Uvoro TV Business .

  • Home
  • Uvoro TV Business .

Uvoro TV Business . Kenya region.
(3)

Uvoro TV is among Kenya's best TV channels broadcasting in English & kiswahili.We take pride in the provision of indispensable source of information, music, and entertainment while strengthening the civic and cultural life of the larger Mt.

Naibu Kiongozi wa Chama cha Justice and Freedom Party (JFP), Reuben Kigame, ametangaza nia yake ya kuwania urais katika ...
28/07/2025

Naibu Kiongozi wa Chama cha Justice and Freedom Party (JFP), Reuben Kigame, ametangaza nia yake ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Akizungumza katika mahojiano na runinga ya kitaifa siku ya Jumatatu, Julai 28, 2025, mwanamuziki huyo wa nyimbo za injili alisema kuwa kampeni yake itajengwa juu ya misingi ya uongozi wa maadili, uadilifu na tabia bora.


Seneta Mteule Karen Nyamu Amuunga Mkono Rais Ruto, Asema Hana Wasiwasi na Wakosoaji.Seneta mteule Karen Nyamu amesema ku...
28/07/2025

Seneta Mteule Karen Nyamu Amuunga Mkono Rais Ruto, Asema Hana Wasiwasi na Wakosoaji.

Seneta mteule Karen Nyamu amesema kuwa hakuna mtu anayeweza kumtatiza Rais William Ruto au kumkosesha usingizi, akieleza kuwa Rais amepitia changamoto nyingi hadi kufikia mamlaka ya juu nchini.

“Eti kuna mtu anajidanganya anaweza kumkosesha Rais Ruto usingizi, mtu ambaye amepambana na marais hadi akawa rais mwenyewe?” alihoji Nyamu.

Akizungumza kwa msimamo thabiti, Nyamu alisisitiza kuwa Rais Ruto alichaguliwa na Mungu, na kwamba yeye pamoja na wafuasi wake hawataogopa kuzungumza kwa ujasiri.

“Tuko pamoja nawe. Tutazungumza kwa ujasiri kwa sababu tunajua tuko upande wa haki,” aliongeza.


Polisi katika eneo la Molo, Kaunti ya Nakuru, wamemk**ata kijana mwenye umri wa miaka 16 kwa tuhuma za kumuua mama yake ...
28/07/2025

Polisi katika eneo la Molo, Kaunti ya Nakuru, wamemk**ata kijana mwenye umri wa miaka 16 kwa tuhuma za kumuua mama yake kufuatia mzozo wa kifamilia uliozuka siku ya Ijumaa.

Kamanda wa Polisi wa Molo, Timon Odingo, alieleza kuwa kijana huyo alimshambulia mama yake, Beth Wanjiku mwenye umri wa miaka 48, kisha akajaribu kuficha mauaji hayo kwa kumzika katika kaburi la kina kifupi ndani ya nyumba ya zamani katika boma lao.

Odingo alisema kijana huyo alikiri kutekeleza kitendo hicho kutokana na hasira baada ya mama yake kukataa kumweleza jina la baba yake.

“Inadaiwa kwamba alimhoji mama yake kuhusu baba yake, lakini mama hakutoa taarifa yoyote. Hapo ndipo kijana alimpiga hadi akafariki kisha akamzika kwa siri,” alisema afisa huyo.


Wakazi wa Embu wameapa kumpokea Mukunji katika daraja la Rupingazi na kutembea naye hadi Cylet k**a ishara ya mshik**ano...
26/07/2025

Wakazi wa Embu wameapa kumpokea Mukunji katika daraja la Rupingazi na kutembea naye hadi Cylet k**a ishara ya mshik**ano.



Mbunge wa Manyatta, Gitonga Mukunji, anatarajiwa kupokelewa kwa mapokezi makubwa leo, Jumamosi Julai 26, mjini Embu kuan...
26/07/2025

Mbunge wa Manyatta, Gitonga Mukunji, anatarajiwa kupokelewa kwa mapokezi makubwa leo, Jumamosi Julai 26, mjini Embu kuanzia saa saba mchana.

Hafla hiyo inatarajiwa kuwavutia wakazi kwa maelfu pamoja na viongozi wa kisiasa kutoka maeneo mbalimbali, ikiwa ni ishara ya kuonyesha mshik**ano na uungwaji mkono mkubwa kwa Mukunji kutoka kwa wananchi na wafuasi wake.


Wafanyabiashara wawili wa Mji Wa Embu walipata majeraha  leo baada ya kutokea makabiliano makali kati yao na maafisa wa ...
25/07/2025

Wafanyabiashara wawili wa Mji Wa Embu walipata majeraha leo baada ya kutokea makabiliano makali kati yao na maafisa wa kaunti waliokuwa wakitekeleza oparesheni ya kuwafurusha kutoka kituo cha Manyatta, Embu. Tukio hilo lilizua mvutano mkali, na kusababisha magari ya uchukuzi wa umma (PSV) kuondoka haraka eneo hilo. Baadhi ya matatu ziliharibiwa, huku vioo vyake vikivunjwa wakati wa vurugu.

Polisi walijaribu kuingilia kati na kutawanya umati wa wananchi waliokuwa na hasira, lakini walishindwa kudhibiti hali hiyo. Mashuhuda walitaja matumizi ya nguvu kupita kiasi na maafisa wa kaunti kuwa chanzo cha vurugu hizo, wakisema walikuwa wakiwahangaisha wafanyabiashara waliokuwa wakitafuta riziki ya kila siku.

