R Kay

R Kay Welcome to R Kay. Digital Journalist. Content Creator. Football Reporter. Teacher. R Kay Yanga Sc Fan Page
(1)

  “Uganda tumecheza nao mechi nyingi sana tangu nimeanza kucheza timu ya taifa, nadhani kesho tutuwafunga bila shaka” “K...
26/12/2025

“Uganda tumecheza nao mechi nyingi sana tangu nimeanza kucheza timu ya taifa, nadhani kesho tutuwafunga bila shaka”

“Kila mmoja anaweza kushinda lakini kwetu huu ni mchezo wa ushindi, tunajua wamejipanga na sisi tuko tayari kwa ajili ya ushindi hatuna jambo jingine zaidi ya ushindi. Tunawaheshimu uganda ila tunataka ushindi.” - Simon Msuva akizungumzia kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Uganda kundi A.



 Unaambiwa katika mechi ambazo zinasubiriwa sana kuwavutia watu ni Tunisia vs Nigeria. Mechi zao za ufunguzi wote walish...
26/12/2025


Unaambiwa katika mechi ambazo zinasubiriwa sana kuwavutia watu ni Tunisia vs Nigeria.

Mechi zao za ufunguzi wote walishinda. Nigeria akimpiga Tanzania 2-1 huku Tunisia akimuwasha bila huruma Uganda kwa 3-1. Hivyo wote wana pointi 3 kwa tofauti ya magoli.

Baada ya kufanikiwa kuzichukua pointi kutoka nchi za Afrika Mashariki, sasa wataenda kuvaana wao kwa wao. Wakubwa kwa wakubwa katika soka.

Hii itakuwa mechi ya kuviziana sana na yenye mbinu mno kwani kila mmoja anataka kuliongoza kundi.

Unadhani au unatarajia matokeo yatakuwaje baada ya dakika 90?

Tuandikie 👇

Usisahau ku follow page yetu 👉 R Kay


Kesho jumamosi tar 27 Disemba 2025 linakuja Dabi moja kali la Afrika Mashariki. Ni Tanzania v Uganda kwenye michuano ya ...
26/12/2025

Kesho jumamosi tar 27 Disemba 2025 linakuja Dabi moja kali la Afrika Mashariki. Ni Tanzania v Uganda kwenye michuano ya .

Tanzania walichapwa 2-1 na Nigeria wakati Uganda walicharazwa 3-1 na Tunisia. Kwa hivyo, timu hizi mbili zitakuwa zikitafuta ushindi wao wa kwanza baada ya kupoteza zile za ufunguzi. Hiki ndicho kitafanya mechi ya kesho kuwa kali, ngumu na tamu kuitazama. Usiikose!

Toa maoni yako kuhusu mpambano huu 👇👇

Nifollow👉 R Kay





Young Africans Sports Club wamethibitisha kuwa mechi yao ya tar 4 Disemba dhidi ya   itakuwa maalumi kwa ajili ya goliki...
02/12/2025

Young Africans Sports Club wamethibitisha kuwa mechi yao ya tar 4 Disemba dhidi ya itakuwa maalumi kwa ajili ya golikipa bora sana kwa sasa kwenye Djigui Diarra yaani .

Hivi karibuni hasa ukirejea mchezo wao dhidi ya wapenzi na wanachama wa YangaSc wameonesha kupendezwa mno na kiwango cha golikipa Diarra. Alifanya uokoaji muhimu mara kadhaa na kuisaidia club yake kufanikiwa kutoka na clean sheet japo pia hawakushinda mechi hiyo.

Kabla ya kupangwa kwa , wapenzi kadhaa wa YangaSc walifanya changizo la pesa lililofikia takribani milioni mbili na kupitia ndugu aitwaye walimkabidhi Diarra pesa hiyo mara walipowasili Airport wakitokea Algeria.

Nini maoni yako?
Tuandikie 👇
Follow R Kay

   Makocha wauchambua mchezo waoEnzo Mareska wa Chelsea "Tulikuwa na timu nzuri zaidi zaidi yao kwenye 11 vs 11 lakini t...
01/12/2025


Makocha wauchambua mchezo wao

Enzo Mareska wa Chelsea
"Tulikuwa na timu nzuri zaidi zaidi yao kwenye 11 vs 11 lakini tukiwa na wachezaji 10, ni ngumu zaidi lakini tulishughulika vilivyo."

Mikel Arteta wa Arsenal
" Kwa ujumla nadhani k**a hutakishinda kikosi cha watu 10 kwa dakika 45 lazima ukatishwe tamaa. Lakini yapaswa ujue wiki tuliyokuwa nayo, mpinzani ni mgumu. "

Nini maoni yako kuhusu mechi hii?
Tuandikie 👇

Follow and Like R Kay

*Stade Malien vs Simba SC : Résumé du Match*Le match entre Stade Malien et Simba SC s'est terminé par une victoire de St...
01/12/2025

*Stade Malien vs Simba SC : Résumé du Match*

Le match entre Stade Malien et Simba SC s'est terminé par une victoire de Stade Malien avec un score de 2-1. Le match a eu lieu le 30 novembre 2025 au Stade du 26 Mars à Bamako, dans le cadre de la Ligue des Champions de la CAF.

*Détails du Match*

- *Score final* : Stade Malien 2-1 Simba SC
- *Buts* : Taddeus Nkeng (16') et Ismaila Simpara (23') pour Stade Malien, Neo Maema (54') pour Simba SC
- *Possession du ballon* : Stade Malien 33%, Simba SC 67%
- *Tirs au but* : Stade Malien 16, Simba SC 14

*Réaction de l'Entraîneur*

L'entraîneur de Simba SC, Dimitar Pantev, a exprimé sa déception après le match, déclarant que ses joueurs n'ont pas joué à leur niveau.

