Radio5tz

Radio5tz Radio 5 is one of Tanzania's most popular Swahili speaking radio station, broadcasting news and entertainment

News segment comprises of accurate; soft and hard local, international and national news. Entertainment segment encompasses Blues, Afro vibes and R&B, of both local (African) and international flavors that provide a rare source of relaxation in the hectic world we live in.

HUYU NDIYE SEMIO SONYO (UNCLE SONYO) – RADIO 5 FM ARUSHABaada ya kuonekana k**a Miongoni mwa Watangazaji BORA wa mikoani...
13/07/2025

HUYU NDIYE SEMIO SONYO (UNCLE SONYO) – RADIO 5 FM ARUSHA

Baada ya kuonekana k**a Miongoni mwa Watangazaji BORA wa mikoani kupitia Platform ya nina haya yakusema.

Katika anga ya redio nchini Tanzania, vipaji vingi vinaibuka, lakini ni wachache sana wanaoweza kusimama imara kwa muda mrefu na kudhihirisha ubora wa hali ya juu katika utangazaji na uzalishaji wa vipindi. Moja ya majina hayo machache ni Semio Sonyo, anayejulikana zaidi k**a Uncle Sonyo wa Radio 5 FM ya Arusha.

Uncle Sonyo si mtangazaji wa kawaida. Ni kipaji kinachoweza kuibua hisia, kuelimisha, kuburudisha na kuchochea fikra za wasikilizaji kwa wakati mmoja. Kutoka kwenye vipindi vya habari, burudani, michezo hadi vipindi maalum vya kijamii na kitaifa — Sonyo amekuwa akidhihirisha uwezo mkubwa wa kitaaluma na ubunifu wa hali ya juu huyu ni Kiraka (Mult Purpose Presenter).
Ni moja kati ya watangazaji nchini Tanzania wenye uwezo mkubwa katika kufanya Mahojiano katika nyanja zote,Elimu,Siasa,Uchumi Afya Mazingira,Kilimo,michezo na hata Burudani.

Sauti yake ya kuvutia, uchambuzi makini, maandalizi ya kina na namna anavyomiliki hewani ni vitu vinavyomtofautisha. Hata katika mazingira ya ushindani mkubwa, Uncle Sonyo ameendelea kuwa chaguo la wengi, si tu katika Jiji la Arusha, bali pia mikoa mingine na hata wasikilizaji wa mtandaoni kote nchini.

Katika ulimwengu wa redio unaohitaji ubunifu wa kila siku, Sonyo ameweza kudumu kwa ubora usiopungua. Anaeleweka, anakubalika, anaheshimika na zaidi ya yote, anastahili tuzo ya kitaifa, si kwa upendeleo, bali kwa haki inayotokana na kazi yake ya kipekee.

Uncle Sonyo ni alama ya vipaji vya mikoani vinavyostahili kung’ara kitaifa. Ni wakati sasa mchango wake utambuliwe rasmi – kwa jina, kwa kazi, na kwa tuzo.
Ahsante Radio Doctor kwa Jicho makini la kumuona

11/07/2025

Silent Ocean tunakukumbusha wewe mfanyabiasharaumuhimu wa kuagiza mapema na kusafirisha bidhaa zako kabla ya changamoto za biasharaHazijaongezeka. Katika kipindi hiki cha pilikapilika nyingi, kuwa wa kwanza sokoni kuna faida kubwa.Kuwa wa kwanza na SILENT OCEAN, agiza na Safirisha Mapema kuliwahi soko. !

Tunawatakia Watanzania wote heri ya Sikukuu ya Sabasaba!
07/07/2025

Tunawatakia Watanzania wote heri ya Sikukuu ya Sabasaba!

Mtangazaji mwandamizi wa  Yakubu Simba, amejitosa rasmi kwenye mchakato wa kugombea nafasi ya Udiwani kwa kuchukua na ku...
02/07/2025

Mtangazaji mwandamizi wa Yakubu Simba, amejitosa rasmi kwenye mchakato wa kugombea nafasi ya Udiwani kwa kuchukua na kurejesha fomu ya kuwania nafasi hiyo katika Kata ya Daraja Mbili, Jijini Arusha.

Hatua hiyo inaashiria dhamira yake ya kuwatumikia wananchi kupitia uongozi wa kisiasa, akiweka mbele ajenda za maendeleo na ustawi wa jamii. Simba anajiunga na orodha ya wanahabari wachache wanaoamua kutumia uzoefu wao katika kushughulikia changamoto za kijamii kupitia vyombo rasmi vya uongozi.

