Light Of Salvation Church in Mwanza

Light Of Salvation Church in Mwanza GOD IS ONE

25/10/2024

BIBLIA NI NENO LA MUNGU LILILO HAI

Katika Biblia Yako Soma
Zaburi 119: 9-11,105;
Waebrania 4:12; Marko 4:21-29.
Mstari Wa Kukariri
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema (2Tim 3:16, 17).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Je, unaamini kuwa Neno la Mungu ndilo lenye mamlaka yote katika maisha?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Jitahidi kutenga muda maalum kila siku kwa ajili ya kutulia na kutafakari. Tekeleza mpango wa kusoma Biblia. Andaa alama saba za kuweka katika Biblia yako pale unapoachia kusoma ili uweze kupapata kirahisi utakapoendelea kupasoma tena wiki inayofuata.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Kutoka katika 2Fal 22:8-13 na 2Fal 23:1-32 andika mageuzi yote aliyoyafanya mfalme Yosia baada ya kulisikia neno la Mungu.
Tafakari Andiko Hili
Mathayo 7:24-27
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Ujerumani.
Idadi ya watu: 80,000,000. Idadi ya Wakristo ni 75%
Ujerumani Mashariki maskini na Ujerumani Magharibi tajiri sasa zimeungana. Makanisa ya zamani yanapoteza watu. Uamsho unatakiwa haraka

1. Biblia Ni Neno La Mungu
Kwa kila mwamini neno la Mungu ni la kipekee na la thamani kubwa. Kwa karne nyingi zilizopita watu wengi wametoa maisha yao katika kuhifadhi kweli ya neno la Mungu kwa ajili yetu ili tupate kusoma. Kwa kuzingatia thamani kubwa ya neno la Mungu, na andiko kutoka Mk 4:21, swali ni hili, ‘Biblia iko wapi katika maisha yako?’
Je, imefichwa mbali;
Au imewekwa mahali pa juu ili ipate kumulika kila eneo la maisha yako?
2. Baraka Katika Neno La Mungu
Neno lake li hai, linanena nawe na kutenda kazi ndani yako (Ebr 4:12,13).
Neno lake ni kioo kinachokufanya ujione ulivyo kadiri unavyoendelea kulisoma. Neno lake kamwe halitakufanya ujidanganye mwenyewe, wala kuficha ukweli (Yak 1:22-24) (Mk 4:22).
Neno lake litakuandaa kikamilifu ili uwe, na ufanye kile Mungu anachotaka (2 Tim 3:15-17).

Kuanzia ulipokuwa mtoto hadi sasa umeyajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupa hekima unayoihitaji kwa ajili ya kupata wokovu kwa imani katika Kristo Yesu. Maandiko yote yana pumzi ya Mungu na yanafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki, ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
Inasemekana, na ndivyo ilivyo, kwamba Biblia ni Mwana wa Mungu katika maandishi, kwa sababu Yesu anaitwa ni Neno, na vilevile anaitwa Kweli (Yn 1:1).
Je, Unataka Kufanikiwa Na Kustawi?
Basi fanya yale Yoshua aliyoagizwa kufanya (Yos 1:8). Na k**a unataka kustawi kwa kila kitu zingatia Zab 1:1-3.
3. Je, Unaposoma Unasikia?
Je, umewahi kugundua kuwa unaposoma neno la Mungu ‘unasikia’ kwa ndani na si kwa masikio ya nje? Hiyo ni sauti ya Mungu. Yapasa tuwe makini na kile tunachosikia kwa sababu kwa kipimo kilekile tunachotumia, ndicho tutakachopimiwa (Mk 4:24).
4. Je, Unalitumiaje Neno La Mungu?
Unalitumia hilo neno kufanya upya moyo wako (Rum 10:17).
Unalitumia hilo neno kufanya upya mawazo yako Rum 12:2).
Unalitumia hilo neno kufanya upya maneno yako (Rum 10:10) (Mit 18:2).
Ulitumie hilo neno kufanya upya matendo yako (Yn 14:15).
Ulitumie hilo neno kuimarisha ushindi wako. Shetani hakuwa na usemi Yesu aliposema, ‘Imeandikwa’! (Mt 4:1-11)-zingatia mistari ya 4,7 na 10.
Litumie Neno Kuhuisha Maombi Yako
Waamini wa kwanza mara kwa mara walinukuu maandiko ili yawaongoze katika maombi, na Mungu alijibu haraka (Mdo 4:23-31). Iwapo utaomba kwa kutumia neno la Mungu, yafuatayo yataanza kutokea:
Kwanza, unapanda mbegu ya neno.
Kisha kwa uvumilivu katika kuliomba neno, na saburi, huja masuke. Na kwa kadiri unavyoendelea kuwa na imani kwa Mungu na katika neno lake, huja ngano pevu, nafaka kukomaa na hatimaye mavuno.
(Mk 4:14, 26-29) (Isa 55:10, 11) (Mwa 8:22).

