Msumba News Blog

Msumba News Blog Blog hii inajihusisha na machapisho ya kuhabarisha,kuelimisha na kuburudisha.

05/04/2025
PSSSF YATOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KWA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA TEFMFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma ...
05/04/2025

PSSSF YATOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII KWA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA TEF

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma PSSSF umetoa elimu ya Hifadhi ya Jamii na utekelezaji wa shughuli za Mfuko tangu ulipoanzishwa mwaka 2018, mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) unaofanyika kwenye Ukumbi wa Parokia ya Familia Takatifu Bombambili Kanisa Katoliki jimbo Kuu Songea, mkoani Ruvuma Aprili 4, 2025.

Akitoa mada mbele ya wajumbe hao, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi, Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama PSSSF, Bw. Yesaya Mwakifulefule, alisema, Mfuko umekuwa ukitekeleza majukumu yake ipasavyo ya Kusajili Wanachama, Kukusanya Michango, Kulipa Mafao na Kuwekeza.

“ Thamani ya Mfuko wa PSSSF imefikia trilioni 10, haya ni mafanikio makubwa ya Mfuko tangu ulipoanzishwa mwaka 2018.” Amesisitiza Bw. Mwakifulefule.

Aidha, Mfuko unajivunia kufanya mapinduzi makubwa katika utioaji wa huduma zake, ambapo kwa sasa umeqachana na matumizi ya karatasi katika kuwahudumia wanachama na badala yake huduma zote zinatolewa kupitia mtandao maarufu PSSSF Kidijitali, alisema.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bw. Deodatus Balile, amepongeza taasisi zilizosaidia kuwezesha kufanyika kwa mkutano huo ambapo PSSSF imepewa tuzo ya shukrani kwa kuwa miongoni mwa taasisi hizo.

MATIBABU YA MACHO KUFANYIKA BURE JIJINI TANGA.TAASISI ya Bilal Muslim Mission of Tanzania  Leo April 5,2025  imeanza zoe...
05/04/2025

MATIBABU YA MACHO KUFANYIKA BURE JIJINI TANGA.

TAASISI ya Bilal Muslim Mission of Tanzania Leo April 5,2025 imeanza zoezi la matibabu ya macho Bure kwa wananchi wa halmashauri ya Jiji la Tanga ikiwa ni katika jitihada za kukabiliana na matatizo mbalimbali ya macho ikiwemo mtoto wa jicho ambapo tafiti zilizofanyika zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 50 ya wananchi Mkoani Tanga wamemeathirika na tatizo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu amesema kuwa taasisi hiyo ambayo inafanya kambi hiyo kwa mara ya pili jijini hapa kutoka ile ya mwaka 2019 ambapo zaidi ya wananchi 3,000 waligundulika na tatizo la mtoto wa jicho na walipatiwa matababu, dawa pamoja na Miwani bure.

"Wadau wetu kutoka Bilal Muslim Mission of Tanzania wanakuja tena Tanga kwaajili ya kuiendesha kambi hii kubwa ya macho bure tulifanya mwaka 2019 niliwaomba na nashukuru Wamekubali ombi letu la kuja kutoa huduma hii kwa siku tatu kuanzia jumamosi hadi jumatatu katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara"

"Huduma zitakazotolewa katika kambi hii kubwa ni kupima na kupewa Miwani bure, watu wana kumbukumbu 2019 tulitoa Miwani zaidi ya elfu tatu kwa wakazi wa Jiji la Tanga ambao walipimwa na kukutwa na changamoto za macho"

"Lakini kambi hii itatoa dawa bure kwa watu ambao watapimwa na kukutwa na changamoto za macho na kutoa ushauri wa afya ya macho bure kutoka kwa madaktari bingwa wa macho na pia itatoa huduma za kusafisha mtoto wa jicho nure kabisa" alisema Ummy

Aidha mbunge huyo ameipongeza na kumshukuru taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania Kwa utayari wao wa kuendeleza ushirikiano ili kuwasaidia wananchi Kwa kushirikiana na ofisi ya mganga Mkuu wa wilaya hiyo kupitia kambi hiyo ambayo imedhaminiwa na kampuni ya simu za Mkononi ya Yas.

