15/08/2026
Washiriki mbalimbali wa mafunzo ya usimamizi wa ujenzi yaliyoandaliwa na Tanzania Roads Association (TARA) kwa kushirikiana na TANROADS na TARURA wamewashukuru waandaaji wa mafunzo hayo, wakisema yamekuwa chachu ya kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Baadhi ya washiriki waliozungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo kwa siku ya tatu , hususan mada kuhusu matumizi ya Akili Bandia (Artificial Intelligence - AI) iliyowasilishwa na mtaalamu kutoka Afrika Kusini, Mhandisi Peter, wamesema teknolojia hiyo itarahisisha utekelezaji wa kazi na kupunguza muda unaotumika kuandaa nyaraka na makabrasha ya miradi ya ujenzi.
Akizungumza baada ya kupokea mafunzo hayo, mshiriki kutoka Bodi ya Wasajili wa Wahandisi (ERB)Dododma,Mhandisi Lightness Mrema, amesema mafunzo hayo yataleta tija kubwa kwa wakandarasi, wasimamizi wa miradi na wadau wengine wa sekta ya ujenzi kwa kuboresha utunzaji wa kumbukumbu, kuongeza ufanisi na kurahisisha utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi.
Naye mshiriki kutoka Namibia, Mhandisi Jonas, amesema ameridhishwa na mafunzo hayo na kueleza kuwa yameongeza uelewa wake kuhusu matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa miradi ya ujenzi.
Aidha, Mhandisi Jonas amesema matumizi ya Akili Bandia (AI) yana uwezo wa kuleta matokeo chanya katika sekta ya barabara na ujenzi kwa kuongeza kasi, usahihi na ubora wa utekelezaji wa miradi.
Tanzania Roads Association(TARA) Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini - TARURA