Halisi Naturalist

Halisi Naturalist A safe space for real-life stories & community advice. 💡
💌 Send your story (anonymous), let’s learn and grow together. Be real, Be natural, Be positive.
(1)

Nina jamaa yangu ambaye tumeshibana sana, langu lake na lake ni langu, nilimwamini sana kiasi kwamba hata nikisafiri nam...
21/08/2025

Nina jamaa yangu ambaye tumeshibana sana, langu lake na lake ni langu, nilimwamini sana kiasi kwamba hata nikisafiri namwagiza aende nyumbani kwangu akaniangalizie mazingira, na likitokea tatizo mimi sipo namwagiza yeye analimaliza, hata mimi hivyo hivyo kwake.
Viashiria vilianza kwa mke wangu kumsifia sana jamaa, mara ooh ni mpole, anajitambua, na sifa kibao, mwanzo niliona kawaida ila kwa baadae nikaanza kuona k**a inazidi.

Baada ya muda mrefu kupita makucha yao yakaanza kujitokeza, jamaa yangu alikuwa anapenda kuja kwangu hata k**a hakuna inshu ya muhimu tuliyoongea, na akija tu mood ya mke wangu inabadirika, anaanza kuchangamka na kuongea vizuri, kucheka cheka sana, inshort anafurahia uwepo wa rafiki yangu.
Katika uchunguzi wangu wa kina nikagundua rafiki yangu anatembea na mke wangu, na pia nilishasikia tetesi kutoka kwa majirani.

Ikabidi nitenge muda nimuulize mmoja mmoja kwakweli wote walikataa, ikabidi niweke mtego, nikajifanya nimepata safari ya kikazi, nikamuomba rafiki yangu asikanyage kwangu kwani nina mashaka nae, niliongea kwa sauti ya utani "Wewe jamaa sitaki ukanyage kwangu huu muda ambao sipo nyumbani maana nina mashaka na wewe, nikirudi tutaongelea hili zaidi" akajifanya amenielewa, ushauri mwingi eti nijiamini niache dhana, n.k
Nikachukua Bag langu nikaondoka, nikaenda lodge fulani ambayo haiko mbali sana na nyumbani kwangu nikatulia hapo, mpaka saa 6 usiku ndio nikachukua uber nikarudi nyumbani, kumbuka nilimuaga wife nitakaa wiki moja.

Nilishuka kwenye gari nikanyata mpaka dirishani, dirisha la chumbani, maana nyumba yangu imekaa k**a L na dirisha limetazamana na barabara ya mtaa, nikasimama hapo muda mrefu, rafiki yangu hakuwa ndani ila mke wangu nilisikia alikuwa anaongea na simu kwa mahaba na mwanaume niliyehisi ni yule rafiki yangu japo sikuwa na uhakika, nikasikiliza machache k**a dakika 10, nikaondoka kurudi lodge.
Nikiwa njiani narudi kuna jirani yangu alinitumia sms "Babu jinga mali yako yaliwa" ikabidi nimpigie, hakufunguka sana akasema we tumia akili, nikamwambia nipe code japo kidogo akasema we tuma mtu unaye muamini aje kwako hapa mengine hayanihusu.
Ikabidi nirudi, safari hii niliingia moja kwa moja na nilipogonga mlango kwa nguvu, mke wangu alikuja na jazba, we nani unagonga mlango hivyo usiku watu wamepumzika? Nikabadili sauti na kujifanya wa k**e, nikasema "Ni mimi", nilijua hatanitambua ila atleast asijue k**a ni mimi mume wake.

Akafungua mlango nikazama ndani na mlango kwa kusukuma kwa nguvu na yeye akaangukia ndani, sikuamini nilichokiona, kumbe muda ule natoka baada ya kusikilizia dirishani jamaa alikuwa njiani anaelekea kwangu, na muda naingia ndani alikuwa sebuleni amevaa taulo yuko anakula, halafu alivyokuwa fala eti anavaa taulo yangu, aliponiona alihamaki sana, wote walihamaki na kuvurugwa sana, nilisimama mlangoni nikiwa nimeegemea mlango nawatazama, natetemeka kwa hasira ila najaribu kujituliza, nilikuwa nawaza mengi linatoka hili linaingia hili, je nimrukie shingoni ning'oe koromeo, nfate kisu, nichukue panga, nitoboe macho, yaani mawazo yalikuwa yanapishana, alipiga magoti jamaa yangu na kulia kwa hofu nimsamehe.

Sijui ilikuwaje, nikamwambia sintowafanya chochote ila beba huyo mwanamke uende ukaishi nae kwako, inaonekana mnapendana sana, kwahiyo ni vyema mkaishi pamoja, mimi simuhitaji naona hata yeye hanihitaji pia ndio maana yuko na wewe, sasa muondoke ili mume huru na mapenzi yenu halafu na mimi nitatafuta aliye na mapenzi na mimi.
Siwatanii niko serious, na endapo mtafata haya maelekezo basi nitawasamehe bila chembe ya kinyongo ila mkijaribu kuongeza neno k**a ''Nisamehe, sirudii tena, na misamaha yoyote mtanitibua tuingie kwenye vita kali ya mauwaji".
Wewe ni mwanaume k**a mimi sidhani k**a neno msamaha linaweza kufuta ukweli kuwa umemlala mke wangu, kwahiyo mi naona jambo jema huyo akawe mke wako wewe."