Ni Muhimu Kuwapa Wengine Neno La Mungu
Ni muhimu kwa sababu ye yote mwenye neno la Mungu anaweza kuokolewa na kupewa zaidi, mathalani: uponyaji, uhuru, uongozi, baraka na ustawi, kwa kuliamini. Lakini mtu asiye na hilo neno la Mungu ili kuliamini na kulifanyia kazi, hana baraka yo yote katika hizo zilizotajwa, na atapoteza hata hicho alichonacho, yaani maisha yake na nafsi yake milele (Mk 4:25).
5. Unapataje Kulisikia Neno?
Mungu amefanya iwe rahisi sana kuisikia sauti yake. Wewe kaa peke yako na Yeye, na kisha fungua Biblia yako. Kiri udhaifu wako na omba kujifunza kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Chukua muda kutafakari yale uliyosoma na kusikia, kwa sababu kwa njia hiyo utashangaa kuona jinsi Mungu atakavyozungumza na wewe na kujibu maswali yako.
Nikiwa mwamini mpya sikuyajua mambo haya. Nilihudhuria kwenye kusanyiko la maombi na kimyakimya niliomba kwa ajili ya kazi yangu, nikamwombea mke wangu na watoto kwa sababu ya matatizo yote tuliyokuwa nayo. Baada ya muda mfupi nilihisi msukumo wa kuichukua Biblia yangu na ikafunguka yenyewe katika Zaburi ya 128. Na nilipoanza kusoma Mungu alinistusha na baadaye akanipooza kwa neno lake akiuambia moyo wangu:
“Wamebarikiwa wote wamchao Bwana na kutembea katika njia zake.
Utakula matunda ya kazi yako, baraka na kustawi vitakuwa vyako.
Mkeo atakuwa k**a mzabibu uzaao, na wanao k**a matawi ya mtende mezani pako”.
Naliliamini neno la Mungu na leo hii, baada ya miaka kadhaa kupita naweza kuona jinsi Mungu alivyoitunza ahadi yake kwa kuibariki familia yangu na kazi yangu.
6. Namna Ya Kufurahia Usomaji Wa Biblia
Watu wengi huanza na kitabu cha Mwanzo na baadaye huacha wanapokutana na sehemu ngumu katika Agano la Kale ambazo hawazielewi. Sisi sote tunapenda kula vyakula mbalimbali siku kwa siku, na hivyo ndivyo ilivyo hata kwa chakula cha kiroho. Jaribu kufuata mpangilio ufuatao nawe utapata mlo tofauti kila siku. Kila siku soma Zaburi za kuabudu na Mithali kwa ajili ya kupata hekima.
Jumatatu
Hadithi za watu mashuhuri na za historia ya Biblia. Anza na kitabu cha Mwanzo na kuendelea hadi kitabu cha Esta.

Jumanne
Taarifa za watu waliomjua Yesu vizuri. Anza na injili ya Mathayo na kuendelea hadi ya Luka.
Jumatano
Tembea katika vilima na mabonde ya ushairi. Anza na kitabu cha Ayubu hadi Wimbo Ulio Bora.
Alhamisi
Nyaraka za upendo kutoka kwa Yohana. Anza na injili yake, ikifuatiwa na nyaraka zake, na kuishia na Ufunuo wake.
Ijumaa
Unabii wa Biblia. Anza na Isaya na kuendelea hadi Malaki; utastaajabu.
Jumamosi
Nyaraka kutoka kwa watu mashuhuri wa Mungu. Anza na Warumi, endelea hadi Petro na Yuda.
Jumapili
Tembelea makanisa yaliyo hai na misheni zilizoko mstari wa mbele kwa kusoma kitabu cha Matendo ya Mitume.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

UWEZA WA JINA LA YESU
Mtume Paulo anasema katika Waraka wake kwa Wakolosai sura ya tatu na mstari wa kumi na saba kuwa; “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.”
Hii ina maana ya kuwa, tukila tule katika Jina la Yesu Kristo. Tukilala tulale katika Jina la Yesu Kristo. Tukizungumza tuzungumze katika jina la Yesu Kristo. Tukiimba tuimbe katika jina la Yesu Kristo. Tukitembea tutembee katika jina la Yesu Kristo. Tukisafiri tusafiri katika jina la Yesu Kristo. Tukilima shambani tulime katika jina la Yesu Kristo; na kadhalika.
Kwa nini tunatakiwa tufanye mambo yote katika jina la Yesu Kristo? Jina hili la Yesu Kristo lina sehemu gani katika maisha yetu ya kila siku?
K**a tunatakiwa kufanya mambo yote katika jina la Yesu Kristo, kwa nini hatufanyi hivyo?
Ukitafakari maagizo tuliyopewa katika biblia utaona ya kuwa, maisha yetu yote yanalitegemea jina hili la Yesu Kristo.
K**a mambo yetu yote yanatakiwa yafanyike kwa jina la Yesu, basi ni muhimu tujifunze zaidi na zaidi kila siku juu ya jina hili la ajabu.
Ni maombi yangu kwa Mungu Baba, katika jina la Yesu Kristo ya kuwa maneno yaliyomo katika somo hili yatachochea kwa upya kiu iliyomo ndani yako ya kutaka kufahamu zaidi siri iliyomo ndani ya jina la Yesu Kristo.

