Halisi Naturalist

Halisi Naturalist Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Halisi Naturalist, Digital creator, Dar es Salaam.
(1)

✨ Safe space for real stories & community advice
🌱 Plant identification & African medicine traditions
πŸ”¬ Connecting science & culture
πŸƒ Nature heals

πŸ“± WhatsApp: +255788900445
πŸ“Bukombe Geita Tanzania

Ni dawa ya macho, ni dawa ya kuongeza utamu 🀭, ni kinga, ni dawa kwa watoto waliobembendwa, ni dawa inatumika kuua uchaw...
27/12/2025

Ni dawa ya macho, ni dawa ya kuongeza utamu 🀭, ni kinga, ni dawa kwa watoto waliobembendwa, ni dawa inatumika kuua uchawi ikichanganywa na dawa nyingine.

Unataka nikuelekeze kwa shida gani nilizotaja hapo?
Karibu πŸ‘‹

23/12/2025

Boda boda wangekuwa wambea ndoa nyingi sana zingekufa.🀐

Utasikia "Nina boda wangu"πŸ‘‹

22/12/2025

Jinsi unavyoweza kutumia kivumbasi kujitibu magonjwa na kuondoa mikosi, nuksi, na kusafisha nyota.

UTAJUAJE K**A WEWE NI MTU FULANI KWENYE ULIMWENGU WA KIROHO! UNA NGUVU KUBWA ZA KIROHO.Unaweza kuwa na kipaji au kipawa ...
22/12/2025

UTAJUAJE K**A WEWE NI MTU FULANI KWENYE ULIMWENGU WA KIROHO! UNA NGUVU KUBWA ZA KIROHO.

Unaweza kuwa na kipaji au kipawa katika ulimwengu wa kiroho lakini wewe haujui, na haufanyi chochote ili kipawa chako kikusaidie maishani pamoja na kusaidia watu wengine.
Kuwa na nguvu hizo kuna maana kubwa sana kwako, na wakati mwingine unaweza kuishi maisha magumu sana kwasababu tu umeshindwa kujitambua wewe ni nani na unatakiwa uishi vipi.

Hizi ni dalili 10 moja wapo zinazoweza kukueleza kuwa wewe ni mtu special katika ulimwengu huu wa kiroho...
1. Unasikia sauti za mwongozo ndani yako.
Watu wenye vipawa vya kiroho mara nyingi huwa na hisia kali (intuition), hii hujitokeza k**a mwongozo wa ndani au β€œsauti” inayokupa ufahamu, ushauri au mwelekeo.
Inaweza kuwa waongozaji wa kiroho au malaika walinzi wanaowasiliana nawe kupitia mawazo au sauti ya ndani, sio lazima sauti k**a sauti ila ni hisia fulani ambazo zinakujia kukupa mwongozo na ukiufata unakuwa salama na kufanikiwa jambo husika. Tambua una kipawa cha kiroho.

2. Una huruma (empathy) kubwa sana.
Baadhi ya watu wenye vipawa vya kiroho huweza kuhisi kwa undani nishati na hisia za watu wengine. Hii huwafanya wawe na huruma ya hali ya juu.
Unaweza kutambua ishara ndogo za kihisia na nishati kutoka kwa watu na mazingira yao. Kadri ufahamu wako wa kiroho unavyoongezeka, ndivyo unavyokuwa na huruma na uelewa zaidi kwa wengine.
Mtu akikueleza jambo lake utalielewa zaidi hata ya alivyoeleza kwasababu wewe una jicho la rohoni na hivyo itakupa huruma sana, hata k**a hajaeleza unaweza kuhisi tu na kumuonea huruma, hii inasababisha uwe na desturi ya kujali wengine zaidi kuliko unavyojijali wewe. πŸ˜”

3. Unahisi muunganiko mkubwa na asili/nature.
K**a una kipawa cha kiroho, asili hukupa hisia ya kujiona mpya, imara na mwenye nguvu kubwa. Kukaa karibu na asili hukufanya ujihisi umetulia na umepoa vizuri.
Unahisi uhusiano wa kina wa kiroho na ulimwengu wa asili, na kuiona k**a udhihirisho wa nishati ya kimungu au chanzo cha msukumo wa kiroho.
Ndio maana unaweza kukaa hata kwenye mito au bahari au kwenye miti ukajisikia vizuri sana kuliko ukakae bar, club, n.k

4. Hisia zako za kunusa na kuonja ni nyeti sana.
Kugundua harufu au ladha ambazo wengine hawazioni au kuhisi, Katika imani za kiroho na tiba asilia, inaaminika kwamba huo ni wakati wa mwamko wa kiroho.

