China Xinhua News

China Xinhua News We are public media for the public good. We never end our quest for facts and truth. Objectivity. Fairness. Balance.
(753)

We don't pursue corporate interests, nor will we ever yield to the pressure of ideological stigmatization and political bias. This page offers news from across the globe in Swahili language

Jumla ya uwezo wa umeme wa maji uliowekwa katika mkoa wa Sichuan, kusini-magharibi mwa China, umevuka kiwango cha kihist...
19/12/2025

Jumla ya uwezo wa umeme wa maji uliowekwa katika mkoa wa Sichuan, kusini-magharibi mwa China, umevuka kiwango cha kihistoria cha kilowati milioni 100, sawa na takribani robo moja ya uwezo wote wa kitaifa.
Sichuan, inayojulikana k**a “mkoa wa mito elfu moja,” ina rasilimali nyingi za umeme wa maji. http://xhtxs.cn/8Yk

Upanuzi wa ajabu wa nishati mbadala ya China umevutia sifa za kisayansi duniani, huku majarida ya kitaaluma ya Science n...
19/12/2025

Upanuzi wa ajabu wa nishati mbadala ya China umevutia sifa za kisayansi duniani, huku majarida ya kitaaluma ya Science na Nature yakiangazia wiki hii mabadiliko ya nishati safi ya nchi hiyo k**a moja ya hatua muhimu zaidi za kutia moyo za 2025. http://xhtxs.cn/8Yi

Katika mchanganyiko huu wa picha, watu wanaonekana wakijifurahisha katika bustani ya Harbin Ice-Snow World huko Harbin, ...
19/12/2025

Katika mchanganyiko huu wa picha, watu wanaonekana wakijifurahisha katika bustani ya Harbin Ice-Snow World huko Harbin, mkoa wa Heilongjiang kaskazini mashariki mwa China. Harbin Ice-Snow World, ni bustani kubwa zaidi duniani ya mandhari ya barafu na theluji, ilifunguliwa rasmi kwa msimu huu siku ya Jumatano, ikizindua toleo lake la kuvutia zaidi, likiwa na vivutio vya kihistoria, huduma za uangalifu na sanamu nzuri za barafu katika eneo la hifadhi lenye ukubwa wa mita za mraba milioni 1.2. http://xhtxs.cn/8Yh

Mkusanyiko huu wa picha unaonyesha Piramidi ya ngazi iliyoko katika nekropoli ya Saqqara, karibu na Giza nchini Misri, a...
19/12/2025

Mkusanyiko huu wa picha unaonyesha Piramidi ya ngazi iliyoko katika nekropoli ya Saqqara, karibu na Giza nchini Misri, ambayo ni mojawapo ya majengo ya kale zaidi duniani, ikijulikana k**a piramidi ya kwanza kabisa kujengwa katika historia ya ustaarabu wa binadamu. http://xhtxs.cn/8XN

Rais wa Ghana John Dramani Mahama ameahidi utayari wa Accra kuunga mkono juhudi za kurejesha na kujenga upya za Jamaica ...
19/12/2025

Rais wa Ghana John Dramani Mahama ameahidi utayari wa Accra kuunga mkono juhudi za kurejesha na kujenga upya za Jamaica kufuatia uharibifu uliosababishwa na Kimbunga Melissa.
Hatua hiyo kutoka Ghana ilikuwa katika roho ya uhusiano wa kihistoria ndani ya familia ya Kiafrika-Karibea na katika roho ya ushirikiano wa Kusini-Kusini, Mahama alisema katika hafla ya kuashiria kutumwa kwa kikosi cha wahandisi wa kijeshi wa Ghana kwenda nchi ya Caribbean kusaidia kazi inayoendelea ya ujenzi na kutoa misaada.
Alibainisha kuwa Ghana imetoa cedi milioni 10 za Ghana (karibu dola za Marekani 869,500) k**a msaada wa kibinadamu kwa Jamaica, Cuba, na Sudan. http://xhtxs.cn/8XM

Je utanunua maua kwa mpenzi wako? Siku ya Wapendanao kwa kawaida huchangia kati ya asilimia 30 hadi 35 ya mauzo ya maua ...
19/12/2025

Je utanunua maua kwa mpenzi wako? Siku ya Wapendanao kwa kawaida huchangia kati ya asilimia 30 hadi 35 ya mauzo ya maua mwaka, alisema Clement Tulezi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Maua la Kenya. Mauzo ya maua ya Kenya yanatarajiwa kufikia takriban tani 280,000 mwaka 2025, kutoka tani 260,000 mwaka 2024, kutokana na mseto wa soko, chama cha sekta hiyo kilisema. http://xhtxs.cn/8XL

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) siku ya Alhamisi lilimchagua rais wa zamani wa Iraq Barham Ahmed Salih k**a Kamish...
19/12/2025

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) siku ya Alhamisi lilimchagua rais wa zamani wa Iraq Barham Ahmed Salih k**a Kamishna Mkuu wa Wakimbizi wa Umoja wa Mataifa, kumrithi Filippo Grandi wa Italia.
Katika taarifa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alikaribisha kuchaguliwa kwa Salih kwa muhula wa miaka mitano kuanzia Januari 1, 2026.
Kulingana na taarifa hiyo, Salih alihudumu k**a rais wa Iraq kuanzia 2018 hadi 2022 na ana taaluma ya utumishi wa serikali kwa zaidi ya miongo mitatu nchini Iraq na Mkoa wa Kurdistan. xhtxs.cn/8Xa

