
11/07/2024
DROO YA CAF CL & CAFCL NI LEO
Kwa mujibu wa mfumo wa CAF kwenye klabu bingwa Afrika kupanga mechi za awali wana jumla ya makundi matatu, ambapo kuna timu tano ambazo hazitocheza hatua ya awali ( Preliminary) timu hizo ni Al Ahly, Esperance, Mamelodi, Petro na TP Mazembe.
Kisha kuna timu nne (4) ambazo zinatambuliwa k**a HIGHEST RANKED yaani ziko na alama nyingi kwenye mfumo wa CAF ambazo timu hizo ni YANGA 🇹🇿, Pyramids, Raja na CR Belouzdad.
Kiufundi ukichukua hizo timu tano za juu kisha ukijumlisha na hizo nne basi unaenda kupata jibu ya timu bora Afrika kwa mujibu wa CAF kwenye klabu bingwa Afrika, Premier Club Competitions.
Lakini bado Yanga ataanzia hatua za awali sambamba na hao wenzake watatu, ni timu tano tu hazitoanzia hatua za awali.
Kwa upande wa Kombe la Shirikisho timu ambazo hazitaanzia hatua ya awali zipo 12 ambazo ni;
SIMBA SC- Tanzania
RS BERKANE- Morocco
FC LUPOPO- DR Congo
STADE MALIEN- Mali
ENYIMBA FC-Nigeria
ASEC MIMOSAS- Ivory Coast
ZAMALEK SC- Misri
USM Alger- Algeria
AS Vita- DR Congo
SHEKUKHUNE FC- Zambia
EL MASRY- Misri
CS Sfaxien- Tunisia