"Napenda sana kuwaalika wakazi wote wa wilaya ya Tanga kujitokeza kwa wingi kuanzia saa mbili asubuhi mpaka sasa tisa na nusu, naomba watu wafike mapema wapewe huduma " alisisitiza Mbunge huyo.

"Mimi k**a mbunge wa Jimbo la Tanga niwashukuru sana Bilal Muslim Mission of Tanzania Kwa kukubali ombi letu kuja kufanya kambi hii bure lakini jambo hili tunashiriana na ofisi ya mganga ya wilaya ya Tanga chini ya

DKT. EMMANUEL NCHIMBI AZUNGUMZIA SEKTA YA KILIMO NAKUTOA SULUHU YA UJENZI WA SOKO LA KISASA IKIWEMO STEND YA KISASA WILA...
04/04/2025

DKT. EMMANUEL NCHIMBI AZUNGUMZIA SEKTA YA KILIMO NAKUTOA SULUHU YA UJENZI WA SOKO LA KISASA IKIWEMO STEND YA KISASA WILAYANI NAMTUMBO

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM na Mgombea Mwenza wa Urais 2025 Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi,amewashukuru wananchi wa Namtumbo kwa mapokezi ya Kishindo,akipeleka pia salamu za upendo za Mwenyekiti wa Chama Taifa na Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani,ametumia nafasi hiyo pia kueleza namna ambavyo anafurahishwa Mno na uhai wa Chama cha Mapinduzi,ambacho kinaendelea kujibu changamoto za Wananchi.

Dkt. Nchimbi ameyasema hayo leo April 03,2025 Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma Wakati akizungumza na Wananchi,amewapongeza Wananchi wa Namtumbo kwa kushika nafasi ya pili Kimkoa katika Mkoa wa Ruvuma kwa uzalishaji wa Mazao ya aina mbalimbali,wakishika pia nafasi ya kwanza kwa uzalishaji wa zao la Tumbaku”Mnatoa heshima kubwa kwa Mkoa wenu kwa uchapakazi wenu kwa uchapakazi wenu,endeleeni kuchapakazi tunajivunia,tukisema tunatoka Mkoa wa Ruvuma halafu tunaanza kutaja Wilaya zetu kwa Mbwembwe kwa sababu tunajua Mnalinda heshima ya Nchi yetu,tuendelee kuchapakazi tukijua kazi ni kipimo cha utu”

Katibu Mkuu wa CCM amesema Miaka 10 Mfululizo Tanzania inajitosheleza kwa Chakula,akiutaja Mkoa wa Ruvuma kuwa ni miongoni mwa Mikoa Mitano (Big 5) hapa Nchini ambayo inazalisha chakula kwa Wingi,hivyo amewakumbusha Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) na Wizara ya Kilimo Nchini Kuhakikisha Wakulima wanapata Mbegu kwa urahisi kwa kuzisambaza kwa wakala walio karibu yao.amewataka ASA Kuongeza uzalishaji wa Mbegu hizo.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Namtumbo Mhe. Vitta Kawawa ametumia nafasi hiyo Kuishukuru Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kwa kujibu Changamoto za Maji Namtumbo ambapo ametoa zaidi ya Bilioni 7 na Utekelezaji wa Mradi huo utaanza muda mfupi ujao,ameshukuru kwa miradi mingine iliyotekelezwa Jimboni kwake ikiwemo miradi ya Shule za Sekondari zimejengwa na Madarasa 207,zaidi ya Bilioni 6 zikitumika kwenye Sekta ya afya,akiutaja pia upungufu wa Watumishi nakuwepo kwa baadhi ya changamoto za Barabara ya Mtwara pachani kwenda Lusewa Mpaka Tunduru akiomba itengene

Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng. Yahya Samamba akiwa na Kamishna wa Madini Dkt. AbdulRahman Mwanga pamoja na watendaji ...
03/04/2025

Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng. Yahya Samamba akiwa na Kamishna wa Madini Dkt. AbdulRahman Mwanga pamoja na watendaji wengine kutoka Tume ya Madini akiwemo Katibu Mtendaji Eng. Ramadhan Lwamo tayari wamewasili katika eneo la Porcupine North - Makongorosi Wilayani Chunya kushuhudia uzinduzi wa Mgodi Mpya wa Kampuni ya Shanta Gold Mining Co.Ltd.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa  Mhe. Mohamed Mchengerwa akitoa maelezo wakati wa kik...
02/04/2025