Ziwa Sayram lililoko katika Wilaya ya Bortala katika Mkoa wa Xinjiang, kaskazini magharibi mwa China, limeonekana likiwa...
18/12/2025

Ziwa Sayram lililoko katika Wilaya ya Bortala katika Mkoa wa Xinjiang, kaskazini magharibi mwa China, limeonekana likiwa limefunikwa na mandhari ya baridi yenye kuvutia. Picha ya anga iliyopigwa tarehe 16 Desemba 2025, ilionyesha uzuri wa ziwa hilo pamoja na milima iliyofunikwa na theluji, ikibainisha hali ya baridi kali na mandhari ya asili yenye kuvutia katika eneo hilo. http://xhtxs.cn/8Wz

Mkusanyiko huu wa picha unafichua uzuri wa Soko la Safafeer, alama ya kihistoria katikati ya Baghdad. Kwa karne nyingi, ...
18/12/2025

Mkusanyiko huu wa picha unafichua uzuri wa Soko la Safafeer, alama ya kihistoria katikati ya Baghdad. Kwa karne nyingi, soko hili limekuwa kitovu cha ufundi wa shaba, likijulikana kwa muundo wake wa mapambo yanayong'aa na kuvutia. xhtxs.cn/8Vj

Katika picha hizi, watu wanaonekana wakipokea milo ya bure katika kituo cha makazi cha watu wasio na makazi huko New Yor...
18/12/2025

Katika picha hizi, watu wanaonekana wakipokea milo ya bure katika kituo cha makazi cha watu wasio na makazi huko New York City, Marekani, Desemba 17, 2025. http://xhtxs.cn/8Wx

Wapiganaji kutoka kundi la waasi la March 23 Movement (M23) Jumatano walianza kujiondoa kutoka katika nafasi zao huko Uv...
18/12/2025

Wapiganaji kutoka kundi la waasi la March 23 Movement (M23) Jumatano walianza kujiondoa kutoka katika nafasi zao huko Uvira, mji wa kimkakati mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), mwandishi wa habari wa Xinhua alishuhudia.
"Uhamaji wa vikosi vya AFC/M23 kutoka mji wa Uvira unaendelea na utakamilika ifikapo kesho," kiongozi wa kisiasa wa M23 Bertrand Bisimwa alisema kwenye mitandao ya kijamii X, akiwataka wakazi wa eneo hilo kuwa watulivu.
Uvira, iliyoko karibu na mpaka wa Burundi kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika, ilikuwa kituo cha utawala cha muda cha Kivu Kusini baada ya mji mkuu wa mkoa, Bukavu, kuanguka kwa M23 mnamo Februari.
Wachambuzi na vyanzo vya ndani vimeonya kwamba kupotea kwa Uvira kunaweza, baada ya muda, kufungua njia kuelekea kusini mashariki mwa DRC, ikiwa ni pamoja na Haut-Katanga, eneo muhimu la kiuchumi. Mapigano pia yameripotiwa kusini zaidi katika maeneo ya Baraka na Fizi ya Kivu Kusini. http://xhtxs.cn/8Wy

Watafiti kutoka Israel, Ujerumani na Ufaransa wamebuni mbinu mpya ya vinasaba inayorahisisha kutenganisha mbu wa kiume n...
18/12/2025

Watafiti kutoka Israel, Ujerumani na Ufaransa wamebuni mbinu mpya ya vinasaba inayorahisisha kutenganisha mbu wa kiume na wa k**e, hatua muhimu kwa utekelezaji wa programu za kudhibiti mbu kwa kiwango kikubwa, Chuo Kikuu cha Kiebrania cha Jerusalem kilisema katika taarifa yake Jumatano.
Programu hizo huachilia mbu wa kiume waliotiwa utasa pekee katika mazingira ya asili ili kudhibiti kusambaa kwa magonjwa hatari k**a Dengue, Zika na Chikungunya. Kutenganisha na kuondoa mbu wa k**e ni muhimu kwa kuwa ni mbu wa k**e pekee wanaong’ata binadamu na kusambaza magonjwa.
Mbinu hiyo mpya, iliyochapishwa katika jarida la Nature Communications, hutumia uhariri wa jeni kuwafanya mbu wa kiume kuwa na rangi nyeusi na wale wa k**e kupauka, tofauti ya wazi ya mwonekano unaowezesha utenganishaji wa haraka na sahihi zaidi. Hatua hiyo inasaidia kushinda changamoto kubwa iliyokuwepo katika programu za kudhibiti mbu.
Kwa sasa, mbinu za kutenganisha mbu kwa kuzingatia jinsia hutegemea tofauti za ukubwa wa mbu wachanga, njia ambazo ni za polepole, zinahitaji nguvu kazi nyingi, na wakati mwingine huruhusu mbu wa k**e wanaong’ata kupenya na kuachiliwa kimakosa. xhtxs.cn/8Vo

Address

Ring Road Kilimani
Nairobi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when China Xinhua News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share