Mufindi fm Radio

Mufindi fm Radio Ukurasa Maalumu wa Radio ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi. Mufindi Fm 107.3Mhz

LUHAGA MPINA ATIMKIA ACT-WAZALENDO..Aliyekuwa Mbunge wa Kisesa Mkoani Simiyu kupitia CCM, Luhaga Mpina ametangazwa rasmi...
05/08/2025

LUHAGA MPINA ATIMKIA ACT-WAZALENDO..

Aliyekuwa Mbunge wa Kisesa Mkoani Simiyu kupitia CCM, Luhaga Mpina ametangazwa rasmi kuhamia Chama cha ACT Wazalendo.

Luhaga Mpina amepokelewa katika Ofisi za ACT-Wazalendo, Vuga Visiwani Zanzibar leo August 05,2025 na Viongozi wa Chama hicho akiwemo Zitto Kabwe na Katibu Mkuu Ado Shaibu.


Ingawa majina ya wagombea waliopita kwa kura za wajumbe yametangazwa rasmi katika maeneo mbali mbali, laki maamuzi ya ma...
05/08/2025

Ingawa majina ya wagombea waliopita kwa kura za wajumbe yametangazwa rasmi katika maeneo mbali mbali, laki maamuzi ya majina hayo bado yapo mikononi mwa vikao vya kamati kuu CCM.

Je,Wajumbe unawapa asilimia ngapi kwenye Maamuzi yao...?


WAJUMBE WAMPA KURA ZA NDIYO LUQMAN MUFINDI KASKAZINI..Ndugu Luqman Mehrab ameongoza kura za maoni CCM kuwania nafasi ya ...
04/08/2025

WAJUMBE WAMPA KURA ZA NDIYO LUQMAN MUFINDI KASKAZINI..

Ndugu Luqman Mehrab ameongoza kura za maoni CCM kuwania nafasi ya ubunge Jimbo la Mufindi Kaskazini kwa kupata kura 3,798 Akifuatiwa na Mbunge aliyemaliza Muda wake, Ndugu Exaud Kigahe aliyepata Kura 488.


MAFINGA MJINI MWAMBA NI VILLA....Ndugu Dickson Lutevele (Villa) ameibuka na ushindi katika kura za maoni za ubunge ndani...
04/08/2025

MAFINGA MJINI MWAMBA NI VILLA....

Ndugu Dickson Lutevele (Villa) ameibuka na ushindi katika kura za maoni za ubunge ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Mafinga Mjini.

Ndugu Villa Amepata Kura 1219 akifuatiwa na Agrey Tonga Kura 878 na Ndugu Cosato Chumi Akipata kura 376.

Matokeo haya ni ya awali na yanatokana na mkutano mkuu wa mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM kwa ajili ya kumpata mgombea atakayewakilisha chama hicho katika Uchaguzi Mkuu ujao Matokeo hayo yametangazwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Mufindi Clemence Bakuli.


MSINGWA NA JESCA "OUT" IRINGA MJINI..Fadhili Ngajiro ameongoza Kura za maoni CCM kuwania ubunge wa jimbo la Iringa mjini...
04/08/2025

MSINGWA NA JESCA "OUT" IRINGA MJINI..

Fadhili Ngajiro ameongoza Kura za maoni CCM kuwania ubunge wa jimbo la Iringa mjini kwa kupata kura 1899 akifuatiwa na Wakili Moses 1523 huku Mchungaji Peter Msigwa akipata Kura 477 Kutoka kwa wajumbe, naye Mbunge aliyemaliza Muda wake Jesca Msambatavangu amepata kura 408 na Nguvu Chengula kura 181.


WAJUMBE WAMPITISHA CHANGOLO MAKAMBAKO....Mgombea wa nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Makambako kupitia Chama Cha Mapinduzi (...
04/08/2025

WAJUMBE WAMPITISHA CHANGOLO MAKAMBAKO....

Mgombea wa nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Makambako kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, ameibuka mshindi kwa kishindo baada ya kujizolea kura 6,151 kutoka kwa wajumbe wa chama hicho. Chongolo amewashinda wapinzani wake akiwemo Deo Sanga, aliyepata kura 470, kwa mujibu wa matokeo ya jumla kutoka kata zote za jimbo hilo.