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa akitoa maelezo wakati wa kikao cha majumuisho ya Uchambuzi wa Mpango na Bajeti ya Mafungu 28 yanayosimamiwa na Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa mwaka 2025\/26 kwenye k**ati ya kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) leo tarehe 02.04.2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tan...
02/04/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zitaendelea kusimamia kwa dhati na kwa haki misingi ya demokrasia na kuhakikisha wananchi wanatumia haki yao ya kikatiba ya kushiriki uchaguzi kwa uhuru, kwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kuchagua viongozi wenye sifa wanaowataka katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizindua Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025 katika hafla iliyofanyika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani. Ametoa wito kwa wananchi wote hususan vijana kuwa waangalifu na watu wasioitakia mema nchi kwa kuepuka kutumiwa vibaya kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani.

Makamu wa Rais amesema Wadau wote wa uchaguzi, hususan vyama vya siasa wanahimizwa na kukumbushwa kuwa wana wajibu mkubwa katika kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika katika hali ya amani na utulivu, kwa kuendesha kampeni zenye staha na kuzingatia Sheria na miongozo mbalimbali ya uchaguzi. Ameongeza kwamba Uchaguzi Mkuu unafanyika kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 42(2) na 65, Sheria ya Uchaguzi Na. 1 ya Mwaka 2024 pamoja na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar Na. 4 ya mwaka 2018.

Halikadhali Makamu wa Rais ameagiza Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoa ushirikiano wa hali ya juu kwa wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, ili waweze kutekeleza jukumu la kizalendo walilokabidhiwa la kuhakikisha kuwa wanawafikia wananchi na kuwapa taarifa sahihi kuhusu sera, mipango, miradi na mikakati ya Serikali katika kuwaletea Maendeleo.

Vilevile Makamu wa Rais amesema Mbio za Mwenge pamoja na mambo mengine zitaangazia masuala ya lishe bora, mapambano dhidi ya rushwa, mapambano dhini ya VVU na UKIMWI, mapambano dhidi ya dawa za kulevya pamoja na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria.

Wananchi wametakiwa kukopa mikopo inayotolewa na Serikali na Taasisi rasmi ili kujiepusha na udhalilishaji unaoweza kuto...
02/04/2025

Wananchi wametakiwa kukopa mikopo inayotolewa na Serikali na Taasisi rasmi ili kujiepusha na udhalilishaji unaoweza kutokea kutokana na kukopa mikopo yenye  masharti magumu kutoka kwa Taasisi zisizo rasmi na kwa  Wakopeshaji Binafsi.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Mkoa wa Mwanza, Bw. Binuru Shekidele, alipokutana na Timu ya Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha na Taasisi zake, ambayo ipo mkoani Mwanza kutoa elimu ya fedha kwa wananchi wa  makundi mbalimbali.

Aliongeza kuwa mikopo rasmi inayotolewa na Serikali na Taasisi zilizoidhinishwa hufuata taratibu za kisheria ambazo zinalinda haki za wakopaji na kuhakikisha wanapata huduma za kifedha kwa masharti nafuu.

“Mikopo rasmi kutoka serikalini ina masharti nafuu, riba ya chini, na inalenga kuwawezesha wananchi kuboresha maisha yao bila kuingia kwenye matatizo ya kifedha”, alisema Bw. Shekidele.

Alifafanua kuwa ni muhimu kwa wananchi kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu masharti ya mikopo wanayochukua ili kuhakikisha wanakopa kwa uangalifu na kulipa kwa wakati bila kuingia katika changamoto zisizo za lazima.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii na Mratibu wa Huduma Ndogo za Fedha, Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Bw. Jacob Nkungu, aliwashauri watoa huduma za fedha kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu zilizotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT)  ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi bila kuwakandamiza.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya elimu ya fedha mkazi wa Sengerema, Bw. Boniface Maxmilian, alishauri elimu ya fedha ifike kwa wananchi wote katika ngazi zote ili waweze kuwa na uelewa mpana wa masuala ya fedha ikiwemo kufahamu mikopo salama, kuwa na uelewa wa masuala ya bajeti na kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha.

