Uzalendo wa Kitanzania

Uzalendo  wa Kitanzania UKURASA HURU WA KUCHAMBUA & KUJADILI MADA MBALIMBALI ZA SIASA, UCHUMI & JAMII. Hapa Kazi Tu

Ukurasa Maalumu Wa kutoa, Kuchambua Na Kujadili Habari Mbalimbali za Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa.

Naibu Katibu Mkuu wa Makanisa ya Ufufuo na Uzima (GCTC), Askofu Maximilian Machumu Kadutu (Mwanamapinduzi), amesema akau...
20/07/2025

Naibu Katibu Mkuu wa Makanisa ya Ufufuo na Uzima (GCTC), Askofu Maximilian Machumu Kadutu (Mwanamapinduzi), amesema akaunti zote za kifedha za kanisa hilo zimefungwa bila kufuatwa utaratibu, hatua ambayo imeathiri vibaya huduma za kiroho kwa mamilioni ya waumini nchini.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, siku ya Jumamosi tarehe 19 Julai 2025, Askofu Kadutu amesema akaunti hizo zimefungwa bila kuwahoji viongozi wa kanisa ambao ndio wateja wa benki, jambo linalokwenda kinyume cha haki za kisheria.

"Akaunti zote za kifedha za kanisa zimefungiwa (frozen) bila kufuata utaratibu wa kisheria wa kuulizwa kwa wateja wenyewe ambao ni wahusika wa kanisa hilo", ameeleza.

Aidha amesema mpaka sasa makanisa yote 2,112 ya GCTC yamefungwa nchini nzima, huku waumini zaidi ya milioni 6 wakinyimwa haki yao ya msingi ya kuabudu na miongoni mwao wakik**atwa wakiwemo wanawake, wazee na vijana.

"Waumini zaidi ya milioni 6 wamenyimwa haki ya kuabudu. Maaskofu, wachungaji, na wafanyakazi wa kanisa wamepoteza ajira, huduma na wito wa kazi ya Mungu", amesema Kadutu.

Askofu Kadutu amesema kuwa tangu kufungwa kwa makanisa hayo, tayari ni wiki ya saba waumini wa Ufufuo na Uzima hawajapata huduma za kiroho ipasavyo kwani kuna wakati walilazimika kukusanyika nje ya kanisa kwa ibada ambako huko nako hawakuabudu kwa amani kutokana na ulinzi mkali wa polisi.

"Baadaye, tarehe 4 Juni 2025, uongozi wa kanisa uliwasilisha shauri mahak**ani kuomba zuio dhidi ya barua hiyo, lakini mpaka leo mahak**a haijatoa uamuzi wowote, huku waumini wakiendelea kuteseka na kukosa ibada kila wiki, leo tunaingia wiki ya 7 bila waumini kupata huduma za kiroho, bila waumini kujua kustakabali wa jambo hilo, siyo kutoka kwa Waziri, siyo kutoka Mahak**ani", ameeleza.

20/07/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Paul Ghemela, Emanuel Jp

17/07/2025
Papa Mpya ametangazwa ni Kardinali Robert  Francis Prevost na amechagua jina la Papa Leo XIV.Asante Mungu kwa zawadi ya ...
08/05/2025

Papa Mpya ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost na amechagua jina la Papa Leo XIV.

Asante Mungu kwa zawadi ya Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki

PAPA FRANCIS AFARIKI DUNIA, SAMIA ATUMA SALAAM ZA RAMBIRAMBI•Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Kiongozi wa Kanisa Ka...
21/04/2025

PAPA FRANCIS AFARIKI DUNIA, SAMIA ATUMA SALAAM ZA RAMBIRAMBI

Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisko. Katika kipindi chote cha miaka 12 akiwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisko ameishi maisha yake k**a mwalimu na kiongozi aliyefundisha na kuhimiza ustawi na maendeleo ya watu pamoja na kudumisha amani.

Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninatuma salamu za pole kwa waumini wote wa Kanisa Katoliki hapa nchini na duniani kote.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi.

Amina.

08/04/2025

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amesema siku ya uchaguzi mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu, chama hicho kitaitisha maandamano ya kuuzuia uchaguzi usifanyike.

Kauli hiyo ya Lissu, inajibu swali kuhusu mbinu ambayo chama hicho itaitumia kuzuia uchaguzi kuendana na ajenda yake ya ‘No Reforms, No Election’ (bila mabadiliko, hakuna uchaguzi).

Lissu amesema hayo leo, Jumatatu Aprili 7, 2025 wakati akihutubia mkutano wa hadhara Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara katika ziara ya kutoa elimu kuhusu ‘No Reforms, No Election.’

