Sunrise Radio Tz

Sunrise Radio Tz SUNRISE RADIO INAHAKIKISHA UNAPATA HABARI ZILIZO NA UHUAKIKA KUTOKA KILA KONA YA TANZANIA NA NJE YA TANZANIA

09/05/2026

*Dkt Samia: Tunafikiria kuwawezesha mitaji wafungwa wanapotoka gerezani*

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka Serikali yake ianze kufikiria mpango wa kuanzishwa mfuko maalumu katika Jeshi la Magereza, utakaochangiwa fedha ambazo wafungwa watakaotoka gerezani na ujuzi, wapewe mitaji ya kuanzia maisha.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Jumamosi Mei 9, 2026 alipozungumza wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo ya uongozi ngazi ya juu kozi namba 48 kwa mwaka 2025/26 katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania.

Amesema Serikali imeendekea kufanya mageuzi ya mifumo kwa kuweka kipaumbele katika urekebishaji wa tabia za wafungwa unaofungamanishwa na ujuzi na maandalizi ya mfungwa kurejea katika jamii akiwa na tabia njema na mchango kwa ustawi wa maendeleo.

Pamoja na kuwa na ujuzi, amesema changamoto inabaki wanapotoka wanakwenda kufanya nini na wanaanzaje ilihali hawana mitaji.

"Nilikuwa nanong'ona na Mkuu wa Jeshi na Waziri, kuanza sasa kufikiria sera ya kuanza kuwachangia magereza. Kuwe na mfuko maalumu kwa wale wafungwa wanaotoka na ujuzi mzuri waanze kupatiwa chochote cha kwenda kuanzia kazi," amesema.

Ametaka magereza kufanya utafiti kuhusu sababu za wafungwa kurejea magerezani hata wanapomaliza vifungo vyao.

05/05/2026

Ruto amsifu Rais Samia kwa uongozi imara

Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto, amempongeza Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi bora na kusimama imara wakati wa vurugu za Oktoba 29,2025.

Aidha, amempongeza kwa mchango wake katika kuimarisha uhusiano wa pande mbili na ushirikiano wa kikanda kati ya Tanzania na Uganda.
Rais Ruto ametoa pongezi hizo mbele ya Bunge la Tanzania, wakati akilihutubia leo Mei 5, 2026, ikiwa ni ziara yake ya kwanza nchini tangu awamu ya pili ya utawala wa Rais Samia.

Rais Ruto pia ameeleza kufurahishwa kwake na namna Rais Samia anavyosimamia maendeleo na kuendeleza mshik**ano wa karibu zaidi kati ya nchi jirani.

“Ninapaswa kuupongeza uongozi bora wa Rais Samia Suluhu Hassan katika mkutano huu, hasa kwa kusimama imara,” amesema Rais Ruto.

04/05/2026
*Dkt Samia:Serikali imeanza kulipa madai ya wafanyakazi*Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan...
01/05/2026

*Dkt Samia:Serikali imeanza kulipa madai ya wafanyakazi*

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imeanza kulipa malimbikizo ya madeni ya hifadhi ya jamii, posho za likizo na uhamisho.

Pia, imeanza kulipa na itaendelea kulipa malimbikizo ya mishahara, akiahidi mchakato kuwa endelevu kulingana na tathimini inayoendelea.

Dkt Samia ameeleza hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’, yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.

“Hatuletewi madai tukalipa hapo hapo, lazima tutathimini na yale yanayothibitika ni halali tumeanza kuyalipa,” amesema Rais Dkt Samia.

29/04/2026

*Tume: Rais Samia ameonesha dhamira ya kufanya uchunguzi na kupata ukweli*

Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imesema Rais Samia Suluhu Hassan, alionesha dhamira ya kweli ya kufanya uchunguzi ili kupata ukweli.

Mjumbe wa Tume hiyo, Prof. Ibrahim Juma, ameyasema hayo leo Aprili 28, 2026, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema Jumuiya ya Kimataifa inataka kufahamu mambo mawili ambayo ni k**a Tanzania ina dhamira ya kufanya uchunguzi wa kina na uwajibikaji.

“Kwa Rais Samia kuunda Tume ya Uchunguzi ni dhamira tosha kwamba tunataka kufanya uchunguzi, tunatafuta ukweli, tunatafuta ushahidi na tukishapata hizi taarifa ndio tunaamua suala la uwajibikaji,” amesema Prof. Juma.
Amesema hukumu ya Mahak**a Kuu ilisema si kazi ya tume kutoa hukumu, kutaja waliohusika na akitajwa mtu akakimbilia Mahak**a Kuu itaamuru aya zote zilizomtaja zifuwe.

