Radio Mbiu

Radio Mbiu Karibu tushirikiane

Ni Ukurasa wa Kituo cha Radio Mbiu inayopatikana Mkoani Kagera katika masafa ya 104.9 Fm, na ukurasa huu unakupatia habari mbali mbali ya kile kinachojiri ndani na nje ya mkoa wa Kagera katika matukio ya Dini na Kijamii..

Karibu Msikilizaji katika marudio ya kipindi cha Ijue Litrujia ya Kanisa katoliki.www.radiombiu.co.tz104.9fm
29/10/2025

Karibu Msikilizaji katika marudio ya kipindi cha Ijue Litrujia ya Kanisa katoliki.
www.radiombiu.co.tz
104.9fm

Mtakatifu Alphonsus RodriguezMtakatifu Alphonsus Rodriguez alizaliwa tarehe 25 Julai 1532 huko Segovia, Hispania. Baba y...
29/10/2025

Mtakatifu Alphonsus Rodriguez
Mtakatifu Alphonsus Rodriguez alizaliwa tarehe 25 Julai 1532 huko Segovia, Hispania. Baba yake alikuwa mfanyabiashara.

Alisoma katika shule ya wa Jesuit huko Alcala, lakini akarudi nyumbani kutokana na kifo cha baba yake. Akiwa Segovia, aliamua kufanya biashara, ambayo baba yake alikuwa akifanya.

Alioa, akapata watoto watatu.Lakini watoto hao wote walikufa katika vipindi tofauti.Baadae mke wake pia alikufa.

Mtakatifu Alphonsus aliamua kuuza biashara zake, na akaomba kujiunga na shirika la wa Jesuit. Lakini hakukubaliwa ,kutokana na Kiwango chake kidogo cha elimu,na udhaifu wa afya yake.

Lakini mwaka 1571 Januari 31 ,alipokelewa na shirika la wa Jesuit, k**a Brother, mlei. Akapewa mafundisho mbalimbali, kisha akatumwa kufanya kazi katika kisiwa cha Majorca.

Hapo alifanya kazi k**a mbeba mizigo katika chuo cha wa Jesuit cha Montesion kwa miaka 20.Akawa rafiki wa kila mtu, akiwa mnyenyekevu.Akashauri wanafunzi, pamoja na watu waliokuwa hapo kwa busara Na nyakati zingine akaandika nyaraka tofauti za mafundisho.

Mtakatifu Alphonsus alikufa tarehe 31 October 1617.Alitangazwa mwenye heri mwaka 1825, na mwaka 1888 akatangazwa Mtakatifu.

Watakatifu wengine wa leo ni
Mt. Abraham Kidunaia
Mt. Narcissus
Mt. Abraham wa Rostov
Mt. Anne
Mt. Bond
Mt. Colman wa Kilmacduagh
Mt. Cuthbert Mayne
Mt. Donatus wa Corfu
Mashahidi wa Douai
Mt. Elfleda
Mt. Ermelinda
Mt. Eusebia
Mt. Gaetano Errico
Mt. Hyacinth
Mt. John of Autun
Mt. Kennera
M/h. Maria Restituta
Mt. Maximilian
Mt. Terence wa Metz
Mt. Theodore
Mt. Zenobius
Mtakatifu Alphonsus, Wenye heri na Watakatifu wengine wote wa leo, Mtuombee.
www.radiombiu.co.tz

Msikilizaji karibu ushiriki kipindi cha Night whisper, uwalaze unono watu watatuwww.Radio Mbiu.co.tz104.9 Fm
28/10/2025

Msikilizaji karibu ushiriki kipindi cha Night whisper, uwalaze unono watu watatu

www.Radio Mbiu.co.tz
104.9 Fm

Msikilizaji karibu tusali Sala ya rozari takatifu ya Fatima pamoja na Sala za jioni. leo jumanne tunatafakari matendo ya...
28/10/2025

Msikilizaji karibu tusali Sala ya rozari takatifu ya Fatima pamoja na Sala za jioni. leo jumanne tunatafakari matendo ya uchungu

www.Radio Mbiu.co.tz
104.9 Fm

Msikilizaji mpendwa karibu tusali Sala ya Malaika wa Bwana na masifu ya jioniwww.Radio Mbiu.co.tz104.9 Fm
28/10/2025

Msikilizaji mpendwa karibu tusali Sala ya Malaika wa Bwana na masifu ya jioni

www.Radio Mbiu.co.tz
104.9 Fm

28/10/2025

📹 PICHA JONGEFU II WAZAZI TIMIZENI WAJIBU WENU
▪ Mhashamu Jovitus Francis Mwijage Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba, ameendelea kusisitiza juu ya malezi ya Baba na Mama sio kuwaachia jukumu hilo waangalizi nyumbani.
Kwa undani wa homilia hii tembelea ukurasa wetu wa Youtube Radio Mbiu, usisahau kuwashirikisha na wengine, asante.
www.radiombiu.co.tz

