SMILE FM TZ

SMILE FM TZ Radio � Broadcasts, Advertisements production,Events plan

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI DAMBIA – HYDOM MANYARA.Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, imer...
14/03/2026

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI DAMBIA – HYDOM MANYARA.

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, imeridhisha na mradi wa maji Dambia Hydom, unaotekelezwa na Wakala wa Maji safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), wakiwa katika ziara ya kamati hiyo Mkoa wa Manyara.

Kamati hiyo, imeridhishwa baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa tangi la maji lililopo katika kijji cha Harsha kata ya Bashay, wilaya ya Mbulu lenye uwezo wa lita millioni mbili wenye thamani ya shilingi bilioni 41.2 fedha kutoka Serikali kuu na wafadhili unaotarajiwa kuhudumia jumla ya vijiji 21, ambapo mpaka sasa jumla ya vijiji vinne vimeanza kunufaika na mradi huo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jackson Kiswaga amesema wameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo na ubora wa kazi inayoendelea, ambapo ,ameahidi kuwa kamati ya Bunge itaishauri serikali kuongeza bajeti ya sekta ya maji ili kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi katika maeneo yote ya nchi, na kuwataka wananchi kuulinda mradi huo ili uweze kudumu kwa muda mrefu.

Akizungumza kwa niaba ya Seeikali, Mkuu wa Wilaya ya mbulu, Michael Semindu amesema Serikali wilayani humo itaendelea kusimamia na kulinda miundombinu ya mradi ili iwezeb kudumu na kuwahudumia wananchi kwa muda mrefu.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mhandisi Walter Kirita ameeleza mikakati ya kuwafikishia huduma ya maji kwa wananchi na namna wanayoshirikiana na serikali ya wilaya katika kuulinda mradi huo.

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Manyara, Mhandisi James Kionaumela amesema kupitia mradi huo, vijiji vinne vimeweza kukusanya mapato ya shilingi milion 1.2.

Cc.

HABARI MAALUM | CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI – DAR ES SALAAMDar es Salaam.Viongozi wa juu kutoka serikalini, sekta binafsi,...
14/03/2026

HABARI MAALUM | CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI – DAR ES SALAAM

Dar es Salaam.
Viongozi wa juu kutoka serikalini, sekta binafsi, taasisi za umma pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama wamehitimisha Kozi ya Viongozi wa Juu wa Serikali (Capstone Course) katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania – National Defence College (NDC).

Miongoni mwa wahitimu wa kozi hiyo ni mfanyabiashara na kiongozi wa sekta binafsi nchini, David Damian Mulokozi, ambaye alishiriki pamoja na viongozi wengine waandamizi wakiwemo Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali, viongozi wakuu wa taasisi za umma, maafisa waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.

Kozi hiyo ya kiwango cha juu huwaleta pamoja viongozi kutoka sekta mbalimbali za uongozi ili kujadili kwa kina masuala muhimu yanayohusu usalama wa taifa, uchambuzi wa mazingira ya kimkakati, uongozi wa kitaifa pamoja na mipango ya muda mrefu ya kulinda rasilimali na maslahi ya Tanzania.

Katika mafunzo hayo, washiriki walijadili pia nafasi ya uchumi wa taifa, maendeleo ya viwanda, teknolojia na usimamizi wa miundombinu muhimu ya kimkakati katika kuimarisha uthabiti wa taifa na kuharakisha maendeleo endelevu ya nchi.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa nyaraka za kuhitimu mafunzo hayo, Mulokozi alisema maarifa na uzoefu walioupata katika chuo hicho utasaidia kuimarisha uwezo wa viongozi katika kufanya maamuzi ya kimkakati yanayolenga kulinda na kuendeleza maslahi mapana ya taifa.

Amesema ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, taasisi za umma pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa taifa imara, lenye uchumi thabiti na usalama wa kudumu.

Kozi ya National Defence College (NDC) inahesabiwa kuwa miongoni mwa mafunzo ya juu ya kimkakati nchini yanayolenga kuandaa viongozi wenye uwezo wa kuchambua na kukabiliana na changamoto za kiusalama na maendeleo ya taifa katika dunia ya kisasa.

“Tanzania imara inajengwa kwa uongozi wenye maono, uzalendo na uwajibikaji wa pamoja,” alisema Mulokozi.

Ni EID VIBES FESTIVAL 🙌🙌 Unapangaje kukosa?? Kutakuwa na burudani Baaabkubwa, Vuta picha huku yupo Dogo Janja ukigeuka u...
10/03/2026

Ni EID VIBES FESTIVAL 🙌🙌 Unapangaje kukosa??

Kutakuwa na burudani Baaabkubwa, Vuta picha huku yupo Dogo Janja ukigeuka unakutana na Fido Vato 🔥🔥🔥🙌 huku Mikono ya Dj Mkali DJ PEK ikihusika 🫰

Hii si ya kukosa, Taarifa hii ikufikie mkazi wa Manyara na Viunga vyake, mwambie mwenzako amwambie mwenzake kuwa burudani hii utaipata AYAREN LIFE STYLE HOTEL kwa udhamini wa Mati superbrand Ltd, CRDB bank pamoja na Redio yako namba moja Smile Fm 🙌

Usipange Kukosa 🔥🙏

Cc.




Hongera kwa wanawake wote wanaofanya dunia kuwa bora zaidi.Cc.
08/03/2026

Hongera kwa wanawake wote wanaofanya dunia kuwa bora zaidi.

