Meridian Sport

Meridian Sport Ukurasa wako namba moja wa habari za michezo Tanzania na kimataifa!

Nyota wa tenisi kutoka Japani, Naomi Osaka, ameamua kujiondoa katika mashindano ya WTA 1000 ya Cincinnati ili kupata mud...
09/08/2025

Nyota wa tenisi kutoka Japani, Naomi Osaka, ameamua kujiondoa katika mashindano ya WTA 1000 ya Cincinnati ili kupata muda wa kupumzika na kujiandaa kikamilifu kuelekea US Open inayotarajiwa kuanza Agosti 24.

Uamuzi huo unakuja siku chache baada ya Osaka kushindwa kunyakuwa taji la pili mfululizo, akipoteza fainali ya Montreal dhidi ya bingwa chipukizi kutoka Canada, Victoria Mboko. Wakati wawili hao wakipambana kwenye fainali ya Montreal, mashindano ya Cincinnati tayari yalikuwa yameanza. Kwa mujibu wa ratiba, washindi wa Montreal walikuwa wamepewa nafasi ya kuingia moja kwa moja kwenye raundi ya pili ya Cincinnati.

Hata hivyo, Mboko alitangaza kujiondoa mara baada ya kushinda Canadian Open, wakati Osaka naye alisubiri kwa muda kabla ya kutoa uamuzi huo. Osaka alikuwa amepangwa kumenyana na Linda Noskova, huku Mboko akitarajiwa kumenyana na Diana Shnaider.

Benjamin Sesko amefichua sababu zilizomfanya achague kujiunga na Manchester United, licha ya mvutano mkali wa usajili ul...
09/08/2025

Benjamin Sesko amefichua sababu zilizomfanya achague kujiunga na Manchester United, licha ya mvutano mkali wa usajili uliokuwa ukihusu jina lake. Jumamosi asubuhi, United ilithibitisha rasmi kumchukua Sesko kutoka RB Leipzig kwa dau linaloweza kufikia pauni milioni 74.

Akiweka wazi uamuzi wake, Sesko alisema kuwa haikuwa tu historia ya Manchester United iliyomvutia, bali zaidi ni maono ya baadaye ya klabu hiyo. “Historia ya Manchester United bila shaka ni ya kipekee, lakini kinachonipa hamasa zaidi ni mustakabali wake,” alisema Sesko. “Tulipojadili mradi wa klabu, ilikuwa wazi kila kitu kiko tayari ili timu hii iendelee kukua na kushindania mataji makubwa tena hivi karibuni.

Kiungo wa Klabu ya Manchester City, Rodri anaendelea kuuguza majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa kombe la Dunia la vil...
09/08/2025

Kiungo wa Klabu ya Manchester City, Rodri anaendelea kuuguza majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa kombe la Dunia la vilabu huku ikipambana kuhakikisha anakua sawa kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Uingereza. Kiungo huyu wa kati alikosa sehemu kubwa ya msimu wa 2024/25 baada ya kupata jeraha kubwa la kuvunjika kwa ligamenti ya mbele ya goti mwezi Septemba mwaka jana.

Majeraha hayo yalikuja wakati ambao Manchester City wanategemea mshindi huyo wa Ballon d’Or 2024 kusaidia kuirejesha timu yao kwenye kiwango cha juu katika ligi ya England baada ya msimu mgumu uliopita.

Hata hivyo, Guardiola amefichua kuwa Rodri alipata jeraha jingine katika mchezo wa mtoano wa robo fainali dhidi ya Al-Hilal, uliofanyika Marekani. “Rodri anaendelea kuimarika, lakini alipata jeraha kubwa katika mchezo wa mwisho dhidi ya Al-Hilal,” alisema Guardiola.

SAMATTA KUCHEZA LIGI KUU YA UFARANSA 2025/26Ni rasmi sasa aliyekuwa mchezaji wa PAOK ya Ugiriki na nahodha wa timu ya Ta...
06/08/2025

SAMATTA KUCHEZA LIGI KUU YA UFARANSA 2025/26

Ni rasmi sasa aliyekuwa mchezaji wa PAOK ya Ugiriki na nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mbwana Ally Samatta amejiunga rasmi na klabu inayokipiga huko Ligi kuu ya Ufaransa yaani LIGUE 1 inayofahamika k**a Le Havre.

