02/02/2020
Shalom wana wa Mungu.
Somo la Jana👇
UZIMA WA MILELE/WOKOVU WA MILELE
Tuanze na Yohana 3:16
"Ili kila amwaminiye asipotee Bali awe na uzima wa milele"
Katika uzima tuliopewa na Kristo k**a matokeo ya Ku mwamini, tumepewa huu uzima milele. Uzima katika Kristo tuko nao milele.
Sio uzima wa Siku kadhaa, halafu ni uzima ambao tunao kwa kuamini tu, sio kwa matendo yetu, k**a ni hivi mwamini huna matendo ya kufanya ili huu uzima uendelee kuwepo kwako. Mpango wa Baba ni kwamba ukimuamini anakupa uzima wote wote, sio wa mkopo, wala hakupi uzima ulifungamanishwa na majukumu ya kuutunza kwa matendo au kwa kutotenda.
K**a ambavyo tumeupokea uzima bure kwa kuiamini kazi ya msalaba, unakaa milele bure, ndio maana ni uzima wa milele
Ndio maana Warumi 8:1 anasema
1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
Uzima wa milele na hukumu havikai sehemu moja
Yohana 3:16
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Anasema kila amwaminiye asipotee, Bwana Yesu sio mwongo, k**a umemwamini Kristo hakuna kupotea unao uzima wa milele,
Na hupotei kwa sababu njia ya kwenda kwa Baba ni Yesu Kristo, anasema yeye ndiye njia na kweli na uzima mtu haendi kwa Baba isipokuwa kwa njia ya yeye, ndio maana yoyote anaeifuata njia ya Kristo hajapotea amefika kwa Baba.