BundafmTz

BundafmTz Ngurumo ya Jamii 92.1mhz

06/06/2026

DKT SAMIA AITANGAZA TANZANIA KATIKA JUKWAA LA DUNIA

Rais Dk Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuiweka Tanzania kwenye ramani ya uchumi wa dunia, baada ya kushiriki Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg nchini Urusi.

Jukwaa hilo limewakutanisha zaidi ya washiriki 24,000 kutoka zaidi ya nchi 140, wakiwemo wakuu wa nchi, wawekezaji na viongozi wa makampuni makubwa duniani.

Kupitia ushiriki huo, Tanzania imepata fursa ya kutangaza vivutio vyake vya uwekezaji katika sekta za madini, nishati, utalii, kilimo na usafirishaji.

Hatua hiyo inaendelea kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Shirikisho la mpira wa Miguu Duniani   limepiga marufuku matumizi ya VUVUZELA kwenye michuano ya Kombe la dunia 2026.Mba...
06/06/2026

Shirikisho la mpira wa Miguu Duniani limepiga marufuku matumizi ya VUVUZELA kwenye michuano ya Kombe la dunia 2026.

Mbali na Mavuvuzela chupa za maji pia hazitaruhusiwa katika michuano hiyo inayotarajia kuanza Juni 11, 2026.

Hazijatajwa sababu rasmi za KUZUIA Mavuvuzela ila kuhusu chupa za maji imetajwa kua ni sababu za kiusalama.


06/06/2026

SAKATA LA KIWANJA KILICHOMEZWA NA BARABARA PASIANSI LAFIKA KWA RC MTANDA

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameagiza kuchukuliwa hatua mbalimbali kufuatia mgogoro wa Kiwanja Na. 491, Kitalu "M" kilichopo Pasiansi, baada ya kubainika kuwa eneo hilo limepitiwa na barabara ya umma iliyosajiliwa na TARURA.

Hatua hiyo imekuja baada ya Bw. Salum Gidion kuwasilisha malalamiko yake Juni 5, 2026 akidai kuzuiwa kuendeleza kiwanja hicho na Diwani wa Kata ya Kiseke kwa maelezo kuwa eneo hilo ni sehemu ya barabara.


06/06/2026

PUTIN: TANZANIA NI KIUNGO MUHIMU KATI YA AFRIKA MASHARIKI NA MASOKO YA DUNIA

Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ameitaja Tanzania kuwa lango muhimu linalounganisha Afrika Mashariki na masoko ya dunia, akisisitiza kuwa nafasi ya nchi hiyo inaendelea kuwa ya kimkakati katika mfumo mpya wa uchumi wa dunia.

Akizungumza Juni 5 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) 2026, Putin amesema Tanzania ina nafasi inayofanana na ile ya Uzbekistan katika Asia ya Kati, kwa kuwa ni kiungo muhimu kinachounganisha uchumi wa kikanda na vituo vikubwa vya biashara duniani.

"Tanzania ina nafasi k**a hiyo katika Afrika Mashariki," amesema Putin wakati akizungumzia nchi ambazo nafasi zao za kijiografia na uhusiano wao wa kiuchumi zinazozifanya kuwa madaraja muhimu yanayounganisha maeneo mbalimbali ya dunia.

Ameeleza mataifa yanayoweza kuoanisha maendeleo yao ya ndani na mahusiano imara na vituo vipya vya ukuaji wa uchumi duniani yanazidi kuwa na umuhimu mkubwa kadiri mifumo ya biashara ya kimataifa inavyoendelea kubadilika.

Putin pia amegusia kile alichokitaja kuwa ni mabadiliko yanayoendelea katika mfumo wa biashara ya dunia, akisema biashara ya kimataifa inajiondoa katika misingi yake ya awali iliyowekwa chini ya Shirika la Biashara Duniani (WTO).

Kauli hizo zinakuja wakati Tanzania ikiendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika miundombinu ya usafirishaji, maendeleo ya bandari na kuimarisha mtandao wa biashara wa kikanda, hatua zinazozidi kuimarisha nafasi yake k**a lango kuu la biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.


04/06/2026

RAIS SAMIA ATOA SHAHADA YAKE KWA WANAFUNZI, WALIMU NA WAZAZI

RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan ameitoa shahada ya heshima ya uzamivu aliyotunukiwa nchini Urusi kwa wanafunzi, wazazi na walimu wanaopambana kuboresha maendeleo ya nchi kwa kutumia elimu.

Akizungumza mara baada ya kutunukiwa shahada hiyo ya honoris causa, Rais Samia amesema ameipokea tuzo hiyo kwa unyenyekevu mkubwa lakini anaamini ni kwa niaba ya wengi wengine.

kutokana na uongozi usio kifani na mchango wake kwa maendeleo ya taifa lake.

Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN) cha Patrick Lumumba kimempa Rais Samia heshima hiyo kwa sababu ya uongozi uliotukuka na jitihada zake za kuiletea Tanzania maendeleo.

Nilipopata taarifa ya kupewa hadhi hii, niliona kwamba hii heshima si yangu pekee bali ni kwa wale wote ambao elimu ina maana kwao. Kwa walimu wanaofundisha kote, kwa wanafunzi want guys maarifa na kwa wazazi wanaopambana kusomesha watoto wao.

“ Jina la chuo hiki, likichukua jina la mmoja wa viongozi wanamapinduzi wa Afrika la Patrice Lumumba ni kielelezo cha ushahidi wa uhusiano unaojali ukombozi, utu na umoja wa kweli,” alisema.

RUDN ni miongoni mwa vyuo mashuhuri duniani – kikijipatia sifa kutokana na kusomesha kada ya wasomi wa miaka ya mwanzoni ya Uhuru barani Afrika, Asia na Amerika ya Kusini na kujulikana kwa jina la Patrice Lumumba.

Shahada hiyo ya heshima ya RUDN ni ya nane kwa Rais Samia tangu aingie madarakani mwaka 2021.


04/06/2026

SAMIA AWAKUMBUKA LUMUMBA NA NYERERE

RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan amesifu mchango wa Chuo Kikuu cha Urafiki cha Watu wa Urusi (RUDN) katika ukombozi wa nchi za Afrika akisema kimesadifu maono ya viongozi wa zama za ukombozi wa Bara la Afrika.

Rais Samia ameyasema hayo jijini Moscow, Urusi wakati wa tukio la kutunukiwa kwake Shahada ya Heshima ya Uzamivu (Honoris Causa) na chuo hicho kutokana na uongozi uliotukuka na mchango wake katika maendeleo ya taifa.

Akizungumza mara baada ya kupewa heshima hiyo, Rais Samia alisema amepokea shahada hiyo kwa unyenyekevu mkubwa ukizingatia historia kubwa ya chuo hicho katika kipindi cha miaka 60 iliyopita.

“Jina la Patrice Lumumba ambalo chuo hiki kilipewa kilisadifu jukumu kubwa ambalo mwanamapinduzi huyo wa Afrika na viongozi wenzake wa Afrika waliona k**a wajibu mkubwa wa uongozi.

“Kwamba elimu inatakiwa isiwe tu kuingia darasani bali ni mlango wa ukombozi, utu, maendeleo na uhusiano wa kuheshimiana. Historia ya chuo hicho imesadifu maono yao na kwa hakika heshima waliyonipa ni kubwa” alisema.

RUDN imekuwa na mahusiano ya muda mrefu na Tanzania, kikiwa kimesomesha zaidi ya Watanzania 1,100 tangu kianzishwe mwaka 1960 iliyopita na sasa wanafunzi wa Kitanzania 72 wanapata mafunzo katika ngazi mbalimbali chuoni hapo.

Rais Samia anakuwa Rais wa karibuni zaidi kupewa heshima hiyo na chuo hicho, huku marais wengine sita wakiwa wamewahi kupewa tuzo hiyo. Baadhi ya marais hao ni Sam Nujoma wa Namibia, Thabo Mbeki wa Afrika Kusini na Olesegun Obasanjo wa Nigeria.

Vyuo vikuu vingine saba ambavyo vimewahi kumtunukia Rais Samia shahada za namna hiyo ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Jawahral Nehru nchini India, Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki, Nasarawa nchini Nigeria, Chuo Kikuu cha Anga cha Korea Kusini, Chuo Kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA).

Rais Samia yuko nchini Urusi katika ziara ya kitaifa iliyoanza jana na itahitimishwa kesho baada ya kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi wa St. Peterburg nchini hapa.


04/06/2026

RAIS SAMIA ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA URUSI

CHUO Kikuu mashuhuri nchini Urusi leo kimemtunukia shahada ya heshima ya Uzamivu (honoris causa) Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na uongozi usio kifani na mchango wake kwa maendeleo ya taifa lake.

Chuo hicho kinachojulikana kwa jina la Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN) ni miongoni mwa vyuo mashuhuri duniani – kikijipatia sifa kutokana na kusomesha kada ya wasomi wa miaka ya mwanzoni ya Uhuru barani Afrika, Asia na Amerika ya Kusini na kujulikana kwa jina la Patrice Lumumba.

Akipokea shahada hiyo ya heshima – ya nane tangu aingie madarakani, Rais Samia alisema amepokea tuzo hiyo kwa unyenyekevu mkubwa na haichukulii k**a yake binafsi.