28/04/2026

*Tume yatoa sababu za kutotaja majina ya wahusika kwenye ripoti*
Mjumbe wa Tume ya Uchunguzi wa ghasia wakati na baada ya uchaguzi, Profesa Ibrahim Juma, amesema ripoti haijataja majina ya wahusika kwasababu za kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 28, 2026, amesma wahusika wangeweza kwenda mahak**a kuu na kuchukua hatua za kuiamuru tume kufuta aya zote zilizowataja kwenye ripoti kwasababu hawakupewa haki ya kusikilizwa.
“Mhusika ambaye angetajwa angeomba amri na aya zote tunazomtaja bila kumpa nafasi ya kuusikilizwa zingefutwa kwenye ripoti.
“Katika Mahak**a ya Kenya imeshawahi kufanya hivyo na Mahakamu ya Juu ya Canada imeshawahi kukutana na hoja hiyo kwamba kuna watu walitajwa na tume lakini hawakupewa nafasi ya kusikilizwa ikabidi aya zote zinazowatajwa ziondolewe,” amesema Prof. Juma.
Amesema hivyo tume ilichukua tahadhari hiyo kutokana na walichukua uzoefu walionao.

28/04/2026

Prof. Juma: Mahak**a Kuu iliipa Tume uhalali

Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imesema Mahak**a Kuu iliwapa
uhalali kisheria wa kuwapo na kufanya kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mjumbe wa Tume, Prof. Ibrahim Juma, amesema uhalali wa Tume hii ulithibitishwa na Mhak**a Kuu ya Tanzania.

“Wengi wamekuwa wakihoji uhalali wa tume yetu. Nataka kuweka rekodi sawa. Mahak**a Kuu ya Tanzania, katika Shauri Namba 12 la Mwaka 2025, ilitoa uamuzi wa wazi kuwa Rais ana mamlaka kikatiba kuunda tume za uchunguzi, na kwamba Tume hii imeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32,” amesema Prof. Juma.

Ameongeza kuwa uamuzi huo ulitolewa baada ya baadhi ya watu kufungua kesi mahak**ani kupinga uwepo wa Tume. “Jaji amesema wazi: Tume hii ni halali. Kazi zake ni halali. Ushahidi uliokusanywa ni halali.”

Prof. Juma ameeleza kuwa kinga hiyo ya kisheria ndiyo iliyoiwezesha Tume kuwaita na kuwahoji wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa mikoa, mak**anda wa polisi, viongozi wa vyama vya siasa, na wananchi wapatao 63,603 bila woga.

“Tusingeweza kukamilisha kazi hii k**a tusingekuwa na ngao ya kisheria kutoka Mhimili wa Mahak**a,” amesisitiza.

Tume imeshakabidhi Ripoti yake kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 23 Aprili, 2026.

“Uhalali wa ripoti hii haukutoka Ikulu pekee ulithibitishwa na Mahak**a. Kilichobaki sasa ni Watanzania kuisoma, kuijadili, na taasisi husika kuchukua hatua stahiki,” amethibitisha Prof. Juma.

14/04/2026

*Wamiliki mabasi: Huduma zinaendelea hatugomi, Serikali sikivu imetusikiliza*

Tunaposema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Sikivu tunamaanisha.Hii limedhiirika baada ya Serikali kupokea na kuahidi kuyafanyia kazi maombi ya wasafirishaji.

Wasafirishaji hao wakiwemo wamiliki wa mabasi ya masafa marefu na daladala walipanga kufanya mgomo kesho Jumapili (Aprili 12) kutokana na gharama za uendeshaji kuwa juu kutokana na bei za mafuta.

Kwa kutambua hilo, Serikali ya awamu sita kupitia Waziri mwenye dhamana ya uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amekutana na wadau hao na kuahidi kuzifanyi kazi changamoto zote zinazowakabili.

“Tarehe 8 tuliotoa rai ya kusisitisha usafiri, lakini bahati nzuri Serikali sikivu inayongozwa na Dkt Samia imetuma Waziri Mbarawa kutusikiliza, tulikuwa na kikao kizuri, tumesikilizana matatizo yetu na wameyachukua na kuyafanyia kazi,” amesema Priscu John Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania.

Wamiliki hao wametoa hofu abiria nchini wakiwataka kuendelea na mchakato wa kufanya ‘booking’ za safari kwa kuwa usafiri utakuwepo.

Address

P. O. Box 11064
Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sunrise Radio Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sunrise Radio Tz:

Share

Category