Halisi Naturalist

Halisi Naturalist Real talk. Good vibes. Content that feeds the mind, heart & soul 💯❤️
Nature, truth, and wellneness. Be real. Be natural. Be positive.

25/07/2025

Tumshauri mwenzetu huyu na yeye atapitia comment zetu.

Boss wangu alisafiri nje ya mji na familia yake k**a kawaida yake, amekuwa akisafiri na familia kila wapatapo nafasi, sa...
24/07/2025

Boss wangu alisafiri nje ya mji na familia yake k**a kawaida yake, amekuwa akisafiri na familia kila wapatapo nafasi, safari hii hakuniambia watarudi lini, kwa hiyo niliendelea kufanya kazi yangu k**a kawaida, mimi ni mlinzi hapa kwake, muda mwingi nakaa getini, lakini kuna siku ghafla nikapata ujumbe kwenye simu wa muamala wa 1,600,000. Ziliingia moja kwa moja kwenye akaunti yangu, sikumjua aliyetuma, lakini ule muamala ulionekana k**a umetoka kwa mfanyabiashara fulani Katika akili yangu niliwaza hivyo, nikaamini huenda amekusea tu kutuma, labda Mungu alikuwa amenikumbuka hatimaye.

Nilitumia sehemu ya hela kununua nguo nzuri, viatu, na marashi ya bei ghali, vitu ambavyo sikuwa nimewahi kumudu, hata nikampigia msichana mmoja mrembo aliyekuwa hanitaki kabisa kisa hali yangu, nikampeleka kwenye mgahawa mzuri kisha tukalala hotelini kwa siku 5 mfululizo 300,000 ikaisha.
Nikamwachia hela ya chakula na kodi jumla ya 360,000. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilijihisi k**a mfalme, nikawapa vijana wa mtaani ambao ni washikaji zangu waenjoy na wao kwa vinywaji 120,000, sikuwa najua kabisa k**a nilikuwa najichimbia kaburi mwenyewe.

Baada ya wiki moja, boss wangu akanipigia simu. Akauliza k**a niliona pesa alizotuma 1.6M, kabla sijajibu, akaniambia hiyo pesa ndiyo mshahara wangu wote wa mwaka 2025, na ameongezea kidogo ili nipate ya kujikimu.
Akaeleza kuwa yeye na familia yake wamepata visa ya kuhamia nje ya nchi, na kwa kuwa hatakuwa anapata uwezekano wa kunitumia kila mwezi, aliamua kunilipa mapema ili nisihangaike. Moyo wangu ukastuka, simu niliyokuwa nimeshika ikanidondoka mkononi, kila kitu kilianza kuonekana cheusi, nikahisi moyo wangu unauma. Tayari nilikuwa nimeshatumia karibu hela yote maana ilikuwa imebaki k**a 240,000 tu.
Nilikuwa nafikiria labda nimepata bahati, sikuwahi kufikiria k**a ni mishahara yangu ya mwaka mzima.

Sasa sijui nifanye nini, yule msichana bado alikuwa ananipigia kuniuliza aje tena tuendeleze starehe zetu? lakini naona aibu kubwa inakuja, sintaweza kumwangalia tena machoni, itawezekanaje ku enjoy kutoka sasa hadi Desemba na 240,000 tu?

Sina amani, ninasikitika tangu usiku mpaka sasa sielewi, tafadhali kila mtu hapa, nisaidieni, nifanye nini? Nitapona vipi kutokana na kosa hili? Najihisi mjinga sana na nimevunjika moyo.

Kuna siku nilikutana na mtu ambaye alinisumbua sana kwa kunifuatilia licha ya mimi kutokuwa na nia yoyote ya kimapenzi n...
24/07/2025

Kuna siku nilikutana na mtu ambaye alinisumbua sana kwa kunifuatilia licha ya mimi kutokuwa na nia yoyote ya kimapenzi naye, lakini hakuwa tayari kukubali "Hapana" k**a jibu.
Mtu huyo alikuwa ananitumia zawadi mara kwa mara, ikiwa ni pamoja na maua na pesa lakini nilirudisha zote kwa sababu nilihisi sio vizuri kula vitu vyake wakati hisia zangu hazipo hata chembe kwake.
Nilimueleza kwa uwazi kwamba sina hisia zozote za kimapenzi kwake na sitakuwa tayari kuanzisha mahusiano na yeye.

Licha ya juhudi zangu za kuweka mipaka na yeye, alichukia na akaanza kuandika mambo mabaya kuhusu wanawake kupitia mitandao ya kijamii, akionyesha kuwa wanawake hupenda kuishia kwa watu wasiowathamini na kuwacha wanao wathamini, jambo la kukera zaidi ni kwamba alikuwa akini-tag kwenye post zake hizo, kutokana na tabia yake niliamua kumblock.

Wakati huo nilikuwa kwenye mahusiano, lakini baadaye niligundua kuwa mpenzi wangu alikuwa ananicheat, baada ya mahusiano hayo kuisha, yule mwanaume aliyekuwa ananisumbua alijitokeza tena, na kwa namna fulani aligundua kilichotokea kati yangu na ex wangu, na alionekana kufurahia matatizo yangu, nilimwambia wazi kuwa licha ya kilichotokea kati yangu na aliyekuwa mpenzi wangu, bado simtaki kimapenzi, alikasirika sana na akaniambia ataendelea kunifuata hatokata tamaa.

