KBC Radio Taifa

KBC Radio Taifa Ukurasa Rasmi wa KBC Radio Taifa. Intelsat

(Free to air)


1.
(690)

Sikiliza KBC Radio Taifa:

92.9 FM: Nairobi na viunga vyake, Central, South Rift Valley na Eastern Provinces

90.4 FM: Meru, Isiolo na Laikipia

88.6 FM: Nyanza, Western na Central Rift Valley

100.8 FM: Mombasa na viunga vyake

87.7 FM: Nyeri na maeneo ya Mlima Kenya pia Mashariki mwa Kenya

104.1 FM: Nakuru na viunga vyake

103.3 FM: Kisii na viunga vyake

90.1 FM: Malindi na viunga vyake

9

3.3 FM: Kapenguria, Kacheliba, Kitale, Eldoret, Kabarnet na Marakwet

104.5 FM: Magharibi na Nyanza hadi Mashariki mwa Uganda


96.9 FM: Voi, Taveta, Wundanyi, Loitokitok, Mtito Andei, Machinery, Kibwezi na Kilifi,

89.9 FM: Namanga na Kaskazini mwa Tanzania

88.6 FM: Lodwar na viunga vyake

89.3 FM: Lokichoggio na viunga vyake


93.1 FM: Garsen, Hola, Witu, Mpeketoni, Lamu, Manda Island, Mokowe, Faza island Gongoni

92.9 FM: Naivasha, Mai Mahiu, Suswa, Mau Narok, Gilgil na Ol kalou


Pia tuko kwenye Satellite:


A. NSS 12- 57ₒE

* Frequency-11.026GHZ
* Symbol Rate - 9690
* FEC-3/4



DVBS

Horizontal

2. 1S1O-68.5ₒE

* Frequency-3964GHZ
* Symbol Rate-7415
* FEC-3/5



DVBS 2

Vertical

B.Entelsat (DSTV)

( Scrambled)


W7-36ₒ E

* Frequency 11766GHZ
* Symbol Rate -27500
* FEC -3/4

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed akiwa na Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta.   ^FN
03/06/2026

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed akiwa na Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta.

^FN

Mshambuliaji wa Denmark, Rasmus Hojlund atimkia Napoli kwa Mkataba wa Kudumu.    ^FN
03/06/2026

Mshambuliaji wa Denmark, Rasmus Hojlund atimkia Napoli kwa Mkataba wa Kudumu.

^FN

“Watoto wanachoma shule sababu wanaona wazazi wao wakichoma mali ya watu kwa maandamano. Ile tabia tumekuwa nayo ndiyo w...
03/06/2026

“Watoto wanachoma shule sababu wanaona wazazi wao wakichoma mali ya watu kwa maandamano. Ile tabia tumekuwa nayo ndiyo watoto wanafuata na tukiona wanachoma shule tusishtuke.” - Gavana Susan Kihika.
^FN

Shule ya Moi Forces Academy Lanet Yawaagiza Wazazi Kuwachukua Wanafunzi wa Gredi ya 10 na Kidato cha Tatu. Hatua hiyo im...
03/06/2026

Shule ya Moi Forces Academy Lanet Yawaagiza Wazazi Kuwachukua Wanafunzi wa Gredi ya 10 na Kidato cha Tatu. Hatua hiyo imechukuliwa k**a tahadhari kufuatia kuongezeka kwa visa vya utovu wa nidhamu na ghasia za wanafunzi.

^FN

03/06/2026

Rais wa Tanzania Samia Suluhu anatarajiwa Kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

^FN

03/06/2026

Jumla ya wachezaji 1,248 kutoka mataifa 48, watashiriki kipute cha Kombe la Dunia, kati ya tarehe 11 mwezi huu na Julai 19, katika mataifa ya Mexico,Canada na Marekani.

Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Loreto , Limuru yafungwa kwa muda usiojulikana baada ya vurugu za wanafunzi usiku.   ...
03/06/2026

Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Loreto , Limuru yafungwa kwa muda usiojulikana baada ya vurugu za wanafunzi usiku.

