Mjasiriahabari

Mjasiriahabari Ili kuendeleza harakati za mageuzi na mabadiliko tumelenga kuhakikisha kwa pamoja tunajenga Tanzania

02/06/2025
HabariIliyovunjika💥Mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam Bw Iqbal (Baghdad) amefariki dunia. Kwa mujibu wa taarifa...
31/05/2025

HabariIliyovunjika💥

Mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam Bw Iqbal (Baghdad) amefariki dunia.

Kwa mujibu wa taarifa zilizitufikia hivyi punde bw Iqbal amefariki dunia nchini Saudia Arabia kwenye mji mtakatifu wa Madina, alipokwenda hivyi karibuni kwa ibada za hijja.

Bwa Iqbal atak*mbukwa kupitia mradi mkubwa wa ujenzi wa majengo maarufu kwenye wilaya ya Kigamboni yaitwayo Dege Villege ambao ulikuwa ni ubia wa kampuni yake na shirika la Hifadhi ya jamii wakati huo likiitwa NCCF.

Pia ni mmiliki wa majengo mbalimbali ya biashara katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Taarifa zaidi tutaziweka kadiri zitakavyotujia.

Innallillah Wainna Ilayka Rajj'uun.

25/05/2025

Je k*mshambulia raisi wa nchi kwa kutumia jinsia, imani, mavazi, kabila ni kukua kwa demokrasia au ni kukosa muelekeo wa siasa zetu.

Je unaona kuna haja ya siasa zetu kushughulika na ubinafsi wa mtu au kiongozi badala ya kushindana kwa kutizama sera?

Una maoni gani juu ya hoja hizi?

Katika michezo ya Olimpiki ya walemavu inayoendelea, wanariadha wengi hasa wasioona wanahitaji mwongozaji kwenye mbio za...
07/09/2024

Katika michezo ya Olimpiki ya walemavu inayoendelea, wanariadha wengi hasa wasioona wanahitaji mwongozaji kwenye mbio zao.

Hii inamaanisha ili wanariadha washinde, waongozaji lazima wafanye mazoezi kwa nguvu kubwa k**a washindani.

Somo hilo linadhihirishia kwamba wakati mwingine ili kushinda, unahitaji nguvu ya mtu ambaye hashindani lakini kwa kutumia nguvu zake, unaweza kufikia dhahabu.

Kila mtu anahitaji mtu wa aina hiyo katika maisha ili kufikia mafanikio.

K**a unaye mtu wa aina hiyo mtumie au share naye kuonyesha kutambua mchango wake, unaweza k*m tag kutaja jina lake na k*muandikia ujumbe hapa chini.

Tuma na ya kutolea! 💥💭Wasichana wa Australia watasafiri kutoka Australia hadi Kanada na kutumia dola 2,000 kwa tikiti ya...
05/09/2024

Tuma na ya kutolea! 💥💭

Wasichana wa Australia watasafiri kutoka Australia hadi Kanada na kutumia dola 2,000 kwa tikiti ya ndege ambayo ni karibu Shs Milioni tano za kitanzania na kusafiri umbali wa saa 17 kwa ndege k*mtembelea mwanaume.

Wasichana wa Kimarekani watatumia zaidi ya dola 2,500 ambazo ni zaidi ya Shs Milioni saba za kitanzania kununua tiketi ya ndege na kusafiri karibu masaa 9 dakika 30 kwa ndege kutoka Amerika hadi Uingereza k*mtembelea mwanamume na pia k*mnunulia zawadi za thamani.

Wasichana wa Ulaya watatumia zaidi ya euro 2,000 ambayo ni karibu milioni 6 za kitanzania kununua tikiti ya ndege ya kuruka masaa 17 kutoka Ulaya hadi Asia k*mtembelea mwanamume.

Lakini msichana wa kitanzania hawezi kusafiri safari ya dakika 15 ambayo haiwezi kugharimu zaidi Shs 3000 k*mtembelea mwanamume lazima ataomba nauli na ya kutolea na bado atamwambia jamaa wa kitanzania anahitaji mwanaume mzuri na anayejali.

Mdau ameshare na sisi, Vipi kuna ukweli au tatizo kutumia mfano huu? Je ni kweli wanawake wanatumia mitizamo potofu kwenye uhusiano? Au wanawake wengi wanakabiliwa na Ukata?

Mwanasoka mwingine mweusi ambaye huwenda maisha yake yakavurugika ni Ngolo Kante, nyota wa zamani wa Chelsea na mshindi ...
05/09/2024

Mwanasoka mwingine mweusi ambaye huwenda maisha yake yakavurugika ni Ngolo Kante, nyota wa zamani wa Chelsea na mshindi wa kombe la dunia akiwa na timu ya taifa ya Ufaransa.

