16/11/2025
SURA YA TATU:
Baada ya kumaliza kufua nguo za mtoto, mikono ilikuwa imechoka sana. Viganja vilianza kupasuka, na sabuni ilikuwa imeikausha ngozi na kuifanya iwashwe. Lakini sikulalamika. Nilijifuta mikono kwa kipande cha kitambaa na nikaingia ndani kumwambia Wakili Gina.
“Mama... nimemaliza kufua,” nilisema kwa sauti ya chini, nimesimama kwenye mlango wa jiko.
Hakuniangalia hata. Macho yako busy kwenye simu yake. “Vizuri. Sasa nenda jikoni ukaoshe sahani zote. Hakikisha sufuria zinang’aa, la sivyo...”
Nikatikisa kichwa na kuingia.
Wakati huo, tumbo langu linaunguruma kwa njaa. Sikuwa nimekula chochote tangu asubuhi. Lakini chakula kilikuwa si kitu cha kwanza kwenye akili yangu. Nilitaka nimalize kila kazi ninayopewa kabla sijakumbana na kelele tena.
Nilimaliza kuosha vyombo, nikasafisha kaunta za jikoni, na kufagia. Hatimaye nikakaa na kula wali uliobaki kwenye sufuria. Ulikuwa wa baridi na hauna ladha, lakini ulikuwa bora kuliko kutokula kabisa. Angalau tumbo langu linapata kitu.
Baada ya kula, nikaenda chumbani kwangu, nikachukua begi la shule, na kuanza kufanya home work. Ilikuwa tayari ni usiku sana, zaidi ya saa nne. Usingizi ulinitesa, lakini nilijilazimisha kumaliza.
Kabla sijalala kwenye godoro langu dogo, nikapiga magoti pembeni ya kitanda na kusali.
“Mungu baba, naomba nilinde tena usiku huu. Tafadhali usiruhusu nipoteze tumaini. Nimechoka, lakini bado naamini kwako. “
Nikazungumza na Mungu k**a rafiki pekee niliyekuwa naye.
Asubuhi iliyofuata, niliamka mapema sana k**a kawaida. Nilifagia sebuleni, nikaweka viti vizuri, nikasafisha mbele ya nyumba, kisha nikaingia jikoni kutayarisha uji wa mtoto. Baada ya kufanya kila kitu, nikajiandaa kwenda shule. Msaidizi wa nyumbani alikuwa amepumzika tu. Sijui labda alikuwa amepewa adhabu, lakini nilifanya kila kitu ili kuepuka matatizo.
Shuleni hakukuwa rahisi pia. Walimu wangu bado walikuwa wanalalamikia maendeleo yangu.
“Ulikuwa mmoja wa wanafunzi wetu bora,” mwalimu wangu wa Kiingereza alisema kwa huzuni. “Tumaini, kuna nini kinachokusumbua?”
Sikuweza kujibu. Nikaangalia chini, kwenye miguu yangu.
Ningewezaje kueleza kuwa usiku wangu nautumia kufua nguo na kudeki? Kwamba silali kwa wakati, moyo wangu umechoka, na akili yangu haina nafasi ya kusoma?
Wakati wa mapumziko, nikakaa peke yangu chini ya mti wa muembe. Rebecca alikuwa ameenda kununua vitafunwa, lakini mimi sikuwa na pesa. Niliangalia juuangani, nikiyafikiria maisha yangu.
Nilirudi nyumbani baadae alasiri. Nilipofungua mlango, nilimuona Bwana Amos—yule aliyewahi kuniita “malikia wake”—amekaa sebuleni anaangalia TV. Nikatabasamu na kukaa karibu yake, nikiamini tutaongea na kucheka k**a zamani.
Lakini hakuniangalia hata.
“Tafadhali Tumaini, niko bize sasa hivi. Sina muda wa kuchezea,” alisema.
Nikasimama taratibu na kuondoka. Machozi yalijaa machoni..
Nikaingia chumbani na kufungua vitabu vyangu. Sikutaka kulifikiria. Nilitaka kusoma na kusahau matatizo yangu.
Mtoto alikuwa na msaidizi wa nyumbani. Nikasikia wanacheka na kucheza.
Lakini amani haikudumu.
Baada ya saa moja, nikasikia mlango wa mbele unagongwa kwa nguvu. Bi Gina alikuwa amerudi kutoka kazini, na kwa sauti ya hatua zake, nikajua kuna jambo. Ilikuwa ni k**a amebeba hasira za ofisini kuja nazo nyumbani.
Nikakaa kimya chumbani kwangu, nikajifanya sijaona. Mara ghafla—
BANG!
Mlango ukafunguliwa kwa nguvu, na kabla sijasema “Shikamoo mama,” kofi moto likatua kwenye shavu langu.
PAAHH!!
Nikapiga yowe na kushika uso wangu.
“Hujasikia nilipokuita?” akafoka.
“S-sikusikia mama... nilikuwa nasoma,” nilijibu kwa kigugumizi, machozi tayari yanatiririka.
Kabla sijamaliza kusema, kofi lingine likaja. PAAHH!!
“Nyamaza! Kwa hiyo mimi muongo? Mtoto wa hovyo kweli wewe! Umeanza kuwa na kiburi ndani ya nyumba yangu, eeh?”
Nikataka kuzungumza, kuomba msamaha, lakini mdomo wangu unatetemeka. Nilikuwa nalia bila kujizuia. Shavu langu lilikuwa linawaka moto. Mwili wangu wote ukawa unatetemeka kwa hofu.
Alinishika kwa mkono na kunivuta hadi jikoni. “Nenda ukaoshe chupa ya mtoto! Msichana mvivu!”
Nilifanya alivyosema, nikiwa bado nalia. Chupa ilikuwa safi, lakini niliiosha tena mara tano ili kuhakikisha.
Nilipokuwa naiosha, nikanong’ona, “Mungu naomba nisaidie... nimechoka... nisaidie...”
Nilipomaliza, nikaenda chumbani kwangu na kufunga mlango kimya kimya. Nikakaa kitandani na kulia k**a mtoto mchanga. Moyo wangu ulikuwa mzito. Uso wangu ulikuwa umevimba. Nafsi yangu haikuwa na amani tena.
Nilitazama darini na kujiuliza, “Kwa nini mimi? Nimekosea nini? Kwa nini nateseka hivi?”
Nikalia hadi usingizi ukanipitia.
Hakuna aliyekuja kuniangalia.
Hakuna aliyeniuliza k**a nipo salama... Kwao, nilikuwa k**a mzigo tu.
Lakini kwangu, bado niliamini kitu kimoja...
Tumaini... Kwa sababu hicho ndicho kitu pekee kilichobaki.
Inaendelea...