Savvy Media Live

Savvy Media Live MAONI YAKO FB,INSTAGRAM@SAVVY MEDIA LIVE. SIKILIZA SAVVY FM 105.3
LISTEN ONLINE: SAVVY FM ARUSHA.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azzan Zungu (Mb), ametangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, ...
11/12/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azzan Zungu (Mb), ametangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea leo tarehe 11 Desemba 2025 Jijini Dodoma.

Katika taarifa hiyo, Spika Zungu amesema:
“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Peramiho. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.”

Aidha, Ofisi ya Bunge ikishirikiana na familia ya marehemu imesema inaendelea kuandaa mipango ya mazishi na taarifa zaidi zitatolewa mara zitakapokamilika.

“Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina,”

09/12/2025

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi kutoka Makao Makuu Dodoma kupitia kwa msemaji wa jeshi Hilo Kamanda Misime mchana huu imesema Hali ya nchi iko salama na shwari kabisa na vyombo vya ulinza na usalama vinaendelea kutekeleza jukumu lake la kulinda wananchi na. Mali zao waendelee kuwa watulivu na kusherehekea sikukuu ya Disemba 09, 2025 wakiwa majumbani mwao.

Kamanda Misime amesema wananchi wapuuzie picha mjongeo zinazoendelea kusambazwa mtandaoni na kwamba ni za leo Disemba 09, 2025 kwani picha hizo ni za Oktoba 29, 30 na 31, 2025 wanazisambaza kwa Lengo la kupotosha umma ili uamini kuwa maandamano yamefanyika jambo ambalo ni uzushi na uongo mkubwa.

tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Disemba 09, 2025, Tanzania ikiadhimisha miaka 64 ya...
09/12/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Disemba 09, 2025, Tanzania ikiadhimisha miaka 64 ya uhuru wa Tanzania bara, ametangaza kuwasamehe wafungwa 1,036, wafungwa 22 kati yao wakiachiliwa huru na wengine 1,014 wakipunguziwa adhabu zao.

Kulingana na taarifa iliyosainiwa na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. George Simbachawene, Ikulu imeeleza kuwa ni matarajio ya serikali kuwa wafungwa walioachiwa huru watarejea tena katika jamii kushirikiana na wananchi katika ujenzi wa Taifa na kujiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.

Miongoni mwa waliosamehewa ni wafungwa wagonjwa wenye magonjwa ya kudumu au sugu ambao wapo katika hatua za mwisho pamoja na wafungwa wazee wenye umri wa miaka 70 au zaidi- Vyote vikitakiwa kuthibitishwa na jopo la waganga wa Wilaya na Mikoa.

Aidha wengine walionufaika na msamaha huo ni wafungwa wa k**e walioingia na ujauzito gerezani au wenye watoto wanaonyonya au wasionyonya waliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na kuendelea pamoja na wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili wasio na uwezo wa kufanya kazi.

Aidha wamesamehewa pia wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kuwekwa kizuizini (under president's pleasure) ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka kumi au zaidi




08/12/2025

Ujumbe wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu Maadhimisho ya Sikukuu ya Uhuru.





Usikose kufuatilia kipindi cha Tunza Dunia kupitia Savvy FM 105.3 Arusha  kila siku ya Jumatano saa 3:30  asubuhi na mar...
05/12/2025

Usikose kufuatilia kipindi cha Tunza Dunia kupitia Savvy FM 105.3 Arusha kila siku ya Jumatano saa 3:30 asubuhi na marudio ijumaa 6:30 mchana ambapo mada kuu wiki hii Matumizi ya biogas vijijini jinsi inavyoboresha maisha ya familia.

Host :




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewanasihi Viongozi wa Dini na Wa...
05/12/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewanasihi Viongozi wa Dini na Waumini kuhimizana kulinda Amani ya Nchi na kuwa tayari kuiombea kwa dhamira ya kudumisha Utulivu.

Dkt. Mwinyi ametoa nasaha hizo leo, tarehe 05 Disemba 2025, wakati akijumuika na Waumini katika Sala ya Ijumaa na Dua Maalum ya Kumshukuru Mwenyezi Mungu pamoja na kuliombea Taifa, iliyofanyika katika Msikiti wa Gombani, Mkoa wa Kusini Pemba.

