanya ninachosema au nitakurudisha kwenye kituo cha watoto yatima ulikotoka!”

Machozi yakaanza kujikusanya tena. Sikusema kitu. Nilienda kufua nguo za mtoto.
Nilipoingia bafuni, niliona mashine ya kufua ikiwa imewashwa. Dada wa kazi alikuwa chumbani kwake.
Nikaenda nyuma ya nyumba, nikainama juu ya beseni, na kuanza kufua nguo moja baada ya nyingine kwa mikono yangu. Nilipokuwa nafua, machozi yalianguka ndani ya maji. Ninalia kimya kimya, kwa sababu hakuna aliyekuwa anajali.
Hakuna aliyefahamu maumivu ninayopitia.
Nikatazama juu angani na kunong’ona, “Mungu, tafadhali usinisahau... Jina langu ni Tumaini... lakini naanza kulipoteza.”

Inaendelea...

SURA YA KWANZA:Jina langu ni Tumaini... Sikuja duniani kwa shangwe au furaha, bali kwa maumivu na kukataliwa. Nilizaliwa...
12/11/2025

SURA YA KWANZA:

Jina langu ni Tumaini... Sikuja duniani kwa shangwe au furaha, bali kwa maumivu na kukataliwa. Nilizaliwa nje ya ndoa—ndiyo, hilo ndilo neno sahihi, nje ya ndoa. Mama yangu alikuwa msichana mdogo, wa miaka 16 aliyepata ujauzito bila kujua afanye nini na maisha yake. Aliificha mimba yake kwa kila mtu hadi ilipofikia mwisho wa kufichwa.

Baada ya kunizaa, hakuniangalia hata mara ya pili. Nilikuwa na miezi miwili tu aliponitelekeza mbele ya kituo cha kulelea watoto yatima. Ilikuwa alfajiri, jua halikuwa limechomoza vizuri. Alinifunga kwa khanga chakavu, akaweka kipande cha karatasi pembeni yangu kilichoandikwa, “Jina lake ni Tumaini. Tafadhali mtunze.” Kisha akaondoka.

Majaliwa ya Mwenyezi Mungu kwa huruma yake siku hiyo, kwani dada mmoja wa Kanisa Katoliki aitwaye Dada Matilda, aliyekuwa anakiongoza kituo hicho, ndie aliyeniokota. Alisema alikuwa njiani kuelekea kwenye sala ya asubuhi ndipo alisikia kilio chaa mtoto kwa sauti ya upole. Mtoto huyo nilikuwa mimi. Alininyanyua kwa taratibu, akanibusu kwenye paji la uso, na kunong’ona, “Uko salama sasa, mwanangu.”

Hapo ndipo safari yangu ilipoanza.

Maisha katika kituo cha watoto yatima hayakuwa mabaya hata kidogo. Kwa hakika, kilikuwa ndicho mahali pekee nilipoona k**a nyumbani. Nililelewa kwa upendo na uangalizi mkubwa. Dada Matilda alikuwa k**a mama kwangu na kwa wengine wote. Alikuwa anatuimbia nyimbo na kutusimulia hadithi kutoka kwenye Biblia. Nilimzoea kumwita “Mama Matilda.” Nilipofikisha miaka miwili, tayari nilikuwa natambua sauti na sura za watoto wengine. Kituo kilijaa kicheko. Hatukuwa na kila kitu, lakini tulikuwa na upendo. Tulikuwa na amani.

Shuleni, nilijulikana k**a yule msichana mwenye akili kutoka kituo cha watoto yatima. Walimu wangu walikuwa wanasema mimi ni tofauti na wa kipekee. Nilijifunza haraka na kila mara nilikuwa wa kwanza darasani. Nilikuwa naliwakilisha darasa langu kwenye mashindano ya maswali na mijadala, na kila niliporudi na cheti, Mama Matilda alikuwa ananiita “Binti yangu ni star.”

Kisha tukio moja lilitokea nilipofikisha miaka mitano, tukio lililobadilisha maisha yangu.

