05/09/2025
Kuna kaka ambaye pale nyumbani kwetu shangazi yake ni jirani yetu, hivyo alikuwaga anaishi kwa shangazi yake, nilimfahamu kwa kumuona pale kwa shangazi yake, alikuwa mkubwa mimi mdogo hivyo alikuwa ananifundisha masomo ya sayansi mimi na binamu zake, baadae tukawa na mazoea nikawa namuita kaka k**a binamu zake, kwakweli tangu nianze kuwajua wanaume sijawahi kuona mwanaume ambaye ana nidhamu k**a yule, hakuwahi kunitongoza alinichukulia k**a mdogo wake na mimi nilimpenda kwa hilo nikamuheshimu sana na kumchukulia k**a kaka yangu.
Baadae aliondokaga maana alikuwa mwalimu wa kujitolea katika shule moja, hivyo akaenda kujiendeleza, alikaa huko na mimi nik**aliza shule nikaendelea na mengine, inshort tulipotezana.
Sasa kumbe alifanya kazi nyingi Dar za kuajiriwa mwisho akaajiriwa na kampuni kubwa, na kupitia kampuni hiyo maisha yake yakabadirika sana, akawa tajiri japo sio sana kabisa, alifungua kampuni yake akawa kila anayemuweka anamuharibia kazi zake, akaanza kunitafuta mimi, maana tabia zangu huwa ni uaminifu, upole, usikivu na pia nina akili sana za kuchangaanua mambo (kwa maelezo yake) hilo ndio lilimvutia sana kwangu mpaka akaanza kunitafuta nikae kwenye biashara zake, pia alikuwa anajua niko wapi na nafanya nini kutokana na story alizopewa na mmoja wa binamu zake ambaye ni rafiki yangu.
Alifanikiwa kunipata na kunieleza kila kitu kuhusu kampuni yake, maelezo aliyonipa yalinivutia maana yalikuwa yamenyooka na nikaona nikienda kufanya hiyo kazi nitafanikiwa, mimi nikaenda na kweli nilifanya kazi kwa moyo mmoja, niliogopa kuchukua hata shilingi mia tu, nilikuwa na uamimifu wangu k**a kawaida maana kingine ni mtu wa dini sana so naogopa dhambi, nilimsaidia kukamilisha dili zake nyingi ambazo zilikuwa zimekwama mpaka akanipa zawadi ya bajaji, alininunulia bajaji mpya nikampa kijana awe anaendesha alete hesabu kila siku.
Siku moja akaniambia niende kumuelekeza kitu mke wake ambaye yeye anafanya biashara fulani, nikaenda, lengo kumuelekeza ili kuongeza ufanisi wa kazi yake kwa mafanikio zaidi, nilipofika pale nilimweleza yote ambayo mume wake amesema lakini cha ajabu alinambia "ishia hapo hapo, sitaki kusikia huo ujinga wenu, k**a ni kuelekeza nenda mkaelekezane huko huko" khaa! Nikashangaa! Kwani nini shida wifi yangu, akasema nimemaliza we ondoka, nikaenda kumwambia kaka majibu yote niliyopewa na wifi.
Kaka akasema achana nae huyo hajitambui.
Nikaendelea na kazi, ikafika hatua akafungua ofisi nyingine mkoa mwingine, ambapo huo mkoa na yeye alihamishiwa kazi huko huko, so akawa na ofisi mbili, akasema niende kwenye ile ofisi mpya kwasababu mimi ni mzoefu nikaiinue, na hii ya zamani tuweke msimamizi mwingine, nikakubali, lakini akaniambia nitafikia kwake, yote nikakubali, sasa nina miezi mitatu niko hapa kwake cha moto nakiona, yaani utadhani nimekaa hapa miaka 10.
