GADI TV

GADI TV GADI TV ni televisheni ya Mtandaoni ambayo inajihusisha na kutoa maudhui ya Kijamii na Kisiasa.
(1)

"Tumeondokewa na kiongozi mahiri, aliyependa nchi yake na kazi zake, niwaombe familia msiba huu ni mtihani na ni mzito s...
13/12/2025

"Tumeondokewa na kiongozi mahiri, aliyependa nchi yake na kazi zake, niwaombe familia msiba huu ni mtihani na ni mzito sana, shik**aneni, pendaneni, msisikilize maeno yakuwagawa, mmepata bahati ya kuwa na mama mwenye wema, endelezeni wema wake...
..Mungu amjalie amuweke pema, amuondolee adhabu zote na safari yake yakwenda peponi iwe nyepesi" Spika wa Bunge la Tanzania, M***a Azzan Zungu akizungumza katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma, wakati wa ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho Marehemu Jenista Mhagama, Disemba 13, 2025.

"Baada ya uchaguzi matokeo kutangazwa, alipata changamoto ya kuaguka ghafla, kidogo akapoteza fahamu wakati huo, alinifa...
12/12/2025

"Baada ya uchaguzi matokeo kutangazwa, alipata changamoto ya kuaguka ghafla, kidogo akapoteza fahamu wakati huo, alinifahamisha yeye mwenyewe, lakini tunaambiwa pia na hapa karibuni alianguka tena, na hii imetokea tena...
..kwa hiyo inatufundisha kwamba kwa viongozi na watanzania kwa ujumla tuna wajibu mara kwa mara kuangalia afya zetu, pengine unaweza kuwa na tatizo la moyo hujui" Kauli aliyozungumza Waziri wa Afya, Mhe Mohamed Mchengerwa akiwa nyumbani kwa Marehemu Jenista Muhagama leo Disemba 12, 2025, Jijini Dodoma.

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama. Ninatoa po...
11/12/2025

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama. Ninatoa pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa M***a Azzan Zungu, wananchi wa Jimbo la Peramiho, familia, ndugu, jamaa na marafiki...
..kwa miaka 38, Mheshimiwa Mhagama amekuwa mwanachama mahiri wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kiongozi wa vijana, kiongozi wa wanawake, waziri katika awamu mbalimbali na mnasihi wa wengi katika siasa na maisha...
..Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina." Andiko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii kufuatia kifo cha mbunge huyo kilichotokea Disemba 11, 2025, Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania M***a Azzan Zungu (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Perami...
11/12/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania M***a Azzan Zungu (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea leo tarehe 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma.

"Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Peramiho, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu," amesema Mhe. Spika katika taarifa yake ambayo ameitoa kwa Umma hivi punde.

Mwanamke anayefahamika kwa jina la Marry Timotheo mkazi wa Kijiji cha Garijembe kata ya Tembela mkoani Mbeya, anadaiwa a...
10/12/2025

Mwanamke anayefahamika kwa jina la Marry Timotheo mkazi wa Kijiji cha Garijembe kata ya Tembela mkoani Mbeya, anadaiwa amemuua mtoto wake mwenye umri wa miaka 10 aitwae Scola Athanas, baada ya kuanza kumuadhibu na kumpiga na kitu kizito kichwani kwa madai kuwa amezidi utukutu.

Katika taarifa ya jeshi la polisi ambayo imetolewa leo, imeeleza kuwa mtuhumiwa huyo alitenda tukio hilo Desemba 09, 2025, na kisha kushirikiana na jirani yake kwa kuchukua mwili wa mtoto huyo na kwenda kuutupa kwenye shamba lakaribu na nyumba yake.

Aidha, Taarifa hiyo imesema kuwa mwanamke huyo pamoja na jirani huyo wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa hatua zaidi za kisheria.

Baada ya Tanzania kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru hapo jana, huku baadhi ya watu wakisherekea wakiwa majumbani mwao kufuat...
10/12/2025

Baada ya Tanzania kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru hapo jana, huku baadhi ya watu wakisherekea wakiwa majumbani mwao kufuatia wito wa serikali kuwa wasiokuwa na shughuli za ulazima wasalie kwenye makazi yao, Jeshi la Polisi nchini limetoa shukrani kwa wananchi wote kwa kukutotii kauli za waliokuwa wanataka zifanyike vurugu kupitia siku hiyo.

