Halisi Naturalist

Halisi Naturalist A safe space for real-life stories & community advice. ๐Ÿ’ก
๐Ÿ’Œ Send your story (anonymous), letโ€™s learn and grow together. Be real, Be natural, Be positive.
(1)

06/09/2025

Kwanini upendo uliompa mama yako kabla ya kuingia kwenye ndoa, ukishaingia tu unapungua? Wamama wanavyotupenda kwa moyo 1 eti tunaanza kuwaona kawaida tu๐Ÿค”

Hivi mwanamke unapataje ujasiri wa ku-cheat wakati kiasili mwanamke anatakiwa awe wa mwanaume mmoja?  ๐ŸซขMaana wanaume kia...
06/09/2025

Hivi mwanamke unapataje ujasiri wa ku-cheat wakati kiasili mwanamke anatakiwa awe wa mwanaume mmoja? ๐Ÿซข
Maana wanaume kiasili ni wa wanawake wengi, je nyie hiyo asili ya kuwapanga wanaume wawili au zaidi mmeitoa wapi mbona sio asili yenu aliyo waumba nayo Mungu? ๐Ÿค”๐Ÿค”๐Ÿ™†โ€โ™‚๏ธ

Mara nyingi huwa nacomment matatizo yanayowasibu wenzangu ila haya yangu nayo naona pia yanazidi kunichanganya zaidi.Kip...
06/09/2025

Mara nyingi huwa nacomment matatizo yanayowasibu wenzangu ila haya yangu nayo naona pia yanazidi kunichanganya zaidi.
Kipindi cha nyuma mwezi wa nane nilikuletea ujumbe nikiomba ushauri kuhusiana na changamoto ya kiafya iliyokuwa inanisumbua, usiku nikilala, pumzi kukata nikiwa usingizini mwili kulegea, kuhishiwa nguvu, nashindwa kuongea, nikijigusa mwili wangu nahisi ganzi, mapigigo ya moyo kupungua kwa asilimia kubwa, kuwa na wasiwassi na nafsi kutanga tanga.
Nilipata daktari ambaye aliweza kuangalia afya yangu kwa kina na kisha aliniambia kuwa niko na "sleep paralysis" ambayo mara nyingi hutokea mtu anapolala ila yangu iko tofauti sana na sio ya kawaida, alinipa baadhi ya dawa kisha alinishauri pia nitafute walimu nifanyiwe visomo.
nilifuata ushauri wake, na visomo nilifanyiwa ila baada ya visomo sasa nik**a niliamsha mambo mengine.

Vitimbi vilianza kwa namna nyengine, yaani nakumbuka ilikuwa jumapili nikiwa narudi nyumbani saa nane mchana, nilipishana na mwanamke aliyekuwa kavaa nguo nyeusi amejifunika mpaka masikio yake unaona sura tu tu, yule mwanamke macho yake yalikuwa meupe hakuwa na mboni, alafu yalikuwa k**a yana makengeza kila jicho lake lilikuwa limeangalia upande wake, alipita kando yangu akiniangalia vibaya sana mwili wangu ulisisimka, hofu ikanijaa sana nikaomba sana huku nikiwa natembea kwa upesi, nilipoangalia nyuma sikumuona tena sjui alienda wapi yule mwanamke,
ila juzi usiku kuamkia jana kuna paka walikuja mlangoni kwangu usiku, nilikuwa nimetoka kuoga naingia ndani nikaona paka kwa nyuma yangu mweupe ananyata ila kutizama upande mwengine nikaona wengine watatu wameongozana kila paka anakuja na njia yake alafu wakasimama mlangoni kwangu.

