FABI Sports ANGLE

FABI Sports ANGLE Pata Taarifa mbalimbali za Michezo
(1)

Matokeo ya mechi zote za jana michuano ya Kombe la Dunia ngazi ya klabu
20/06/2025

Matokeo ya mechi zote za jana michuano ya Kombe la Dunia ngazi ya klabu


01/06/2025
LIGI Kuu ya NBC, Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika  itarejea Mei 2 kwa mchezo kati ya Simba itakayokuwa mwenyeji wa...
30/04/2025

LIGI Kuu ya NBC, Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika itarejea Mei 2 kwa mchezo kati ya Simba itakayokuwa mwenyeji wa timu ya Mashujaa kutoka mkoani Kigoma.

Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa KMC Complex uliopo mkoani Dar es Salaam ikiwa ni mchezo wa mzunguko wa 24 uliosogezwa kutokana na timu ya Simba kuwa na ratiba ya michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Baada ya mchezo huo timu ya Simba itakuwa na kibarua kingine ugenini katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar watakapokutana na timu ya JKT Tanzania waliyoifunga 1-0 kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza kwa bao la Jean Ahoua aliefunga kwa mkwaju wa penati dakika za nyongeza.

Mei 8 itaikaribisha timu ya Pamba katika uwanja wa KMC Complex kabla ya kwenda ugenini kuvaana na timu ya KMC kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.

Tanzania Football Federation

BASHUNGWA AFUNGUA LIGI YA DK. SAMIA & KYOMBO - MISSENYIWaziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb), a...
19/04/2025

BASHUNGWA AFUNGUA LIGI YA DK. SAMIA & KYOMBO - MISSENYI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb), amezindua Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Dk. Samia & Kyombo Cup 2025 katika Uwanja wa Mashujaa, Bunazi, wilayani Missenyi, mkoani Kagera, leo tarehe 19 Aprili 2025.

Mashindano hayo yameandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Missenyi, Dkt. Florent Laurent Kyombo, na yanatarajiwa kushirikisha timu 20 kutoka kila kata ya wilaya hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Bashungwa amesema kuwa mashindano hayo yatasaidia kuibua vipaji vya michezo kwa vijana, kuimarisha afya, kuendeleza mshikamano na kudumisha upendo miongoni mwa vijana na wakazi wa Wilaya ya Missenyi.

“Mhe. Mbunge kwa kushirikiana na Madiwani wameonyesha dhamira ya dhati katika maendeleo ya michezo ndani ya Wilaya ya Missenyi. Ligi hii siyo tu burudani bali pia ni fursa kwa vipaji chipukizi. Naomba vijana kutoka kata zote 20 mshiriki kwa moyo wa upendo na mshikamano,” alisema Mhe. Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa ametoa wito kwa waamuzi na wasimamizi wa mashindano hayo kuhakikisha wanatenda haki wakati wa michezo yote, ili ligi hiyo imalizike kwa amani na kutimiza malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Missenyi, Dkt. Florent Kyombo, amesema kuwa mashindano hayo yanalenga kuimarisha mahusiano na mshikamano kati ya vijana na wananchi wa kata zote 20 za wilaya hiyo.

Katika hafla ya uzinduzi, ambayo ilizikutanisha timu za kata za Kyaka na Mtukula, timu zote shiriki zilipatiwa vifaa mbalimbali vya michezo, ikiwemo jezi, mipira, vifaa vya mazoezi, pamoja na fedha kwa ajili ya maandalizi ya mechi.

MAFUNZO YA VARKozi maalum ya Teknolojia ya Msaidizi wa Video (VAR) iliyofanyika kwa takribani siku 5 kwenye ukumbi wa uw...
18/04/2025

MAFUNZO YA VAR

Kozi maalum ya Teknolojia ya Msaidizi wa Video (VAR) iliyofanyika kwa takribani siku 5 kwenye ukumbi wa uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam imefungwa rasmi leo Aprili 18, 2025 ikijumisha waamuzi 20 kutoka Tanzania Bara na Visiwani ikiwa ni mwendelezo wa Kozi hiyo yenye jumla ya moduli 6 mpaka kuhitimisha.

Kozi hiyo ambayo ni sehemu ya mkakati wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuhakikisha nchi inakuwa na waamuzi waliobobea kwenye matumizi ya teknolojia hiyo ya kisasa inayotumika kusaidia kutoa maamuzi sahihi uwanjani imefungwa rasmi Kwa awamu ya pili na Mkurugenzi wa Sheria, Habari na Masoko wa TFF Boniface Wambura ambaye pia ndio msimamizi Mkuu wa Kozi hiyo inayowezeshwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Akizungumza baada ya kufunga rasmi awamu ya pili ya Kozi hiyo Mkurugenzi wa Sheria, Habari na Masoko wa TFF, Boniface Wambura aliwapongeza waamuzi waliomaliza mafunzo hayo na kuwataka kwenda kutumia vyema ujuzi walioupata kwa maendeleo ya soka la Tanzania.

Aidha Wambura alieleza kuwa Kozi hiyo ni mwendelezo na kwamba TFF itaendelea kuwekeza kwenye teknolojia hiyo Kwa kutoa elimu Kwa waamuzi wengi zaidi na hata kuzalisha wakufunzi wazawa ili kuhakikisha usimamizi wa mechi nchini unaendana sawa na mabadiliko kulingana na wakati Kwa kufuata viwango vya kimataifa.

“Tunahitaji kuona mabadiliko chanya kwenye usimamizi wa mechi nchini, hivyo kupitia VAR tunaamini tutapunguza malalamiko dhidi ya waamuzi.

Ikumbukwe kozi hiyo ni hatua muhimu kuelekea maandalizi ya matumizi rasmi ya VAR katika mechi za ligi kuu ya NBC na mashindano mbalimbali yatakayofanyika ndani ya Tanzania.

Tanzania Football Federation

VIKOSI MECHI ZA LEO Real Madrid C.F.  VS Arsenal Inter  VS
16/04/2025

VIKOSI MECHI ZA LEO

Real Madrid C.F. VS Arsenal

Inter VS

Arsenal become the first team EVER to score seven goals in an away Champions League knockout match! They beat PSV 7-1 in...
05/03/2025

Arsenal become the first team EVER to score seven goals in an away Champions League knockout match! They beat PSV 7-1 in their last 16 first leg! 😲

FFABI Sports ANGLE@ Clavery

UEFA CHAMPIONS
05/03/2025

UEFA CHAMPIONS

Kocha mpya wa Kagera Sugar FCFabius Clavery
05/03/2025

Kocha mpya wa Kagera Sugar FC

Fabius Clavery

Huu hapa ‘Mkeka’ wa wasimamizi wa   🔥       TTBConlineTTanzania Football Federation
05/03/2025

Huu hapa ‘Mkeka’ wa wasimamizi wa 🔥


TTBConlineTTanzania Football Federation

REAL SOCIEDAD 🇪🇸 VS MAN UTD🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿
21/02/2025

REAL SOCIEDAD 🇪🇸 VS MAN UTD🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿



Address

Bukoba

Telephone

+255756321374

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FABI Sports ANGLE posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to FABI Sports ANGLE:

Share