Big Bros Media

Big Bros Media 📻 Welcome to Big Boss Radio, where the heartbeats of Tanzania unite! 🇹🇿🎵 No worries! And the best part?
(1)

"Welcome to Big Boss Radio (BBR), your vibrant community radio station and online TV hub, right here in the heart of Dar es Salaam! 📻📺🌆

Since our inception in 2018, BBR has become the heartbeat of the youth, delivering a unique blend of news, information, sports, and lifestyle content that resonates with our dynamic audience. 🎙️📰🏀🌟

We're not just about music; we're your go-to source for staying

in the know. Our programming is enhanced with timely news reports, traffic updates, and weather forecasts, ensuring you're always ahead of the game. 🚗🌦️

Can't be with us in person? We beam our broadcast to Dar es Salaam and beyond via live online streaming, making it easy for you to tune in from anywhere on the planet. You can catch up on all your favorite shows with our free podcasts available on our website. 🌍🎧

Our lineup of shows is designed to entertain, inform, and inspire. Dive into the sounds of 'Asubuhi Yetu,' experience the thrill of 'Sports Center,' explore the local scene with 'Tash*titi za Mtaa,' and savor 'Quality Time' on air. 🎶🎤🎉

Meet the friendly faces behind the microphone:
- Teddy Mzirai
- Fadhili Rashid
- Rashidi Hassan Mzee
- Flora Lugongo

BBR is more than just a radio station; it's a vibrant community that celebrates the spirit of Tanzania. Join us on this exciting journey, where every day is a new adventure in sound and stories! 🇹🇿🎵📻 "

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki maadhimisho ya Sik...
25/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki maadhimisho ya Siku ya Mashujaa katika uwanja wa Mashujaa, Mtumba Jijini Dodoma leo, tarehe 25 Julai, 2025.


Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Maadhimisho ya s...
25/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa katika uwanja wa Mashujaa Mtumba Jijini Dodoma tarehe 25 Julai, 2025.


Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na mkewe Brigitte wamewasilisha kesi ya kuchafuliwa jina dhidi ya mshawishi wa mrengo w...
25/07/2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na mkewe Brigitte wamewasilisha kesi ya kuchafuliwa jina dhidi ya mshawishi wa mrengo wa kulia Candace Owens, ambaye anadai kuwa mke wa rais wa Ufaransa alizaliwa akiwa mwanaume.

Kesi iliyowasilishwa siku ya Jumatano katika jimbo la Delaware nchini Marekani, ilisema Owens amekuwa akieneza “hadithi zisizo za kawaida na kuwaharibia jina”.

Owens amerudia mara kwa mara madai hayo kwenye podcast yake maarufu na chaneli za mitandao ya kijamii, na mnamo mwezi Machi 2024 alisema kwamba angeweka hatarini “sifa yake kitaalam” kwa imani kwamba Bi Macron “ni mwanaume”.
Katika kipindi cha podikasti yake iliyotolewa Jumatano, Owens aliendeleza madai yake na kuzungumza juu ya kesi hiyo akisema: “Huu ni upuuzi”
Owens alimdhihaki mke wa rais wa Ufaransa na kuelezea kush*takiwa naye k**a “mkakati wa wazi na wa kukata tamaa…”.

Dhana ambayo imesambaa kwa miaka mingi kwenye mitandao ya kijamii inadai kuwa Bi Macron alizaliwa akiwa mwanaume kwa jina la Jean-Michel Trogneux, ambaye ni kaka yake.

Owens ameeneza dhana hiyo kwa watazamaji wake, ikiwa ni pamoja na karibu wafuasi 7m kwenye mtandao wa X. Mapema mwaka huu alitoa mfululizo wa video unaoitwa ‘Becoming Brigitte’.

Upande wa Macron ulisema katika taarifa iliyotolewa na mawakili wao kwamba walimwomba Owens mara kwa mara kufuta madai hayo, lakini “hatimaye waliamua kupeleka suala hilo mahak**ani kwa sababu ndiyo njia pekee iliyosalia kupata suluhu”.

“Kampeni ya Bi Owens ya kumharibia sifa ilibuniwa kutunyanyasa na kusababisha maumivu kwetu na familia zetu na kuvutia nadhari na sifa mbaya,” ilisema taarifa hiyo.


Vita imezidi kupamba moto baada ya Rapper  kumjibu  kuhusu kile alichosema kufanyiwa fitna za kufungwa kisa wizi ambao  ...
25/07/2025

Vita imezidi kupamba moto baada ya Rapper kumjibu kuhusu kile alichosema kufanyiwa fitna za kufungwa kisa wizi ambao ameweka wazi kuwa Hakuhusika kwa lolote.

