Meridian Sport

  • Home
  • Meridian Sport

Meridian Sport Ukurasa wako namba moja wa habari za michezo Tanzania na kimataifa!

Rasmi sasa Kylian Mbappe atavaa jezi namba 10 pale Real Madrid kwa msimu ujao. Ikumbukwe kuwa namba hiyo ilikuwa inavali...
24/07/2025

Rasmi sasa Kylian Mbappe atavaa jezi namba 10 pale Real Madrid kwa msimu ujao. Ikumbukwe kuwa namba hiyo ilikuwa inavaliwa na Luca Modric ambaye alidumu kalbuni hapo miaka 10.

Mbappe alipotua Real alikabidhiwa jezi namba 9, huku akiondoka k**a mfungaji bora wa msimu uliopita. Je Kylian msimu ujao atapata mafanikio gani mbele ya kocha mkuu Xabi Alonso?

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni k**a vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Klabu ya Chelsea imeibuka kuwa bingwa wa Kombe la Dunia la vilabu hapo jana baada yakuitandika PSG mabao 3-0. Mabao hayo...
14/07/2025

Klabu ya Chelsea imeibuka kuwa bingwa wa Kombe la Dunia la vilabu hapo jana baada yakuitandika PSG mabao 3-0. Mabao hayo yote yalifungwa kipindi cha kwanza na Cole Palmer (2) na Joao Pedro (1).

Chelsea chini ya Enzo Maresca wanakuwa timu ya kwanza kuchukua ubingwa wa mashindano haya huko Marekani ambayo mwaka huu yamekuja kwa mfumo mpya kwa kushirikisha timu 32 kutoka mabara yote Duniani.

Je vipi huko mkeka wako ulisalimika?. Matokeo haya umeyapokeaje?

Meridianbet inakukumbusha kupiga pesa kwa kucheza michezo ya kasino ya mtandaoni k**a vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Kiungo wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand, ameonya kuwa klabu hiyo inaweza kujikuta ikidhalilika zaidi msimu ...
10/07/2025

Kiungo wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand, ameonya kuwa klabu hiyo inaweza kujikuta ikidhalilika zaidi msimu huu iwapo watashindwa kumsajili mshambuliaji hatari Victor Osimhen.

Ferdinand amesisitiza kuwa Osimhen ndiye mshambuliaji wa kati ambaye United wanamhitaji kwa sasa, na kuongeza kuwa ni "aina ya mchezaji ambaye klabu hiyo imekuwa ikimlilia kwa muda mrefu."

Ameeleza kuwa kushindwa kumpata staa huyo wa Nigeria kutakuwa pigo kubwa, hasa wakati huu ambao kikosi cha United kinakosa mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao kwa uthabiti msimu mzima.

Nyota wa Liverpool, Luis Díaz, anazidi kuhusishwa na vilabu vya Barcelona na Bayern Munich, huku mustakabali wake ukiwa ...
10/07/2025

Nyota wa Liverpool, Luis Díaz, anazidi kuhusishwa na vilabu vya Barcelona na Bayern Munich, huku mustakabali wake ukiwa kitendawili kinachovuta macho ya mashabiki wa soka barani Ulaya.

Kwa sasa, Barcelona wanaendelea kuwa na matumaini, lakini wanakumbwa na changamoto za kifedha na masuala ya usajili. Klabu hiyo inahitaji kuhakikisha Díaz anasajiliwa rasmi kabla ya tarehe 31 Agosti, vinginevyo mkataba utahitaji kipengele cha fidia (compensation clause), jambo ambalo linaweza kuwa kikwazo.

Wakati huo huo, Bayern Munich wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri zaidi. Klabu hiyo ya Ujerumani ipo tayari kutuma ofa ya €60 milioni pamoja na nyongeza ya hadi €20 milioni k**a bonasi, ofa ambayo inaweza kufikia mahitaji ya Liverpool.

Kwa upande wa Liverpool, msimamo ni kwamba Díaz si mchezaji wa kuuzwa, isipokuwa wakipokea ofa inayokaribia €80 milioni au zaidi. Klabu hiyo bado inamthamini sana mshambuliaji huyo ambaye ana mkataba hadi mwaka 2027.

Jordan Henderson, Nahodha wa zamani wa Liverpool na kiungo mkongwe wa England, ameachana rasmi na klabu ya Ajax baada ya...
10/07/2025

Jordan Henderson, Nahodha wa zamani wa Liverpool na kiungo mkongwe wa England, ameachana rasmi na klabu ya Ajax baada ya kuamua kutoongeza mkataba wake wa mwaka mmoja zaidi, ambao ungeendelea hadi mwaka 2026.

Henderson, mwenye umri wa miaka 34, alijiunga na Ajax mwezi Januari 2024 kwa mkataba wa miezi 18 baada ya kipindi kifupi kisicho na mafanikio sana katika Ligi ya Saudi Arabia. Akiwa Ajax, alicheza mechi 37 na kufunga bao moja, huku akipewa pia unahodha na kocha mpya Francesco Farioli, jambo lililodhihirisha umuhimu wake ndani ya kikosi.

