Savvy Media Live

Savvy Media Live MAONI YAKO FB,INSTAGRAM@SAVVY MEDIA LIVE. SIKILIZA SAVVY FM 105.3
LISTEN ONLINE: SAVVY FM ARUSHA.

Watu tisa wamefariki dunia mapema Leo katika kijiji cha Kambi ya Nyasa wilaya ya Chemba mkoani Dodoma.Taarifa iliyotolew...
18/09/2025

Watu tisa wamefariki dunia mapema Leo katika kijiji cha Kambi ya Nyasa wilaya ya Chemba mkoani Dodoma.

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema watu watano akiwemo dereva wa basi walifariki hapo hapo na wengine wanne wamefariki baada ya kufikishwa hospitali.

  FLEVA SAVVY FM ARUSHA  Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na   ...
18/09/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

tupo na mwekezaji

Usikose pia

Wachimbaji wako ni .g

Baruti na

Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter

Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Watanzania kuwa uchaguzi m...
18/09/2025

Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Watanzania kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu utafanyika kwa usalama , akisisitiza kuwa uchaguzi ni takwa la kidemokrasia na siyo vita.

Slide👉👉

hmwinyi




‎Idara ya Uhamiaji Wilaya ya Mbogwe, mkoani Geita, imefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 34 kutoka nchi za Burundi na ...
17/09/2025

‎Idara ya Uhamiaji Wilaya ya Mbogwe, mkoani Geita, imefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 34 kutoka nchi za Burundi na Rwanda, kufuatia oparesheni maalum ya kiusalama iliyoendeshwa kwa weledi mkubwa.

‎Oparesheni hiyo ilisimamiwa na Afisa Uhamiaji wa Wilaya ya Mbogwe, Mrakibu wa Uhamiaji SI Amir Ally Abbasi, chini ya uratibu wa Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACI James Andrew Mwanjotile, Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Geita.

‎Oparesheni hiyo inatekelezwa kwa mujibu wa maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania, CGI Dkt. Anna Peter Makakala Ili kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Taifa kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 2025.

‎Wahamiaji hao walinaswa kupitia msako maalum uliolenga yombo vyote vya usafiri vinavyoingia Wilaya ya Mbogwe kupitia barabara kuu inayoelekea Kahama huku lengo kuu likiwa ni kudhibiti wimbi la uhamiaji haramu linaloathiri usalama wa taifa.

‎SI Abbasi, aliwaonya kwa msisitizo wamiliki wa vyombo vya usafiri – hususan mabasi madogo (Hiace) na malori – kuacha mara moja tabia ya kuwahifadhi au kuwabeba wahamiaji haramu, kwani elimu ya kutosha imeshatolewa kupitia maafisa wa uhamiaji, hivyo sasa ni wakati wa utekelezaji wa sheria bila shuruti.

‎Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Mbogwe imeeleza kuwa itaendelea na misako, ukaguzi, na uchunguzi katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo na viunga vyake ili kukabiliana na tatizo la uhamiaji haramu, hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.





Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dk Emmanuel Nchimbi akiwasalimia wananchi ...
15/09/2025

Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dk Emmanuel Nchimbi akiwasalimia wananchi wa Mombo katika Jimbo la Korogwe Vijijini leo Septemba 15, 2025 na kuwaomba kura kwa ajili ya wagombea wa CCM wa nafasi ya urais, ubunge na madiwani ifikapo Oktoba 29, mwaka huu.

Dk Nchimbi ameanza siku yake ya kwanza mkoani Tanga kufanya mikutano ya kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025.


Mahakama Kuu Masijala ya Dar es Salaam imeyakataa mapingamizi yaliyowekwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kwenye ke...
15/09/2025

Mahakama Kuu Masijala ya Dar es Salaam imeyakataa mapingamizi yaliyowekwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kwenye kesi ya Uhaini inayomkabili.