Siku moja tukakutana kwenye sherehe moja, alijaribu kuzungumza na mimi lakini nilihama eneo hilo kwa sababu sikupenda kelele na pia niliona hakuwa na ustaarabu, alikuwa ananiongelesha akiwa karibu sana na sikio langu akiniuliza maswali yasiyo na maana k**a “unatoka saa ngapi? Uko na nani?” Nilikuwa tayari moyoni nimeshamchulia k**a mpuuzi tu na mtu asiye mwema, hivyo sikuwa tayari kuzungumza naye.
Alikuwa akinitazama tu, mpaka nikashindwa kunywa kinywaji changu kwa sababu sikuwa comfortable kabisa, alinifanya nijisikie vibaya sana.

Mpenzi wangu mpya alifika nilipokuwa nimekaa na tukaondoka kwenda kukaa pengine, tulipotoka, cha kushangaza ni kwamba alijitokeza tena, wakati huu nilikuwa peke yangu kwa sababu mpenzi wangu alikwenda msalani, nilijisikia hofu na kutokuwa na amani.
Alifika kwenye meza yetu na kuketi pale ambapo mpenzi wangu alikuwa ameketi, na akasema, “Huyo ndiye mpenzi wako?” Sikujibu. Kisha akasema, “Unapenda watu wenye pesa, naona hivyo, labda ndiyo maana hunipendi kwa sababu unafikiri sina pesa.” Akaanza kuniambia eti anataka anioneshe salio la bank nikamwambia sitaki.

Alikasirika na kuanza kuniita majina mabaya, hasira zikampanda mpaka nikashangaa, wanaume wote wangekuwa wanatongoza hivyo hivi ingekuwaje! Nilijisikia vibaya sana, lakini bahati nzuri mpenzi wangu alirudi na akauliza nini kinaendelea hapa, nilimweleza mpenzi wangu, akamuita mlinzi, na jamaa akatolewa nje kwa nguvu, alipokuwa akitolewa, alikuwa anatishia kunidhuru pamoja na mpenzi wangu.

Alitusubiri nje, na tulipokuwa tunaondoka, ghafla alijitokeza na kumvamia mpenzi wangu, wakaanza kupigana, bahati nzuri, mpenzi wangu alijitetea, na watu walikusanyika na kuwazuia.
Tulipata teksi na kuondoka kurudi nyumbani. Mpenzi wangu akasema, “Tumsh*taki.” Nilikuwa na wasiwasi kwa sababu sitaki matatizo, lakini mpenzi wangu alisisitiza kuwa anajaribu kunilinda kwa sababu hatujui mpango wake unaofuata ni upi, hatimaye nilikubali, na tukafungua kesi ya shambulio, hivi sasa navyoongea yuko mikononi mwa polisi.

Lakini tatizo ni kwamba, familia yake inaniomba msamaha na eti kwamba nimsihi mpenzi wangu aachane na kesi hiyo, hasa mama yake ambaye huja nyumbani kwangu mara kwa mara kunisihi niwasamehe, kila anapokuja huleta mboga za majani au zawadi nyingine za shambani, na japokuwa mara nyingi hukataa, huendelea kusisitiza.

Naomba ushauri wako, mtu huyu ananitisha, sasa hivi nimechanganyikiwa sana.

😓😓 Hii imetokea Geita, ama kweli dunia uwanja wa vita daah!.Kuna jamaa wawili walikuwa marafiki sana, jamaa mmoja anaitw...
24/07/2025

😓😓 Hii imetokea Geita, ama kweli dunia uwanja wa vita daah!.
Kuna jamaa wawili walikuwa marafiki sana, jamaa mmoja anaitwa Masanja mwingine anaitwa Jose, Sasa katika urafiki wao walikuwa wanatembeleana yaani kila mmoja ana access ya kwenda nyumbani kwa mwingine,
Huyu Masanja kumbe alikuwa anamtamani mke wa Jose, na siku zote anapoenda nyumbani kwa Jose kumbe anammezeaga mate,
Basi akaja akamtongoza yule mwanamke akakataa mwanzoni na kumwambia kuwa sio vizuri maana wewe ni shemeji na ni rafiki wa mume wangu, sitaki kuwagombanisha, Masanja kwa kujiamini akaongeza bidii na alipogundua kuwa Jose ndio kikwazo cha mwanamke kukubali ombi lake.

inasemekana akaanza kusuka mipango ya kumuua (hakuna mwenye ushahidi ila walihisi tu kutokana na yaliyoendelea kufanyika) 😓 akishirikiana na mwanamke yaani mke wa Jose, ili baadae wawe wapenzi na wasihofie chochote, na kweli jamaa hakuchukua round, k**a baada ya mwezi jamaa amefariki majirani wakashangaa kumuona Masanja anaenda kulala kwa Jose, ikawa mazoea mpaka baadhi ya watu vijiweni wakawa wanamsema vibaya jamaa,
Ikafika hatua Masanja akamgeuza k**a mke, muda wowote anaenda asubuhi anatoka na taulo bila chembe ya aibu, ilikuwa k**a ajabu kutokana na alivyokuwa ameshibana na Jose.

Mke wa Masanja alikuwa na stress sana juu ya mwenendo wa mume wake, maana alikuwa analala nje, anapotea hata wiki, hamjali kwa lolote, akaanza kumfatilia mume wake na kumtisha kuwa ataenda polisi kutoa siri zote anazozijua endapo hatarudi nyumbani, basi Masanja akarudi nyumbani kwake kumpoza mkewe, Masanja akawa akilewa anamwambia mke wake kuwa "Usijali mke wangu mi siwezi kukutupa, yule mwanamke mi siwezi kumuoa namchezea tu maana sijaona mwanamke mchafu k**a yule, ananuka nyeti na hajui kuoga"
Mke wa masanja akawa akiambiwa neno lolote pakikucha anaenda kumueleza yule mke wa jose k**a vile kumtusi au kumtambia ili aachane na mumewe.

