05/03/2026
MLIMPA MTOTO WENU JINA AKALIA MPAKA MLIPOBADILISHIA NDIO AKANYAMAZA
Makabila ya Mkoa wa Mara hutoa majina kutokana na majira ya hali ya hewa, na matukio mengine mfano vipindi vya mvua, ataitwa Wambura, vipindi vya kulima mtoto ataitwa Malima, kipindi cha viazi vingi basi mtoto ataitwa Manumbu na kipindi kikiwa na nyasi nyingi anaitwa Manyasi.
Tamaduni nyingi za mkoa wa Mara Watu walikuwa hawawezi kuita jina la htoto bila kuzingatia majira, pengine unaweza mtoto anaweza pewa jina ambalo ni la urithi kwa maana wazee wameona linafaa, na jina likimkataa basi mtoto atalia sana mpaka atakapobadilishwa apewe jina lingine.
Hata hivyo kutokana na utandawazi watu hawazingatiimila na desturi sana wenyewe watakavyoamua kuita jina wanaita pengine wanaangalia mpira wa Biashara United na Young African wakivutiwa na mchezaji ndio wanaenda kupachika jina kwa mtoto.
Biblia Mwanzo 17:5-15 Mungu alifanya marekebisho ya majina ya Abramu na sarai kwa kutoa herufi ziizo kuwa zimekaa mahali pasipo takiwa na kuziweka panapo takiwa ikiwa ni pamoja na kuziondoa kabisa zile ambazo zilikuwa hazihitajiki katika muundo wa majina yao.
Marekebisho hayo yalifanyika wakati anaenda kuwapa mtoto, hivyo inamaana kuwa muda wote walio kuwa wanateseka kuhusu mtoto tatizo lilikuwa kwenye hizo herufi ilizo kuwa zimekaa pasipo takiwa katika majina yao, Kutoka Abramu ikawa Ibrahimu, na kutoka sarai ikawa sara.
Kuna herufi I mwisho wa jina la sarai imeondolewa na kuwekwa mwanzo wa jina la abrahamu iliwapate mtoto (kwa abrahamu imeongezwa herufi H na I katikati ya jina). K**a herufi i peke yake ilimpa sarai mateso yote hayo ya ugumba mpaka uzeeni mwake.
lipokuja kutolewa na Mungu ndipo akapata kicheko basi herufi za majina yetu si zakupuuzwa kabisa, kwakuwa zimebeba maana kubwa sana katike maisha yetu, huenda kuna herufi moja tu kwenye jina lako ndo iliyo zuia usipate kazi, elimu, mke au mume na kuweka mateso pasipo wewe mwenyewe kujua.
Follow Timber TZA