Mufindi fm Radio

Mufindi fm Radio Ukurasa Maalumu wa Radio ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi. Mufindi Fm 107.3Mhz

KARIAKOO DERBY: NGAO YA JAMII 2026➡️ Mchezo Ni Mapumziko 🔰1️⃣🦁0️⃣⚽ Albert Kangwanda Umekionaje Kipindi Cha Kwanza...? Un...
12/08/2026

KARIAKOO DERBY: NGAO YA JAMII 2026

➡️ Mchezo Ni Mapumziko

🔰1️⃣
🦁0️⃣

⚽ Albert Kangwanda

Umekionaje Kipindi Cha Kwanza...? Una Kipi Cha Kuzungumza?

12/08/2026

SIMBA KWENYE MCHEZO WA LEO WANA PRESHA ZAIDI KULIKO YANGA...

Simba wanaingia kwenye mchezo wa leo wakiwa na presha kubwa zaidi ukilinganisha na Yanga, hasa kutokana na matarajio makubwa ya mashabiki na umuhimu wa matokeo katika mchezo huo.

Kwa upande wa Yanga, timu hiyo inaweza kuingia uwanjani ikiwa na utulivu zaidi, huku Simba wakitakiwa kuonyesha kiwango kikubwa na kupata matokeo yatakayowaridhisha mashabiki wao.

10/08/2026

Vikosi vya Simba Sports Club na Young Africans Sports Club vinaendelea kuvutia kutokana na kuwa na wachezaji wenye uwezo na ubora katika maeneo mbalimbali ya uwanja.

Kwa kuangalia ubora wa wachezaji kutoka pande zote mbili, Simba na Yanga zinaonekana kuwa na vikosi vyenye ushindani mkubwa, huku kila timu ikiwa na nyota wanaoweza kubadilisha matokeo ya mchezo wakati wowote.

10/08/2026

SULEMANI MWALIMU ATAMWEKA NJE DOUMBIA KWENYE KIKOSI CHA KWANZA CHA SIMBA...?

Swali limeibuka miongoni mwa mashabiki wa Simba Sports Club kuhusu nafasi ya mshambuliaji Ibrahim Doumbia katika kikosi cha kwanza, baada ya Selemani Mwalimu kuonyesha kiwango kinachowapa matumaini mashabiki.

Doumbia ameongezwa kwenye safu ya ushambuliaji ya Simba kuelekea msimu wa 2026/27, huku Mwalimu akiwa miongoni mwa washambuliaji wanaotarajiwa kupigania nafasi katika kikosi hicho..?

PROGRAM 🔊

08/08/2026

MKUU WA IDARA YA KILIMO MUFINDI DC AELEZEA KILIMO CHA MUFINDI....

Mkuu wa Idara ya Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, Damas Lubuva, ameelezea hali ya kilimo katika Wilaya ya Mufindi, pamoja na shughuli mbalimbali za kilimo zinazofanywa na wakulima wilayani humo.

Damas ameyasema hayo wakati akizungumza katika Banda la Mufindi lililopo kwenye Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambapo Halmashauri ya Mufindi inashiriki Maonesho ya Nane Nane.

Amesema maonesho hayo ni fursa muhimu ya kutangaza na kuonesha shughuli za kilimo zinazofanyika Mufindi, huku yakitoa nafasi kwa wakulima kupata maarifa, masoko na kuunganishwa na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo.

08/08/2026

MAZIWA KUTOKA MUFINDI YAKUBALIKA SOKONI.......

Maziwa yanayozalishwa na wafugaji kutoka Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa, yameendelea kupata umaarufu na kukubalika sokoni kutokana na ubora wake.

Hayo yameelezwa katika Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambapo bidhaa mbalimbali za mifugo kutoka Mufindi zimeoneshwa kwa wananchi na wadau wa sekta ya mifugo.

RAIS SAMIA: TANZANIA KUFIKIA ASILIMIA 9.4 KATIKA MAENDELEO YA KILIMO.........Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sa...
08/08/2026

RAIS SAMIA: TANZANIA KUFIKIA ASILIMIA 9.4 KATIKA MAENDELEO YA KILIMO.........

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania iko kwenye kasi kubwa ya maendeleo ya kilimo na kwamba, kwa mwenendo uliopo, nchi inaweza kufikia asilimia 9.4 ifikapo mwakani.

Rais Samia ameyasema hayo leo, Agosti 8, 2026, katika kilele cha Sikukuu ya Nane Nane mkoani Dodoma, akisisitiza kuwa maendeleo yanayopatikana katika sekta ya kilimo yanaipa Tanzania nafasi ya kutambuliwa miongoni mwa nchi zinazoendelea kwa kasi katika kilimo. Maonesho ya Nane Nane 2026 yanafanyika Agosti 1–8.

08/08/2026

SABABU ZA ASALI YA MGOLOLO KUWA BORA...

Mfugaji na mfanyabiashara wa asali kutoka Mgololo, Wilaya ya Mufindi, amesema moja ya sababu zinazofanya asali ya Mgololo kuwa bora ni mazingira ambayo nyuki huzalisha asali hiyo.

Amesema nyuki hupata maua katika mashamba ya miti, jambo linalowezesha kupata malighafi ya kutosha na kuchangia ubora wa asali inayozalishwa.

Ameeleza hayo akiwa katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambako yanafanyika Maonesho ya Nane Nane, huku akibainisha kuwa ufugaji wa nyuki na uzalishaji wa asali ni fursa muhimu kiuchumi kwa wananchi wa Mgololo na Wilaya ya Mufindi.

AFISA MTENDAJI AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA KWA KUMUUA MKEWE.....Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu aliyekuwa A...
08/08/2026

AFISA MTENDAJI AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA KWA KUMUUA MKEWE.....

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemhukumu aliyekuwa Afisa Mtendaji wa Kata ya Gongolamboto, Dominic Mushi (34), kunyongwa hadi kufa, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mkewe, Diana Hugo, kwa kumnyonga.

Mushi alidaiwa kumuua mkewe Diana Hugo Oktoba 14, 2024, katika eneo la Kinyerezi Kichangani, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Diana, ambaye alikuwa mfanyakazi wa Benki ya NMB, Tawi la Airport, aliuawa kwa kunyongwa na baadaye mwili wake ulikutwa kitandani ukiwa umetokwa na damu katika maeneo ya puani, masikioni na mdomoni.

Katika maelezo ya awali aliyoyatoa kituo cha polisi, Mushi alidai kuwa kele­le za kuomba msaada alizokuwa akizitoa mke wake usiku huo zilikuwa ndoto, akieleza kuwa mke wake alikuwa na tabia ya kutoa sauti usiku.

08/08/2026

Address

Mafinga Iringa
Mafinga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mufindi fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mufindi fm Radio:

Shortcuts

Share

Category