GADI TV

GADI TV GADI TV ni televisheni ya Mtandaoni ambayo inajihusisha na kutoa maudhui ya Kijamii na Kisiasa.

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefiwa na mume wake aitwae Hafidh Ameir Hassan aliye...
07/09/2026

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefiwa na mume wake aitwae Hafidh Ameir Hassan aliyekuwa akipatiwa matibabu ya maradhi ya moyo Zanzibar.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi amethibitisha taarifa hiyo, na kusema Hafidh amefariki leo Septemba 7, 2026, na taratibu za mazishi zinaendelea Kizimkazi Zanzibar.

06/09/2026

Baada ya kijana anayefahamika kwa jina la Erick Pallangyo mkazi wa kata ya Aker wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, kujenga barabara yenye urefu wa mita sabini kwa kiwango cha zege, hatimaye Uongozi wa wilaya hiyo umempatia tuzo pamoja na kumpeleka kutalii, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika jamii.

01/09/2026

Baada ya Godlisten Malisa kuachiwa na Jeshi la polisi mkoa wa Arusha, na taarifa kutolewa kwa umma na jeshi hilo, ikidai kuwa alikuwa akichunguzwa kuhusiana na tuhuma za kijinai, Malisa amesimulia namna alivyok**atwa hadi kuachiwa kwake asubuhi ya leo Septemba 01, 2026.

Askari mwenye namba H. 1796, Koplo Mwita, inadaiwa akiwa amefungiwa kwenye chumba cha mahabusu kutokana na tuhuma za kij...
31/08/2026

Askari mwenye namba H. 1796, Koplo Mwita, inadaiwa akiwa amefungiwa kwenye chumba cha mahabusu kutokana na tuhuma za kijinai zinazomkabili mkoani Tanga, amechukua uamuzi wa kujinyonga ndani ya chumba hicho na kusababisha kupoteza maisha.

Katika taarifa ya Jeshi la polisi mkoani humo, ambayo imetolewa hivi punde, Agasti 31, 2026, imesema kuwa Askari huyo alikutwa amefariki dunia Agosti 27, 2026 majira ya saa moja na dakika tatu usiku, ndani ya chumba hicho.

Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa uchunguzi wa kisayansi umefanyika huku ndugu wakishuhudia, na methibitika kuwa chanzo cha kifo chake nikukosa hewa kutokana na kujinyonga.

Kadhalika, imesema kabla ya kifo chake, alikuwa ameshikiliwa na wenzake watano wenye vyeo mbalimbali, pamoja na afisa mmoja, ambapo wote kwapamoja wanakabiliwa na tuhuma za kijinai.

Mwanafunzi wa darasa sita katika shule ya msingi Ilboru wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, aitwae Dickson Jonasi (12), ana...
31/08/2026

Mwanafunzi wa darasa sita katika shule ya msingi Ilboru wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, aitwae Dickson Jonasi (12), anadaiwa amejinyonga hadi kufariki dunia, baada kutoa ahadi siku za nyuma, kuwa itafika wakati atajinyonga kutokana na kutopendwa na baba yake na kunyimwa chakula wilayani humo.

Katika tukio hilo ambalo limetokea leo asubuhi Agasti 31, 2026, mama mkubwa wa marehemu huyo amesema Dickson alisema “atajiua maana baba yangu anipendi, bibi yangu, baba yangu, [wa]naninyima chakula"

Aidha, Mama huyo amesema kuwa alimsihi mtoto huyo asijinyonge, lakini katika hali isiyokuwa yakawaida asubuhi ya leo aligoma kwenda shuleni na kisha kujinyonga.

"... [baada ya ahadi ya kujinyonga] nikamwambia, habari yakusema utajiua utaenda Jehanamu, usijiue, kila siku jioni njoo unidai chakula. Maoni yangu, baba hampendi k**a mwanae" amesema Mama mkubwa.

Kadhalika, Zakayo Lukumai ambaye ni mmoja wa familia hiyo amesema, mtoto huyo amekumbana na manyanyaso makali kutoka kwa mama wa kambo ambaye aliwahi kusema "nafuu nimpe mbwa chakula, kushinda nimpe huyu kijana".

Hata hivyo, Baba wa mtoto huyo amekana kumtesa mtoto huyo, nakusema mtoto huyo amekuwa chini ya uangalizi wa bibi yake, tangu aachane na mkewe wa kwanza miaka mitatu iliyopita.
...............................................................................
Tamko la tahadhari (disclaimer); taarifa hii inalenga kutoa habari ya kuelimisha, na si kuhamasisha, kuhimiza, au kuhalalisha kujidhuru au kujiua.

Kufuatia tukio la kijana anayefahamika kwa jina la Mathias Damian (17) mkazi wa kata ya Magugu wilaya ya Babati mkoani M...
31/08/2026

Kufuatia tukio la kijana anayefahamika kwa jina la Mathias Damian (17) mkazi wa kata ya Magugu wilaya ya Babati mkoani Manyara, kufariki dunia kiutata, huku uume wake na sehemu zingine zikiwa zinatokwa damu nyingi, Familia ya kijana huyo imeiomba serikali ifanye uchunguzi wa kina, badala ya tukio hilo kuhusishwa na ajali ya gari.

