Big Bros Media

Big Bros Media 📻 Welcome to Big Boss Radio, where the heartbeats of Tanzania unite! 🇹🇿🎵 No worries! And the best part?
(1)

"Welcome to Big Boss Radio (BBR), your vibrant community radio station and online TV hub, right here in the heart of Dar es Salaam! 📻📺🌆

Since our inception in 2018, BBR has become the heartbeat of the youth, delivering a unique blend of news, information, sports, and lifestyle content that resonates with our dynamic audience. 🎙️📰🏀🌟

We're not just about music; we're your go-to source for staying

in the know. Our programming is enhanced with timely news reports, traffic updates, and weather forecasts, ensuring you're always ahead of the game. 🚗🌦️

Can't be with us in person? We beam our broadcast to Dar es Salaam and beyond via live online streaming, making it easy for you to tune in from anywhere on the planet. You can catch up on all your favorite shows with our free podcasts available on our website. 🌍🎧

Our lineup of shows is designed to entertain, inform, and inspire. Dive into the sounds of 'Asubuhi Yetu,' experience the thrill of 'Sports Center,' explore the local scene with 'Tash*titi za Mtaa,' and savor 'Quality Time' on air. 🎶🎤🎉

Meet the friendly faces behind the microphone:
- Teddy Mzirai
- Fadhili Rashid
- Rashidi Hassan Mzee
- Flora Lugongo

BBR is more than just a radio station; it's a vibrant community that celebrates the spirit of Tanzania. Join us on this exciting journey, where every day is a new adventure in sound and stories! 🇹🇿🎵📻 "

Rais Samia Suluhu amemteua David Kafulila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART)....
02/10/2025

Rais Samia Suluhu amemteua David Kafulila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART).

Kafulila ni Kamishna Mkuu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).


“Sasa hivi tutakuwa na jumla ya mabasi 90, haya 60 mapya na yale 30 ya bluu. Tunaamini ugumu huu utapungua kwa kiasi kik...
02/10/2025

“Sasa hivi tutakuwa na jumla ya mabasi 90, haya 60 mapya na yale 30 ya bluu. Tunaamini ugumu huu utapungua kwa kiasi kikubwa. Lakini makampuni mengine manne yaliyobaki yote yanaleta mabasi […] Baada ya hapo tunaamini jijini Dar es Salaam njia zetu zote zitakuwa na mabasi yanayopita.” – Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa


02/10/2025

Ziara ya Chris Brown yatajwa kuwa ndio ziara Bora Kwa Sasa.


02/10/2025

Nyimbo ya Amanda ya imedhidi kupasua anga kimataifa na kushika chati za juu.


02/10/2025

Msanii amekerwa na warekodi Maudhui mitandaoni.


Kocha wa zamani wa Yanga SC na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini Nasredine Nabj raia wa Tunisia kwa sasa yupo Tanzania, kit...
02/10/2025

Kocha wa zamani wa Yanga SC na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini Nasredine Nabj raia wa Tunisia kwa sasa yupo Tanzania, kitu ambacho kinazidisha uvumi kuwa huenda akajiunga na Yanga SC au Simba SC.

Yanga SC wanae Kocha wao Roman Folz lakini inatajwa kuwa hawaridhishwi na mwenendo wa timu licha ya kukaa nae muda mfupi ila Simba SC haina Kocha kabisa Mkuu baada ya Fadlu Davids kuamua kuondoka.

Nabi ameamua kuzijibia taarifa hizo baada ya kuwepo mitandaoni muda mrefu zikichochewa na uwepo wake nchini kitu ambacho amesema amekuja kwa mambo yake binafsi.

"Nimeona watu wanasema nimekuja hapa kwa ajili ya Simba, wengine wanasema Yanga, hapana! Nipo hapa kwa safari yangu binafsi, nadhani hii ni mara ya tatu nakuja hapa, Tanzania ni nyumbani ndio maana napenda sana kuja hapa, tangu nimefika sijakutana na kiongozi yeyote wa Simba wala Yanga, nikimaliza mambo yangu nitaondoka”- Nasreddine Nabi.


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejibu ripoti iliyotolewa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human R...
02/10/2025

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejibu ripoti iliyotolewa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch (HRW), iliyodai kuwa ukandamizaji wa kisiasa umeongezeka wakati taifa hilo linapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema, taarifa iliyotolewa na HRW Septemba 29, 2025, kuwa sio sahihi na ni za kupotosha huku ikikanusha pia taarifa za kutekwa kwa raia nchini humo.

“ Madai kuwa kuna kupungua kwa uhuru wa kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025 si ya kweli,” Taarifa hiyo imesema.

“Katiba ya nchi inatoa haki ya kuishi, usalama na uhuru kwa kila Mtanzania,” Taarifa hiyo imeongeza.

Ikijibu taarifa ya HRW, Tanzania imesema ipo tayari wakati wote kushirikiana na taasisi yoyote inayotafuta taarifa sahihi.

Taarifa ya HRW ilisema kuwa mamlaka nchini Tanzania zimekandamiza upinzani na wakosoaji wa chama tawala, zinanyamazisha vyombo vya habari, na zimeshindwa kuhakikisha uhuru wa tume ya uchaguzi.

“Mamlaka ya Tanzania inapaswa kuchukua hatua za haraka kulinda uadilifu wa uchaguzi wa Oktoba, ambao kwa sasa uko katika hatari kubwa,” alisema Nomathamsanqa Masiko-Mpaka, mtafiti wa Afrika katika Human Rights Watch.

“Mamlaka inahitajika kujizuia kukandamiza upinzani na vyombo vya habari, na badala yake hushiriki katika mageuzi yenye maana ili kuhakikisha uchaguzi huru, wa haki na wa kuaminika,” Taarifa ya HRW ilisema.