Naye Afisa Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Santley Kibakaya, alisema kuwa baada ya kutoa mafunzo ya elimu ya fedha kwa wananchi wa makundi mbalimbali wananchi watabadilisha utaratibu wa maisha, ikiwemo kuacha kukopa kwenye Taasisi ambazo sio rasmi, kuwashirikisha wenza wao kabla ya kuchukua mikopo na kutotumia mali za fam

UFAFANUZI KUHUSU MZAZI ANAYEDAI KUBADILISHIWA MTOTO
02/04/2025

UFAFANUZI KUHUSU MZAZI ANAYEDAI KUBADILISHIWA MTOTO

Wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2025
02/04/2025

Wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2025

Waziri wa Madini na Mbunge wa Dodoma Mjini Anthony  Mavunde ameshiriki uzinduzi wa ujenzi wa visima vya maji nchini ili ...
29/03/2025

Waziri wa Madini na Mbunge wa Dodoma Mjini Anthony  Mavunde ameshiriki uzinduzi wa ujenzi wa visima vya maji nchini ili kusaidia kuwezesha kilimo cha umwagiliaji .

Uzinduzi huo ulioongozwa na mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi .Rosemary Senyamule umefanyika hii leo katika kata ya matumbulu Mkoani hapa ikiwa ni mojawapo ya maeneo yaliyopo ndani ya mradi ambapo visima 68,000 vinatarajiwa kuchimbwa nchi nzima.

Aidha Mavunde ametoa pongezi kwa Waziri wa kilimo na Tume ya umwagiliaji kwa  jitihada walizozionesha katika kuwasaidia wakulima wa zabibu mkoani hapa kuondokana na kazia ya ukosefu wa maji katika mashamba yao .

"Yote haya yanafanyika hapa lengo likiwa ni  kuhakikisha mkulima wa zabibu anapata soko la uhakika ,natamani kumuona mkulima wa zabibu kawa na maringo na zabibu yake "alisema Waziri Mavunde .

SHEIKH WA MKOA WA DAR ES SALAAM: PSSSF MMEONYESHA UPENDO  KUFUTURISHA WATOTO WENYE UHITAJI.MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa...
28/03/2025

SHEIKH WA MKOA WA DAR ES SALAAM: PSSSF MMEONYESHA UPENDO KUFUTURISHA WATOTO WENYE UHITAJI.

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umewafuturisha watoto wenye uhitaji wa kituo cha Chakuwama kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam na kuwapatia zawadi mbalimbali.

MWEZI mtukufu wa Ramadhan, unafundisha kufanya mambo mengi mema na kufuturisha wenye uhitaji, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Abdul-Razaq Badru alisema, katika iftar hiyo iliyofanyika Alhamisi ambayo iliwahusisha pia Mwenyekiti wa Bodi ya PSSSF, Bi. Joyce Mapunjo, baadhi ya wajumbe wa bodi, Menejiment na watumishi wa Mfuko wa Mkoa wa Dar es Salaam.

""Tunamuomba Mwenyezi Mungu apokee ibada hii; Kwa niaba ya wanachama wa PSSSF ambao tunatunza amana zao na kuwekeza ili wanapostaafu waweze kulipwa vizuri tutaendelea kutoa sadaka na kushirikiana na jamii inayotuzunguka k**a sehemu ya kutimiza wajibu wetu," alisema Badru.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar ameipongeza kwa sadaka ya kufuturu pamoja na watoto wa Kituo cha CHAKUWAMA ikiwa ni pamoja na kuwapatia zawadi mbalimbali.

"Kitendo hiki cha kukusanya watoto hawa na kutoa zawadi kwao, ni utekelezaji wa maelekezo ya Mwenyezi Mungu ambaye amesisitiza upendo kwa watu wengine.

MOI YAANDIKA HISTORIA KWA KUANZA KUFANYA UPASUAJI WA UBONGO KWA KUTUMIA AKILI UNDE.Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo M...
28/03/2025

