GADI TV

GADI TV GADI TV ni televisheni ya Mtandaoni ambayo inajihusisha na kutoa maudhui ya Kijamii na Kisiasa.

"Vunjo tutatafuta namna gani tutakavyo komboa mtu mmoja mmoja hasa kwenye suala la ajira, elimu na mikopo mbalimbali ina...
01/08/2025

"Vunjo tutatafuta namna gani tutakavyo komboa mtu mmoja mmoja hasa kwenye suala la ajira, elimu na mikopo mbalimbali inayotolewa na halmashauri zetu, inahitaji mtu makini wakufuatilia, mniamini mimi Prosper Daudi Tesha ninatosha kwenye nafasi ya ubunge...
..mimi nipo tayari kuwatumikia na nipo tayari kutumwa, wazee hampaswi kuhangaika tena, sasa hivi mnapaswa mtulie mnitume mimi kijana wenu niwatumikie." Mjumbe wa Mkutano Mkuu CCM Taifa, Mkurugenzi wa Kampuni ya RGI na Mwenyekiti wa madini ya vito Taifa (FEMATA), Ndugu Prosper Daudi Tesha akizungumza mbele ya wajumbe wa CCM katika Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro Agosti 01, 2025.

Siku chache baada ya msanii wa vichekesho nchini, Anastanzia Mahatane maarufu k**a Ebitoke (27), kudai kuwa yupo mkoani ...
01/08/2025

Siku chache baada ya msanii wa vichekesho nchini, Anastanzia Mahatane maarufu k**a Ebitoke (27), kudai kuwa yupo mkoani Mtwara akieleza kuwa iwapo k**a atakuwa ametekwa au kuuawa rafiki yake ndiye atakuwa amehusika, Jeshi la Polisi mkoani humo limesema Ebitoke amechanganyikiwa kutokana na maisha yake kumuendea vibaya.

"Ebitoke alipatikana Julai 31, 2025 majira ya saa 11:00 jioni akiwa katika fukwe za Msanga Mkuu akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa na hakuwa ametekwa wala kutumbukizwa shimoni k**a alivyodai awali...
..uchunguzi wa awali, umebaini kwamba ndugu Anastanzia Mahatane alifika mkoani Mtwara tangu April 2025 na kufika katika hotel moja iliyopo Msanga Mkuu na kuomba hifadhi kwa watu waliokuwa wanafahamiana kabla ya maisha yake kumuendea vibaya huko alipokuwa." Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara Issa Suleiman.

Aidha, Jeshi la Polisi limeeleza kuwa kwa sasa msanii huyo anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara na limewaomba ndugu na jamaa zake kufika mkoani humo kwa ajili ya kumsaidia au kumchukua.

Ikumbukwe kuwa Julai 30, 2025 Ebitoke alichapisha taarifa kwenye ukurasa wake wa Instagram akidai kuwa kwa sasa yupo mkoani Mtwara na ikiwa atauawa au kutekwa basi atakaye kuwa amehusika ni rafiki yake.

"Nafasi tunayo iomba ni nzito sana na ni muhimu sana, kwa lugha nyepesi tunaweza kusema ni wakati sahihi kupata mtu wa a...
01/08/2025

"Nafasi tunayo iomba ni nzito sana na ni muhimu sana, kwa lugha nyepesi tunaweza kusema ni wakati sahihi kupata mtu wa aina yangu ili tufukie yale mabonde yaliyokuwepo na kuifanya Arusha yetu ibaki nyuma kwa miaka mingi...
..nyinyi ni mashahidi kazi nilizozifanya katika mkoa wetu na huo ni mwaka mmoja muulize jirani yako akija miaka mitano itakuwaje?." Ndug, Paul Makonda akinadi sera zake mbele ya wajumbe wa CCM katika kata ya Olasiti Jijini Arusha Aug 01, 2025.

01/08/2025

Mjumbe wa Mkutano Mkuu CCM Taifa , Mkurugenzi wa Kampuni ya R-GI na Mwenyekiti wa Madini ya Vito Taifa (FEMATA), Prosper Daudi Tesha, akiomba kura za maoni kutoka kwa wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, ili kupata ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu.

"Mimi mnanifahamu na nimeacha kazi ili mnipe kazi, kwasababu kazi niliyoiomba naijua na naiweza, sasa nimewaza mambo hay...
01/08/2025

"Mimi mnanifahamu na nimeacha kazi ili mnipe kazi, kwasababu kazi niliyoiomba naijua na naiweza, sasa nimewaza mambo haya unapokwenda kupiga kura za maoni, nikiwa mimi ndiye uliye niwekea alama ya tiki jua uchaguzi mkuu wa Octoba 29 wewe utabadilika kuwa wakala wa CCM, najua mnafahamu kazi ya wakala wenye D mbili mmeelewa...
..lakini jambo la pili mimi utakaye nipigia kura za maoni nikateuliwa na chama chetu cha CCM kupeperusha bendera, nikawa Mbunge wa Jimbo, nitaweka utaratibu wa kila mwaka kuweka mkutano mkuu wa kuwaeleza nini nimefanya kwa mwaka huo." Ndug, Paul Makonda akinadi sera zake mbele ya wajumbe wa CCM katika kata ya Sokoni One Jijini Arusha Julai 31, 2025.

