06/12/2025
π Hongera Sana, Albert Mwanyasi! π
Pongezi nyingi kwa Albert Mwanyasi wa SIFA 107.7 FM VOI kwa kufanya makuu tena katika Tuzo za Association of Grassroot Journalists Kenya (AGJK) zilizokamilika hapo jana!
Albert, ambaye alikuwa Mwanahabari Bora wa Mwaka 2022 wa AGJK, amerudi kwa kishindo na kuibuka Mshindi wa Pili (1st Runners-Up) katika tuzo mbili muhimu:
π Tuzo ya Uandishi wa Uchunguzi (Investigative Reporting)
π Tuzo ya Uandishi wa Masuala ya Ardhi, Makazi na Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi. (Land, Housing, and Climate Resilience Reporting)
Tuzo hiyo hiyo ambayo Mike Kwoba wa SIFA FM Marsabit aliibuka mshindi.
Kazi yako inaendelea kugusa jamii, kuibua hoja nzito, na kuangazia simulizi za watu wa kawaida. Tunajivunia ufanisi wako, ustahimilivu na kujituma kwako katika kuhabarisha na kuelimisha jamii. Hongera sana kwa kurejea na kungβara kwa upekee, Albert!
Hongera pia kwa Susan Mbodze wa SIFA FM Marsabit kwa kushinda Award ya Uandishi wa Michezo, Sanaa na Utamaduni.
π» Na shukrani za pekee kwa SIFA FM Marsabit kwa kuibuka Kituo Bora cha Radio ya Jamii mwaka huu! Mnafanya kazi ya kuleta mabadiliko na kuinua sauti za jamii kote nchini.
π Asante AGJK kwa kutambua mchango wa wanahabari wa ngazi ya jamii na kuendelea kuhimiza uandishi wenye athari kwa wananchi.
Hapa ni safari ya mafanikio zaidi, athari zaidi, na nuru zaidi kwa SIFA FM na familia nzima ya wanahabari wa grassroots! π