Walikaa kimya wamejiinamia, nikamwambia mke wangu, naomba usimame ukachukue kila kilicho chako sasa hivi, akawa anataka kuomba msamaha anakuja kunishika miguu nilimpiga teke la mdomo meno mawili ya juu yakaanguka hapo hapo, midamu hiyo ikamtoka na sikujali wala nini, nikamwambia rafiki yangu, wewe chumbani kwangu bila shaka unapajua, nyanyuka uende ukamsaidie mpenzi wako kukusanya matambala yake muondoke kwangu, tena fanyeni haraka, akasimama na kuanza kuelekea chumbani, mimi nikaingia chumba kingine kuchukua mazaga mengine ya mke wangu, rafiki yangu akaitumia k**a chance kukimbia, alipita pale mlangoni k**a radi, akakimbia.

Usiku ule sikumgusa mwanamke maana niliona naweza kumuua au kumdhuru kwa hasira nilizokuwa nazo, nikamtoa nje nikafunga mlango, alilala nje nadhani itakuwa jikoni, kesho yake niliita waungwana nikawaeleza, na tukapanga zoezi la kumpeleka mke wangu kwa yule jamaa, tuliita gari ikabeba mizigo, na yule mwananmke mpaka kwa jamaa yangu, sikumkuta alikuwepo mke wake, tukamueleza kila kitu mke wake, tukashusha mizigo na mke wangu tukamuacha pale sisi tukaondoka zetu.
Mke wa jamaa akaanza mara ooh haujafata taratibu ulitakiwa umrudishe kwao umpe talaka mbele ya washenga maana akiumia utaulizwa na maneno mengi, nikamwambia anayetakiwa kumpeleka kwao sio mimi ni mume wako ambaye ndiye mume wake pia, na kuhusu talaka wala asijali imeshapita hiyo, yeye k**a hajaridhika ndio afunge safari aende kwao akajieleze ilikuwaje sio mimi, kwanza huo muda sina.
Nilivyofika pale kwangu, nilifunga nyumba nikaondoka kwenda kwenye ile lodge na simu zote nikazima, baadae nikapata wazo nikasajili laini mpya nikawa nawasiliana na watu muhimu,
Nilikaa lodge wiki ikabidi nipange chumba sehemu, nikalipa kodi ya miezi mitatu, nikanunua godoro, na ndoo ya kuogea, nikaishi hapo, nilikuwa naenda kulala tu.

Sikutaka kutafutwa na msuruhishi yeyote wala kiongozi yeyote, nilitaka niwe huru, nipate muda wa ku heal, nipate muda wa kuwa peke yangu bila kuingiziwa virus zozote kichwani kuhusu yule mwananmke wala ndoa.
Ni siku moja tu nilifunga safari mpaka pale nikaenda kumchapa talaka yake, mi nikatembea.
Jamaa yangu alituma watu wengi sana waje kunitafuta kazini lakini kila aliyenieleza upuuzi wake nilimpa onyo kali sana asirudie.

Walihangaika kunitafuta bila mafanikio, hata wa kwetu hawakujua nipo wapi isipokuwa mama yangu tu, nae alinitunzia siri.
Mwisho yule mke wangu alimng'ang'ania jamaa yangu akasema haondoki na lazima atamuoa maana yeye ndiye kamvunjia ndoa yake, akamwambia njia pekee ya kutomuoa na kumtoa pale kwake ni kumuua tu basi.
Mke wa jamaa nae kikawaka ikabidi aondoke, wakabaki wasaliti wawili na wakaanza kuishi japo mwanzo waligombana ila mwisho wakaishi.

Nilirudi kwenye nyumba yangu nilipo karibia kuoa, na mwisho wa siku nikaoa, nikawa napata habari kuwa yule mke wangu haelewani na jamaa kila siku ni vita na makesi yasiyoisha, mwanamke akawa mkatili kwa watoto wa jamaa na kubwa zaidi alianza kumsaliti na wanaume wengine pasipo jamaa kujua, maana kazi zake za kusafiri, ni dereva wa halimashauri moja hivi hapa nchini.

Nasikia jamaa anajuta mno, na Mungu asivyo athumani mwanamke niliyenae sasa ana unafuu mkubwa sana kuliko yule, yule alikuwa na kamdomo sana, akifungulia mdomo wake unaweza sema ni zile speaker za club, alikuwa na makelele sana nilikuwa navumilia tu, k**a unavyojua wanaume asilimia 95 tusichokipenda kwa mwanamke ni makelele, dharau, so alikuwa ameshanikera sana sikuwa na jinsi tu, alikuwa na kiburi sana, kwakweli nashukuru ni k**a jamaa yangu alinisaidia kutoa bomu ndani ya nyumba yangu, yeye alijikuta mjanja kumbe bwege tu na sasa anajuta.

Binafsi nimejifunza kitu hapa 👏👏

(Tuma jambo lako inbox unalohitaji kushauriwa, au kushare, zingatia uandishi wako, kuhariri ni kazi sana makosa yakiwa mengi.🙏)

Samahani mimi nina shida, nina miaka 28, tangu nianze form two 2012 nilikuwa addicted kwenye uraibu wa kujichua na kuang...
21/08/2025

Samahani mimi nina shida, nina miaka 28, tangu nianze form two 2012 nilikuwa addicted kwenye uraibu wa kujichua na kuangalia picha chafu mwaka wa 13 huu na madhara yake yananitesa mno, nina uume mdogo sana nchi 3 ukisimama mwembamba nikitoa manii zinatoka hazina nguvu kabisa, nahitaji msaada kwa ndugu wasomaji wako, je dawa gani naweza tumia isiyo na madhara ya asili isitoke kwa waganga wa kienyeji, nateseka nahitaji kuwa katika mahusiano naogopa naitaji kuitwa baba pia.
Nisaidie naumia nakosa raha amani nashindwa kufanya chochote sababu nakosa umakini stress zinanifanya nazeeka, nilikuwa kijana mwenye muonekano mzuri sana ila maisha yamenipiga mpaka nahisi ni madhara ya nyeto na p**n.

