Halisi Naturalist

Halisi Naturalist Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Halisi Naturalist, Digital creator, Dar es Salaam.
(1)

โœจ Safe space for real stories & community advice
๐ŸŒฑ Plant identification & African medicine traditions
๐Ÿ”ฌ Connecting science & culture
๐Ÿƒ Nature heals

๐Ÿ“ฑ WhatsApp: 0788900445
๐Ÿ“Bukombe Geita Tanzania

16/11/2025

Andika tatizo lako la kiroho au kibaolojia, unalotaka nizungumzie tiba yake.
๐Ÿ‘‡

16/11/2025

Spiritual intuition (uwezo wa kuona mambo kabla hayajatokea) eidha kwa kuhisi, kuota ndoto, n.k
K**a wewe ni mmoja wapo tambua umepewa zawadi na Mungu, usiipuuzie.

Moja ya sababu inauowafanya wanaume wengi duniani waathirike kisaikolojia ni hii, na kwa bahati mbaya wengi wamekuwa ni ...
10/11/2025

Moja ya sababu inauowafanya wanaume wengi duniani waathirike kisaikolojia ni hii, na kwa bahati mbaya wengi wamekuwa ni wa kupenda miujiza ndio maana hata kupona kwao imekuwa kazi.

Tatizo umedumu nalo ndani ya mwaka mzima au miaka, lakini unataka ulitatue ndani ya siku moja kisa tu umeambiwa hii ni dawa ya miti shamba.

Tambua kuwa huwa kuna sababu, na hizo sababu huwa ziko mbali mbali, na zote hutatuliwa kwa dawa fulani fulani.
Kwa mfano Umeshajaribu kutumia unga wa mizizi na magome ya muegea tatizo hili halijaisha, Umeshatumia miti kadhaa bado haujapona, unaamua kukata tamaa.
Hii haitakiwi na sio njia pekee ya kumaliza tatizo lako.
Tafuta chanzo cha tatizo lako kwanza, na usiwe mwepesi kukata tamaa.

09/11/2025

K**a una mimba na unaambiwa ipo nje ya mfuko wa uzazi, au unaambiwa imekimbilia mgongoni, au unaambiwa imepanda juu kifuani, na mengine mengi kuhusu mimba na mfuko wa uzazi, dawa ndio hii.

Huu ni mti wa mkale, au mbono, au mbono kaburi, yote ni majina yake.
Utazame vizuri usije ukachanganya.

Note: Pinga panga moja tu tawi lidondoke chini

09/11/2025

Parinari curatellifolia (Umunazi)

Ni mti mkubwa unaopatikana sana Afrika Mashariki, Kusini na Kati.
Mti unakuwa mrefu (hadi mita 10โ€“20).

Matunda ni ya duara, rangi ya hudhurungi au ya udongo, yana nyama laini na tamu yakiwa yameiva sana, lakini yana ukakasi yakiwa mabichi au hayajaiva vizuri, ni matunda yenye harufu k**a ndizi mbivu.
Ndani kuna mbegu moja kubwa ngumu.

๐Ÿˆ Faida za Matunda ya mti huu

1. Hupatikana k**a chakula cha asili chenye nguvu nyingi.

2. Lenye vitamini C, madini ya chuma, na antioxidants zinazosaidia mwili kupambana na uchovu na sumu.

3. Husaidia kuboresha mmengโ€™enyo wa chakula na kuongeza kinga.

๐ŸŒฟ Matumizi ya Mizizi na Magome (Katika tiba Asilia)
Katika tiba za jadi, mizizi ya Parinari curatellifolia au umnazi hutumika kwa mambo mengi, hasa ikiwa ni katika:-

Maumivu ya mgongo na kiuno

Magonjwa ya mifupa (rheumatism)

Maumivu ya tumbo

Malaria

Maambukizi ya ngozi
Sababu: Mizizi na magome yake yana misombo ya kiasili k**a flavonoids, triterpenoids, na saponins, ambayo huondoa uvimbe, vidonda, na maumivu, huweka vilainishi, n.k (anti-inflammatory na analgesic).

07/11/2025

Tuishi kwa hekima, busara na upendo, ujana huisha, mali huisha, uzuri huisha, ila amali zako njema, utu wako, na upendo hudumu milele hata k**a haupo tena duniani.