Cc.

Smile FM Radio inakutakia heri ya siku yako ya kuzaliwa! 🎉🎂Tunakutakia afya njema, furaha tele na mafanikio katika kila ...
06/03/2026

Smile FM Radio inakutakia heri ya siku yako ya kuzaliwa! 🎉🎂

Tunakutakia afya njema, furaha tele na mafanikio katika kila hatua ya maisha yako. Mungu akuzidishie miaka mingi yenye baraka, upendo na mafanikio. Endelea kuwa baraka kwa wengine.



WAKALI WA LOCATION 🫰Hapa ni wapi??
05/03/2026

WAKALI WA LOCATION 🫰

Hapa ni wapi??

Mwamuzi wa kati Nassoro Mwinchui kutoka mkoani Tanga amekabidhiwa Dabi ya Yanga na Simba inayotarajiwa kupigwa kwenye Uw...
27/02/2026

Mwamuzi wa kati Nassoro Mwinchui kutoka mkoani Tanga amekabidhiwa Dabi ya Yanga na Simba inayotarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar Jumapili Machi 1, 2026 kwenye Uwanja wa New Amaan.

Kwa mujibu wa ratiba ya waamuzi iliyotolewa leo Ijumaa Februari 27, 2026, pambano hilo linatarajiwa kuchezwa saa 2:15 usiku huku Mwinchui akisaidiwa na waamuzi wasaidizi Kassim Mpanga (Dar es Salaam) na Hamdan Saidi (Mtwara).

Mwamuzi wa akiba katika mchezo huo atakuwa Ramadhan Kayoko (Dar es Salaam).




Takwimu za michezo sita baina ya Yanga na Simba:• Simba 1–5 Yanga• Yanga 2–1 Simba• Yanga 1–0 Simba• Simba 0–1 Yanga• Ya...
27/02/2026

Takwimu za michezo sita baina ya Yanga na Simba:

• Simba 1–5 Yanga
• Yanga 2–1 Simba
• Yanga 1–0 Simba
• Simba 0–1 Yanga
• Yanga 2–0 Simba
• Yanga 1–0 Simba

Jumapili kinaumana, unaona timu gani ikifanya vizuri Katika mchezo huo?? Maoni yako yatasomwa kwenye KAMATI YA MICHEZO ya Smile FM kuanzia Saa 8:00 Mchana 📌

klabu ya Yanga imeibuka na ushindi mnono wa mabao (5-0) dhidi ya maafande JKT Tanzania na kurejea kileleni kwenye msimam...
26/02/2026

klabu ya Yanga imeibuka na ushindi mnono wa mabao (5-0) dhidi ya maafande JKT Tanzania na kurejea kileleni kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Mohamed Hussein Zimbwe JR, Laurindo Dilson Maria Aurelio "Depu",Mudathir Yahya Abbas,Prince Dube pamoja na Shekhan Khamis.

Yanga imefikisha alama (28) baada ya kucheza michezo (10) wakishinda mechi (9) na suluhu/sare (1) huku wakifunga jumla ya mabao (27) na kuruhusu nyavu zao kutikiswa mara (2) pekee.

TAKWIMU ZA YANGA KWENYE MECHI ZAKE (10) ZA NBCPL 2025/26

Mechi= 10
Ushindi= 09
Sare/Suluhu= 01
Kupoteza= 00
Alama= 28
Mabao ya Kufunga= 25
Mabao ya Kufungwa= 02

NB: Kituo kinachofuata ni Zanzibar kwenye Derby ya Kariakoo, Wataleta timu??

Cc:

Haya hapa madhara ya Mvua Kubwa na upepo mkali unaoendelea katika maeneo mbalimbali ya mji wa Babati 🙌Tupo imara katika ...
26/02/2026

Haya hapa madhara ya Mvua Kubwa na upepo mkali unaoendelea katika maeneo mbalimbali ya mji wa Babati 🙌

Tupo imara katika kuhakikisha haupitwi na jambo lolote, endelea kusikiliza Smile FM Radio kila siku kupitia Masafa ya 95.3 lakini tufuatilie katika mitandao yetu yote ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali za uhakika 📌🙏

2026 FANYA KWELI 🫰

25/02/2026

Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Manyara, Michael Mwakasungula amewataka madereva wa serikali kuzingatia Sheria na kanuni za Usalama Barabarani.

Wito huo ameutoa wakati akizungumza katika kipindi cha TUBONGE cha Smile FM Radio.

Katika mazungumzo hayo, amesema kuwa inaleta picha mbaya kwa gari la serikali kuvunja Sheria zilizowekwa na serikali hivyo amewataka madereva hao kuwa mfano bora wa kufuata Sheria za Usalama Barabarani ili jamii iweze kutii Sheria hizo.

Sikiliza Smile FM Radio kila siku kupitia Masafa ya 95.3 ili uwe wa Kwanza kuhabarika, tufuate pia kwenye mitandao yetu yote ya kijamii Instagram, Facebook, YouTube na TikTok kwa habari mbalimbali za uhakika.

Cc.

Address

Negamsi
Babati
255

Opening Hours

Monday 05:00 - 00:00
Tuesday 05:00 - 00:00
Wednesday 05:00 - 00:00
Thursday 05:00 - 00:00
Friday 05:00 - 00:00
Saturday 05:00 - 00:00
Sunday 05:00 - 00:00

Telephone

+255684728971

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SMILE FM TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SMILE FM TZ:

Share

Category