Savvy Media Live

Savvy Media Live MAONI YAKO FB,INSTAGRAM@SAVVY MEDIA LIVE. SIKILIZA SAVVY FM 105.3
LISTEN ONLINE: SAVVY FM ARUSHA.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amesema Mkoa huo unaandika historia mpya kupitia uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kw...
30/07/2025

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amesema Mkoa huo unaandika historia mpya kupitia uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kwala na miradi mingine mikubwa ya kimkakati itakayofanyika Julai 31, 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 30, 2025 katika eneo la tukio, Kunenge alieleza ,maandalizi ya hafla hiyo yamekamilika na amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo la kihistoria.

“Tunaweka historia mpya mkoani Pwani, Huu ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kujenga uchumi wa viwanda na kuimarisha miundombinu ya kisasa,” alieleza Kunenge.

Alieleza Rais Samia atazindua Bandari Kavu ya Kwala, safari ya treni ya mizigo kupitia reli ya kisasa (SGR), mapokezi ya mabehewa ya MGR, na Kongani ya Viwanda ya Kwala – mradi mkubwa uliogharimu takribani trilioni 6.

Katika kongani hiyo, Rais Samia atazindua viwanda saba vilivyokamilika na kuanza uzalishaji pamoja na kutembelea viwanda vingine vitano vilivyopo katika hatua mbalimbali za ujenzi.




  FLEVA SAVVY FM ARUSHA Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na   t...
30/07/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

tupo na mwekezaji music

tupo na

Usikose pia

Kwenye ni

Wachimbaji wako ni .g

Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili Uwanja wa Ndege wa Songea, mkoani Ruvuma...
30/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili Uwanja wa Ndege wa Songea, mkoani Ruvuma tayari kwa safari ya kuelekea Wilayani Namtumbo kwa ajili ya Uzinduzi wa Kiwanda cha Majaribio cha Uchenjuaji Madini ya Urani cha Mantra Tanzania Limited, tarehe 30 Julai, 2025.








Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa,  imepitisha rasmi majina ya wagombea wa nafasi mbalimb...
29/07/2025

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, imepitisha rasmi majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo ubunge na uwakilishi kwaajili ya kwenda kupigiwa kura na wajumbe watakaochagua mgombea mmoja ambaye atasimama kukiwakilisha Chama katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba mwaka huu.

Taarifa rasmi iliyotolewa leo Jumanne Julai 29,2025 katika Ofisi za Chama hicho Jijijini Dodoma na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM CPA Amos Makalla imeeleza kuwa Katika Jimbo la Bumbuli walioteuliwa uteuzi wa awali ni sita huku aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo January Makamba akitupwa nje katika kinyang'anyiro hicho .







  FLEVA SAVVY FM ARUSHA  Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na   ...
29/07/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

tupo na

Usikose pia

Kwenye ni

Wachimbaji wako ni g
Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter

Tanzania inauhitaji mkubwa wa nyumba kutokana na kasi ya ukuaji wa miji nchini ambapo inakadiriwa kuwa na mahitaji ya ny...
28/07/2025

Tanzania inauhitaji mkubwa wa nyumba kutokana na kasi ya ukuaji wa miji nchini ambapo inakadiriwa kuwa na mahitaji ya nyumba 26,840,909 ifikapo 2050 ili kukidhi mahitaji wa watu milioni 118.1.

Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kufungua semina kuhusu makazi, ujenzi na maendeleo ya miji kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wawekezaji wa sekta ya Milki kutoka Japan Julai 28, jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuna uhitaji mkubwa wa nyumba nchini ili kukidhi mahitaji watu katika maeneo mbalimbali nchini.

“Tanzania tuna uhitaji mkubwa wa nyumba kwa sababu ukiangalia miaka ya 1967, ukuaji wetu katika miji ulikuwa asilimia 6.2 tu, lakini katika sensa ya mwaka 2022 ukuaji katika miji yetu umekwenda asilimia 34.9 ambao ni ukuaji wa kasi kubwa sana na inatarajiwa kufikia asilimia 59 ifikapo mwaka 2050, hatua inayofanya nchi yetu kuwa moja ya nchi zenye miji inayokuwa kwa kasi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara” amesema Waziri Ndejembi.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ...
28/07/2025

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Jijini Dodoma tarehe 28 Julai, 2025.



hmwinyi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amesisitiza umuhimu wa kuchukua ...
28/07/2025

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amesisitiza umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti na za pamoja katika kuimarisha mifumo ya chakula ili kuhakikisha ushiriki endelevu wa Tanzania katika ajenda za maendeleo ya kimataifa.

