Halisi Naturalist

Halisi Naturalist Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Halisi Naturalist, Digital creator, Dar es Salaam.
(1)

Naturalist English https://www.facebook.com/share/1C1qtPhTKd/

๐ŸŒฑ Plant identification & African medicine traditions
๐Ÿ”ฌ Connecting science & culture
๐Ÿƒ Nature heals

๐Ÿ“ฑ WhatsApp: +255788900445
๐Ÿ“Bukombe Geita Tanzania

Mnaponunua viwanja msikae kizembe, dunia inaenda kasi sana, mtu anaitaka pesa yako kwa namna yoyote ile hana muda na mad...
06/08/2026

Mnaponunua viwanja msikae kizembe, dunia inaenda kasi sana, mtu anaitaka pesa yako kwa namna yoyote ile hana muda na madhara yatakayo kupata huko mbeleni.
Mtihani sana.

JINI MAHABA, VIFUNGO, NUKSIK**a una jini mahaba, una vifungo, una nuksi.Chukua majani ya kisamvu (mti wa muhogo ile miku...
04/08/2026

JINI MAHABA, VIFUNGO, NUKSI

K**a una jini mahaba, una vifungo, una nuksi.

Chukua majani ya kisamvu (mti wa muhogo ile mikubwa kwa ajili ya mboga)

-Nunua Ambari nyeupe original (hazipatikani kirahisi na ni gharama kuanzia 150,000 kwenda mbele).
-Nunua halititi, Karafuu maiti, Alimiti, Aliki zamda.
-Nunua kitunguu saumu

Ponda au twanga kisamvu hicho ukichanganya na kitunguu saumu, weka ambari, pia changanya na dawa nilizotaja hapo juu, kijiko kimoja kila dawa, baada ya kuchanganya dawa zote kamua upate maji yake, hifadhi, na yale mabaki, yakaushe, utapika nyungu uwe unajifukiza, na ukimaliza kujifukiza jipake yale maji ya dawa uliyokamua.

Unaweza pia twanga kisamvu na dawa zote uanike ili upate unga wake, uwe unaoga kijiko kimoja asubuhi na usiku.

Utajipaka mwili wote mara mbili kwa siku yaani asubuhi na usiku muda wa kulala.
Tumia mpaka siku 21 kisha uone hali yako inaendeleaje.

K**a unaendelea vizuri, jini mahaba haji tena kufanya s*x na wewe, milango imefunguka, basi endelea na dawa mpaka miezi 6.

Hiyo na ni dawa ya kwanza, nitaendelea kuwapa dawa zingine kwa tatizo hilo hilo.

NOTE: Unaweza kuendelea na dua na maombi ikiwa ulikuwa kwenye program hiyo, hakuna shida, haizuii kabisa, na unaweza kufanya manuwizi au kuombea kabla haujatumia.

Jitahidi ku-share na wengine wapate, usiwe mbinafsi wenye shida ni wengi sana. ๐Ÿ™

Follow us Halisi Naturalist Tanzania

02/08/2026

JINI MAHABA (SPIRITUAL HUSBAND OR WIFE)

Huyu ni jini mshenzi mwenye kuangamiza maisha ya watu wengi sana, leo mamilioni ya watu duniani wanaishi maisha ambayo si yao kwasababu ya huyu kiumbe, tambua kuwa Spiritual husband (mume wa kiroho) au spiritual wife (mke wa kiroho) ni kiumbe wa ulimwengu wa roho ambaye amejifungamanisha na mtu kana kwamba ni mwenzi wake wa ndoa.

Wakati mwingine kiumbe huyo humvaa mtu tangu akiwa mtoto na hukua nae mpaka anaingia utu uzima, anakuwa anakujua nje ndani, anajua kila kitu kuhusu wewe, anajua udhaifu wako na uimara wako uko wapi, huyu kumuepuka sio jambo la mchezo, unahitaji kujitoa zaidi ya unavyoweza kufikiria, ana uwezo wa kukushawishi ufanye mambo fulani kwa kukuwekea mitego kulingana na jinsi anavyokujua kitabia na akafanikiwa kukuingiza kwenye mtego.

Huyu anayekuingia ukiwa mtoto mara nyingi ni wa kutoka kwenye generation ya ukoo wako, ni spirits za kutoka kwenu eidha umamani au ubabani,
Na wengi wameona ni ngumu kumtoa na kumuepuka wakaamua kuungana nae, yaani wakaamua kumkubali na kuishi nae kwa makubaliano, naposema makubaliano namaanisha unaingia nae makubaliano kwamba akuache huru katika jambo hili na lile na wewe utamuacha huru katika jambo hili na lile, lakini si kila mtu anaweza kukubaliana nae ndio hapo linapokuja swala la kupambana ili kuhakikisha unamuepuka na kuishi huru kwenye maisha yako.

