BundafmTz

BundafmTz Ngurumo ya Jamii 92.1mhz

08/08/2026

SAMIA: TUMEIFUNGUA NCHI KIBIASHARA, UWEKEZAJI

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kutafuta masoko ya ndani na nje ya nchi kwa ajili ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi, akisisitiza kuwa Tanzania imefungua milango zaidi kwa biashara na uwekezaji.

Rais Samia amesema hayo leo, Agosti 8, 2026, wakati akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wakulima (Nanenane) Kitaifa yaliyofanyika katika Viwanja vya John Malecela, Nzuguni, Dodoma.

Amesema hatua hiyo inalenga kuwawezesha wazalishaji kupata masoko ya uhakika huku ikiendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

“Tumeifungua nchi kibiashara na uwekezaji na tunaendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje, sambamba na mwelekeo wa Dira yetu ya Taifa unaoipa sekta binafsi asilimia 70 ya utekelezaji wake,” amesema Rais Samia.


Mchambuzi wa masuala ya siasa, jamii na maendeleo, Habibu Mchange, ameibua maswali kuhusu kauli ya mwanaharakati Maria S...
08/08/2026

Mchambuzi wa masuala ya siasa, jamii na maendeleo, Habibu Mchange, ameibua maswali kuhusu kauli ya mwanaharakati Maria Sarungi Tsehai ya kumhimiza Makamu wa Rais, Dk. Emmanuel Nchimbi, kuendelea kupigania misimamo yake “ndani kwa ndani”.

Sarungi alitoa kauli hiyo katika ujumbe wake uliosomeka: “Nchimbi we piga kwenye mshono na usiende kokote, ni humo ndani kwa ndani pambana.”

Akizungumzia kauli hiyo, Mchange amesema ameshangazwa na namna baadhi ya wakosoaji wakubwa wa Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake wanavyoweza kujitokeza kumuunga mkono mmoja wa viongozi wakuu wa Serikali.

Kwa mujibu wa Mchange, hali hiyo inaibua mjadala kuhusu maana ya kauli ya “kupambana ndani kwa ndani” na ni changamoto zipi ambazo Nchimbi anatakiwa kukabiliana nazo.

“Maria anampenda Nchimbi lakini anaichukia Serikali ambayo Nchimbi ni kiongozi namba mbili? Anaipinga CCM lakini anamtetea mmoja wa viongozi wake wakuu? Na anaposema Nchimbi apambane ndani kwa ndani, apambane na nani?” amehoji Mchange.

Mchange amesema mjadala huo unapaswa pia kuangaliwa kwa kuzingatia historia ya kisiasa ya Nchimbi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), akirejea matukio na mijadala mbalimbali ya kisiasa iliyohusishwa na jina lake katika vipindi tofauti.

Ametaja pia mijadala ya mwaka 2015 kuhusu mchakato wa uteuzi wa mgombea mwenza wa CCM, ambapo Dk. Samia Suluhu Hassan aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa marehemu Rais John Magufuli, hatua iliyochangia safari yake ya kisiasa hadi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande mwingine, Mchange amesema kauli na mijadala ya hivi karibuni inayomhusu Nchimbi imeendelea kutoa nafasi kwa wadau mbalimbali kutafsiri na kujadili nafasi yake ndani ya Serikali na CCM.

Hata hivyo, Mchange amesisitiza kuwa madai yoyote kuhusu uwepo wa ushirikiano kati ya Nchimbi na wanaharakati au wanasiasa wa upinzani yanapaswa kuwasilishwa pamoja na ushahidi, badala ya kutegemea hisia au tafsiri za kisiasa.


08/08/2026

WAKAZI WAJIPANGA KUPOKEA WAGENI TAMASHA LA KIZIMKAZI

Siku chache kabla ya kuanza kwa Tamasha la Kizimkazi litakalofanyika Agosti 12 hadi 14 mwaka huu, wakazi wa Kizimkazi wamesema maandalizi yamekamilika kwa ajili ya kuwapokea wageni wanaotarajiwa kushiriki tukio hilo linalolenga kukuza utalii, biashara na uchumi wa buluu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi hao wamesema wamejipanga kuhakikisha wageni wanapata huduma bora, mazingira salama na mapokezi mazuri yatakayowawezesha kufurahia tamasha hilo kwa utulivu.

Mkazi wa Kizimkazi Mkunguni, Thabit Khamis Majisu, amesema jamii imejipanga kuhakikisha wageni wote wanapata huduma bora na uzoefu mzuri utakaoifanya Kizimkazi kuendelea kujulikana zaidi ndani na nje ya Zanzibar.

Kwa upande wake Mkazi wa Mkunguni, Lila Mikidadi Mwinyi, amesema wakazi wa Kizimkazi wameungana kufanya usafi katika mitaa na maeneo ya umma ili kuonyesha utayari wao wa kuwapokea wageni, hatua inayolenga kuimarisha taswira ya Kizimkazi k**a kitovu cha utalii, biashara na uwekezaji.

Tamasha hilo lenye kaulimbiu "Kizimkazi Kumenoga: Shangwe na Fursa" linatarajiwa kufungua fursa za uwekezaji, kukuza utalii, biashara na maendeleo ya jamii.


07/08/2026

MIAKA 30 YA BONGO FLEVA SASA ZAMU YA KIZIMKAZI

Tamasha la Kizimkazi litafanyika kuanzia Agosti 12–14, 2026 likiwa na kaulimbiu “Kizimkazi Kumenoga: Shangwe na Fursa.” Jiandae kushuhudia burudani mbalimbali zitakazopamba tamasha hilo sambamba na shughuli za utamaduni, utalii, biashara na fursa za uchumi wa buluu.

Karibu Kizimkazi kushiriki shangwe na kujionea fursa


07/08/2026

SAMIA : ANAYEHARIBU MIONDOMBINU ANALIHUJUMU TAIFA, TUSIKUBALI TUILINDE

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewataka Watanzania kuwa walinzi wa mali za umma, akieleza kuwa mtu anayeharibu miundombinu hiyo, anateketeza kodi za wananchi.

Samia amefafanua kuwa fedha inayokusanywa na Serikali, kisha kutolewa k**a mchango katika utekelezaji wa miradi, hizo ni kodi za wananchi, hivyo hawatakubali ziteketezwe kiuhalisi.

Dkt Samia ameeleza hayo leo Agosti 7,2026 wakati akifungua na kutembelea Mradi wa Mabasi Yanayoenda Haraka Awamu ya Pili (BRT II) katika barabara ya Kilwa, Chang’ombe, Sokoine na Kawawa jijini Dar es Salaam.

“Anayefanya hivyo anachelewesha maendeleo ya Taifa, anarudisha nyuma Taifa, analihujumu Taifa, ni adui wa Taifa letu, tusikubaliane nao,” amesema Dkt Samia

Mbali na hilo, Rais Samia amewahisi vijana kutambua kuwa Tanzania ndio nyumbani hakuna kwingine, hivyo wasikubali kutumika bali watunze kila kilichomo nchini.

“Uharibifu wa miundombinu unaibebesha nchi gharama kubwa ya kuirejesha kwa kutumia fedha ambazo zingekwenda kutumika katika miradi mingine. Hakuna faida ya kufanya hivyo, zaidi ya huduma na shughuli za kiuchumi kudhoofika na kasi ya maendeleo ya Taifa kudorora,” amesema Rais Samia.


07/08/2026

MAJAJI WA UGANDA, NAMIBIA WATEULIWA NA RAIS SAMIA TUME YA GHASIA ZA UCHAGUZI

Rais Samia Suluhu Hassan leo Agosti 7, 2026 amezindua Tume ya Rais ya Uchunguzi wa Wahusika wa Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria katika Matukio ya Ghasia Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, yenye Makamishna sita, wakiwamo majaji wawili kutoka nje ya nchi.

Uzinduzi huo umefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, ukifuatia uteuzi wa wajumbe wa tume hiyo uliofanywa Mei 18, 2026. Kuundwa kwa tume hiyo kunatekeleza moja ya mapendekezo ya Tume ya Kuchunguza Matukio ya Vurugu Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, iliyoongozwa na Jaji Mstaafu Mohamed Chande Othman.

Tume hiyo inaongozwa na Jaji wa Mahak**a ya Rufani, Jaji Shabani Lila, ambaye ni Mwenyekiti na Kamishna. Makamishna wengine kutoka Tanzania ni Jaji Mstaafu Gad Mjemmas, Jaji Mstaafu Awadh Bawazir na Jaji Mstaafu Aishieli Sumari, wote wakiwa ni majaji wastaafu wa Mahak**a Kuu.

Makamishna kutoka nje ya nchi ni Petrus Tileinge Damaseb wa Namibia na Cheborion Barishaki kutoka Uganda.

Damaseb anahudumu k**a Naibu Jaji Mkuu wa Mahak**a ya Juu ya Namibia na pia ni Jaji Mkuu wa Mahak**a Kuu ya Namibia, huku Barishaki akiwa Jaji wa Mahak**a ya Rufani ya Uganda, ambayo pia hufanya kazi k**a Mahak**a ya Kikatiba ya Uganda, pamoja na kuwa Jaji wa Kitengo cha Rufani cha Mahak**a ya Haki ya Afrika Mashariki.


Mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Mossi Nduwumwe, amekamilisha rasmi uhamisho wake kutoka Singida Black Stars kwenda...
07/08/2026

Mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Mossi Nduwumwe, amekamilisha rasmi uhamisho wake kutoka Singida Black Stars kwenda kwa mabingwa wa Algeria, MC Alger.

Hatua hiyo imekuja baada ya mazungumzo kati ya klabu hizo kukamilika kwa mafanikio, huku MC Alger ikimtambulisha rasmi nyota huyo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Klabu hiyo ilimkaribisha Nduwumwe kwa ujumbe wa "Welcome to Mouloudia", ikithibitisha kukamilika kwa usajili wa mshambuliaji huyo aliyekuwa akifuatiliwa kwa karibu kutokana na kiwango chake bora.

Nduwumwe anaondoka Singida Black Stars baada ya kuwa na msimu mzuri wa nusu mwaka tangu alipojiunga na klabu hiyo mwezi Januari akitokea Flambeau du Centre FC ya Burundi.

Licha ya kucheza nusu msimu pekee katika Ligi Kuu ya NBC, mshambuliaji huyo alimaliza akiwa mfungaji bora wa ligi kwa mabao 17, mafanikio yaliyomvutia mabingwa hao wa Algeria na kufanikisha uhamisho wake.


07/08/2026

BWAKILA NDANI YA MELI

07/08/2026

BWAKILA MAKABILA YOTE KIZIMKAZI FESTIVAL

07/08/2026

BWAKILA KARIAKOO DERBY

Address

Bunda

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BundafmTz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BundafmTz:

Shortcuts

Share