Radio5tz

Radio5tz Radio 5 is one of Tanzania's most popular Swahili speaking radio station, broadcasting news and entertainment

News segment comprises of accurate; soft and hard local, international and national news. Entertainment segment encompasses Blues, Afro vibes and R&B, of both local (African) and international flavors that provide a rare source of relaxation in the hectic world we live in.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt.Hussein Ali Mwinyi, amehimiza kuimarishwa kwa diplomasia...
09/09/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt.
Hussein Ali Mwinyi, amehimiza kuimarishwa kwa diplomasia ya uchumi baina ya Zanzibar na Japan.

Akizungumza Ikulu Zanzibar leo tarehe, 9 Septemba, 2025 na Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mhe. Anderson Gukwi Mutatembwa, Dkt.
Mwinyi alisema Japan ina wawekezaji wengi ambao Zanzibar inawakaribisha kuwekeza hususan katika uchumi wa buluu, biashara ya mwani, utalii, michezo, mafuta na gesi.

Aidha, alibainisha kuwa Zanzibar inalenga kuanzisha viwanda vya kuzalisha bidhaa za baharini na hivyo ni muhimu kuvutia wawekezaji zaidi kutoka Japan.

Kwa upande wake, Balozi Mutatembwa alimhakikishia Rais Dkt. Mwinyi kuweka mkazo katika kusimamia ushirikiano wa kiuchumi na miradi ya maendeleo kati ya Japan na Tanzania, ikiwemo Zanzibar.

Tanzania imeona tukio la kupatwa kwa Mwezi kwa sehemu na kikamilifu leo, Septemba 7, 2025, tukio litakalodumu takriban m...
07/09/2025

Tanzania imeona tukio la kupatwa kwa Mwezi kwa sehemu na kikamilifu leo, Septemba 7, 2025, tukio litakalodumu takriban masaa sita na kuwa la kwanza kujitokeza tangu mwaka 2022 kwa namna ya pekee . TMA ilitoa muongozo wa awamu na muda wake, huku tukio likiwa na umuhimu mkubwa wa kisayansi na kwa umma.

Tunawatakia Mawlid njema Waislamu wote Mwenyezi Mungu alete kheri, amani na baraka katika maisha yenu.
05/09/2025

Tunawatakia Mawlid njema Waislamu wote Mwenyezi Mungu alete kheri, amani na baraka katika maisha yenu.

Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Ngarenaro iliyopo Jijini Arusha Bw. M***a Lu...
03/09/2025

Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Ngarenaro iliyopo Jijini Arusha Bw. M***a Luambano (50) na mlinzi wa Shule hiyo Bw. Olais Mollel (33) kwa tuhuma za ukatili dhidi ya mwanafunzi wa darasa la saba (jina limehifadhiwa) mwenye umri wa miaka 13.

Akitoa taarifa hiyo leo Septemba 03, 2025 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Justine Masejo amesema watuhumiwa hao kwa kutumia mnyororo Septemba 01, 2025 waliufunga mguu wa mwanafunzi huyo kwenye dawati na kisha kumfungia ndani ya chumba cha darasa kwa madai ya kuwa ni mtoro.

Aidha, amebainisha kuwa wanaendelea kukamilisha upelelezi wa tukio hilo na pindi utakapokamilika taratibu nyingine za kisheria zitafuata.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limetoa wito kwa wananchi kuendelea kufichua matukio ya uhalifu katika jamii ili waendelee kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria dhidi ya wote watakaobainika.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limetoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa katika baadhi ya mitandao ya kijamii ikielez...
30/08/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limetoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa katika baadhi ya mitandao ya kijamii ikieleza kuwa Bw. Gasper Temba (30) ametekwa Jijini Arusha.

Akifafanua tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema kuwa taarifa sahihi ni kwamba Bw. Gapser Temba ambaye ni mkazi wa Arusha hajatekwa, bali amek**atwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma zinazomkabili za kughushi Nyaraka.

SACP Masejo amebainisha kuwa tukio hilo llilifunguliwa huko Jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa amek**atwa kwa mujibu wa sheria na taratibu nyingine za kisheria zinafuata.

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limetoa onyo kwa watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuacha kusambaza taarifa ambazo hawana uhakika zinazoweza kusababisha taharuki katika jamii.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Justine Masejo, amewataka wanachama wa M...
28/08/2025

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Justine Masejo, amewataka wanachama wa Mtandao wa Polisi Wanawake (TPF NET) mkoani humo kufanya kazi kwa nidhamu, kujiamini na kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo, hususan kutokana na nafasi ya Arusha k**a kitovu cha utalii na miradi mikubwa ya serikali.

