Time TV.

Time TV. Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Time TV., TV Channel, Arusha.

18/07/2025

Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba Humphrey Polepole ametoa wito kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi kutokukalia kimya matukio ya aina yoyote ya uvunjifu wa haki za wengine kwani yatahatarisha amani na kupunguza imani ya chama hicho kwa wananchi.

Polepole ameyasema hayo leo Julai 18, 2025 katika mkutano wake anaoufanya na waandishi wa habari kwa kutumia mitandao.

“kuhusu haki kwanza CCM msione aibu kuzungumza kuhusu haki huwezi kupata amani bila haki, inaanza haki halafu inakuja amani na msingi wa uongozi wa CCM ni kuheshimika watu na haki” amesema Polepole

Hata hivyo ameongeza akisema “haki ni muhimu haki za watu wetu na haipendezi kuona watu wanapokwa haki zao na chama kimekaa kimya haikubaliki kabisa”

18/07/2025

Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, amesema kuwa anapinga vikali vitendo vya utekaji na kudai kuwa dada yake alitekwa.

Kauli hiyo ameitoa kupitia video ya moja kwa moja (live) aliyoirusha kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, akigusia pia masuala ya kisiasa na mwenendo wa chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika video hiyo, Polepole amesema tukio la utekaji wa dada yake limeacha doa la kihisia kwake binafsi na ni sehemu ya sababu zinazomfanya kuwa na msimamo mkali dhidi ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Aidha, Polepole ambaye pia ni kada wa muda mrefu wa CCM, ameeleza kutoridhishwa kwake na namna baadhi ya masuala yanavyoendeshwa ndani ya chama hicho, akisema kuwa ni muda wa kujitathmini na kusikiliza sauti ya wananchi.

Kwa upande mwingine, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amethibitisha kupokea taarifa kutoka kwa dada wa Polepole kuhusu tukio hilo, akisema kuwa jalada la uchunguzi lilifunguliwa mara baada ya kupokea malalamiko hayo.

18/07/2025

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeeleza kuwa limepokea taarifa za kutekwa na kurejeshwa kwa mwanamke aliyejitambulika kwa jina la Christina Hezroni Polepole Kinyangazi, mwenye umri wa miaka 52, mkazi wa Bahari Beach, Mtaa wa Kitumba, Kinondoni.

18/07/2025

Kupitia ukurasa wake wa Instagram saa sita usiku Julai 18, 2025 Humprey Polepole ameandika, "Watu wameruka ukuta wa nyumbani kwa dada yangu Bahari Beach wamemwambia dada yangu wamefuata taarifa. Ninakwenda kujiridhisha. Sina tatizo kabisa, nilishamwambia Mungu wa Mbinguni na anajua nina yeye tu."

17/07/2025

Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amefunguka kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Mwaka 2050.

Pia ameuliuzwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wake juu ya No Reform No Election ambapo haya ndiyo yalikuwa majibu yake.

17/07/2025

Mwenyekiti Mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe amesema licha ya Serikali kufanya kazi kubwa kuandaa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, lakini bado haijakiri kuhusu demokrasia na ‘mabaya’ yaliyotokea miaka 25 iliyopita.

Akizungumza na wanahabari katika viunga vya Jakaya Kikwete Jijini Dodoma, Mbowe amesema Dira hiyo imetaja mafanikio katika demokrasia ikiwemo uchaguzi huru na haki, jambo ambalo sio kweli na alitegemea serikali ingeweza kukiri makosa kupitia Dira hiyo na kuanza ukurasa mpya.

17/07/2025

Tunapozindua dira 2050, tujielekeze katika vitendo zaidi kuliko maneno. Wazee wetu walisema lisilobudi hutendwa, hawakusema lisilobudi husemwa. Sasa tuna tabia ya kusema sana kuliko kutenda. Na mtu wa sekta binafsi alilitupa kwetu serikalini lakini hii ni tabia ya Watanzania sote. Kwa hiyo sasa serikali, sekta binafsi wananchi tutende zaidi kuliko kusema,” Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

17/07/2025

Sijui Mbowe alimdanganya nini Kitila akaenda CHADEMA - Dkt. Kikwete

16/07/2025

Mhe. alivyofikishwa na kuondolewa katika Mahak**a Kuu Kanda ya Dar es salaam leo tarehe 16 Julai 2025.

16/07/2025

Leo Julai 16, 2025 shauri la Maombi ya Merejeo lililofunguliwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu limeahirishwa mpaka tarehe 12/08/2025.

Lissu anaiomba mahak**a itamke kwamba siku 09/06/2025(kwenye shauri namba 8606/2025 la kuchapisha taarifa za uongo) Hakimu Mfawidhi Geoffrey Mhini alitoa maamuzi ya upande mmoja ya kuruhusu upande wa jamhuri kuleta baadhi ya mashahidi ambao sio askari kutoa ushahidi kwa siri.