Kada wa CCM Wilaya ya Rufiji, Shaban Matwebe, ambaye awali alilalamikia kunyimwa fomu ya kuwania ubunge jimbo la rufiji,...
01/07/2025

Kada wa CCM Wilaya ya Rufiji, Shaban Matwebe, ambaye awali alilalamikia kunyimwa fomu ya kuwania ubunge jimbo la rufiji, hatimaye amekabidhiwa rasmi fomu hiyo leo, na kuingia kwenye kinyang’anyiro hicho kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Matwebe amesema licha ya changamoto alizokumbana nazo, ikiwemo kushikiliwa na Polisi na vitendo vya kukatisha tamaa, amedhamiria kusimama imara hadi mwisho kwa mujibu wa taratibu za chama. Anatarajiwa kushindana na Mbunge aliyepo madarakani, Mohamed Mchengerwa, ambaye tayari amechukua fomu ya kutetea nafasi yake.

Mwanahabari na aliyewahi kuwa msemaji wa vilabu vya Simba na Yanga, Haji Manara, amejitosa rasmi kwenye kinyang’anyiro c...
01/07/2025

Mwanahabari na aliyewahi kuwa msemaji wa vilabu vya Simba na Yanga, Haji Manara, amejitosa rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kwa kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Udiwani wa Kata ya Kariakoo, Jimbo la Ilala, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Manara amechukua fomu hiyo wakati zoezi la uchukuaji fomu za kugombea Ubunge na Udiwani kupitia CCM likiendelea nchi nzima, huku watia nia mbalimbali wakiendelea kujitokeza katika ofisi za chama hicho kuwania nafasi za uongozi kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Msomi na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mary Jimmy Malle,amejitosa rasmi katika kinyang’anyiro cha kug...
01/07/2025

Msomi na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mary Jimmy Malle,amejitosa rasmi katika kinyang’anyiro cha kugombea Ubunge wa Viti Maalum Elimu ya Juu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Malle amechukua fomu mapema leo katika ofisi za CCM jijini Arusha.

Zoezi la uchukuaji fomu ndani ya CCM linaendelea kote nchini, huku chama hicho kikitoa wito kwa wanachama wenye sifa, maono na uzalendo kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.

Mwandishi mkongwe wa habari na mtangazaji mahiri, Salim Kikeke, amejiunga rasmi katika mchakato wa kisiasa baada ya kuch...
01/07/2025

Mwandishi mkongwe wa habari na mtangazaji mahiri, Salim Kikeke, amejiunga rasmi katika mchakato wa kisiasa baada ya kuchukua fomu ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Moshi Vijijini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hatua hiyo ya Kikeke imekuja wakati zoezi la uchukuaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia CCM likiendelea kote nchini. Zoezi hilo linahusisha watia nia wa nafasi za Ubunge na Udiwani, ambao wameendelea kujitokeza kwa wingi katika ofisi za chama hicho.

Salim Kikeke, amewahi kufanya kazi na vyombo mbalimbali vya habari ndani na nje ya nchi.

Kwa kuchukua fomu hiyo, Kikeke amejiunga na orodha ya watu mashuhuri wanaojitosa katika siasa, akilenga kuwatumikia wananchi wa Moshi Vijijini kwa kutumia uzoefu na mtazamo mpana alioupata katika nyanja ya mawasiliano na masuala ya kijamii.

Zoezi la uchukuaji fomu linaendelea katika mikoa yote ya Tanzania.

Viongozi mbalimbali Wachukua Fomu za Ubunge Kupitia CCMNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amechuk...
30/06/2025

Viongozi mbalimbali Wachukua Fomu za Ubunge Kupitia CCM

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea tena Ubunge wa Jimbo la Bukombe, kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Bukombe, Leonard Mwakalukwa.

Katika Jimbo la Arumeru Mashariki, aliyewahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo mwaka 2012, Joshua Nassari, naye amechukua fomu Juni 30, 2025, kuwania ubunge kupitia CCM. Nassari pia amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya mbalimbali ikiwemo Monduli na Iramba.

Mrisho Gambo, aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini 2020 2025, amechukua fomu ya kugombea tena jimbo hilo. Gambo pia amewahi kuwa Mkuu wa Mkoa na Wilaya ya Arusha.

Kwa upande wa Viti Maalum, Katibu wa Uchumi na Fedha UVCCM Mkoa wa Kilimanjaro, Comrade Happy J. Shirima, amechukua fomu kuwania nafasi hiyo kupitia CCM.

Zoezi la uchukuaji fomu linaendelea nchi nzima likihusisha watia nia wa nafasi za Ubunge na Udiwani.

🧠 UJUMBE NA MADA YA AFYA YA AKILI –KUPITIA  KIPINDI CHA MORNING TZ  kinachorushwa na Radio FM.Kwa kushirikiana na Mwezes...
11/06/2025

🧠 UJUMBE NA MADA YA AFYA YA AKILI –KUPITIA KIPINDI CHA MORNING TZ kinachorushwa na Radio FM.

Kwa kushirikiana na Mwezeshaji na Daktari wa Afya ya Akili Dr Pascal King’iria na Shirika la chini ya Mradi wa Arusha-re-Innovation.

Habari za leo mwananchi na msikilizaji wa Morning Tz! Kesho tunakuletea ujumbe na elimu muhimu kuhusu afya ya akili, tukiangazia umuhimu wake katika maisha ya kila siku – hususan kwa wazazi,watoto na vijana wetu.