Mimi wakati huo nilikuwa nimefunga mlango natizama kuna design ambazo zilitengenezwa kwenye mlango wangu wa chuma waeza chungulia ukaona nje, hao paka walianza kulia sauti za ajabu ajabu k**a watu, nilishindwa kuvumilia nilisoma dua kisha nikawafukuza, ila asubuhi nilipoamka nilimuona mdogo wangu wapili wa k**e akichungulia chungulia sehemu kwa mshangao, nilipoenda kutazama niliona paka watano wanafanya mapenzi hadharani, tena wanasubiriana kwa zamu huku wakipiga kelele.

Nilichukua jiwe nikawafukuza wakatawanyika, sasa maajabu niliyoyaona leo, nyumbani sisi tuna mifugo mbuzi kumi na moja, sasa mdogo wangu wa tatu wa kiume alizipeleka malishoni asubuhi akazifunga akarudi nyumbani, kisha jioni nikaenda kwa ajili yakuzifungua, ila cha ajabu sasa kuna mbuzi moja nimeifungua ikaning'ata kwenye paja, nikiwa nainama ili niifungue ilikuwa imejifunga funga na kamba yake kwenye mti, nikaipiga kidogo ikaniachia ila bado ikawa inanisogelea usoni sasa huku inaniangalia kwa hali isiyo ya kawaida, kisha nikainuka huku nashangaa, ikaniuma kwa mkono ikanikaza hapo haitaki kuniachilia, nikaipiga kibao ikaniacha, ila hilo jambo limenishtua nikaiacha nikarudi nyumbani.

Sikuifungua tena, nikaenda kumsimulia mama niliyoyaona kule, kiukweli mama ameshtuka sana alikuwa anakunywa maji pia akayaacha akaniangalia kwa huruma sana kisha akaniambia nimuonyeshe nilipoumwa, kiukweli hali ile imemshtua mama kulikuwa na alama ya meno japo haikunikata, ndugu zangu hawana raha mpaka sasa wanawasiwasi mno๐Ÿ˜ข.

Najiuliza haya majanga jamani mpaka nakosa raha, si yule mwanamke bado ananitafakarisha akilini, na haya mengine, sielewi kabisa, naombeni ufumbuzi. ๐Ÿ™

Habari ndugu, sasa mi nina kisa kimoja hivi, mimi nimeajiriwa kwenye wizara fulani hivi, nimeoa na nina watoto wawili, k...
06/09/2025

Habari ndugu, sasa mi nina kisa kimoja hivi, mimi nimeajiriwa kwenye wizara fulani hivi, nimeoa na nina watoto wawili, katika kazi za kiserikali nilihamishiwa sehemu fulani ndio nafanyia kazi na familia nimeiacha kwangu ila kuna umbali kidogo siwezi kwenda kwenye familia mara kwa mara kwa sababu ya majukumu ya kazi.

Suala ni hivi nilipohamia nilipata hawala/tuseme mjane sababu mume wake alipata ajali akafariki akamwachia mali na biashara zake, anaziendeleza, watoto wake wanasoma shule nzuri kiujumla ana maisha yake ingawa na mimi nilimfungulia mke wangu biashara zake maana muda mwingi anakuwa na biashara zake hadi inafikia kipindi hata hanikumbuki k**a zamani.
Sasa hawala ananipenda sana na ananijali sana kuliko mke wangu, mke wangu anamfahamu na anamheshimu na hataki kuingilia maisha yangu.

Tatizo hataki niongee na mwanamke yoyote tofauti na mke wangu, shida yake ana wivu sana nikimuaga naenda kwenye familia yangu hapendi, naondoka namuacha hajapenda, kingine nikiongea na wafanyakazi wake anamaindi na anawamaindi.
Naomba msaada kwa wadau najinasuaje na sitaki kumuumiza maana tangu mume wake afariki hapendi mtu yoyote tofauti na mimi na yupo tayari kuwa mke wa pili na mimi sitaki mke wa pili na sitaki kumuumiza mke wangu.๐Ÿ˜ซ๐Ÿ˜“

