Arusha One Fm 101.7

Arusha One Fm 101.7 Arusha one Fm Redio Ni moja ya redio bora kabisa kutokea kaskazini mwa Tanzania, huku ikiwa inapatikana katika mikoa Ya Tanga, Kilimanjaro, Singida na

  Mahak**a Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam Julai 18,2025 imemuhukumu kutumikia kifungo cha miaka 30 jela na fai...
21/07/2025

Mahak**a Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam Julai 18,2025 imemuhukumu kutumikia kifungo cha miaka 30 jela na faini ya shilingi milioni moja Prince Deogratius Daniel mwenye umri wa miaka 45, mkazi wa Bamba Gezaulole Manispaa ya Kigamboni Dar es Salaam baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka binti mwenye umri wa miaka 15 mwanafunzi wa kidato cha kwanza

Akisoma hukumu hiyo Mh Nestory Baro amesema kuwa Mahak**a imeridhishwa na ushahidi uliowasilishwa Mahak**ani hapo ambapo pasi na chembe ya shaka umemuunganisha Mtuhumiwa huyo kutenda kosa hilo.

Awali imeelezwa kuwa Mtuhumiwa alimchukua binti huyo kijiji kwa mama yake Novemba 11,2023 na kuahidi kuwa yeye na mkewe ambaye yupo Dar es Salaam watamlea na kumsomesha binti yake ili kumsaidia ulezi kutokana na hali duni ya maisha aliyonayo.

Baada ya binti kufika kwenye nyumba ya huyo baba yake mlezi hakuwahi kumuona mke wake na badala yake mnamo mwezi Disemba 2023 tarehe asiyoikumbuka majira ya usiku alimbaka kwa mara ya kwanza binti huyo na kumkataza kuongea na majirani. Mei 20,2024 majira ya saa Prince Deogratious alimbaka tena binti huyo na baada ya hapo binti aliweza kuwahadithia majirani na kumfikisha kituo cha Polisi kwa hatua za kisheria na kupelekea kutiwa hatiani.

21/07/2025

Moto mkubwa umeikumba meli ya KM Barcelona VA karibu na pwani ya Indonesia, na kuwalazimu abiria kuruka baharini katika hali ya kutisha huku watu wengi wakihofiwa kufariki dunia kwa kunsa ndani ya meli hiyo

Moto huo ulizuka saa 1;30 usiku kwa saa za huko siku ya leo Jumapili, ripoti zinasema.

Picha na video za kuutisha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha abiria wakiruka ndani ya maji, wengi wao wakiwa wamevalia jaketi za kuokoa maisha za rangi ya chungwa, huku moto huo ukiiteketeza meli hiyo

  Siku moja baada ya mlinzi wa kushoto Mohamed Hussein "Zimbwe Jr" kutangaza kuachana na Klabu ya Simba, hii leo Meneja ...
21/07/2025

Siku moja baada ya mlinzi wa kushoto Mohamed Hussein "Zimbwe Jr" kutangaza kuachana na Klabu ya Simba, hii leo Meneja wa habari na mawasiliano wa klabu hiyo amewataka mashabiki wa timu hiyo kutokuwa wanyonge kwa maamuzi hayo.

Aidha Ahmed amesema uamuzi uliofanyika ni kwa maamuzi sahihi kwa pande zote na hakuna aliyepata hasara.

"Kwenye hili agano sio Simba sio Tshaba ambae amepata hasara kila mmoja amenufaika na maamuzi haya. Ndugu zangu Wana Simba kwa hili tutembee kifua mbele tumefanya maamuzi kwa kuangalia Simba bora ya kesho. Wala tusiingie ubaridi kwa kua anaenda upinzani wameshaenda wengi na hakuna maajabu"- Ahmed Ally Simba SC.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali iliyosababisha vifo vya watu wawili ak...
21/07/2025

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali iliyosababisha vifo vya watu wawili akiwemo aliyekuwa diwani wa kata ya Solwa, Awadh Hafiz pamoja na mwanamke mmoja ambaye jina lake halijafahamika.

Akizungumza kwa simu , Magomi amesema ajali hiyo imetokea eneo la Ibadakuli, Barabara ya Shinyanga mjini katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga baada ya basi la abiria kuigonga bajaji ya iliyokuwa imebeba abiria,

“Taarifa hiyo ninayo mezani, lakini sipo katika eneo la kazi ninaweza kukupa taarifa zaidi nikifika kazini, ila taarifa niliyonayo ajali imetokea maeneo ya Ibadakuli barabara ya kuelekea Shinyanga mjini,” amesema Kamanda Magoma.

