08/06/2026
Mtakatifu Medard, Askofu
Mtakatifu Medard, alizaliwa mwaka 456 huko Salency, Ufaransa. Baba yake aliitwa Nectard na mama yake Protogia. Walikuwa miongoni mwa familia zilizoheshimika.
Mtakatifu Medard alikuwa na tabia njema, akimcha Mungu tokea utotoni mwake. Alikuwa mwema kwa maskini. Hata chakula chake alichotayarishiwa akiwa katika kuchunga wanyama wa baba yake malishoni, alikuwa akigawana na wale wasio na chakula.
Mtakatifu Medard, alisoma maandiko matakatifu chini ya uangalizi wa Askofu wa jimbo, ambaye alishangazwa sana na ufahamu wake.
Mwaka 490 Mtakatifu Medard alipata daraja la upadri na mwaka 530, alipata daraja la Uaskofu na kuwa Askofu wa Vermand. Baadae alihamia katika jimbo la Noyons ambalo lilikuwa salama, kutokana na uvamizi wa kabila za Huns na Vandals.
Papa Hormisdas alimuhamisha tena kwenda jimbo la Tournai, ambako alifanya kazi njema, na kubatiza wenyeji wengi waliokuwa wapagani. Aliheshimiwa pia na mfalme Clotaire.
Mtakatifu Medard alikufa mwaka 545 baada ya kuugua kwa muda.
Watakatifu wengine wa leo ni
Mt. William wa York
Mt. Bron
Mt. Calliope
Mt. Clodulf wa Metz
Mt. Edgar wa amani
Mt. Eustadiola
Mt. Gildard
Mt. Heraclius wa Sens
Mt. Jacques Berthieu
Mt. Levan
Mt. Maximinus wa Aix
Mt. Melania
Mt. Muirchu
M/h. Pacificus wa Cerano
Mt. Robert wa Frassinoro
Mt. Sallustian
Mt. Severinus
Mtakatifu Medard, Wenyeheri na Watakatifu wengine wote wa leo, mtuombee.
www.radiombiu.co.tz