Mchana mmoja wenye jua kali, gari kubwa jeusi aina ya Jeep liliingia kwenye uwanja wa kituo. Nakumbuka jinsi sisi watoto tulivyokimbia kwenda kuona ni nani amekuja. Mwanaume aliyevaa shati jeupe safi alishuka, akifuatiwa na mwanamke mrembo aliyevaa miwani ya bei ghali na mkoba wa kisasa. Hiyo ndiyo siku niliyokutana na Bwana Amos na Wakili Gina. Walionekana matajiri, wa kisasa, na kila kitu nilichowaza kuhusu familia kamili.

Baada ya kuzungumza na Mama Matilda na kuzungumza nami, waliamua kunichukua k**a mtoto wao. Siku hiyo, Mama Matilda aliniita chumbani kwake, akanishika mikono, na kusema, “Tumaini, maisha mapya yanakaribia kuanza. Nenda ukang’ae, mwanangu.”

Nilifurahi sana, lakini pia nililia kwa sababu nilikuwa nawaacha yeye na baadhi ya marafiki zangu. Alinibusu kwenye paji la uso kwa mara ya mwisho na kunipa mkufu mdogo wenye msalaba. “Hii itakulinda,” alisema. Nilivaa shingoni na sikuwahi kuutoa.

Kuishi na Bwana Amos na Wakili Gina ilikuwa k**a ndoto. Hawakujaaliwa kupata mtoto, hivyo walinipa upendo na uangalizi wote ambao mtoto angehitaji. Chumba changu kilikuwa k**a cha malkia. Nilikuwa na toys, nguo, na vitabu. Nilijiunga na moja ya shule bora jijini Dar es Salaam. Marafiki zangu shuleni walikuwa wananionea wivu. Hawakujua kuwa nilikuwa mtoto niliyekataliwa.

Bwana Amos alikuwa karibu sana nami. Alinisaidia na kazi za shule na kunisimulia hadithi kabla ya kulala. Wakili Gina, ingawa alikuwa mkali, alikuwa mwema pia. Aliniletea zawadi na kupika chakula ninachokipenda. Niliwaita Baba na Mama, na kwa moyo wangu wote niliamini kuwa hatimaye niko nyumbani.

Muda ulipita. Nilikuwa darasa la saba, najiandaa kwa mitihani ya mwisho. Walijivunia sana mafanikio yangu. Nilisoma kwa bidii na nikafaulu kwa alama za juu. Kulikuwa na sherehe kubwa nyumbani siku hiyo. Mama alipika pirau na kuku wa kukaanga. Baba alininunulia begi jipya la shule na kuahidi kunipeleka Dodoma. Nilijisikia wa pekee. Nilijisikia kupendwa.

Kisha nikaingia sekondari, na maisha yaliendelea kuwa mazuri hadi jambo fulani likabadilisha.

Nilipokuwa kidato cha tatu, nilianza kugundua kuwa Mama alikuwa amebadilika. Alikuwa na huzuni na hasira mara kwa mara. Mwanzoni sikuelewa. Nilidhani labda alikuwa amechoka au ana msongo wa kazi. Lakini siku moja, Baba alirudi mapema na kusema, “Mama yako ni mjamzito!”

Nilifurahi sana. Hatimaye, nilikuwa naenda kuwa dada mkubwa. Nilicheza na kuimba nyumbani, nikimwambia kila mtu kuwa nitakuwa dada. Lakini polepole, mambo yakaanza kubadilika.

Mama aliacha kuzungumza nami k**a zamani. Alikuwa ananifokea kwa mambo madogo. Wakati mwingine alinipigia kelele bila sababu. Nikikosea kitu, alinita majina ya kunidhalilisha. Hata wasaidizi wa nyumbani walianza kunidharau. Baba hakuwa karibu k**a awali. Alianza kutumia muda mwingi na mke wake mjamzito au kazini. Alipokuwa nyumbani, hakuona hata jinsi nilivyokuwa natendewa.

Siku mtoto alipozaliwa, wakiume mwenye afya, ndio siku maisha yangu yalibadilika kabisa.

