Mpili TV

Mpili TV Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mpili TV, News & Media Website, Mbezi, Dar es Salaam.

Vijana wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Karagwe, wakiongozwa na Mwenyekiti wao Alexius Syli...
15/10/2025

Vijana wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Karagwe, wakiongozwa na Mwenyekiti wao Alexius Sylivester, wamefanya hamasa kubwa ya kumkaribisha Mgombea Urais wa CCM, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye anatarajiwa kuzungumza na wananchi na wanachama wa CCM katika mkutano wa kampeni utakaofanyika leo, tarehe 15 Oktoba 2025, katika Uwanja wa Bashungwa โ€“ Kayanga.

Akizungumza wakati wa maandalizi hayo, Alexius alimpongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake thabiti na kwa kuendelea kulinda amani, umoja na ustawi wa Watanzania, mambo yanayowezesha wananchi kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa uhuru na kuleta maendeleo endelevu.

Hamasa hiyo iliyoenea katika mitaa yote ya mji wa Kayanga ilijaza nguvu ya mapenzi, furaha na uzalendo kwa wananchi, huku vijana wakionyesha ari na shauku ya kumpokea Mama wa maendeleo, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

BASHUNGWA AWAALIKA WANANCHI KUMPOKEA DKT. SAMIA KARAGWEMgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe ambaye pia ni Mjumbe wa Halmas...
14/10/2025

BASHUNGWA AWAALIKA WANANCHI KUMPOKEA DKT. SAMIA KARAGWE

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Innocent Bashungwa, amewaalika Wananchi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya za Karagwe na Kyerwa kuhudhuria mkutano wa kampeni za Mgombea Urais wa CCM, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, utakaofanyika kesho tarehe 15 Oktoba 2025 katika uwanja wa Bashungwa โ€“ Kayanga.

Bashungwa ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera kujitokeza kwa wingi kumpokea Dkt. Samia na kuonesha umoja, upendo na imani, akisisitiza kuwa katika uongozi wake Rais Samia ameleta mafanikio makubwa ya maendeleo katika sekta mbalimbali nchini.

โ€œNitumie nafasi hii kuwakaribisha muungane nasi kumkaribisha Rais wetu Dkt. Samia. Tumuoneshe upendo, shukrani na mapenzi yetu, kwani Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mambo makubwa sana hapa Karagwe na katika mkoa wetu wa Kagera,โ€ amesema Bashungwa.

Aidha, Bashungwa amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Kagera kujitokeza katika maeneo yao kulingana na ratiba ya kampeni, ambapo Dkt. Samia anatarajiwa kufanya mikutano ya hadhara tarehe 15 hadi 16 Oktoba 2025 katika majimbo mbalimbali ya mkoa huo.

Simba SC imemtambulisha rasmi Dimitar Pantev  ๐—ธ๐˜‚๐˜„๐—ฎ ๐—ธ๐—ผ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ ๐—บ๐—ธ๐˜‚๐˜‚ ๐˜„๐—ฎ klabu hiyo ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฎ๐—ฑ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ kuondoka kwa aliyekuwa kocha mkuu ๐—ธ...
03/10/2025

Simba SC imemtambulisha rasmi Dimitar Pantev ๐—ธ๐˜‚๐˜„๐—ฎ ๐—ธ๐—ผ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ ๐—บ๐—ธ๐˜‚๐˜‚ ๐˜„๐—ฎ klabu hiyo ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฎ๐—ฑ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ kuondoka kwa aliyekuwa kocha mkuu ๐—ธ๐—ผ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ ๐—™๐—ฎ๐—ฑ๐—น๐˜‚ Davids

Asanteni sana kwa kuendelea kutuamini.
02/10/2025

Asanteni sana kwa kuendelea kutuamini.

Baada ya kufanya kampeni katika zaidi ya mikoa 16 nchini, Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania k...
29/09/2025

Baada ya kufanya kampeni katika zaidi ya mikoa 16 nchini, Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea na ziara yake ambapo Septemba 29 amewasili katika Wilaya ya Pangani, Mkoa wa Tanga, ikiwa ni mkoa wa 18 alioufikia tangu kuanza kwa kampeni mwaka huu.

Siku moja kabla, Septemba 28, Dkt. Samia alifanya kampeni zake mkoani Pwani, mkoa wa kimkakati katika kuendeleza mapinduzi ya kiuchumi nchini. Katika hotuba yake, alisisitiza dhamira ya Serikali ya kuongeza thamani ya rasilimali na bidhaa zinazozalishwa nchini kwa lengo la kuongeza tija katika sekta ya viwanda na kuvutia wawekezaji.

Miongoni mwa miradi ya kimkakati aliyoitaja ni pamoja na ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, Reli ya Kisasa (SGR), na miundombinu ya barabara inayolenga kuunganisha mkoa huo na maeneo mengine muhimu ya kiuchumi.

Lengo kuu la miradi hiyo ni kuimarisha uchumi wa ndani kupitia uongezaji thamani wa mazao na bidhaa, kuimarisha ajira kwa Watanzania, na kuongeza uwezo wa nchi kujitegemea kiuchumi.

Mapokezi makubwa yamemsubiri Dkt. Samia Pangani, ambako wananchi wamejitokeza kwa wingi, wakiwa na shauku ya kusikiliza sera, mikakati na ahadi za CCM kuhusu maendeleo ya wilaya yao na taifa kwa ujumla.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hajjat Fatma Mwassa, wameungana ...
29/09/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hajjat Fatma Mwassa, wameungana na Maaskofu, Mapadri, Viongozi wa Kanisa Katoliki na waumini kushiriki Misa Takatifu ya mazishi ya Hayati Askofu Mkuu Novatus Rugambwa, Balozi wa Baba Mtakatifu.

Misa hiyo Takatifu imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora, Kardinali Protase Rugambwa, katika Kanisa Kuu Katoliki Jimbo la Bukoba, mkoani Kagera, leo tarehe 29 Septemba 2025.

Viongozi mbalimbali na wanafamilia walishiriki Misa hiyo, akiwemo Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Mhashamu Wolgang Pisa; Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Mkuu Angelo Acattino; Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba, Mhashamu Jovitus Mwijage; pamoja na Mapadri, Watawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha, na waamini kutoka ndani na nje ya mkoa wa Kagera.

Kikosi cha Simba SC
28/09/2025

Kikosi cha Simba SC

Kikos cha Simba SC
25/09/2025

Kikos cha Simba SC

TAARIFA KWA UMMA
23/09/2025

TAARIFA KWA UMMA

22/09/2025

21/09/2025

Address

Mbezi
Dar Es Salaam

Telephone

+255755990645

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mpili TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mpili TV:

Share