GADI TV

GADI TV GADI TV ni televisheni ya Mtandaoni ambayo inajihusisha na kutoa maudhui ya Kijamii na Kisiasa.
(2)

"Kuna kipindi nilipotea hapa mjini nikiwa mkuu wa mkoa [wa Arusha], na nikaanza kutafutwa, na wengine mlinitafuta kwa ng...
21/09/2025

"Kuna kipindi nilipotea hapa mjini nikiwa mkuu wa mkoa [wa Arusha], na nikaanza kutafutwa, na wengine mlinitafuta kwa nguvu kubwa, ukweli nilikuwa naumwa, nililishwa sumu, yasingekuwa maombi ya Watanzania na Mungu kumuinua Rais Dkt. Samia Suluhu Haasan kusimamia matibabu yangu, nilitakiwa nife mwaka jana...
..ninapokuja mbele yenu kwa unyenyekevu mkubwa nikiwambia nahitaji maombi, mengine sina nafasi yakuyaeleza, lakini wako watu walitamani kuondoa uhai wangu katika nyakati tofauti tofautiā€ Mgombea Ubunge jimbo la Arusha Mjini (CCM), ndugu Paul Makonda akizungumza kwenye ukumbi wa Huduma ya Mbingu Duniani, Septemba 21, 2025.

21/09/2025

Kufuatia tukio la mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Veronica Muhale (40) mkazi wa Kitongoji cha Maweni kata Endagaw wilaya ya Hanang mkoani Manyara, kudaiwa amemkata mume wake uume usiku, na kisha kuutupa nje ya nyumba yao kwa tuhuma za wivu wa kimapenzi, hatimaye mapya yameibuka kuwa mwanamke huyo aliwahi kufanya jaribio la kutaka kumuua mumewe kwa sumu, lakini mpango huo ukashindikana.

Inaelezwa kuwa mwezi Julai, 2025, Mwanamke huyo aliagiza sumu ya panya na baadae akapanga jaribio la siri la kutaka kumuua mwanaume huyo kwa kutumia sumu hiyo, lakini mmoja wa watoto wa baba huyo, alishtukia mpango huo na kumnusuru baba yake na kifo.

Aidha, inaelezwa kuwa baada ya jaribio hilo kushindikana, mwanamke huyo alinunua kisu kipya na kukiweka chini godoro, na ilipofika Septemba 19, 2025, ndipo akatenda tukio hilo ambalo limemuacha mume wake na ulemavu wakudumu akibakia bila uume.

Kwa mujibu wa viongozi wa eneo hilo wamesema kuwa baada ya kukuta uume huo nje ya nyumba ya mwaume huyo waliuweka kwenye chombo na kuingiza ndani, na kisha kumchukua mhanga huyo na kumpeleka Hospitali ya mkoa wa Manyara kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa baada ya mwanamke huyo kutenda tukio hilo, alikimbilia mikononi mwa Jeshi la polisi.

Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Veronica Muhale (40) mkazi wa Kitongoji cha Maweni kata Endagaw wilaya ya Hanan...
20/09/2025

Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Veronica Muhale (40) mkazi wa Kitongoji cha Maweni kata Endagaw wilaya ya Hanang mkoani Manyara, anadaiwa amemkata mume wake uume usiku, na kisha kuutupa nje ya nyumba yao, kisa wivu wa kimapenzi.

Inaelezwa kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Septemba 19, 2025 wilayani humo, ambapo mara baada ya mwanamke huyo kutenda tukio hilo inadaiwa alijisalimisha mikononi mwa polisi, na mumewe kukimbizwa Hospitali ya mkoa wa Manyara kwa matibabu zaidi.

"Nikweli uume wake ulikatwa, niliukuta umetupwa hapa nje, kiungo hiki tukakiweka kwenye chombo, tukarudisha ndani" Mwenyekiti wa kitongoji cha Maweni, ndugu Mohamed Ramadhani.

"Niwatoe hofu kwamba tarehe zile zakupiga kura hakutakuwa na vurugu yoyote, tokeni kwa wingi kapigeni kura, vyombo vya u...
20/09/2025

"Niwatoe hofu kwamba tarehe zile zakupiga kura hakutakuwa na vurugu yoyote, tokeni kwa wingi kapigeni kura, vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga vyema kuilinda nchi hii, na mimi ndio Amiri Jeshi Mkuu ninayesema hapa...
..tumejipanga vyema kuilinda nchi hii, kwa hiyo hakutakuwa na nywinywi wala nywinywinywi" Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na wananchi wa Pemba, Septemba 20, 2025.