Ikawa kila Masanja anapoenda kwa mke wa Jose yote waliyoongea anaenda kumwambia mke wake, na mke wake hakai nayo anaenda kutamba kwa mke wa jose, ndipo yule mke wa Jose akakasilika sana akaanza kumpa vitisho kuwa ataitoa siri yao ya mauwaji ili k**a ni jela waende wote tu yaani liwalo na liwe.

Masanja akaona hapa ishakuwa noma ikabidi akae mbali na mke wa Jose, lakini ndugu wa Jose walikuwa na tetesi juu ya kuondoka ndugu yao na walijua mtuhumiwa namba moja ni mke wake lakini kwakuwa hawakuwa na ushahidi wa kutosha hiyo kesi iliisha kikawaida sana.
Walichofanya walienda kuchukua watoto kwa yule mwanamke wakaenda kuwalea wao.
Yule mwanamke dunia aliiona chungu na mwisho wa siku alikusanya vilago vyake akaondoka kwenda kwao, akatelekeza nyumba, ikabidi ndugu waichukue ile nyumba.
Imetokea miaka mitatu iliyopita.

Umejifunza nini?

Nimekuwa kwenye mahusiano na mpenzi wangu kwa miaka minane mpaka sasa, lakini hanihudumii kwa chochote kile, anachofanya...
23/07/2025

Nimekuwa kwenye mahusiano na mpenzi wangu kwa miaka minane mpaka sasa, lakini hanihudumii kwa chochote kile, anachofanya ni kunipigia simu kunijulia hali, na kunipeleka kwenye chakula cha jioni siku ya kuzaliwa au Krismasi, kisha tunaenda kulala kwake, zaidi ya hapo hajali nitakula nini au nitavaa nini.

Ingawa alinisaidia kunitafutia hii kazi ninayofanya sasa, lakini najihisi k**a niko single kwa sababu najinunulia kila kitu mwenyewe.
Kwa hiyo nataka kuachana na uhusiano huu sioni k**a kuna faida yoyote.
Labda kuna mawazo mapya naweza pewa before sijamuacha nipostie

Baada ya kujifungua mtoto, mwanaume wangu na baba yake waliniita kwao kwa ajili ya mazungumzo.Baba yake alisema kuwa kwa...
23/07/2025

Baada ya kujifungua mtoto, mwanaume wangu na baba yake waliniita kwao kwa ajili ya mazungumzo.
Baba yake alisema kuwa kwa sababu nimezaa mtoto wa kiume, basi anatupa ile ardhi iliyo pembeni ya nyumba yake ili mimi na mpenzi wangu tujenge nyumba yetu tuishi hapo, ingawa hatukuwa tumeoana rasmi, nilikubali.
Mwaka uliofuata, mpenzi wangu alinisihi tuanze kujenga, jambo ambalo nililikubali na kuanza kujenga kwa kutumia pesa zangu.

Wakati huo, mpenzi wangu hakuwa na kazi, lakini biashara yangu ilikuwa inaniingizia kipato kizuri. Kwa hiyo, nilijenga nyumba kubwa ya vyumba vitano kwa nguvu zangu mwenyewe.
Baada ya miezi sita tangu kumaliza ujenzi, tabia ya mume wangu ilianza kubadilika taratibu. Nilivumilia hadi nilipoona hali inazidi kuwa mbaya, ndipo nikamueleza baba yake na kaka yake mkubwa.
Waliahidi kuzungumza naye, lakini sikuona mabadiliko yoyote katika tabia yake kwangu.
Hali ilipozidi kuwa ngumu kuvumilia, nilienda tena kwao kwa wazazi, safari hii baba yake akapanga siku ya kikao cha suluhu.

Asubuhi hiyo nilijitayarisha, nikaoga kisha nikaenda kwenye kikao sebuleni kwa baba yake.
Mpenzi wangu alikuwepo, pamoja na kaka zake wawili wakubwa, dada zake wawili mkubwa na mdogo na baba yake pia.
Baada ya dakika k**a tano ya kukaa kimya huku wakibonyeza simu zao, baba yake aliniuliza kuhusu kile nilichosema kinatokea kati yangu na mwanae.
Nikawaeleza kila kitu.

Baba yake akamgeukia na kumuuliza tatizo ni nini. Yeye akajibu hakuna tatizo, ila hawezi kunioa kwa sababu anataka kumuoa mpenzi wake wa zamani.
Nilishangaa sana kusikia maneno hayo kutoka kwake.
Cha kusikitisha zaidi ni kwamba wote waliunga mkono uamuzi wake hata baba yake alisema hawawezi kumchagulia mke mtoto wao wa kiume.
Dada yake mkubwa akasema si kila uhusiano lazima uishie kwenye ndoa, na kwamba k**a kaka yao amesema hawezi kunioa, basi ni vyema niondoke tu, Mungu ataniletea mume wangu mwenyewe.
Na baba yake akasema “Amina” kwa hilo.

Nikawauliza sasa kuhusu ile nyumba niliyowajengea peke yangu, wote wakajibu kwa pamoja kuwa nibebe nyumba yangu niondoke nayo, wao wabaki na ardhi yao.

Sijui la kufanya, tafadhali niwekee story hii nipate ushauri.

Trust me wanaume wengi wako ndani ya nyumba zao, lakini hawapo nyumbani, k**a unaelewa maana ya nyumbani' ni mahali amba...
23/07/2025

Trust me wanaume wengi wako ndani ya nyumba zao, lakini hawapo nyumbani, k**a unaelewa maana ya nyumbani' ni mahali ambapo unahisi uhuru kimwili, kiakili, na kihisia.
Lakini wanaume wengi wanarudi baada ya kazi, wanaketi kwenye kochi, wanashika simu zao, wanakula chakula cha jioni, halafu wanaenda kulala. Inshort wapo kimwili, lakini kiakili na kihisia wameshatoka zamani, wakifika kwenye nyumba zao wananyamaza, wanapooza, hawajihusishi tena na chochote wanasubiri pakuche waondoke.

