SMILE FM TZ

SMILE FM TZ Radio � Broadcasts, Advertisements production,Events plan

⚽🔥 Jana ilikuwa   … wiki hii tunasubiri  !👉 Swali ni moja tu: nani ata funika zaidi mwaka huu? 🤔Tuambie maoni yako hapa ...
11/09/2025

⚽🔥 Jana ilikuwa … wiki hii tunasubiri !
👉 Swali ni moja tu: nani ata funika zaidi mwaka huu? 🤔

Tuambie maoni yako hapa 👇

Taasisi isiyo ya serikali ya Mati foundation,imekabidhi pikipiki zinazotumia nishati ya umeme kwa watu wenye ulemavu mko...
09/09/2025

Taasisi isiyo ya serikali ya Mati foundation,imekabidhi pikipiki zinazotumia nishati ya umeme kwa watu wenye ulemavu mkoa wa Manyara ili kuwasaidia kufanya shughuli zao kwa ufanisi.

Hafla ya makabidhiano imeongozwa na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Mati super brand ltd,inayozalisha na kusambaza vinywaji changamshi,David Mulokozi ambaye amekiri watu wenye mahitaji maalumu katika jamii wanahitaji kujenga uchumi na kustawi.

“ Mati super brand tumekabidhi pikipiki kwa mati foundation kwa ajili ya ndugu zetu wenye ulemavu hasa ziwasaidie katika shughuli zao”..Mulokozi.

MATI TECHNOLOGIES LTD YALETA MAPINDUZI TEKNOLOJIA YA NDEGE NYUKI DRONE.Kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kampuni ...
03/09/2025

MATI TECHNOLOGIES LTD YALETA MAPINDUZI TEKNOLOJIA YA NDEGE NYUKI DRONE.

Kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kampuni tanzu Mati Technologies imekuja na teknolojia ya kisasa ya Ndege nyuki (drone) kwa ajili ya sekta ya kilimo na huduma nyingine za kijamii ili kuongeza ufanisi.

Hatua hii inalenga kuongeza tija, kupunguza gharama na kurahisisha kazi kwa wakulima na taasisi mbalimbali nchini.

Akizungumzia hatua hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Mati Group of Companies, Bw. David Mulokozi, amesema kampuni hiyo imeamua kuwekeza kwenye teknolojia ya drone zitakazotumika kunyunyizia dawa mashambani, kupima maeneo, kupanda mbegu, kusafirisha mizigo, kusaidia kaguzi mbalimbali nk.

Mulokozi ameeleza kuwa drone hizo zinazotengenezwa ndani ya nchi zitauzwa kuanzia shilingi milioni 17 kulingana na mahitaji ya mteja, hali itakayowawezesha wakulima wengi kuzimudu kulinganisha na Gharama kubwa za uagizaji bidhaa hizo nje ya nchi.

Mkuu wa wilaya ya Babati,Emmanuela Kaganda amesema mwenge wa uhuru utazindua jengo la kisasa la utawala lilipopo Bagara ...
14/07/2025

Mkuu wa wilaya ya Babati,Emmanuela Kaganda amesema mwenge wa uhuru utazindua jengo la kisasa la utawala lilipopo Bagara ziwani.

Kaganda ameeleza hayo wakati akifafanua ujenzi wa miradi hiyo kwa wana habari,ambapo amebainisha jengo hilo la ofisi ya utawala limejengwa na wananchi kwa kushirikiana na halmashauri.

"tutatembelea ofisi za serikali ya mtaa zilizojengwa na nguvu za wananchi kwa kushirikiana na halmashauri bagara hapa ziwani"Kaganda.

Kaganda ameongeza kuwa mwenge wa uhuru utatembelea miradi 16 katika halmashauri zote za wilaya hiyo,ambapo miradi 8 mjini na mengine 8 vijijini.

Hata hivyo miradi mitano itawekewa mawe ya msingi,miradi mitano itazinduliwa na miradi mingine itakayosalia itashuhudiwa na mwenge wa uhuru.

Miradi yote katika halmashauri zote mbili za wilaya ya Babati imetumia takribani bilioni 10.

Mwenge wa uhuru utapokelewa Galapo katika halmashauri ya Babati vijijini.

Mkurugenzi wa shirika la KINNAPA, Abraham Akilimali, ametoa wito kwa waandishi wa habari na jamii kuendeleza kampeni ya ...
02/07/2025

Mkurugenzi wa shirika la KINNAPA, Abraham Akilimali, ametoa wito kwa waandishi wa habari na jamii kuendeleza kampeni ya kuhamasisha sera ya kuwarejesha watoto wa k**e shuleni, akisema ni muhimu wazazi waelimishwe kuhusu haki hiyo. Amepongeza waandishi wa habari kwa mchango wao katika kufichua visa vya ukatili na kusaidia jamii kuelewa umuhimu wa elimu kwa mtoto wa k**e.

Afisa maendeleo wa KINNAPA, Paulina Ngurumwa, amesema kupitia mfuko wa kusaidia watoto wa k**e waliokatiza masomo, wamefanikiwa kuwapatia cherehani tano k**a mtaji wa kuwawezesha kiuchumi. Afisa maendeleo ya jamii wa mkoa, Lilian Bujune, amepongeza juhudi za shirika hilo katika kuanzisha mabaraza na vilabu vya watoto ili kupaza sauti dhidi ya ukatili.