Mbwana mwenye umri wa miaka 32 alikuwa ni mchezaji huru kabla yakujiunga na Le Havre kwa mkataba wa mwaka 1 pekee.

Samatta amekuwa ni mchezaji mwenye mafanikio makubwa kuliko mchezaji yoyote yule Tanzania kwani mpaka sasa ameshacheza vilabu vikubwa Duniani ikiwemo Aston Villa ya Uingereza, Fenerbahce ya Uturuki, KRC Genk na Royal Antwerp za Ubelgiji pamoja na PAOK ya Ugiriki.

Je Samatta ataweza kupachika mabao mangapi kule Ufaransa?

Mteja wa Meridianbet endelea kubashiri na wakali wa ubashiri Tanzania kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya1000 yapo hapa.

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, inatarajia kushuka dimbani hii leo saa 2 usiku kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, ...
02/08/2025

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, inatarajia kushuka dimbani hii leo saa 2 usiku kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, kuanza kampeni ya kuwania ubingwa wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) kwa kuvaana na timu ya Burkina Faso.

Huu ni mchezo wa ufunguzi wa fainali hizo, ambazo kwa mara ya kwanza zimeandaliwa kwa ushirikiano wa nchi tatu za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda. Michuano itapigwa kwenye miji minne ya ukanda huo, Dar es Salaam, Zanzibar, Nairobi na Kampala, na inahusisha jumla ya timu 19 zilizopangwa katika makundi manne.

Bingwa mtetezi wa CHAN ni Senegal, ambaye anasubiri kuona nani atakuwa tishio kwao mwaka huu.

Manchester United inaripotiwa kumvizia mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Randal Kolo Muani, baada ya dili lake la kuj...
02/08/2025

Manchester United inaripotiwa kumvizia mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Randal Kolo Muani, baada ya dili lake la kujiunga na Juventus kudorora.

Kwa mujibu wa ripoti, nyota huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 26, ambaye alijiunga na PSG mwaka 2023 akitokea Eintracht Frankfurt ya Ujerumani, alikosa nafasi ya kudumu kikosini na alihamishiwa kwa mkopo Juventus mwezi Januari alipomaliza akiwa na mabao 10 katika mechi 22 kwenye mashindano yote.

Hata hivyo, mipango ya kumfanya kuwa mchezaji wa kudumu Turin imekwama kutokana na changamoto za kifedha kwa Juventus, ambao sasa wanalazimika kuuza baadhi ya nyota wao ili kupata fedha za kufanikisha usajili huo.

Kijana mwenye kipaji kikubwa kwenye safu ya ulinzi kutoka Ajax, Jorrel Hato, amekamilisha vipimo vya afya na kusaini mka...
02/08/2025

Kijana mwenye kipaji kikubwa kwenye safu ya ulinzi kutoka Ajax, Jorrel Hato, amekamilisha vipimo vya afya na kusaini mkataba wa miaka saba na Chelsea, huku akiandaliwa kuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Enzo Maresca msimu huu mpya.

Beki huyo mwenye umri wa miaka 19 anajiunga rasmi na The Blues baada ya kuonyesha ubora mkubwa akiwa na Ajax, ambapo tayari amecheza zaidi ya mechi 110 katika mashindano yote, rekodi ya kipekee kwa kijana wa umri wake. Msimu uliopita pekee, Hato alicheza mechi 50, 31 kati ya hizo kwenye Eredivisie, akiibeba safu ya ulinzi ya majogoo wa Amsterdam kwa ujasiri mkubwa.

Nahodha wa Tottenham Hotspur na nahodha wa timu ya taifa ya Korea Kusini, Son Heung-Min, ametangaza rasmi kuwa ataondoka...
02/08/2025

Nahodha wa Tottenham Hotspur na nahodha wa timu ya taifa ya Korea Kusini, Son Heung-Min, ametangaza rasmi kuwa ataondoka kwenye klabu hiyo majira haya ya joto, na tayari klabu ya Los Angeles FC kutoka MLS inaongoza mbio za kumnasa.

Son, ambaye amekuwa nguzo ya Spurs kwa kipindi cha muongo mzima, ametimiza ndoto yake ya kutwaa taji akiwa na Tottenham mwezi Mei, walipoibuka mabingwa wa Europa League kwa ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Manchester United, mafanikio yaliyovunja ukame wa miaka 17 bila kombe kwa klabu hiyo ya London Kaskazini.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari nchini Korea Kusini, kabla ya mechi ya kirafiki dhidi ya Newcastle siku ya Jumapili, Son alifichua kuwa huu ni wakati sahihi wa kutafuta changamoto mpya.

