Safari Media

Safari Media Safari Media is a News/Media Company
Subscribe youtube channel now
www.youtube.com/channel/UCGml3vag_bwtdS_o7lp3YpA?sub_confirmation=1

17/07/2025

ZIFAHAMU SABABU ZA KIZZ DANIEL KUBADILISHA JINA LAKE

Hizi ndio sababu zilizopelekea msanii kutoka nchini Nigeria Kizz daniel kubadilisha sehemu ya jina lake mwaka 2017

Msanii huyo alikuwa amesainiwa kwenye lebo inayofahamika k**a G World Wide Entertainment ambayo ilisimamia haki miliki za album ya kwanza ya msanii huyo inayofahamika k**a New Era

Usikose kusikiliza kipindi cha burudani cha Baab kubwa one xtra kinachoruka kupitia Safari radio kila siku ya jumatatu mpaka ijumaa kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi jioni

Ungana na na

WASIMAMIZI WA UCHAGUZI MTWARA NA LINDI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI Wasimamizi wa Uchaguzi kutoka katika mikoa y...
17/07/2025

WASIMAMIZI WA UCHAGUZI MTWARA NA LINDI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI

Wasimamizi wa Uchaguzi kutoka katika mikoa ya Mtwara na Lindi, wametakiwa kuzingatia sheria na kanuni za uchaguzi wakati watakapokuwa wakisimamia zoezi hilo linalotarajiwa kufanyika mwezi October mwaka huu.

Ushauri huo umetolewa na mratibu wa mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu Tanzania tawi la Mtwara Bi.Sesilia Sepanjo wakati akihitimisha mafunzo hayo leo Julai 17,2025 yaliyoandaliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Sesilia ambaye alifunga mafunzo hayo kwa niaba Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Balozi Omari Ramadhani Mapuri amewakumbusha washiriki hao juu ya kuzingatia sheria na kanuni za Uchaguzi Mkuu 2025.

"Nawakumbusha pia mkazingatie kiapo cha kutunza siri, kwani kutokufanya hivyo ni kinyume cha sheria kunakoweza kupeleka kuchukuliwa hatua" amesisitiza.

Kwa upande wake Kidawa Matara, ambaye ni Mshiriki wa mafunzo kutoka Halmashauri ya Mtwara, ameeleza kuwa mafunzo hayo yamesaidia kuwakumbusha mambo muhimu ambayo watapaswa kuyazingatia wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.

Mafunzo hayo ya siku tatu yalifunguliwa rasmi julai 15, 2025 yakiwajumuisha jumla ya washiriki 138 kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara huku mada 12 zikiwasilishwa na wataalam mbalimbali.

Mafunzo hayo yamewahusu Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi, ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi na Maafisa Ununuzi kutoka Mikoa ya Mtwara na Lindi.

✍️ Bryson Mshana

MJUMBE WA INEC MHE. BALOZI OMARI MAPURI AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA MTWARAMjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Ba...
15/07/2025

MJUMBE WA INEC MHE. BALOZI OMARI MAPURI AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA MTWARA

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Balozi Omari Mapuri akiongozana na watendaji wengine, wamefika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo Julai 15,2025.

Lengo la ziara hiyo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilikuwa kusalimia na kufanya mazungumzo mafupi, wakati wakielekea kwenye uzinduzi wa mafunzo ya siku tatu ya wasimamizi wa uchaguzi kutoka Mikoa ya Lindi na Mtwara, yaliyoanza kwenye Ukumbi wa Benki Kuu Mjini Mtwara tarehe 15 julai 2025.

Mafunzo hayo yanahusisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi, ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi na Maafisa Ununuzi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mhe.Balozi Mapuri amewakumbusha washiriki kuzingatia weledi wakati wote watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao.

Vilevile amesisitiza juu ya wasimamizi hao kuwashirikisha wadau wote uchaguzi, vikiwemo vyama vya siasa katika kila hatua inayowataka kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria.

Mafunzo hayo pia yanaendelea katika mikoa mbalimbali nchini, kwa lengo la kuhakikisha kuwa wasimamizi wa uchaguzi wanafikiwa na elimu ya kutosha kabla ya kuanza mchakato wa uchaguzi.

Awali mafunzo hayo yalitanguliwa na Watendaji hao wa Uchaguzi kula kiapo, kilichoongozwa na Mhe.Hakimu Allex Kalagaza Robert.