Nilikuwa nashauriwa na jamaa zangu kuwa nikitafuta mwanamke bikra itakuwa sawa maana hajui chochote, lakini nimefeli licha ya kuwapata bikra k**a wawili, inchi 3 ni ndogo sana bro hata k**a ni bikra kuna namna anakuwa anafeel kutotoshelezwa kwenye tendo, mfano kuna mmoja nilikuwa nae mimi ndio nimemuanza, alikuwa mdogo kabisa hata kumvunja ile bikra ilikuwa ni mtihani mzito sana kwangu, pili kwa baadae alianza kuniambia hasikii furaha na kuniuliza mbona picha anazoziona mitandaoni za wanaume maumbile yao ni tofauti na mimi, alianza mpaka kunilinganisha na watoto anao waogeshaga kwao, lile jambo liliniuma sana kiasi kwamba nikakata tamaa, hata vile nilivyokuwa najitahidi nikiwa nae nikajikuta nashindwa kabisa.

Naombeni msaada jamani, maana nateseka, juwe> amini sina demu naogopa aibu, natamani na mimi niwe na demu nioe niwe na watoto, hata nguvu zenyewe ni k**a sina sasa sijui ni kutokana na hofu au ndio hilo tatizo.

(You can share this information to others but without editing and putting your name. This information has been copy righted under Halisi Naturalist, any form of plagiarism or data manipulation will be regarded as an offence.)

Mumi ni mwanamke wa miaka 35 sasa, nilikuwa na mpenzi wangu tukiwa kijijini naweza sema ndiye alikuwa mchumba wangu tuli...
20/08/2025

Mumi ni mwanamke wa miaka 35 sasa, nilikuwa na mpenzi wangu tukiwa kijijini naweza sema ndiye alikuwa mchumba wangu tuliopanga kuoana. Niliamini kwa silimia 100 kuwa yule ndiye atakuwa mume wangu, nilikuwa nampenda sana, na daima nilijitunza kwa ajili yake ili atakavyo nioa anikute bikra iwe heshima kwangu na kwake pia.
Nilitongozwa na watu wengi lakini moyo wangu niliufunga na kufuli zito sana, kila nilichofanya nilitanguliza maslahi ya maisha yetu ya baadae.
Rafiki zake walimshauri alale na mimi anitoe bikra kwamba ndio sintomsahau pia wakamwambia asipolala na mimi wengine watalala na mimi, yote hayo aliniambia na nikamwambia hakuna kitu k**a hicho, mimi najitambua na nimeshaamua kukuchagua wewe, siwezi kurudi nyuma kwasababu yoyote ile.

Tulipomaliza form four nilimwambia tuoane lakini alikataa, akasema kwakuwa yeye amefaulu lazima asome ili maisha yetu yawe mazuri baadae, nilifurahi sana kwa akili yake hiyo niliona ni mtu mwenye future na nikazidisha upendo na kujiamini kuwa niko sehemu salama.
Hata mimi darasani nilikuwa naakili sana, katika wanafunzi wa k**e nilikuwa eidha wa kwanza au wa pili ila cha ajabu mtihani wa form four wa mwisho nilifeli (kuna sababu kubwa ilifanya nifeli ipo siku ukiniruhusu nitakusimulia).
Basi yeye akaenda shule na mimi nilibaki kijijini, nikikataa wachumba wengi sana waliokuja kunioa, posa nyingi zilikataliwa, nikiwa namsubiri mchumba wangu tuliyeahidiana kuoana.

Kumbe mchumba wangu kwao hawakuwa na uwezo wa kumsomesha hivyo kuna mwanamke alimsomesha, huyo mwanamke sijui ilikuwaje kuwaje akamsomesha, ila ni wa huko huko mjini sio wa kijijini kwetu, mpenzi wangu hakuwahi kuniambia hapo kabla k**a anasomeshwa, lakini hata angeniambia nisingeweza kumsaidia maana hali ya kwetu k**a ya kwao tu.
Likizo alikuwa anakuja kijijini tunaongea na mambo yanaenda vizuri, lakini wakati wote huo alikuwa ananisisitiza nilale nae, nikawa namkatalia namwambia tusubiri ndoa, mwenzangu akawa hanielewi analazimisha mpaka tunagombana.
Likizo moja alikuja k**a baada ya siku mbili huyo mwanamke anayemsomesha na yeye akaja kijijini, kwakweli mchumba wangu alinitambulisha na kuniambia ni ndugu yake wa mjini, ila hakusema kuwa anamsomesha.

Kila siku nikipata muda nilikuwa naenda kumchotea maji mama yake, naosha vyombo, nafua nguo, n.k na kuna baadhi ya kazi alikuwa ananitafuta ili kuniagiza, inshort kwao walikuwa wananijua k**a mimi ni mchumba wa mtoto wao.
Miaka ilienda hajaja kijijini mpaka ak**aliza chuo na hatimaye kupata ajira, na mimi nilikuwa nafanya vikazi vya hapa na pale napata visenti vya matumizi na kusaidia saidia nyumbani, mama yake hakuwa na shida hata tukikutana alikuwaga akiniuliza k**a nimeongea na mwanae, ananipa updates zote, alipokuja kijijini nilimuuliza kuhusu swala letu, akaniambia nisubiri bado anajipanga atanioa tu nisijali.
Lakini akaja kunitamkia maneno hayo 😓
"Siamini k**a wewe ni bikra, yaani miaka yote hiyo ujitunze eti mpaka ndoa kwanza, we utakuwa umeshatumika sasa unaogopa kunipa penzi lako ili nisigundue k**a umetumika nikaahirisha" kingine unatakiwa ujue mwanamke mwisho kusubiri mwanaume ni miaka mitatu tu, kwani umri kwa mwanamke ni kitu cha kuzingatia sana, sasa hivi ungekuwa na watoto wawili au watatu".

