Mufindi fm Radio

  • Home
  • Mufindi fm Radio

Mufindi fm Radio Ukurasa Maalumu wa Radio ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi. Mufindi Fm 107.3Mhz

29/07/2025

Mchakato wa kutangaza rasmi majina ya wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Uchaguzi Mkuu wa 2025 unaoongozwa na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, Unaendeleaje Sasa Jijini Dodoma.


BASI LA GONGA NA KUUWA WANAFUNZI 6 JIJINI MBEYA...Wanafunzi sita wa Shule ya Sekondari Chalangwa, Wilaya ya Chunya mkoan...
26/07/2025

BASI LA GONGA NA KUUWA WANAFUNZI 6 JIJINI MBEYA...

Wanafunzi sita wa Shule ya Sekondari Chalangwa, Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wamefariki baada
ya kugongwa na basi lenye namba za usajili T DCE 194 YUTONG linalomilikwa na Kampuni ya Safina linalofanya safari zake Lualaje Mbeya majira ya saa 11:30 alfajiri barabara kuu ya Chunya Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na mmoja amefariki akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Chunya na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.

ACP Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.


MAREKEBISHO MADOGO YA KATIBA CCM YAPITA KWA ASILIMIA 99.8..…...ChamaChama Cha Mapinduzi (CCM) kimepitisha marekebisho ma...
26/07/2025

MAREKEBISHO MADOGO YA KATIBA CCM YAPITA KWA ASILIMIA 99.8..…...

ChamaChama Cha Mapinduzi (CCM) kimepitisha marekebisho madogo ya katiba yake ya mwaka 1977 (toleo la Mei 2025), kwa asilimia 99.8 ya kura za wajumbe wa mkutano maalum uliofanyika kwa njia ya mtandao.

Marekebisho hayo ni pamoja na kuongezwa kipengele kinachoruhusu k**ati kuu kuongeza idadi ya wagombea wa ubunge, ujumbe wa Baraza la Wawakilishi pamoja na udiwani watakaoshiriki kura za maoni.

Matokeo ya kura hiyo yametangazwa rasmi na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Idara ya Oganaizesheni, Issa Haji Ussi Gavu, ambaye amesema kuwa jumla ya wajumbe 1,915 walishiriki katika upigaji kura kati ya wajumbe 1,931 waliotarajiwa.


WASIMAMIZI  UCHAGUZI MKUU WATAKIWA KUSIMAMIA SHERIA........Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ( INEC ) Jaji wa...
23/07/2025

WASIMAMIZI UCHAGUZI MKUU WATAKIWA KUSIMAMIA SHERIA........

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ( INEC ) Jaji wa Mahak**a ya Rufaa, Jacobs Mwambegele amewataka waratibu na wasimamizi wa uchaguzi kuzingatia yale waliyojifunza kuhusu sheria mpya za uchaguzi, hasa kwa wale walioomba kupiga kura moja ya Rais katika maeneo ya magereza na kuzingatiwa kwa mchakato kwa maeneo yaliyobainishwa kuwa na mgombea mmoja .

Hayo ameyasema leo wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa waratibu wasimamizi na wasimamizi wasaidizi ngazi ya jimbo pamoja na maafisa ununuzi kutoka mikoa miwili Shinyanga na Simiyu mwenyekiti wa uchaguzi jaji wa mahak**a ya rufaa Jacobs Mwambegele.

Jaji Mwambegele amesema kupiga kura ya Rais nje ya kituo kwa waliojiandikisha na namna ya kusimamia uchaguzi kwenye maeneo yenye mgombea mmoja na Magerezani ni moja ya mambo machache ambayo hayakuwepo kwenye sheria zilizopita na hakuna mwenye uzoefu nayo.


WAZIRI AWESO AKAGUWA MRADI WA MAJI MAFINGA.....Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, Ametembelea na kukaguwa Mradi wa Maji m...
22/07/2025

WAZIRI AWESO AKAGUWA MRADI WA MAJI MAFINGA.....

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, Ametembelea na kukaguwa Mradi wa Maji mjini Mafinga ambapo mradi huo unaotekelezwa na Serikali kwa gharama ya zaidi shilingi bilioni 48.

Katika ziara hiyo pia, Waziri Aweso amekutana na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Kikosi 841 Mafinga, Kanali Issa Daudi Chalamila, ambapo walikubaliana kumaliza ugumu uliokuwa umejitokeza kutokana na chanzo cha maji kilichozungukwa na eneo la jeshi.

Mradi huo wa maji una umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Mafinga kwani utakapokamilika utawezesha huduma ya majisafi katika mji wa Mafinga kufika asilimia 95 kutoka 65 zinazopatikana kwa sasa, ambapo takribani watu 95,505 watanufaika na huduma ya maji bora.


KAMATI YA LISHE MUFINDI DC YAZINDUA JIKO DARASA......Kamati ya lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imefanya ziara ...
20/07/2025

KAMATI YA LISHE MUFINDI DC YAZINDUA JIKO DARASA......

Kamati ya lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imefanya ziara kata ya Ihanu na Mdabulo na kukagua utekelezaji wa afua za lishe.

Akiongoza k**ati hiyo Mwenyekiti wa k**ati ambae ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Ndg, Mashaka Mfaume.