MOI YAANDIKA HISTORIA KWA KUANZA KUFANYA UPASUAJI WA UBONGO KWA KUTUMIA AKILI UNDE.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeanza rasmi upasuaji wa ubongo kwa kutumia teknolojia ya akili unde 'Brain Lab- Neuro Navigation System' ambayo husaidia wataalam kufanya upasuaji wa uvimbe kwenye ubongo  kwa ufanisi mkubwa (high efficiency & accuracy) kupitia tundu dogo hivyo kupunguza muda wa upasuaji na wa mgonjwa kukaa wodini baada ya upasuaji huo.
Hayo yamebainishwa leo Alhamisi Machi 27, 2025 na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Taasisi hiyo.
Dkt. Mpoki amesema Taasisi ya MOI ndiyo hospitali ya kwanza Tanzania kufanya upasuaji wa ubongo kwa kutumia akili unde.
"Kwa mara ya kwanza katika nchi yetu (Tanzania) leo tumefanikiwa kufanya upasuaji wa ubongo kwa kutumia kifaa maalum ( Brain Lab- Neuronavigation System) ambacho kinamuongoza daktari kuanzia kupanga upasuaji kabla ya kufungua fuvu, wakati wa upasuaji wenyewe kwa tundu dogo kwenye fuvu na kuwezasha kumuongoza mpasuaji iwapo uvimbe umeisha wote kabisa. Teknolojia hii ambayo haitumii mionzi ya  X- Ray" ni salama kabisa kwa wataalam na mgonjwa anayepata matibabu, amesema Dkt. Mpoki
Aidha, Dkt. Mpoki ameongeza kuwa upasuaji huo umeongozwa na daktari bingwa mbobezi  mzawa kwa kushirikiana na madaktari kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornell New York cha nchini Marekani na kutoa wito kwa Watanzania wenye matatizo ya uvimbe au watakaogundulika kuwa na uvimbe kwenye ubongo kufika katika Taasisi hiyo kupatiwa matibabu.
Naye, Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu, Dkt. Laurent Lemeri Mchome amesema kwamba ushirikiano kati ya Chuo kikuu cha Weill Cornell New York Marekani na MOI ulianza mwaka 2008 ambapo kwa mwaka huo Taasisi hiyo ilikuwa na madaktari bingwa wabobezi watatu tu, lakini hadi mwaka huu (2025) kuna madaktari bingwa 15 na wengine wanaendelea kupatiwa mafunzo na amewatoa wasiwasi Watanzania kuwa upasuaji huo kwa kutumia akili unde ni bora na salama kabisa.

REA YAPONGEZWA KWA UHAMASISHAJI WA MATUMIZI YA NISHATI BORADC Chikoka asisitiza utunzaji wa miundombinu ya umemeMkuu wa ...
27/03/2025

REA YAPONGEZWA KWA UHAMASISHAJI WA MATUMIZI YA NISHATI BORA

DC Chikoka asisitiza utunzaji wa miundombinu ya umeme

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Mhe. Juma Chikoka amewapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kuendelea kuhamasisha matumizi bora ya nishati kwa Watanzania wote.

Mhe. Chikoka amebainisha hayo leo Machi 27, 2025 kwa Wataalam wa REA waliofika kujitambulisha ofisini kwake kueleza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya REA mkoani Mara.

Aidha, ameiomba REA kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu gharama za kuunganisha umeme, utunzaji wa mazingira, tahadhari za umeme na elimu kuhusu utunzaji wa miundombinu ya umeme ili kupata umeme wa uhakika.

NAIBU WAZIRI MAHUNDI AWAASA WANANCHIWA IFUCHA KULINDA MIUNDOMBINU YA MAWASILIANO.Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano n...
27/03/2025

NAIBU WAZIRI MAHUNDI AWAASA WANANCHI
WA IFUCHA KULINDA MIUNDOMBINU YA MAWASILIANO.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amewataka
wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda miundombinu ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinadumu
na kuwa bora zaidi.

Naibu Waziri Mahundi alitoa kauli hiyo tarehe 26 Machi, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya mawasiliano katika Jimbo la Tabora Kaskazini katika Kata ya Ifucha na kuongeza kuwa miradi ya mawasiliano inajengwa kwa gharama kubwa, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kushiriki katika kuitunza na kuilinda miundombinu hiyo dhidi ya uharibifu au wizi.

Naibu Waziri Mahundi amezitaka kampuni za simu kuhakikisha wanalipa walinzi wa minara ya mawasiliano kwa wakati ili kuongeza ari ya wafanyakazi hao kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

"Rais Dkt. Samia anapenda amani, na anapoleta miradi ya maendeleo k**a hii, anapenda muitumie kwa amani," alisisitiza Naibu Waziri Mahundi.