Upendo wote ulielekezwa kwake. Nyumba iliyokuwa k**a kasri sasa niliiona k**a gereza. Sikuruhusiwa kumkaribia mtoto. Nilikuwa napewa kazi nyingi, na nikikosea, niliadhibiwa. Mama alikuwa anasema, “Unatakiwa kushukuru tulivyokutoa kwenye kituo cha watoto yatima!” Maneno yake yaliniumiza kila mara.

Fikiria kunituma sokoni peke yangu, binti mdogo, kununua vyakula. Na nikichelewa kurudi, alikuwa anafokasana, “Unataka kukimbia na pesa zangu?” Baba hakusema chochote. Alikuwa anaangalia kimya. Mtu aliyewahi kuniita malaika wake sasa ananiona k**a mgeni.

Sikuweza kuelewa kosa langu ni nini. Niilipenda familia yangu. Niliwaombea. Nilisaidia kwa kila njia niliyoweza. Lakini bado, nilinyanyaswa.

Hapo ndipo nilipoanza kuelewa kuwa labda, labda tu, upendo si wa milele kila wakati. Lakini sikupoteza tumaini. Jina langu ni Tumaini, baada ya yote.

Na hii ni mwanzo tu wa simulizi yangu.

Inaendelea...

12/11/2025

SEHEMU YA KUMI:Bibi yake Bianca akamtazama kwa sauti nzito akasema, “Mjukuu wangu, sasa lazima uwaangamize wote wanaokuz...
11/11/2025

SEHEMU YA KUMI:

Bibi yake Bianca akamtazama kwa sauti nzito akasema, “Mjukuu wangu, sasa lazima uwaangamize wote wanaokuzuia. Usionyeshe huruma.”

Bianca akatikisa kichwa taratibu, macho yake mekundu kwa hasira. Mara moja, bibi yake akatoweka hewani, akamuachia nguvu za kutosha kuleta maafa. Bianca akatoweka papo hapo na kutua hospitalini ambako Frederick alikuwa amelala.

Alipoingia tu, hospitali nzima ikageuka kuwa giza totoro. Frederick, ambaye alikuwa ameanza kupata nafuu, akaanza kutetemeka kitandani. Moyo wake ukadunda kwa kasi k**a unataka kutoka. “Kuna nini tena? Ee Mungu, tuhurumie,” akanong’ona, akashika blanketi kwa nguvu.

Mama akaitoa yake haraka. Hakupoteza muda, akasimama katikati ya chumba kwa ujasiri na kuanza kuomba kwa sauti.

“Yesu! Shika usukani. Yesu! Pigana vita hii.” Sauti yake ilikuwa na nguvu ingawa mwili wake ulikuwa dhaifu.

John, aliyekuwa ndani pia, hakuweza kupambana na Bianca. Badala yake, akajificha haraka ndani ya kabati kubwa pembezoni mwa chumba. Kutoka hapo, alikuwa anachungulia kupitia tundu dogo, akashuhudia kila kitu. Miguu yake ilikuwa inatetemeka, lakini ndani yake aliomba Mama asikate tamaa.

Kicheko cha Bianca kikavuma chumbani. “Hahahaha! Mnadhani maombi yenu yanaweza kunizuia? Nina nguvu msizoweza kustahimili.” Akanyosha mikono mbele, akaachia miale ya moto wa ajabu hewani. Lakini Mama hakusogea hata kidogo. Aliendelea kushika rozari na kuomba.

Bianca akaguna kwa hasira na kumuita tena bibi yake. Ghafla, mchawi mzee akaonekana pembeni yake. Wote wawili wakaanza kuachia nguvu zilizotikisa jengo la hospitali. Madirisha yakagongana, mashine zikaanza kupiga kelele bila mpangilio, na Frederick akapiga kelele kitandani, “Mama! Tafadhali usiache kuomba!”

Sauti ya Mama ikazidi kuwa dhaifu, lakini hakukubali kushindwa. Akapiga magoti, rozari bado mkononi, akasema kwa sauti ya chini, “Bwana ndiye nguvu yangu. Sitatikisika.”

Daktari na wauguzi wawili, wakasikia kelele, wakaingia haraka. Lakini walipoingia tu, nguvu zilizokuwa zinazunguka chumbani ziliwatupa chini. Wakapoteza fahamu.