Timu ya Taifa ya Tanzania imeanza na ushindi katika Mashindano ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani (CHAN...
02/08/2025

Timu ya Taifa ya Tanzania imeanza na ushindi katika Mashindano ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani (CHAN 2024) baada ya kuifunga Burkina Faso 2-0.

Mchezo huo wa kundi B ulikuwa ni mchezo wa ufunguzi wa michuano ya CHAN2024.

Magoli ya Taifa Stars yamefungwa na Abduli Suleiman "Sopu" dakika ya 45 na Muhammad Husen akifunga goli la pili dakika ya 74 ya Mchezo.

✍️Umeuonaje mchezo wa leo...???


WAGOMBEA CCM MAFINGA, WAJIPAMBANUA KWA SERA THABITI........Katika kuelekea upigaji wa kura za maoni ndani ya Chama cha M...
01/08/2025

WAGOMBEA CCM MAFINGA, WAJIPAMBANUA KWA SERA THABITI........

Katika kuelekea upigaji wa kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya kumpata Mgombea wa nafasi ya ubunge jimbo la Mafinga Mjini, Wagombea mbalimbali wamejitokeza kujinadi mbele ya wajumbe wa chama hicho, huku wakipambanisha sera na maono yao kwa ajili ya kuleta maendeleo ndani ya jimbo hilo.

Wagombea wa nafasi hiyo ya Ubunge katika jimbo hilo, Julai 31, 2025 wamekutana na wajumbe wa Kata ya Boma, Kata ya Upendo na Kata ya Wambi, ambapo Mratibu wa Kampeni za ubunge kura za maoni (CCM) Maines Kiwelu ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya siasa wilaya ya Mufindi amewasihi wajumbe kutafakari kwa makini sera zilizotolewa na wagombea katika kufanya maamuzi na kuwataka waache makundi.

Akizungumza katika nyakati tofauti na wajumbe wa kata ya Boma na Upendo, mbunge anayemeliza muda wake (anayetetea) nafasi hiyo ya ubunge ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Cosato David Chumi ameeleza mafanikio na dhamira yake ya dhati ya kuendelea kushirikiana na wana Mafinga katika nafasi hiyo, akiweka wazi dhana yake ya kazi zinaongea.

Mgombea Mwingine wa nafasi hiyo ya ubunge ndani ya CCM ni Agrey Tonga ambaye amewaahidi mapinduzi ya maendeleo iwapo watampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho.

Wengine ni Dickson Nathan Lutevele, Mendrad Kigola na Dkt. Bazil Lwisijo Tweve ambao wameomba ridhaa kwa wajumbe huku wakieleza vipaumbele mbalimbali iwapo wakiaminiwa.


Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara kupitia mitandao yake ya kijamii  imetangaza Tarehe ya Msimu mpya wa Ligi Kuu bara Kuwa 1...
31/07/2025

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara kupitia mitandao yake ya kijamii imetangaza Tarehe ya Msimu mpya wa Ligi Kuu bara Kuwa 16/09/2025.

29/07/2025

Mchakato wa kutangaza rasmi majina ya wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Uchaguzi Mkuu wa 2025 unaoongozwa na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, Unaendeleaje Sasa Jijini Dodoma.


BASI LA GONGA NA KUUWA WANAFUNZI 6 JIJINI MBEYA...Wanafunzi sita wa Shule ya Sekondari Chalangwa, Wilaya ya Chunya mkoan...
26/07/2025

BASI LA GONGA NA KUUWA WANAFUNZI 6 JIJINI MBEYA...

Wanafunzi sita wa Shule ya Sekondari Chalangwa, Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wamefariki baada
ya kugongwa na basi lenye namba za usajili T DCE 194 YUTONG linalomilikwa na Kampuni ya Safina linalofanya safari zake Lualaje Mbeya majira ya saa 11:30 alfajiri barabara kuu ya Chunya Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na mmoja amefariki akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Chunya na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.

ACP Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.


Address

Mafinga Iringa
Mafinga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mufindi fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mufindi fm Radio:

Share

Category