
11/10/2025
Klabu ya Fountain Gate kesho Jumapili, itafanya tamasha ndogo la kutambulisha wachezaji wake wapya watakaotumika msimu huu. Tamasha hilo lililopewa jina la Tanzanite Day, litafanyika kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, uliopo Wilaya ya Babati mkoani Manyara.
Hatua hiyo inakuja baada ya timu hiyo kupewa ruhusa ya kusajili wachezaji wake wapya, ambao walikwama kuingia kwenye mfumo baada ya kufungiwa kusajili kutokana na madeni.