Vita ikazidi kuwa kali. Bianca na bibi yake wakaanza kuihisi nguvu ya maombi ya Mama. Chumba kikaanza kutetemeka kana kwamba tetemeko la ardhi linapita. Ghafla, bibi akaguna kwa maumivu. Mwili wake ukaanza kufifia. Akamgeukia Bianca na kusema, “Mjukuu wangu, nguvu zake ni kubwa mno. Lazima tuondoke sasa hivi, la sivyo hutaweza kupona tena!”

Bianca akapiga kelele, “Hapana! Bibi, tusiondoke. Sijashindwa!”

Lakini bibi akatikisa kichwa. “Hili linatuzidi. Umebaki peke yako.” Kisha akatoweka, akamuacha Bianca.

“Hapanaaa! Usiondoke, Bibi!” Bianca akalia kwa uchungu. Macho yake yakageuka mekundu kabisa, akaachia nguvu kubwa moja kwa moja kwenye kifua cha Mama. Nguvu hiyo ikampiga Mama, akayumba na kuanguka chini.

Wote walidhani huo ndio mwisho, lakini Mama akashika kifua chake, akaguna kwa maumivu, na bado akasema kwa sauti ya chini, “Yesu… Yesu… k**ata usukani.” Akaweza kusimama tena, machozi yanamtoka, na akaendelea kuomba kwa sauti kubwa zaidi.

Ghafla, radi kubwa ikapiga kutoka kusikojulikana. Mwanga mkali wa umeme ukaingia chumbani na kumpiga Bianca kwa nguvu. Akalia kwa uchungu na kuanguka kwa kishindo. Mara moja, giza likatoweka. Taa za hospitali zikawaka tena, na kila kitu kikawa kimya.

Daktari akapata fahamu na kukimbilia kumkagua Mama, ambaye sasa alikuwa amelala sakafuni. Akaomba msaada wa haraka, na wakamsafirisha hadi wodi nyingine kwa matibabu ya dharura.

Frederick, bado yupo kitandani, akaunyanyua mkono wake dhaifu na kusema, “Asante Yesu. Asante Bwana.” Machozi yakamtiririka.

Bianca, hata hivyo, bado alikuwa hai. Alikuwa amelala chini, nusu mfu lakini anapumua. Frederick hakupoteza muda, akaagiza polisi waitwe. Ndani ya dakika chache, maafisa wawili wakaingia chumbani. John pia akatoka mafichoni, anapumua kwa nguvu, shati lake likiwa limejaa jasho.

Bianca, akiwa na pingu mikononi, alijaribu kutoweka, lakini nguvu yake haikufanya kazi. Nguvu zake zilikuwa zimeisha. Bibi yake hakuwepo tena. Alikuwa peke yake. Akaanza kulia k**a mtoto. “Tafadhali… tafadhali msiniue. Nitakiri kila kitu.”

Mama, ingawa alikuwa dhaifu, akarudishwa chumbani kwa kiti cha magurudumu. Frederick, John, daktari, na polisi wote walikuwepo.

“Unazungumzia nini?” Frederick akauliza kutokea kitandani,.

“Anataka kusema jambo,” daktari akasema kwa utulivu.

“Sawa basi, tunakusikiliza,” John akaongeza.

Bianca akalia na kumtazama mume wake. “Mume wangu, samahani. Sikupanga mambo yaishie hivi. Enzi za chuo, uliponiambia unampenda rafiki yangu na si mimi, nilihisi kudharauliwa. Nikaamua kumuua, kisha nikatumia juju ili umsahau na unipende mimi tu.”

“Ee Yesu Kristo!” John akapiga kelele, akafunika mdomo wake. “Unaweza kuwa muovu kiasi gani?”

Macho yakamtoka Fredrick. Wakati huo, kumbukumbu zikaanza kumrudia. Uchawi ukaanza kuvunjika. Akakunja ngumi, akajaribu kusimama kitandani kwa hasira, lakini Mama na daktari wakamzuia haraka.

Mama akamtazama Bianca moja kwa moja machoni na akauliza, “Na sufuria?”