Mwanamke nae akiona hali hiyo anaanza kujisikia k**a mwanamke asiye na mume japo yupo ndani ya ndoa, anajiona ana mtu ndani ya nyumba lakini hana wa kuzungumza naye, ana mtu wa kushiriki nae kitanda kimoja lakini si yaliyomo moyoni mwake, anajisikia kutoonekana, kutosikilizwa na polepole anaanza kufa ndani kwa ndani kihisia, hatimaye anabadirika mazima.

Leo nataka niongee na wewe mwanamke...

Tambua, ndoa iko mikononi mwako, mwanamke ndiye moyo wa nyumba, damu ya familia, na dira ya kizazi kijacho, mwanamke mjinga huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe, kwa maneno yake(kamdomo), kwa kiburi chake, kwa kutokujali, na kwa kutokutambua nafasi yake k**a mjenzi wa familia.
Lakini mwanamke mwenye hekima, hata wakati wa dhoruba, hujifunza kunyamaza ili asikilize kwa makini, huomba hekima, huwa na heshima, na huongea kwa upole tena hoja za msingi. Mwanamke anayejitambua anajua kwamba upendo haujengwi kwa maneno matamu tu, bali kwa tabia njema, uvumilivu, na heshima.

Tambua, hakuna nyumbani bila uwepo wa mwanamke, mwanamke ndiye anayefanya nyumba iwe na ladha, iwe na amani, iwe na uzuri wa kipekee, mwanamke anaweza kugeuza nyumba ya kawaida kuwa paradiso ya familia, au akaifanya iwe jela isiyovumilika.
Nyumba yoyote imara, ndoa yoyote imara, hujengwa na mwanamke, Yes! Kwa busara yake hutuliza migogoro. Kwa tabasamu lake huleta faraja, kwa usafi wake hujenga heshima, kwa kufanya maombi huombea mume na watoto wake bila kuchoka.

Mwanamke, tambua nguvu ulizonazo.
Usione k**a wewe ni wa pili au mfuasi tu, Wewe ni kiini, ni msingi, ni kiunganishi cha familia. Usipambane kuwa mwanaume au kujilinganisha na mwanaume, usijifanye kuwa juu ya mumeo, pambana kuwa mwanamke wa kipekee anayemsaidia mwanaume wake kuwa bora. Sio kwa kushindana naye, bali kwa kumtia moyo na kumwelekeza kwa upendo.
Mwanamke mjanja haongei kila kitu.
Anajua muda wa kusema na muda wa kunyamaza. Anajua nguvu ya kimya chenye hekima, anajua si kila tatizo linatatuliwa kwa lawama, bali mengine kwa maombi, subira, na maongezi laini ya upendo.

Leo baada ya kusoma ujumbe huu wa Halisi Naturalist fanya uamuzi mpya.
Usiwe chanzo cha migogoro, kelele, na vurugu nyumbani, badala yake, kuwa chanzo cha upendo, maombi, na utulivu.
Watoto wako wanakuangalia, mume wako anategemea faraja yako, japo kuwa unamuona amebadirika tambua wewe unaweza kuwa sababu ya yote hayo, jikague kisha rekebisha unapokosea, na hata k**a unajiona hauna hatia bado unayo nafasi ya kumrekebisha ili ndoa yenu isimame tena, kumbuka mwanaume ni k**a mtoto na wewe ni k**a mama, mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, anaweza kuchelewa kuiona thamani yako lakini ipo siku isiyo na jina utaibuka mshindi, Mungu yuko katikati ya kila jambo la kheri na kwa shetani sio pa kudumu ni pa muda tu.

Ndoa ni uwanja wa mapambano ya kiroho, kihisia, na kiakili, mwanamke mjanja hajitoi mapema. Hujifunza, hurekebisha, na kusimama imara.
Hata wewe unaweza.
✍️✍️✍️✍️

Wanaume watatu kutoka Nigeria walik**atwa hivi karibuni katika jaribio la kushangaza la kusafiri kwenda Dubai bila kugun...
23/07/2025

Wanaume watatu kutoka Nigeria walik**atwa hivi karibuni katika jaribio la kushangaza la kusafiri kwenda Dubai bila kugundulika. Wakiwa wamevaa mavazi marefu, vitambaa vya kichwani, na nikabu, walijifananisha na wanawake Waarabu kwa lengo la kukwepa mamlaka na kuonekana k**a wasafiri wa k**e. Vipodozi na mavazi yao vilikuwa vya kushangaza kwa jinsi vilivyoandaliwa kwa umakini na ustadi mkubwa, lakini jinsi walivyokuwa wakitembea ilisababisha kutiliwa shaka kwenye vituo vya ukaguzi wa uhamiaji.
Tembea yao haikuwa na chembe ya k**e kiasi cha kutiliwa shaka.

Mamlaka ziligundua haraka ujanja huo na kuwatia nguvuni. Picha za mabadiliko yao zilishangaza mitandao ya kijamii na kusambaa kwa kasi. Wakati baadhi ya watu waliona ujanja huo kuwa wa ujasiri na hata wa kuchekesha, tukio hilo liliibua pia mijadala kuhusu hali ya maisha kuwa ngumu na umasikini ndio vichochezi vya juhudi zao za kutaka kusafiri bila kibali, huwenda walichochewa na fursa au hali ya maisha, kitendo hiki cha ujasiri kilionekana k**a mfano wa kushangaza wa jinsi watu wanavyoweza kufanya lolote ili kutimiza ndoto zao.