Huyu ukishindwa kumdhibiti, ukawa wa kutumia dawa kwa mzaha au unafanya maombi kwa mzaha, unatumia dawa baadae unachoka unaacha, unafanya maombi unachoka unaacha, yaani ile hali ya kujidanganya au kudanganywa utatumia dawa siku chache eti umemaliza, aloo pole sana maana cha moto utakiona, maana unakuwa umeingia nae kwenye vita, atahakikisha maisha yako yanakuwa zaidi ya jehanamu katika kila eneo.

Kiumbe huyu huweza kuonyesha wivu kwa mahusiano ya mtu, hivyo atasababisha migogoro ya kimapenzi, kuvunjika au kuwafanya watu wasioe wala kuolewa kabisa.
Amini usiamini kuna watu wengi sana wanaishi na kiumbe huyu na maisha yao ya mahusiano ni k**a hadithi fulani ya kustaajabisha.

Dalili za kuwa una kiumbe huyu nimeshazieleza kwenye video zilizopita, nitaendelea kuleta masomo mengine zaidi kumuhusu.

Hii ni sehemu ya kwanza, sehemu ya pili itakujia na nitaeleza dawa mbali mbali ambazo unaweza kuwa unatumia ili kuendelea kutafuta nusura na hatimaye uwe huru na maisha yako.

Usiache ku-share sadaka hii, lakini pia naomba u follow page yetu nyingine ambayo tutakuwa tunaweka video hizi za tiba, comment ya kwanza itakuwa na link ya page hiyo.

Asanteni sana.

Nywele au ndevu za mahindi ni mujarabu kwa mtu mwenye matatizo ya kukojoa kitandani, mwenye matatizo ya miguu kuuma au k...
01/08/2026

Nywele au ndevu za mahindi ni mujarabu kwa mtu mwenye matatizo ya kukojoa kitandani, mwenye matatizo ya miguu kuuma au kuwaka moto, na mgonjwa wa P.I.D

1. Chemsha hizo nywele muhusika awe anakunywa mara 3 kwa siku, siku 7

2. P.I.D chemsha nywele hizi kisha chukua ndimu katakata vipande vidogo vidogo tia ndani ya sifuria la ndevu hizi, chemsha kwa moto mdogo si mkali, baadae chuja, kunywa glass moja kutwa mara 2 kwa siku 14.

3.Miguu inayouma, kuwaka moto, kuwasha, n.k, utachukua maganga ya mayai, ponda ponda kisha changanya na ndevu hizi, chukua ndimu tatu kata vipande vinne kila moja, weka na chumvi ya mawe, kisha pika dawa yako, ikichemka ipua na weka kwenye beseni au kalai, utaiacha ipunguze moto kisha utie miguu yako ndani ya maji hayo ya dawa ya moto kiasi, kaa humo kwa dakika 10 mpaka 15, ukishatoa miguu kwenye maji hayo pakaa mafuta ya asili ya ndimu kwenye miguu yako.
Hakikisha maeneo yanayouma zaidi ndio yanalengwa zaidi bila kusahau unyayo wa mguu.

Unaweza kunywa glass moja ya maji ya ndevu za mahindi, mara tatu kwa siku wakati ukiendelea na zoezi hili.
Fanya utaratibu huo kila siku mpaka upone.

Tunasaidiana maarifa tu ndugu zangu, basi nawaomba msiwe wachoyo, fanyeni kushare na wengine waone. ๐Ÿ™

Mmea unaitwa Kivumbasi, kinachojulikana pia k**a Holy Basil au Tulsi, ni mmea unaoheshimiwa kwa karne nyingi katika maen...
31/07/2026

Mmea unaitwa Kivumbasi, kinachojulikana pia k**a Holy Basil au Tulsi, ni mmea unaoheshimiwa kwa karne nyingi katika maeneo mbalimbali ya Asia, hasa India, Afrika na maeneo mengine duniani.

Mbali na matumizi yake ya kiafya, mmea huu umepewa nafasi ya pekee katika mila, desturi, na imani za kiroho za jamii nyingi duniani,
Sio hadithi tu bali kwa waliowahi kuutumia wanajua ufanisi wake katika tiba za kiroho na kisayansi pia.

