Injili Tv

Injili Tv Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Injili Tv, TV Channel, Moivaro, Arusha.

Kwa Matangazo ya Injili, Kupromote Nyimbo za Injili, Mafundisho, Huduma ya Maombi na Maombezi, Ushuhuda, wasiliana nasi kwa WhatsApp Na +255763071635 Mungu akubariki

Mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka Rwanda, Gloriose Musabyimana, anayejulikana zaidi kwa jina la Gogo, amefariki dunia ...
05/09/2025

Mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka Rwanda, Gloriose Musabyimana, anayejulikana zaidi kwa jina la Gogo, amefariki dunia nchini Uganda akiwa na umri wa miaka 36 baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa ripoti ya kitabibu kutoka Kyegera Doctors Center jijini Kampala, Gogo alifariki usiku wa Septemba 3, 2025. Taarifa hiyo imethibitishwa pia na Bikem Uwayesu, rafiki na mwakilishi wake wa karibu aliyekuwa naye katika ziara hiyo.

Uwayesu alisema Gogo alisafiri kutoka Rwanda tarehe 28 Agosti kuelekea Mbarara, Uganda, kuhudhuria mkutano wa injili uliofanyika kuanzia Agosti 29 hadi 31. Baada ya hapo, alielekea jijini Kampala kuendelea na shughuli za matangazo ya kazi zake za muziki.

Hata hivyo, mara baada ya kuwasili Kampala, alipatwa na maradhi. Awali walidhani ni hali ya kawaida kwani aliwahi kukumbwa na tatizo hilo kabla, lakini ghafla afya yake ilizorota.

Alikimbizwa hospitalini lakini alifariki dunia mara tu alipofikishwa.

Gogo alijulikana kupitia nyimbo zake za injili zilizovuma mitandaoni, hususan wimbo wake Blood of Jesus. Wimbo huo ulipata umaarufu wa kimataifa baada ya msanii kutoka Afrika Kusini, David Scott maarufu k**a The Kiffness, kuufanyia remix na kuuongeza ala za muziki wa tarumbeta na piano, kisha kuusambaza kupitia TikTok na YouTube mnamo Januari 2025.

Remix hiyo tayari imeangaliwa zaidi ya mara 780,000 kwenye YouTube.

Gogo aliwavutia wapenzi wengi wa muziki wa injili ndani na nje ya Rwanda. Kifo chake kimeacha simanzi kubwa katika tasnia ya muziki wa injili Afrika Mashariki, huku wapenzi na wadau wa muziki wakimtaja k**a upotevu mkubwa kwa kanisa na jamii ya muziki wa injili.

Bwana Yesu Asifiwe!Tunawakaribisha kwenye semina ya neno la Mungu, Kigoma Mjini katika uwanja wa Mwanga Sokoni. Semina i...
05/09/2025

Bwana Yesu Asifiwe!
Tunawakaribisha kwenye semina ya neno la Mungu, Kigoma Mjini katika uwanja wa Mwanga Sokoni. Semina inaanza tarehe 04 hadi 07 Septemba 2025, kwanzia saa 9 alasiri hadi saa 12 jioni. Semina itakuwa LIVE kupitia channel yetu ya Youtube, Upendo TV na redio mbali mbali. Mjulishe na Mwingine na Mungu awabariki.

Karibu ushiriki kongamano la 17 la maombi ya kitaifa, tarehe 29 Julai -01 Agosti 2025 katika Ukumbi wa Maombi Ndachi, Do...
14/07/2025

Karibu ushiriki kongamano la 17 la maombi ya kitaifa, tarehe 29 Julai -01 Agosti 2025 katika Ukumbi wa Maombi Ndachi, Dodoma mjini. Kufika ni tarehe 28 Julai 2025 na kuondoka tarehe 02 Agosti 2025.
Jiandikishe kwa mratibu wako wa mkoa. Kwa mawasiliano zaidi piga
Arusha: +255745525225 au +254736501081
Dar: +255742525225
Mungu awabariki.

19/12/2024

Mama yake Martha Mwaipaja Jamani Jamani

Maombi imegawanyika katika Sehem kuu mbili(1)Maombi ya kuongea na (2)Maombi ya KusikiaWatu wengi hupenda Maombi ya kuong...
07/09/2024

Maombi imegawanyika katika Sehem kuu mbili
(1)Maombi ya kuongea na
(2)Maombi ya Kusikia
Watu wengi hupenda Maombi ya kuongea,
Maana maombi ya kuongea ni wewe kupeleka hitaji lako kwa Mungu, Maombi ya Kusikia ni wewe Kusikiliza Anachohitaji Mungu, Maombi ya kusikia yanapatikana kwa wewe kusoma Neno la Mungu, Unaposoma Neno maana yake unasikiliza Alichosema, Anachosema au Anachoagiza Mungu,
"KUMBUKUMBU LA TORATI 28:1-14 Inasema
"Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;
na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.
Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.
Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.
Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.
Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.
BWANA atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.
BWANA ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako.
BWANA atakuweka uwe taifa takatifu kwake, k**a alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya BWANA, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.
Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la BWANA, nao watakuwa na hofu kwako.
BWANA atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi BWANA aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.
Atakufunulia BWANA hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.
BWANA atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;
msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.
Amen Amen
Mt Paul .