Halisi habari yako! Naomba nishauriwe๐Ÿ™. Mama yangu kwenye ndoa yake ya kwanza alizaa Watoto wa4, inasemekana mume wake h...
06/09/2025

Halisi habari yako! Naomba nishauriwe๐Ÿ™. Mama yangu kwenye ndoa yake ya kwanza alizaa Watoto wa4, inasemekana mume wake huyo alikuwa anampiga mpaka mama anazimia pia alikuwa ni muwindaji wa wanyama polini so anasema kuna muda alikuwaga anamelekezea Gobole/ bunduki anataka kumuua, mama alipo choka akarudi kwao ndio akakutana na baba yangu wakanizaa mimi, na baba yangu alikuwa bado kijana mdogo familia ya baba wakamwambia huwezi oa mwanamke ambaye alisha olewa na kuzaa watoto wa4, kwaiyo babu akamtafutia baba binti akamuozesha.

Mimi niliishi kwa mama ila baba alikuwaga anakuja kunichukua naenda kwake kutembea, sasa mama baada ya kuona mwanaume aliyekuwa anataka kumuoa amebadiri mawazo ghafla na kaozeshwa binti akakata tamaa kuhusu baba, na haikupita muda mrefu akapata mbaba mwingine, ni mwalimu wakawa wanaishi pamoja ila yule baba akaja kahamishwa mkoa mwingine ikabidi mama na mimi tuhamie huko huko, ilileta ugomvi sana kati ya baba na mama kwani baba yangu alikuwa hataki mimi niende na mama na kipindi hicho baba na mkewe walikuwa tayari wana Watoto 2.

Mama akasema siwezi acha mwanangu aelelewe na mama wa kambo, basi tukaishi huko na tulikaa k**a miaka 4 hapo mimi niko darasa la 3, mama akabeba mimba ya yule mwalimu lakini maisha yalikuwa magumu sana sababu yule baba alikuwa amesha pata mwanamke mwingine nje, mama alipambana sana, mdogo wangu alizaliwa kwenye mazingira magumu mno, yule mwalimu alikuwa anatoa pesa kwa shida sana, hapo toka tuhamie huko baba yangu mzazi alishawahi kuja mara moja tu, nakumbuka alikuja na mahidi k**a gunia mbili lakini mama alilalamika sana na kwa hasira akasema "umeambiwa nimeshindwa kulisha huyu mtoto" walijibishana sana baba akazira/akasusa, hakuwahi kumtafuta tena alikaaa kimya basi maisha yanasonga mpaka nik**aliza shule.

Sikufaulu, ikumbukwe mama alipoondokaga kwa mume wa kwanza aliwaachaga watoto wake wote wa4, yule mkubwa alikuwa amesha olewa jijini Dar, kwa hiyo nilipo maliza shule dada alimuomba mama niende kuishi kwake ili nimsaidie majukumu ya kulea Watoto wake, mume wa dada yangu akaanza kunitaka kimapenzi kiukweli nilikataa nikaona hapa nitawagombanisha,
nilitafuta kazi za ndani bila kumwambia dada nikatoroka nikaenda kufanya kazi nilikua nalipwa mshahara mdogo sana nakumbuka ilikua sh 17,000 tu kwa mwezi ๐Ÿ˜”, nilivumilia nikakaa miaka 2 nikijichanga na baadaye nilimwambia dada niko wapi na malengo yangu yalikuwa kujifunza cherehani kushona, kweli nilifanikiwa kupata pesa nikaja kumuomba dada "naomba nikae kwako huku nikiwa najifunza kushona" dada alikubali huwezi amini nilikua naamka mapema mno, kuna mama ntilie nilimuomba kibarua nikawa nikifika nasaidia kuchota maji na kazi za asubuhi ikifika saa 4 naenda kujifunza kushona, natoka saa 12 jioni napita tena kwa mama ntilie kumuoshea vyombo na masufulia mpaka saa mbili, alikuwa ananipa buku na mia mbili tu ๐Ÿ˜”, hiyo yote ilikua ni kumkwepa shemeji tusionane.