Sasa katika uwanja wa komenti wa post msanii Alishusha ujumbe wake kuhusu kile alichosema jambo ambalo limemfanya mke mtu kushuka katika uwanja wa komenti na kumjibu kuwa apunguze wivu

Swipe kusoma alichoandika


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea Chuo Kikuu cha Kilimo cha Belarus (Belarusian State Agrarian Technical Universit...
25/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea Chuo Kikuu cha Kilimo cha Belarus (Belarusian State Agrarian Technical University - BSATU) na kufanya mazungumzo na viongozi wa chuo hicho wakiongozwa na Mkuu wa Chuo, Bw. Romaniuk Nikolai.
 
Mazungumzo hayo yamefanyika leo (Jumatano, Julai 23, 2025) kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo hicho jijini Minsk ambapo masuala ya ushirikiano baina ya vyuo vikuu vya Tanzania vikiwemo vya Sokoine na DIT yalijadiliwa.
 
Waziri Mkuu aliwaeleza viongozi wa chuo kikuu hicho jinsi Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ilivyoboresha sera ya elimu ambayo inataka elimu ya amali na stadi za ufundi ziwe sehemu muhimu katika mitaala ya mafunzo yanayotolewa nchini kote.
 
Aliwaeleza viongozi hao juu ya hati ya makubaliano kwenye sekta ya elimu iliyosainiwa jana mbele ya Waziri Mkuu wa Belarus na kwamba sasa ni wakati muafaka wa kuangalia namna ya kuandaa ziara za mafunzo, kubadilishana wanafunzi na wahadhiri ili kujengeana uwezo kwa pande zote mbili.
 
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo Kikuu cha BSATU, Bw. Romaniuk Nikolai alimhakikishia Waziri Mkuu kwamba chuo hicho kipo tayari kuanza majadiliano na viongozi kutoka Wizara ya Elimu ambao wamefuatana na Mheshimiwa Waziri Mkuu ili waone ni kwa namna gani wanaweza kuanza kutekeleza mambo yaliyojadiliwa.
 
Alimweleza Waziri Mkuu kwamba Chuo Kikuu hicho ambacho kilianzishwa mwaka 1954, kinaongoza nchini humo kwa kutoa mafunzo kwenye fani za uhandisi, uchumi na utawala na kinashirikiana na taasisi na mashirika rafiki 39 (affiliate organisations) yanayojihusisha na masuala ya kilimo na uundaji wa mitambo ya kilimo na zana za kisasa.
 
Alisema wanalenga zaidi fani za kitaalamu kwenye ufugaji wa wanyama na mitambo ya kilimo (animal husbandry and agricultural mechanisation) ambapo asilimia 70 ya mafunzo yanayotolewa chuoni hapo, hufanyika kwa vitendo (practicals) na kisha mwanafunzi anapewa wiki 28 za kwenda nje ya chuo kufanya mafunzo kwa vitendo (internship).


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Waziri Mkuu wa Belarus, Alexander Turchin  na kujadiliana naye masuala ya uweke...
23/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Waziri Mkuu wa Belarus, Alexander Turchin na kujadiliana naye masuala ya uwekezaji, biashara, nishati, madini, elimu, afya, teknolojia na kilimo kwenye kikao kilichofanyika leo (Jumanne, Julai 22, 2025) ofisini kwa mwenyeji wake, mtaa wa Sovetskaya, jijini Minsk.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Mkuu Majaliwa alimweleza mwenyeji wake kuwa, mbali na kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia anataraji kuwa ziara hiyo itaongeza chachu ya nchi hiyo kushirikiana na Tanzania kwenye masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji, elimu, afya na upatikanaji wa zana za kisasa kwenye kilimo kutokana na fursa mbalimbali zilizoko nchini.

Alisema mazungumzo yao yamefungua milango ya kuimarisha uwekezaji, fursa za biashara na masomo katika vyuo vya elimu ya juu, na kwamba wamekubaliana na mwenyeji wake kuwa Mawaziri wake na Naibu Makatibu Wakuu walioko kwenye ziara hiyo wakutane ili kuanza majadiliano rasmi ya kufanikisha nia ya kampuni ya Minsk Tractor Plant OJSC ya kuleta kiwanda k**a hicho nchini.

Aliwaeleza baadhi ya wajumbe wa kikao hicho wanaotoka Chama cha Wafanyabiashara cha Belarus kwamba hivi sasa Tanzania imepunguza muda wa kupata leseni, imeongeza maeneo ya uwekezaji (TISEZA) na imeboresha sheria za kikodi ili kuhamasisha uwekezaji nchini.

