04/06/2026
POLISI YATHIBITISHA ASHLY ALIJINYOKA KITIKANA NA STRESS
Jeshi la Polisi Zanzibar limesema kifo cha Mwanamtandao wa Marekani, Ashly Robinson maarufu k**a โAshlee Jenaeโ kimetokana na kujinyonga kwasababu ya msongo wa mawazo.
Kauli ya Polisi inakuja ikiwa ni siku 57 zimepita tangu Ashlee kukutwa katika chumba chake cha Hoteli Visiwani humo, Aprili 8, 2026 akiwa amejinyonga.
Akitoa ufafanuzi leo Juni 4, 2026 kuhusu uchunguzi uliobainika kwenye tukio hilo, Naibu Kamishna wa Polisi Zanzibar ambae pia ni Naibu Kamishna wa Makosa ya Upepelezi Zanzibar, Zubeir Chembere amesema hakuna aliyebainika kumuua Ashlee zaidi ya kujinyonga na msongo wa mawazo.
Chembere amesema uchunguzi ulibaini kwenye simu yake kulikua na jumbe zilizokuwa zikiashiria kutaka kujiua ikiwemo Ashlee kuiuliza Akili Mnemba (Chart GBT ) kuhusu dawa kiasi gani anaweza kutumia ili kujitoa uhai wake. Ashlee alienda Zanzibar akiwa na mumewe mtarajiwa Joe McCann.