"Uongozi ni mbio za kupokezana kijiti kwahiyo wale ambao hawajateuliwa tunawaomba wawe na uvumilivu, waendelee kuwa wana...
31/07/2025

"Uongozi ni mbio za kupokezana kijiti kwahiyo wale ambao hawajateuliwa tunawaomba wawe na uvumilivu, waendelee kuwa wanachama watiifu wa CCM na wasiingie katika vishawishi vyovyote vile vinavyoweza kutia dosari uaminifu wao kwa Chama chetu...
..wale [Watia nia] walioachwa waamini kwamba kuna kesho, wale wote waliokuwa na ndoto watulie tu, wajue nchi ina wasomi wengi, sio lazima uwe wewe, wenzako wakipata watakie kila la kheri." Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Ally Hapi akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma Julai 31, 2025.

"Niliona watu walipoona Ridhiwani kapita bila kupingwa wakasema oh unajua hakuna demokrasia, hata uchaguzi uliopita haku...
31/07/2025

"Niliona watu walipoona Ridhiwani kapita bila kupingwa wakasema oh unajua hakuna demokrasia, hata uchaguzi uliopita hakua na mpinzani ndani ya CCM...
..na kabla ya hapo, hata ule uchaguzi mwingine hakuwa na mpinzani pia kwahiyo unashangaa safari hii?." Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa uzinduzi wa Usafirishaji wa Mizigo kwa SGR Kwala mkoani Pwani Julai 31, 2025.

31/07/2025

Mkurugenzi wa Kampuni ya R-GI na Mwenyekiti wa Madini ya Vito Taifa (FEMATA), Prosper Daudi Tesha, akiomba kura za maoni kutoka kwa wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, ili kupata ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu.

"Chama cha Mapinduzi ambacho mimi ni mwanachama na kiongozi wake, kimetoa maamuzi tuyapokee na kuyakubali.....tushirikia...
30/07/2025

"Chama cha Mapinduzi ambacho mimi ni mwanachama na kiongozi wake, kimetoa maamuzi tuyapokee na kuyakubali...
..tushirikiane na viongozi wetu, kuhakikisha kwamba utaratibu utakaotumika unakwenda vizuri...
..kwasababu ukivurugika inaweza ikajengeka dhana kwamba mbunge alikuwepo amenuna akavuruga mambo." Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye hajateuliwa na CCM kugombea nafasi hiyo kwa awamu nyingine January Makamba.

"Mtoto wangu alienda kwa jirani kucheza na mwenzie, baada ya muda kidogo nikamtuma kaka yake akamlete aje alale, kaka ya...
29/07/2025

"Mtoto wangu alienda kwa jirani kucheza na mwenzie, baada ya muda kidogo nikamtuma kaka yake akamlete aje alale, kaka yake akaja akaniambia kuwa Michelle hataki kuja amesema anabaki kwa dada wa jirani...
..basi nikaenda mwenyewe huko kwa huyo dada nikamkuta anawalisha chakula watoto wake na wakwangu, basi mtoto wa huyo dada wa jirani akamwambia mama yake nataka niende nje nikakojoe...
..alivyosema hivyo na mtoto wangu nae akataka atoke nje, basi wakatoka wote, kwahiyo mtoto wangu alivyotoka ndio hakurudi tena." Lucia Mboya Mama mzazi wa mtoto Michelle Amani (2) ambaye alipotea katika mazingira tata Julai 26, 2025 na kisha mwili wake ukakutwa mtoni akiwa amefariki Julai 27, 2025 katika kata ya Sinoni Jijini Arusha.

29/07/2025

Ni mama mzazi wa Neema Mwakalukwa akiwa anaangua kilio mbele ya jeneza la mwanae ambaye Julai 24, 2025 alikutwa amefariki dunia katika nyumba ya kulala wageni iliyopo kata ya Murieti Jijini Arusha.

Neema ambaye awali alitambulika kwa jina Precious, Inadaiwa alikutwa chumbani akiwa amefariki dunia huku mwanaume aliyeingia naye katika chumba hicho akiwa haonekani.

Aidha, Inaelezwa kuwa Neema alikuwa ni mfanyakazi wa nyumba hiyo na hakuwa na muda mrefu toka aanze kazi katika nyumba hiyo kwa lengo la kufanikisha kuwalisha watoto wake watatu.

Mkurugenzi wa Kampuni ya R-GI na Mwenyekiti wa Madini ya Vito Taifa (FEMATA), Prosper Daudi Tesha ameteuliwa na CCM kugo...
29/07/2025

Mkurugenzi wa Kampuni ya R-GI na Mwenyekiti wa Madini ya Vito Taifa (FEMATA), Prosper Daudi Tesha ameteuliwa na CCM kugombea nafasi ya ubunge katika Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GADI TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to GADI TV:

Share