Waziri Kombo ametoa kauli hiyo wakati wa kikao kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania jijini Addis Ababa, Ethiopia, ambapo anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Pili wa Mfumo wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (UNFSS+4).

Katika mkutano huo Waziri Kombo amepokea taarifa kuhusu maandalizi ya mkutano kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Innocent Shiyo, ambaye alieleza kuwa mkutano huo ni jukwaa la kipekee kwa Tanzania kushiriki katika kujenga ajenda ya kimataifa ya kilimo, kukuza usalama wa chakula, na kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Noel Kaganda, amewasilisha taarifa ya kiufundi akieleza kuwa mkutano huo unalenga kutathmini utekelezaji wa mageuzi ya mifumo ya chakula kwa misingi ya haki za binadamu, usawa wa kijinsia, utawala bora, na ulinganifu wa sera za kitaifa na kimataifa.







  FLEVA SAVVY FM ARUSHA Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na   t...
28/07/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

tupo na mwekezaji

tupo na

Usikose pia

Kwenye ni

Wachimbaji wako ni .g

Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) nchini Tanzania imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, utakaohusisha nafasi ...
26/07/2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) nchini Tanzania imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, utakaohusisha nafasi ya Rais, wabunge na madiwani, utafanyika siku ya Jumatano, tarehe 29 Oktoba 2025.

Akizungumza katika uzinduzi wa ratiba ya uchaguzi huo jijini Dodoma leo, Mwenyekiti wa INEC, Jaji wa rufaa Jacob Mwambegele, amesema maandalizi ya uchaguzi huo yameanza rasmi na kuainisha tarehe muhimu katika kalenda ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa Jaji Mwambegele, utoaji wa fomu za uteuzi kwa wagombea wa nafasi ya Rais na Makamu wa Rais utafanyika kati ya Agosti 9 hadi 27, 2025. Aidha, ameongeza; "Tarehe 27 Agosti 2025 itakuwa siku ya uteuzi wa wagombea wa kiti cha rais na makamu rais, uteuzi wa wagombea ubunge na uteuzi wa wagombea udiwani", alisema Jaji huyo.

Kwa upande wa kampeni, Tanzania Bara itakuwa na kipindi cha kampeni kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 28, huku Tanzania Zanzibar kampeni zikiendeshwa kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 27, ili kupisha upigaji wa kura ya mapema.

"Tarehe 29 Oktoba, 2025 siku ya Jumatano itakuwa ndio siku ya kupiga kura", alisema Mwambegele, kuhusu uchaguzi huo unaolenga kuwapa wananchi fursa ya kidemokrasia kuchagua viongozi wao wa ngazi mbalimbali.



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinatarajia kufanya Mkutano Mkuu Maalum kwa njia ya mtandao kesho, Julai 26, 2025, ambapo ajen...
25/07/2025

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinatarajia kufanya Mkutano Mkuu Maalum kwa njia ya mtandao kesho, Julai 26, 2025, ambapo ajenda kuu itakuwa kufanya marekebisho madogo ya Katiba ya chama hicho

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi, Uenezi na Mafunzo CPA Amos Makala, amesema hayo leo Julai 25, jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mkutano huo mkuu maalum.

CPA Makala, amesema kumekuwepo na maneno mengi kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mkutano huo unatarajiwa kufanyika kwa njia ya mtandao.

Pia, amesema kwamujibu wa katiba ya Chama cha Mapinduzi CCM, inawaruhusu kufanya mkutano mkuu maalum kwa njia ya mtandao pale wanapoona inafaa.

Vile vile, amesema hadi sasa maandalizi ya mkutano huo yamekamilika na kwa mara ya kwanza watu watakwenda kushuhudi chama hicho kikifanya mkutano mkuu wake kwa njia ya mtandao.


Ghala la kuhifadhia magodoro lililopo katika Mtaa wa Kasese Kata ya Mkolani Jijini Mwanza linalodaiwa kuwa mali ya, Thom...
25/07/2025

Ghala la kuhifadhia magodoro lililopo katika Mtaa wa Kasese Kata ya Mkolani Jijini Mwanza linalodaiwa kuwa mali ya, Thomas Sospeter limeteketea kwa moto pamoja na baadhi ya vibanda vya Wafanyabiashara na wajasiliamali vilivyokuwa pembezoni.

Mrakibu Msaidizi wa jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mwanza, Deusdedith Rutta amesema chanzo cha moto huo bado hakijafahamika huku akiwapongeza wananchi kwa kuchukua hatua za mapema kuanza kudhibiti moto huo usilete madhara makubwa.



Address

P. O. BOX 14070
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Savvy Media Live posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share