GADI TV

GADI TV GADI TV ni televisheni ya Mtandaoni ambayo inajihusisha na kutoa maudhui ya Kijamii na Kisiasa.

02/06/2026

Baada ya mbunge wa Jimbo la Katavi, Thomas Kampala, kuchangia hoja bungeni akishauri kuhusu mmomonyoko wa maadili kwenye Jamii, June 01, 2026, amesema kuwa endapo ushauri wake hautafanyiwa kazi na serikali, Wizara ya viwanda na biashara iandae pampasi kwa ajili ya vijana kwa miaka ya 30 ijayo.

02/06/2026

Baada ya kuwepo kwa madai kuwa kuna wanafunzi wawili wakike wanaosoma shule ya msingi wanauzwa kwa siri kingono na mwanamke mmoja aliyeamua kuwafungia ndani ya chumba chake katika kata ya Baraa Jijini Arusha, Binti mmoja ambaye tunampa jina la Chausiku, ameibuka na kueleza jinsi mwanamke huyo alivyokuwa akiwatafuta wanaume kwa ajili vitendo hivyo Jijini humo.

Binti huyo akizungumza na waandishi wa habari, mbali na kusimulia mbinu anazotumia mwanamke huyo, amedai kuwa amenusurika kuingizwa kwenye biashara hiyo baada ya kutafutiwa mwaname asiyemjua huku akitakiwa kwenda kundishiriki naye tendo hilo la kingono.

Ikumbukwe inaelezwa kuwa baada ya tukio hilo kubainika na kuzua taharuki kwa wananchi, uongozi wa eneo husika walimchukua mwanamke huyo na kisha kumpeleka mikononi mwa jeshi la polisi Jijini humo.

01/06/2026

Wanafunzi wawili wa shule ya msingi waliokuwa wanatafutwa na wazazi wao baada ya kutokuonekana nyumbani kwao kwa takribani siku nne katika kata ya Baraa Jijini Arusha, hatimaye wamepatikana, huku ikidaiwa kuwa wamekutwa kwenye chumba cha mwanamke mmoja wakiwa wanatumikishwa kingono na wanaume tofauti tofauti Jijini humo.

Inaelezwa kuwa tukio hilo limebainika, Mei 31, 2026, baada ya ndugu wa mmoja wa watoto hao kufika anapoishi mwanamke huyo anayefahamika kwa jina moja la Linnah, kwa lengo lakumweleza kuhusu upotevu wa watoto hao, k**a iwapo amewaona popote, lakini ghafla baada ya mlango kufunguliwa ndugu huyo aliwaona watoto hao wakiwa ndani ya chumba hicho.

01/06/2026

Kufuatia kuwepo kwa kampeni ya kuchanja chanjo ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa inayoendeshwa na shirika la Mbwa wa Afrika Jijini la Arusha, hatimaye wananchi wamenufaika na zoezi hilo na kueleza kuwa idadi ya vifo vya binadamu ambavyo vilikuwa vinasababishwa na kuumwa na mbwa mwenye kichaa vitapungua.

Inakadiriwa kuwa, kila mwaka hapa nchini Tanzania, watu 1500 huwa wanapoteza maisha kutokana na kuumwa na mbwa mwenye changamoto hiyo.

Katika zoezi hilo ambalo limetolewa siku za mapumziko (Weekend), Mei 30, 2026 na Mei 31, 2026, linatarajiwa kutolewa tena June 07, hadi 08, 2026, Jijini humo.

29/05/2026

Baada ya kukadiriwa kuwa, watu 1500 huwa wanapoteza maisha kila mwaka Nchini, kutokana na kuugua kichaa cha mbwa, hatimaye Uongozi wa hospitali ya Mbwa wa Afrika, umekuja na kampeni ya kuchanja chanjo ya ugonjwa huo kwa mbwa wote wa mitaa katika Jiji la Arusha, bila malipo, ikiwa nisehemu yakupunguza idadi ya vifo hivyo.

Uongozi huo ukizungumza na GADI TV Mei 28, 2026, umesema kuwa kampeni hiyo imekuja ikiwa sehemu ya mikakati ya kuhakikisha kuwa kila mbwa aliyepo kwenye mtaa anachanjwa ili kuepukana na ugonjwa huo hatari unaoweza kuambukizwa binadamu.

Aidha, inaelezwa kuwa chanjo hiyo itaanza kutolewa kuanzia Mei 30, 2026 kwenye vituo maalum vilivyotengwa kila kata ndani ya jiji hilo, k**a ambavyo inaonekana katika kipeperushi hiki, huku siku ya juma mosi na juma pili kwa kila wiki, ikiwa ndio siku zilizotengwa kwa ajili ya zoezi hilo.

Kadhalika, Uongozi huo umesema kuwa utendaji kazi wa hospitali hiyo, ni pamoja na kutibu mbwa koko wa mitaani ambao wamekuwa wakipata majeraha kutokana na kugongwa na magari barabarani, ambapo wakati mwingine baadhi ya mbwa hulazimika kulazwa wodini na baadae kuruhusiwa baada ya kupona.