Aliwaeleza fursa nyingine za kuwekeza Tanzania ni uwepo wake kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jumuiya ya kikanda ya SADC na Eneo Huru la Biashara barani Afrika (ACfTA) pamoja na uwepo wa nchi sita zinazoizunguka Tanzania na hazina bandari (land-locked countries) ambazo zina wakazi wengi.

Katika kikao hicho, Mawaziri Wakuu wote wawili walishuhudia utiaji saini wa hati tatu za makubaliano na maktaba mmoja baina ya mawaziri wa nchi hizo mbili. Hati hizo zilizosainiwa leo zinahusu mashauriano ya kisiasa; makubaliano ya kuendeleza sekta ya kilimo na sekta ya elimu.

Aidha, mkataba uliosainiwa leo ni baina ya Chama cha Wafabiashara, Viwanda na Kilimo ya Tanzania (TCCIA) na Chama cha Wafabiashara wa Belarus unaolenga kukuza ushirikiano wa kibiashara baina ya nchi hizo mbili.


Wananchi wajasiriamali kupitia makundi wanawake, vijana na wenye ulemavu wamehimizwa kuchangamkia fursa na kuchukua miko...
23/07/2025

Wananchi wajasiriamali kupitia makundi wanawake, vijana na wenye ulemavu wamehimizwa kuchangamkia fursa na kuchukua mikopo isiyokuwa na riba, inayotolewa na Serikali kupitia asilimia 10 za mapato ya ndani ya halmashauri zao.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe.Kenani Laban Kihongosi alipokutana na wakazi wa Arusha kwa makundi ya wafanyakazi na wamiliki wa saluni pamoja na kundi la waendesha bodabodada, bajaji na maguta, Jijini Arusha Julai 22,2025.

Mhe.Kihongosi amesema kuwa, Serikali imetoa fursa hiyo ili kuwawezesha wananchi wajasiriamali wasio na uwezo na sifa za kukopesheka kwenye taasisi nyingine za kifedha ili waweze kukuza mitaji yao ya biashara sambamba na kujikwamua kikuchumi hivyo ni wakati wao wa kuchangamkia fursa hiyo.

Ametoa mfano wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ambalo tayari lina shilingi Bilioni 5.5 kwa ajili ya kuwakopesha wajasiriamali wenye sifa kwa makundi hayo na kuwasisitiza kujiunga kwenye vikundi na kwenda kupata fedha hizo ambazo Serikali imetenge kwa ajili yao.

"Jamani ndugu zangu msiogope, hapa Jiji la Arusha kuna shilingi Bilioni 5.5, tumieni fursa hii adhimu, nendeni mkakope fedha zisizo na riba, fedha ambazo masharti yake sio magumu k**a ilivyo kwa Taasisi za kifedha, fuateni taratibu mpate fedha zipo kwa ajili yenu" Ameweka wazi Mhe.Kihongosi

Hata hivyo, amewasisitiza wajasiriamali hao, kufanya biashara zao huku wakiwa na malengo ya maendeleo na sio kutumia pesa zao vibaya na kuishia kwenye majuto na kulalamika, kwa kuwa unapoweza kutunza kidogo unachopata ni rahisi kijifanyia shughuli za maendeleo kutokana na kidogo kinachopatikana.

"Pesa unayopata hakikisha unaipangilia na kuitumia vizuri, hakuna pesa ndogo, hicho hicho kidogo kipangilie na kukitumia vizuri, wenye mafanikio huanzia chini, k**a vijana msitamani maisha ya wengine, riziki unayoipata ndio Mungu amekupangia jipange kupambana na maisha kwa fedhq hiyo unayoipata kupitia biashara yako hiyo hiyo unayoiita ndogo" Ameshuri Mhe. Kihongosi.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Zanzibar inahitaji waw...
23/07/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Zanzibar inahitaji wawekezaji zaidi, hususan katika sekta ya utalii na uwekezaji, ambazo ni sekta za kipaumbele kwa ukuaji wa uchumi.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada, Mhe. Randeep Sarai, aliyefika Ikulu Zanzibar leo tarehe 22 Julai 2025.

Rais Dkt. Mwinyi ameishukuru Serikali ya Canada kwa kuendelea kutoa misaada ya maendeleo kwa Tanzania, ikiwemo Zanzibar.

Ameeleza kuwa misaada ya nchi hiyo katika sekta ya elimu na afya imekuwa na mchango mkubwa katika kuleta mageuzi ya kimkakati ya kuimarisha huduma za afya na maendeleo ya elimu hapa nchini.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amemueleza Waziri Randeep kuwa bado zipo fursa nyingi zaidi za kuwekeza Zanzibar, huku akibainisha uwepo wa sera na vivutio maalum kwa wawekezaji wanaowekeza visiwani humo.