Nikamuuliza una maana gani kuniambia hivyo mbona k**a unanitukana bila kosa? Akasema am sorry k**a umechukia, yakaisha siku hiyo.
Kesho yake nikapigiwa na namba mpya, kumbe alikuwa yule dada aliyemsomesha, akaniambia mchumba wangu ni mume wake mtarajiwa na ndio maana alimsomesha, kwahiyo nikae pembeni makubwa yasije yakanikuta.
Nilichoka roho na mwili, hapo hapo nikamtafuta mchumba wangu kumuuliza, akasema puuza hizo taarifa sio za kweli.
Lakini nilikaa na mawazo sana, Kaka Halisi tambua kuwa wakati huo nilikuwa na miaka 28 na bikra kabisa, ni ngumu sana kuamini kwa dunia ya leo lakini ndio ukweli wenyewe sina sababu ya kudanganya, nilisemwa mengi sana wengine wakisema eti nina jini mahaba, wengine wakisema mie hanithi kwamba kitovu kiliangukia ukeni, wengine wakiniita majina ya ajabu, na wapo waliosema kuwa mpenzi wangu amenifunga kichawi.
Lakini hayo yote hayakuwa kweli, ilikuwa ni maamuzi yangu binafsi na nilifanikiwa kuidhibiti tamaa yangu, kingine kilichonisaidia ni ile hofu ya Mungu maana nimekuzwa katika maadili ya dini sana.

Muda ulizidi kwenda kunioa hanioi na sioni progress yoyote, kila nikimuuliza anakwepa kwa kuleta story nyingine, siku moja mama yake alikuja nyumbani na kuniambia kuwa mwanae hana mpango wa kunioa ananidanganya tu, "Nimeshamshauri sana akuoe lakini hanielewi analeta vijisababu ila nimegundua yule mwanamke wa mjini aliyemsomesha ndio anatembea nae na sio muda wanaweza kuoana wale, naumia sana binti yangu ila sina jinsi, maana watoto wa siku hizi hamuambiliki"
Kwa maelezo ya mama yake nilianza kuunganisha doti, nikagundua mchumba wangu ameshindwa kuniambia ukweli kwa aibu ila anatamani sana kuniambia. Nikamtafuta kumuuliza taarifa alizosema mama hakujibu kitu, yaani halisi ni aliganda kwenye simu k**a vile mtandao unasumbua, mwisho akasema nitakutafuta baadae akakata simu.

Kila nikimtafuta kumuuliza anafanya michezo hiyo hiyo, niliumia sana, jamani kumbe moyoni huwa kuna vidonda vinavyoletwa na mawazo? Nilikuwa naumia moyo hata upepo ukipita, halisi upepo ti.
Nikikohoa naumia, nikipiga chafya naumia, aisee k**a moyo haukutoboka kipindi kile hautakuja kutoboka tena, nilimaliza wiki silali usiku na mchana mpaka nikitazama kitu naona maluelue kwa kizunguzungu, nilikonda sana, niliharisha sana, nilikuwa k**a mdudu sijui mdudu gani 😭,
Nilijaribu njia za aina zote mpaka kukesha kwa mtumishi naombewa lakini wapi, nikaenda mpaka kwa mwamposa kuombewa nikae sawa lakini wapi. Na alipokuja kuweka chumvi kwenye kidonda ni pale aliponitamkia kwa kinywa chake kuwa "Nisamehe sana nimekupotezea muda ila naumia na najuta sana Mungu akusaidie upate mume mwema huwenda mimi sio mwema kwako na sio riziki yako, nachoweza kusema naomba uwe huru kuolewa kuanzia sasa" akakata simu na kutoa laini kabisa, nilipiga sana lakini sikuwahi kumpata tena.

Nilisemwa sana kijijini hasa wanaume nilio wakataa walininyima sana amani, niliamua kubeba vilago vyangu nikaenda Morogoro kwa shangazi yangu, nikahamia huko, shangazi alinisaidia sana tena sana maana ilibaki kidogo ninywe sumu, na hilo wazo nilikuwa nalo tangu niko kule nyumbani, alinisaidia kunituliza, na mama kila akipiga alinipa maneno ya faraja, mwaka ulivyoisha nilikuwa sawa kabisa, hata nilivyosikia ameoa sikushtuka nilisema tu "Alhamdulilah".
Nilitafutiwa kazi fulani nikawa nafanya na pale nyumbani palikuwa na bustani ya mboga mboga, zamu yangu ya kumwagilia ilikuwa jioni nikirudi hivyo nilikuwa busy na nilikuwa naenjoy.

Kuna mwanaume nilimpata, sababu ya kumuamini yule mwanaume na kuamua kuwa nae, alikuwa mtu wa dini sana, alikuwa na roho nzuri sana, alikuwa mtulivu mno yaani sio mtu wa mademu kabisa, uzuri wa bahati alikuwa anaishi hapo hapo kwa shangazi so mwenendo wake niliuona tangu nafika mazingira yale, na hata mtaani sifa zake njema nilizisikia kwa watu, watu waliposikia nipo nae walishangaa maana na yeye walisha muhisi vibaya kumbe katulia tu.
Tulipoanza mahusiano haikuchukua hata miezi 6 tukaoana, tulifunga ndoa na tukahamia dodoma, kwahiyo tunaishi dodoma sehemu moja wanapaita Nkuhungu.
Yule mchumba wangu wa zamani mwaka uliopita alienda nyumbani kwetu kunitafuta akamkuta dada yangu kule, akamuuliza mengi lakini dada yangu ni kauzu hakumweleza chochote kuhusu mimi alimwambia "Ungetaka kujua kuhusu yeye usingemfanyia ule ushetani, kwahiyo sitaki maswali".
X akamwambia dada mwambie mdogo wako namtafuta sana, na pia nisaidie kuniombea msamaha, k**a hajaolewa niko tayari kumuoa.
Dada alivyonipigia nilimwambia usirudie kumsikiliza tena huyo ibilisi, je ningejichanganya nikalala nae kipindi kile akanipa mimba kwa bahati mbaya sasa hivi siningekuwa naitwa single mother na maneno ya kejeli juu kutoka kwa wanaume!?.
Dada usimjibu tena na wala usinipe taarifa yake yoyote kuanzia sasa, yaani hata akifa sitaki kujua."

