Radio Mbiu

Radio Mbiu Karibu tushirikiane

Ni Ukurasa wa Kituo cha Radio Mbiu inayopatikana Mkoani Kagera katika masafa ya 104.9 Fm, na ukurasa huu unakupatia habari mbali mbali ya kile kinachojiri ndani na nje ya mkoa wa Kagera katika matukio ya Dini na Kijamii..

KHERI KWA SIKU YA KUZALIWA Tuungane kuwatakia kheri na matashi mema kwa tarehe mfanano ya kuzaliwa, Padre Benedict Kweya...
08/06/2026

KHERI KWA SIKU YA KUZALIWA
Tuungane kuwatakia kheri na matashi mema kwa tarehe mfanano ya kuzaliwa, Padre Benedict Kweyamba, Paroko Msaidizi Parokia ya Ilemera Jimbo Katoliki Bukoba na Padre Deogratias Rweyemamu, ambaye yupo mapumziko nyumba ya kulea wazee St. Oscar, Parokia ya Kagondo, Jimbo Katoliki Bukoba.

Kheri ya mwaka mpya Padre Benedict Kweyamba na Padre Deogratias Rweyemamu, Mungu awajalie afya njema na Mama Maria azidi kuwabeba katika utume wenu.
www.radiombiu.co.tz

Karibu tusali Sala ya Malaika wa Bwana na Sala ya Mchana, tunaongozwa na Masista wanao soma Chuo Kikuu Kishiriki cha Mwe...
08/06/2026

Karibu tusali Sala ya Malaika wa Bwana na Sala ya Mchana, tunaongozwa na Masista wanao soma Chuo Kikuu Kishiriki cha Mwenyeheri Maria Jordan, Jimbo Katoliki Morogoro.

Studio upo na Brigitha Msasalaga

Karibu ushiriki kipindi cha Salam za Pole au Pongezi, ambapo utawatakia neno la pongezi ndugu ,jamaa na rafiki kwa neema...
08/06/2026

Karibu ushiriki kipindi cha Salam za Pole au Pongezi, ambapo utawatakia neno la pongezi ndugu ,jamaa na rafiki kwa neema na Baraka anazo jaliwa na Mwenyezi Mungu, pia utapata nafasi ya kumpa pole ndugu, jamaa na rafiki anayepitia changamoto mbalimbali za kimaisha.

Studio upo na Brigitha Msasalaga

Mtakatifu Medard, AskofuMtakatifu Medard, alizaliwa mwaka 456 huko Salency,  Ufaransa. Baba yake aliitwa Nectard na mama...
08/06/2026

Mtakatifu Medard, Askofu
Mtakatifu Medard, alizaliwa mwaka 456 huko Salency, Ufaransa. Baba yake aliitwa Nectard na mama yake Protogia. Walikuwa miongoni mwa familia zilizoheshimika.

Mtakatifu Medard alikuwa na tabia njema, akimcha Mungu tokea utotoni mwake. Alikuwa mwema kwa maskini. Hata chakula chake alichotayarishiwa akiwa katika kuchunga wanyama wa baba yake malishoni, alikuwa akigawana na wale wasio na chakula.

Mtakatifu Medard, alisoma maandiko matakatifu chini ya uangalizi wa Askofu wa jimbo, ambaye alishangazwa sana na ufahamu wake.

Mwaka 490 Mtakatifu Medard alipata daraja la upadri na mwaka 530, alipata daraja la Uaskofu na kuwa Askofu wa Vermand. Baadae alihamia katika jimbo la Noyons ambalo lilikuwa salama, kutokana na uvamizi wa kabila za Huns na Vandals.

Papa Hormisdas alimuhamisha tena kwenda jimbo la Tournai, ambako alifanya kazi njema, na kubatiza wenyeji wengi waliokuwa wapagani. Aliheshimiwa pia na mfalme Clotaire.

Mtakatifu Medard alikufa mwaka 545 baada ya kuugua kwa muda.