Nilifanikiwa kujua kushona, miaka kadhaa ikapita nikapata mchumba nikaolewa na sasa nina watoto watatu namshukuru Mungu, ila tatizo linalo nisumbua ndugu Halisi Naturalist natamani sana kwenda kumuona baba yangu.
Hivi karibuni k**a miaka 5 tumekuwa tukiwasiliana na baba, mama alikubali japo kishingo upande, ila inaonekana hapendi niwasiliane nae kabisa, shida inakuja nikimwambia nataka kwenda kumuona baba ataniambia maneno mabaya na makali mpaka naogopa, na mm sitaki kumkwaza, yaani nimegundua hata baba wa mdogo wangu hataki hata kusikia anawasiliana na mdogo wangu, ila mumewe wa kwanza anawasiliana vizuri na watoto wake wanne,

Na pia aliwaruhusu kwenda kwa baba yao, tatizo lipo kwangu na mdogo wangu yaani baba zetu hataki hata kuwasikia kabisa k**a baba yangu yaani sijawahi mpa hata mia, ila yeye ndio anaweza kuniambia "mwanangu hela hiyo ya wajukuu zangu wanunulie hata kuku wale, naweza kufa sijawaona ila wale hata pesa ya babu yao".
Natamani sana kwenda ila naogopa ninaweza kwenda nikapata matatizo je mama yangu ntamwambiaje!๐Ÿ˜“ naomba nishaurini plz nipo dilema. Nitafatilia comment zote jamani ๐Ÿ™

Naombeni mbinu mnazotumia kudumu na mchepuko wanawake wenzangu, nashindwa kubalance kati ya mume wa ndani na mchepuko.Ha...
05/09/2025

Naombeni mbinu mnazotumia kudumu na mchepuko wanawake wenzangu, nashindwa kubalance kati ya mume wa ndani na mchepuko.

Halisi Naturalist habari yako! mimi ni mama mwenye umri wa miaka 31 naishi na mme wangu na tumebahatika kupata watoto 2, bwana mwaka 2020 mme wangu alibadilika sana, yeye si mtu wa matusi, wala kashifa ila nilichoka kihisia, kwasababu alikuwa si mtu wakuipenda nyumba yake, alikuwa ni mtu anaefanya kaz kwenye migodi, hela anapata sana wala si mchoyo anaweza akatuma pesa wala hata hujamuomba lakini asikanyage nyumbani hata miezi 6, na sio mbali anapofanyia kazi.

Kusema ukweli hali hiyo ilikuwa inanikosesha amani, rafiki zake aliokua anafanya nao kazi walikuwa wanakuja kwenye familia zao yeye anaishia kuwaagiza mtaenda kuwaona na kwangu, wananifikishia taarifa tu.
Ukiwa mwanamke kwa hali hiyo kuna mengi ya kufikirisha, unawaza pengine ni sababu ya wanawake ndio maana ananifanyia hivi, basi maisha yakasonga japo nilikua najizilisha, nanuna, nafoka, lakni wapi, jibu lake ni nina kazi nyingi, kuna usemi usemao liziki ya mbwa iko kwenye nyayo nikaona ya kaz gan kupata bikra ya ukubwani na kuugua chekelea!, nikabadili life style nikawa naoga vizuri, navaa vizuri, nakula kwa wakat, nikaanza na kibiashara cha kupotezea mawazo, Mungu mwema akaniletea na mbaba wa makamo tu 40years.