Basi kumbe mama yake ananyanyaswa na mke wake wake, nasikia haishi kunitaja mdomoni mwake, leo hii wananikumbuka baada ya kuniona wa nini, nashukuru Mungu kumpata mume wangu huyu, najiona mwenye bahati kuliko wanawaks wote, maana naposoma visa humu najiuliza ewe Mungu mimi nimekupa nini hata unibariki na mwana wako huyu! Hata tukilala njaa hata tukikosa nitaona kawaida as long as tunaamani.
Mume wangu sidhani k**a ni wa sayari hii na moja ya kitu najichunga nacho ni ulimi, sipendi kusema maisha yetu kwa majirani wala marafiki maana najua ni maisha ambayo kila mwanamke anayatamani hasa kwa kipindi hiki ambacho wengi wapo kwenye fasheni ya umalaya na usaliti so kwa kusema kwangu naweza kukaribisha fitina ndani.

Aisee kwa sasa anahangaika, nasikia ananilaumu sana huko kwanini nimeolewa, anasema kumbe sikumpenda niliigiza, k**a ningempenda nisingeolewa eti ndio maana baadhi wakifiwa na waume zao au wake huwa hawaoi tena, hao ndio wenye upendo, namuona k**a tahira, na vile habari zake nazisikia juu juu basi nachekaga tu.
Kutesa kwa zamu.

NB: Hiki kisa mdogo wako wa k**e au mwanao wanafaa sana kukisoma, usiache kuwatag, usione aibu, mimi naanza na Swaakid

HALISI, Mimi nilioa mwanamke tukafanikiwa kuzaa watoto watano, tumewalea mpaka wamekuwa na huyu wa mwisho kwa sasa yupo ...
20/08/2025

HALISI, Mimi nilioa mwanamke tukafanikiwa kuzaa watoto watano, tumewalea mpaka wamekuwa na huyu wa mwisho kwa sasa yupo darasa la 4, niliwahi kupata wazo la kuhama hapa ninapoishi na kubadirisha biashara, maana biashara zangu ilikuwa za msituni sasa changamoto huwa ni nyingi sana nikaona bora nibadirishe.
Huwa nafanya biashara za mbao na asali kwa vibali maalumu lakini licha ya kuwa na vibali bado changamoto zipo za kutosha tu.

Kuna rafiki yangu yupo chalinze huko akawa ananishawishi nihamie huko na mimi nikaona ni sawa tu nikihama mkoa kutoka tabora kwenda huko, ikabidi nimshirikishe mke wangu, nikamwambia yote, lakini cha kushangaza mwenzangu alikataa katu katu na kuniona k**a nimevurugwa, nilijaribu kumuelewesha lakini wapi, yeye akawa anasema "ooh miaka yote tunalima mpunga, mahindi, maharage, karanga na tunapata mazao ya kutosha, tunauza kufanya maendeleo mengine na chakula kinabaki tele, hatujawahi kuhangaika chakula wala matumizi sasa kinachokukimbiza kwenda huko ni nini? Mara ooh je tukienda huko mambo yakawa tofauti na huku tulishapauza hawa watoto tutawaleaje na watarithi nini na unajua ni watoto wa kiume?" Actually watoto wangu wote ni wa kiume.

Nikamwambia mimi ni mwanaume siwezi kufeli kizembe k**a unavyodhani, mpaka kukwambia inamaana nimeshafanya utafiti wangu kwa kina, lakini aliendelea kunipinga, basi huo ukawa ndio ugomvi wetu ndani, maana kwenye hizi ndoa kwa stage niliyofikia mimi ya kuishi na mke miaka mingi na kuzaa watoto 5 hiyo ni stage kubwa sana so maamuzi lazima yahusike pande zote, ila ningekuwa nimeishi nae muda kidogo na mtoto mmoja wawili ningefata akili za vijana wa kisasa vijana wa 2000, 90, ambao huamua kuachana ila najua waliofika level yangu wanaelewa ugumu wa kufanya maamuzi hayo, wanajua nachokizungumzia, watoto wadogo hawawezi kunielewa na ndio hukimbilia kuachana mara nyingi.

Basi mimi niliendelea kutia presha kwake ili akubali, na rafiki yangu wa chalinze aliendelea kunitia moto niwahi kwenda huko, ilifikia hatua tukawa hatuelewani vizuri, basi yule mwanamke akaniambia anataka kwenda kwao kusalimia, kwakuwa huo ni utaratibu tumekuwa tukiufanya , maana kuna muda nasafiri mimi kwenda nyumbani, muda mwingine yeye anasafiri, basi nilimruhusu aende akasalimie.
Alienda na kuniambia atakaa wiki 2, nikashangaa mwezi umekata, kumpigia kumuuliza akaniambia mama yake ni mgonjwa na hakuna wa kumuangalia, mimi nikaona hii ndio chance acha niuze mashamba, viwanja, nyumba na kila kitu ili akirudi akute kila kitu tayari, nitatumia uanaume wangu kumtuliza na atatulia tu.

