Big Bros Media

Big Bros Media ๐Ÿ“ป Welcome to Big Boss Radio, where the heartbeats of Tanzania unite! ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐ŸŽต No worries! And the best part?
(1)

"Welcome to Big Boss Radio (BBR), your vibrant community radio station and online TV hub, right here in the heart of Dar es Salaam! ๐Ÿ“ป๐Ÿ“บ๐ŸŒ†

Since our inception in 2018, BBR has become the heartbeat of the youth, delivering a unique blend of news, information, sports, and lifestyle content that resonates with our dynamic audience. ๐ŸŽ™๏ธ๐Ÿ“ฐ๐Ÿ€๐ŸŒŸ

We're not just about music; we're your go-to source for staying

in the know. Our programming is enhanced with timely news reports, traffic updates, and weather forecasts, ensuring you're always ahead of the game. ๐Ÿš—๐ŸŒฆ๏ธ

Can't be with us in person? We beam our broadcast to Dar es Salaam and beyond via live online streaming, making it easy for you to tune in from anywhere on the planet. You can catch up on all your favorite shows with our free podcasts available on our website. ๐ŸŒ๐ŸŽง

Our lineup of shows is designed to entertain, inform, and inspire. Dive into the sounds of 'Asubuhi Yetu,' experience the thrill of 'Sports Center,' explore the local scene with 'Tash*titi za Mtaa,' and savor 'Quality Time' on air. ๐ŸŽถ๐ŸŽค๐ŸŽ‰

Meet the friendly faces behind the microphone:
- Teddy Mzirai
- Fadhili Rashid
- Rashidi Hassan Mzee
- Flora Lugongo

BBR is more than just a radio station; it's a vibrant community that celebrates the spirit of Tanzania. Join us on this exciting journey, where every day is a new adventure in sound and stories! ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐ŸŽต๐Ÿ“ป "

POLISI YATHIBITISHA ASHLY ALIJINYOKA KITIKANA NA STRESS Jeshi la Polisi Zanzibar limesema kifo cha Mwanamtandao wa Marek...
04/06/2026

POLISI YATHIBITISHA ASHLY ALIJINYOKA KITIKANA NA STRESS

Jeshi la Polisi Zanzibar limesema kifo cha Mwanamtandao wa Marekani, Ashly Robinson maarufu k**a โ€˜Ashlee Jenaeโ€™ kimetokana na kujinyonga kwasababu ya msongo wa mawazo.

Kauli ya Polisi inakuja ikiwa ni siku 57 zimepita tangu Ashlee kukutwa katika chumba chake cha Hoteli Visiwani humo, Aprili 8, 2026 akiwa amejinyonga.

Akitoa ufafanuzi leo Juni 4, 2026 kuhusu uchunguzi uliobainika kwenye tukio hilo, Naibu Kamishna wa Polisi Zanzibar ambae pia ni Naibu Kamishna wa Makosa ya Upepelezi Zanzibar, Zubeir Chembere amesema hakuna aliyebainika kumuua Ashlee zaidi ya kujinyonga na msongo wa mawazo.

Chembere amesema uchunguzi ulibaini kwenye simu yake kulikua na jumbe zilizokuwa zikiashiria kutaka kujiua ikiwemo Ashlee kuiuliza Akili Mnemba (Chart GBT ) kuhusu dawa kiasi gani anaweza kutumia ili kujitoa uhai wake. Ashlee alienda Zanzibar akiwa na mumewe mtarajiwa Joe McCann.


ZAIYLISSA AMPA ONYO KALI DULA MAKABILAAliyekuwa mke wa Dulla Makabila, Zaiylissa amempa onyo kali mwanamuziki huyo akimt...
01/06/2026

ZAIYLISSA AMPA ONYO KALI DULA MAKABILA

Aliyekuwa mke wa Dulla Makabila, Zaiylissa amempa onyo kali mwanamuziki huyo akimtaka kuacha kutafuta kiki kupitia jina lake.

"Kwako Dulla Makabila. Nafikiri nimekaa kimya kwa muda mrefu kuhusu wewe. Licha ya yote ambayo umekuwa ukiyatenda, leo naomba nizungumze nawe kwa nia njema."

