Uzalendo wa Kitanzania

Uzalendo  wa Kitanzania UKURASA HURU WA KUCHAMBUA & KUJADILI MADA MBALIMBALI ZA SIASA, UCHUMI & JAMII. Hapa Kazi Tu

Ukurasa Maalumu Wa kutoa, Kuchambua Na Kujadili Habari Mbalimbali za Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa.

RAIS Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewajibu watu wanaomzushia kifo akisem...
10/10/2025

RAIS Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewajibu watu wanaomzushia kifo akisema yeye ni mzima wa afya wala haumwi na kichomi, huku akiwaarifu wanaomuombea mabaya wataugua wao na atashiriki mazishi yao

Dkt. Kikwete ameyasema hayo leo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani alipopewa nafasi ya kusalimia wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu.

“Kuna watu wananizushia mara nimekufa, wengine wanasema ninaumwa. Mimi ni mzima wa afya, afya yangu ni nzuri, sina ninapougua, wataugua wao na nitashiriki mazishi yao” — amesema Dkt. Kikwete

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema kuwa limeanza kufanyia kazi taarifa za kudaiwa kutekwa aliyekuwa Balozi wa Tanz...
06/10/2025

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema kuwa limeanza kufanyia kazi taarifa za kudaiwa kutekwa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi hilo Oktoba 6, 2025, Jeshi la Polisi la Tanzania limesema kuwa limeona taarifa zinazosambaa kwenye Mitandao ya Kijamii na ndugu wa Polepole kuwa ametekwa, likisisitiza kuwa limeanza kufanyia kazi taarifa husika ili kupata ukweli wake.

Wakati huohuo, Jeshi hilo limesema kuwa linaendelea kumsubiri Polepole aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini humo.

Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph kabila amehukumiwa adhabu ya kifo na Mahak**a ya Kijeshi ya nc...
01/10/2025

Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph kabila amehukumiwa adhabu ya kifo na Mahak**a ya Kijeshi ya nchini humo baada ya kupatikana na hatia ya makosa kadhaa ikiwemo 'uchochezi'.

Kabila ambaye ana umri wa miaka 54 alifunguliwa mashtaka mnamo mwezi Juni kwa makosa ya uchochezi, uhalifu wa kivita na ushirikiano na kundi linalopigana na vikosi vya serikali mashariki mwa nchi hiyo la M23.

Serikali mjini Kinshasa inamshutumu Kabila kwa kushirikiana kwa ukaribu na Rwanda pamoja na kundi la waasi la M23 ambalo limeitika miji muhimu mashariki mwa Kongo.

 #"Natambua pia yapo maeneo yenye changamoto kati ya wakulima na wafugaji ikiwemo Nanyumbu na maeneo mengine lakini tuna...
26/09/2025

#"Natambua pia yapo maeneo yenye changamoto kati ya wakulima na wafugaji ikiwemo Nanyumbu na maeneo mengine lakini tunayafanyia kazi na moja kati ya hatua tunazizichukua mkitupa ridhaa ndani ya miaka mitano ijayo ni pamoja na kuendelea kupima maeneo ya wafugaji kila tutakapopata eneo na nilisema tutatoka ekari Milioni tatu kwenda mpaka sita.

"Hiyo ni ili wafugaji wapate maeneo maalumu wakafuge kitaalamu na wakulima waendelee na kilimo chao," Dk. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM akizungumza na wananchi wa Mtwara Mjini leo.

Ameongeza akisema; "Mkitupa ridhaa na tunapoendelea mbele tutaendelea kutafuta masoko ya uhakika na sio tu kwa Korosho lakini kwa mazao yote tunayozalisha nchini ikiwemo ufuta na mbaazi na tutaendelea kuvutia wawekezaji kwaajili ya ujenzi wa viwanda vya kuchakata korosho katika Kongani ya viwanda iliyopo pale kijiji cha Maranje katika Wilaya ya Mtwara.

"Tutaendelea pia kusimamia kwa karibu vyama vya Ushirika ili kuondoa ubadhirifu wa fedha za washirika lakini pia ucheleweshaji wa malipo kwa wakulima. Tunavijenga viwe taasisi tunazoweza kuzitegemea katika uendeshaji wa kilimo chetu nchini. Katika hatua nyingine k**a mnavyojua tumeanzisha benki ya ushirika ili iweze kutoa huduma bora kwa vyama vya ushirika katika kuendeleza kilimo chetu," amesema Dk. Samia.

  ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu imepita njia isiyo ya kawaida ya kusini kuelekea New York, akikwepa anga y...
25/09/2025

ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu imepita njia isiyo ya kawaida ya kusini kuelekea New York, akikwepa anga ya Ulaya kutokana na hofu ya uwezekano wa kuk**atwa na Mahak**a ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Ndege hiyo imeonekana kupaa kusini na kufuata njia ndefu ya kipekee, ikilenga kukaa mbali na nchi zilizotia saini Mkataba wa Roma ambazo zinaweza kuhitajika kutekeleza vibali vya kuk**atwa endapo itatua kwa dharura.

Njia iliyochaguliwa ni tofauti sana, kwani inakwepa uwezekano wa kutua kwa dharura katika mojawapo ya nchi ambazo zinaweza kumweka Netanyahu katika hatari ya kuingia kwenye mkondo wa sheria.