RATIBA YA KUUAGA MWILI
23/08/2024

RATIBA YA KUUAGA MWILI

Kuokoka ni kumkiri Yesu Kuwa Bwana na kuzaliwa kwa mara ya pili, Kuzaliwa na Mungu, Yohana 3, Biblia inasema amewekewa M...
07/08/2024

Kuokoka ni kumkiri Yesu Kuwa Bwana na kuzaliwa kwa mara ya pili, Kuzaliwa na Mungu, Yohana 3,
Biblia inasema amewekewa Mwanadamu kuishi mara moja, na baada ya kuishi ni kufa, na baada ya kufa ni hukumu, Uwezo wa Mtu kutengeneza maisha yake ni akiwa hai, Ila anapokufa Mungu atajua pa kumuweka, hapatakuwa tena na uwezo wa kumuombea, Maana huyu mtu alipokuwa hai alisikia injili kupitia Watumishi wa Mungu akapuuza, Yesu alituonya akasema k**a ilivyokuwa kipindi cha Nuhu na Safina, watu walimpuuza alipokuwa akiwaambia watu walimpuuza waliendelea kula kunywa kuuza na kununua hadi ile siku ilipowajia ghafla gharika ikawaangamiza, ndivyo itakavyokuwa hata Siku yako Usipoamini leo, hata kwa habari ya lazaro na yule tajiri, Tajiri alipokufa alifika kwenye mateso aliomba arudi tena duniani kuwaambia hata ndugu zake huko kuna mateso wabadilike, lakini alinyimwa akaambiwa wapo watumishi wa Mungu wawasikilize wao wasipowaamini wao hata afufuke mtu kutoka kwa wafu hawatamwamini. Hivyo Wakati uliyekubalika ni sasa, na saa ya wokovu ni leo. Mt Paul fb Prince Paul

Swali la Leo??
20/06/2024

Swali la Leo??

MAOMBI YA  KUOMBEA NYUMBA YAKOZaburi 91:1-16"Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi. Ni...
06/06/2024

MAOMBI YA KUOMBEA NYUMBA YAKO

Zaburi 91:1-16
"Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu
Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu nitakayemtumaini.
Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji,
Na katika tauni iharibuyo.
Kwa manyoya yake atakufunika,
Chini ya mbawa zake utapata kimbilio;
Uaminifu wake ni ngao na kigao.
Hutaogopa hofu ya usiku,
Wala mshale urukao mchana,
Wala tauni ipitayo gizani,
Wala uele uharibuo adhuhuri,
Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako.
Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume!
Hata hivyo hautakukaribia wewe.
Ila kwa macho yako utatazama,
Na kuyaona malipo ya wasio haki.
Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;
Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.
Mabaya hayatakupata wewe,
Wala tauni haitaikaribia hema yako.
Kwa kuwa atakuagizia malaika zake
Wakulinde katika njia zako zote.
For he shall give his angels charge over thee, to keep Mikononi mwao watakuchukua,
Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
Utawakanyaga simba na nyoka,
Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.
Kwa kuwa amekaza kunipenda
Nitamwokoa; na kumweka palipo juu,
Kwa kuwa amenijua Jina langu.
Ataniita nami nitamwitikia;
Nitakuwa pamoja naye taabuni,
Nitamwokoa na kumtukuza;

Kwa siku nyingi nitamshibisha,
Nami nitamwonyesha wokovu wangu.
Amen Amen

Swali la leo??? Injili Tv
27/05/2024

Swali la leo??? Injili Tv

26/05/2024

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Ngalemi Hipolite, Luka Junior, Lowasa Paha, Israel Town

MAOMBI KUHUSU ULINZI FAMILIA YAKO Zaburi 121:1-8[1]Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi? [...
16/05/2024

MAOMBI KUHUSU ULINZI FAMILIA YAKO

Zaburi 121:1-8

[1]Nitayainua macho yangu niitazame milima,
Msaada wangu utatoka wapi?

[2]Msaada wangu u katika BWANA,
Aliyezifanya mbingu na nchi.

[3]Asiuache mguu wako usogezwe;
Asisinzie akulindaye;

[4]Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,
Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

[5]BWANA ndiye mlinzi wako;
BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

[6]Jua halitakupiga mchana,
Wala mwezi wakati wa usiku.

[7]BWANA atakulinda na mabaya yote,
Atakulinda nafsi yako.

[8]BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,
Tangu sasa na hata milele.
Amen Ame

Address

Moivaro
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Injili Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Injili Tv:

Share

Category