✍️ Bryson Mshana

INEC YAENDESHA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA UCHAGUZI KATIKA MIKOA YA  MTWARA  NA LINDITume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC),...
15/07/2025

INEC YAENDESHA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA UCHAGUZI KATIKA MIKOA YA MTWARA NA LINDI

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetoa mafunzo kwa Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi, ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi na Maafisa Ununuzi kutoka Mikoa ya Mtwara na Lindi.

Mafunzo hayo ambayo yameenda sambamba na washiriki kula kiapo cha uaminifu, yanafanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Benki Kuu Tanzania tawi la Mtwara, kuanzia leo Tarehe 15-17 Julai 2025.

Ufunguzi wa mafunzo hayo umefanywa na Mhe.Balozi Omari Ramadhani Mapuri ambaye ni Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, aliyesisitiza juu ya washiriki kuzingatia weledi wakati wote watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao.

"Napenda kuwakumbusha kuwa uteuzi wenu umezingatia uaminifu,uadilifu,uzalendo, kwa kuzingatia haya mmeteuliwa kwa mujibu wa sheria kusimia uendeshaji wa uchaguzi katika maeneo yenu ya uchaguzi "

"Dhamana mliyopewa ni kubwa,nyeti na muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu hivyo Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi inayo imani kuwa mtasimiamia vema zoezi hili hadi litakapokamilika"

Kuhusu ushiriki wa wadau, Balozi Omari Mapuri amesisitiza juu ya wasimamizi hao kuwashirikisha wadau wote uchaguzi, vikiwepo vyama vya siasa katika kila hatua inayowataka kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria.

Awali Mhe.Bozi Omari akiwa na watendaji wengine wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, walitembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, ambapo walikuna na mwenyeji wao Kanali Patrick Sawala.

Mafunzo hayo pia yanaendelea katika mikoa mbalimbali nchini, kwa lengo la kuhakikisha kuwa wasimamizi wa uchaguzi wanafikiwa na elimu ya kutosha kabla ya kuanza mchakato wa uchaguzi.

Awali mafunzo hayo yalitanguliwa na Watendaji hao wa Uchaguzi kula kiapo, kilichoongozwa na Mhe.Hakimu Allex Kalagaza Robert.

✍️ Bryson Mshana

FAIDA ZA TUNDA AINA YA BUNGO KWA AFYA YA BINADAMUMatunda haya ni adimu sana, hunda ni muda mrefu tangu  umeyala au hujaw...
13/07/2025

FAIDA ZA TUNDA AINA YA BUNGO KWA AFYA YA BINADAMU

Matunda haya ni adimu sana, hunda ni muda mrefu tangu umeyala au hujawahi kabisa kuyaonja!

Hata hivyo matunda haya bado yanapatikana, na yanaweza kuliwa k**a yalivyo au kutengenezwa kuwa juisi tamu na ya kipekee—moja ya juisi bora kabisa niliyowahi kuonja!

Faida za Bungo, kwanza ni chanzo kizuri cha Vitamini C – huimarisha kinga ya mwili, na vilevile hutoa nishati ya haraka kwa mwili lakini pia ni matunda ya kuburudisha, hasa wakati wa joto.

Tafuta matunda ya Bungo sokoni kwako – usikose ladha na faida zake za kiafya!



JE, UNAZIJUA FAIDA ZA UJI WA NJUGU MAWE KWA WATOTO?Kwa kzazi au mlezi, iama ulikuwa hufahamu Uji wa Njugu Mawe ni chaguo...
11/07/2025

JE, UNAZIJUA FAIDA ZA UJI WA NJUGU MAWE KWA WATOTO?

Kwa kzazi au mlezi, iama ulikuwa hufahamu Uji wa Njugu Mawe ni chaguo la busara na lishe bora kwa watoto na familia kwa ujumla.

Faida kuu za uji huubni hizi zifuatazo,

Una kiasi kikubwa cha Protini, kinachosaidia kujenga misuli imara katika mwili wa mtoto, unachangia ukuwaji wa mifupa yenye nguvu, muhimu kwa watoto na vilevile hutoa nishati ya kutosha kwa ukuaji na shughuli za kila siku.

Unaweza kununua uji wa njugu mawe uliochanganywa tayari au ukachagua kusindika nafaka nyumbani kwa njia ya asili.

Anza leo kuwapatia watoto wako mlo kamili – chagua uji wa Njugu Mawe, lishe sahihi kwa afya bora!



11/07/2025

WATANZANIA TULINDE MIUNDOMBINU YA UMEME, TULIPE BILI ZETU - DKT. BITEKO

‘’Nataka niseme mbele yenu ndugu zangu, Mhe. Rais Samia ndio Kinara wa kufanya haya yote yafanikiwe amefanya uwekezaji mkubwa kwenye Sekta ya Nishati na ndio maana kwenye bajeti iliyopita Wizara hii imepata Shilingi Trilioni 2.3 kikubwa anataka wananchi wapate umeme wa uhakika,’’ alisema Dkt Biteko.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ameyasema hayo Julai 10, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension na Kinyerezi II Jijini Dar es Salaam.

