31/08/2026
Mwanafunzi wa darasa sita katika shule ya msingi Ilboru wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, aitwae Dickson Jonasi (12), anadaiwa amejinyonga hadi kufariki dunia, baada kutoa ahadi siku za nyuma, kuwa itafika wakati atajinyonga kutokana na kutopendwa na baba yake na kunyimwa chakula wilayani humo.
Katika tukio hilo ambalo limetokea leo asubuhi Agasti 31, 2026, mama mkubwa wa marehemu huyo amesema Dickson alisema “atajiua maana baba yangu anipendi, bibi yangu, baba yangu, [wa]naninyima chakula"
Aidha, Mama huyo amesema kuwa alimsihi mtoto huyo asijinyonge, lakini katika hali isiyokuwa yakawaida asubuhi ya leo aligoma kwenda shuleni na kisha kujinyonga.
"... [baada ya ahadi ya kujinyonga] nikamwambia, habari yakusema utajiua utaenda Jehanamu, usijiue, kila siku jioni njoo unidai chakula. Maoni yangu, baba hampendi k**a mwanae" amesema Mama mkubwa.
Kadhalika, Zakayo Lukumai ambaye ni mmoja wa familia hiyo amesema, mtoto huyo amekumbana na manyanyaso makali kutoka kwa mama wa kambo ambaye aliwahi kusema "nafuu nimpe mbwa chakula, kushinda nimpe huyu kijana".
Hata hivyo, Baba wa mtoto huyo amekana kumtesa mtoto huyo, nakusema mtoto huyo amekuwa chini ya uangalizi wa bibi yake, tangu aachane na mkewe wa kwanza miaka mitatu iliyopita.
...............................................................................
Tamko la tahadhari (disclaimer); taarifa hii inalenga kutoa habari ya kuelimisha, na si kuhamasisha, kuhimiza, au kuhalalisha kujidhuru au kujiua.