Katika taarifa ambayo imetolewa na jeshi la polisi Nchini leo Disemba 10, 2025, kwa imesema "Tunawashukuru na kuwapongeza wananchi wote kwa nafasi zao kwa namna wanavyoendelea kuwakataa na kuwapuunza wale wanaohamasisha na kuchochea vurugu na ukiukwaji wa sheria za nchi kupitia mitandao ya kijamii na njia nyingine"

06/12/2025

Mzee wenye umri wa miaka 73 anayefahamika kwa jina la John Kombe mkazi wa kata ya Kirua Vunjo Magharibi mkoani Kilimanjaroinadaiwa ameuawa na kisha mwili wake kufungiwa kwa siri dukani kwake alipokuwa akilala, mara baada ya kumaliza shughuli zake za siku dukani hapo mkoani humo.

Katika tukio hilo ambalo limetokea Novemba 29, 2025, inaelezwa kuwa mwili wa mzee huyo ulionekana ukiwa unatokwa damu sehemu masikioni, puani na mdomoni, ikiwa ni mara baada Maofisa wa Jeshi la polisi kuvunja mlango wa duka hilo ambao ulifungwa na watu wasiojulikana wanaodaiwa kutenda tukio hilo la kinyama.

Aidha, Juhudi za kulitafuta Jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro zinaendelea kwa taarifa zaidi.

📌KWA TAARIFA ZA MATUKIO WASILIANA NASI KWA NAMBA 0743 888 555 /CALL & WHATSAPP.

01/12/2025

Kijana anayefahamika kwa jina la Victor Baltazari mkazi wa kata ya Kirua Vunjo Kusini wilaya ya Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro, anadaiwa amemvua marehemu nguo aina ya jora na kisha kuvaa nakumbilia kusikojulikana baada ya kubaka na kuua wilayani humo.

Inaelezwa kuwa Marehemu huyo anayetambulika kwa jila la Involatha Hilary (49) alitendewa ukatili huo wakati usiojulikana kwenye nyumba aliyokuwa akilala peke yake, ambapo mchana wa Novemba 23, 2025 mwili wake ulibainika umefichwa kwenye shamba lililopo karibu na nyumba hiyo, huku nguo za mtuhumiwa zikiwa katika eneo hilo.

Aidha, inaelezwa kuwa baada ya tukio hilo kuwa wazi, baadhi ya watu walianza kuelezea jinsi walivyomshuhudia mtuhumiwa akiwa anakimbia mitaani huku akiwa amevaa kijora cha marehemu.

Kadhalika, GADI TV tunaendelea kulitafuta Jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro kwa taarifa zaidi.

30/11/2025

Kufuatia tukio la mwanaume anayefahamika kwa jina la Baraka Melami (40) mkazi wa kata ya Kimnyaki wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, kudai kuwa alikatwa uume wake na mkewe usiku Novemba 19, 2025, kwasasa mwanaume huyo amerejea nyumbani akitokea hosptalini huku akitumia mpira kwa ajili yakujisaidia haja ndogo.

Mwanaume huyo akizungumza na GADI TV akiwa nyumbani kwake wilayani humo, ameomba msaada kwa Mashirika au watu binafsi waweze kumsaidia k**a iwapo itawezekana achongewe mfano wa uume ili uweze kumsaidia kutoa haja ndogo.

Aidha, ikumbukwe kuwa mwanaume huyo alidai kuwa mkewe alimkata uume wake baada kumuhamasisha kufanya tendo la ndoa usiku wa Novemba 19, 2025, huku sababu za kufanya hivyo akiwa hazijui.

26/11/2025

Familia ya marehemu mzee Hashim Zorawanga iliyopo wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro ambayo inaeleza kuwa iliachiwa nyumba na mzee huyo iliyopo kwenye kiwanja namba 15 kitalu "E" katika eneo hilo, wameiomba serikali iwasaidie kupata haki, ikiwa ni baada ya ndugu yao kufungua kesi mahak**ani na kisha kupewa ushindi kuhusu umiliki wa nyumba hiyo, licha ya namba ya hati iliyotumika kuamua kesi hiyo ikiwa ni tofauti naya nyumba yao.

25/11/2025

Ni mama mzazi wa Jenifer Jovin maarufu kwa jina la Niffer akiwa anaangua kilio katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo Novemba 25, 2025, baada ya mwanae kurudishwa gerezani, huku washtakiwa aliokuwa nao pamoja katika mashtaka ya uhaini wakiwa wamefutiwa mashtaka hayo na kuachiwa huru.

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) amewafutia mashtaka na kuwaachia huru washtakiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wa...
25/11/2025

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) amewafutia mashtaka na kuwaachia huru washtakiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhaini katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, huku mfanyabiashara wa vipodozi Jenifer Jovin maarufu kwa jina la Niffer, pamoja na ndugu Mika Lucas Chavala wakirudishwa rumande kutokana na kutofutiwa mashtaka hayo.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GADI TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to GADI TV:

Share