Hata hivyo, uongozi huo unaeleza kuwa, hulazimika kupita mitaani nakuwakusanya mbwa wenye changamoto mbalimbali nakufikisha hospitalini hapo, ambapo wengine hutibiwa kwa kufanyiwa upasuaji, baada ya kufanyiwa vipimo kwa kutumia vifaa vya kisasa.

28/05/2026

Mwanamke mmoja aitwae Rosemary Willium ambaye ni mmiliki wa kituo cha kutoa huduma kwa Waraibu katika kata ya Sokoni One Jijini Arusha, amedai kuwa kutokana na baadhi ya vijana kuingia kwenye uraibu ngono pamoja na vileweshi, na kupelekea athari mbalimbali za kiafya miongoni mwao, amenzisha kituo hicho maalum cha kutoa msaada wa huduma za uraibu, k**a sehemu ya kutoa msaada kwa jamii yake.

Rosemary akizungumza na GADI TV akiwa kituoni hapo, amesema urahibu wa ngono, k**ari na vileweshi, umekuwa ni mwanzo wa vijana wengi kushindwa kutimiza ndoto zao kwa wakati, hivyo huduma hiyo inaweza kubadili mwelekeo hasi kwa vijana hao.

20/05/2026

Baada ya mwanamke anayefahamika kwa jina la Jenipha Paskali (28) mkazi wa kata ya Olasiti Jijini Arusha, kueleza kuwa kila wiki anatumia shilingi laki sita kusafisha damu yake kutokana na figo zake kushindwa kufanya kazi, na wasamaria wema kumsaidia kulipia gharama kwa muda wa miezi minne, hatimaye muda huo umekwisha, na sasa anaendelea kukandamizwa na changamoto hiyo bila msaada wowote.

Ikumbukwe kuwa Jenipha alieleza GADI TV kuwa tatizo la figo zake kushindwa kufanya kazi, lilikuja mara baada ya kuishi maisha ya kutokunywa maji ya kutosha mwilini, ambapo mwili wake ulianza kuvimba ghafla kutokana na changamoto hiyo.

Unaweza kuwasiliana na Jenipha kwa msaada zaidi kupitia namba yake 👉🏻 +255 740 540 489.

19/05/2026

Bibi anayefahamika kwa jina la Tsino Marmo mkazi wa kata ya Rothia wilaya ya Karatu mkoani Arusha, amedai kuwa amejikuta katika hali ya sintofahamu baada ya kikundi cha watu kutaka kumpokonya kimabavu shamba lake lenye ukubwa wa hekari 10, licha ya Mahak**a kumpa haki ya kumiliki shamba hilo mkoani humo.

Bibi huyo akizungumza na GADI TV, amesema kuwa shamba hilo linalong'ang'aniwa na kikundi cha watu hao ambao ni ndugu zake, alipewa na baba yake mdogo k**a sehemu ya ahsante baada ya kumuuguza baba huyo kwa kipindi cha miaka 23 alipokuwa akigua, huku ndugu wengine wakijiweka mbali naye.

——————————————————————————
🎥 ukiwa na tukio la kihabari usisite kutupigia simu, namba zetu ni hizi 👉🏻 0743 888 555 (WhatsApp & Call)

Kufuatia tukio la kijana aitwae Alvin Asei (pichani) mkazi wa Kirua Vunjo Magharibi mkoani Kilimanjaro, kujikuta katika ...
18/05/2026

Kufuatia tukio la kijana aitwae Alvin Asei (pichani) mkazi wa Kirua Vunjo Magharibi mkoani Kilimanjaro, kujikuta katika hali ya majuto makali baada ya kudaiwa amemuua rafiki wa baba yake, kutokana na tuhuma kuwa rafiki huyo alitaka kwenda kumsemea kuwa amekunywa pombe, Jeshi la polisi mkoani humo limesema kuwa Alvin yupo chini ya ulinzi wa Jeshi hilo kwa hatua nyingine za kisheria.

Ikumbukwe kuwa punde baada ya tukio hilo kutokea Mei 12, 2026, Alvin aliambia GADI TV kuwa alitenda tukio hilo kwa kutumia kifaa cha kukatia majani (Mundo), baada ya marehemu kumjeruhi sehemu ya kichwa kwakutumia fimbo ya mkahawa.

Disclaimer: Disturbing Image!
——————————————————————————
🎥 ukiwa na tukio la kihabari usisite kutupigia simu, namba zetu ni hizi 👉🏻 0743 888 555 (WhatsApp & Call)

14/05/2026

Katika tukio la mzee Thomas Silayo ambaye ni mkazi wa wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, kuawa na mtu anayedaiwa ni ndugu yake, baada ya mzee huyo kushinda kesi ya ardhi iliyokuwa ikipigwa na upande wa ndugu huyo, Dada wa marehemu amesema kuwa mdogo wake amekufa kifo cha mateso makali kwa kukatiwa mguu na mkono juu gogo k**a mnyama.

" [kijana] alianza kumshambulia baba yake mkubwa, wakachukua mguu wakaweka juu ya gogo wakaukata hadi ukakatika [pamoja] na mkono" amesema dada huyo.

Ikumbukwe kuwa taarifa ya Jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro, ilisema kuwa mtuhumiwa wa tukio hilo anaendelea kusakwa tangu atende tukio hilo, Mei 8, 2026.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GADI TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to GADI TV:

Share