5. Mara nyingi unaota ndoto zilizo wazi (lucid dreams).
Ndoto zilizo wazi ni pale unapojua kuwa unaota na wakati mwingine unaweza kudhibiti ndoto hiyo. Watu wengi hupata ndoto hizi kwa mazoezi maalum.
K**a unaota ndoto za aina hii kwa urahisi bila juhudi kubwa, hiyo ni ishara ya kipawa cha kiroho.

6. Unahisi shinikizo eneo la jicho la tatu (third eye).
Jicho la tatu linahusishwa na chakra ya sita, inayojulikana k**a ajna, ambayo inahusiana na nuru, ufahamu wa ndani na ufahamu wa juu.
Ukihisi shinikizo kwenye paji la uso, juu ya katikati ya nyusi ya jicho la kushoto na kulia hilo huchukuliwa k**a uanzishaji wa kituo hiki cha nishati, hiyo ni ishara ya kipawa cha kiroho.

7. Wanyama na wadudu wanavutiwa na wewe.
Wanyama huvutiwa kwa asili na watu wenye vipawa vya kiroho kwa sababu hutoa nishati ya utulivu na ambayo ni chanya.
Mara nyingi wanyama huwa wapole kwako hata bila kuwapa chakula mara kwa mara k**a wengine wafanyavyo, wadudu wanakufata mno na kukupandia, unaweza kukaa sehemu hamna sisimizi ila dakika sifuri wameshajaa mwilini mwako ukashangaa wametoka wapi. K**a ndiyo, huo ni ushahidi wa hisia na nishati zako chanya.

8. Unahisi nguvu isiyoonekana ikikuvuta kihisia au kiakili.
Watu wenye vipawa vya kiroho huwa makini zaidi kwa nishati zilizojificha na uwepo wa viumbe wa kiroho. Huwa na ufahamu mkubwa wa nishati au viumbe vya kiroho vinavyowazunguka.
K**a unahisi mguso mwilini, hisia za kuwa hapa kuna kitu kimeingia au kimekaa hata ukiwa peke yako, hiyo ni ishara chanya kwamba una kipawa hicho.

9. Huamka kati ya saa tisa hadi kumi usiku/alfajiri.
Saa hizi za alfajiri huhusishwa na mabadiliko ya nishati, kuongezeka kwa shughuli za kiroho, au muunganiko wa kina na ulimwengu wa kiroho. Mara nyingi huitwa saa ya mwamko wa kiroho.
K**a unaamka mara kwa mara au unakuwa na usingizi hafifu wakati huo, inaashiria una kipawa cha kiroho.

10. Unapenda tafakuri (meditation) mara kwa mara
Watu wenye vipawa vya kiroho huvutiwa na tafakuri au meditation ili kupata amani ya ndani na utulivu kutokana na hali yao ya kuwa na hisia nyeti.
Kupitia tafakari, unafikia viwango vya juu vya fahamu na kuungana na nguvu ya juu au ulimwengu.

Zipo dalili nyingine nyingi tu, ila kwa leo nitaishia hapo, jikague wewe ni nani, unatakiwa uishi vipi uache kipi ili maisha yako yawe na balance.

Halisi Naturalist

Bint El Sudan oil ni manukato ya asili ya Afrika yanayotumika duniani kote, yanasifika kwa harufu nzuri, kali na ya bina...
21/12/2025

Bint El Sudan oil ni manukato ya asili ya Afrika yanayotumika duniani kote, yanasifika kwa harufu nzuri, kali na ya binafsi, yanatumika sana kiroho, yaani yapo k**a manukato lakini pia kwa madhumuni ya kiroho na ibada. Mara nyingi hupakwa kwenye viganja vya mikono na shingoni kwa mvuto, huongezwa kwenye maji ya kuoga kwa ajili ya kujitakasa, au hutumika kwenye sherehe k**a harusi kwa kuongeza baraka, ustawi na kinga dhidi ya nguvu hasi.
Huwa ni mafuta, perfume, sabuni na pia ipo ya unga.
Nenda kaulize maduka ya dawa za asili huwa yanauzwa.