JE UNAZIJUA FAIDA ZINAZOPATIKANA KWENYE MBEGU ZA UFUTA?Mbegu za ufuta hazitumiki sana katika milo yetu ya kila siku, lak...
10/07/2025

JE UNAZIJUA FAIDA ZINAZOPATIKANA KWENYE MBEGU ZA UFUTA?

Mbegu za ufuta hazitumiki sana katika milo yetu ya kila siku, lakini k**a hutumii mbegu hizi kwenye mlo wako, tambua unakosa faida nyingi muhimu za kiafya.

Mbegu za ufuta ni chanzo kizuri cha mafuta yenye afya, kalsiamu na virutubisho vingine vinavyosaidia kuimarisha kinga ya mwili, kupunguza hatari ya magonjwa, na kuzuia kuzeeka kwa haraka.

Njia rahisi za kutumia mbegu za ufuta:

- Nyunyizia kidogo kwenye saladi au kachumbari
- Tumia kwenye vyakula vilivyookwa k**a mikate au keki
- Changanya kwenye uji, supu au wali
Hata kwa kiasi kidogo, faida zake kiafya ni kubwa. Pata mbegu za ufuta kwenye soko lako la karibu na uanze kuzipa nafasi kwenye mlo wako wa kila siku.


09/07/2025
HERI YA SIKUKUU YA SABASABA KWA WADAU WOTE WA SAFARI RADIO.89.3 MTWARA88.9 LINDI88.5 RUVUMA
07/07/2025

HERI YA SIKUKUU YA SABASABA KWA WADAU WOTE WA SAFARI RADIO.

89.3 MTWARA
88.9 LINDI
88.5 RUVUMA

Jumla ya vikundi 50 vya wajasiliamali wanaojihusisha na ubanguaji wa korosho na wakulima wa korosho wamepatiwa mafunzo y...
05/07/2025

Jumla ya vikundi 50 vya wajasiliamali wanaojihusisha na ubanguaji wa korosho na wakulima wa korosho wamepatiwa mafunzo ya kuongeza thamani zao la korosho na kiwanda cha prosperity Agro industry kwa kushirikiana na NMB foundation na Rabo foundation ya nchini uholanzi.

Mafunzo hayo yaliyotolewa kwa wiki moja kuanzia june 30 hadi july 04 / 2025 yamefanyika kwenye kiwanda cha prosperity agro kilichopo Newala mjini ambapo washiriki 200 wamehitimu kwenye mafunzo hayo ya awamu ya kwanza kati yao vikundi 30 ni washiriki kutoka Newala mjini na vikundi 20 Kutoka wilayani Ruangwa kwa lengo la kuwaongezea ujuzi wakulima na wajasiliamali ili kuwaongezea kipato kupitia zao la korosho.

Akizungumza katika kufunga mafunzo hayo mkurugenzi wa kampuni ya prosperity agro bwana Haroun Maarifa amesema mafunzo hayo ni mkakati wa kiwanda hicho na wadau wake kuhakikisha kazi wanayoifanya wakulima na wabanguaji inawanufaisha

Kwaupande wake mkuu wa wilaya ya Newala alhaji mwangi rajabu kundya amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa serikali kwani ni dhamira ya rais kuhakikisha kila mkulima anapata stahiki sahihi kwa kile anachozalisha

Nao washiriki wa mafunzo hayo wamemshukuru mkurugenzi wa kiwanda hicho bwana Haroun Maarifa na wadau wake kwa kuandaa mafunzo hayo kwani yamewaongezea uelewa katika mchakato wote wa kubangua korosho na kwa kuwahakikishia kupata masoko kupitia kiwanda hicho.

04/07/2025

SADC YAIPONGEZA TANZANIA KUFANIKISHA MKUTANO WA M300

Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Umeme wa Zimbabwe, Dkt. July Moyo, ameipongeza Tanzania kwa kuandaa na kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Nishati Afrika wa Misheni 300 (M300) ambao ulifanyika kwa mafanikio.

Pia, Dkt. Moyo amezishukuru Nchi wanachama zilizohudhuria katika mkutano huo muhimu uliofanyika jijini Dar es Salaam.





Address

Arusha
<<NOT-APPLICABLE>>

Telephone

+255652462770

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Safari Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share