'Nafikiri sasa umefika mwisho wa kufanya mambo unayoyafanya kwangu. Inatosha. K**a ni kuniimbia, nafikiri tayari umejaza albamu nzima ukinihusu."

"Ninaamini wewe ni msanii mzuri na mwenye kipaji. Si lazima utumie kiki. Na hata k**a unaona ni sawa kufanya kiki, tafadhali zisiwahusu mimi tena. Nimechoka."

"Naomba uniache niishi kwa amani yangu. NB: Mimi ni mke wa mtu, hivyo tafadhali heshimu ndoa yangu."

"ONYO: Sitaki kukusikia tena ukiniongelea kwenye mahojiano yako. Sitaki pia kuona ukiniposti tena kwenye kurasa zako za mitandao ya kijamii. Asante." - Zaiylissa.


31/05/2026

MSANII BARNABA ALIA KWA UCHUNGU STUDIO ZAKE KUUNGUA MOTO,SOMA ALICHOANDIKA

UCHUNGU MKUBWA SANA NINAOPATA KUTOKA TAHARIFA STUDIO ZANGU ZA ( HIGHTABLESOUND ENTERTAINMENT COMPANY LTD : ZIMEUNGUA MOTO USIKU HU KUANZKA SAA 2: 30 KAMILI LEO MUDA HU NIKIWA NIMETOKA KWENYE SHOW YANGU YA MALKIA WA NGUVU ARUSHA BAADA YA KUFIKA NILIKUA NATUKIO KIJICHI KWA KINA MAMA ZANGU | NIMEPITA OFFICEN KWANGU NA KUSALIMIA NIKAENDA NYUMBANI K**A DK 15 | NAPIGIWA PANAWAKA ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ™Œ๐Ÿพ๐Ÿ˜ฉ๐Ÿ˜ฅ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ MUNGU WANGU WA MBINGUNI NINAKUSHUKURU KWA HILI NINAAMINI UNANIPITISHA KWNEYE NJIA SAHIHI DAIMA NIMETOKA KUFANYA RENOVATION WEEK MBILI NYUMA KWA GHARAMA KUBWA NA MUZIKI NDO KAZI YANGU HI SEHEMU INATEGEMEWA NA VIJANA WENGI MOYO UNANIUMA NIMELIA SANA KWA UCHUNGU NIMEKOSA NGUVU KABISA NASIKITIKA KUSEMA HQ/ YETU IMEKUA MAJIVU HOOO MUNGU BABA ASANTE KWA HI BARAKA NIMEPOKEA NA NITAANZA UPYA NAJUA KAZI ZETU NGUMU ILA DAH MAISHA YANATUFUNZA NA ILI NIMELIPOKEA K**A FUNZO

MWISHO | NAPENDA KUTOA SHUKRANI ZA DHATI KWA MAJIRANI ZANGU : MAMA MWENYE NYUMBA WANGU MAMA MAMY
WATU WAKARIBU MJUMBE WANGU
WADOGO ZANGU WOTE HIGHTABLE SOUND
๐Ÿคฒ๐Ÿฝ๐Ÿ™๐Ÿพ BILA KUSAHAU JESHI LA POLICE @๐Ÿ‘ฎโ€โ™€๏ธ
NA TEAM NZIMA YA FIRE ๐Ÿ”ฅ ASANTENI
ASANTE MAMA YANGU KIPENZI MAMA MAMY MWENYE NYUMBA WANGU NIMEKAA HAPO MIAKA ZAIDI YA 11 SASA ILA LEO HILI TUMSHUKURU MUNGU MAMA YANGU KIPENZI NAJUA UNAUMIA KWA UPENDO MKUBWA KIJANA WAKO ILA ASANTE KWA KUA NAMI MUDA WOTE LEO

