Savvy Media Live

Savvy Media Live MAONI YAKO FB,INSTAGRAM@SAVVY MEDIA LIVE. SIKILIZA SAVVY FM 105.3
LISTEN ONLINE: SAVVY FM ARUSHA.

Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kaya zisizo na uwezo kwa kutoa Shilingi bilion...
11/05/2026

Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kaya zisizo na uwezo kwa kutoa Shilingi bilioni 48.8 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi wa makundi maalum kupata huduma za afya kwa uhakika.

Kupitia utekelezaji huo, jumla ya kaya 172,297 tayari zimefikiwa na kuingizwa kwenye mpango huo, huku wanufaika 463,228 wakianza kupata huduma mbalimbali za matibabu katika vituo vilivyosajiliwa nchini.

Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya Fungu 52 kwa mwaka 2026/27 Waziri wa Afya Mhe. Omary Mchengerwa amesema kuwa, utekelezaji huu unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kujali hali yake ya kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya safari ya kuelekea huduma jumuishi za afya kwa wananchi wote.

Katika kuimarisha sekta ya afya sambamba na utekelezaji wa mpango huo, mabaraza na bodi za kitaaluma yameendelea kusimamia ubora wa huduma kwa kusajili wataalam wa afya 14,310, hatua inayoongeza nguvu kazi muhimu kwa utoaji wa huduma nchini.

Amesema kuwa kuhusu upatikanaji wa huduma za matibabu, jumla ya maduka ya dawa 330 yamesajiliwa pamoja na watarajali 3,004, huku vituo vya kutolea huduma za afya 3,643 vikisajiliwa ili kuongeza upatikanaji wa huduma karibu na wananchi.

Katika kuhakikisha taaluma na maadili yanaendelea kuzingatiwa hususan wakati huu wa kuhudumia wananchi wengi zaidi kupitia mfumo wa Bima ya Afya, vituo binafsi vya afya 654 vimekaguliwa ili kuhakikisha vinakidhi viwango na kutoa huduma salama kwa wananchi.

Mafanikio hayo yanaakisi hatua kubwa ya Serikali katika kujenga mfumo imara wa afya unaojali usawa, ubora na upatikanaji wa huduma kwa wote, huku Bima ya Afya kwa Wote ikiendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.





11/05/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 11, 2026 amekutana na Rais wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Alvaro Lario, jijini Nairobi, Kenya, ambapo wamejadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano katika sekta ya kilimo na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Mwigulu amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na IFAD katika maeneo mbalimbali ikiwemo kilimo himilivu cha tabianchi, maendeleo ya kilimo biashara, mapinduzi ya kidijitali katika sekta ya kilimo pamoja na uwezeshaji wa vijana na wanawake kiuchumi.



Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Moh...
11/05/2026

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amefanya uteuzi wa Wenyeviti, Wajumbe na Makatibu wa Kamati za Usalama Barabarani katika mikoa yote 31 ya Kipolisi nchini.​

Uteuzi huo umefanyika leo, jijini Dar es Salaam ukiwa na lengo la kuimarisha mfumo wa usimamizi wa usalama barabarani na kuhakikisha kuwa mikakati ya kuzuia ajali inatekelezwa kwa ufanisi​.

Akizungumza mara baada ya kutia saini orodha ya Viongozi wa Kamati hizo katika kikao kazi na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza, SACP William Mkonda amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara unaimarika na kupunguza ajali zinazoweza kuepukika.

Uteuzi huu umezingatia kikamilifu Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 (R.E 2023), Sehemu ya VII, kuanzia kifungu cha 110 hadi 113, ambavyo ndivyo vinavyotoa mamlaka ya kuundwa kwa Baraza la hilo.

Aidha, Mhe. Ayoub ametumia mamlaka aliyopewa chini ya Kanuni ya 15 ya Kanuni za Baraza (TS Namba 392/1986), inayompa Mwenyekiti uwezo wa kutoa maelekezo ya utekelezaji wa majukumu ya Baraza hilo kisheria.

Kadhalika kikao hicho kilikuwa ni sehemu ya Maandalizi ya kikao kijacho cha Baraza la Taifa la Usalama barabarani. Uteuzi huu wa viongozi wa mikoa unakuja kufuatia hatua ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, kumteua Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani.
tanzania

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa , ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuidhinisha kiasi cha Shilin...
11/05/2026

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa , ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuidhinisha kiasi cha Shilingi trilioni 1.8 kwa ajili ya Matumizi ya Wizara hiyo katika mwaka wa fedha 2026/27 Fungu 52.

Waziri Mchengerwa ameyasema hayo leo Mei 11, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi Trilioni 1.148 ambazo ni sawa na asilimia 64 ya bajeti iliyotengwa zinaombwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, amesema kuwa kati fedha hizo, fedha za ndani ya nchi ni shililingi Bilioni 789.45 na kiasi cha shilingi Bilioni 358.56 zinatoka kwa washirika wa maendeleo.