Kwa sasa hali bado ni tete, huku wito ukitolewa kwa utulivu na viongozi wa eneo hilo pamoja na serikali ya kaunti kuchukua hatua za haraka kurejesha amani na utulivu katika eneo hilo.


Rais William Ruto amepata uhuru wa  kuendelea na ujenzi wa kanisa la thamani ya Shilingi bilioni 1.2 ndani ya Ikulu, baa...
25/07/2025

Rais William Ruto amepata uhuru wa kuendelea na ujenzi wa kanisa la thamani ya Shilingi bilioni 1.2 ndani ya Ikulu, baada ya mahak**a kukataa kutoa agizo la kuusimamisha ujenzi huo huku ikipanga kusikiliza kesi mbili zilizowasilishwa kupinga mradi huo tarehe 22 Septemba 2025.

Hatua hiyo ilijiri baada ya Mwanasheria Mkuu Dorcas Oduor kuwasilisha pingamizi, akisema kuwa mahak**a ya kikatiba haina mamlaka ya kushughulikia kesi zinazohusu matumizi ya ardhi. Kwa mujibu wa wakili wake Emmanuel Bitta, Mahak**a ya Mazingira na Ardhi ndiyo yenye uwezo wa kushughulikia masuala k**a hayo.

"Mahak**a hii imezuiwa wazi na Ibara ya 165(5)(b) ya Katiba, ikisomwa pamoja na Ibara ya 162(2)(b) na Sehemu ya 4 na 11 ya Sheria ya Mahak**a ya Mazingira na Ardhi, kushughulikia mizozo inayohusu matumizi, umiliki au hati ya ardhi, ikiwemo ardhi ya umma," alieleza Bitta.


Mahak**a imempa msanii wa Mugithi na afisa wa polisi, Samuel Muchoki almaarufu Samidoh, dhamana ya kujikimu ya Shilingi ...
25/07/2025

Mahak**a imempa msanii wa Mugithi na afisa wa polisi, Samuel Muchoki almaarufu Samidoh, dhamana ya kujikimu ya Shilingi 200,000, hatua inayomzuia kuk**atwa kufuatia madai ya kutowajibika kazini.


Mbunge mteule Sabina Chege amesema kuwa Naibu Rais Kithure Kindiki ndiye kiongozi wa kisiasa mwenye ushawishi mkubwa na ...
25/07/2025

Mbunge mteule Sabina Chege amesema kuwa Naibu Rais Kithure Kindiki ndiye kiongozi wa kisiasa mwenye ushawishi mkubwa na cheo cha juu zaidi katika eneo la Mlima Kenya kwa sasa.

Akizungumza kwenye runinga moja siku ya Ijumaa, Julai 25, 2025, Sabina alieleza kuwa Kindiki pekee ndiye anayestahili kuwaunganisha viongozi wa eneo hilo na kufanya maamuzi muhimu.


Mfanyabiashara Godfrey Mwasiaga Kakan Maiyo ameahidi kuwa hatatetemeka katika kusema ukweli kwa wenye mamlaka, licha ya ...
25/07/2025

Mfanyabiashara Godfrey Mwasiaga Kakan Maiyo ameahidi kuwa hatatetemeka katika kusema ukweli kwa wenye mamlaka, licha ya kuk**atwa hivi karibuni na maafisa wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI).

Akizungumza kwenye runinga moja ya hapa nchini siku ya Ijumaa, Julai 25, 2025, Maiyo alieleza kuwa tukio hilo limemfunza kuwa na hekima na tahadhari katika matumizi ya maneno yake.


Mwanaume   mmoja busia  amehukumiwa kifungo cha maisha jela na mahak**a ya Malaba baada ya kupatikana na hatia ya kumuua...
25/07/2025

Mwanaume mmoja busia amehukumiwa kifungo cha maisha jela na mahak**a ya Malaba baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mwendeshaji wa boda boda mnamo Agosti 17, 2023.

Hakimu Mkuu wa Mahak**a ya Malaba, Ocharo Momanyi, alipata Geoffrey Wafula Malunda na hatia ya kumuua Jeremiah Otwane Papa kabla ya kutoweka na pikipiki yake pamoja na simu ya mkononi.

Mahak**a iliambiwa kuwa Malunda, pamoja na washukiwa wengine ambao hawakuwapo mahak**ani, walimvamia na kumjeruhi Papa katika eneo la Upland Estate lililoko mjini Malaba, Kaunti ya Busia.


Gavana wa Kaunti ya Embu, kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, ametangaza kuwa bajeti ya mwaka wa kifedha 2025/2...
24/07/2025

Gavana wa Kaunti ya Embu, kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, ametangaza kuwa bajeti ya mwaka wa kifedha 2025/2026 imesainiwa rasmi leo. Amesema bajeti hiyo inalenga kuimarisha uwekezaji wa kimkakati katika sekta muhimu, kwa madhumuni ya kuboresha utoaji wa huduma, kuongeza ufanisi, na kuinua viwango vya maisha ya wakazi wa kaunti hiyo.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wakuu wa kaunti akiwemo Spika wa Bunge la Kaunti Mheshimiwa Thiriku, Kiongozi wa Wengi Mheshimiwa Murithi Kobole, Kiongozi wa Wachache Mheshimiwa Mbaka, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Mheshimiwa Edwin Murithi.


Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uvoro TV Business . posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uvoro TV Business .:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share