Amesema basi la abiria lilitaka kulipita gari lingine bila kuchukua tahadhari na kwenda kuigonga babaji hiyo.
Amesema kwenye ajali hiyo, watu wawili wamefariki dunia akiwamo aliyekuwa diwani wa Solwa, Awadh Hafiz na mwanamke mmoja ambaye jina lake halijafahamika.

“Lakini pia imejeruhi watu kadhaa ambao idadi haijafahamika, nitakapo fika eneo la tukio nitatoa taarifa kamili ,” amesema Magomi.

19/07/2025

Mfanyabiashara mwenye asili ya Uturuki, Alptekin Aksoy (52) ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana waliokuwa wakitumia pikipiki.

Tukio hilo limetokea leo Julai 18, 2025 saa 5:30 asubuhi katika eneo la Kinondoni Makaburini, jijini Dar es Salaam.

  Balozi wa Marekani nchini Uturuki na Mjumbe Maalumu wa Syria Tom Barrack amesema kuwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin N...
19/07/2025

Balozi wa Marekani nchini Uturuki na Mjumbe Maalumu wa Syria Tom Barrack amesema kuwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na mkuu wa mamlaka ya mpito nchini Syria Ahmad al-Sharaa waMEkubaliana kusitisha mapigano kwa msaada wa Uturuki, Jordan na nchi jirani.

"Tunatoa wito kwa Druze, Bedouins, na Wasunni kuweka chini silaha zao na kufanya kazi na watu wengine walio wachache kujenga utambulisho mpya wa Syria," Barrak alisema katika chapisho kwenye akaunti yake ya Twitter.

Siku ya Jumatano, Israel ilianzisha mashambulizi ya anga dhidi ya Damascus, yakilenga majeshi ya serikali ya kusini, na kutaka waondoke, ikisema wakati huo ililenga kulinda kuwalinda watu wa jamii ya Druze ya Syria

  Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameelezea masikitiko yake baada ya shambulizi la Israel dhidi ya kanisa pekee...
18/07/2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameelezea masikitiko yake baada ya shambulizi la Israel dhidi ya kanisa pekee la Kikatoliki kuwaua watu watatu na kuwajeruhi watu wengine huko Gaza jana Julai 17,2025.

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki wa Jimbo kuu la Jerusalem amesema watu wengine 10 pia walijeruhiwa katika shambulio dhidi ya Kanisa la Familia Takatifu mjini Gaza, akiwemo padri wa parokia hiyo.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo wa XIV(14) ameelezea kuhuzunishwa na mauaji hayo na kutoa wito wa usitishaji mapigano mara moja huku pia akielezea matumaini yake makubwa ya mazungumzo na maridhiano ya upatikanaji wa amani ya kudumu katika ukanda huo.

  Klabu ya Yanga imemtangaza kiungo mkabaji Moussa Balla Conte akitokea katika klabu ya CS Sfaxien kwa mkataba wa miaka ...
18/07/2025

Klabu ya Yanga imemtangaza kiungo mkabaji Moussa Balla Conte akitokea katika klabu ya CS Sfaxien kwa mkataba wa miaka miwili.

Mguinea huyo mwenye umri wa miaka 21 anakwenda kuchukua nafasi ya Khalid Auch ambaye amemaliza mkataba wake ndani ya mabingwa hao mara nne mfululizo wa ligi kuu Tanzania Bara.

Watoto watatu wa familia moja wamekutwa wamefariki dunia baada ya nyumba waliyokuwa wanaishi kuungua moto.Watoto hao Mem...
17/07/2025

Watoto watatu wa familia moja wamekutwa wamefariki dunia baada ya nyumba waliyokuwa wanaishi kuungua moto.

Watoto hao Membe Ndama (7), Mwaru Ndama (2)na Sayi Ndama (1)walikuwa wakiishi na wazazi wao katika Kijiji cha Nambilanje, Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, John Imori amesema kuwa tukio hilo limetokea jana Jumatano Julai 16, 2025 saa 11 jioni katika Kijiji cha Nambilanje.

Kamanda Imori amefafanua kuwa baba na mama wa watoto hao walitoka kwenda kuchota maji na kuchimba viazi hivyo waliwaacha watoto hao nyumbani, ambapo Sayi alikuwa amelala na wenzake walikuwa wakicheza nje ya nyumba hiyo.

