Mufindi fm Radio

Mufindi fm Radio Ukurasa Maalumu wa Radio ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi. Mufindi Fm 107.3Mhz

RDO WAHAMASISHA VIJANA KUPIGA KURA OCTOBER 29....Shirika la Maendeleo (RDO) limeendelea kuonesha uzalendo na kujitolea k...
25/10/2025

RDO WAHAMASISHA VIJANA KUPIGA KURA OCTOBER 29....

Shirika la Maendeleo (RDO) limeendelea kuonesha uzalendo na kujitolea katika kuhamasisha ushiriki wa wananchi, hususan vijana, katika masuala ya kitaifa hasa katika uchaguzi mkuu unaofanyika Jumatano ya Oktoba 29.

Kupitia ufadhili wao RDO kwa mashirika la MMADEA na Action for Change yaliyopewa kibali cha kutoa elimu ya Mpiga kura na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Oktoba 23 wametoa elimu ya Mpiga kura kwa vijana wa Vyuo vya ufundi vilivyopo mjini Mafinga, kuelekea uchaguzi Mkuu wa Madiwani, Wabunge na rais, katika ukumbi wa chuo cha Ufundi Lutherani kilichopo Mji Mafinga mkoani Iringa.

Vyuo hivyo vya Mafunzo na Ufundi stadi vilivyoshiriki ni Pamoja na Chuo cha RDO Mafinga, chuo cha Mafunzo NAJA, Chuo cha Misitu na bidhaa za misitu (Fwitic) Pamoja na Chuo cha Mafunzo Lutherani (Mwenyeji).

Akizungumza Mratibu wa Vyuo vya RDO Tanzania Ndg. Obadia Ngailo amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo vijana na kuwapa uelewa sahihi kuhusu umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu, ikizingatiwa kuwa wengi wao tayari wana sifa za kupiga kura katika uchaguzi huu.

Naye Mkufunzi wa mafunzo hayo, Ndg. Raphael Mtitu ambaye ni Mkurugenzi wa shirika la MMADEA linaloendesha hughuli zake mkoani Iringa, na Renatus Mpiluka ambaye ni Mratibu wa Shirika la Action for Change wamewahimiza vijana kujitokeza kuchagua viongozi wanaowataka badala ya kuwaachia wengine kufanya maamuzi kwa niaba yao.


Endelea kutusikiliza redioni na ujishindie zawadi kali zaidi ya zote!Fuatilia vipindi vyetu, shiriki promosheni zetu na ...
23/10/2025

Endelea kutusikiliza redioni na ujishindie zawadi kali zaidi ya zote!
Fuatilia vipindi vyetu, shiriki promosheni zetu na wewe unaweza kuwa mshindi wa pikipiki, mafuta au vifaa vya kifahari nyumbani!

GESI YENTE, Kila mtu apate!

DC LINDA AHAMASISHA MUFINDI KUPIGA KURA OCTOBER 29 2025...Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mh. Dkt Linda Salekwa ametoa wito kw...
23/10/2025

DC LINDA AHAMASISHA MUFINDI KUPIGA KURA OCTOBER 29 2025...

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mh. Dkt Linda Salekwa ametoa wito kwa wananchi wilayani Mufindi kujitokeza kwa wingi kupiga kura akiitaja kura k**a kichocheo muhimu katika kuamua mustakabali wa Maendeleo ya Wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza na vyombo vya habari Mkuu huyo wa Wilaya Mh. Dkt.Salekwa, amesema hatua ya Wananchi kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura ni hatua muhimu katika kuimarisha misingi ya demokrasia na kuleta Maendeleo endelevu.

Aidha Dkt Linda amewataka wananchi kutokukubali upotoshaji unaoendelea katika mitandao ya kijamii kuhusu Uchaguzi mkuu, amesema wapotoshaji wana nia ovu kwa maendeleo ya jamii hivyo wananchi wanapaswa kupuuza uzushi na kujiandaa kikamilifu kwaajili ya kupiga kura juma lijalo oktoba 29 Mwaka huu.

Mbali na hayo Dr Salekwa amewataka waananchi kujiepusha na vitendo vyovyote vitakavyoashiria vurugu hali itakayosababisha ukosefu wa amani na utulivu wakati wa uchaguzi jambo ambako halitovumiliwa na vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na rais mwaka 2025, unafanyika ukiwa ni uchaguzi wa Saba kufanyika tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 huku ukibebwa na kauli mbiu ya Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura.