Mathias Focus, Afisa Ustawi wa Jamii Babati Mji, amesema ukatili wa kijinsia unafumbiwa macho na jamii kutokana na changamoto za kiuchumi na mila kandamizi, huku akisisitiza umuhimu wa kuripoti. Takwimu zinaonesha kupungua kwa visa vya ukatili kutoka 330 mwaka 2022 hadi 56 katika nusu ya kwanza ya 2025.

Afisa elimu taaluma Babati DC, Judith Fransis Materu, amesema wanafunzi 21 wameweza kurejea shuleni, wakiwemo wasichana 10, na amempongeza Rais Samia kwa kuruhusu mashirika kusaidia elimu ya mtoto wa k**e.

Shirika la KINNAPA kupitia miradi yake ya JOINT ACTION GRANT (JUG) na EDUCATION CHAMPION NETWORK (ECN) - NIPE NAFASI, linaendeleza juhudi za kuwarejesha watoto wa k**e waliokatisha masomo kwa kuwawezesha kielimu na kiuchumi, likilenga kuongeza uelewa wa jamii na kushawishi serikali kuongeza bajeti ya elimu. Kwa zaidi ya miaka 30, KINNAPA limekuwa likitekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali.

Leo hii tunapita kwenye Instagram akaunti ya Koplo Gabariel aka Nyumbu Mjanja  anayo mengi ya kusimulia.Usikose kuanzia ...
22/06/2025

Leo hii tunapita kwenye Instagram akaunti ya Koplo Gabariel aka Nyumbu Mjanja anayo mengi ya kusimulia.Usikose kuanzia Saa 4 hadi 5 Asubuhi kupitia Smile FM 95.3 Manyara . Host wako ni Muziki

♦️Mara ya kwanza kufika Dar mwenyeji wake alimzimia simu,baadae kuibiwa na kushuhudia misala kibao ndani ya jiji la Dar....
08/06/2025

♦️Mara ya kwanza kufika Dar mwenyeji wake alimzimia simu,baadae kuibiwa na kushuhudia misala kibao ndani ya jiji la Dar.
♦️ *Lakini anasema haondoki Dar*

Msanii anafunguka yote kwenye THE CHECKUP Jumapili hii kupitia SMILE FM 95.3 Dodoma Saa 4-5 Asubuhi
Ngoma 5 kutoka Trend ya AudioMack zinaongeza burudani

Host wako ni na Musiki

DUDE   Ametambulishwa zaidi katika nafasi ya tapeli kwenye uigizaji,jambo ambalo mtaani inampa wakati mgumu kuaminika.La...
01/06/2025

DUDE
Ametambulishwa zaidi katika nafasi ya tapeli kwenye uigizaji,jambo ambalo mtaani inampa wakati mgumu kuaminika.Lakini ni Mpenzi wa Soka na Shabiki wa Yanga. Wiki hii kupitia post zake za Instagram tutazungumza
🔸Social media
🔸Soka
🔸Utapeli
🔸Maisha
Top 5 ya ngoma za Soka Zilizotazamwa zaidi kupitia Youtube zitagonga speaker zako pia.Jumapili hii Saa 4-5 Asubuhi kwenye Radio yako SMILE FM 95.3 Manyara

Hosted by Music Report

TUNAKUKARIBISHA*KUSIKILIZA @ Smile FM 95.3 MHZJumatano 28/05/2025Saa 11:00JioniTutakua  na Samuel MandariAfisa Uhusiano ...
27/05/2025

TUNAKUKARIBISHA
*KUSIKILIZA @ Smile FM 95.3 MHZ

Jumatano 28/05/2025
Saa 11:00Jioni

Tutakua na
Samuel Mandari
Afisa Uhusiano – TANESCO Manyara

Ataelezea jinsi ya:
⚡ Kuomba umeme kwa kutumia simu
📲 Kupitia App ya NIKONEKT au *152*00 #
💬 Kuwasiliana na TANESCO kwa njia ya simu bila malipo kwa namba 180.

👂 Sikiliza! Usipitwe!

25/05/2025
Huu ndio ukweli kuhusu PHD ya Msanii Chemical♦️Mafanikio♦️Elimu♦️MuzikiLive kutoka Scotland UK  anazungumza kwa mara ya ...
18/05/2025

Huu ndio ukweli kuhusu PHD ya Msanii Chemical
♦️Mafanikio
♦️Elimu
♦️Muziki
Live kutoka Scotland UK anazungumza kwa mara ya kwanza na kwenye THE CHECKUP huku tukisikiliza ngoma 5 zinazofanya vizuri UK (Official HipHop and R&B Single Chart)

Jumapili hii Tarehe 18 Mei 2025 hapa Smile FM 95.3 Manyara kuanzia saa 4:00-5:00 Asubuhi


Address

Negamsi
Babati
255

Opening Hours

Monday 05:00 - 00:00
Tuesday 05:00 - 00:00
Wednesday 05:00 - 00:00
Thursday 05:00 - 00:00
Friday 05:00 - 00:00
Saturday 05:00 - 00:00
Sunday 05:00 - 00:00

Telephone

+255684728971

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SMILE FM TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SMILE FM TZ:

Share

Category