Ngolo Kante amemuoa mwanamke wa kizungu, mwingereza anayeitwa Jude Littler.

Jude Littler alikuwa mke wa zamani wa Djibril Cisse, pia mwanasoka mwingine mweusi wa zamani.

Walioana kutoka 2005 hadi 2012 baada ya kuachana naye mwishoni mwa maisha yake ya soka. Kwenye mchakato wa kuachana mwanamke huyu alichukua sehemu kubwa ya utajiri wa Jibril Cisse kwa mujibu wa sheria za Uingereza.

Miaka 2 baadaye, Ngolo Kante alikutana na Jude Littler kwenye klabu ya usiku na walioana muda mfupi baadaye.

Jude Littler ana umri wa miaka 48 huku Ngolo Kante akiwa na umri wa miaka 33, anamzidi umri wa miaka 15.

Cha kusikitisha zaidi ni kwamba alikuwa na watoto 3 kwa mumewe wa zamani Djibrin Cisse ambaye Ngolo Kante sasa anawaita watoto wake.

Ngolo hana mtoto wake mwenyewe kwani mwanamke huyo alimwambia hataki tena kuzaa.

Ngolo Kante bado anacheza soka na analipwa pesa nyingi sana Al Ahli ya Saudia.

Swali kuu hapa, wakati kazi yake itakapokwisha je ndoa hiyo itadumu? Na je suala la kugawana mali Ngolo atatoka salama? .

Inaonekana wanaume wa Kiafrika hawajifunzi kutokana na makosa ya mwenzao, je tatizo hili la vijana wa kiafrika kutokuwa makini huko ulaya na mitego ya wanawake wa kizungu ni mipango maalumu ya kuwafilisi vijana wa kiafrika?

Isitoshe yule bibi ni mzee sana kwa mtu k**a Ngolo Kante, bora kwa Jibril Cisse anao watoto wake. Vipi Ngolo ambaye hata mtoto hana?

Nini tunaweza kujifunza hapa?

Je ungependa tuichambue stori hii kuona muendelezo wake? Like ili tujue

Tuhuma dhidi ya   MariaSarungi, anapaswa kuzijibu.  ashughulikie na kutupa majibu ya maswali haya kwa undani na kututosh...
22/08/2024

Tuhuma dhidi ya MariaSarungi, anapaswa kuzijibu.

ashughulikie na kutupa majibu ya maswali haya kwa undani na kututosheleza.

Wito wa Uwazi na Uwajibikaji:

Ingawa ni jambo la kupongezwa kutetea haki na uhuru wa kusema, kanuni hizi lazima ziwe ni msingi katika uaminifu na uwajibikaji.

hivi karibuni ametufundisha jambo muhimu juu ya uwajibikaji:

"K**a kuna tuhuma zinazochafua taasisi na kugusa maslahi ya wengi unatakiwa kujibiwa na wanaotuhumiwa bila kujali nani amesema”

Kutokana na misingi hiyo, Shangazi MariaSTsehai anahimizwa kutoa maelezo ya wazi na ya kina kuhusiana na madai ya hivi karibuni yanayosambaa kwenye mitandao kuwa amekuwa akijipatia Mamilioni ya shilingi kutokana na harakati zake anazofanya.

Utawala wa sheria na haki una uhusiano usioweza kutenganishwa na uwazi, kwa msingi huo ni lazima na sharti muhimu kwa shangazi kuonyesha uwajibikaji

MariaSTsehai ashughulikie na kutupa majibu ya maswali yafuatayo:

➡️ Ruzuku ya Ford Foundation:

Je, ni kweli kwamba amepokea ruzuku au ufadhili kutoka kwa Ford Foundation?

➡️ Wafadhili kutoka nje:

Je, harakati zake zina wafadhili ambao si raia wa Tanzania?

➡️ Kuhamishwa hadi Nairobi:

Je, ni sahihi kwamba amehamishia makazi yake nchi jirani, jiji la Nairobi?

➡️ Maslahi Binafsi:

Je, anajibu vipi mtizamo miongoni mwa Watanzania ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiamini kwamba harakati zako zinasuk*mwa zaidi na maslahi binafsi kinyume na dhamira ya dhati ya kuwatumikia wale wasio na sauti.

Ni muhimu kwa Shangazi atoe majibu ya uhakika kwa maswali haya, na kuhakikisha kwamba matendo yake yanawiana na kanuni za uwazi, uwajibikaji, na manufaa zaidi ya Watanzania.

"Tizama tuhuma zinazosambaa kwenye comment"

Address

Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mjasiriahabari posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mjasiriahabari:

Share