ATUHUMIWA KUMUUA MKEWE, KISHA KUMTUPA KISIMANI- ISALAVANU.....Mwanaume mmoja, anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 3...
09/10/2025

ATUHUMIWA KUMUUA MKEWE, KISHA KUMTUPA KISIMANI- ISALAVANU.....

Mwanaume mmoja, anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30-35, Mkulima na mkazi wa Kijiji cha Isalavanu, kata ya Isalavanu wilayani Mufindi mkoani Iringa, anayejulikana kwa jina la Lemi Soveyage anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Iringa kwa tuhuma za kumuua mke wake Fediana Ngowo (26-28) na kisha kuutupa mwili wake katika kisima cha maji.

Tukio hilo limegundulika siku ya Jumanne Oktoba 07, 2025, baada ya mtuhumiwa huyo kuripoti kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho, ndipo k**ati ya Ulinzi na usalama wa Kijiji ikafanya upelelezi wa eneo ambalo inatajwa aliondokea mama huyo na kukuta miburuzo inayoonesha mtu alikuwa akiburuzwa, ambapo walifuatilia mpaka eneo hilo la kisima, na walipochungulia ndani ya kisima hicho wakabaini kuwa, kuna mtu.

Akisimulia tukio hilo Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kidegemanga kilichopo Kijiji hapo Ndg. Jumanne Mwilongo, amesema Jumatatu ya Oktoba 06 mwaka huu, Mtuhumiwa alifika na kuripoti, akidai kuwa mke wake haonekani tangu siku ya Jumapili kuamukia hiyo Jumatatu ya oktoba 06 na kwamba anamtafta.

Inaelezwa kuwa, kabla ya tukio, wawili hao walikuwa na ugomvi ambapo siku ya jumapili ya Oktoba 06, mashuhuda walisikia yowe na Kwenda kuamulia ugomvi huo na kufanikiwa kuutuliza ambapo baadaye inaelezwa kuwa, ugomvi huo ukarejea tena.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho cha Isalavanu Ndg. Huruma Mpinga amesema kuwa, baada ya kufanya msako wa kumtafta mwanamke huyo (Marehemu kwa sasa) na kuupata mwili wae, walimhoji mtuhumiwa na alikiri kuwa ametekeleza tukio hilo kwa bahati mbaya.


KILUMBE , LUQUMAN WAMNADI KIGAHE IHALIMBA Naibu Katibu Mkuu wa  Jumuiya ya Wazazi Tanzania bara (CCM Taifa) Ndg. Kilumbe...
08/10/2025

KILUMBE , LUQUMAN WAMNADI KIGAHE IHALIMBA

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania bara (CCM Taifa) Ndg. Kilumbe Ng'enda amemnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Exaud Kigahe kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 29 Oktober 2025.

Ng'enda amefika Katika Kijiji cha Nundwe Kata ya Ihalimba Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa ambapo mbali na kumuombea kura mgombea Urais kupitia CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan Ndg. Ng'enda akimuombea kura Kigahe amewaambia Wananchi kuwa Kigahe ni mtu sahihi kwani ameaminiwa na Serikali kwa kuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara kwa muda mrefu.

Kwa upande wake Mh. Exaud Kigahe akiwaomba Wananchi wamchague ameeleza kuwa Maendeleo ni hatua hivyo watarajie mambo mazuri zaidi iwapo atashinda kwa muhula ujao.

Mbali na hayo mmojawapo wa waliokua watia nia wakati wa mchakato wa kura za Maoni Ndg. Luqman Merhab amemuombea Kigahe kura za Kishindo na CCM kwa ujumla akieleza kuwa mchakato wa kura za Maoni ushapita hivyo ni muda wa kukipambania Chama cha Mapinduzi.


Shamba la Miti Sao Hill limefungua pazia la elimu ya udhibiti wa majanga ya moto kwa mwaka 2025-2026 kwa kukutana na vio...
01/10/2025

Shamba la Miti Sao Hill limefungua pazia la elimu ya udhibiti wa majanga ya moto kwa mwaka 2025-2026 kwa kukutana na viongozi wa serikali za mitaa kutoka katika maeneo yote ya shamba hilo ikiwa ni juhudi za kuendeleza ustawi wa uhifadhi wa mazingira na kilimo cha miti wilayani Mufindi.