NAMIBIA: WOTE NI WANAWAKE RaisMakamu wa RaisWaziri mambo ya NjeWaziri wa UlinziWaziri wa Fedha Waziri mambo ya ndani Waz...
23/03/2025

NAMIBIA: WOTE NI WANAWAKE
Rais
Makamu wa Rais
Waziri mambo ya Nje
Waziri wa Ulinzi
Waziri wa Fedha
Waziri mambo ya ndani
Waziri wa Usalama

Kamarada Balozi Humphrey PolepoleUnadhani nafasi ipi inamfaa ndani ya CCM?
09/03/2025

Kamarada Balozi Humphrey Polepole

Unadhani nafasi ipi inamfaa ndani ya CCM?

Akiongea mbele ya Wanawake wa Arusha leo March 02,2025, Makonda amesema;"Kuanzia kesho kila Mwanaume, k**a kweli wewe ni...
03/03/2025

Akiongea mbele ya Wanawake wa Arusha leo March 02,2025, Makonda amesema;

"Kuanzia kesho kila Mwanaume, k**a kweli wewe ni Mwanaume na huyo Mke uliyenaye au Mpenzi uliyenae unampenda, kuanzia kesho tunaanza challenge hapa Arusha Wanaume kupost Wake zao, kuanzia March 03 hadi March 07,2025 kila Mwanaume anatakiwa kumpost Mke wake, ukiona haujapostiwa njoo tufanye maombi hapa March 08,2025 na Dkt. Samia"

"Kwakuwa March 08 ni siku ya Wanawake hiyo tutaacha kuitumia kwa ajili ya Wake zetu, kwa mfano Mimi nimemuambia Baba yangu mzazi ampost Mke wake na Mimi nitampost Mke wangu, kuanzia kesho tuone Wanawake wanaopendwa na Wanaume zao na ukiona haujapostiwa March 08 uje usikilize hotuba ya Dkt. Samia ndio itakayokuponya"

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imefuta adhabu ya kadi nyekundu kwa mchezaji wa Namungo, Derick Mukombozi, ali...
23/02/2025

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imefuta adhabu ya kadi nyekundu kwa mchezaji wa Namungo, Derick Mukombozi, aliyoadhibiwa na mwamuzi wa mchezo wa Namungo FC dhidi ya Simba SC.

Kamati imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa maelezo yaliyopo kwenye ripoti ya mwamuzi hayana ushahidi wa kutosha unaoendana na marejeo ya picha mjongeo.

Aidha, mchezaji wa Namungo, Daniel Amoah ameadhibiwa kwa kutozwa faini ya shilingi 500,000, kwa kosa la kuonekana akimwaga vimiminika kwenye goli, jambo lililohusianishwa na vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina.

Askari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na wenzao wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tan...
22/02/2025

Askari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kushirikiana na wenzao wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Jeshi la Polisi Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, wamemuua fisi katika Kijiji cha Kimali ambaye alikuwa akiwasumbua wakazi wa eneo hilo.

Fisi huyo aliyeuawa anadaiwa kuwa na alama ya jina la mtu upande wa paja lake la kushoto, huku akiwa na shanga shingoni.

Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Anna Gidarya amewataka wananchi wote wilayani humo wanaomiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria kuzisalimisha haraka kwa wahusika wa uhifadhi, kabla ya hatua kali hazijachukuliwa dhidi yao.

Kumekuwepo na matukio ya fisi kushambulia watoto kuanzia majira ya saa moja usiku katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Itilima.

Takwimu zilizotolewa wilayani Itilima zinaonyesha kuwa kuanzia mwaka 2024 hadi sasa watu nane wamefariki dunia baada ya kushambuliwa na fisi na wengine 17 wamejeruhiwa, huku fisi 16 wakiuawa katika kipindi hicho.

MWENYEKITI CHADEMA TUNDU LISSU ASEMA CHADEMA HAINA FEDHA ZA KUENDESHA CHAMA, AOMBA MICHANGO YA WANACHAMA!"Nisiwadanganye...
21/02/2025

MWENYEKITI CHADEMA TUNDU LISSU ASEMA CHADEMA HAINA FEDHA ZA KUENDESHA CHAMA, AOMBA MICHANGO YA WANACHAMA!

"Nisiwadanganye, tunahitaji fedha kwenye Chama za kufanyia shughuli. Tuna upungufu wa kutisha wa fedha kwa ajili ya shughuli za Chama, wiki ijayo nimeambiwa tutafanya huo utaratibu wa namna ya kupata fedha za Chama. Msiniulize Mwenyekiti umekuta nini huko ulipoingia kwasababu sitajibu na sitajibu kwasababu jibu halitakuwa zuri sana"

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uzalendo wa Kitanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uzalendo wa Kitanzania:

Share