Nikaanza kutafuta wateja na nikawaambia rafiki zangu wanisaidie, wateja walikuwa wanakuja wakiangalia wanasema wanarudi lakini hawarudi, yaani wenye viwanja jirani yangu walikuwa wanauza eti mimi mwenye viwanja vizuri vipo sehemu nzuri ina maji ukichimba kisima nikawa sipati wateja, nilihangaika lakini sikuwahi kupata mteja hata mmoja, sio wa kiwanja, sio shamba, sio nyumba, sio pikipiki yaani mpaka nikashangaa kabisa.
Siku moja nimerudi nyumbani nikakuta mwanangu wa mwisho na yule wanaefatana hawapo, kuuliza naambiwa kuwa mama yao alikuja kuwachukua, kha! Nikabaki nashangaa tu, ikabidi nifunge safari kesho yake mpaka kwao, hapakuwa mbali ni kijiji jirani, nilipofika niliuliza ni kitu gani kimemtoa nyumbani ikiwa mimi sijamfukuza, mwanamke akasema amegundua mimi sijitambui kwahiyo ameniacha ili akili inikae sawa, na ikishakaa sawa atarudi.

Aloo ile ilikuwa dharau moja kubwa sana kwa upande wangu na hapo hapo nikajiapiza moyoni kuwa nitamkomesha huyu mwanamke.
Baadae nilirudi nyumbani ila wale watoto niliwaacha nikawaambia mkitaka kurudi nyumbani mnakaribishwa anytime, mkitaka kwenda kwa mama yenu mko huru, mke wangu alikuwa ananipigia simu kila siku ila kurudi nyumbani hataki, jambo ambalo lilikuwa linanishangaza.
Mpaka nikawa namuuliza wewe k**a umeona kwenu ndio bora kuliko kwako hizo simu ni za nini? Akawa ananiambia wewe ni mume wangu na baba wa watoto wangu lazima nikupigie kujua hali yako.
Nikaona analeta dharau, nikawa sipokei simu zake, ila swala la mimi kutafuta wateja sikumwambia.

Nikaanza kutafuta mke mwingine wa kuoa, ili nimuoee mke wa pili akili imkae sawa, kila mwanamke niliyempata kwa baadae naona hafai namuacha, au yeye anaweza kuniona simfai akaniacha, daah yaani ikawa mvurugano huku na kule, nakwambia sikufanikiwa kuoa mpaka yule mwanamke alivyorudi nyumbani.
Aliniambia neno likanitafakarisha wiki nzima "Najua huwezi kuuza chochote unahangaika bure tu"
Nikajiuliza amejuaje? Ameambiwa na nani? Nikamuweka chini kumuhoji alikuwa akinicheka kwa dharau tu, akaongeza "kuuza huwezi, kuoa huwezi, we fanya kazi za maana acha kufanya kazi zisizo na faida".
Kengele ikagonga kichwani ndeeeen nikajua hapa kuna kitu.
Nikajua kwa vyovyote vile ushirikina umetumika.

Nikamsimulia jamaa yangu mmoja akanipeleka kwa mganga, mganga huyo akasema mke wako amekufunga usioe, na amekufunga usiweze kuuza kitu chochote, na amefanya yote hayo sio kwasababu anataka mali sana bali kwa ajili ya watoto wenu, analinda urithi wa watoto.
Nilikasilika sana nikamuomba we nifungue haijalishi nia yake mi sijali, mali nilitafuta mimi sikupewa na baba yangu na wao watatafuta za kwao, hilo ni jasho langu, nikijisikia nitawapa nisipojisikia siwapi maana hata mimi hakuna aliyenipa bali nilisota mwenyewe so sitaki kupangiwa kwenye jasho langu.
Wale wateja baadhi waliojikata wakaanza kuniuliza k**a nilishauza, mwanamke kusikia hivyo alianza
Kuvurugwa sana, mpaka ikafikia hatua akaanza kukimbilia kwenye sheria.
Alivyoenda kwenye sheria nilisitisha kwanza ili nione hali inaendaje.
Ndani ugomvi ukazidi nikaamua nitafuta mchepuko wa kunituliza kichwa, kwakuwa ni bingwa wa kunifatilia aligundua hilo mapema tu, alivyoona hivyo akaanza kuwalisha sumu watoto wangu, kuwa nataka kuuza pote wasipate chochote kwamba akili yangu yote ipo kwa mchepuko wangu sio wao tena, nikawa naona mapokezi tofauti ya watoto, wananitazama tofauti kiasi kwamba nagundua kuwa wananichukia, kwanza nikiwa nyumbani sio k**a zamani hata kukaa na mimi tuongee hawataki tena. K**a huyu mkubwa aliwahi kunitajia jina la mchepuko wangu "Baba mtaani wananitania kuwa fulani ni mama mdogo wangu, sijui ni kweli?" mpaka nilijisikia vibaya sana na kuona mke wangu hatendi jambo jema kuwaingiza watoto kwenye mambo yetu.

Sasa nauliza nashtakiwa kwa lipi, hapo kosa langu ni nini? Mali ni zangu, mke ni wangu na mimi ndio namiliki familia, kuna ubaya gani nikipanga mipango yangu iwe ni kuuza mali zangu mwenyewe au laa? Maana nilitumia uugwana na taratibu za ndoa mwenzangu hakunielewa, na lengo langu lilikuwa kuhama mkoa tukafanye maish pengine, kwahiyo niendelee kutii sheria zake wakati mimi ndio mwanaume na ndio mwenye mali, nimezitafuta mwenyewe sikurithi popote.
Na je huko kwenye sheria anaweza kushinda au laa? Maana sielewi kabisa, naombeni ushauri nifanye maamuzi gani?