Mhe.Mchengerwa ameliambia Bunge kuwa, Wizara ya Afya imepanga kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 652.236 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambayo ni sawa na asilimia 36 ya bajeti iliyotengwa. Amefafanua kuwa kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi Bilioni 516, 323 ni kwa ajili ya mishahara ya Watumishi wa Afya na kiasi cha shilingi Bilioni 135, 913 zitatumika kwa ajili ya matumizi mengineyo

“Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali Watanzania na kuiwezesha Wizara ya Afya kupatiwa fedha nyingi katika miaka mitano iliyopita ambapo Nchi yetu imeendelea kuwa miongoni mwa nchi chache afrika zinazotoa matibabu kwa gharama nafu”amesema Mchengerwa.

Mwisho, Mhe. Mohamed Mchengerwa Waziri wa Afya ameliomba Bunge kuidhinisha kiasi cha jumla ya shilingi Trilioni 1.8 katika mwaka wa fedha 2026/27,amesema kupatika kwa bajeti hiyo kutasaidia kutekeleza shughuli mbalimbali zilizopangwa ikiwemo vipaumbele vyote 11 ambavyo vimelenga kuiweka Tanzania kuwa mfano kwa utoaji bora wa huduma za afya kwa Wananchi Barani Afrika.

tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluh Hassan ameipongeza timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu ...
11/05/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluh Hassan ameipongeza timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu chini ya miaka 20 kwa kufuzu kushiriki kombe la dunia mwaka 2026.

"Ninaipongeza Timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Miguu chini ya miaka 20 (Tanzanite Queens), kwa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2026. Ushindi wenu ni historia na heshima kubwa kwa nchi yetu, ikiwa ni mara ya kwanza Tanzania kufuzu kushiriki mashindano hayo.

Ninaielekeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na mamlaka zote zinazohusika kufanya maandalizi bora yatakayoiwezesha timu yetu kuiwakilisha vyema Tanzania na Afrika Mashariki katika mashindano hayo." Ameandika Rais Samia kwenye kurasa zake za mitandao


Na Mwandishi Wetu, Kilombero, Morogoro.TAASISI ya Utafiti wa Wanyampori Tanzania (Tanzania Wildlife Research Institute- ...
11/05/2026

Na Mwandishi Wetu, Kilombero, Morogoro.

TAASISI ya Utafiti wa Wanyampori Tanzania (Tanzania Wildlife Research Institute- TAWIRI) imeanza zoezi la kuyafunga mikanda ya visukuma mawimbi makundi ya tembo Wilaya yaKilombero, ikiwa ni Matumizi ya Technolojia kusadia kufuatilia makundi ya tembo yanayoleta changamoto kwenye maeneo ya wananchi.

Zoezi hilo linaongozwa na Mtafiti na Daktari wa wanyamapori kutoka TAWIRI, Dkt. Mikidadi Mtalika huku pia wakishirikiana na TANAPA na Wadau wa Six-Rivers Africa.

" teknolojia ya mikanda ya visukuma mawimbi vinasaidia kuwa na uhifadhi endelevu wa tembo sambamba na usalama kwa jamii.

Aidha zoezi hili ni endelevu kwa mwezi huu k**a ilivyo utafiti hauna ukomo" Imebainisha taarifa ya TAWIRI.

TAWIRI yenye makao yake makuu Njiro, Arusha, Ni taasisi ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, yenye jukumu la kufanya, kuratibu, na kusimamia tafiti za wanyamapori kwa uhifadhi endelevu na utalii nchini.

Lakini pia ikiwa na lengo kuu la kutoa ushauri wa kisayansi na taarifa sahihi kwa ajili ya usimamizi na uhifadhi endelevu.


08/05/2026

Wajumbe wa mabaraza ya Kata wametakiwa kuwa chachu ya amani katika jamii kwa kutatua migogoro kwa haki bila upendeleo na kutaisaidia mahak**a kupunduza mrundikano wa kesi baada ya kuanza kutatuliwa ngazi za chini.

Katibu Tawala Wilaya ya Singida Naima Chondo ametoa wito huo wakati akizungumza na wajumbe hao walipokuwa kwenye mafunzo ya namna ya utendaji kazi ya mabaraza ya Kata.

Nao Wajumbe wanaiomba jamii kutumia chombo hicho kabla ya kwenda ngazi zingine.