Shamba hilo linalosimamiwa na wakala wa huduma za misitu nchini (TFS) kila mwaka limekuwa na utaratibu wa kuelimisha jamii inayoizunguka kuhusu majanga ya moto na athari zake hali inayosaidia kuzuia na kupungua kwa matukio ya uchomaji moto katika hifadhi za msitu huo na mashamba ya wananchi.

Akizungumza na viongozi waliohudhuria kikao kazi kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi uliopo eneo la bomani mjini Mafinga, Katibu tawala wilaya ya Mufindi Ndugu Ruben Chongolo amesema suala la kutokomeza moto linawezekana ikiwa kutaimarishwa mawasiliano na mahusiano ya wote waliopo katika mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu.

Nae Mhifadhi mkuu wa shamba hilo PCO Tebby Yoram amesema elimu wanayoitoa kwa viongozi wa serikali za mitaa na wananchi kwa ujumla inalenga kuifanya rasilimali ya misitu inayowekezwa kwa gharama kubwa inakuwa salama na kuleta tija kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Washiriki waliohudhuria kikao kazi hicho ni pamoja na maafisa tarafa,watendaji wa kata,vijiji na mitaa pamoja na wenyeviti wa vijiji huku malengo ni kuhakikisha elimu hii kwa mwaka huu inatolewa katika vijiji 25.


Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Joseph Kabila, amehukumiwa kifo kwa akiwa hayupo mahak**ani kw...
30/09/2025

Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Joseph Kabila, amehukumiwa kifo kwa akiwa hayupo mahak**ani kwa makosa ya uhalifu wa kivita na usaliti.

Madai dhidi yake yanahusu tuhuma kwamba Kabila amekuwa akiliunga mkono kundi la M23, kundi la waasi lililoharibu na kusababisha madhara makubwa katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo.

Kabila alipatikana na hatia Ijumaa na mahak**a ya kijeshi kwa makosa ya usaliti, uhalifu dhidi ya binadamu, na uhalifu wa kivita ikiwemo mauaji, unyanyasaji wa kingono, mateso na uasi.


'Rafiki wa Bintie' yaendeleza uwezeshaji kwa WasichanaMradi wa Rafiki wa Bintie, unaofadhiliwa na Rafiki Australia Tanza...
30/09/2025

'Rafiki wa Bintie' yaendeleza uwezeshaji kwa Wasichana

Mradi wa Rafiki wa Bintie, unaofadhiliwa na Rafiki Australia Tanzania, umeendelea na jitihada za kuwawezesha watoto wa k**e kwa kugawa jumla ya pakiti 500 za taulo za k**e katika shule mbili za Halmashauri ya Mji Mafinga, mkoani Iringa.

Katika zoezi hilo, shule ya sekondari Kinyanambo imenufaika kwa kupokea pakiti 395, huku shule ya msingi Mkombwe ikitarajia kukabidhiwa pakiti 105 kesho, Oktoba 1.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Mradi huo, Saum Zidadu, amesema lengo kuu ni kuhakikisha watoto wa k**e wanapata mahitaji muhimu ya afya ya uzazi ili kuepukana na hali wanazokutana nazo na kupelekea utoro na kushuka kwa ufaulu wakati wa hedhi.

Bi. Zidadu ameongeza kuwa, tangu waanze mradi huo, wamekuwa wakishirikiana kwa ukaribu na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi, kupitia ofisi yake, katika kuhakikisha ndoto za watoto wa k**e zinatimia kwa kupata vifaa vya kujistiri.

Kwa upande wake, Hezroni Uhaula, aliyekuwa Katibu wa Mbunge na Naibu Waziri huyo, amesema msaada huo utawajengea ujasiri wasichana hao shuleni na kuimarisha mahudhurio yao.


FT: Mbeya City 0-0 Yanga SC
30/09/2025

FT: Mbeya City 0-0 Yanga SC

30/09/2025

ASKOFU MWAGALA ATOA TAARIFA YA PADRI KIBIKI.....

Askofu Mkuu Jimbo katoliki Mafinga Vincent Cosmas Mwagala, Ametoa taarifa kuhusiana na tukio la kupotea kwa Padri na kuonekana tena Jijini Mbeya.