Pichani ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ndugu Paul Makonda, akiwa ana...
20/09/2025

Pichani ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ndugu Paul Makonda, akiwa anamuombea Muumini wa Huduma ya Radio Safina, mara baada ya kushiriki ibada iliyofanyika Septemba 20, 2025, katika ukumbi wa Huduma hiyo mkoani humo.

Mbali na Maombezi hayo, Makonda amesema niya yake yakugombea Ubunge katika Jimbo la Arusha Mjini, nikuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo k**a sehemu ya kutimiza kusudi la Mungu lililopo ndani yake.

20/09/2025

Mwanaume anayefahamika kwa jina la Lucas Kaaya mkazi wa kata ya King'ori wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, amedai kuwa ameacha ajira iliyokuwa ikimpa mshahara wa shilingi milioni nne kwa mwezi na kwenda kugombea nafasi udiwani, lengo lake likiwa nikutaka kuhudumia Jamii kwa ukubwa ukilinganisha na elimu yake ya Shahada ya uzamili ya Uhasibu maarufu k**a Masters.

Kaaya akizungumza na GADI TV akiwa wilayani humo, amesema ameona elimu yake isiishie kuhudumia familia yake pekee, badala yake itumike kuhudumia jamii kubwa kulingana na ukubwa wa elimu hiyo ambayo ilitokana na watu maskini kujichanga kifedha na kumsomesha hadi kufikia alipo kwasasa.

"Watekaji walinipigia simu kwamba unamfahamu mtu fulani ambaye ni mtoto wangu, nikasema namfahamu, [wakasema] tumemchuku...
18/09/2025

"Watekaji walinipigia simu kwamba unamfahamu mtu fulani ambaye ni mtoto wangu, nikasema namfahamu, [wakasema] tumemchukua huyu binti tunaelekea naye maeneo ya kuelekea Tabora, nikasema tatizo ni nini?, wakaniambia watatoa taarifa baadae...
..baadae wakatoa taarifa kwamba wanahitaji kiasi fulani cha pesa, baada ya hapo wakanirushia Clip ya video ya mateso ya mtoto wangu, basi ilinipelekea kuwapatia kiasi kidogo cha pesa ili angalau mtoto apunguziwe maumivu" Dkt. Mabula Mahande akielezea jinsi aliyopigiwa simu na watu waliokuwa wamemteka binti yake aitwae Shyrose Mahande (21), ambapo inadaiwa baada ya simu hiyo aliuawa na kuchomwa moto huko mkoani Mbeya.

Inaelezwa kuwa, Shyrose alikuwa Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Mzumbe ndaki ya Mbeya kitivo cha sheria.

Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya, limesema linaendelea na uchunguzi wa kina na wakisayansi kuwabaini wahusika wa tukio hilo.

16/09/2025

Wanafunzi wawili ambao niwahitimu wa darasa la saba katika shule msingi maarufu kwa jina la Tengeru English Medium iliyopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, inadaiwa wamewekewa kizuizi kuwa hawaruhusiwi kuondoka eneo la shule hiyo, hadi wazazi wao wamalizie kulipa ada wanayodaiwa.

Wanafunzi hao wawili kati ya wanafunzi 36 waliohitimu Septemba 11, 2025 katika shule hiyo, inaelezwa kuwa waliwekewa kuzuizi hicho na uongozi wa shule hiyo hadi wazazi wao watakapo kamilisha kuwalipia ada zao, mmoja akiwa anadaiwa shilingi milioni moja na laki moja na mwingine shilingi laki nane.

Aidha, Inaelezwa kuwa wanafunzi hao ambao ni jinsia mbili tofauti, wamekuwa wakiishi kwa kula chakula kinacholetwa na wazazi wao wakati wakiwa kizuizini hapo.

Ikumbukwe kuwa, shule hiyo kwasasa ipo kwenye maandalizi ya kubadilishiwa jina, ndio maana unaona jina tofauti katika geti lao.

13/09/2025

Mfanyabiashara anayeuza Popkoni anayefahamika kwa jina la Gasper Kitomary mkazi wa wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, amedai kuwa anaingiza faida ya shilingi elfu 50 kwa siku kupitia biashara hiyo, baada ya kuitengenezea mtaji kwenye ajira aliyokuwa akifanya na kulipwa elfu 70 kwa mwezi.