Mtaani kwetu kuna familia mama ana urafiki nao, inshort mama ambaye ndio mji kwenye hiyo familia ni rafiki wa mama yangu...
19/08/2025

Mtaani kwetu kuna familia mama ana urafiki nao, inshort mama ambaye ndio mji kwenye hiyo familia ni rafiki wa mama yangu, sasa yule mama ana mtoto wake ambaye alikuwa ameolewa huko Mwanza na akafanikiwa kuzaa watoto wanne, isivyo bahati huyo dada aliachika kwa mume wake kwahiyo hivi sasa naongea na wewe yuko kwao hapo.

Kuna siku mama aliniambia ana jambo la muhimu anataka kuongea na mimi, ikabidi nikamsikilize, jambo lenyewe aliniambia kuwa "Mwanangu wewe kwa sasa umekuwa sana tu lakini nashangaa mpaka sasa haujaoa sijajua nini shida, tuyaache hayo mimi nataka umuoe yule mama fulani", akimaanisha yule aliye achika yuko kwao.
Nikamuuliza ni kitu gani kimekufanya uniambie nimuoe yule dada mwenye watoto wanne na ameachika wakati unajua fika mimi sina mtoto na sijawahi kuoa! Hivi unakisikia unachoongea? Akaniambia hilo ni jambo la kawaida, wameoa mitume watu wanawazidi we nani?! Nikashtuka na kujiuliza hivi ananipima au yuko serious.
Akaniambia unatakiwa umuoe k**a inshu ni watoto tutalea, mimi ni mama yako nina maana kubwa ambayo wewe huwezi kujua na siwezi kukutakia mabaya bali mema,
Nilimuomba aniambie hiyo maana yake hakutaka kuniambia.
Mimi nikafupisha tu, "Huyo mwanamke simuoi na sitaki unieleze tena chochote kuhusu yeye" ameachika we unajua kilichomfanya aachike? Akajibu kuachika yeye ndio wa kwanza? Mbona wanaachika wenye makosa na wasio na makosa kila siku! Ni mambo ya kawaida hayo kwa kizazi cha sasa.

Sikutaka kujibizana nae sana, nikaaga nikaondoka, basi siku zilizoendelea, meseji, simu anazopiga ni kuhusu mimi kumuoa huyo mwanamke, kila muda namkatalia lakini hanielewi.
Nikaona hapa dawa ni kutafuta mwanamke wa kuoa, mademu niliokuwa nae hakuna hata mmoja niliyeona anafaa kuolewa na mimi, ikabidi niende kwa mjomba huko ifakara ndani ndani nikamueleza jambo langu akanitafutia binti mzuri sana na mwenye heshima, maana anaijua familia yao nje ndani, nikaenda nyumbani kuongea na wazazi na picha niliwaonesha, ila cha kushangaza walikataa katu katu wakasema mwanamke anayenifaa ni yule mama.
Aloo hili jambo lilinishtua kiasi kwamba nikaanza kuwahisi vibaya wazazi wangu, najua wamenilea vizuri ila sasa mmmh wanasema moyo wa binaadamu ni kichaka 😔.
Yule binti alikuwa ananipa presha ili kuona jambo la ndoa linaisha k**a nilivyomuahidi alivyoona nasua sua alinipiga chini na mpaka sasa ameshaolewa huko Zanzibar, niliumia sana maana alikuwa mwanamke kweli kweli, yaani ukisikia mwanamke Bro yule alikuwa mwanamke, amelelewa maadili ya dini na ana heshima kubwa mno ila kizembe tu nimempoteza.

Kilichoniponza kikubwa licha ya ruhusa ya wazazi ni uchumi wangu, maana nilitegemea mzee ndio anilipie mahari 😓 daah, siku moja mimi nilimfata yule dada wanaetaka nimuoe na nikamuomba tuongee wawili, nilimuuliza kwanini wazazi wangu wanalazimisha nikuoe una kitu gani cha special ambacho umewadanganyia na kuwazuzua kiasi hicho? Akasema hata mimi sikujua k**a kuna huo mpango ndio nimesikia kwako, akaapa viapo vyake vyote ikabidi niondoke zangu.
Wazazi nimewaambia mimi yule dada simtaki, sio kisa kuachika wala watoto ila simtaki tu, yaani simpendi na sina hisia nae, wakaniambia ukimuoa utampenda na utakuwa na hisia nae.
Mpaka hapa sielewi cha kufanya, sijui niwakatae mazima nihame mkoa, sijui nifanye nini, hebu naombeni mawazo mapya wakuu.

Halisi fanya kushare hiki kisa changu na mimi nishauriwe but sorry k**a kuna makosa ya kiuandishi 🙏

(You can share this information to others but without editing and putting your name. This information has been copy righted under Halisi Naturalist, any form of plagiarism or data manipulation will be regarded as an offence.)

K**A MWANAUME: ADUI MKUBWA WA MWANAUME YUPO KATIKATI YA MAPAJA YA MWANAMKE.Katika safari ya mwanaume kuelekea mafanikio,...
19/08/2025

K**A MWANAUME: ADUI MKUBWA WA MWANAUME YUPO KATIKATI YA MAPAJA YA MWANAMKE.

Katika safari ya mwanaume kuelekea mafanikio, adui wa kwanza na wa hatari zaidi sio mtu fulani asiye kupenda, sio adui wa kibiashara, sio mfumo wa kijamii au serikali, bali ni TAMAA YA NGONO.
Kwa sababu tamaa hii ni k**a moto, endapo utafanikiwa kuitawala basi moto huo unaweza kuleta nuru na joto la kukufaa kwenye maisha, lakini huo moto ukiachwa bila mipaka unaweza kuchoma na kuteketeza ndoto, malengo na heshima yako k**a mwanaume.