Katika hotuba yake, Dkt. Mwinyi amemshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuijalia Zanzibar kuendelea kuwa na hali ya Amani na Utulivu kabla, wakati na baada ya Uchaguzi. Amewahimiza Waumini kuendeleza maombi na dua zao kila wanapopata nafasi, akisisitiza kuwa kila Muumini ana daraja lake mbele ya Mwenyezi Mungu, hivyo ni wajibu kwa kila mmoja kumuomba Mola aiweke nchi mbali na majanga.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Afisi ya M***i, Sheikh Khalid Ali Mfaume, amewataka Waumini wa Kiislamu kuendelea kufuata miongozo ya Mtume Muhammad (SAW) kwa kumuomba Mwenyezi Mungu katika kila jambo linalowakabili katika maisha yao ya kila siku.

Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba.

hmwinyi


Jeshi la Polisi nchini Tanzania limepiga marufuku maandamano yanayohamasishwa katika mitandao ya kijamii kwa kuyaita maa...
05/12/2025

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limepiga marufuku maandamano yanayohamasishwa katika mitandao ya kijamii kwa kuyaita maandamano ya amani ya Disemba 09, 2025 kutokana na kutofuata taratibu kulingana na sheria ya Polisi pamoja na kujaa viashiria vingi vya uhalifu na uvunjifu wa sheria na taratibu.

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Disemba 05, 2025 kwa Vyombo vya habari na msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime, imesema hatua hiyo imefikiwa pia kutokana na mbinu za kihalifu ambazo zimebainika wakihamasishana kuzitumia kuanzia tarehe 09 Disemba, maandamano hayo yamekosa aifa za kisheria kuyaruhusu kuweza kufanyika.

"Mtu yeyote anayepanga kufanya maandamano sheria inamtaka kuwasilisha kwa maandishi notisi kuhusu kufanyika kwa maandamano hayo kwa Afisa Polisi msimamizi wa eneo husika akiainisha sehemu yatakayofanyika maandamano hayo, muda, madhumuni na maelezo mengine k**a Waziri atakavyotangaza kwa notisi mara kwa mara kwenye gazeti la serikali." Imesema taarifa ya Polisi.

Polisi pia imesema maandamano hayo yanakosa sifa kutokana na wanaohamasisha maandamano kuwa na silaha kwani wamekuwa wakiwataka waandamanaji ikiwa hawana mafunzo ya kutumia silaha asishike silaha siku hiyo bali awaachie wengine waliopata mafunzo ya kutumia silaha hizo.

Aidha waandamanaji pia wamekuwa wakihamasishana kupitia mitandao ya kijamii kuhakikisha kuwa bandari ya Dar Es Salaam haifanyi kazi, kufunga barabara zote za kuingia na kutoka nje ya nchi pamoja na kwenda kwenye Hospitali za umma na za binafsi kuzuia huduma za matibabu, suala ambalo ni kinyume na sheria za nchi.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa watanzania na wasio watanzania ambao wapo ndani ya Tanzania wayakatae yanayohamasishwa na kutoshiriki katika maandamano hayo, wito ukitolewa pia kutoa taarifa kupitia namba 111, 112, 0699 998899 na 0787 668306 pale watakapoona tukio lenye viashiria vya uhalifu sehemu walipo.
tanzania

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewataka Vijana na Wanaharakati kutafuta njia sahihi ya kudai haki...
04/12/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewataka Vijana na Wanaharakati kutafuta njia sahihi ya kudai haki ikiwemo mazungumzo mezani akiwaasa kuwa vita na vurugu avijawahi kusaidia bali upelekea kupotea kwa amani huku akitolea mfano wa nchi ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo takribani ni zaidi ya miaka thelathini wanaitafuta amani ambayo imepotea.

Ametoa kauli hiyo wakati wa Mkutano wa Pili unaohusisha Pande Tatu ikiwemo Serikali ya Tanzania, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani UNHCR ambapo pia walitumia mkutano huo kusaini nyaraka zinazoelezea Mpango wa Urejeshwaji wa Wakimbizi 86256 waliopo hapa nchini ambapo pia Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,Shabani Bihango na Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani nchini Tanzania,Barbara Dotse waliishukuru Tanzania kwa kuhifadhi wakimbizi hao kwa muda unaozidi miaka thelathini.



Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Gabriel Makalla mapema leo Disemba 04, 2025  ameupokea na kuzungumza na Ujumbe wa ...
04/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Gabriel Makalla mapema leo Disemba 04, 2025 ameupokea na kuzungumza na Ujumbe wa Umoja wa Mabunge duniani (IPU), ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano mkubwa wa Mabunge unaotarajiwa kufanyika Mkoani Arusha na kuhusisha Maspika, Wabunge na Viongozi zaidi ya 1500 kutoka kote duniani.

Ujumbe wa IPU umeongozwa na Balozi Ande Filip, akiongozana na Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa Geneva,Uswisi Dkt. Hoyce Temu ambapo katika maelezo yake Balozi Ande amesema katika Mkutano huo, Mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wa Tanzania.

"Tanzania ni Mwenyeji na sababu kubwa ni ushiriki na historia yake katika IPU na kikubwa zaidi ni namna wao wanavyoiona Tanzania na sisi tumewahakikishia tupo tayari kuwapa ushirikiano kufanikisha mkutano huo mkubwa wa Kihistoria." Amesema Mhe. Makalla.

Mhe. Makalla amesema Mkutano huo ni fursa kwa Wananchi wa Arusha na Tanzania kwa ujumla na ukija wakati mzuri katika kudhihirisha amani, usalama na utulivu uliopo nchini na kuaminika kwa Tanzania Kimataifa, akiwataka wananchi kujiandaa kutumia fursa za ujio wa mkutano huo kiuchumi.

Kwa Upande wake Balozi Ande kwaniaba ya Maafisa wengine wa IPU, amesema Mkutano huo wa Kimataifa utafanyika kwa siku sita Jijini Arusha na kulingana na ratiba, washiriki wake kutoka kote duniani watakuwa na zaidi ya siku sita Mkoani Arusha ili kuwapa fursa ya kutembelea maeneo ya kihistoria na Vivutio vya Utalii vilivyopo Arusha na maeneo mengine ya jirani.





Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azzan Zungu, amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya ...
04/12/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azzan Zungu, amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya Mabalozi wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya wakiongozwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Mhe. Christine Grau walipomtembelea leo tarehe 4 Desemba, 2025 katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, walizungumza kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya, ikiwa ni pamoja na kuimarisha diplomasia ya kibunge (Parliamentary Diplomacy).

Kikao hicho kimehudhuria na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania ambao ni Balozi wa Finland, Balozi wa Hispania, Balozi wa Italia, Balozi wa Ubelgiji na Balozi wa Ujerumani.

tanzania



  FLEVA SAVVY FM ARUSHA  Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na Us...
04/12/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

Usikose pia

Wachimbaji wako ni

Baruti na

Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amemuagiza mkandarasi wa Kampuni ya GESI Espanola, kuongeza kasi y...
03/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amemuagiza mkandarasi wa Kampuni ya GESI Espanola, kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wa usimikaji wa taa za kuongezea ndege kwenye Kiwanja cha Ndege Arusha.

CPA Makalla ametoa agizo hilo, leo Desemba 03, 2025 alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 11, akisisitiza kuwa Serikali ya awamu ya sita imeidhinisha kiasi hicho cha fedha, lengo likiwa ni kuwezesha ndege kutua kwa saa 24 kwa siku, k**a mkakati wa kukuza utalii na kuwa na mazingira rafiki ya usafiri wa ndege.

"Ninawaelekeza Meneja na Mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi, huu ndio muda wa kuleta vifaa vyote ambavyo havijafika site, ikiwemo taa na genereta. Meneja endelea kumsimamia mkandarasi alete vifaa vyote ambavyo anasema ameshaviagiza nje ya nchi, sitapenda kusikia visingizio, nitakuja hapa mara kwa mara." Amesema CPA Makalla.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa maboresho hayo ya Kiwanja cha ndege licha ya kuongeza idadi ya miruko ya ndege kwa siku, unakwenda kutimiza ahadi ya Rais Samia aliyoahidi kutokana kukua kwa sekta ya utalii, inayokwenda sambamba na ongezeko la idadi ya watalii wanaofika nchini hususani katika mkoa wa Arusha.



✈️

Address

P. O. BOX 14070
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Savvy Media Live posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share