Awali, akitoa taarifa kuhusu mnara huo, Kaimu Meneja wa Muko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Bw. Shirikisho
Mpunji alisema kuwa mara huo ni miongoni mwa minara 758 ya mawasiliano inayojengwa kwa ruzuku ya Serikali kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali ambapo Serikali imechangia shilingi milioni 109 kwa ajili ya ujenzi wa mnara huo unahudumia wakazi wa kijiji cha Kazima.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Yas Kanda ya Kati, Bw. Saidi Iddy, alisema mnara huo ulianza kufanya kazi tangu Septemba 2024 na kwa sasa unahudumia wakazi wapatao 5,200 wa Kata ya Ifucha.

SERIKALI YAJA NA MKAKATI WA KUWAENDELEZA WACHIMBAJI WADOGO KUFIKIA UWEKEZAJI MKUBWA WA MADINI.▪️ Waziri Mavunde aelekeza...
27/03/2025

SERIKALI YAJA NA MKAKATI WA KUWAENDELEZA WACHIMBAJI WADOGO KUFIKIA UWEKEZAJI MKUBWA WA MADINI.

▪️ Waziri Mavunde aelekeza kuwepo na mpango maalum wa kuwatambua wachimbaji wanaofanya vizuri

▪️ Mfuko wa Dhamana wa Wizara ya Fedha kutumika kuongeza mtaji kwa wachimbaji

▪️ STAMICO yapewa jukumu kuongeza vifaa zaidi vya Utafiti wa madini kwa ajili ya wachimbaji wadogo

▪️ Wachimbaji waandaa maandamano makubwa kumpongeza Rais Samia

Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameeleza ķuwa, Serikali kupitia Wizara ya Madini imekuja mkakati maalum wa kuwawezesha Wachimbaji Wadogo kupiga hatua zaidi na kufaulu na hatimaye kumiliki migodi mikubwa kupitia mpango maalum utakaorahisisha upatikanaji wa mitaji, teknolojia ya kisasa, na kuwajengea uwezo endelevu wa uchimbaji na kibiashara.

Amebainisha hayo leo Machi 27, 2025 Jijini Dodoma wakati akizungumza katika Mkutano maalum na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA) kwa lengo kujadili masuala mbalimbali yanayohusu Sekta ya Madini ili kuboresha uendelezaji na usimamizi wa shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa manufaa ya sekta na taifa kwa ujumla.

Waziri Mavunde, amesema kuwa mpango huo utasaidia Wachimbaji Wadogo kupiga hatua na kuwa Wachimbaji wa Kati, hatimaye kuwa wamiliki wa migodi mikubwa inayochangia kikamilifu katika Pato la Taifa na uchumi kwaujumla.

✅️ *Waziri Mavunde Aelekeza Kuwepo na Mpango Maalum wa Kuwatambua Wachimbaji Wanaofanya Vizuri*

Mhe. Mavunde amewaelekeza watendaji wa Wizara kupitia Tume ya Madini kuandaa mfumo wa kutambua Wachimbaji Wadogo wanaofanya vizuri katika shughuli za uchimbaji ili waingie kwenye mpango maalum wa kuwawezesha kwa awamu hatimaye kupiga hatua na kuona manufaa ya uchimbaji wao.

“Sote tunafahamu mchango wa Wachimbaji Wadogo katika maduhuli ya Serikali, hivyo tunataka kuona wachimbaji wadogo wanakuwa wachimbaji wa kati na hatimaye kuwa wakubwa. Tunatengeneza mfumo wa kuwatambua wale wenye bidii, weledi, katika sekta ili kuwawezesha hadi kufikia hatua ya kumiliki migodi mikubwa, tunataka miaka michache ijayo kuwepo na mabilionea Wakitanzania waliotokana na Sekta hii” amesema Waziri Mavunde.

GST YASAINI HATI YA MAKUBALIANO (MoU) NA TAASISI YA JIOSAYANSI NA RASILIMALI MADINI YA KOREA KUSINI KIGAM•Watanzania kuj...
27/03/2025

GST YASAINI HATI YA MAKUBALIANO (MoU) NA TAASISI YA JIOSAYANSI NA RASILIMALI MADINI YA KOREA KUSINI KIGAM

•Watanzania kujengewa uwezo kwenye kada ya Jiosayansi na Utafiti wa Madini

Wizara ya Madini kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) na Taasisi ya Jiosayansi na Rasilimali Madini ya Korea Kusini (KIGAM) zimetia saini Hati ya Makubaliano (MoU) ya kufanya tafiti za pamoja za Jiosayansi.