Daah sema make up artist alikuwa konyo sana 🤣🤣🤣❤️❤️

Mi mama mkwe wangu anavyonipenda kuna muda nashtuka, sijui kuna ajenda gani nyuma yake, napenda anavyonipenda ila nimean...
22/07/2025

Mi mama mkwe wangu anavyonipenda kuna muda nashtuka, sijui kuna ajenda gani nyuma yake, napenda anavyonipenda ila nimeanza kuwa na maswali mengi kichwani.
Mwaka jana mtoto wake (mume wangu) alitaka kumuoa binti mmoja, akawa anasumbua sana ndani, siunajua mwanaume akishapata mwanamke mpya anakuwa k**a anachanganyikiwa hivi, dharau kibao, na kukuona si kitu.
Basi mimi nilivyoona dharau zimezidi ndani pamoja na manyanyaso ya hapa na pale, nikaamua kwenda kwa mama mkwe wangu kushtakia, basi nikamueleza yote, akaniambia nisijali matatizo uataisha, nirudi nyumbani atakuja kesho, sisi tulikuwa tunaishi mjini yeye kijijini.
Kweli kesho yake alikuja mida ya jioni, akalala siku moja kisha akarudi palipokucha.
Usiku ule baada ya kuongea mawili matatu na sisi
alielekea chumba cha wageni kulala, na dakika chache baadae aliniita.

Nikaenda chumbani alipokuwa, akaniambia "mwanangu usiwe mjinga, pambana, mwanaume siku zote anatulizwa, mwanaume bila kutulizwa ndoa haiwezi kudumu hata sisi ujanani mwetu tuliwatuliza ndio maana unaona tumezeeka nao, huyo mwanangu akioa huyo mwanamke habari yako itaishia hapo, kwanza kwa uwezo gani alionao kumiliki wanawake wawili? wajukuu zangu watapata maisha magumu sana endapo riziki hii ndogo aipatayo ikigawanywa, na ukiona ameoa mwingine tambua kuwa ataharibika jumla, ataendelea kuoa na kuacha, mimi k**a mama yake sitaki mwanangu aharibike, kwahiyo nitakupa dawa umtilie kwenye chakula au kinywaji"

Akanipa dawa na nikafanya alivyonielekeza, kweli mwanaume akatulia, akaanza kunipenda na kunijali, akaachana na yule mwanamke na michepuko yake yote, tukaishi kwa furaha sana, nyumba yetu ilikuwa ya mfano mpaka wanawake wenzangu wakawa wananiuliza nimewezaje! Sikuwahi kuwaambia zaidi niliwaambia wawaheshimu waume zao, wachunge ndimi na tabia zao watapendwa, ingawa najua hata mimi nilikuwa hivyo ila haikusaidia chochote.

Kinachonishangaza mpaka kuja kwako kuomba ushauri, ni kwamba huyu mama mkwe huwa anawapa dawa hata wakwe zake wengine walioolewa na watoto wake wa kiume, sijajua kuhusu watoto wake wa k**e maana sijafatilia, na amekuwa na mazoea ya kunipa dawa mara kwa mara kila anapokuja kututembelea, najiuliza kwanini dawa anazonipa anataka niweke kwenye chakula tunachokula wote? Ananiambiaga tule wote na mume wangu kwamba dawa itamshika muhusika tu ambaye ni mume wangu, na kinginr najiuliza kwanini ananipa dawa nimpe mwanae wa kumzaa!

Hilo linanishangaza sana, tukiacha matokeo ya dawa ambayo yamekuwa chanya na faida kubwa kwa upande wangu na familia kwa ujumla.
Maana akipatacho anakileta k**a kilivyo nyumbani tunapanga wote mikakati ya kufanya na akitoka kazini anarudi nyumbani mapema, starehe yake ni mpira kwahiyo k**a kuna mechi huwa namwambia akaangalie haijalishi atarudi saa tisa za usiku sina wasiwasi kuhusu hilo, maana alisema yeye hapendi kuangalizia nyumbani mechi, anapenda kuangalia ukumbini ndio ana enjoy, na mimi sina tatizo na hilo.
Huyu mama mkwe hawezi kuwa na ajenda yoyote kwa baadae kweli, je kuna mwingine amewahi kukutana na mama mkwe k**a wangu labda! Halisi Naturalist nipostie plz.

Story yenye funzo kubwa., "Baba yangu hakuwahi kuamini kwamba ningeweza kuwa mtu wa maana, sio kwa sababu nilikuwa mvivu...
22/07/2025

Story yenye funzo kubwa., "Baba yangu hakuwahi kuamini kwamba ningeweza kuwa mtu wa maana, sio kwa sababu nilikuwa mvivu au mkaidi, bali kwa sababu mimi sikuwa Clement.
Clement kaka yangu mkubwa alikuwa mtoto wa kwanza, fahari ya familia. Alikuwa na akili za watoto kumi. Kijana wa aina ile ambao majirani hutumia k**a mfano wanapowakaripia watoto wao.

Alipofaulu mtihani wake kwa alama za juu, pale home tulisherehekea k**a vile harusi.
Baba aliuza moja ya viwanja vyake ili kumpeleka Clement chuo kikuu cha binafsi, pia alikopa pesa mpaka kanisani ili kuongezea.
Wakati huo nilikuwa kidato cha pili, nilimwambia Baba nataka kujifunza ushonaji baada ya kumaliza shule.
Alinikatisha tamaa kwa maneno yake. “Mshonaji? Niliyajua haya maana kidogo wewe mwenzetu una akili iliyolala sana wala sijashtuka." Mtoto wa kiume unawaza kushona vitenge" niliumia moyoni ila sikusema kitu.
Nikaanza kusoma kwa bidii, lakini hakuna kilichobadilika sana, nilikuwa na uelewa wa wastani darasani, sikuwa kilaza wala genius.