Akizungumzia Uchaguzi Mkuu ujao, Dkt. Mwinyi ameihakikishia Canada kuwa uchaguzi huo utakuwa huru, wa amani na utulivu, kutokana na kuimarika kwa mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa uliosaidia kuwaunganisha wananchi na kudumisha hali ya amani na utulivu kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, hali ambayo anaamini itaendelea hata wakati na baada ya uchaguzi.

Naye Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada, Mhe. Randeep Sarai, ameihakikishia Zanzibar kuendelea kwa ushirikiano na utekelezaji wa programu mbalimbali za maendeleo zinazofadhiliwa na nchi hiyo, hususan katika sekta za elimu na afya.


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt  ametoa Tsh Bilioni kwa ajili ya mikopo kwa wanawake,vijana na watu wenye u...
23/07/2025

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt ametoa Tsh Bilioni kwa ajili ya mikopo kwa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ambapo kwa Mkoa wa Arusha mikopo hiyo imeongezeka mara kumi kutoka shilingi Bilioni 3.08 mwaka 2021 hadi shilingi Bilioni 13.55 mwaka 2025.

Vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo pia vimeongezeka kutoka 721 mwaka 2021 mpaka 1,380 mwaka 2025 vimenufaika ikiwa ni ongezeko la vikundi 659.

Aidha, kwa ngazi ya kitaifa ameongeza mikopo hiyo kwa zaidi ya mara tatu ambapo wakati anaingia madarakani mwaka 2021, mikopo iliyotolewa ilikua ni kiasi cha shilingi bilioni 22.3 na mwaka 2025 iliongezeka na kufikia bilioni 82.84 ikiwa ni ongezeko la shilingi bilioni 60.54 sawa na 271%.


Baadhi ya vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania bara (NBC Premier League) ,vimeonyesha nia ya kuhitaji saini ya win...
23/07/2025

Baadhi ya vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania bara (NBC Premier League) ,vimeonyesha nia ya kuhitaji saini ya winga wa mpira Marijani Twaibu Abdallah (23),aliyemaliza mkataba na klabu yake ya Big Man Fc inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara.

Vilabu k**a Pamba jiji Fc,Mashujaa Fc ,Dodoma jiji Fc pamoja na Tanzania Prisons vipo katika vita ya kuhitaji kuinasa saini ya nyota huyo ikiwa ni pamoja na vilabu vingine vilivyopanda ligi kuu k**a Mbeya City na Mtibwa ambavyo navyo vimeonyesha kuvutiwa na mchezaji huyo aliyeonyesha kiwango bora sana akiwa na klabu ya Big Man Fc msimu uliopita kwenye ligi daraja la kwanza.

Twaibu ambaye anauwezo wa kucheza nafasi za Winga namba 7,10 na 11 akiwa Uwanjani,ameshawahi kupita katika vilabu kadhaa ikiwemo Kundemba Fc ya Zanzibar,Ihefu Fc,na Stand United ya shinyanga,Lakini kubwa zaidi katika historia ya mchezaji huyu alishawahi kufanya majaribio katika baadhi ya klabu za nchini Rwanda.


📌RATIBA YA UTEUZI WA WAGOMBEA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU 2025
23/07/2025

📌RATIBA YA UTEUZI WA WAGOMBEA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU 2025


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, leo tarehe 22 Julai 2025, ameendelea na ziara yake rasmi nchini Belarus kwa kutembelea maen...
22/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, leo tarehe 22 Julai 2025, ameendelea na ziara yake rasmi nchini Belarus kwa kutembelea maeneo muhimu ya uzalishaji na ushirikiano wa kimkakati.

Akiwa katika mji wa Minsk, Mheshimiwa Majaliwa alitembelea kiwanda cha Belmedpreparaty, ambacho ni maarufu kwa utengenezaji wa dawa za binadamu.

Aidha, Waziri Mkuu pia alitembelea kiwanda cha Minsk Tractor Plant, ambacho kinajihusisha na utengenezaji wa matrekta na mitambo ya kisasa ya zana za kilimo. Ujumbe wa Tanzania ulijionea teknolojia ya hali ya juu inayotumika katika uzalishaji wa vifaa hivyo.

Wakati wa ziara hiyo, pamoja na viongozi wengine, Waziri Mkuu aliambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Cosato Chumi.

Mheshimiwa Majaliwa pia aliweka shada la maua katika mnara wa mashujaa wa Jamhuri ya Beralus.

Kwa ujumla, ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Tanzania kuimarisha mahusiano ya kimataifa kwa manufaa ya wananchi, hasa katika sekta muhimu za maendeleo k**a afya na kilimo.


Address

Kinondoni

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Big Bros Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Big Bros Media:

Share