Uzalendo wa Kitanzania

Uzalendo  wa Kitanzania UKURASA HURU WA KUCHAMBUA & KUJADILI MADA MBALIMBALI ZA SIASA, UCHUMI & JAMII. Hapa Kazi Tu

Ukurasa Maalumu Wa kutoa, Kuchambua Na Kujadili Habari Mbalimbali za Kiuchumi, Kijamii na Kisiasa.

Aliyewahi kuwa Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mbunge wa Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagam...
11/12/2025

Aliyewahi kuwa Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mbunge wa Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama amefariki Dunia leo leo tarehe 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma.

Taarifa ya kifo chake imetolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. M***a Azzan Zungu kupitia taarifa ya Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma Ofisi ya Bunge, Dodoma leo Desemba 11, 2025.

"Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Peramiho, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu," amesema Mhe. Spika.

“Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya Marehemu inaratibu mipango ya mazishi na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa. Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi, Amina.” — imesema taarifa hiyo.

 #“Serikali inajua idadi ya vituo vya Mwendokosi vilivyochomwa, inajua idadi ya magari, pikipiki na majengo ambayo yamec...
01/12/2025

#“Serikali inajua idadi ya vituo vya Mwendokosi vilivyochomwa, inajua idadi ya magari, pikipiki na majengo ambayo yamechomwa lakin haijui Idadi ya watu waliouwawa kwenye maandamano Oktoba 29". , Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), Padre Charles Kitima

  NEWS | Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa waziri mkuu wa tanzania.Jina la Mwigulu ambaye ni M...
13/11/2025

NEWS | Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa waziri mkuu wa tanzania.

Jina la Mwigulu ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi limewasilishwa bungeni leo Novemba 13, 2025 ambapo wabunge wanatarajiwa kupiga kura ya kumthibitisha muda mfupi ujao.

  NEWS! Jioni hii Jeshi la Polisi limewaachia kwa dhamana viongozi wakuu wa Chama waliokuwa wanawashikilia, viongozi hao...
10/11/2025

NEWS!
Jioni hii Jeshi la Polisi limewaachia kwa dhamana viongozi wakuu wa Chama waliokuwa wanawashikilia, viongozi hao ni Mhe. John Heche (Makamu Mwenyekiti Bara) Mhe. Amani Golugwa (Naibu Katibu Mkuu Bara) Mhe. Godbless Lema (Mjumbe wa Kamati Kuu na Mhe. Boniface Jacob (Mwenyekiti Kanda ya Pwani).

 : SAMIA ATEUA WABUNGE WATANO, YUMO ABDULA AL MWINYI. RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Ha...
10/11/2025

: SAMIA ATEUA WABUNGE WATANO, YUMO ABDULA AL MWINYI. RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mamlaka aliyonayo chini ya Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, amewateua wafuatao kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kwa mujibu ya taarifa ya leo Novemba 10, 2025 iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi na kusainiwa na Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, alioteuliwa ni pamoja na Dkt. Dorothy Onesphoro Gwajima, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, Abdullah Ali Mwinyi, Balozi Khamis M***a Omar, Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho.

  Golugwa, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) bara, amekamatwa na jeshi la polisi, akiwa n...
08/11/2025

Golugwa, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) bara, amekamatwa na jeshi la polisi, akiwa nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

  Mgombea wa nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Tulia ...
08/11/2025

Mgombea wa nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Tulia Ackson, Novemba 7 2025 ametangaza rasmi kujiondoa katika kugombea nafasi hiyo.

  Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemteua aliyekuwa Mgombea Mwenza wa Urais kupitia CHAUMMA, Devotha Minja pamoja na S...
08/11/2025

Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemteua aliyekuwa Mgombea Mwenza wa Urais kupitia CHAUMMA, Devotha Minja pamoja na Sigrada Mligo kuwa Wabunge wa Viti Maalum wa chama hicho.

08/11/2025

la Polisi nchini kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limesema linaendelea na msako mkali wa kuwatafuta wale wote waliopanga, kuratibu na walioshiriki kuharibu mali za umma na za watu binafsi katika maeneo mbalimbali nchini Oktoba 29, 2025.

Aidha, limetangaza kuwa linawasaka Josephat Gwajima, Brenda Rupia, John Mnyika, Godbless Lema, Machuku Kadutu, Deogratius Mahinyila, Boniface Jacob, Hilda Newton, Award Kalonga na Amaan Golugwa huku likiwataka wajisalimishe mara moja.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uzalendo wa Kitanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Uzalendo wa Kitanzania:

Share