Mtumishi Lameck

28/04/2024

Church!

"And I will give you pastors according to mine heart, which shall feed you with knowledge and understanding." - Jeremiah 3:15 KJV

"And he gave some, apostles; and some, prophets; and some, evangelists; and some, pastors and teachers; for the perfecting of the saints, for the work of the ministry, for the edifying of the body of Christ:" - Ephesians 4:11-12 KJV

"Let us hold fast the profession of our faith without wavering; (for he is faithful that promised;) and let us consider one another to provoke unto love and to good works: not forsaking the assembling of ourselves together, as the manner of some is; but exhorting one another: and so much the more, as ye see the day approaching." - Hebrews 10:23-25 KJV

25/04/2024

Pentecost Part 4

One of the reasons John the Baptist was sent by God, was to be a witness that Jesus is Christ, God manifest in flesh.

"There was a man sent from God, whose name was John." - John 1:6

"John bare witness of him, and cried, saying, This was he of whom I spake, He that cometh after me is preferred before me: for he was before me." - John 1:15 (John 1:10).

John was born before Jesus. As God, Jesus was before John.

Jesus came to bring the New Marriage Covenant of Grace to replace the Old Marriage Covenant of the Law.

"For the law was given by Moses, but grace and truth came by Jesus Christ." - John 1:17

"And I knew him not: but that he should be made manifest to Israel, therefore am I come baptizing with water...he that sent me to baptize with water, the same said unto me, Upon whom thou shalt see the Spirit descending, and remaining on him, the same is he which baptizeth with the Holy Ghost. And I saw, and bare record that this is the Son of God." - John 1:31, 33-34

The “Son of God” is God manifest in flesh (the body of God).

"Again the next day after John stood, and two of his disciples; and looking upon Jesus as he walked, he saith, Behold the Lamb of God! And the two disciples heard him speak, and they followed Jesus." - John 1:35-37

"After these things came Jesus and his disciples into the land of Judaea; and there he tarried with them, and baptized." - John 3:22

"And they came unto John, and said unto him, Rabbi, he that was with thee beyond Jordan, to whom thou barest witness, behold, the same baptizeth, and all men come to him." - John 3:26

"Ye yourselves bear me witness, that I said, I am not the Christ, but that I am sent before him." - John 3:28

"He that hath the bride is the bridegroom: but the friend of the bridegroom, which standeth and heareth him, rejoiceth greatly because of the bridegroom's voice: this my joy therefore is fulfilled." - John 3:29

Jesus was bringing His New Covenant, baptizing. When we are baptized in the name of Jesus, we forsake the world and covenant our faithfulness to Jesus. Our baptism is our blood covenant of marriage. We become the bride of Christ. (1John 2:15-17).

24/04/2024

Pentecost Part 3

It seems to be no coincidence that the first miracle of Jesus was at a wedding. God had a mission to fulfill: to give His life for His wife. His death would release His people from the marriage covenant that brought death, so they could enter the marriage covenant that brought life.

The miracle of the wedding at Cana points to Christ’s death, burial, and resurrection.

The account begins with, "And the third day…” - John 2:1 KJV

I count fourteen times in the New Testament that “the third day” refers to Christ’s resurrection.

I count eleven times that “hour” is mentioned concerning Christ’s death.

"And when they wanted wine, the mother of Jesus saith unto him, They have no wine. Jesus saith unto her, Woman, what have I to do with thee? mine hour is not yet come." - John 2:3-4 KJV

There is only one other time that Jesus called His mother “woman,” and that was at the cross. (John 19:26).

It appears that Jesus turning the water into wine represents His New Covenant. The wine that Jesus brought forth in His miracle at the wedding was the good wine, surpassing the wine that was brought out at the beginning of the feast.

"When the ruler of the feast had tasted the water that was made wine, and knew not whence it was…the governor of the feast called the bridegroom, and saith unto him, Every man at the beginning doth set forth good wine; and when men have well drunk, then that which is worse: but thou hast kept the good wine until now." - John 2:9-10 KJV

"This beginning of miracles did Jesus in Cana of Galilee, and manifested forth his glory; and his disciples believed on him." - John 2:11 KJV

Apostle Paul speaks of the glory of the New Covenant of the Spirit compared to the glory of the Old Covenant Law. In fact, that first glory was not glorious at all compared with the overwhelming glory of the new way.

"But if the ministration of death, written and engraven in stones, was glorious, so that the children of Israel could not stedfastly behold the face of Moses for the glory of his countenance; which glory was to be done away: How shall not the ministration of the spirit be rather glorious?" - 2 Corinthians 3:7-8 KJV [See 9-11}.

To be continued…

Address

Aruscha

Telephone

+255624411668

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Light Of Salvation Church in Mwanza posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Light Of Salvation Church in Mwanza:

Share