Nchi zote zilizotia saini Mkataba wa Roma, mkataba ambao Mahak**a ya Kimataifa ya Uhalifu inafanya kazi chini yake, zina wajibu wa kutekeleza hati za kuk**atwa zinazotolewa na ICC.

Wasiwasi umeongezeka huko Jerusalem kwamba katika kesi ya kutua kwa dharura, nchi hizi zingechagua kutekeleza majukumu yao ya kisheria.

Nchi nne zilizotia saini mkataba huo na kutangaza nia ya kujiondoa na mahak**a hiyo ni Israel, Sudan, Marekani na Urusi.

.Asanteni sana wananchi wa Ndanda, Ruangwa na MtamaShughuli ni watu, na ninyi mmeuishi msemo huu kwa kufika kwa wingi kw...
25/09/2025

.Asanteni sana wananchi wa Ndanda, Ruangwa na Mtama

Shughuli ni watu, na ninyi mmeuishi msemo huu kwa kufika kwa wingi kwenye mikutano ya kampeni zetu ili kusikiliza sera na mipango ya Chama cha Mapinduzi (CCM) juu yenu na Taifa letu, ili Oktoba 2025 mtupe ridhaa ya kuendelea kuwatumikia.

Chama cha Mapinduzi ni chama cha kazi, chama kinachojali utu wa wananchi wote na pia ndicho chenye nia, uwezo, historia na mikakati ya kuendelea kujenga Tanzania imara yenye amani, umoja, haki, mshik**ano na fursa kwa wote.

TANZIA:  ABASS MWINYI AMEFARIKI DUNIA LEO SEPTEMBA 25,2025 Mtoto wa Marehemu Ali Hassan Mwinyi, Abbas Mwinyi ambae ni Ka...
25/09/2025

TANZIA: ABASS MWINYI AMEFARIKI DUNIA LEO SEPTEMBA 25,2025
Mtoto wa Marehemu Ali Hassan Mwinyi, Abbas Mwinyi ambae ni Kaka wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Mwinyi Leo Septemba 25 amefariki Dunia akiwa Hospitali ya Lumumba Mjini Unguja. Abbas Mwinyi ni Mtoto wa Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi ambae kabla ya umauti wake alikua Msemaji wa Familia mara baada ya kifo cha Baba yao.

24/09/2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alijikuta akitembea kwa miguu katikati ya viunga vya jiji la New York Jumatatu, baada ya gari lake kuzuiwa kutokana na msafara wa Rais wa Marekani Donald Trump kufunga barabara. Macron, aliyekuwa njiani kuelekea kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNGA), alilazimika kushuka kwenye gari lake na kuanza kutembea pamoja na wasaidizi wake, baada ya polisi wa New York kuwaeleza kuwa barabara zote zimefungwa kwa ajili ya msafara wa Trump. Katika tukio hilo la kipekee, Macron alionekana kuchukulia hali hiyo k**a dhihaka na urafiki, akimpigia simu Rais Trump kumweleza kilichomfika. Tazama mkasa husika na kisha toa maoni yako kwa mfano ingekuwa Uganda, Kenya au kwengineko, alafu rais wa taifa jirani kazuiwa na polisi kwa sababu inayofanana na hiyo. Mfano tu!! tujadiliane.

"Chama cha Mapinduzi na serikali zake ndizo zinazoweza kufanya kazi ya kuinua hali na utu wa Mtanzania. Tumefanya miaka ...
23/09/2025

"Chama cha Mapinduzi na serikali zake ndizo zinazoweza kufanya kazi ya kuinua hali na utu wa Mtanzania. Tumefanya miaka mitano iliyopita tuna imani na tunajiamini tunaweza kufanya miaka mitano inayokuja." - Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu kwenye kampeni Nanyumbu, Mtwara

  TUNATIKI
23/09/2025

TUNATIKI

Abiria wanaotumia usafiri wa Mwendokasi wameshuka kupitia madirishani katika Kituo cha Magomeni Mwembechai, jijini Dar e...
23/09/2025

Abiria wanaotumia usafiri wa Mwendokasi wameshuka kupitia madirishani katika Kituo cha Magomeni Mwembechai, jijini Dar es Salaam, baada ya basi walilokuwa wakisafiria kusimamishwa na polisi kwa madai ya kuzidisha abiria kupita kiasi.

Tukio hilo lilitokea leo asubuhi, majira ya 08:25, ambapo abiria hao walikuwa wakitokea Kimara kuelekea katikati ya jiji.

Baadhi ya abiria walikuwa wametokeza vichwa na sehemu za miili yao nje ya madirisha na wengine kukaa juu ya basi hilo huku wakiimba nyimbo mbalimbali, zikiwemo zenye maneno ya malalamiko k**a vile "hatumtaki!"

Chanzo cha hali hiyo kinadaiwa kuwa ni changamoto kubwa ya usafiri katika maeneo ya Kimara na Mbezi, ambapo abiria wanasema wamekuwa wakikaa vituoni kwa muda mrefu tangu alfajiri bila kupata magari ya kutosha kuwapeleka mjini.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uzalendo wa Kitanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uzalendo wa Kitanzania:

Share