Clement aliporudi nyumbani likizo, Baba alikuwa akichinja kuku wawili, jambo ambalo hakuwahi kutufanyia sisi wengine.
Siku moja nilimsikia Baba akimwambia mgeni,
“Clement atakuwa mtu mkubwa ila yule mwingine! Tumuachie Mungu, bado sana kwakweli”
Yule “mwingine” nilikuwa mimi.
Ikafika time halafu Clement akahitimu chuo.
Usiku wa sherehe ya kuhitimu kwake, Baba alilia kwa furaha huku ameshikilia chupa ya malt, anakunywa kwa raha zake. Akasema:

“Furaha yangu imetimia leo! Uwekezaji wangu uko karibu kuzaa matunda!”
Sote tuliamini hivyo pia mpaka pale mambo yalivyoanza kubadilika.
Clement alianza kukaa muda mrefu ndani ya chumba chake, akaacha kutoka nje, kula hataki anakula biscuit na soda, kula ni mara chache tu, Usiku mmoja tukamkuta nyuma ya nyumba akinusa kitu kutoka kwenye mfuko wa nailoni, macho mekundu k**a moto.

Siku hiyo Baba alianguka kwa mshtuko.
Ikagundulika Clement alikuwa akitumia dawa za kulevya tangu mwaka wake wa tatu chuoni. Hakuwahi kumwambia mtu pale home ilikuwa siri yake,
Vitu vikaanza kupotea nyumbani, saa ya mkononi ya Baba, hereni za dhahabu za Mama alizopewa na rafiki yake aliye nje ya nchi.
Hata feni ya sebuleni alipita nayo pia, ni wazi kuwa Clement alihitaji pesa kwa ajili ya dawa zake.
Yule kijana wa dhahabu alianza kubadirika kwa kasi.

Aliingia na kutoka kwenye kituo cha kurekebishia tabia kwa miaka miwili na wakati ambao hakuwa huko, alikuwa akiibia watu mtaani na nyumbani.
Ila mimi nilipomaliza sekondari, nilimsihi Mama amuombee Baba Rasheed ambaye ni mshonaji wa mtaani kwetu maarufu anikubali k**a mwanafunzi, nikaanza kujifunza fani hiyo.
Wakati Clement bado alikuwa akipambana kurudi kwenye hali yake mimi nilifungua duka langu la kwanza, japo halikuwa kubwa, lilikuwa la hadhi ya chini.
Halafu nikapata mashine yangu ya kwanza ya kisasa ya kushonea maana nilikuwa najichanga mdogo mdogo.

Mama alikuwa akilia wakati mwingine akinisaidia kupiga pasi nguo za wateja. “Mungu anaona kila kitu, atatusaidia “we endelea tu."
Pia alikuwa akimuombea sana Kaka na alikonda sana kwa mawazo ya kumuwaza bro.
Baba alipata stroke, hakukuwa na wa kumkimbilia.
Clement alikuwa rehab, Edwin mdogo wetu wa mwisho, bado alikuwa shule, hivyo nikachukua jukumu la kumsomesha na kuangalia mazingira ya nyumbani.

Nikagharamia bili za hospitali, nikalipia dawa zake. Nikalipa mtaalamu wa mazoezi aliyekuwa akija kila jioni, ilikuwa ni biashara yangu ya ushonaji iliyobeba mzigo ambao Baba alifikiri ni Clement tu angeweza kuubeba.
Nilipata bahati ya kupata tenda kubwa sana ya kushona suti za k**e na kiume kwenye kampuni fulani, ambapo jina langu likatamba kazi zikawa nyingi kubwa kubwa, ofisi ilikuwa sana na niliajiri wengi sana,
Ikabidi ninunue kigari cha kutembelea nijipongeze, nikaipeleka mpaka pale home sio kwa kujionesha, nilikuwa tu nataka wazazi wajisikie vizuri juu yangu.

Baba alikuwa kwenye baraza, amechoka na amedhoofika, alinitazama kwa muda mrefu, kisha akasema:
"Mwanangu nisamehe nilikosea.”
Hakuwa na hotuba ndefu, maneno matatu tu ambayo nilisubiri miaka mingi kuyasikia.
Na siku hiyo, kwa mara ya kwanza kabisa, alinibariki kwa dua nzuri.
Hapa nilipo familia inanitegemea mimi, na riziki zinafunguka nashukuru Mungu, ni hayo tu bro nikikuwa najaribu ku-share experience yangu.

✍️ Dah hapa kuna funzo kubwa....

Sio kila nyota hung'aa kwa makelele.
Nyingine hung'aa kimya kimya, gizani zikisubiri kutambuliwa.

Baba alimchagua Clement, lakini maisha yalinichagua mimi.
Na mwisho wa yote, haikuwa akili kubwa iliyookoa familia , bali ni uaminifu na uthabiti kwa kile alichokiamini ."

Usimkatie tamaa mtoto yeyote.
Sio kila mbegu huota kwa wakati mmoja, lakini kila moja inastahili maji, mwanga, na jua.

Wazazi wana matarajio makubwa sana kwetu, tuheshimu mchango wao, tusiwaangushe.

1. Usimpende mtu kwa akili zako zote, isipokuwa yule aliyekupenda kwa moyo wake wote. Soma tena…✍️2. Anza na Mungu kila ...
21/07/2025

1. Usimpende mtu kwa akili zako zote, isipokuwa yule aliyekupenda kwa moyo wake wote.
Soma tena…✍️

2. Anza na Mungu kila jambo, usikubali ushauri wa shetani kwenye jambo lolote. Maombi kwanza, mengine baadaye.

3. Usijali wanaokuzungumzia vibaya, hata ukinyamaza watazungumza, ukijibu watazungumza, wadharau tu wataumia na watashangaa kwanini wanakurushia mawe lakini hayakupati.