Nilivyokuwa mbili kasoro nikamdanganya sijaolewa nalea watoto mwenyewe, nikaingia nae kwenye mahusiano, nikaacha kabisa kumsumbua mume wangu, nikaamua kumuacha afanye kazi zake kwa uhuru bila kumuomba aje nyumbani nimemmiss, toka niache kumsumbua baba watoto wangu akabadilika sana akawa mtu sasa wakuja nyumbani na kukaa mwezi, yaan wakati namhitaji alikuwa shingo juu juu k**a kangaroo, mie huyo na penzika jaman na mme wa mwenzangu kwa raha zangu eti na yeye anajirudi!๐Ÿ˜“

Baba huyu ni romantic haki ya mama, ngoja niende kwenye point embu nipostie wanipe japo ka ushauri, je wamama wenye michepuko yenu mnawezaje kugawa upendo maana mimi sina hamu kabisa kwa sasa na mme wangu, imagine akinihitaji yaani tu pumzi yake kwenye kifua changu nahis k**a mbwa amenidandia๐Ÿ˜“
akigusa nyonyo nyie nyie kwanza nausikia mdomo k**a sijui ananuka hivi, halafu domo la moto sana nasikia k**a naungua, zaid ya hapo inabidi nijikaze k**a naendesha baiskel kwenye kilima kirefu, najisikia vibaya sana kukutana nae kimwili sijui nitaishije jamani ๐Ÿ™†โ€โ™‚๏ธ, nishaurini nasoma comment

05/09/2025

JINSI YA KUJITIBU JINI MAHABA KWA MAJANI YA MUHOGO PART 2

Sikiliza mwanzo mpaka mwisho usiruke ukaja kuchanganya mambo.

Hii ndio sadaka yangu ya leo.๐Ÿ™

05/09/2025

Wanawake mtuambie...
Hivi mnapotoka ku-cheat huwa mnawatazamaje waume zenu? Na moyoni amani inakuwepo kabisa au?!

05/09/2025

Ni vita kubwa kumuondoa jini mahaba kwenye maisha yako, Usifanye mzaha na huyu jini, atakuharibia maisha yako vibaya mno, utaishi kwenye misukosuko na mateso ya kila aina, utatamani mpaka kujiua maana vifungo utakavyofungwa hakuna wa kuweza kuvifungua mpaka nafsi yako iwe na utayari wa 100%.

Sikiliza kwa makini ni jinsi gani utatumia mti wa muhogo kumuondoa.๐Ÿ™
Ukiwa na haraka za kupeleka mbele video usinilaumu baadae.

Hakuna kitakachokuponya isipokuwa imani yako thabiti.
Omba sana, sali sana, tumia dawa, atakimbia mwenyewe, na Mungu ndiye.mjuzi zaidi๐Ÿ™

PART 2 imeshapostiwa na nimeeleza kila kitu.

05/09/2025

Dalili zinazoonesha kuwa kuna wanga wanakuwinda wakufanye msukule, fanya hivi kujinasua.

(Nimetumiwa sms na mtu aliyejiita mchawi sijui kweli sijui si kweli atajua mwenyewe. Kikubwa mimi natoa msaada, natoa sadaka najua nitapata ujira wangu kwa aliye juu, sitishiki na binaadamu yeyote aliyejipa mamlaka.)

Tunaendelea na darasa la mti wa muhogo....
Next video itahusu jinsi gani utumie mti huu kujitibia JINI MAHABA. Asanteni sana๐Ÿ™

Kuna kaka ambaye pale nyumbani kwetu shangazi yake ni jirani yetu, hivyo alikuwaga anaishi kwa shangazi yake, nilimfaham...
05/09/2025

Kuna kaka ambaye pale nyumbani kwetu shangazi yake ni jirani yetu, hivyo alikuwaga anaishi kwa shangazi yake, nilimfahamu kwa kumuona pale kwa shangazi yake, alikuwa mkubwa mimi mdogo hivyo alikuwa ananifundisha masomo ya sayansi mimi na binamu zake, baadae tukawa na mazoea nikawa namuita kaka k**a binamu zake, kwakweli tangu nianze kuwajua wanaume sijawahi kuona mwanaume ambaye ana nidhamu k**a yule, hakuwahi kunitongoza alinichukulia k**a mdogo wake na mimi nilimpenda kwa hilo nikamuheshimu sana na kumchukulia k**a kaka yangu.