28/10/2025
Msikilizaj karibu tusali kwa pamoja Sala ya Rozari ya Huruma ya Mungu pamoja na Rozari Takatifu ya Fatima.www.radiombiu....
28/10/2025

Msikilizaj karibu tusali kwa pamoja Sala ya Rozari ya Huruma ya Mungu pamoja na Rozari Takatifu ya Fatima.

www.radiombiu.co.tz

Msikilizaji karibu katika kipindi cha Pro life Utetezi wa uhai, mada inayozungumziwa ni nguvu ya familia katika kutetea ...
28/10/2025

Msikilizaji karibu katika kipindi cha Pro life Utetezi wa uhai, mada inayozungumziwa ni nguvu ya familia katika kutetea uhai.

www.radiombiu.co.tz

Kumbukumbu ya Watakatifu Simeon na Yuda, MitumeMtakatifu SimeonMtakatifu Simeon mtume, alizaliwa huko Yudea, Uyahudi, wa...
28/10/2025

Kumbukumbu ya Watakatifu Simeon na Yuda, Mitume

Mtakatifu Simeon
Mtakatifu Simeon mtume, alizaliwa huko Yudea, Uyahudi, wakati wa utawala wa Warumi. Alikuwa pia ndugu wa Bwana Yesu. Alikuwa mmoja kati ya mitume 12 wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Tunaona anatajwa katika maandiko (Matendo 1:13, Luke 6:15, Mathayo 10:4 Marko 3:18) na alikuwa mmoja kati ya wanafunzi makini.

Tunaona pia baada ya Pentekoste, aliendelea kukaa Jerusalem pamoja na Yakobo. Na alipouwawa Yakobo, Simeon alikemea vitendo vibaya vya Wayahudi. Ikatokea machafuko ambayo yalisababisha Mtakatifu Simeon kukimbilia ng'ambo ya mto Jordan, katika mji mdogo ulioitwa Pella. Alirudi tena Jerusalem na kuchaguliwa kuwa Askofu

Lakini baadae naye alik**atwa akashtakiwa kwa kuwa mkristo na akahukumiwa kuuwawa. Baada ya mateso makali, akauwawa kwa amri ya Atticus, gavana wa Warumi.

Mtakatifu Yuda, Mtume
Mtakatifu Yuda mtume , alizaliwa Galilaya, Uyahudi, nyakati za utawala wa Warumi, katika karne ya 1. Alikuwa mwana wa Clopas.

Alikuwa ni kaka wa Yakobo mtume, pia alikuwa na undugu na Bwana Yesu, Alikuwa mmoja kati ya mitume 12 wa Bwana wetu Yesu Kristo. Katika maandiko tunamuona katika Luka 6:16, matendo 1:13, Yohana 14:22 , Mathayo 13:55, Marko 6:3 na Jude 1:1.

Baada ya Pentekoste, Mtakatifu Yuda alianza kuhubiri na kufundisha, katika miji ya Judea, Samaria, Idumaea, Syria, Mosepotamia, na Lyidia.

Alirudi Jerusalem mwaka 62, kumsaidia Mtakatifu Simeon ambaye alichaguliwa kuwa Askofu wa Yerusalemu.

Aliondoka tena akienda Armenia, ambako aliendelea na kumuhubiri Kristo. Mtakatifu Yuda nae aliuwawa kwa ajiri ya kushikiria imani yake huko huko Armenia, katika karne hiyo hiyo ya kwanza.

Mabaki yake pamoja na ya Mtakatifu Simeon yapo katika Basilica la Mtakatifu Peter huko Roma.

Watakatifu wengine wa leo ni
Mt. Abraham
Mt. Anastasia II
Mt. Anglinus
Mt. Eadsin
Mt. Faro
Mt. Ferrutius
Mt. Fidelis of Como
Mt. Godwin
Mt. Honoratus wa Vercelli
Mt. Joachim Royo
Mt. John Dat
Mt. Remigius
Mt. Salvius
Watakatifu Simeon na Yuda Mitume, Wenyeheri na Watakatifu Wengine wote wa Leo, Mtuombee.
www.radiombiu.co.tz

Msikilizaj karibu tusali kwa pamoja Sala ya Rozari Takatifu ya Fatima, leo tunasali na kutafakari Matendo ya Uchungu.www...
28/10/2025

Msikilizaj karibu tusali kwa pamoja Sala ya Rozari Takatifu ya Fatima, leo tunasali na kutafakari Matendo ya Uchungu.
www.radiombiu.co.tz

Address

Bunena
Bukoba
35101

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00
Saturday 08:00 - 16:00
Sunday 09:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Mbiu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Mbiu:

Share

Category