Rasmi sasa Kylian Mbappe atavaa jezi namba 10 pale Real Madrid kwa msimu ujao. Ikumbukwe kuwa namba hiyo ilikuwa inavali...
24/07/2025

Rasmi sasa Kylian Mbappe atavaa jezi namba 10 pale Real Madrid kwa msimu ujao. Ikumbukwe kuwa namba hiyo ilikuwa inavaliwa na Luca Modric ambaye alidumu kalbuni hapo miaka 10.

Mbappe alipotua Real alikabidhiwa jezi namba 9, huku akiondoka k**a mfungaji bora wa msimu uliopita. Je Kylian msimu ujao atapata mafanikio gani mbele ya kocha mkuu Xabi Alonso?

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni k**a vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Klabu ya Chelsea imeibuka kuwa bingwa wa Kombe la Dunia la vilabu hapo jana baada yakuitandika PSG mabao 3-0. Mabao hayo...
14/07/2025

Klabu ya Chelsea imeibuka kuwa bingwa wa Kombe la Dunia la vilabu hapo jana baada yakuitandika PSG mabao 3-0. Mabao hayo yote yalifungwa kipindi cha kwanza na Cole Palmer (2) na Joao Pedro (1).

Chelsea chini ya Enzo Maresca wanakuwa timu ya kwanza kuchukua ubingwa wa mashindano haya huko Marekani ambayo mwaka huu yamekuja kwa mfumo mpya kwa kushirikisha timu 32 kutoka mabara yote Duniani.

Je vipi huko mkeka wako ulisalimika?. Matokeo haya umeyapokeaje?

Meridianbet inakukumbusha kupiga pesa kwa kucheza michezo ya kasino ya mtandaoni k**a vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Kiungo wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand, ameonya kuwa klabu hiyo inaweza kujikuta ikidhalilika zaidi msimu ...
10/07/2025

Kiungo wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand, ameonya kuwa klabu hiyo inaweza kujikuta ikidhalilika zaidi msimu huu iwapo watashindwa kumsajili mshambuliaji hatari Victor Osimhen.

Ferdinand amesisitiza kuwa Osimhen ndiye mshambuliaji wa kati ambaye United wanamhitaji kwa sasa, na kuongeza kuwa ni "aina ya mchezaji ambaye klabu hiyo imekuwa ikimlilia kwa muda mrefu."

Ameeleza kuwa kushindwa kumpata staa huyo wa Nigeria kutakuwa pigo kubwa, hasa wakati huu ambao kikosi cha United kinakosa mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao kwa uthabiti msimu mzima.

Nyota wa Liverpool, Luis Díaz, anazidi kuhusishwa na vilabu vya Barcelona na Bayern Munich, huku mustakabali wake ukiwa ...
10/07/2025

Nyota wa Liverpool, Luis Díaz, anazidi kuhusishwa na vilabu vya Barcelona na Bayern Munich, huku mustakabali wake ukiwa kitendawili kinachovuta macho ya mashabiki wa soka barani Ulaya.

Kwa sasa, Barcelona wanaendelea kuwa na matumaini, lakini wanakumbwa na changamoto za kifedha na masuala ya usajili. Klabu hiyo inahitaji kuhakikisha Díaz anasajiliwa rasmi kabla ya tarehe 31 Agosti, vinginevyo mkataba utahitaji kipengele cha fidia (compensation clause), jambo ambalo linaweza kuwa kikwazo.

Wakati huo huo, Bayern Munich wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri zaidi. Klabu hiyo ya Ujerumani ipo tayari kutuma ofa ya €60 milioni pamoja na nyongeza ya hadi €20 milioni k**a bonasi, ofa ambayo inaweza kufikia mahitaji ya Liverpool.

Kwa upande wa Liverpool, msimamo ni kwamba Díaz si mchezaji wa kuuzwa, isipokuwa wakipokea ofa inayokaribia €80 milioni au zaidi. Klabu hiyo bado inamthamini sana mshambuliaji huyo ambaye ana mkataba hadi mwaka 2027.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Meridian Sport posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Meridian Sport:

Share