Tundu Lissu aliweka mapingamizi mahakamani hapo akipinga namna kesi ya Ukabidhi (Committal) ilivyoendeshwa kwenye mahakama ya Kisutu. Baadhi ya mapingamizi aliyoyaweka ni Uhalali wa Mahakama ya Kisutu kuendesha Committal wakati mtuhumiwa (Mhe. Lissu) alikamatwa wilaya ya Mbinga mkoa wa Ruvuma na Uahirishwaji kiholela wakati wa kesi. Jaji Kiongozi wa kesi hiyo, Dunstan Ndunguru.

Mahakama ya Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga,  imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtuhumiwa Grayson Muze Msem...
11/09/2025

Mahakama ya Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtuhumiwa Grayson Muze Msemo (miaka 55), Mkristo, Muinjilisti na mkazi wa Raskazoni – Tanga, hapo jana Septemba 10, 2025 baada ya kupatikana na hatia ya kosa la kubaka mtoto mwenye umri wa mwaka 1 na miezi 4. Awali, imeelezwa mahakamani kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 1 Septemba 2025 katika eneo la Funguni Street, Pangani.

Akisoma hukumu tarehe 10 Septemba 2025 majira ya saa 13:00, Mheshimiwa Husna Mwiula, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Pangani, alisema kuwa mahakama imeridhika na ushahidi uliowasilishwa na kumhukumu mtuhumiwa kifungo cha miaka 30 jela ili iwe fundisho kwa jamii na kuhakikisha haki inatendeka.
tanzania

Usikose kusikiliza kipindi cha    ambacho kinakujia kila Ijumaa kuanzia saa 10.15 hadi 11: 00 jioni kupitia Savvy FM 105...
11/09/2025

Usikose kusikiliza kipindi cha ambacho kinakujia kila Ijumaa kuanzia saa 10.15 hadi 11: 00 jioni kupitia Savvy FM 105.3 Arusha. Utapata kusikia mijadala mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu na kwa Ijumaa hii utapata kusikia kuhusiana na ilani za uchaguzi ya vyama vya siasa.

Host:





WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Septemba 11, 2025 amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa konga...
11/09/2025

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Septemba 11, 2025 amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa kongamano la Nne la Kitaifa  la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza linalofanyika katika ukumbi wa hotel ya Malaika Beach jijini Mwanza.

Washiriki wa kongamano hilo ni wadau wa maendeleo, wakurugenzi wa halmashauri, wataalam kutoka nje na ndani ya Serikali pamoja na viongozi kutoka Mataifa mbalimbali ya Afrika na nje ya Afrika.

kaulimbiu  ya Kongamano ni “Kuimarisha uwezo wa Ufuatiliaji na Tathmini kwa Jamii ili kuwezesha utendaji bora na maendeleo endelevu”.




Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa leo Septemba 11, 2025 amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa kong...
11/09/2025

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Septemba 11, 2025 amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa kongamano la Nne la Kitaifa  la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza linalofanyika katika ukumbi wa hotel ya Malaika Beach jijini Mwanza.

Washiriki wa kongamano hilo ni wadau wa maendeleo, wakurugenzi wa halmashauri, wataalam kutoka nje na ndani ya Serikali pamoja na viongozi kutoka Mataifa mbalimbali ya Afrika na nje ya Afrika.

kaulimbiu  ya Kongamano ni “Kuimarisha uwezo wa Ufuatiliaji na Tathmini kwa Jamii ili kuwezesha utendaji bora na maendeleo endelevu”.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮...
11/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 amewasili na kupokelewa na maelfu ya wananchi wa wilaya ya Uyui waliojitokeza kwa wingi bila kujali itikadi za vyama vyao vya kisiasa, kwaajili ya kumlaki na kumsikiliza katika kunadi sera za CCM na ahadi zake.

Rais Dkt. Samia yupo mkoani Tabora akiendelea na mikutano yake ya kampeni za Urais kupitia CCM ambapo siku ya leo Alhamis tarehe 11 Septemba 2025 atakuwa na mikutano katika wilaya hii ya Uyui kisha ataelekea wilaya ya Urambo na kumalizia Kaliua.



Address

P. O. BOX 14070
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Savvy Media Live posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share