Kwa wale wenye majini au mapepo mabaya hii Bint el sudan hawaiwezi, maana inavuta kila nguvu mbaya iliyoko ndani yako, sasa ukiitumia utapata shida k**a kichwa kuuma, kuishiwa nguvu, kizunguzungu, n.k lakini k**a uko safi kiroho haujavamiwa na hao viumbe hautoona shida hizo.

Paka kiasi kidogo kwenye viganja vya mikono, shingo, paji la uso (temples), na nyuma ya masikio kabla ya kutoka.

Ongeza matone machache kwenye losheni isiyo na harufu kali au mafuta ya mwili pia unaweza changanya na manukato mengine.

Ongeza matone machache kwenye maji ya kuoga ili kujitakasa, ondoa nuksi na kuinua hali ya kiroho.

Tumia kwenye dua au ibada kuvutia mapenzi, ustawi, bahati njema na nishati chanya.

Ulinzi: Jumuisha kwenye maombi au paka kwenye milango na vifaa vya kazi kwa ulinzi wa kiroho na kufukuza bahati mbaya.

Epuka kuingiza kwa macho na mdomo.

Halisi Naturalist

19/12/2025

1. Ni ngumu sana kumshauri mtu anayekaribia kutapeliwa..
2. Ni ngumu sana kumshauri mwanamke aliyependa..
3...
4...!?

19/12/2025

Mwaka huu uko unaisha haujalazwa kitanda cha hospital, Mshukuru Mungu.

Asante Mungu πŸ™

16/12/2025

NOTE: Ukifanya kwa ambaye sio halali yako haitashika πŸ™†β€β™‚οΈ

16/12/2025

Ikiwa maisha yako ni kitabu, je kitabu hicho kitakuwa na jina gani..?

Mimi "Tenda wema ila usitegemee malipo"

16/12/2025

Kuhisi k**a kuna vitu vinatembea mwilini chini ya ngozi, tumboni, kichwani au sehemu nyingine, kunaweza kusababishwa na mambo kadhaa. Si lazima iwe jambo la kiroho tu k**a uchawi na majini, pia kuna sababu za kiafya, na kisaikolojia.
Mfano matatizo ya neva (nerve issues), Peripheral neuropathy, Upungufu wa vitamin B12
Kisukari
πŸ‘‰ Husababisha hisia k**a: kutambaa, kujaa hewa, msisimko, au vitu vinapita.
Msongo wa mawazo & wasiwasi (Anxiety / stress),
Akili inapochoka sana, mwili huanza kutoa hisia za uongo
Dalili huongezeka ukiwa peke yako au ukifikiria sana
Hormonal imbalance, Thyroid
Mabadiliko ya homoni (hasa wanawake)

Madhara ya dawa au vitu mfano dawa za presha,
Pombe, bangi, au kuacha ghafla dawa fulani.

Allergy au skin irritation

Sababu za kisaikolojia, Formication
πŸ‘‰ Hii ni hali ya kitabibu ambapo mtu huhisi k**a wadudu wanatembea chini ya ngozi.

USISAHAU KU-SHARE

Hakuna ugonjwa wa ngozi ambao haya majani yatashindwa kuutibu.Tupeane maarifa..Tuambie mti huu mnautumiaje huko kwenu..πŸ™
15/12/2025

Hakuna ugonjwa wa ngozi ambao haya majani yatashindwa kuutibu.

Tupeane maarifa..
Tuambie mti huu mnautumiaje huko kwenu..πŸ™

15/12/2025

Mti huu unaitwa mti wa umunazi, unatibu magonjwa ya kiuno na mgongo kwa usahihi, unatibu matatizo ya mayai ambayo hayakomai vizuri, gono kaswende, n.k

Maandalizi na matumizi kwa yote niliyotaja.
Chukua mizizi tengeneza unga wake.
Kunywa nusu kijiko katika glass ya maji moto x2 kwa siku, siku 7.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Naturalist posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Naturalist:

Share