Write by

08/05/2026

WATU watano wamefariki dunia papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani iliyohusisha lori la mizigo lililokuwa limebeba shehena ya vinywaji baridi aina ya Pepsi pamoja na basi kubwa la abiria la kampuni ya SHABBIBY, baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso katika eneo la Kijiji cha Tanangozi, Kata ya Mseke, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Imeelezwa kuwa lori hilo la mizigo lilikuwa likitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam, huku basi kubwa la abiria la likiwa safarini kutoka Dodoma kwenda Mbeya.

Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa Dkt Alfredy Mwakalebela alisema walipokea miili mitano ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo sambamba na majeruhi 28 ambao walipatiwa matibabu katika hospitali hiyo.

Kiongozi wa kijeshi wa Mali, Assimi Goïta, amejiteua kushika wadhifa wa Waziri wa Ulinzi, akiongeza jukumu hilo juu ya n...
05/05/2026

Kiongozi wa kijeshi wa Mali, Assimi Goïta, amejiteua kushika wadhifa wa Waziri wa Ulinzi, akiongeza jukumu hilo juu ya nafasi yake ya sasa ya Rais wa mpito.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kuuawa kwa aliyekuwa Waziri wa Ulinzi, Sadio Camara, katika mashambulizi yaliyoripotiwa kuratibiwa na kundi la JNIM kwa kushirikiana na waasi wa FLA.

Camara alitajwa kuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano wa kijeshi kati ya Mali na Urusi, hatua ambayo ilisaidia kuongeza uwezo wa jeshi katika kupambana na makundi ya waasi. Kifo chake kinachukuliwa k**a pigo kubwa kwa juhudi za usalama nchini humo.

Kwa mujibu wa mabadiliko hayo mapya, Goïta sasa atasimamia moja kwa moja vyombo vya ulinzi na usalama, akisaidiwa na Mkuu wa Majeshi, Oumar Diarra, ambaye ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ulinzi.


Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto CGH, amewasili nchini Tanzania kwa Ziara ya Kitaifa ya Siku Mbili, Mei ...
04/05/2026

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto CGH, amewasili nchini Tanzania kwa Ziara ya Kitaifa ya Siku Mbili, Mei 4 na 5, 2026.

Mheshimiwa Ruto atapokelewa kwa gwaride la heshima na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Dar es Salaam ambapo pia watafanya mazungumzo ya uwili ili kuimarisha uhusiano wa Tanzania na Kenya.

Mapema kesho, Mei 5, 2026, Mheshimiwa Ruto atalihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma kabla ya kuhitimisha ziara yake.




Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Mei Mosi, 2026 kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanya...
01/05/2026

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Mei Mosi, 2026 kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani kwa Mkoa wa Arusha, amewataka waajiri wa Mkoa wa Arusha kuwasilisha kwa wakati michango ya wafanyakazi wao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii k**a ambavyo sheria za nchi zinawataka kufanya hivyo, akihimiza pia uwajibikaji kwa wafanyakazi ili kuweza kuwa na sauti katika madai ya haki katika maeneo yao ya kazi.

Mhe. Makalla ametoa rai hiyo kwenye Viwanja vya michezo vya kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha, akisisitiza pia kuhusu uadilifu na ushirikiano mzuri na waajiri wao ili kuweza kufikiwa kwa malengo waliyojiwekea, akikemea pia uharibifu wa makusudi wa miundombinu ya huduma za kijamii, akiagiza kuchukuliwa hatua kwa watakaobainika kuharibu miundombinu hiyo.

Mhe. Makalla ametumia hotuba yake pia kuwataka wananchi wa Mkoa wa Arusha kujiandaa kikamilifu kuchangamkia fursa za Ujio wa mkutano wa kimataifa wa Bunge la Dunia (IPU), ambapo wajumbe zaidi ya 3,000 wanatarajiwa kushiriki katika Mkutano huo utakaofanyika kati ya Oktoba 3-10, 2026 kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano AICC, akihimiza wafanyakazi pia kujiandaa katika kutoa huduma nzuri kwa wageni watakaofika katika maeneo yao kwaajili ya malazi, chakula na kadhalika.

"Aliyepo sokoni atafaidika kwasababu hoteli zitanunua bidhaa sokoni kwaajili ya vyakula, mwenye usafiri atafaidika na mwenye hoteli naye atafaidika- kwahiyo mnyororo ule wa thamani utamgusa kila mtu. Hii ni fursa ya biashara kwa wakazi wa Arusha na zaidi wapo ambao watakuja na familia na watatenga siku za kwenda kutalii, hivyo wadau wa utalii pia watafaidika na sisi k**a wafanyakazi katika maeneo mbalimbali tuwajibike pia kuwahudumia vizuri ili waione Tanzania k**a sehemu nzuri na salama ili baadae warudi tena kwaajili ya kutalii na kufanya uwekezaji katika Mkoa wetu." Amesema Mhe. Makalla.




Address

P. O. BOX 14070
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Savvy Media Live posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share