Upande wa Jamhuri uliwasilisha viapo ambavyo vimesainiwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kingine kilisainiwa na SACP Faustine Mafwele vikieleza kuwa mashahidi ambao sio askari watoe ushahidi wa kificho kutokana na kile kilichodaiwa kuwa hofu juu ya usalama wao kwani wamekuwa wakitishiwa na wafuasi wa Lissu.

Hata hivyo leo Lissu aliingizwa katika chumba cha mahak**a majira ya saa nne na robo ambapo uliibuka mzozo baina yake, Mawakili wake na Askari Magereza kwa kile alichodai Lissu kuwa ni Askari Magereza kutaka kuchukua baadhi ya nyaraka zake jambo ambalo aliwataka mawakili wake wakiongoza na Wakili Mwandamizi Mpale Mpoki kuiambia mahak**a itolee ufafanuzi k**a jambo hilo ni sahihi au lah.

Mawakili wa Lissu waliwasilisha jambo hilo mbele ya Jaji Elizabeth Mkwizu wakitoa vifungu mbalimbali vya kisheria juu ya haki za mfungwa na upande wa Jamhuri ukaieleza mahak**a juu ya uhalali wa askari hao kuhitaji kuchukua na kukagua nyaraka ili kuhakikisha usalama kwani Lissu kwa sasa ni mtuhumiwa katika kesi ya uhaini hivyo anahitaji kuwa na ulinzi.

Jaji Mkwizu baada ya kusikiliza hoja za pande zote amesema atatoa uamuzi wa malalamiko ya Lissu ya kutokutendewa haki na yale maombi ya kupinga uamuzi wa mashahidi wa kificho.

16/07/2025

"Mnajua vyema kwamba Chadema wamesema hawaingii kwenye uchaguzi mpaka tufanye Reforms na modality yao wanayoisema, wanasema watazuia uchaguzi. Nataka nitoa ushauri kwa unyenyekevu sana, ni kweli Sisi CCM tunaweza kuamua kuendelea na uchaguzi na tukafanya uchaguzi na tukashinda lakini kushinda uchaguzi sio jambo kubwa sana, kuitawala nchi ambayo imemegukameguka kwasababu ha makovu ya uchaguzi ndiyo jambo kubwa zaidi, kuiletea nchi maendeleo iliyomeguka kutokana na makovu na majeraha ya uchaguzi ni kazi ngumu sana.

Sisi k**a CCM tunaweza kuamua kwamba tuendelee- tutaendelea na tutashinda. Lakini ebu jaribu kuwaza tangu siku unapoapishwa kuna watu wanaendelea kukupinga mpaka utakapomaliza miaka yako mitano, yaani kuna watu hawakuingia kwenye uchaguzi, hawakushiriki, pengine hawakutambui halafu wanaanza kukupinga tangu siku unapoapishwa mpaka utakapotoka miaka mitano. Maendeleo utayaletaje? Utapata matatizo na Jumuiya za kimataifa na ndani ya nje utapata matatizo utashindwa kwenda kwa kasi kwa maendeleo yetu k**a inavyotakiwa na itakuwa sio vizuri.

Mimi nashauri kwamba, CCM ina wanachama zaidi ya milioni kumi na kitu, hatuhitaji kuogopa, tuamue kuwaruhusu hawa wa Chadema kuwapa reforms chache ambazo zinaweza kufanyika kwasasa, tuwape a minimal reform, haichukui muda. Tuwape, tuingie nao kwenye uchaguzi. Kwani wewe hufahamu kwamba CCM ina wanachama zaidi ya Milioni kumi na kitu?ambao wapo tayari? kwanini tuingine kwenye mchezo halafu tunayecheza naye hayumo? Ni sawasawa na kuingia kwenye mechi huku kuna Simba, huko inatakiwa iwe Yanga, halafu Yanga haipo, tunacheza wenyewe halafu tunapiga goli, si mechi.

Nashauri sana badala ya kuendelea na No Reforms, No election, CCM awepo mtu wa kutafakari. Mimi k**a mwanachama wa CCM na k**a Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM na pia Mtanzania, nashauri sana tungeamua kukubali kufanya hiyo reforms, najua shughuli za Bunge zimesitishwa lakini uhai wa Bunge bado upo mpaka mwezi wa nane, zitafutwe wiki mbili au tatu, zitengenezwe reforms wanazozihitaji hata k**a sio zote, lakini ziwe chache zitakazowafanya waingie kwenye uchaguzi halafu waingie tuwapige, reforms zimefanyika, wameingia, tunawapiga."-Askofu Josephat Gwajima

16/07/2025

Gwajima aunga mkono kuhusi hoja wanayo idai CHADEMA ya kuhutaji Reforms kufanyika illi waingie kushiriki uchaguzi

Address

Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Time TV. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category