Mke wake ananitukana sana, nikiamka asubuhi ananitukana, nikitoka chooni anaingia kuweka uchafu halafu anatoka nje kuja kusema mimi ndio nimeweka uchafu, muda wa kula kuna vyakula ananizuia nisile anasema ni kwa ajili yake na wanae, mfano kuna nililala saa 8 usiku maana kaka hakuwepo alisafiri kidogo, muda wa kulala ulivyofika nilienda chumbani kwangu nikakuta pamefungwa, nauliza nani kafunga na funguo ziko wapi hakuna aliyejibu, wote walikaa kimya hadi wadada wa kazi, nikaishiwa pozi nikarudi sebuleni kukaa, mida ya saa 7 k**a na nusu akapita mdada wa kazi ndio akanionesha ilipo tena kwa kunyata na kisha akakimbia asikutwe.
Nilitafakari nikaona hapa sio bora niondoke, nikampigia simu kaka hakupokea usiku huo, ila asubuhi k**a saa 1 akanitafuta, nikamuelezea yote na nikamwambia nataka nihame hapa nikaishi kwingine, nipange kwangu, akasema subiri mpaka nirudi, nikavumilia, tena naamka asubuhi mapema naenda kazini narudi jioni kabisa lakini bado mwanamke huyu anakuwa mkorofi kwangu, Kaka alivyorudi hakuweza kumuuliza kitu mke wake maana anamuogopa sana, ni mwanaume mpole sana na mwanamke ni mcharuko, anampelekesha mpaka najiuliza hivi huyu ni mwanaume kamili kabisa!
Kaka anatukanwa huyu ๐ค, anaambiwa matusi mazito mazito, kuna siku nimesikia anamwamnia "wewe na mbwa tofauti yenu ni kutembea, huko kazini wewe ni boss ila hapa nyumbani ni mbwa k**a mbwa zingine, kwanza kwa lipi nikunyenyekee kwani unakunya moto?"
Nilishangaa sana ila sikuwa na la kusema, kaka anajiinamia tu k**a kondoo anatikisa kichwa.
Ilifika muda akanitafutia nyumba nikahama pale kwake, cha ajabu mke wake ametuma watu waje wanifanyie fujo hapa ninapokaa, nikawauliza kwani kosa langu ni nini? Wakaniambia anasema umekaa kiwiziwizi utamuibia mume wake kwahiyo hakutaki, acha kazi ondoka kwenu.
Kwakweli niliona k**a amejipanga na ana dhamira ya kunidhuru pasipo kosa lolote.
Nikamwambia kaka acha mi niache hii kazi naona imeingiliana na mambo ya kifamilia, imeshakuwa ngumu sana.
Akaniambi kwa gharama yoyote ile nisiache kazi, "akaniambia wewe ndio sababu mpaka sasa niko mzima sijachanganyikiwa, sina mtu wa kuongea nae magumu ninayopitia kwenye maisha yangu, sina wazazi labda ningeongea nao, wanaume wenzangu siwezi waambia naogopa fedheha, ninapoona kuna mtu yupo karibu mwenye moyo k**a wako nafarijika na kuendelea kuvumilia, naamini ni mapito ipo siku Mungu atanipa jibu la swali langu.
K**a unavyoona nyumbani nateswa sana, nimekuwa k**a mfungwa huru, natukanwa k**a mtoto mdogo, sina sauti, kila kitu anapanga yule mwanamke, napitia wakati mgumu sana ila nikiangalia wanangu napata faraja pia maana nawapenda sana,
Naomba usiondoke maana kazi zikifa ndio nitapitishwa mpaka kisu cha moto mgongoni."
Nilishindwa kumwambia lolote nikayamezea moyoni, nikishangaa ni mwanaume wa namna gani. Ila nikamwambia siwezi nataka nikapate changamoto mpya sehemu nyingine.
Nimemwambia naondoka jumatatu, bado ananisihi nisiondoke, na tangia jana hayuko sawa, hata kula hali, mke wake anamwambia ukisusa sie twala, hana hata muda wa kumuuliza anapitia changamoto gani, daah hizi ndio ni balaa, sasa nikimtazama najikuta namuonea huruma kweli ๐ญ,
Sijui nifanyeje nafsi inaniuma ๐, ni mtu mwema sana masikini ila mke wake sasa ๐.