Afya ya akili siyo ukosefu wa magonjwa ya akili tu, bali ni hali ya mtu kuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha, kufanya kazi kwa ufanisi, na kushiriki vyema katika jamii. Katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, tunahimizwa kuwekeza muda na upendo kwa watoto wetu – kuhakikisha wanapata msaada wa kihisia na kijamii unaowajenga kiakili.

Kwa ushirikiano na shirika la SOS Children’s Villages, tunawakumbusha wazazi, walezi na jamii kwa ujumla:
🔹 Sikiliza mtoto wako bila hukumu
🔹 Mpe nafasi ya kuongea kuhusu hisia zake
🔹 Tafuta msaada wa kitaalamu pale unapoona mabadiliko ya kitabia au kihisia
🔹 Fanya mazoezi, kula vizuri, na tenga muda wa kupumzika – haya yote huimarisha afya ya akili

Daktari wetu wa afya ya akili anasisitiza: “Mtoto mwenye afya nzuri ya akili leo ni msingi wa taifa imara kesho.”

Tuungane pamoja kujenga mazingira salama, yenye upendo na msaada wa kiakili kwa watoto wote.

🌱 Afya ya akili ni haki ya kila Mzazi, mtoto ,na Kijana..Tuilinde, tuiheshimu,tuihudumie.

Ongea na jamii nzima kupitia kifungashio hapo chini.. cha jumbe muhimu kuhusu Afya ya Akili.

1.”Afya ya akili ni sehemu ya afya yako yote. Jali akili yako.”

2.”Unapojisikia kulemewa, ni sawa kuomba msaada. Usinyamaze.”

3.”Kuzungumza kuhusu hisia zako ni ishara ya nguvu, si udhaifu.”

5.”Msongo wa mawazo unatibika. Tafuta msaada mapema.”

6.”Afya ya akili huanza na kujipenda. Jitunze.”

7.”Tuchukulie afya ya akili kwa uzito k**a tunavyochukulia afya ya mwili.”

8.”Ni sawa kutokuwa sawa. Hatua ya kwanza ni kukubali.”

9.”Unapohisi huzuni au hofu kupita kiasi, ongea na mtu unayemwamini.”

10.”Tuko pamoja. Hakuna haja ya kupambana peke yako.”

11.”Afya ya akili ni haki ya kila mtu. Usiachwe nyuma.”

🇵🇹 URENO YAANDIKA HISTORIA YATWAA TAJI LA UEFA NATIONS LEAGUE KWA MARA YA PILI!Katika mchezo wa kusisimua uliopigwa jiji...
08/06/2025

🇵🇹 URENO YAANDIKA HISTORIA YATWAA TAJI LA UEFA NATIONS LEAGUE KWA MARA YA PILI!

Katika mchezo wa kusisimua uliopigwa jijini Frankfurt, Ujerumani timu ya taifa ya Ureno imeibuka kidedea na kutwaa taji la UEFA Nations League kwa mara ya pili katika historia, baada ya kuifunga Hispania kwa mikwaju ya penalti tano kwa tatu, kufuatia sare ya mabao mawili kwa mawili ndani ya dakika 120 kwenye dimba la Deutsche Bank Park.

Hispania ilianza kwa kasi, ikipata mabao mawili kipindi cha kwanza kupitia Martín Zubimendi dakika ya 21, na Mikel Oyarzabal dakika ya 45.

Lakini vijana wa kocha wa Ureno walionesha ujasiri wa hali ya juu Nuno Mendes alisawazisha dakika ya 26, kisha akatoa pasi murua kwa Cristiano Ronaldo aliyefunga bao la pili dakika ya 61 likiwa goli lake la 138 kwenye michuano ya kimataifa!

Baada ya dakika 120 kukamilika bila mshindi, mchezo uliamuliwa kwa penalti. Ureno walipachika penalti zao zote tano, huku Hispania wakikosa moja tu – penalti ya Álvaro Morata, iliyookolewa kwa ustadi mkubwa na mlinda mlango Diogo Costa.

Penalti ya mwisho ikafungwa na Rúben Neves na Ureno wakaibuka kidedea kunyakua Kombe hilo, mara ya pili!

Ureno ndiyo taifa la kwanza kushinda UEFA Nations League mara mbili mara ya kwanza mwaka 2019, na sasa tena mwaka huu 2025!

Nuno Mendes wa Ureno, ndiye mchezaji bora wa mchezo aliyefunga bao na kutoa pasi ya goli.

Katika msimu huu wa Idd, tunawatakia nyote amani, upendo na mshik**ano. Iwe ni wakati wa ibada, shukrani na kusherehekea...
06/06/2025

Katika msimu huu wa Idd, tunawatakia nyote amani, upendo na mshik**ano. Iwe ni wakati wa ibada, shukrani na kusherehekea pamoja na familia na jamii.

Address

Njiro Block J
Arusha
P.O.BOX15883

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio5tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio5tz:

Share

Category