Commentez 👇

Suivez-moi par R Kay

  Hatua ya makundi Stade Malien de Bamako ilicheza na Simba SC leo, Novemba 30, 2025, saa 16:00 UTC kwenye uwanja wa Sta...
30/11/2025

Hatua ya makundi

Stade Malien de Bamako ilicheza na Simba SC leo, Novemba 30, 2025, saa 16:00 UTC kwenye uwanja wa Stade du 26 Mars, Bamako. Matokeo ya mchezo huu ni Stade Malien de Bamako 2-1 Simba SC.

Takwimu za Mchezo

Umililiki wa Mpira_: Stade Malien de Bamako 33%, Simba SC 67%
- _Jumla ya Mashuti_: Stade Malien de Bamako 16, Simba SC 14
- _Mashuti ya Laba_: Stade Malien de Bamako 7, Simba SC 4

Mabao

Taddeus Nkeng (16') - Stade Malien de Bamako
Ismaila Simpara (23') - Stade Malien de Bamako
Neo Maema (54') - Simba SC

Timu ya Kwanza

- Stade Malien de Bamako: N'Golo Traoré, Abdoul Bode, Ismaila Simpara, Babe Diarra, Francis Awine, Ahmadou Bello, Ibrahim Camara, Mamadou Traoré, Ousmane Coulibaly, Taddeus Nkeng, Moussa Diallo
- Simba SC: Yakoub Suleiman, Shomari Kapombe, Rushine De Reuck, Wilson Nangu, Anthony Richard Mligo, Joshua Mutale, Jean Charles Ahoua, Elie Mpanzu, Neo Maema, Naby Camara, Seleman Mwalimu.

Jambo gani la ajabu umelishuhudia leo?

Una maoni gani kuhusu mchezo huu?

Tuandikie 👇

Kisha follow R Kay

Kuna raia wanajiuliza, *Yanga wana jezi ngapi? " Msiwajibu. Wapuuzeni. Si wanajua kuhesabu 😂
30/11/2025

Kuna raia wanajiuliza, *Yanga wana jezi ngapi? "

Msiwajibu. Wapuuzeni. Si wanajua kuhesabu 😂

  VITA YA LONDON DERBY LEOLeo tena tutashuhudia mechi kubwa na kali. Arsenal akialikwa Stamford Bridge na Chelsea huku A...
30/11/2025

VITA YA LONDON DERBY LEO

Leo tena tutashuhudia mechi kubwa na kali. Arsenal akialikwa Stamford Bridge na Chelsea huku Arsenal wakitarajia kuendeleza uongozi wa ligi. Chelsea, wakiwa nafasi ya pili, watajaribu kuondoa gap kati yao kwa kuzisaka pointi 3 muhimu.

Ni leo Jumapili Novemba 30, 2025 kwenye dimba la Stamford Bridge, jijini London.

Arsenal wanaingia kwenye kipute hiki wakiwa na kumbukumbu tamu ya kuwaadabisha Spurs 4-1 na Bayern Munich 3-1 katika mechi zao mbili za mwisho. Chelsea, kwa upande wao, nao wameshinda mechi mfululizo ikiwemo ile waliyomwadabisha Barcelona kwa 3-0 kwenye kipute cha Champions League.

Timu hizi mbili zinatinga dimbani leo zikiwana majeruhi kadha.

Kwa Arsenal, Leandro Trossard ana mashaka kutokana na muscle injury huku Viktor Gyokeres na Kai Havertz bado wanapona polepole majeraha yao.

Kwa Chelsea, Cole Palmer anaweza kupatikana baada ya kupona hasa kile kidole gumba chake.

Watabiri wameonesha Arsenal anaweza kushinda mpambano huu. Wakitabiri ushindi wa Chelsea 1-2 Arsenal.

Je, Arsenal wataendelea kukaa pale juu, au Chelsea watafanya yao?

Tuandikie 👇

Bila kusahau ku follow R Kay kwa updates zaidi baada ya mechi.

Unaambiwa Waarabu ilibidi wajiulize swali. "Oya hivi tulicheza na YangaSc au Atletico Madrid" Dadeki na bado 😂
30/11/2025

Unaambiwa Waarabu ilibidi wajiulize swali. "Oya hivi tulicheza na YangaSc au Atletico Madrid" Dadeki na bado 😂

Simba SC Tanzania Mzigoni Tena LeoClub ya Simba aka wanalunyasi watakuwa kwenye jukumu lingine leo katika kuipambania nc...
30/11/2025

Simba SC Tanzania Mzigoni Tena Leo

Club ya Simba aka wanalunyasi watakuwa kwenye jukumu lingine leo katika kuipambania nchi na club yenyewe kwenye mechi ya group stage dhidi ya Stade Malien ugenini kule Mali.

Baada ya kupoteza mchezo wao katika karata yao ya kwanza hapa nyumbani , leo wana kazi nzito ya kutaka kujiweka kwenye mazingira salama ili kuweza kuvuka hatua ya makundi.

Mechi inatarajiwa kupigwa kuanzia milango ya saa 1:00 za usiku kwa saa za hapa Tanzania.

Mtakie mnyama kheri kupitia komenti hapo chini.

Tuandikie 👇

Usisahau ku follow na ku like R Kay kwa updates za hapo baadaye.

Address

Arusha

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

+255676783387

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when R Kay posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share