Gasper akizungumza na GADI TV amesema kupitia mshahara wa shilingi elfu 70 aliokuwa akilipwa kwa mwezi, aliamua kudunduliza hadi akanunua mashine yakutengeneza Popkoni yenye thamani ya shilingi milioni mbili na laki sita, na kupitia mashine hiyo ikafanikiwa kuleta mashine zingine tano kwa ajili ya shughuli hiyo.

Aidha, Gasper amesema kupitia kazi hiyo amefanikiwa kumsomesha ndugu yake ambaye kwasasa ni Injinia wa masuala ya umeme, hatua hiyo ikiwa ni njia mojawapo ya kuisaidia familia yake iliyokuwa katika lindi la umaskini.

Kadhalika, Gasper amesema kwasasa anawafanyakazi 11 ambao wanamtegemea kwa kila kitu, na kupitia biashara hiyo anaweza kuwalipa mishahara na kubakia na faida ya shilingi elfu 50 kwa siku.

"Leo mmetuhumu yule kijana [ameiba parachichi], ameuliwa, anajitetea wapi?, hivi unalizwa na Mungu, ehee umemuua kwasaba...
13/09/2025

"Leo mmetuhumu yule kijana [ameiba parachichi], ameuliwa, anajitetea wapi?, hivi unalizwa na Mungu, ehee umemuua kwasababu gani?, parachichi, kweli parachichi la mia mbili likachukua uhai wa mtu, hakuna mali wala chochote ambacho kinalingana na uhai wa binadamu...
..serikali haitochekea vitendo vya kihuni vya namna hii, hawa [watu saba] tumewak**ata tutawafikisha Mahak**ani" Kauli ya Mkuu wa mkoa wa Iringa ndugu Kheri James aliyoitoa Septemba 13, 2025, akiwa nyumbani kwa kijana aliyeuawa kwa madai kuwa ameiba parachichi mkoani humo.

Waandishi wa habari wawili waliokuwa wanashikiliwa kwa siku saba na jeshi la polisi mkoa wa Arusha kwa tuhuma za kuendes...
12/09/2025

Waandishi wa habari wawili waliokuwa wanashikiliwa kwa siku saba na jeshi la polisi mkoa wa Arusha kwa tuhuma za kuendesha televisheni za mtandaoni zisizokuwa na leseni, hatimaye leo Septemba 12, 2025, wameachiwa kwa dhamana.

Waandishi hao ni Baraka Lucas (kushoto) anayehudumu kwenye televisheni ya mtandaoni inayofahamika kwa jina la JAMBO TV pamoja na Ezekiel Mollel (kulia) anayehudumu Manara TV.

Kwa umoja, Waandishi wa habari mkoa wa Arusha, wametoa shukrani kwa Viongozi wao pamoja na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kinacho ongozwa na Rais, Wakili Boniface Mwabukusi, kwa namna walivyoshirikiana na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDS), kuhakikisha waandishi hao wanapata dhamana kwa mujibu wa sheria.

09/09/2025

Mzee mmoja anayefahamika kwa jina la Daniel Mbwambo mkazi wa Bondeni kati kata ya Terati Jijini Arusha, anadaiwa amemuua mke wake, ikiwa ni siku chache zimepita tangu apatanishwe naye na kuchoma baadhi ya vitu vinavyotajwa kuwa nivya kiganga Jijini humo.

Mashuhuda wa tukio hilo wakizungumza na GADI TV wamesema Septemba 7, 2025, majira saa tano usiku, mzee huyo alisikika akiwaita majirani kwa sauti ya juu akiwa amesimama nje ya nyumba yake, na mara baada ya majirani kufika eneo hilo aliingia ndani ya nyumba yake na kujifungia, na kutoa kauli kuwa anaomba aitishiwe Jeshi la polisi, huku wakati huo damu zikiwa zinatoka chini ya mlango wa nyumba hiyo.

Kwa mujibu wa mashuhuda, wawili hao walikuwa hawaishi pamoja kwa zaidi ya miaka miwili lakini kwa kipindi cha mwezi mmoja mwanamke huyo alionekana amerejea nyumbani kwa mzee huyo na baadae tukio hilo likatokea.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GADI TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to GADI TV:

Share