“Nilipopata taarifa ya kupewa hadhi hii, niliona kwamba hii heshima si yangu pekee bali ni kwa wale wote ambao elimu ina maana kwao. Kwa walimu wanaofundisha kote, kwa wanafunzi want guys maarifa na kwa wazazi wanaopambana kusomesha watoto wao.

“ Jina la chuo hiki, likichukua jina la mmoja wa viongozi wanamapinduzi wa Afrika la Patrice Lumumba ni kielelezo cha ushahidi wa uhusiano unaojali ukombozi, utu na umoja wa kweli,” alisema.

Rais Samia alitumia hotuba yake ya kupokea heshima hiyo kwa kueleza kuhusu umuhimu wa elimu akisema imebadili maisha ya watu na mataifa mbalimbali.

“Hakuna taifa linalotaka kuachwa nyuma katika dunia ya sasa yenye mabadiliko makubwa katika maeneo k**a vile akili mnemba na sayansi za mashine. Jambo kubwa kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla si kwamba tuingie kwenye ushindani au la bali ni namna gani tutaingia kwenye ushirikiano na kufaidika na mabadiliko haya,” alisema.

Tukio hilo lilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Sayansi na Elimu ya Juu wa Urusi, Konstantin Mogilevsky, ambaye katika hotuba yake alisema Rais Samia ametoa mchango mkubwa katika ukuzaji wa elimu nchini kwake katika kipindi cha miaka yake sita madarakani.

RUDN imekuwa na mahusiano ya muda mrefu na Tanzania, kikiwa kimesomesha zaidi ya Watanzania 1,100 tangu kianzishwe mwaka 1960 iliyopita na sasa wanafunzi wa Kitanzania 72 wanapata mafunzo katika ngazi mbalimbali chuoni hapo.

Rais Samia anakuwa Rais wa karibuni zaidi kupewa heshima hiyo na chuo hicho

USHIRIKIANO WA TANZANIA NA URUSI KUNUFAISHA WANANCHI KUPITIA UWEKEZAJI Rais wa Urusi, Vladimir Putin, amesema biashara k...
04/06/2026

USHIRIKIANO WA TANZANIA NA URUSI KUNUFAISHA WANANCHI KUPITIA UWEKEZAJI

Rais wa Urusi, Vladimir Putin, amesema biashara kati ya nchi hiyo na Tanzania imeendelea kukua kwa kasi, huku kiwango kikiongezeka kati ya asilimia 20 hadi 25 kwa mwaka 2025.

Amefafanua kuwa hatua hiyo inayodhihirisha kuimarika kwa ushirikiano wa kiuchumi na kunufaisha wananchi wa pande wa Urusi na Tanzania.

Rais Putin ameeleza hayo leo Jumatano Juni 3,2026 wakati mazungumzo na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Ikulu ya Kremlin Rais Putin akieleza kuwa mesema ukuaji huo unaonyesha kuimarika kwa ushirikiano wa kiuchumi na mahusiano ya kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili, yanayoaadhimisha miaka 65 ya uhusiano wa kidiplomasia.

Kiongozi huyo wa Urusi amesema kuwa ongezeko hilo ni hatua muhimu, lakini akasisitiza kuwa bado kuna fursa nyingi za kuongeza biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Urusi.

Rais Putin amezitaja sekta za madini, usafiri na usafirishaji, afya na elimu kuwa miongoni mwa maeneo yenye nafasi kubwa ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.

Naye, Rais Samia amesema ziara yake itaimarisha ushirikiano na kukuza fursa za maendeleo kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na Urusi.


03/06/2026

RAIS SAMIA ALIVYOPOKEWA NA RAIS PUTIN IKULU YA KREMLIN

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokutana na Rais wa Urusi katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, Urusi leo Jumatano Juni 03, 2026.

Dk. Samia yuko nchini Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais Putin, katika ziara inayolenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi pamoja na kukuza ushirikiano katika sekta za uwekezaji na biashara.

03/06/2026

RAIS SAMIA AWEKA SHADA KABURI LA MASHUJAA URUSI

Rais Samia Suluhu Hassan leo ameweka shada la maua katika Kaburi la Mashujaa jijini Moscow Urusi kwa heshima ya wananchi na askari zaidi ya milioni 20 waliopoteza maisha wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

Rais Samia yuko katika ziara ya kitaifa ya siku tatu nchini Russia ambalo leo mchana anatarajiwa kukutana na mwenyeji wake, Rais Vladimir Putin, katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa kabla ya mkutano huo, viongozi hao wawili wanatarajiwa kuzungumza kwa kina kuhusu masuala anuai yakiwemo biashara, uchumi, uwekezaji na kilimo.

Kesho Rais Samia ataongoza mkutano wa wafanyabiashara wa Tanzania na Russia na pia kuzungumza katika Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi utakaofanyika katika jiji la St. Petersburg.

Address

Bunda

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BundafmTz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BundafmTz:

Share