4. Mafanikio hayaji kwa kubahatisha yanakuja kwa nidhamu, juhudi, na neema ya Mungu.

5. Ukijifunza kutulia kimya wakati wengine wanakuchokoza, utakuwa umefikia hatua ya juu sana ya hekima, na mwisho wa yote ushindi wako itakuwa ni 'HESHIMA'.

6. Acha kulalamika kila siku, ongea na Mungu kuliko watu, unaowalalamikia hawajali k**a unavyodhani, Mungu ndiye mwenye majibu ya kweli.

7. Si kila anayekusaidia anakupenda, wengine wanatengeneza deni la kukutawala baadaye.

8. Amini ndoto zako zaidi ya hofu zako, maana Mungu haweki ndoto moyoni mwako kwa bahati mbaya.

9. Ukiona mtu anakudharau, usipoteze muda kujinyanyua ili uthibitishe lolote, usijibu, we endelea kupambana tu, huko juu ndiko kuna jibu bora.

10. Usitamani maisha ya watu wengine hujui gharama ya machozi nyuma ya tabasamu unalo liona kwao.

11. Marafiki wa kweli sio wale wanaocheka na wewe, chagua kwenda na wale wanaolia na wewe.

12. Mapenzi ya kweli hayaumizi k**a wasemavyo, kinachoumiza ni tamaa, uongo, na matarajio ya upande mmoja.

13. Ukitaka Mungu asikie haraka, lia naye kwa unyenyekevu, si kwa maneno mengi bali moyo wa toba.

14. Usimwombe Mungu akunyanyue haraka, bali muombe akujenge imara kabla ya kukuinua ili wakati amekuinua usiwe mtihani kwa wengine bali uwe neema kwa wengine.

15. Kila siku unayoishi ni fursa mpya ya kutengeneza historia, usiiache ipite bure.

16. Ukikaa na wenye hekima, utakuwa na maneno ya maana na vitendo ya hekima, ukikaa na wapuuzi na wewe utakuwa mpuuzi.

17. Jifunze kusema “hapana” kwa upole lakini kwa msimamo' pale unapohitaji kusema hapana, ni silaha ya kulinda amani ya moyo wako.

18. Usiweke moyo wako mahali pa muda kwa kujipa imani patakuwa pa kudumu, utajilaumu maishani mwako na hautaweza kurekebisha.

19. Wanaokufuatilia kwa siri wanaweza kuwa mashahidi wa mabadiliko yako, endelea kusonga mbele kimya kimya.

20. Ukitaka kuponya moyo wako, samehe hata k**a hukutendewa haki, Mungu huona, Mungu hulipa.

KALAMU 20 ZA HALISI NATURALIST

Nadhani kuna kalamu moja au zaidi zimekugusa, endelea kubarikiwa, tukutane wakati mwingine, kwa kalamu zangu 20 nyingine, nawapenda sana na Mungu awabariki daima.
Follow Halisi Naturalist na share makala hii.

Nikiona wanaume wanasema mitandaoni eti hatuoi single mother huwa naumia sana moyoni, naona k**a dunia haina huruma kwa ...
21/07/2025

Nikiona wanaume wanasema mitandaoni eti hatuoi single mother huwa naumia sana moyoni, naona k**a dunia haina huruma kwa mwanamke, naona k**a mwanamke ni kiumbe cha nyongeza tu hapa duniani ingawa bila mwanamke dunia haiwezi kuwa sehemu salama kabisa.
Kingine ninachoshangaa kwanini kosa moja la mwanamke linachukuliwa kwa uzito sana na kulaaniwa vikali kuliko makosa 1000 ya mwanaume? Hapa ndipo nakuja kwenye ile point kuwa mwanamke ni kiumbe cha kuonewa always tangu dunia iumbwe.

Mimi sio muumini wa feminism na kwa namna moja au nyingine naona feminism ina haribu baadhi ya mifumo sahihi ya kimaisha, lakini kwa upande mwingine feminism ni mfumo ulioanzishwa duniani ili kumpa nafuu mwanamke, ili kumtua mzigo mwanamke, maana manyanyaso yamezidi sana kwetu 😔,
Wazungu wanacho haribu ni kuiweka juu feminism na kuishusha chini masculinity, hapo ndio wanaharibu, lakini positive masculinity naikubali kwasababu mwanaume lazima awe mwanaume, nachokataa ni manyanyaso ya mwanamke hapa duniani.

Imagine mtu anakudanganya anakupenda unamuamini anakuzalisha kwa matumaini kuwa atakuoa, au anakuoa kabisa ila akisha kuzalisha anakukimbia, then mwanaume huyo huyo anashika bango na kusema sioi single mother, hivi hata mbele za Mungu k**a kweli kuna haki huyu mwanaume si mtenda dhambi mkubwa sana!?
Kwenye baadhi ya mambo yanayo wanufaisha wanasema "mwanamke ni kiumbe dhaifu" ni mwepesi kurubunika, ni mwepesi kudanganyika, ila wakisha kuharibu hawasemi tena wewe ni dhaifu wanasema wewe ni shetani kwanini ulikubali! Wanasahau ulaghai wote na nguvu zote walizotumia kukuvua heshima yako.

Kaka halisi usione naongea haya yote ukadhani nimekurupuka, mimi nimezaliwa katika familia ya wake wengi, mama na wake wengine wa baba walikuwa hawaelewani hata kidogo, wivu, uchawi kurogana, kupigana ilikuwa ndio life style ya familia yetu, na kibaya zaidi wote walikuwa sehemu moja yaani nyumba tatu zilizokuwa karibu karibu.
Nilipo maliza form four nilifaulu ila baba akawa hana pesa za kunipeleka advance maana nilifaulia mkoa mwingine, ikabidi msamalia mmoja ajitokeze kunisomesha, ni baba mmoja jirani yetu.