05/11/2025

Kuna wale ambao wana mikosi sugu, wanatumia dawa lakini mambo yao hayafanikiwi, wanapata nafuu siku chache then wanarudi pale pale, watu hao walikuwa na bahati lakini kwa sasa ni mikosi tu na matatizo.
Tumia dawa hii itakusaidia sana kuondokana na hali hiyo.

Huu mti unaitwa Mvugo au mgobore, ni mti ambao una kazi nyingi sana za kiroho, za kibaiolojia, mfano kusaidia matatizo ya uzazi kwa mwanamke mjamzito na asiye mjamzito, mambo ya limbwata ya mapenzi, kutoa mikosi na vifungo sugu, kuongeza riziki/mauzo kwa biashara n.k ni mengi mno.

Tazama video mpaka mwisho, ukiuliza swali ambalo jibu lake lipo kwenye hii video sintolinibu.
Asanteni sana na karibuni sana.

Hii ni sadaka yangu kwako naomba na wewe uitoe kwa wengine kwa ku-share

Vilivyotajwa ni
Mvugo/mgobore
Almiti
Nyambilagiza
Mjusi/Lizard

03/11/2025

Tumekuwa offline kwa muda mrefu hapa Tanzania, k**a umerudi online nyoosha kidole tujuane ๐Ÿ‘†

Niliwa-miss sanaaa

Niwape videos leo au niwaache kwanza bado mnatiki..!Nawasalimu waungwana ๐Ÿ™
29/10/2025

Niwape videos leo au niwaache kwanza bado mnatiki..!

Nawasalimu waungwana ๐Ÿ™

28/10/2025

Kwani youtube kuna nini eti?

28/10/2025

๐ŸŒฟ Huu mmea kwa kilugha unaitwa Mfuruka 'Umufuruka' kitaalamu unaitwa 'Senna Didymobotrya' au african senna ๐ŸŒฟ

Ni mmea wa familia ya Fabaceae wenye faida nyingi za kitabibu.
Mmea huu umekuwa ukitumika katika tiba za kiasili na umethibitishwa na tafiti kadhaa za kisayansi.

Matumizi na Faida Zake

1. Matatizo ya tumbo na matumbo/utumbo

Husaidia kuondoa kuvimbiwa, gesi, na matatizo ya tumbo.
Sennosides zilizomo ndani yake husaidia kuchochea mzunguko wa chakula kwenye utumbo kwa urahisi.

2. Kutibia minyoo
Huondoa wadudu wa tumbo kwa ufanisi mzuri.

3. Afya ya vivimbe
Kutibu uvimbe, hemorrhoids/bawasiri harara, mapunye, na magonjwa sugu ya ngozi.

4. Afya ya ini na damu
Huongeza utendaji wa ini na kusaidia kusafisha damu. Ila k**a tayari una tatizo la ini usitumie๐Ÿ“

5. Kuondoa sumu mwilini
Inasaidia mwili kuondoa uchafu, kuchochea usafi wa seli, na kusaidia afya ya misuli na mifupa.

6. Hutibu arthritis, gout, na kushughulikia baadhi ya magonjwa ya bakteria na fangasi.

Njia za Matumizi

Poda ya majani robo kijiko changanya na maji ya vugu vugu.

Fanya mchanganyiko wa unga wa dawa hii na karafuu, tangawizi, vitunguu swaumu, manjano, kwa kunywa kutoa sumu mwlini.

Tahadhari Muhimu

Mjamzito epuka kutumia, inaweza kusababisha madhara makubwa.

Watoto: Ni salama kwa watoto zaidi ya miaka 2, lakini tu usizidishe kipimo, mg 5-10.

Usizidishe dozi, matumizi makubwa yanaweza kusababisha kuhara, maumivu ya tumbo. N.k

Watu wenye magonjwa ya figo, ini, moyo, au ugonjwa wa inflammatory bowel disease (IBD) wasitumie bila ushauri wa daktari.

Kuingiliana na dawa nyingine: Virutubisho vya mmea huu vinaweza kuingiliana na dawa za moyo, sukari.

Usisahau ku-share sadaka hii kwa wengine.

28/10/2025

Mti uliopigwa na radi una matumizi mengi, huwa unachanganywa na dawa za kinga, kinga dhidi ya wachawi, na vitu vibaya au shari zingine. Mchawi akijipendekeza litakalo mkuta itakuwa historia.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Naturalist posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Naturalist:

Share