Meridian Sport

Meridian Sport Ukurasa wako namba moja wa habari za michezo Tanzania na kimataifa!

Klabu ya Fountain Gate kesho Jumapili, itafanya tamasha ndogo la kutambulisha wachezaji wake wapya watakaotumika msimu h...
11/10/2025

Klabu ya Fountain Gate kesho Jumapili, itafanya tamasha ndogo la kutambulisha wachezaji wake wapya watakaotumika msimu huu. Tamasha hilo lililopewa jina la Tanzanite Day, litafanyika kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, uliopo Wilaya ya Babati mkoani Manyara.

Hatua hiyo inakuja baada ya timu hiyo kupewa ruhusa ya kusajili wachezaji wake wapya, ambao walikwama kuingia kwenye mfumo baada ya kufungiwa kusajili kutokana na madeni.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi kufunguliwa kwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi uliopo Tabora,...
11/10/2025

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi kufunguliwa kwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi uliopo Tabora, baada ya kukamilika kwa marekebisho yaliyokidhi vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu.

Klabu ya Kaizer Chiefs FC imetangaza rasmi kuwapa majukumu ya ukocha wakuu Khalil Ben Youssef na Cedric Kaze, wakiongoza...
11/10/2025

Klabu ya Kaizer Chiefs FC imetangaza rasmi kuwapa majukumu ya ukocha wakuu Khalil Ben Youssef na Cedric Kaze, wakiongoza timu hiyo hadi mwisho wa msimu wa 2025/26. Uamuzi huu umefuatia kuachana kwa maelewano na aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Nasreddine Nabi.

Baada ya kukamilisha usajili wa mastaa wapya kwa mafanikio makubwa, klabu ya Fountain Gate FC iko tayari kuonyesha makal...
08/10/2025

Baada ya kukamilisha usajili wa mastaa wapya kwa mafanikio makubwa, klabu ya Fountain Gate FC iko tayari kuonyesha makali mapya msimu huu. Oktoba 12, mashabiki watafurika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati, kushuhudia tamasha kabambe la kutambulisha kikosi kipya kilichosukwa kwa ustadi na malengo makubwa.

Rais wa Klabu ya Yanga SC na Mwenyekiti wa Chama cha Vilabu Afrika (ACA), Eng. Hersi Said, ameandika historia mpya baada...
08/10/2025

Rais wa Klabu ya Yanga SC na Mwenyekiti wa Chama cha Vilabu Afrika (ACA), Eng. Hersi Said, ameandika historia mpya baada ya kuteuliwa rasmi na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuwa Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Vilabu ya Wanaume Duniani kwa kipindi cha miaka minne (2025–2029).

Klabu ya soka ya Arsenal kutoka Uingereza imethibitisha kumpa mkataba ulioboreshwa rasmi mlinda mlango wao namba moja, D...
08/10/2025

Klabu ya soka ya Arsenal kutoka Uingereza imethibitisha kumpa mkataba ulioboreshwa rasmi mlinda mlango wao namba moja, David Raya, utakaodumu hadi mwezi Juni mwaka 2028. Hatua hii ni sehemu ya mkakati wa klabu hiyo kuhakikisha kuwa nyota wake muhimu anabaki klabuni kwa muda mrefu

Romain Folz, Kocha Mkuu wa Yanga SC amekiongoza kikosi hicho kwenye mazoezi ikiwa ni maandalizi kuelekea mchezo ujao wa ...
08/10/2025

Romain Folz, Kocha Mkuu wa Yanga SC amekiongoza kikosi hicho kwenye mazoezi ikiwa ni maandalizi kuelekea mchezo ujao wa kimataifa, Ligi ya Mabingwa Afrika. Yanga SC imetoka kucheza mchezo wa Ligi Kuu Bara ya NBC dhidi ya Mbeya City uliochezwa Septemba 30 2025 wakatoshana nguvu kwa suluhu ya 0-0.

Simba SC imeendelea kuonyesha makali yake katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26 kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Namu...
02/10/2025

Simba SC imeendelea kuonyesha makali yake katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26 kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Namungo FC, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Oktoba 1, 2025. Ushindi huo umewaweka kileleni kwa pointi 6, sawa na Singida Black Stars, lakini wakiwa na uwiano bora wa mabao.

Licha ya tetesi zinazozagaa mitandaoni na kwenye vijiwe vya soka kuwa Kocha Mkuu wa Yanga SC, Roman Folz, huenda akatupi...
02/10/2025

Licha ya tetesi zinazozagaa mitandaoni na kwenye vijiwe vya soka kuwa Kocha Mkuu wa Yanga SC, Roman Folz, huenda akatupiwa virago, taarifa za ndani kutoka kwa mabosi wa klabu hiyo zinathibitisha kuwa hakuna mpango wa kuachana naye kwa sasa.

Pamoja na Arsenal kupata ushindi wa pili mfululizo katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuichapa Olympiacos 2-0 katika dimb...
02/10/2025

Pamoja na Arsenal kupata ushindi wa pili mfululizo katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuichapa Olympiacos 2-0 katika dimba la Emirates, lakini furaha ya ushindi huo iligubikwa na hofu ya jeraha kwa beki Gabriel Magalhães, ambaye alilazimika kutolewa uwanjani baada ya kugongana na kipa David Raya. Gabriel alionekana akipata matibabu na kuondoka akiwa na maumivu, hali iliyozua wasiwasi kwa mashabiki na wachezaji wa Gunners.

Aston Villa imetangaza rasmi kumsajili kiungo chipukizi mwenye kipaji cha hali ya juu, Mohamed Koné, kutoka klabu maaruf...
02/10/2025

Aston Villa imetangaza rasmi kumsajili kiungo chipukizi mwenye kipaji cha hali ya juu, Mohamed Koné, kutoka klabu maarufu ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast, kitovu cha vipaji ambacho kimewahi kuzalisha nyota k**a Yaya Touré, Kolo Touré, Odilon Kossounou, Karim Konaté na Touré Bazoumana.

Koné, ambaye ni mchezaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 na 23, alihitimu kutoka akademia ya MimoSifcom na kujiunga na kikosi cha kwanza cha ASEC akiwa na umri wa miaka 17 pekee.

Katika usiku wa kihistoria kwenye Uwanja wa Olimpiki jijini Barcelona, mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Pari...
02/10/2025

Katika usiku wa kihistoria kwenye Uwanja wa Olimpiki jijini Barcelona, mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Paris Saint-Germain (PSG), walifanya maajabu kwa kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Barcelona, bao la ushindi likifungwa na Gonçalo Ramos katika dakika ya 90.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Meridian Sport posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Meridian Sport:

Share