
10/10/2025
RAIS Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewajibu watu wanaomzushia kifo akisema yeye ni mzima wa afya wala haumwi na kichomi, huku akiwaarifu wanaomuombea mabaya wataugua wao na atashiriki mazishi yao
Dkt. Kikwete ameyasema hayo leo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani alipopewa nafasi ya kusalimia wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu.
“Kuna watu wananizushia mara nimekufa, wengine wanasema ninaumwa. Mimi ni mzima wa afya, afya yangu ni nzuri, sina ninapougua, wataugua wao na nitashiriki mazishi yao” — amesema Dkt. Kikwete