SIO WAKATI WA KULAUMU MTU YOYOTE LAKINI KILA JAMBO LINATOKEA KWA MIPANGO YAKE MUNGU

ALAHAMDULIAH ๐Ÿ™๐Ÿพ๐Ÿคฒ๐Ÿฝ๐Ÿ˜ฅ๐Ÿ˜ญ

KESHO NILIKUA NIFANYE INTERVIEW PALE SELENA HOTEL NIFANYE PRESS : NAOMBA KUTOA TAHARIFA SITAWEZA KUFANYA PRESS WALA HIGHTABLE SOUND SIRI YANGU YA KIKULACHO NASTOPISHA HAITATOKA KWANZA NAOMBA MNIOMBE NAWASHUKURU WOTE NA MUNGU ATUSAIDIE SOTE ASANTE ๐Ÿ™๐Ÿพ๐Ÿคฒ๐Ÿฝ


Baada ya picha yake kujadiliwa sana mtandaoni, staa wa Singeli, Dulla Makabila ameonyesha kujutia kupiga hii picha. "Sij...
27/05/2026

Baada ya picha yake kujadiliwa sana mtandaoni, staa wa Singeli, Dulla Makabila ameonyesha kujutia kupiga hii picha.

"Sijui ilikuwaje nikakubali kupiga hii picha," ameandika Dulla Makabila huku akiambatanisha na picha yenyewe.


MADAKTARI WATAJA SABABU ZA BINT KUZEEKA GHAFLAMitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini imeendelea kugubikwa na simulizi ...
26/05/2026

MADAKTARI WATAJA SABABU ZA BINT KUZEEKA GHAFLA

Mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini imeendelea kugubikwa na simulizi ya kusikitisha ya Sinenhlanhla Khoza, mama mwenye umri wa miaka 31 kutoka Mtubatuba katika mkoa wa KwaZulu-Natal, ambaye amezeeka ghafla na kuwaawaacha wengi wakishangaa.

Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa mitandaoni, Khoza alikua akiwa na afya njema na aliendelea kuwa kawaida hadi alipofikisha takribani miaka 27, ambapo ngozi yake, viungo vya mwili pamoja na afya yake kwa ujumla vilianza kudhoofika kwa kasi kubwa.

Hali hiyo imezua mjadala mkubwa mtandaoni, huku baadhi ya wataalamu wa afya na wachambuzi wa masuala ya tiba wakidai kuwa huenda anaishi na ugonjwa adimu wa vinasaba unaojulikana k**a Werner Syndrome, ambao mara nyingi hufahamika k**a โ€œprogeria ya watu wazimaโ€, yaani hali inayosababisha mwili kuzeeka kwa kasi isiyo ya kawaida.

Werner Syndrome ni nini?

Werner Syndrome ni ugonjwa wa nadra unaosababisha mwili kuanza kuzeeka mapema zaidi kuliko kawaida, mara nyingi dalili zake zikianza kuonekana mwishoni mwa ujana au katika miaka ya ishirini.

Tofauti na progeria ya watoto, ugonjwa huu hujitokeza ukubwani, jambo linalofanya watu wengi kugundua tatizo hilo wakiwa tayari watu wazima.

Madaktari wanaeleza kuwa watu wanaoishi na hali hiyo wanaweza kukumbwa na matatizo mbalimbali ikiwemo kuzeeka kwa haraka kwa ngozi, kupoteza nywele na kupata mvi mapema, ngozi kukunjamana, uchovu mkubwa, matatizo ya macho na moyo, mifupa kuwa dhaifu, kisukari pamoja na hatari kubwa ya kupata saratani.


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewak**ata raia wanne wa China kwa tuhuma za utekaji wa wafanyabiashara ...
25/05/2026

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewak**ata raia wanne wa China kwa tuhuma za utekaji wa wafanyabiashara wenzao wawili wa Kichina, huku wakitaka kupewa Dola za Marekani milioni 20 (zaidi ya Sh. bilioni 52.5) ili wawaachie.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na K**anda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, tukio hilo lilitokea Mei 14, 2026, saa 4:30 usiku katika majengo pacha ya PSSSF yaliyopo Mtaa wa Mission, Posta Ilala.

Muliro amesema waliotekwa ni Weiyi Chen (64) na Liang Xiolo (44), wote wafanyabiashara na raia wa China, ambao ilidaiwa walivamiwa na kundi la wahalifu wapatao saba na kupelekwa kusikojulikana.