Bianca akatikisa kichwa taratibu. “Sufuria ndio ina siri. Akila tu chakula nilichopika kwa hiyo sufuria, ataeendelea kunipenda mimi tu. Hilo ndilo lilikuwa agano.”

Frederick akatikisa kichwa kwa mshangao. “Kwa nini, Bianca? Nilifanya nini kwako? Unamaanisha ulimuua Sofia… kwa sababu yangu?” machozi yakamtoka.

“Samahani sana,” Bianca akanong’ona.

“Maafisa, mchukueni huyu mwanamke!” Frederick akaamuru kwa hasira. “Hastahili kuonekana tena duniani.”

Polisi wakambeba. Alilia kwa uchungu, “Tafadhali, mume wangu! Usiruhusu wanichukue. Nimebadilika sasa. Tafadhali nisamehe.”

Frederick akapiga kelele, sauti yake inatetemeka kwa hasira. “Ukiniita jina hilo tena, nitafanya kitu ambacho utajutia. Mchukueni!”

Polisi wakambeba kwa nguvu na kuondoka nae. Frederick akaketi kitandani, akainamisha kichwa chake. John akaweka mkono begani kwake, akanong’ona, “Jipe moyo, rafiki yangu.”

Wiki zikapita. Frederick akapona kabisa na kuruhusiwa kutoka hospitali. Mama naye akarejea katika hali yake ya kawaida, uso wake ukang’aa kwa amani.

Waliporudi nyumbani, wakaamua kuiteketeza sufuria ile ya kishetani.

Wakaichukua hadi nje, wakachukua mawe, na wakaiponda ponda na kuimwagia mafuta na kuichoma moto. Lakini bila wao kujua, wakati sufuria ilipokuwa inaungua, Bianca—akiwa rumande—alianza kupiga mayowe ya maumivu. Moto ukaanza kumteketeza. Ngozi yake ikageuka kuwa nyeusi k**a mkaa hadi alipotoa pumzi yake ya mwisho.

Askari, waliogopa walichokiona, wakamzika haraka kwenye moja ya pori kubwa sana ambako mtu hawezi kuingia bila silaha. Hapo ndipo mwisho wa Bianca ulipofika.

MWISHO….

Funzo kwenye Maisha: Uovu unaweza kuonekana kushinda kwa muda, lakini hauwezi kudumu. Uongo, wivu, na nguvu za giza huweza kudanganya mioyo kwa msimu, lakini ukweli, upendo, na nguvu ya Mungu husimama imara daima. Haijalishi itachukua muda gani, kila siri iliyofanywa gizani itafichuliwa na mwanga, na haki itatendeka bila shaka.

SEHEMU YA TISA:John alipoingia ndani, alimsalimia Mama kwa kumbatio la upole. Lakini macho yake yalibaki yanamtazama Bia...
11/11/2025

SEHEMU YA TISA:

John alipoingia ndani, alimsalimia Mama kwa kumbatio la upole. Lakini macho yake yalibaki yanamtazama Bianca. Alikuwa amekaa huku amekunja mikono, k**a alilazimishwa kuwepo pale.

“Sasa kwa kuwa tupo wote humu,” Mama akasema kwa sauti ya upole, “tunaweza kuomba pamoja k**a familia?”

“Ndiyo Mama, bila shaka,” John akajibu haraka.

“Oh, hilo? Ngoja niende kwanza chooni, kisha nitarudi kujiunga nanyi,” Bianca akasema, akijaribu kukwepa.

“Umekuwa ukifanya hivi kila mara, hasa linapokuja suala la maombi. Leo hutaondoka,” Mama akasema kwa msisitizo.

John akamuunga mkono haraka, “Ndiyo Bianca. Kaa. Lazima tuombe pamoja sasa hivi kwa ajili ya mume wako.”

Bianca hakuwa na chaguo. Akavuta pumzi kwa nguvu, akapeperusha macho kidogo, kisha akaungana nao.

Mama akaanza kwa wimbo wa sifa kwa Mungu. Sauti yake ilikuwa tulivu lakini yenye nguvu ya kiroho. John akaungana nae, kwa kupiga makofi. Hali ya kiroho ikaanza kutanda chumbani.