Hafla hiyo ya utiaji saini imefanyika Machi 26, 2025 Jijini Seoul, Korea Kusini wakati ya ziara ya Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa kushiriki Mkutano wa wadau wa madini mkakati ulioandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Korea Kusini kwa kushirikiana na Wizara ya Biashara, Viwanda na Nishati ya Korea Kusini na wadau wa Sekta Binafsi kutoka nchini Tanzania na Korea Kusini.

Hati hiyo pamoja na masula mengine itahusisha mashirikiano kwenye kufanya miradi ya pamoja ya utafiti wa jiolojia, jiokemia na utafiti wa kina wa jiofizikia ili kuibua maeneo mapya yenye madini muhimu na madini mkakati.

Maeneo mengine ya makubaliano hayo ni pamoja na kuendeleza miradi ya pamoja ya utafiti wa majanga ya asili, kujengeana uwezo zaidi wa kitaalam na mafunzo kwenye kada jiosayansi na utafiti wa madini, kufanya tafiti za uchenjuaji madini, kuandaa mifumo ya utunzaji wa taarifa za jiosayansi na kuimarisha maabara ya GST.

Kabla ya hafla ya utiaji saini, Ujumbe wa Tanzania ulipata fursa ya kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Taasisi ya KIGAM ikiwa ni pamoja na masuala ya maabara, utafiti wa njia mbalimbali za uchenjujai madini hususan madini mkakati, utafiti wa teknolojia za utengenezaji wa vifaa vya teknolojia ya kijani ikiwa ni pamoja na betri za magari ya umeme, utambuzi wa majanga ya asili ikiwa ni pamoja na mitetemo na milipuko na kutembelea Chuo cha Jiosayansi na Rasilimali Madini kinachomilikiwa na KIGAM.

Akielezea Ushrikiano huo ulioafikiwa, Dkt. Kiruswa aliishukuru Serikali ya Korea Kusini kupitia KIGAM kwa kukubali kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia GST kufanya tafiti za jiosayansi na kuwajengea uwezo watanzania na kuahidi kufuatilia utekelezaji wa Hati hiyo

MKUU WA MKOA WA NJOMBE: WAWEKEZAJI WA VIWANDA WANAJENGA UCHUMI IMARAMkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amesema ...
26/03/2025

MKUU WA MKOA WA NJOMBE: WAWEKEZAJI WA VIWANDA WANAJENGA UCHUMI IMARA

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amesema kuwa uwekezaji katika viwanda vya kuongeza thamani ya mazao, hususan parachichi, ni hatua muhimu katika kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla.

Akizungumza mbele ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, wakati wa ziara yake katika kiwanda cha kuchakata mafuta ya parachichi kinachomilikiwa na Muricado Fruit Supplies, Mhe. Mtaka alieleza kuwa uwekezaji wa aina hii unatoa fursa kwa wakulima kupata masoko ya uhakika, kuongeza ajira na kuinua pato la taifa.

"Wawekezaji hawa wameamua kuchukua hatua ya kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani ya mazao yetu. Hili ni jambo la kuigwa na linapaswa kuungwa mkono kwa kuwa linachangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii," alisema Mhe. Mtaka.

Aliongeza kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira bora kwa wawekezaji kwa kuboresha miundombinu, upatikanaji wa umeme na sera zinazowiana na maendeleo ya viwanda.

Aidha, aliwahimiza wakulima wa parachichi kuongeza uzalishaji wao kwa kufuata mbinu bora za kilimo, kwani mahitaji ya bidhaa zinazotokana na parachichi yanaongezeka katika soko la kimataifa.

Mhe. Mtaka alihitimisha kwa kusema kuwa Mkoa wa Njombe unaendelea kuwa kinara katika kilimo cha parachichi, na kwamba juhudi za wawekezaji katika sekta hiyo zinapaswa kuungwa mkono na wadau wote ili kufanikisha azma ya Tanzania ya kuwa na uchumi wa viwanda.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Msumba News Blog posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Msumba News Blog:

Share