Askofu Mwagala amesema Padri Jordan Kibiki alikutwa Mbeya akiwa na shida ya Unyongefu wa afya ya akili na hivyo anaendelea na matibabu katika hospital ya Tosamaganga.


KIGAHE AANZA KUSAKA KURA MUFINDI KASKAZINI.....Mgombe Ubunge Jimbo la Mufindi Kaskazini Ndugu, Exaud Kigahe amezindua ra...
27/09/2025

KIGAHE AANZA KUSAKA KURA MUFINDI KASKAZINI.....

Mgombe Ubunge Jimbo la Mufindi Kaskazini Ndugu, Exaud Kigahe amezindua rasmi kampeni zake za Uchaguzi katika Kata ya Ikweha na kuwaomba wananchi wa kata hiyo kuamini kuwa maendeleo ni hatua na tayari hatua hizo zinaonekana katika maeneo yao.

Kigahe ambaye anawania nafasi hiyo kwa muhula wa pili amesema kazi kubwa imefanyika katika jimbo hilo chini ya serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambapo sekta zote muhimu ikiwemo Maji, Barabara,Nishati,Elimu na Afya zimeguswa.

Kwa upande wake Mgombea udiwani kata ya Ikweha Ndugu Alberto Chaula amemtaja Kigahe k**a kiongozi mwenye hulka ya ukimya anayeamini katika utendaji kuliko uzungumzaji jambo ambalo linampa matumaini ya maendeleo makubwa zaidi ikiwa atachaguliwa na wananchi wa kata yake na jimbo zima kwa ujumla.

Katika siku yake ya kwanza ya Kampeni Jimboni Mufindi Kaskazini, Kigahe amefanya mikutano mitatu katika vijiji vya Ikweha,Ugenza,Ukelemi na Uyela katika kata ya Ikweha tarafa ya Sadani huku mikutano k**a hiyo ikitarajiwa kuendelea katika maeneo mengine ya jimbo hilo.


WANANCHI 3000 KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOKA KWA MADAKTARI  WA RAIS SAMIA.......‎‎‎Jumla ya Madaktari bingwa 45 ...
23/09/2025

WANANCHI 3000 KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOKA KWA MADAKTARI WA RAIS SAMIA.......


‎Jumla ya Madaktari bingwa 45 wa Rais Samia wamewasili katika Mkoa wa Iringa kwa lengo la kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kusafiri nje ya mkoa huo kufuata huduma za matibabu.

‎Akizingumza Septemba 22, 2025 wakati wa kuwapokea madaktari hao Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, amesema ujio wa madaktari hao utasaidia kupunguza gharama za wananchi kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma katika hospitali za kanda na mikoa mingine.

‎"Nawasihi wananchi wote kuichukulia uzito fursa hii adimu ambazo Mhe. Rais ametuletea, tujitokeze kwa wingi ili tuweze kufahamu afya zetu kwa kupata uchunguzi wa kibingwa" amesema Mkuu wa Mkoa

‎Naye Mratibu wa zoezi hilo kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mac Donald Ulimbakisye amesema madaktari bingwa wamejipanga kutoa huduma kwa ufanisi mkubwa kwa wagonjwa watakaojitokeza katika maeneo mbalimbali ya mkoa hivyo wajitokeze kwa wingi ili kunufaika na huduma hizo.

‎Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Sylivia Mamkwe amesema huu ni ujio wa awamu ya nne ya madaktari bingwa mkoani humo, ambapo katika awamu ya tatu zaidi ya wananchi elfu mbili walifikiwa na kupata huduma hizo.

‎Huduma zinazotolewa na madaktari hao zinajumuisha fani saba za kibingwa ikiwemo magonjwa ya wanawake na ukunga, magonjwa ya ndani, magonjwa ya kinywa na meno, Upasuaji, usingizi na ganzi, watoto na watoto wachanga na muuguzi bobezi.

‎Huduma hizo zinaanza kutolewa Septemba 22 2025 hadi tarehe Septemba 26 2025, katika hospitali za wilaya za zilizopo katika Halmashauri tano za Mkoa wa Iringa.


Address

Mafinga Iringa
Mafinga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mufindi fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mufindi fm Radio:

Share

Category