TAARIFA KUTOKA TFF.Dirisha la usajili kwaajili ya msimu mpya wa 2025-26 🇹🇿 litafungwa Septemba 7, 2025 saa 5:59 usiku. D...
09/07/2025

TAARIFA KUTOKA TFF.

Dirisha la usajili kwaajili ya msimu mpya wa 2025-26 🇹🇿 litafungwa Septemba 7, 2025 saa 5:59 usiku. Dirisha hilo lilifunguliwa tarehe 01 July na mpaka sasa zimebaki siku 59 pekee.

"Malengo yetu msimu ujao kwenye CAF Champions League ni makundi ila nataka niwahakikishie mashabiki na wanachama tukiing...
09/07/2025

"Malengo yetu msimu ujao kwenye CAF Champions League ni makundi ila nataka niwahakikishie mashabiki na wanachama tukiingia makundi tu kitakachobaki itakuwa ni historia, ila pia tutafanya usajili bora ambao utakidhi vigezo vya sisi kuingia makundi"

Hersi Said, Rais wa Yanga SC.

Azam FC wamethibitisha rasmi kurejea kwa golikipa wa kimataifa wa Tanzania, Aishi Manula, kwa mkataba wa miaka mitatu ut...
09/07/2025

Azam FC wamethibitisha rasmi kurejea kwa golikipa wa kimataifa wa Tanzania, Aishi Manula, kwa mkataba wa miaka mitatu utakaoendelea hadi mwaka 2028.

Manula anarudi Azam FC baada ya takriban miaka 8 tangu aondoke klabuni hapo mwaka 2017 kwenda Simba SC, ambako amekuwa golikipa tegemeo kwa muda wote huo. Ujio wake unaleta uzoefu mkubwa kwenye kikosi cha Azam FC huku wakijiandaa kwa msimu mpya wa mashindano ya ndani na kimataifa.

Klabu ya Bayern Munich imetangaza rasmi kuwa Jamal Musiala amepata majeraha ya kuvunjika kwa mfupa wa mguu (fibula) baad...
09/07/2025

Klabu ya Bayern Munich imetangaza rasmi kuwa Jamal Musiala amepata majeraha ya kuvunjika kwa mfupa wa mguu (fibula) baada ya kuteguka kwa kifundo cha mguu kkwenye mchezo wa robo fainali dhidi ya PSG.

Nyota huyu chipukizi wa Ujerumani sasa atapitia upasuaji katika siku chache zijazo na inasemekana anatarajia kukaa nje kwa kipindi kisichopungua miezi mitano mpaka sita.

Hili ni pigo kubwa kwa klabu na taifa, kwani Musiala alitarajiwa kuwa sehemu muhimu katika msimu unaokuja.

Genoa wako katika mazungumzo ya hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kipa Daniel Peretz kutoka FC Bayern. Klabu hiyo y...
08/07/2025

Genoa wako katika mazungumzo ya hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kipa Daniel Peretz kutoka FC Bayern. Klabu hiyo ya Italia imetuma ofa rasmi kwa Bayern Munich ya mkopo wenye kipengele cha kununua mchezaji huyo moja kwa moja mwishoni mwa msimu.

Makubaliano kati ya pande zote mbili yako karibu kukamilika, huku Peretz akiwa chaguo kuu la Genoa katika nafasi ya mlinda mlango kwa dirisha hili la usajili wa majira ya kiangazi. Mchezaji huyo anatarajiwa kupewa nafasi kubwa ya kucheza, jambo ambalo litakuwa muhimu kwa maendeleo yake

Real Madrid haitapokea ofa yoyote ya mkopo wala uhamisho wa kudumu kwa kinda wao Gonzalo García. Klabu hiyo imeweka wazi...
08/07/2025

Real Madrid haitapokea ofa yoyote ya mkopo wala uhamisho wa kudumu kwa kinda wao Gonzalo García. Klabu hiyo imeweka wazi msimamo wao kwamba kijana huyo hatatolewa kwa timu nyingine, huku akitarajiwa kubaki Santiago Bernabéu kwa msimu huu ujao.

Kocha Xabi Alonso ameripotiwa kuwa na furaha kubwa na maendeleo ya Gonzalo García, na ana mpango wa kumjumuisha kikamilifu kwenye mipango ya timu ya kwanza. Hii ni ishara kwamba Real Madrid wanamuamini kijana huyo k**a sehemu ya mustakabali wa klabu, na hawana mpango wa kumuachia kwa sasa.

Arsenal wamekamilisha hatua zote za awali za usajili wa Christian Nørgaard kutoka Brentford. Vipimo vya matibabu vimekam...
08/07/2025

Arsenal wamekamilisha hatua zote za awali za usajili wa Christian Nørgaard kutoka Brentford. Vipimo vya matibabu vimekamilika bila vikwazo huku Nørgaard akiweka saini mkataba wake mpya, na kinachosubiriwa sasa ni taarifa rasmi itakayotolewa muda wowote kuanzia sasa.

Huduma ya Nørgaard inakuja k**a ongezeko linaloonekana katika kuboresha safu ya kiungo ya Arsenal.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Meridian Sport posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Meridian Sport:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share