Mmea huu huondoa nguvu hasi, huimarisha mazingira ya kiroho, hufungua vifungo vya kichawi na kijini, husafisha nyota, n.k
Mmea huu unaweza kutumia wenyewe tu au kuchanganya na dawa zingine kutokana na shida uliyonayo.
Huko India huamini kwamba harufu ya Tulsi hutuliza akili, huongeza utulivu wa nafsi, na husaidia mtu kuwa na utulivu wakati wa kutafakari au kusali.

Leo nataka niwaeleze jinsi gani mtafanya ili kujifungua na kutengeneza nyota zenu kupitia mmea huu na chumvi, k**a wanakuchukia, riziki haieleweki licha ya juhudi kubwa kwenye utafutaji, mambo yako kuishia njiani, iwe ni kazi, biashara, mahusiano, maradhi.

Basi chukua mmea huu wa kivumbasi twanga au chemsha kisha changanya na chumvi ya mawe na oga kila siku mara mbili yaani asubuhi kabla ya jua kuchomoza na jioni jua linapozama, oga kwa manuwizi, ikiwezekana usiogee chooni, baada ya wiki moja mpaka mbili utaona mabadiliko makubwa.
K**a una mapepo/majini kunywa pia muda huo huo mara mbili, kipimo na glass moja.
Kwakweli itakusaidia sana.

Mungu ameweka siri kubwa katika mimea aliyoiumba, ametuletea tiba ya kila ugonjwa ni jukumu letu kutafuta maarifa sahihi.
Hayo ni machache tu kuhusu kazi za mmea huu, ninayo mengi sana ya kuwaeleza.

Ukiweza kupata dawa hizi, (kwa lengo la kubatilisha uchawi na kupandisha nyota) itakuwa bora zaidi, utazichanganya na mmea huo..
Tafuta Italigula, Muosha fedha, Mweza na Mfumbe.
Uwe unaoga kwa mtililiko huo huo, utanishukuru baadae.

Maarifa haya ni sadaka tu, basi usisite ku-share ili na wengine wapate sadaka hii.
K**a una swali uliza kwenye comments, asante ๐Ÿ™

29/07/2026
Umeshatengeneza chain au bangili ya mbegu hizi na vipande vya mti wa mkata fitina za wachawi (mfumbe) kwa ajili ya kinga...
28/07/2026

Umeshatengeneza chain au bangili ya mbegu hizi na vipande vya mti wa mkata fitina za wachawi (mfumbe) kwa ajili ya kinga dhidi ya vitu vibaya?

Tazama jinsi ya kutengeneza https://www.facebook.com/share/v/1NiXdLMfoK/

Usisahau kufollow page yetu mpya

Chatu k**a nyoka wengine wanaona. Ila hawaoni kwa rangi k**a macho yetu binadamu yanavyoona.Lakini pia Ule ulimi wake un...
21/07/2026

Chatu k**a nyoka wengine wanaona. Ila hawaoni kwa rangi k**a macho yetu binadamu yanavyoona.

Lakini pia Ule ulimi wake unaweza kutambua harufu yako kwa urahisi mnoo.
Maana vile unavyotoka unachukua sampuli za harufu kisha akiurudisha ndani unapeleka juu ya mdomo wake ambapo kuna eneo linalopokea sampuli hizo na kufikisha kwenye ubongo na kutafsiri.

Chatu ameumbwa kwa sheria moja kwamba "Ili aishi basi aue". K**a ilivyo Simba, Chui, Na nyoka wengine. Wanyama wa namna hii wamepewa uwezo mkubwa sana wa kutambua chakula chao. Usifanye makosa ukabaki umeganda k**a wanavyofundisha baadhi ya watu' utaliwa, Chatu ni Hatari sana labda uchezee hawa Chatu waliozoeshwa kucheza na watu kwenye ngoma za asili, ila Chatu Mkubwa wa porini akikuona ujue anaona Chakula.

Na k**a ana njaa hapo hapo anabadili mood anaenda kwenye hali ya uwindaji.
Ni Hatari sana sana. Chatu Mkubwa huwezi kupambana nae kamwe. Akishakurukia anauma na meno yake ambayo yapo mengi na yote yamelala kuelekea nyuma, hivyo kuutoa mguu au mkono wako maana yake unaacha pande kubwa la nyama mdomoni mwake au hata ukifanikiwa utabaki na jeraha kubwa sana.
Na chatu hana sumu anakushika na meno ili akuzungushie mwili wake.
Na akikuzungushia tu hutoki, ana misuli ambayo imeumbwa kwa hio kazi, ina nguvu kubwa mnooo ambayo huwezi hata kumtingisha tu.