Tanzania imelaumu shirika hilo kwa kutoa taarifa za aina hiyo bila kuipatia fursa ya kujibu kabla ya kuchapishwa.

Tanzania imesema kuwa imejipanga kuhakikisha haki za binadamu, demokrasia, utawala bora na sheria vinaheshimiwa kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa 2025.


Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Mangungu amewajibu wanaohoji ni lini Simba SC watakuwa na Kocha mpya baada ya Fadlu David...
02/10/2025

Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Mangungu amewajibu wanaohoji ni lini Simba SC watakuwa na Kocha mpya baada ya Fadlu Davids kuondoka na kujiunga na Raja Casablanca ya Morocco.

Mangungu amewajibu na kusema Simba SC haijaweka deadline ya lini itakuwa na Kocha mpya ila inafanya tathmini na kufanya machaguo sahihi.

Mangungu aliulizwa pia kuhusiana na Kocha wa zamani wa Yanga SC aliyekuwa anaifundisha Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini Nasredine Nabi yupo nchini kwa ajili ya mazungumzo na Simba SC k**a inavyodaiwa?

“Tutakapokuwa tayari tutatoa taarifa (kuhusu Kocha) kwamba nani ambaye tumeingia nae makubaliano ili shughuli zingine ziendelee, sawa mashabiki wana kiu ya kujua ila unapokuwa na kiu unasubiri kinywaji kikufikie”

“Nani ambaye anamuhusisha (Nabi) na Simba?, vigumu mimi kuweza kujibia watu wengine,huyo ambaye anasema anaweza kuwa ana taarifa nzuri zaidi, mkiwasiliana nae yeye anaweza kuwapa hiyo taarifa ila taarifa rasmi ya Simba itatolewa pale itakapokuwa imekamilika”

Simba SC kwa sasa haina Kocha Mkuu baada ya Fadlu Davids raia wa Afrika Kusini kuvunja Mkataba na Simba SC na kuamua kurejea timu yake ya zamani ya Raja Casablanca ya Morocco, Seleman Matola anaendelea kusalia akiwa Kocha Msaidizi.


Mabasi mapya ya Mwendokasi ya Kampuni ya MOFAT leo October 2 2025 yameanza kubeba Abiria wa Mbezi - Kimara ili kuondoa k...
02/10/2025

Mabasi mapya ya Mwendokasi ya Kampuni ya MOFAT leo October 2 2025 yameanza kubeba Abiria wa Mbezi - Kimara ili kuondoa kero kubwa iliyokuwepo katika barabara hiyo ya upungufu pamoja na ubovu wa Mabasi ya Mwendokasi.

Mabasi hayo yameanza kazi asubuhi hii ikiwa ni saa chache tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila atangaze jana ya kwamba kwa agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, baadhi ya Mabasi ya MOFAT ambayo ni maalum kwa njia ya Mbagala yatahamishiwa kwenye barabara Kimara ili kuondoa changamoto ya uhaba wa Mabasi iliyopo kwa sasa.

Mabasi haya mapya leo yameanza kubeba Abiria kwenye barabara ya mwendokasi kuanzia Kimara mwisho kuelekea Gerezani, Kivukoni na Morocco ambapo AyoTV asubuhi hii imeshuhudia Abiria wakipanga mstari kuyapanda mabasi hayo.


Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar es salaam waliodai kuchoshwa na kero na kusuasua kwa huduma za Mabasi ya Mwendokasi, wam...
02/10/2025

Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar es salaam waliodai kuchoshwa na kero na kusuasua kwa huduma za Mabasi ya Mwendokasi, wameyashambulia kwa mawe Mabasi ya Mwendokasi pamoja na Vituo vinne vya Mabasi hayo Jijini Dar es salaam.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maaulum ya Dar es salaam Muliro Jumanne kwenye mahojiano, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa vurugu zimetokea katika Vituo vinne vya Mabasi hayo ambavyo ni Gerezani, Magomeni Mapipa, Usalama na Kagera na kuongeza kuwa tayari Polisi wanawahoji Watu kadhaa kutokana na matukio hayo.

““Kuna fujo zilitokea pale Gerezani na ikaja ikatokea Magomeni Mapipa, Usalama na Kagera kuna gari ilichelewa pale Gerezani kuna Watu wakafanya fujo pale kwa kulishambulia, baadae kuna gari lilikuja pale Mapipa likapata hitilafu Abiria wakashuka na baadhi ya Abiria wakachukua mawe wakaharibu lile gari kwenye baadhi ya vioo” -— ameeleza Kamanda Muliro.

“Kazi yetu kuhakikisha usalama unaimarika, mpaka sasa kuna Watu tunawahoji ambao inadaiwa walikuwa sehemu ya vurumai, pia baadhi walifanya fujo maeneo ya Kituo cha Polisi cha Usalama na pale Kagera baadhi ya magari yakaharibiwa vioo vyake na baadhi ya Vituo vikapata madhara ya fujo zile” - Muliro.

“Polisi walifika na kudhibiti hali ile maeneo ya Kagera sababu mabasi yalikuwa yanapandisha Ubungo mpaka Kimara, hali ile ilithibitiwa na kusema kweli pamoja na sababu mbalimbali zilizokuwa zinaelezwa lakini suala la kuharibu miundombinu ya usafiri ni kosa kisheria hata ukitoa sababu mbalimbali, maeneo ya Kagera lile kundi tulilazimika kuhakikisha kwamba wanajua Polisi amefika pale wakatawanyika pale wakakimbilia maeneo Mburahati” - ameeleza Kamanda Jumanne Muliro.


Address

Namanga
Dar Es Salaam
14111

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Big Bros Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Big Bros Media:

Share