Bianca akawa anajigeuza kwenye kiti, anajikuna mikono, anaonekana kutokaa sawa. Kadri walivyoimba, ndivyo alivyozidi kuwa na wasiwasi. Uso wake ukakunjamana kana kwamba moto usioonekana ulikuwa unamchoma.

Ghafla, Bianca akapiga kelele. Sauti yake ikavuma chumbani. Mama na John wakaongeza sauti zao katika kuomba, kwa mamlaka.

Bianca akapiga kelele tena, akajikunjakunja… kisha akatoweka.

“Asante Yesu!” Mama akalia, akiinua mikono kwa ushindi.

Jonh akabaki na mshangao, akili yake ikihangaika kuelewa kilichotokea.

Masaa yakapita. Frederick akaanza kushtuka. Wakati huo, Mama alikuwa amelala kwenye kiti, huku John akiwa amekaa kimya, akiinamisha kichwa chake kwa tafakuri.

“John… Mama…” Frederick akaita kwa sauti dhaifu, bado anahisi maumivu kichwani.

“Mwanangu, umeamka!” Mama akasema, akimkimbilia kwa furaha.

“Rafiki yangu, umeamka!” John akasema, kisha akaenda haraka kumuita daktari.

Daktari akaingia mara moja, akakagua hali ya Frederick, akarekebisha mashine, na kumuuliza maswali machache. Alipomaliza, akawapa ishara ya kutia moyo kabla ya kutoka nje.

JOhn akamsogelea. “Nimefurahi umeamka, kaka.”

“Asante, rafiki yangu,” Frederick akanong’ona, kisha akakitazama chumba kwa macho dhaifu. “Mke wangu yuko wapi?”

“Hmmm… pata nafuu kwanza. Yuko nyumbani,” Mama akajibu kwa tahadhari.

“Kwanini hayupo hapa nanyi?” Frederick akauliza kwa mshangao.

“Usijisumbue. Tulia,” Mama akasema kwa upole. “Ukishapona vizuri, nitakuambia kila kitu.”

Wakati huo huo, nyumbani, Bianca alikuwa amelala chumbani kwake, anatetemeka kwa hasira na maumivu. Mwili wake ulikuwa k**a unachomwa moto. Hakuweza kusimama.

Kwa mikono aliyoikunja kwa hasira, akasema kwa sauti ya chini, “Nahitaji msaada wake sasa…”

Mara moja, akamwita bibi yake. Hali ya hewa ikabadilika, na ndani ya muda mfupi, mchawi mzee akaonekana, akaingia ndani ya nyumba kwa tabasamu la kishetani.

“Wamekufanyia nini binti yangu?” akauliza kwa sauti ya ukali. “Watalipia gharama kubwa kwa hili,” akasema, kisha akampa binti yake nguvu mpya—nguvu za kutisha.

Bianca akasimama mara moja, macho yake yakiwa mekundu, tayari kumla yeyote atakayemsogelea.

Inaendelea...

**** PATA UPDATE MAPEMA YA SIMULIZI HII KUPITIA WHATSAPP CHANNEL YANGU... Link iko kwenye comment ****

SEHEMU YA NANE:Baada ya muda, Bianca akasimama na kusema, “Mama, nafikiri ni wakati wa kuondoka. Usiku umeingia.”Mama ha...
10/11/2025

SEHEMU YA NANE:

Baada ya muda, Bianca akasimama na kusema, “Mama, nafikiri ni wakati wa kuondoka. Usiku umeingia.”

Mama hakujibu, alikaa kimya tu. John alikwisha ondoka mapema.

“Tutakuja tena kesho,” Bianca akaongeza kwa msisitizo.

Mama hakuwa na chaguo zaidi ya kumfuata kurudi nyumbani.

Walipofika nyumbani, Bianca akampeleka Mama chumbani kwake.

Usiku wa manane, Bianca akaonyesha sura yake halisi. Akabadilika kuwa katika umbo lake la kichawi na kutambaa moja kwa moja hadi chumbani kwa Mama.

