14/03/2026
KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI DAMBIA – HYDOM MANYARA.
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, imeridhisha na mradi wa maji Dambia Hydom, unaotekelezwa na Wakala wa Maji safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), wakiwa katika ziara ya kamati hiyo Mkoa wa Manyara.
Kamati hiyo, imeridhishwa baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa tangi la maji lililopo katika kijji cha Harsha kata ya Bashay, wilaya ya Mbulu lenye uwezo wa lita millioni mbili wenye thamani ya shilingi bilioni 41.2 fedha kutoka Serikali kuu na wafadhili unaotarajiwa kuhudumia jumla ya vijiji 21, ambapo mpaka sasa jumla ya vijiji vinne vimeanza kunufaika na mradi huo.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jackson Kiswaga amesema wameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo na ubora wa kazi inayoendelea, ambapo ,ameahidi kuwa kamati ya Bunge itaishauri serikali kuongeza bajeti ya sekta ya maji ili kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi katika maeneo yote ya nchi, na kuwataka wananchi kuulinda mradi huo ili uweze kudumu kwa muda mrefu.
Akizungumza kwa niaba ya Seeikali, Mkuu wa Wilaya ya mbulu, Michael Semindu amesema Serikali wilayani humo itaendelea kusimamia na kulinda miundombinu ya mradi ili iwezeb kudumu na kuwahudumia wananchi kwa muda mrefu.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Mhandisi Walter Kirita ameeleza mikakati ya kuwafikishia huduma ya maji kwa wananchi na namna wanayoshirikiana na serikali ya wilaya katika kuulinda mradi huo.
Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Manyara, Mhandisi James Kionaumela amesema kupitia mradi huo, vijiji vinne vimeweza kukusanya mapato ya shilingi milion 1.2.
Cc.