โ€œWaliotekwa wamekutwa wamejeruhiwa na kuumizwa maeneo mbalimbali, mmoja hali yake si nzuri amelazwa akiendelea na matibabu,โ€ amesema Muliro.

Muliro amewataja watuhumiwa hao wanaoshikiliwa ni Deng Anqing (49), Fan Zhong (49), Zhang Jianjun (51) na Deng Qiang (40), wote raia wa China.

Imeandikwa na Romana Mallya

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi +255 745-700 710 au 0677-020 701 kwa maelezo zaidi.


24/05/2026

Lazima Watanzania wote wafurahie matunda ya uhuru wa nchi yao. Hakuna mahali panaposema ukishakuwa na mali, ukishakuwa tajiri, wewe ni Mtanzania na nusu na wengine ni nusu Watanzania-Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba


WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMIIWAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema jamii inapasw...
24/05/2026

WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema jamii inapaswa kurejea katika misingi ya malezi ya pamoja na uwajibikaji wa kijamii ili kujenga kizazi chenye maadili, kinachoheshimu viongozi, wazazi pamoja na taasisi za jamii.

โ€œTunataka kujenga jamii inayoguswa na changamoto za wengine. Maadili mema yanaanzia kwenye malezi ya familia na jamii kwa ujumla,โ€ amesema Dkt. Mwigulu.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumapili, Mei 24, 2026 aliposhiriki Ibada ya Pentekoste katika Kanisa Kuu la KKKT Usharika wa Iringa Mjini iliyoongozwa na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Dkt. Blaston Gavile.

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii, malezi ya maadili na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi.

โ€œUshirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini ni jambo kubwa sana katika maendeleo ya nchi yetu. Shule nyingi kongwe na taasisi mbalimbali za huduma zilianzishwa na taasisi za dini kabla hata ya Serikali kuendelea kuzijenga na kuzisimamia,โ€ amesema Dkt. Mwigulu.

Aidha, Waziri Mkuu amesema kuanzia mwaka 2028 Serikali itaanza rasmi utekelezaji wa elimu ya lazima ya miaka 10 kwa watoto wote wa Kitanzania kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne kwa lengo la kuongeza ujuzi na kuwajengea vijana uwezo wa kujitegemea.

โ€œHatusemi shule ya msingi iwe miaka 10, tunasema elimu ya lazima kwa mtoto wa Kitanzania iwe miaka 10 ili watoto wetu wapate maarifa na ujuzi wa kutosha kwa maisha yao ya baadaye,โ€ amesema.

Dkt. Mwigulu amesema hatua hiyo pia inalenga kupunguza changamoto za watoto kuacha shule katika umri mdogo pamoja na kukabiliana na changamoto za ndoa za utotoni kwa kuhakikisha watoto wanabaki shuleni kwa muda mrefu zaidi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amepongeza KKKT Dayosisi ya Iringa kwa kuendelea kuwahudumia watoto yatima na watu wenye mahitaji maalum huku akieleza kuwa Serikali inaendelea kufanya maboresho ya sera na mifumo ya utoaji wa huduma kwa makundi hayo.


23/05/2026

Makonda: Vijana changamkieni fursa mbalimbali za ujio wa Miss World

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na michezo, Mhe. Paul Makonda ametoa wito kwa vijana nchini, kutumia fursa ya ujio wa Mashindano ya Ulimbwende ya dunia ambayo yatafanyika nchini Tanzania 2027 kujiinua.

Mhe. Makonda ametoa wito huo, aliposhiriki katika mbio maalum kuelekea Maadhimisho ya miaka 63 ya kuanzishwa kwa Jumuiya ya Umoja wa Afrika (AU) tarehe 23 Mei 2026 jijini Dar es Salaam.


23/05/2026

Tazama Mwili wa Baozhang ulivyowasili Kiwandani kwake huku Wafanyakazi wakiupokea mwili huo kwa huzuni kubwa

Chini huyo aliuwawa kiwandani kwake Mabibo Jijini Dar es Salaam.na wanaodaiwa kuwa walinzi wa kiwanda hiko jamii ya Wamasai.


Address

Namanga
Dar Es Salaam
14111

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Big Bros Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Big Bros Media:

Share