06/06/2026
BALOZI WETU WA KWANZA MAZOEZINI
Hakuna kustaafu kwenye Afya, Afya ni uwekezaji ,Afya Ndo Mtaji wa kwanza.
Akiungana na dunia katika maadhimisho ya wiki ya usafiri wa baiskeli na faida zake ,Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ameendelea kuonesha mfano kwa kutumia baiskeli kufanya mazoezi ya asubuhi
Mstaafu Majaliwa ameonekana mapema leo asubuhi akiendesha baiskeli katika viunga mbalimbali vya Jiji la Dar es salaam, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kila siku wa kujenga afya na kuimarisha mwili.
Bima Yetu ni Mazoezi ,Kwa mujibu wa Wataalamu wa Afya na Wadau wa Mazoezi, wanatujuza kuwa kuendesha baiskeli ni aina ya mazoezi ya mwili ambayo husaidia kuimarisha moyo , mifupa , mwili kuwa strong na mapafu, kuboresha mzunguko wa damu pale unapokuwa unanyonga pedeli .
Asante Balozi Wetu kwa hamasa hii kubwa ya kulinda Afya zetu kwa kuheshimu mazoezi
•
•