Nguvu ya kiungo kilichomo ndani ya suruali yako inaweza kukufanya uwe kipofu k**a Samsoni, ambaye nguvu zake zote zilitoweka kwa sababu ya tamaa kwa Delila.
Vilevile, ujinga wa tamaa uliofichwa katikati ya mapaja unaweza kukufanya ulie na kuomboleza k**a Mfalme Daudi aliyepoteza amani kwa muda kwa kosa la tamaa.
Hekima ya Kichina inasema: “Yule anayeshinda tamaa zake mwenyewe ni shujaa kuliko yule anayeshinda maelfu vitani.”
Kwa hiyo mwanaume halisi si yule aliye na misuli mikubwa, bali ni yule aliye na udhibiti wa nafsi yake.

Mimi Halisi Naturalist nimewahi kufanya challenge ya kukaa mwaka mzima bila s*x kila baada ya miaka minne kupita na nilipata matokeo chanya sana ambayo mpaka leo nafaidika nayo.
Je, wewe unaweza kuishi mwaka mmoja mzima bila kufanya ngono, ili kujaribu udhibiti wa tamaa zako?
Biblia inasema: “Kimbieni zinaa. Kila dhambi iletwayo na mwanadamu ni nje ya mwili; bali aziniye hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.” (1 Wakorintho 6:18) hivi huu msitari unauelewaje, yaani bro kila dhambi ni nje ya mwili ila ngono tu ndio juu ya mwili wako mwenyewe? Imagine, najua hatuwezi kuwa watakatifu japa tunaongelea Logic, kwahiyo ni ushahidi tosha kwamba ngono inatumaliza sana wanaume.
Qur’an nayo inakataza wazi: “Wala msikaribie zinaa; hakika hiyo ni uchafu na ni njia mbaya.” (Surat Al-Isra 17:32), tafakari neno "Njia mbaya".

Bro tambua ndani ya tendo la ngono kuna pande mbili zenye nguvu,
Kuna Baraka halafu kuna Laana.
Baraka ni pale linapofanyika katika ndoa, kwa heshima na uhalali, inaleta urithi wa kizazi, mshik**ano wa familia na afya ya kiroho.
Laana ni pale linapofanyika nje ya mipaka yake.
So inategemeana ila mimi sintoongelea hili sana maana lipo kiimani zaidi, mi nitakwambia fact.
Kuna maneno ya falsafa ya Kigiriki, Socrates alisema: “Mwanaume asiyejishinda hawezi kuongoza hata familia yake, sembuse mji au taifa.”
So Mwanaume ni kujizuia, si kuacha kila roho ikuvute na kukutawala.

Najua wengi mnaweza msinielewe, hasa wale wenzangu na mimi ambao tumeshakuwa walevi wa ngono, lakini hili jambo kisayansi linasaidia ubongo kuondoa utegemezi wa dopamine unaosababishwa na tamaa za haraka ili kupata furaha.
Inajenga nguvu ya kuamua na kuimarisha nidhamu ya akili, hapa matatizo k**a kupoteza kumbukumbu, kushindwa ku-focus, mood swing, n.k utaishia kuyasikia kwa jirani, leo hii kuna wanaume hawana uwezo wa kutunza kumbukumbu, ni anasahau ndani muda mfupi sana, akili umeshaichosha vya kutosha sasa ni muda wa kuipumzisha.

Inapunguza hatari ya magonjwa yanayoenezwa kwa njia ya ngono.
Itakusaidia kuimarisha misuli na inakuongezea nguvu ya mwili kwa sababu nguvu zitakuwa hazimwagwi ovyo ovyo.
Pia kiroho inakuza ukaribu wako na Mungu kwa sababu unajitoa kujitakasa, maroho yote machafu uliyokusanya kutoka kwa wanawake tofauti tofauti kupitia uasherati yanaanza kulegea na kukosa nguvu maana umeacha kuyalisha chakula yakipendacho (Ngono),
Inaondoa hisia za hatia na aibu, utajiona huru sana na baadae utajiona mwenye furaha mno, (unajitibu psychologically)
Inajenga moyo wa subira, uvumilivu na hekima katika maamuzi ya maisha yako.

La muhimu zaidi k**a unajitafuta, unajenga uchumi wako, unajiandaa kuwa mwanaume atakaye heshimika na kumiliki familia pasipo kuteteleka, ni muhimu sana kukaa mbali na hizi sketi, kaa mbali na bikini, jijenge hao wanawake watakutafuta wenyewe, jijenge kiuchumi, kimwili piga tizi sana, soma vitabu achana na malaya, watakuangamiza bure na hakuna cha maana utapata, starehe ya muda mfupi itakupoteza mazima, najua kuacha hauwezi ila jitahidi na ukishindwa kabisa kabisa kabiiiiisa basi vuta pisi yako moja tulia nayo, malaya hawana shukurani na umalaya ni kaburi.

🌱 Challenge: Jaribu mwaka mmoja bila kufanya ngono ikiwa hujaingia kwenye ndoa, na uone jinsi utakavyokuwa na nguvu mpya kimwili, kiakili na kiroho.
Na wale mlio kwenye ndoa, fanya ujaribu kubaki njia kuu hata kwa mwaka mmoja halafu uone matokeo yatakavyo kuwa, lengo ni kupunguza matumizi ya kiungo chako cha mwili.
Kuna hekima kubwa sana ndani yake ila huwezi kuelewa k**a utalichukulia kwa juu juu.
Lakini pia walioko kwenye ndoa ni bora zaidi kwao kwani madhara tuyapatayo ambao hatujaoa ni mengi sana tofauti na wao.

✍🏽 Na: Halisi Naturalist

(You can share this information to others but without editing and putting your name. This information has been copy righted under Halisi Naturalist, any form of plagiarism or data manipulation will be regarded as an offence.)

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Naturalist posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Naturalist:

Share