^FN

03/06/2026

Nchi za Afrika, hasa zile zilizo katika hatari ya kukumbwa na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola, sasa zinatoa wito wa jitihada za pamoja katika kukabiliana na msambao wa ugonjwa huo. Wito huo umetolewa wakati wa mkutano wa dharura wa makatibu wa afya zaidi ya 60 kutoka barani humo waliokutana kwa njia....

Maafisa wa upelelezi mjini Kisumu wameanzisha uchunguzi kufuatia kupatikana kwa mwili wa mwanamke mwenye umri wa miaka 4...
03/06/2026

Maafisa wa upelelezi mjini Kisumu wameanzisha uchunguzi kufuatia kupatikana kwa mwili wa mwanamke mwenye umri wa miaka 40 akiwa amefariki ndani ya chumba cha wageni (Guest House) katika baa iliyoko eneo la Obunga.

Tukio hilo liliripotiwa baada ya mhudumu wa vyumba kugundua mwanamke huyo alikuwa hajitambui wakati wa shughuli za kawaida za usafi siku ya Jumatatu.

Marehemu alitambuliwa k**a JA*, mkazi wa Obunga. Inadaiwa kuwa mhudumu huyo alimkuta akiwa amelala sakafuni akiwa uchi ndani ya chumba hicho cha wageni na mara moja akabofya kengele ya tahadhari.

Maafisa wa polisi waliofika eneo la tukio walikuta mwili huo ukiwa sakafuni bila majeraha yoyote yanayoonekana kwa nje. Hata hivyo, wachunguzi walibaini povu likimtoka mdomoni na puani mwake, jambo lililozua maswali zaidi kuhusu chanzo cha kifo hicho.

Kulingana na Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chumba hicho cha wageni kilikuwa makazi ya JA kwa takriban mwezi mmoja, na kwamba alikuwa akikitumia kuwapokea wanaume waliokuwa wateja wake.

Wataalamu wa uchunguzi wa eneo la tukio walikagua na kurekodi ushahidi wote muhimu kabla ya mwili kuhamishiwa katika mochari ya Jaramogi Oginga Odinga Teaching and Referral Hospital kusubiri uchunguzi wa maiti (post-mortem).

Kwa sasa, maafisa wa upelelezi wanaendelea na juhudi za kubaini mtu wa mwisho aliyekuwa na marehemu pamoja na mazingira yaliyosababisha kifo chake. Chanzo halisi cha kifo bado hakijajulikana na kitathibitishwa baada ya matokeo ya uchunguzi wa maiti na uchunguzi unaoendelea.

^FN

Mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 22 anayedaiwa kuzuiliwa kwa minyororo kwa muda wa miezi mitano katika boma la mgang...
03/06/2026

Mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 22 anayedaiwa kuzuiliwa kwa minyororo kwa muda wa miezi mitano katika boma la mganga wa kienyeji katika Kaunti ya Kwale ameokolewa na polisi, huku tukio hilo lkiiibua maswali mazito kutoka kwa umma.

Kijana huyo aliyetambuliwa kwa jina Mwatela Dela, alipatikana akiwa amefungiwa ndani ya chumba kilichokuwa kimefungwa na kufuli katika Kijiji cha Mwamanga, eneo la Bongwe-Gombato, huku akiwa amefungwa kwa minyororo mizito kwenye nondo za chuma zilizomeeshwa sakafuni.

Polisi walivamia boma hilo na kufanya operesheni ya uokoaji baada ya babake kijana huyo kupiga ripoti kwamba mwanawe alikuwa akizuiliwa kinyume cha sheria nyumbani kwa mganga huyo wa kienyeji anayefahamika zaidi k**a Dr Baakanda.

^FN

Address

P. O. Box 30456 Harry Thuku Road
Nairobi
00100

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when KBC Radio Taifa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to KBC Radio Taifa:

Share