Baba mzazi wa kijana huyo aitwae Francis Damiani, amesema kuwa tukio la kijana wake kukutwa pabarabarani akiwa amefariki usiku wa Agasti 25, 2026, limekuja siku chache baada ya kijana huyo kupigwa hadharani, akituhumiwa kutumiana ujumbe mfupi (sms) na mke wa mtu, kuhusu mapenzi.

Aidha, Francis amesema kuwa wakati kijana wake akipigwa na mtu anayefahamika kwa jina la Peter, Agasti 23, 2026, (siku mbili kabla ya kifo), kuhusiana na madai hayo, alijaribu kumuombea msamaha lakini aliyekuwa anatoa adhabu alitoa ahadi akisema "nitamalizana na kijana wako tu"

"nikiangalia kwa mimi mzazi, hili sio tukio la [kugongwa] na gari, mtoto wangu ameshambuliwa sana, kuna vitu k**a vya chuma ametobolewa, uume unatoka damu, ubongo unatoka kwenye pua, kichwani kunatoka damu" Francis.

Kufuatia hatua ya Halmashauri Kuu ya CCM kumpendekeza Waziri wa Nishati, Deogratius John Ndejembi, kuwa Makamu wa Rais w...
27/08/2026

Kufuatia hatua ya Halmashauri Kuu ya CCM kumpendekeza Waziri wa Nishati, Deogratius John Ndejembi, kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania, aliyekuwa mtia nia nafasi ya ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki 2025, aitwae Johnson Sarakikya amesema uteuzi wa Ndejembi unaonyesha imani kuwa vijana wamezidi kuaminiwa kwa uchapakazi.

Johnson ametoa andiko akizungumzia hilo katika ukurasa wake wa Instagram, Agasti 27, 2026, ambapo mbali na mambo mengine amempongeza Ndejembi kwa kuaminiwa na Halmashauri kuu CCM, ikiongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameona dhamira ya uwajibikaji wake kwa wakati wote wautendaji wake kazini.

" ... [Ndejembi] tunakuombea kwa Mungu akutunze na kukuongoza katika Majukumu ya kumsaidia Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Uteuzi huu unatupa Imani sana sisi Vijana" Johnson.

“Kamati Kuu imejadili kuhusu suala la nidhamu na maadili ambalo lilikuwa linamkabili Emmanuel Nchimbi, na baada ya kuzin...
26/08/2026

“Kamati Kuu imejadili kuhusu suala la nidhamu na maadili ambalo lilikuwa linamkabili Emmanuel Nchimbi, na baada ya kuzingatia taarifa zote zilizokuwepo, ilithibitika kwamba katiba ya CCM na kanuni zake zilikiukwa...
..hivyo Nchimbi amefukuzwa uanachama” Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, akizungumza na Waandishi wa habari usiku Agasti 26, 2026, Jijini Dar es Salaam.

Mwanaume mmoja ambaye majina yake hayajaweza kufahamika mara moja katika kata ya Mawezi wilaya ya Moshi Mjini mkoani Kil...
24/08/2026

Mwanaume mmoja ambaye majina yake hayajaweza kufahamika mara moja katika kata ya Mawezi wilaya ya Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro, anadaiwa amechoma majengo mawili yaliyokuwa yanatoa huduma ya mahak**a ya mwanzo, na kisha kukimbilia kusikojulikana wilayani humo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi, aliyoitoa leo Agasti 24, 2026, amesema kuwa mtu huyo anayedaiwa kutenda tukio hilo, anadhani kuwa na tatizo la afya akili.

"...alifanikiwa kuingia eneo hili la Mahak**a ya mwanzo, nakuanzisha moto katika maeneo mawili tofauti, wakati utaratibu wa kumk**ata unaendelea akakimbia" Mkomagi.

Aidha, ikumbukwe kuwa majengo hayo yaliyochomwa moto yalikuwa yanatoa huduma za kimahak**a katika siku za nyuma.
.......................................................................

Ukiwa na tukio la kihabari wasiliana nasi kwa namba hizi... 0743 888 555.

23/08/2026

Raia wa Romania aitwae Constantin Catalin Podoleanu (39), mwenye makazi yake eneo la Njiro mkoani Arusha, amek**atwa na vyombo vya usalama, ikidaiwa ni baada ya kukutwa na kadi bandia za bank, zinazohusishwa kuiba fedha za watu.

Katika taarifa ambayo imetolewa na Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha, Agasti 22, 2026, imesema kuwa raia huyo alik**atwa Agasti 20, 2026 katika eneo la Njiro mkoani humo.

👉Ukiwa na tukio la kihabari unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi... 0743 888 555. (Call/WhatsApp).

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GADI TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to GADI TV:

Shortcuts

Share