Hio style ya uuaji ni mbaya sana maana unakufa kwa kukosa hewa, unavunjwa mifupa ukisikia kabisa, yaani unakufa unajiona, na haachii mpaka moyo wako usimame ambao atakuwa anausikia akiwa kakubana pale.

Kuna watu wanadanganyana sana Mtaani utasikia;
1. Chatu akikubana vunja vijiti saba anakuachia akijua mbavu zako zimeshavunjika.
2. Chatu hawezi kumeza mpk akale mlenda ili uteleze mdomoni.
3. Chatu akikukimbiza anarusha mkia kukupiga mtama.
4. Ukimwona chatu chukua kisu kata mdomo wake unapasuka wote mpk mkiani.

Huu ni baadhi ya uongo ila ipo mingi mitaani.

Kifupi ukiona chatu mkubwa KIMBIA, usikimbie k**a mpumbafu kimbia k**a upepo na usifanye kosa la kuingia kwenye maji, huwezi kumuacha chatu kwenye maji hata k**a utakimbia k**a upepo ana speed kali sana kwenye maji, pita mbali naye kabisa.

Mara nyingi chatu huishi kwenye maeneo ya Maji maji (Swamps) au Karibu na mito.
Chatu hupenda kukaa ktk maeneo ambayo yanafanana nae (Camouflage) ni vigumu sana kumwona akiwa kwenye majani kwasabab ya rang yake. Ila yeye anakuona.

Chatu akila mlo mzuri anaweza kukaa mwaka mzima bila kula tena k**a hatopata chakula kingine.

Chatu hatafuni anameza kizima kizima. Yaani unamezwa na nguo zako.

Taya ya chini ya Chatu haijaungana k**a za binadamu. Yaani upande wa kushoto na kulia haujaungana hivyo akiwa anameza taya hizo ndio zinatumika kusukuma k**a ambavyo mikono yako inafanya ukiwa unavuta kamba ya wavu wa samaki.
Lakini pia, husaidia kutanuka upana mkubwa ili kupitisha chakula kikubwa mdomoni.

K**a ilivyo Mbwa, Chatu pia haamini macho yake. Hutumia zaidi Harufu kuliko macho. Na mbwa ni hivyo hivyo ukimrushia jiwe anaona kabisa ni jiwe ila mpk alinuse ndio atofautishe na chakula. Na Chatu hutumia sana pua, na hii husababisha akuk**ate hata ukiwa umeganda hapo.

Ukimwangalia Chatu unamwona mzembe, lkn ni Muuaji mzuri mwenye sura ya upole. Anaua wanyama wenye nguvu kuliko mtu, na wapana kuliko mtu na anameza. Mfano; Simba, Chui, Mamba mbilikimo (Camons) wanauliwa bila shida na kuliwa.
Swala wanamezwa na pembe zao bila shida. Hivyo Mtu amatengenezwa na shape nzuri kumezwa ni Easy meal akikushika.

Mwisho, Chatu hakimbizi windo lake. Anasubiri na ni wavumilivu mnoo. Aweza kaa eneo moja kwa siku nyingi mpaka mnyama mmoja ajichanganye apite hapo na ikiwa wewe utakuja kumuona ameshakuk**ata. Anatembea pole pole sana akiwa nchi kavu ila wkt umeingia kwenye killing site yaani eneo ambalo anaweza kukufikia anajikunja kisha anajinyoosha kwa kasi kubwa kuliko unavyopepesa macho, ni sekunde tu kukufikia, aking'ata anakuweka ule mwili wake basi sisi huku kwako tunaweka Turubai, na rambi rambi tunakusanya.

Lakini pia Chatu ananyatia. Anaweza kusogelea windo lake polepole mnoo kiasi kwamba unahisi hasogei, akifika karibu anak**ata.

HAKUNA ALIYEWAHI KUBANWA NA CHATU MKUBWA AKAFANIKIWA KUTOKA.
WALIOFANIKIWA NI WALE WALIOEPUKA KUBANWA NA CHATU TU, AKIKUBANA NI KIFO ASILIMIA MIA. HIVYO KIMBIA MZEE TENA KIMBIA MBALI UKIONA CHATU MKUBWA.

14/07/2026

Mmea huu unaitwa Mbono kaburi (Green Jatropha / Jatropha curcas)

Majani na utomvu hutumika katika tiba za jadi kusaidia kuponya majeraha na kupunguza uvimbe, lakini pia kwa matumizi ya kiroho kutibia na kuondoa nuksi.

Mmea huu una faida nyingi sana, sikiliza video mpaka mwisho.

Share kwa wengine pia.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Naturalist posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Naturalist:

Shortcuts

Share