Akifungua mafunzo ya mtandao huo Agosti 28, 2025, Kamanda Masejo aliwahimiza wanachama kutumia mafunzo hayo kuboresha utendaji wao na maisha binafsi, huku akiwapongeza kwa mchango wao katika jamii kupitia misaada na elimu dhidi ya ukatili.

Naye Mwenyekiti wa TPF NET Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Debora Lukololo, alisema washiriki wanapata elimu kuhusu ujasiriamali, afya ya akili, masuala ya uzazi, saratani ya shingo ya kizazi na matiti, elimu ya uchaguzi na huduma za upimaji afya bure.

Mafunzo haya ni maandalizi ya kuelekea TPF NET GALA itakayofanyika Agosti 29, 2025, kwa ajili ya kupongeza mafanikio na kuwaaga wastaafu wa mtandao huo.

28/08/2025

ameshare video akifundishwa kiswahili na kufuatia collabo ya ya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Rais wa Chama cha Wana...
27/08/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, leo tarehe 27 Agosti, 2025.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo, ameteua wajumbe tisa wapya wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maend...
19/08/2025

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo, ameteua wajumbe tisa wapya wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), akiwemo mfanyabiashara maarufu Fred Fabian Ngajiro (Fred Vunjabei). Uteuzi huu umefanyika tarehe 18 Agosti 2025 jijini Dodoma, kwa mujibu wa Sheria ya Maendeleo ya Biashara, Sura ya 55, na kuthibitishwa kupitia taarifa rasmi ya Wizara iliyosainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Bi. Suzan Mshakangoto.

Wajumbe walioteuliwa ni: Fred Fabian Ngajiro (Mfanyabiashara), Ahmed Yussuf Baalway - Baraza la Wawakilishi Zanzibar,
Dkt. Hanifa Yusuf Mohamed – Wizara ya Biashara,
Najma Hussein – Chemba ya Wanawake Wafanyabiashara Zanzibar,Radhia Tambwe – Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Oscar Kisanga – Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA),
Laiton Ernesta – Wizara ya Fedha
Happy Kitingati – Wizara ya Kilimo,
Khamis Ahmada Shauri – Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameshiriki katika Mkutano Mkuu wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Barani Afrika (...
14/08/2025

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameshiriki katika Mkutano Mkuu wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Barani Afrika (AU-AIP Water Investment Summit) unaofanyika Cape Town, Afrika Kusini, akiwa Mwenyekiti Mwenza Msaidizi wa Jopo la Ngazi ya Juu la Programu ya Uwekezaji wa Maji Afrika (AIP).

Mkutano huu, unaoratibiwa na Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini na Jopo la AIP, unalenga kushinikiza ajenda ya uwekezaji wa maji kupewa kipaumbele katika mkutano wa G20 utakaofanyika Novemba 2025, Cape Town. Jopo la AIP linaongozwa na Wenyeviti Wenza watatu: Rais wa Namibia, Rais wa Senegal, na Waziri Mkuu wa Uholanzi, likishirikisha pia viongozi wa Afrika na Morocco.

Mkutano umefunguliwa na Rais wa Afrika Kusini na Mwenyekiti wa G20 kwa mwaka 2025, Mheshimiwa Cyril Ramaphosa, na kuhudhuriwa na viongozi akiwemo Mfalme Mswati III wa Eswatini na Rais wa Botswana, pamoja na wadau wa sekta ya maji.

Aidha, Dkt. Kikwete ameteuliwa kuwa miongoni mwa viongozi wakuu watano wa Baraza la Uwezeshaji wa Uenyekiti wa Afrika Kusini wa G20 kwa mwaka 2025, akihudumu k**a Mwenyekiti Mwenza Msaidizi katika masuala ya maji. Wengine ni Rais wa UAE Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan, Waziri Mkuu wa Barbados Mia Mottley, Bw. Bill Gates, na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waombolezaji kabla ya kuaga mwili ...
10/08/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waombolezaji kabla ya kuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Job Yustino Ndugai katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma leo tarehe 10 Agosti, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwafariji wanafamilia wa Spika Mstaafu wa Bunge...
10/08/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwafariji wanafamilia wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Job Yustino Ndugai katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma tarehe 10 Agosti, 2025.

Address

Njiro Block J
Arusha
P.O.BOX15883

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio5tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio5tz:

Share

Category