Baadae aliondokaga maana alikuwa mwalimu wa kujitolea katika shule moja, hivyo akaenda kujiendeleza, alikaa huko na mimi nik**aliza shule nikaendelea na mengine, inshort tulipotezana.
Sasa kumbe alifanya kazi nyingi Dar za kuajiriwa mwisho akaajiriwa na kampuni kubwa, na kupitia kampuni hiyo maisha yake yakabadirika sana, akawa tajiri japo sio sana kabisa, alifungua kampuni yake akawa kila anayemuweka anamuharibia kazi zake, akaanza kunitafuta mimi, maana tabia zangu huwa ni uaminifu, upole, usikivu na pia nina akili sana za kuchangaanua mambo (kwa maelezo yake) hilo ndio lilimvutia sana kwangu mpaka akaanza kunitafuta nikae kwenye biashara zake, pia alikuwa anajua niko wapi na nafanya nini kutokana na story alizopewa na mmoja wa binamu zake ambaye ni rafiki yangu.

Alifanikiwa kunipata na kunieleza kila kitu kuhusu kampuni yake, maelezo aliyonipa yalinivutia maana yalikuwa yamenyooka na nikaona nikienda kufanya hiyo kazi nitafanikiwa, mimi nikaenda na kweli nilifanya kazi kwa moyo mmoja, niliogopa kuchukua hata shilingi mia tu, nilikuwa na uamimifu wangu k**a kawaida maana kingine ni mtu wa dini sana so naogopa dhambi, nilimsaidia kukamilisha dili zake nyingi ambazo zilikuwa zimekwama mpaka akanipa zawadi ya bajaji, alininunulia bajaji mpya nikampa kijana awe anaendesha alete hesabu kila siku.

Siku moja akaniambia niende kumuelekeza kitu mke wake ambaye yeye anafanya biashara fulani, nikaenda, lengo kumuelekeza ili kuongeza ufanisi wa kazi yake kwa mafanikio zaidi, nilipofika pale nilimweleza yote ambayo mume wake amesema lakini cha ajabu alinambia "ishia hapo hapo, sitaki kusikia huo ujinga wenu, k**a ni kuelekeza nenda mkaelekezane huko huko" khaa! Nikashangaa! Kwani nini shida wifi yangu, akasema nimemaliza we ondoka, nikaenda kumwambia kaka majibu yote niliyopewa na wifi.
Kaka akasema achana nae huyo hajitambui.

Nikaendelea na kazi, ikafika hatua akafungua ofisi nyingine mkoa mwingine, ambapo huo mkoa na yeye alihamishiwa kazi huko huko, so akawa na ofisi mbili, akasema niende kwenye ile ofisi mpya kwasababu mimi ni mzoefu nikaiinue, na hii ya zamani tuweke msimamizi mwingine, nikakubali, lakini akaniambia nitafikia kwake, yote nikakubali, sasa nina miezi mitatu niko hapa kwake cha moto nakiona, yaani utadhani nimekaa hapa miaka 10.

Mke wake ananitukana sana, nikiamka asubuhi ananitukana, nikitoka chooni anaingia kuweka uchafu halafu anatoka nje kuja kusema mimi ndio nimeweka uchafu, muda wa kula kuna vyakula ananizuia nisile anasema ni kwa ajili yake na wanae, mfano kuna nililala saa 8 usiku maana kaka hakuwepo alisafiri kidogo, muda wa kulala ulivyofika nilienda chumbani kwangu nikakuta pamefungwa, nauliza nani kafunga na funguo ziko wapi hakuna aliyejibu, wote walikaa kimya hadi wadada wa kazi, nikaishiwa pozi nikarudi sebuleni kukaa, mida ya saa 7 k**a na nusu akapita mdada wa kazi ndio akanionesha ilipo tena kwa kunyata na kisha akakimbia asikutwe.