Watakatifu wengine wa leo ni
Mt. William wa York
Mt. Bron
Mt. Calliope
Mt. Clodulf wa Metz
Mt. Edgar wa amani
Mt. Eustadiola
Mt. Gildard
Mt. Heraclius wa Sens
Mt. Jacques Berthieu
Mt. Levan
Mt. Maximinus wa Aix
Mt. Melania
Mt. Muirchu
M/h. Pacificus wa Cerano
Mt. Robert wa Frassinoro
Mt. Sallustian
Mt. Severinus
Mtakatifu Medard, Wenyeheri na Watakatifu wengine wote wa leo, mtuombee.
www.radiombiu.co.tz

Karibu tusali Sala ya Rozari Takatifu ya Fatima,  Matendo ya Furaha , tunaongozwa na familia ya Ladislaus Chang'a, Jumui...
08/06/2026

Karibu tusali Sala ya Rozari Takatifu ya Fatima, Matendo ya Furaha , tunaongozwa na familia ya Ladislaus Chang'a, Jumuiya ya Bikira Maria Malkia wa Amani, Kigango cha Bikira Maria Mpalizwa Mbinguni, Parokia ya Mtakatifu Yohane Mtume Kikuyu Jimbo kuu la Dodoma.

Studio upo na Brigitha Msasalaga

07/06/2026

PICHA JONGEFU|| MASIFU YA JIONI NTUNGAMO SEMIARI -BUKOBA

Neno la Shukrani na pongezi kutoka kwa Fratel na Padre, wakati wa Ibada ya Masifu ya Jioni, Seminari Kuu ya Mtakatifu Anthony wa Padua- Ntungamo, ibada iliyoambatana na kukabidhi mchango wa kuwezesha utume wa Radio Maria Tanzania, katika Kampeni ya Mariathon 2026, Jimbo Katoliki Bukoba.
www.radiombiu.co.tz

Asante kwa kuendelea kuisikiliza Radio Mbiu sauti ya Faraja kupitia Masafa ya 104.9 fm kutoka Bunena Manispaa ya Bukoba ...
07/06/2026

Asante kwa kuendelea kuisikiliza Radio Mbiu sauti ya Faraja kupitia Masafa ya 104.9 fm kutoka Bunena Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera hapa nchini Tanzania.

Karibu uwalaze unono Ndugu, Jamaa, na Rafiki popote pale walipo kupitia kipindi chako pendwa cha Njozi njema.
Ushiriki wako ni muhimu sana. Karibu

www.radiombiu.co.tz

Studio: Datius-Dismas

07/06/2026

NIMRUDISHIE BWANA NINI KASHERERO -BUKOBA

Karibu utazame wimbo wa shukrani ulivyoimbwa na kwaya ya kigango cha Nshambya wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukrani ya Mavuno ya Familia ya Ma Consolatha Medard, Rafiki wa Radio Maria Tanzania Jimbo Katoliki Bukoba.

Misa Takatifu imeadhimishwa na Padre Egidius Rweyemamu, Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Karoli Lwanga - Kasherero, Jimbo Katoliki Bukoba.

Endelea kusikiliza Radio Maria Tanzania kupitia Masafa;
Bukoba 104.9 FM, Musoma 92.9 FM, Bunda 92.9 FM, Bariadi 95.5 FM, Shinyanga 99.9 FM, Kayanga 102.5 FM, Rulenge Ngara 102.5 FM, Geita 106.1 FM, Mwanza 106.1 FM
www.radiombiu.co.tz



.kampuni100200
(15)

Asante kwa kuendelea kuisikiliza Radio Mbiu sauti ya Faraja kupitia Masafa ya 104.9 fm kutoka Bunena Manispaa ya Bukoba ...
07/06/2026

Asante kwa kuendelea kuisikiliza Radio Mbiu sauti ya Faraja kupitia Masafa ya 104.9 fm kutoka Bunena Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera hapa nchini Tanzania.

karibu katika kipindi cha Nena nami Bwana.

www.radiombiu.co.tz

Studio: Datius-Dismas

Address

Bunena
Bukoba
35101

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00
Saturday 08:00 - 16:00
Sunday 09:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Mbiu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Mbiu:

Share

Category