19/07/2025
UTEUZI WA WAGOMBEA CCM KUFANYIKA JULAI 28......
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla, amezungumza leo Julai 19, 2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama, amesema maandalizi ya Mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama unaendelea vizuri na Wagombea watulie na kwamba Kikao cha uteuzi wa mwisho ni Julai 28, 2025.
Amesema sababu ni wingi wa Wagombea, hivyo kuchukua muda mrefu kuwachambua na mpaka sasa hakuna aliyekatwa wala kufyekwa, bali chama kitafanya uteuzi na Wanachama watapewa taarifa.
"Hakuna mtu aliyekatwa, hakuna mtu aliyefyekwa k**a ilivyoandikwa. Kwa hiyo, mpaka tarehe 28 ndiyo itakuwa taarifa ya mwisho wa uteuzi wa wagombea, hivyo wananchi watulie." - Amos Makalla, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM