Daily Talk

Daily Talk Content Publisher

SAGINI: WANANCHI WAPEWE ELIMU YA KUTOSHA JUU YA KUPANGA MJI WA BUTIAMAMbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Kati...
27/01/2025

SAGINI: WANANCHI WAPEWE ELIMU YA KUTOSHA JUU YA KUPANGA MJI WA BUTIAMA

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akizungumza katika Kikao cha Baraza la Madiwani amewataka wataalamu kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi juu ya mpango Mji wa Butiama ikiwemo kulipa fidia kwa haki eneo la Chuo Kikuu cha Mwl. Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT). Januari 27, 2025

SAGINI: WIZARA YA KATIBA NA SHERIA INAWAFIKIA WATU AMBAO HAWANA UWEZO WA KIWAKILI WAPATE HAKI BILA MALIPOWizara ya Katib...
26/01/2025

SAGINI: WIZARA YA KATIBA NA SHERIA INAWAFIKIA WATU AMBAO HAWANA UWEZO WA KIWAKILI WAPATE HAKI BILA MALIPO

Wizara ya Katiba na Sheria inashirikiana na taasisi mbalimbali ili kuwafikia watu ambao hawana uwezo wa kugharamia huduma za kiwakili waweze kupata haki kwa wakati kwa kutoa msaada wa kisheria bila malipo yoyote.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini wakati alipokuwa akihotubia wananchi kwenye Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia iliyofanyika katika Viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora.

Pia Mhe. Naibu Waziri Sagini alifanikiwa kusikiliza na kuzitolea maelekezo baadhi ya kesi ambazo zilielezwa na wananchi waliofika kupata Huduma za Msaada wa Kisheria.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, amewataka wakazi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kupata huduma za msaada wa kisheria inayotolewa katika Viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora na maeneo mengine yaliyotengwa ili kuepusha changamoto za kisheria ambazo zinaweza kutatulika hata pasina kupelekwa mahak**ani.

Aidha Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi ACP Constantine Mbogambi kwa niaba ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora SACP Richard Abwao amesema kuwa Kampeni ya Msaada wa Kisheria italirahisishia jeshi la polisi kupunguza idadi ya wahalifu kutokana na watu kuwa na elimu ya sheria.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akiwasikiliza Wananchi waliofika kupata Huduma za Msaada wa Kisheri...
26/01/2025

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akiwasikiliza Wananchi waliofika kupata Huduma za Msaada wa Kisheria wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia iliyofanyika katika Viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora

KILICHOTOKEA UJENZI DARAJA LA KIRUMIDaraja la Kirumi lipo katika Kijiji cha Kirumi Kata ya Bukabwa Wilaya ya Butiama mko...
21/01/2025

KILICHOTOKEA UJENZI DARAJA LA KIRUMI

Daraja la Kirumi lipo katika Kijiji cha Kirumi Kata ya Bukabwa Wilaya ya Butiama mkoani Mara lina urefu wa mita 223.3 lilianza kujengwa Mwaka 1978 na Kampuni ya kichina ya H Ang' wakiwa na wazo la kuangusha milima ili kupunguza...

upana na kina cha Mto Mara, lakini walishindwa.

Ilipofika mwaka 1979, zabuni ilichukuliwa na Wakaburu Kampuni ya Morem pia walishindwa hawakuweza kuendelea kutokana na sababu ambazo hazikuwekwa wazi japo walianza kwa kuleta vifaa.

Mwaka 1980 Zabuni ikawaangukia Wahindi Kampuni ya Mauradadi, hawa walianza ujenzi kwa kuchimbia nguzo karibu na kwenye maji.

Walikiona cha moto, maana kulitokea tetemeko kubwa lililosikika hapo Mlima Kirumi na kupelekea kuvunjwa vunjwa nguzo zote na kusukumwa...

mpaka Ziwa Victoria Wilaya ya Musoma.

Mwaka huo huo, wakaingia Kampuni ya lenari (COWIconsult) kutoka nchini Italia, k**a kawaida walipata changamoto k**a walizopitia wenzao ila zikiwa mpya na tofauti na zile za awali. Walijenga na kufanikisha kuweka Jiwe la Msingi.

Rais Mwl. Julius Kambarage Nyerere ndiye aliyekuwa Mgeni Rasmi katika Uwekaji wa Jiwe la Msingi, Hata hivyo siku moja kabla ya hafla tetemeko la ardhi likapita na kusababisha kupasuka kwa Msingi wote ingawa Rais akafika siku ya iliyopangwa kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi.

Ilishindikana Ilibidi waahirishe na Rais Nyerere hakuweza kushuka hata Kwenye gari. Wataliano waliona ni bora kuomba likizo kwenda kwao kwa muda na waliporudi ujenzi uliendelea bila shida hadi kukamilisha.

Mwezi Novemba, Mwaka 1985 Daraja la Kirumi lilifunguliwa na Rais wa Awamu ya Kwanza Mwl. Julius K. Nyerere.

 📍
16/01/2025

📍

WABUNGE MKOANI MARA 2020-2025Jimbo la Mwibara Charles Kajege, Bunda (V) Boniphace Getere, Bunda (M) Robert Maboto, Seren...
14/01/2025

WABUNGE MKOANI MARA 2020-2025

Jimbo la Mwibara Charles Kajege, Bunda (V) Boniphace Getere, Bunda (M) Robert Maboto, Serengeti Amsabi Mrimi, Butiama Jumanne Sagini, Rorya Jafari Chege,Tarime (V) Mwita Waitara, Musoma (M) Vedastus Matayo, Musoma (V) Sospeter Muhongo, Tarime (M) Michael Kembaki.

VITI MAALUMU MKOANI MARA

1. Ester Bulaya
2. Ghati Chomete
3. Esther Matiko
4. Agness Mathew

Follow

Hapa ni Ndutu Safari Lodge kwenye eneo la Uhifadhi la Wanyama Pori la Ngorongoro nchini Tanzania mtalii alipiga picha ik...
10/01/2025

Hapa ni Ndutu Safari Lodge kwenye eneo la Uhifadhi la Wanyama Pori la Ngorongoro nchini Tanzania mtalii alipiga picha ikimuonesha Simba akimlea na kumnyonyesha mtoto wa chui hiki kisa ni cha pekee duniani.

Nyumbu ana maumbile ya wanyama kadhaa; 1. Miguu ya nyuma na kiuno ni umbile la Fisi;2. Mkia ni umbile la Farasi3. Michir...
09/01/2025

Nyumbu ana maumbile ya wanyama kadhaa;
1. Miguu ya nyuma na kiuno ni umbile la Fisi;
2. Mkia ni umbile la Farasi
3. Michirizi ya Pundamilia
4. Pembe ni za Nyati
5. Ndevu ni za Pofu
6. Nywele za mgongoni ni za Pundamilia.

MKUU WA WILAYA TARIME AZINDUA MASHINDANO YA MATIKO CUPNa Timothy Itembe TarimeMkuu wa wilaya Tarime Meja,Edward Gowele a...
08/01/2025

MKUU WA WILAYA TARIME AZINDUA MASHINDANO YA MATIKO CUP

Na Timothy Itembe Tarime

Mkuu wa wilaya Tarime Meja,Edward Gowele amezimdua Ligi ya Matiko Cup itakayoahirikisha Timu 20 za Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara Kwa lengo la kuibua vipaji na kutoa ajira.

Akizindua Mashindano hayo Mkuu huyo aliwataka wadau wote wapenda maendeleo wa michezo kuja kuwekeza na kuanzisha ligi Kwa lengo la kukuza na kuibua vipajimbalimba na kutoa ajira Kwa Vijana na makundi mbalimbali.

Kwa upande wake Mbunge viti Maalumu, Esther Matiko Mdhamini wa Mashindano hayo alisema Ligi hiyo itafanikiwa Kwa gharama ya shilingi milioni zaidi ya 85.6 ndani ya halmashauri ya mji na huwenda Bajeti hiyo ilaongezeka wakati wa mahitimisho baada ya kutamatika

"Ndugu mgeni rasmi Kauli mbiu ya mashindano haya ya Matiko Cup,TUMEPANIA TUNATEKELEZA na shilingi Milioni 85.6 kufanikisha MATOKO CUP 2024/2025 Kwa washiriki ngazi ya mji lakini Matiko Cup tutahakikisha mashindano haya yanashuka chini hadi ngazi ya kata Kwa michuano mbalimbali hata wacheza karata bao na wengine wanashiriki lengo ni kuibua vipaji na kutoa ajira Kwa makundi mbalimbali Katika uzinduzi wa Leo mgeni rasimi ni Timu ya Mpira wa miguu Tarime United na Aluminium wametuzindulia mashindano yetu"amesema Matiko.

Naye Mfanyabiashara ambaye pia ni Mdau wa Maendeleo Daniel Chonchorio amesema ataunga mkono Matiko Cup Kwa shilingi milioni tatu ili kufanikisha Kwa kuwa Gharama inayotumiwa na Matiko Cup ni nyingi kiasi Cha apesheni ya mstaafu Moja wa jeshi la polisi cheo Cha chini.

Katika uzinduzi wa mashindano hayo Jana Timu ya Tarime United FC iliibamiza bao Moja Timu ya Mpira wa miguu Timu ya Aluminium FC bao ambalo lilifungwa Katika dakika za lala salama na mshambiliaji mahiri Jeremia Girigori.

SAGINI AZINYOOSHEA KIDOLE KAMPUNI ZINAZOCHELEWESHA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA MJNUAT- BUTIAMAMbunge wa Jimbo la Butiama na...
06/01/2025

SAGINI AZINYOOSHEA KIDOLE KAMPUNI ZINAZOCHELEWESHA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA MJNUAT- BUTIAMA

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Jumanne Sagini amezitaka Kampuni za Shabdong Hi Speed Dejian Group Co LTD na Comfix and Engineering LTD zinazotekeleza Mradi wa Ujenzi wa majengo ya Hosteli, Cafeteria, Maktaba na Utawala katika Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT) kukamilisha kwa wakati k**a Mkataba unavyoelekeza.

Hayo ameyasema wakati alipokuwa katika Ziara yake ya Kutembelea na kukagua uendelezaji wa Ujenzi wa Chuo hicho katika Kampasi ya Oswald Mang'ombe Butuguri na Makao Makuu yaliopo BAIC Butiama.

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan aliridhia kutoa zaidi ya Bilioni 100, kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Chuo hiki kilichokaa zaidi ya miaka 10 bila kuanza na wanabutiama wana hamu kuona kimekamilika lakini wakandarasi hasa wazawa wameanza kuchelewa japo awali walianza vizuri. Hivyo muongeze nguvu kazi ili kurahisha zoezi kwenda kwa haraka," amesema Sagini.

Aidha, Naibu Waziri Sagini alipokea malalamiko juu ya mawasiliano duni ya simu na Intaneti chuoni hapo, ambapo aliahidi kutatua kwa haraka changamoto hiyo kutokana na sera ya Serikali ilivyodhamiria kufikisha huduma za mawasiliano ya simu na intaneti ya kasi kwa kila mtanzania kwa asilimia 100.

Follow

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula ametoa msaada wa vyakula ikiwemo Mchele na Sukari kwa wananchi wa mitaa ...
05/01/2025

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula ametoa msaada wa vyakula ikiwemo Mchele na Sukari kwa wananchi wa mitaa ya Butindo kata ya Shibula kaya13, Kilabela kata ya Bugogwa kaya 12 na Isanzu kata ya Sangabuye kaya 2 kufuatia maafa ya mvua kubwa zilizoambatana na upepo zilizonyeesha usiku wa kuamkia Januari 02, 2025

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Katibu wa Mbunge Charles David Karoli amesema kuwa mbunge anatoa pole nyingi kufuatia madhara ya mvua hizo ikiwemo kunyeshewa kwa vyakula vilivyokuwa vimehifadhiwa majumbani

'.. Wakati mvua zinanyesha na kuezua mapaa ya nyumba ndani kulikuwa na vyakula, Na baadhi yenu mkajikuta vyakula vimenyeeshewa hivyo Mbunge akaona ipo haya ya kutoa msaada wa vyakula kwa wakati huu wakati tukisubiria hatua nyengine zitakazochukuliwa na Serikali ..' amesema

Aidha Mbunge Dkt Mabula amewashauri wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya mvua zinazoendelea kunyesha ili kujikinga na madhara mengine yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua zinazoendelea maeneo mbalimbali nchini sanjari na kuwapongeza viongozi wa mitaa na kata kwa namna walivyoshirikiana katika kusaidia wananchi waliopatwa na majanga hayo

Swila Dede ni Diwani wa Kata ya Shibula moja ya eneo lililoathiriwa na mvua hizo ambapo amemshukuru Mbunge Dkt Angeline Mabula kwa msaada alioutoa huku akiwataka wananchi wake kumuunga mkono Mbunge huyo na kuwapuuza watu wasiokuwa na nia njema wanaotumia matatizo yao k**a sehemu ya mtaji wa kisiasa na kujinufaisha wao binafsi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Butindo Lucas Andrea amempongeza Mbunge Dkt Angeline Mabula na kwamba wanamuombea Mungu amzidishie pale alipopunguza huku akiwaasa wananchi wake kushirikiana wakati wa kipindi hiki kigumu

Samuel Miza ni miongoni mwa wananchi waliokumbwa na maafa hayo ambapo amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Ilemela huku akiwaasa viongozi wengine kuiga mfano huo

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula pia ameagiza kufanyika kwa tathimini fupi juu ya madhara ya mvua hizo kwa wananchi wote walioguswa na kadhia ili kutoa fursa kwa Serikali kuchukua hatua zaidi kwa kushirikiana na ofisi yake.

SAGINI ASHIRIKI IBADA NA MAZISHI YA MWANASHERIA MKUU MSTAAFU JAJI WEREMAMbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Ka...
04/01/2025

SAGINI ASHIRIKI IBADA NA MAZISHI YA MWANASHERIA MKUU MSTAAFU JAJI WEREMA

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini ameshiriki Ibada na Mazishi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Mstaafu Marehemu Jaji Frederick Werema aliyefariki dunia Desemba 30, 2024 na kuzikwa leo Januari 04, 2025 kijijini kwao Kongoto Kata ya Buswahili Wilaya ya Butiama mkoani Mara.

Akitoa salamu za rambirambi Naibu Waziri Mhe. Sagini amesema kuwa Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro anatoa pole kwa waombolezaji na kuwataka wawe na moyo wa subira pia Serikali inaungana na familia katika kipindi hiki kigumu.

"Marehemu alikuwa ni nembo ya Kijiji hiki cha Kongoto mpaka Taifa hivyo Wizara ya Katiba na Sheria ikiongozwa na Waziri wetu tunaungana na familia na jamii kwa ujumla kuomboleza pia k**a serikali tunaahidi kumuenzi katika yale mema aliyotuachia katika enzi za uhai wake," amesema Sagini.

Aidha Sagini ametoa wito kwa familia ya Jaji Werema kuendelea kushirikiana na wasijiingize katika migogoro ambayo huwa inajitokeza hasa wanapofikia hatua ya mirathi hivyo wagawane mali kwa upendo na amani.

Baadhi ya Viongozi walioshiriki mazishi hayo ni Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari, MNEC Chacha Gachuma, Mwenyekiti Mara Patrick Chandi, Mkuu wa Mkoa Njombe Anthony Mtaka, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Kaimu Mkoa wa Mara Said Mtanda, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Butiama Christopher Siagi, Mkuu wa Wilaya ya Musoma kaimu Butiama Juma Chikoka na Mariam Sagini akiwakilisha kikundi cha Wake wa Viongozi (Millenium)

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula amewafariji wananchi wa Mtaa wa Butindo Kata ya Shibula na Kilabela Kata...
02/01/2025

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula amewafariji wananchi wa Mtaa wa Butindo Kata ya Shibula na Kilabela Kata ya Bugogwa kufuatia maafa yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha usiku wa kuamkia Jumatano ya Januari 02, 2025.

Akizungumza na wananchi waliokumbwa na kadhia hiyo kwa niaba ya Mbunge, Katibu wa Mbunge Charles David Karoli amesema kuwa Mbunge amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za madhara ya mvua zilizotokea usiku wa kuamkia Leo na kwamba anazipa pole kaya 13 zilizoathirika na mvua hiyo huku tathimini ya awali ikionesha athari kubwa iliyopatikana ni uharibifu wa vyakula, kuezuliwa kwa mapaa ya nyumba na watu wawili kujeruhiwa kichwani kwa kuangukiwa na matofali na mbao

'.. Mbunge ameipongeza Serikali kwa juhudi za haraka ilizozichukia katika kukabiliana na maafa haya lakini pia Kamati zetu za nzengo zinazosimamia maafa kwa kusaidia wenzetu na kuwafariji wakati tukisubiria misaada ya wadau wengine," amesema.

Aidha David akaongeza kuwa Mbunge ataendelea kufanya jitihada mbalimbali kuhakikisha wananchi waliopata madhara wanasaidiwa huku akiwaasa kuchukua tahadhari kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Butindo Lucas Andrea amefafanua kuwa mvua iliyoleta madhara ilikuwa imeambatana na upepo mkali pamoja na vidonge vya theluji za barafu na kwamba k**a mtaa wameshatoa kiasi cha fedha kusaidia wananchi katika kukabiliana na maafa ya mvua hizo sanjari na kuwaandalia maeneo ya kujistiri kwa siku kadhaa wakati wakisubiria kurejea kwa hali za maisha ya kawaida ya kila siku

Paschal Mahiba ni Katibu wa CCM Kata ya Shibula ambapo amempongeza na kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt Angeline Mabula kwa kuchukua hatua za haraka katika kuwafariji wananchi waliopatwa na maafa ya mvua huku akiwaasa wananchi wa kata hiyo kuendelea kushirikiana nae katika shughuli za kila siku za maendeleo

Naye Samuel Miza Kayenze ambae ni Moja ya wananchi waliokumbwa na maafa hayo mbali na kumshukuru Mbunge Dkt Angeline Mabula amewataka viongozi wengine kuiga mfano wake kwani amekuwa akijitoa kwa hali na mali na kwa wakati pindi wananchi wake wanapokubwa na majanga mbalimbali.

MBUNGE SAGINI AFUNGUA MWAKA MPYA 2025 KWA KUWAPONGEZA WENYEVITI WA VIJIJI NA VIONGOZI WA MATAWI CCM KWA USHINDI WA ASILI...
01/01/2025

MBUNGE SAGINI AFUNGUA MWAKA MPYA 2025 KWA KUWAPONGEZA WENYEVITI WA VIJIJI NA VIONGOZI WA MATAWI CCM KWA USHINDI WA ASILIMIA 98.1

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amekutana na Wenyeviti wa Vijiji na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya matawi na baadhi ya mabalozi Wilaya ya Butiama kuwapongeza kwa ushindi wa asilimia 98.1 kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na vijiji uliofanyika Novemba 27, 2024.

Akizungumza na Viongozi hao katika hafla hiyo iliofanyika nyumbani kwake Kijijini Kiabakari Kata ya Kukirango leo Januari 01, 2024 Sagini amesema kuwa CCM ilishinda kwa kishindo uchaguzi uliopita kutokana na miradi ya mbalimbali ya kimaendeleo iliyopo katika jimbo lake.

"Wananchi wamekuwa na utulivu katika upigaji kura kwa kutazama miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita yenye Kauli mbiu yake ya Kazi Iendelee inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan hivyo kazi ya ilikuwa ndogo na wapiga wwnanchi walichukua na kuweka waa bila kuwa na mashaka," amesema Mhe. Sagini.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Butiama Christopher Siagi amewataka viongozi hao kujituma na kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kutopoteza uaminifu kwa wananchi waliowaamini mpaka kuwapa ushindi wa kishindo.

Pia Siagi ametumia fursa hiyo kuwapiga marufuku baadhi ya viongozi wa chama wanaojikusanya kwa watu ambao wanahitaji nafasi za ubunge na udiwani ndani ya chama katika uchaguzi ujao.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Butiama, Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Butiama, viongozi wa Dini, Serikali, Vyama rafiki, Mjumbe wa Baraza Kuu UWT Viti Vitano Bara Ndg. Mariam Sagini na Viongozi wa Umoja wa Wanawake (UWT) kutoka Kata zote 18.

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini amefanikisha kiasi cha shilingi 6,798,400/...
30/12/2024

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini amefanikisha kiasi cha shilingi 6,798,400/= , Saruji mifuko 20 na Kondoo wanne kwenye Harambee ya Tamasha la Kongoto 2024 lilofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Kongoto, Kijiji cha Kongoto, Kata ya Buswahili, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara. Desemba 30, 2024

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini kupitia Katibu wake Samson Malima amefanik...
27/12/2024

Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini kupitia Katibu wake Samson Malima amefanikisha kiasi cha shilingi 1,500,000/- katika Harambee ya Uzinduzi wa Albamu ya Kwanza ya "ASANTE MUNGU" ya Kwaya ya Mtakatifu Yuda Thadei Kigango cha Masurura Parokia ya Kiagata, Kata ya Bwiregi Wilaya ya Butiama. Desemba 27, 2024

HIMAYA YA UKOO WA WATENGENEZA MVUA Omugimba mtu mwenye uwezo wa kutengeneza au kuleta mvua Zanaki anatambulika k**a Mtaw...
24/12/2024

HIMAYA YA UKOO WA WATENGENEZA MVUA

Omugimba mtu mwenye uwezo wa kutengeneza au kuleta mvua Zanaki anatambulika k**a Mtawala (CHIEF) inakadiriwa kila kila Omugimba alitawala kati ya miaka 20 hadi 25 kwenye eneo lao la Nyabhikerya Busegwe Omugimba Muse alifikifka karne ya 16.

Orodha ya Abagimba/watawala
1. Muse 2. Kamara 3. Sabayo 4. Bukaba 5. Muya 6. Kagaya 7. Kitamihirwa 8. Mtwema 9. Sibora 10. Muhagazi 11. Kinguya 12. Kyegenya 13. Kisarwa 14. Mzumari Wanani 15. Mwiburi 16. Mukunga 17. Mweya 18. Nyeko 19. Nyarasha 20. Monge 21. Ihunyo 22. Marwa 23. Mazira.

Katika orodha hiyo Muse ndio Omugimba/mtawala pekee mwanamke aliyetawala Zanaki (Buhemba, Bumangi, Busegwe, Butuguri Buruma, Butiama, Muganza na Bukabwa) inaaminika kila Omugimba ni Nabii wa kujua mambo kwa kuota.

Ukoo wa huo unaheshimika kutokana na sifa ya kuleta mvua kwa kutumia imani/ Amasambwa k**a Kambarage, Wambura na Nyakiha-(Nyakiha yupo mpaka sasa anaishi ndani ya ngoma ya Omugimba) amefungiwa katika nyumba ya Omugimba

Mwaka 1998 Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifika kwa rafiki yake katika mji huo kumsalimia rafiki yake aliyesoma naye Mwisenge Chief Marwa Ihunyo na kuomba msamaha wa Vurugu iliyotekea mwaka 1953 dhidi ya Chief Ihunyo Monge na Msaidizi wake Chief Edward Wanzagi.

Baba wa Taifa alikiri kuwa neno Ikulu limetokana na Himaya ya Chief Ihunyo jina lake la Kambarage yaani mzimu unaoishi kwenye mvua limetokana na amasambwa ya himaya hiyo, kuwa muumini wa dini ya katoliki alipelekwa na rafiki yake huyo Chief Marwa Ihunyo kipindi alipomkuta shuleni Mwisenge.


Follow

MFAHAMU CHIEF IHUNYO WA ZANAKI Chief Marwa Ihunyo wa Kabila la Wazanaki alizaliwa Mwaka 1922 katika eneo lao la utawala ...
18/12/2024

MFAHAMU CHIEF IHUNYO WA ZANAKI

Chief Marwa Ihunyo wa Kabila la Wazanaki alizaliwa Mwaka 1922 katika eneo lao la utawala la Nyabhikerya (Ngubwe) Kijiji cha Nyanza Kata ya Busegwe Wilaya ya Butiama alisoma Mwisenge na kufaulu kwenda Bwiru Boys Mwaka 1937 ingawa hakuendelea na shule alirudi nyumbani kuwa msaidizi wa baba yake Chief Ihunyo Monge.

Mwaka 1953 vurugu ziliibuka kwenye mkutano wa baba yake Chief Ihunyo Monge na wafuasi wa Edward Wanzagi katika Kijiji cha Kigori ilipokuwa Ofisi ya Chief hali iliyopelekea kuk**atwa kwa Chief Ihunyo Monge na Kijana wake Marwa Ihunyo walihukumiwa katika Mahak**a ya Wilaya ya Musoma na kufungwa katika Gereza la Musoma.

Mwaka huo Chief Marwa Ihunyo aliachiwa na Baba yake Chief Ihunyo Monge alihamishiwa Gereza la Butimba Mwanza alifariki Mwaka 1953 na kuzikwa makaburi ya Butimba na baadaye mwili wake ulifukuliwa na kusafirishwa kuzikwa nyumbani kwake.

Chief Marwa Ihunyo alisimikwa na kutawala Zanaki Mwaka 1954-2014 na kurithi wake za baba yake zaidi ya kumi pia alioa wake watatu ambao ni Wambura Bukume wa Busegwe, Kambarage Muhindi wa Kijiji cha Buturu na Magori Kirunyire wa Buzahya alifariki Tarehe 13 Mei, 2014.

Akasimikwa Chief Mazira Ihunyo aliyezaliwa 1979 akaanza elimu yake ya Msingi katika Shule ya Msingi Busegwe (Bwana) mpaka mwaka 1994 baadaye alihamishiwa Shule ya Msingi Mwibagi 1996 kufaulu kwenda Songe Farmers Secondary School aliongoza somo la CIVIS katika mtihani wa Taifa wa Kidato cha pili Kanda ya Ziwa na kuhitimu kidato cha Nne mwaka 2000 .

Kwa sasa shule hiyo inajulikana k**a Songe Girls Secondary School ambapo alifaulu kwenda Chuo cha Ualimu Butimba na kumaliza mwaka 2003 na kuajiriwa Wilaya ya Geita ambapo alihamishiwa Busegwe kurithi nafasi ya Uchifu. Chief Mazira Marwa Ihunyo ameoa mke mmoja Nyamuya Wanga wa Buzahya.

Follow

Address

Butiama

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Daily Talk posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share