Mama alikuwa amelala fofofo. Bianca akatabasamu. “Usiku wa leo, nitakuonyesha mimi ni nani kwenye nyumba hii,” akanong’ona.

Lakini cha kushangaza, hakuna kilichofanya kazi. Ilikuwa kana kwamba kuna nguvu isiyoonekana ilikuwa inamlinda Mama.

Akaongeza nguvu, akajaribu tena. Ghafla, shoti k**a ya umeme ikampiga na akatoweka hapo hapo.

Mama akastuka kutoka usingizini, bila kujua kilichokuwa kimetokea. Akaamka na kuanza kuomba, akajifunika yeye na mwanae kwa damu ya Yesu Kristo.

Wakati huo huo, Bianca akarudi chumbani kwake akiwa amekasirika. “Kwa nini siwezi kumdhuru? Kwa nini ana nguvu hivi?” akajiuliza kwa hasira. “Natakiwa kumuita bibi yangu haraka,” akasema, kisha akakaa chini akakunja miguu, akaanza kuimba kwa lugha za ajabu ajabu.

Mara moja, mwanamke mzee mwenye meno ya kahawia yaliyochafuka akaonekana.

“Kuna nini, binti yangu? Kwa nini unaniita usiku huu?” akauliza kwa sauti ya ukali.

Bianca akainama kidogo. “Shikamoo Bibi. Nina changamoto.”

“Nini kinakusumbua, mjukuu wangu?”

“Nashindwa kumdhuru mama mkwe wangu. Najaribu kumtupia ugonjwa wa kumuua, lakini kuna kitu kinanizuia,” Bianca akakiri.

Mwanamke mzee akacheka, meno yake yakang’aa kwenye mwanga hafifu. “Hahaha! Naona nguvu za ajabu na zenye nguvu zinamzunguka. Lakini usijali, nitakupa kitu kitakachozizima hizo nguvu.”

Akacheka tena na kutoweka.

Bianca akatabasamu. “Sitapumzika hadi niimalize familia hii na kuimiliki yote,” akanong’ona na kucheka gizani.

Asubuhi iliyofuata, Mama akaomba kwa bidii kabla ya kutoka chumbani. Akajipikia chakula chake, akala, kisha akaenda sebuleni.

Bianca aliposhuka kupika, Mama akasema kwa utulivu, “Nimeshakula tayari. Nakusubiri tu twende hospitali kumwona mwanangu.”

“Sawa Mama,” Bianca akajibu, akificha huzuni yake.

Baadae siku hiyo, wakaenda hospitali pamoja.

Fredrick alianza kutia matumaini.

“Hii ina maana kila ninachojaribu ni bure?” Bianca akajiuliza kimya kimya, kisha akaweka tabasamu bandia aliposikia mume wake anapata nafuu.

Mama akakaa pembeni ya mwanae, akaendelea kuomba...

Bianca hakuweza kukaa, akatoka nje, huku akifikiria nini cha kufanya.

Akabadilika tena kuwa katika umbo lake la kichawi, na safari hii hakuna aliyemuona. Akaingia hospitalini kwa lengo la kumshambulia mume wake kiroho, lakini maombi ya Mama yalikuwa na nguvu sana kiasi kwamba hakuweza kufanya chochote.

Baada ya majaribio mengi, akatoweka kwa hasira. “Kuna nini kinazuia?” akauliza kwa hasira.

Lakini wakati huo, John akamuona akiwa amesimama nje ya hospitali. “Kuna habari yoyote?” akauliza.

“Unaweza kuingia ndani na ukajionea mwenyewe,” akajibu kwa ukali na kuondoka.

“Mwanamke huyu, hmmm. Nina wasiwasi nae. Kila mara anajifanya k**a mtu aliyepagawa,” John akasema, akatikisa kichwa na kuingia hospitalini.

Inaendelea...

**** PATA UPDATE MAPEMA YA SIMULIZI HII KUPITIA WHATSAPP CHANNEL YANGU... Link iko kwenye comment ****

SEHEMU YA SABA:Nilipotoka chooni, nilimkuta Bianca amevaa tayari kuelekea kazini.“Mpenzi ndio umejiandaa Tayari kabisa?”...
10/11/2025

SEHEMU YA SABA:

Nilipotoka chooni, nilimkuta Bianca amevaa tayari kuelekea kazini.