"Hawa wazazi wa watoto waliofariki walikuwa wametoka na eneo walilokwenda lilikuwa siyo mbali na nyumbani. Baada ya muda kidogo waliona nyumba yao inaungua moto," amesema Kamanda Imori.

Amesema nyumba ilikuwa imeezekwa nyasi jambo lililosababisha kushika moto kwa haraka na kusababisha vifo vya watoto hao watatu.

Kamanda Imori amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni moto uliokuwa kwenye jiko la mawe kushika nyasi za ukuta wa ndani na kusababisha nyumba kuungua.

Miili ya marehemu hao imefanyiwa uchunguzi na Daktari Ezekia Ambekile wa Hosptali ya Wilaya ya Ruangwa na kubaini kuwa chanzo cha vifo ni kukosa hewa baada ya kuungua moto.

"Nimepokea miili ya marehemu muda wa jioni (jana) na kuifanyia uchunguzi kisha kugundua kuwa vifo vyao vilisababishwa na kukosa hewa," amesema Daktari Ambekile.

Baba wa marehemu hao, Ndama Mashauri (33) amesema kuwa wakati wanachota maji na mke wake Mindi Msasu (20) waliona moto unawaka nyumbani kwao na walipofika walikuta watoto wameshafariki.

"Nilitoka mimi na mke wangu kwenda kuchota maji na kuchimba viazi eneo k**a la kilometa 2, tuliwaacha watoto nyumbani mmoja amelala na wawili walikuwa wanacheza, baadaye nikaona nyumba inaungua tulipofika karibu tuliwakuta watoto wetu wote watatu wamefariki dunia," amesema Mashauri.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi kuepuka tabia ya kuwaacha watoto peke yao bila uangalizi.

  Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Sauda Hassan mkazi wa mtaa wa mji wa zamani uliopo kata ya Bariadi mkoani Simiyu a...
17/07/2025

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Sauda Hassan mkazi wa mtaa wa mji wa zamani uliopo kata ya Bariadi mkoani Simiyu amenusurika kifo baada ya moto aliokuwa akitumia kupika maharage kuunguza sofs na hatimaye kusambaa.

kwa mujibu wa mwanamke huyo alitoka kwenda kuongea na bibi yake na aliporudi akakuta moto umeanza kuunguza sofa ambalo lilikuwa jirani na moto huo na badae ukaanza kusambaa.

Jeshi la zimamoto Mkoa wa Simiyu kupitia kaimu k**anda wa jeshi hilo ASF Faustin Mtitu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

  Wanajeshi watatu wa Kenya, wameuwa na wengine wamejeruhiwa baada ya msafara wao kushambuliwa na bomu iliyotegwa ardhin...
16/07/2025

Wanajeshi watatu wa Kenya, wameuwa na wengine wamejeruhiwa baada ya msafara wao kushambuliwa na bomu iliyotegwa ardhini, Mashariki mwa Kanuti ya Lamu, karibu na Somalia

Shambulio hilo lilitokea wakati wanajeshi hao walipokuwa wanafanya ziara katika barabara ya Kiunga na Sankuri, wakati gari lao lilipokanyaga bomu lililotegwa ardhini.

Jeshi la Kenya limethibitisha vifo vya maafisa wake watatu na wangine saba wameripotiwa kujeruhiwa na wanaendelea kupata matibabu.

Aidha, uongozi wa jeshi hilo unasema kwa ushirikiano na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, uchunguzi unaendelea kuhusu tukio hilo.

  Waziri wa Kazi wa Cuba Marta Elena Feitó Cabrera amelazimika kujiuzulu baada ya kutoa maoni ya kukanusha kuwepo kwa om...
16/07/2025

Waziri wa Kazi wa Cuba Marta Elena Feitó Cabrera amelazimika kujiuzulu baada ya kutoa maoni ya kukanusha kuwepo kwa ombaomba katika kisiwa hicho kinachoongozwa na Wakomunisti.

Waziri alikuwa amesema hakuna kitu k**a "ombaomba" nchini Cuba na watu wanaopitia takataka walikuwa, kimsingi, wakifanya hivyo kwa hiari ya kupata "fedha rahisi", k**a alivyoelezea.

Maoni yake, yaliyotolewa katika kikao cha bunge, yalikasolewa na Wacuba ndani na nje ya nchi, na kulaumiwa na rais wa kisiwa hicho, Miguel Díaz-Canel.Alilazimika kujiuzulu hivi karibuni.

Address

Arusha

Telephone

+255767118011

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Arusha One Fm 101.7 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Arusha One Fm 101.7:

Share