Nilitafakari nikaona hapa sio bora niondoke, nikampigia simu kaka hakupokea usiku huo, ila asubuhi k**a saa 1 akanitafuta, nikamuelezea yote na nikamwambia nataka nihame hapa nikaishi kwingine, nipange kwangu, akasema subiri mpaka nirudi, nikavumilia, tena naamka asubuhi mapema naenda kazini narudi jioni kabisa lakini bado mwanamke huyu anakuwa mkorofi kwangu, Kaka alivyorudi hakuweza kumuuliza kitu mke wake maana anamuogopa sana, ni mwanaume mpole sana na mwanamke ni mcharuko, anampelekesha mpaka najiuliza hivi huyu ni mwanaume kamili kabisa!

Kaka anatukanwa huyu ๐Ÿค”, anaambiwa matusi mazito mazito, kuna siku nimesikia anamwamnia "wewe na mbwa tofauti yenu ni kutembea, huko kazini wewe ni boss ila hapa nyumbani ni mbwa k**a mbwa zingine, kwanza kwa lipi nikunyenyekee kwani unakunya moto?"
Nilishangaa sana ila sikuwa na la kusema, kaka anajiinamia tu k**a kondoo anatikisa kichwa.
Ilifika muda akanitafutia nyumba nikahama pale kwake, cha ajabu mke wake ametuma watu waje wanifanyie fujo hapa ninapokaa, nikawauliza kwani kosa langu ni nini? Wakaniambia anasema umekaa kiwiziwizi utamuibia mume wake kwahiyo hakutaki, acha kazi ondoka kwenu.
Kwakweli niliona k**a amejipanga na ana dhamira ya kunidhuru pasipo kosa lolote.
Nikamwambia kaka acha mi niache hii kazi naona imeingiliana na mambo ya kifamilia, imeshakuwa ngumu sana.

Akaniambi kwa gharama yoyote ile nisiache kazi, "akaniambia wewe ndio sababu mpaka sasa niko mzima sijachanganyikiwa, sina mtu wa kuongea nae magumu ninayopitia kwenye maisha yangu, sina wazazi labda ningeongea nao, wanaume wenzangu siwezi waambia naogopa fedheha, ninapoona kuna mtu yupo karibu mwenye moyo k**a wako nafarijika na kuendelea kuvumilia, naamini ni mapito ipo siku Mungu atanipa jibu la swali langu.
K**a unavyoona nyumbani nateswa sana, nimekuwa k**a mfungwa huru, natukanwa k**a mtoto mdogo, sina sauti, kila kitu anapanga yule mwanamke, napitia wakati mgumu sana ila nikiangalia wanangu napata faraja pia maana nawapenda sana,
Naomba usiondoke maana kazi zikifa ndio nitapitishwa mpaka kisu cha moto mgongoni."
Nilishindwa kumwambia lolote nikayamezea moyoni, nikishangaa ni mwanaume wa namna gani. Ila nikamwambia siwezi nataka nikapate changamoto mpya sehemu nyingine.

Nimemwambia naondoka jumatatu, bado ananisihi nisiondoke, na tangia jana hayuko sawa, hata kula hali, mke wake anamwambia ukisusa sie twala, hana hata muda wa kumuuliza anapitia changamoto gani, daah hizi ndio ni balaa, sasa nikimtazama najikuta namuonea huruma kweli ๐Ÿ˜ญ,
Sijui nifanyeje nafsi inaniuma ๐Ÿ˜”, ni mtu mwema sana masikini ila mke wake sasa ๐Ÿ™Œ.

04/09/2025

Ulishawahi kuonewa wivu na mtu uliye msaidia..? Ilikuwaje!

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Naturalist posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Naturalist:

Share