“Mpenzi ndio umejiandaa Tayari kabisa?” nikauliza, sauti yangu ikiwa na wasiwasi.

“Ndiyo, nina mambo mengi ya kufanya ofisini,” akajibu, huku anachukua mkoba wake. Alinifuata, akanibusu haraka shavuni, kisha akaondoka bila kusema neno lingine.

Nikageuka na kukiangalia chakula alichoniachia. Kilikuwa mezani, kinatoa mvuke. Kitu ndani yangu kilikataa, lakini njaa ilikuwa na nguvu zaidi. Ilikuwa k**a kuna kitu kinanivuta kukifuata. Nikawa na mashaka… lakini hatimaye nikasalimu amri.

Chakula kilikuwa kitamu sana kiasi kwamba nilijisahau—nikala kana kwamba nilikuwa sijala wiki nzima. Mama akaingia na kunikuta nakula.

“Mwanangu, huendi kazini leo?” akauliza.

“Nitaenda,” nikajibu haraka, nikiwa bado natafuna. “Nilitaka nile kwanza.”

Akanitazama kwa muda mrefu, akavuta pumzi, kisha akaondoka kimya kimya.

Baada ya muda mfupi, nikavaa na kuondoka kuelekea kazini. Safari ilianza kawaida, jua la asubuhi likiipaka barabara mbele yangu kwa mwanga wa matumaini. Lakini ghafla, nilihisi k**a kuna kitu kinayafunika macho yangu kwa pazia jeusi. Kila kitu kikawa cheusi. Sikuweza kuiona barabara.

Kitu cha mwisho nilichosikia ni mlio mkubwa wa gari langu kugonga kitu kigumu kwa nguvu. Kisha—kimya.

Macho yangu yalikuwa gizani, nilikuwa kitandani hospitalini, nikiwa nimezungukwa na kuta nyeupe na mashine za ajabu. Sikuweza kujisogeza, lakini niliweza kusikia. Mwili wangu ulikuwa k**a jiwe.

“Daktari, nini kimemtokea?” sauti ninayoijua ikauliza kwa wasiwasi. Alikuwa ni John, rafiki yangu wa kazini.

“Aliletwa hapa muda si mrefu uliopita,” daktari akafafanua. “Amepata ajali mbaya sana. Yuko kwenye koma.”

“Ee Mungu! Tafadhali mrudishe rafiki yangu Frederick,” John akalia, akitembea huku na huko kwa huzuni.

Baada ya masaa kadhaa, mama yangu akaingia, uso wake umejaa wasiwasi. Muda mfupi baadae, Bianca akaingia—macho yake yakiwa mekundu.

“Daktari, tafadhali, nini kimempata mume wangu? Naamini yuko salama?” Bianca akauliza kwa sauti ya kutetemeka.

“Mwanangu,mwanangu mimi jamani?” mama yangu akalia kwa uchungu.

Daktari akainua mikono kuwatuliza. “Kila mtu atulie tafadhali. Yuko kwenye hali mbaya, lakini tunafanya kila tuwezalo kuokoa uhai wake.”

“Mungu wangu, tafadhali usimchukue mwanangu wa pekee,” mama akalia kwa uchungu, akitembea huku na huko kwenye korido ya hospitali, ilibaki kidogo aanguke kwa huzuni.

“Mama, tafadhali, tulia,” Bianca akasema kwa upole, akaweka mkono begani mwake. “Hakuna litakalomtokea.”

“Mama, kaa chini tafadhali,” John akaongeza, akamwelekeza kwa upole kwenye kiti.

Lakini wakati wanalia na kuomba, moyo wa Bianca ulikuwa unasherehekea kwa siri. Akajisemea moyoni “Hii hakuweza kuikwepa”

Inaendelea...

**** PATA UPDATE MAPEMA YA SIMULIZI HII KUPITIA WHATSAPP CHANNEL YANGU... Link iko kwenye comment ****

Address

Koinange
Nairobi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Syaga Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share