Lengo la Ziara hiyo ilikuwa Kukagua afua za lishe zinazotekelezwa kwa robo tatu,Kugawa Jiko darasa kwenye Zahanati ya kijiji cha isipii,Kugawa Chakula lishe kwa watoto wenye utapiamlo mkali,kutembelea kaya maskini na kutoa msaada.

Wakiwa ziarani Mwenyekiti wa k**ati alipata nafasi ya kuongea na Wananchi waliojitokeza ambapo amewasisitiza kuwapatia watoto vyakula vyenye mchanganyiko(mlo bora) ili kuepuka udumavu na utapiamlo.


HATIMAE ZIBWE KAAGA MSIMBAZI...Beki wa kushoto wa timu ya simba Mohammed Husseni Zimbwe ametoa shukurani kwa uongozi na ...
19/07/2025

HATIMAE ZIBWE KAAGA MSIMBAZI...

Beki wa kushoto wa timu ya simba Mohammed Husseni Zimbwe ametoa shukurani kwa uongozi na mashabiki wa Simba baada ya kuwatumikia kwa miaka kumi na moja.

➡️Je Zimbwe atakuwa anaelekea timu gani?


WAPIGANAJI WA M23 WASAINI MKATABA WA AMANI CONGO....Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wametia...
19/07/2025

WAPIGANAJI WA M23 WASAINI MKATABA WA AMANI CONGO....

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wametia saini mkataba wa amani unaolenga kumaliza vita Mashariki mwa nchi hiyo.

Makubaliano hayo yanayolenga kumaliza mapigano mashariki ya Congo yanalenga pia kuhakikisha waasi hao wanaondoka katika maeneo wanayoyadhibiti, suala ambalo DRC imekuwa ikisisitiza lifanyike.

Baada ya makubaliaano hayo Umoja wa Afrika umesema makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya M23 na serikali ya Kinshasa ni hatua kubwa na muhimu.




Video☝️: Reuters

UTEUZI WA WAGOMBEA CCM KUFANYIKA JULAI 28......Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos M...
19/07/2025

UTEUZI WA WAGOMBEA CCM KUFANYIKA JULAI 28......

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla, amezungumza leo Julai 19, 2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama, amesema maandalizi ya Mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama unaendelea vizuri na Wagombea watulie na kwamba Kikao cha uteuzi wa mwisho ni Julai 28, 2025.

Amesema sababu ni wingi wa Wagombea, hivyo kuchukua muda mrefu kuwachambua na mpaka sasa hakuna aliyekatwa wala kufyekwa, bali chama kitafanya uteuzi na Wanachama watapewa taarifa.

"Hakuna mtu aliyekatwa, hakuna mtu aliyefyekwa k**a ilivyoandikwa. Kwa hiyo, mpaka tarehe 28 ndiyo itakuwa taarifa ya mwisho wa uteuzi wa wagombea, hivyo wananchi watulie." - Amos Makalla, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM


WATATU WAFARIKI KWA AJALI KILOLO....Ajali hiyo imetokea majira ya saa 12 asubuhi katika barabara kuu ya Morogoro Iringa,...
18/07/2025

WATATU WAFARIKI KWA AJALI KILOLO....

Ajali hiyo imetokea majira ya saa 12 asubuhi katika barabara kuu ya Morogoro Iringa, ambapo gari aina ya Fuso Mini Bus lenye namba za usajili T 562 EBK, lililokuwa likiendeshwa na marehemu Akhan Mpagile (45) mkazi wa Njombe, liligonga kwa nyuma lori aina ya Howo lenye namba T857 DVZ na Trela T460 EAM mali ya kampuni ya Glenrich Transportation Co. Ltd, lililokuwa likisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Iringa likiwa limebeba mzigo wa unga


RAIS SAMIA SULUHU AZINDUA DIRA 2050...Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hasani Leo amezindua Dir...
17/07/2025

RAIS SAMIA SULUHU AZINDUA DIRA 2050...

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hasani Leo amezindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Dira hii ni maoni ya wananchi wote ambapo kwa miaka 25 ijayo wamedhamiria kujenga Taifa jumuishi, lenye ustawi, haki na linalojitegemea.

Naye Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa alinukuliwa akisema maandalizi ya Dira yamefanyika kwa ushirikishwaji wa Wananchi, ambapo zaidi ya Watanzania Milioni 1.17 walitoa maoni yao kupitia njia mbalimbali na zaidi ya Watu 20,000 wakishiriki katika Makongamano ya Kitaifa.

Ameongeza kuwa Dira hiyo ilipitishwa na Bunge, hivyo imepewa nguvu ya Kisheria na hakuna Kiongozi anayeweza kuibadili bila ridhaa ya Bunge tofauti na Dira zilizopita.


RAIS SAMIA AWATEUWA MABEYO NA MWAKYEMBE......Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzani, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi...
16/07/2025

RAIS SAMIA AWATEUWA MABEYO NA MWAKYEMBE......

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzani, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali leo 16 Julai ikiwemo uteuzi wa Jenerali Mstaafu Venance Salvatory Mabeyo ambaye ametewaliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kwa kipindi cha pili.

Pamoja na Dkt. Harrison George Mwakyembe ametewaliwa kuwa Baraza la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kwa kipindi cha pili.


Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mufindi fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mufindi fm Radio:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share