Nikasoma nik**aliza form 6, nikarudi nyumbani kusikilizia majibu, Mungu saidia nikafaulu na hata mkopo nilibahatika kupata wakati nataka kujiunga chuo fulani kikuu Dar es salaam.
Mama mmoja (mke wa baba) alikuwa na wivu sana na mafanikio yangu, alitumia mbinu nyingi kunifelisha lakini akawa anashindwa maana ilibidi niwe najishughulikia mara kwa mara (wenye D 2 wataelewa), basi bwana hatua ya mwisho alimtafuta kaka mmoja na yeye ni jirani akamwambia anitongoze na ahakikishe ananipa ujauzito, atamlipa pesa maana ana urithi wa kiwanja huko kwao ataenda kuuza amlipe, vihela vya vocha akawa anampa sana.

Yule kijana alifurahi kupewa dili hilo maana hata k**a asingeahidiwa pesa angekubali kutokana na mimi nilivyo, nikikuwa mstaarabu sana, sikuwa na mambo ya wanaume kabisa, na ni mrembo mashaallah, basi akanitongoza lakini sikukubali nikamwambia siwezi kutongozwa hivyo, k**a unanipenda na una nia njema na mimi we fika kwa wazazi ukaongee nao, fuata taratibu zote.
Kijana akamwambia mama mdogo yote ndipo waliposuka mpango wa kunitafutia dawa, nikapulizwa dawa za hatari, uchawi ukaniingia nikaanza kuwaza nisiende chuo kabisa, yaani nikajikuta nampenda yule kijana na nikaenda kumtafuta mimi mwenyewe, tukawa wapenzi na katika kulala nae narudi nyumbani nimechelewa natukanwa, inshort nilibadirika sana ikafikia hatua nikahamia kwa huyo kijana ( alikuwa na geto pembeni kidogo ya mji).

Nikaja kupata ujauzito, habari za chuo nikaachana nazo kabisa, so nikajifungua mtoto wa kiume, yule mama mdogo nilimsikia kwa masikio yangu mawili anampongeza yule mzazi mwenzangu, nililia sana na niliumia sana, nilipomuuliza alikataa akasema nimeelewa vibaya,
Baada k**a ya miezi 6 nimejifungua yule kijana akanipa sh laki moja akasema nirudi nyumbani, hana uwezo wa kulipa kodi anataka aende kutafuta maisha mkoani Mbeya akirudi atanichukua, basi nikamuelewa ila nikawa sijui nitarudi rudije nyumbani, nikajikaza nikaenda, Baba alinifukuza mama akawa ananitetea basi na yeye akajumlishwa tukatukanwa sana.
Yule mama mdogo alikuwa upande wa baba anamshawishi nifukuzwe na maneno mengi sana ya kukashfu, anamkashifu mama, eti msomi! Msomi atakuwa huyu!

Ila mwisho nilisamehewa nikakaa nyumbani hapo, kila nikimpigia yule mzazi mwenzangu hapatikani, kumbe alibadili namba, basi ikabidi niwe mpole maana nilifatilia kwa ndugu wanasema alikataa tusikupe namba yake, nimeishi hivyo hadi mtoto akafikisha miaka mitatu, nikawa napata vijikazi vya hapa na pale, katika kujuana na watu nikapata dada fulani ni mkenya, akanisaidia sana kipesa na hata kimawazo mpaka nikawa sana kisaikolojia, hatimaye nikarudi shule na nikafanikiwa kumaliza degree yangu, mtoto kwa sasa ana miaka 6.

Siku moja yule baba wa mtoto alinitafuta k**a miaka miwili nyuma, akaniambia kila kitu walichofanya na mama yangu mdogo, akaniambia yale uliyosikia tukiongea kwenye simu ilikuwa ni ukweli mtupu, kwakweli pole sana na kwasasa najisikia vibaya kuharibu ndoto zako, maana pale mtaani ukisifika sana kwa kuwa mtulivu na msomi mwenye akili, ila tu naomba unisamehe na mimi nilipitiwa na shetani, nilimsikiliza sijajibu chochote nikazima simu na kutafuna ile laini ya simu hapo hapo, sikutaka ibilisi huyo aje anipate hewani hata kwa bahati mbaya tena.
Yule mama mdogo alifanya mengi kwenye familia mpaka akahakikisha baba anaacha wanawake wote akabaki yeye tu.

Kwasasa naishi na mwanangu na mdogo wangu wa mwisho, ila pia nashukuru nimempata mwanaume muungwana sana, nampenda sana maana amenitoa mbali mno, mwezi ujao tutafunga ndoa inshaallah, ila tu huwa naumia na kelele za single mother mitandaoni, japo nimepata wangu ila nawahurumia wenzangu maana si kila single mother ana makosa au labda ni malaya au hajitambui, wengine wamepita mapito k**a yangu na mengine mazito hata zaidi yangu.
Wajinga wachache waoolewa na kuwarudia max zao ndio wanaharibu lakini kiukweli inaumiza sana tena sana, Mungu awafanyie wepesi wenye mitihani k**a yangu.
Hawa wanaume wanaopiga kelele mitandaoni wengi wao ndio wanazalisha wanawake na kuwaacha halafu wanakuja kuwaharibia sifa mitandaoni, inshort ndio mawakala wa shetani.

Nisamehe nimeandika story ndefu ila hata hapo nimefupisha sana.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Naturalist posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Naturalist:

Share